Msanii William Lyimo maarufu Billnass na nyota wa muziki wa Bongofleva Faustina Mfinanga maarufu Nandy wamefunga ndoa.
Wawili hao wamefunga pingu za maisha leo Julai 16, 2022 katika kanisa la KKKT Mbezi Beach, Dar es Salaam.
Billnass na Nandy ni wapenzi wa muda mrefu na siku za hivi karibuni waliutangazia umma kuwa muda si mrefu watakuwa wazazi baada ya kupost picha zikimuonyesha Nandy akiwa mjamzito.
Picha: Clouds Digital
































Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba M. Ndaki (MB) akipata maelezo kuhusiana na huduma zinazotolewa na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kutoka kwa Afisa Utafiti Mifugo wa TVLA Ndg. Msafiri S. Kalloka kwenye uzinduzi wa maonesho ya Mifugo kibiashara yaliyofanyika kwenye uwanja wa maonesho Highland Estate LTD, Ubena Zomozi, Chalinze Julai 15, 2022.
Ndg. Msafiri S. Kalloka Afisa Utafiti Mifugo wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) akitoa maelezo kuhusiana na huduma zinazotolewa na Wakala kwa wanananchi waliotembelea banda la TVLA kwenye uzinduzi wa maonesho ya Mifugo kibiashara yaliyofanyika kwenye uwanja wa maonesho Highland Estate LTD, Ubena Zomozi, Chalinze Julai 15, 2022




















