Friday, 5 June 2020

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya 12 na 13

Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188


ILIPOISHIA   
RPC akaifunua maiti moja na akamuonyesha Tomas maiti ya Selemani D iliyo chakaa kwa kupigwa risasi.
“Hawa jana tu walikuwa hai, wakisherekea pesa nyingi walizo zivuna kwa kumteka nabii Sanga. Ila sasa hivi wapo hapa hawajitambui. Wewe upo hai ila hii bastola yangu ina weza kukulaza na wewe hapa na ukajumuika na hawa wezako. Niambie ni wapi wezako walipo mpeleka nabii Sanga la sivyo, utaungana nao na wewe utaingizwa kwenye jokofu lile pale ukiwa maiti”


RPC alizungumza huku akimuwekea Tomas bastola ya kichwani na kumfanya Tomas kuanza kutetemeka mwili mzima huku akiona mwisho wa maisha yake sasa umefika, tena ana fia ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti.
   
ENDELEA
Kwa woga ulio mtawala Tomas akashindwa kuizuia haja ndogo na kujikuta akijikojolea. RPC hakulijali hizo zaidi ya kuendelea kuzungumza kwa ukali huku akiwa ameishikilia bastola hiyo.
“Kwa nini ulimteka nabii Sanga, nini alikufanyia ikiwa wewe ni mtu wake wa karibu?”
“Ehee…..!!”
“Nini alikufanyia?”
RPC alizungumza kwa ukali na kumfanya Tomas kuanza kukumbuka jinsi alivyo anza mahusiano na mke wa nabii Sanga. Kukolea kwa mapenzi yao kuliwafanya washiriki katika dhambi ya kumteka nabii Sanga ili wazuie mpango wake wa kumfungulia mgahawa na kumnunulia nyumba Magreth.
“Oya andaa hilo jokofu la hapo kwa ajili ya huyu mjinga, nina muua na siri itabaki kati yako mimi na wewe?”
RPC alizungumza huku akimtazama muhudumu wa Mochwari. RPC akaikoki bastola hiyo na kumfanya Tomas kuzidi kuweweseka. Japo ame fanya makosa, ila hatamani kabisa kufa.
“Nitasema ukweli”
Tomas alijikuta akiropoka na kumfanya RPC atoe simu yake mfukoni. Akaweka upande wa kurekodi sauti na kusubiria ukweli ambao Tomas ata ukiri.
“Zungumza nina subiria.”
“Ahaa miezi kadhaa iliyo pita nabii Sanga na mke wake walinipa jukumu la kuwatafutia eneo kubwa la kujenga mji, kule kigamboni. Jukumu la kusimamia mpango huo, alimkabidhi mke wake. Hivyo nilipata muda mwingi sana wa kuongozana na mke wake kwenda kutembelea maeneo mbali mbali ambayo nilikuwa nimeyapata.”
Tomas alizungumza huku akiendelea kutetemeka. RPC hakuishusha bastola yake, hii ni kuhakikisha kwamba Tomas ana zungumza kila kitu.
“Tulijikuta tukianza mahusiano ya kimapenzi na mwana mama huyo”
RPC akastuka sana ila hakuhitaji kuonyesha mstuko huo kwani ana hitaji kufahamu mambo mengi sana kutoka kwa Tomas.
“Tulifanya kwa siri sana. Kadri siku zilivyo zidi kwenda ndivyo jinsi penzi letu lilivyo zidi kuchanua. Kuna siku nabii Sanga alinipigia simu na kuniambia kwamba ana hitaji nimtafutie sehemu ya kufungua Mgahawa na nyumba ya kupanga maeneo ya Mikocheni. Alikuwa na mpango wa kumpangishia binti mmoja ambaye ni muumini pale kanisani kwake”
“Binti huyo ana itwa nani?”
“Magreth. Swala hilo nabii Sanga aliniomba nisimuambie mke wake kabisa. Ila kwa upande mmoja roho iliniuma kuona binti mdogo ana nunuliwa nyumba ya milioni mia tano. Nilimueleza mke wake na mkewe aka toa wazo la kumteka mume wake, hadi wiki ijayo ndio aachiliwe na watekaji ili aende nchini Nigeria kwenye kikao cha wachungaji na manabii”
RPC akajikuta akishusha pumzi taratibu. Katika miaka yote ya kuifahamu familia ya nabii Sanga, hakutarajia kwamba mke wa nabii huyo ipo siku ata fanya kosa kubwa kama hilo.
“Niliwatafuta vijana na nikawapa kazi hiyo na waliweza kuikamilisha kikamilifu”
Tomas alizungumza huku akiendelea kutetemeka kwa woga.
“Kwa hiyo mzizi wa tukio zima ni mke wa nabii SANGA?”
“Ndio”
Taratibu nabii RPC akashusha bastola yake na kuirudisha kiunoni mwake. Aka yahifadhi mazungumzo hayo ya Tomas kwenye simu yake na kuiweka mfukoni.
“Zirudishe hizo maiti”   
Nabii Sanga alimueleza mtu huyo anaye hudumia Mochwari kisha wakatoka katika chumba hicho. Akamuingiza Tomas kwenye gari lake, kabla ya yeye kuingia, akatafuta namba ya kijana wake mmoja na kumpigia.
“Ndio mkuu”
“Upo wapi?”
“Bado nipo nyumbani kwa nabii Sanga.”
“Hakikisha huyo mke wake hatoki kwenda eneo lolote”
“Kwa nini mkuu?”
“Hupaswi kunihoji kwa nini, fwata amri yangu”
“Samahani sana mkuu.”
RPC akakata simu na kuingia ndani ya gari.
“Huyo Magreth ana ishi wapi?”
“Ahaa sifahamu, ila wale vijana mulio waua ndio walimfwatilia msichana huyo na kufahamu ni wapi ana fikishwa na nabii Sanga. Ila kwa mimi sijui”
RPC akamtazama Tomas machoni mwake kwa sekunde kadhaa na kuamini kwamba anacho kizungumza ni kitu cha ukweli. Nabii Sanga akawasha gari hilo na kurudi makao makuu ya polisi. Akakabidhi Tomas kwa vijana wake na akarudishwa mahabusu. RPC moja kwa moja akapitiliza hadi ofisini kwake, akajifungia na kuisikiliza sauti ya Tomas jinsi inavyo toa maelezo hayo.
“Haki ya Mungu hawa wanawake hawaaminiki”
RPC alifikiria huku akitafakari ni jinsi gani anavyo weza kuvumbua mbele ya jamii kesi hiyo ambayo kwa namna moja ama nyingine ina weza kwenda kuligawanya kanisa la nabii Sanga huku naye akiwa ni miongoni mwa waumini wa kanisa hilo.
                                ***
    Magreth akabaki kama alivyo zaliwa huku akimtazama nabii Sanga anaye malizia kuivua suruali yake. Akatembea taratibu hadi kitandani. Akamlaza nabii Sanga chali,huku taratibu akimtazama.. Aibu aliyo kuwa nayo awali, yote ime muondoka. 


Magreth kwa jinsi alivyo pagawishwa na kiasi cha pesa alicho pewa na nabii Sanga, hakuona haja kumbania mzee huyo, huku moyoni mwake akiamini kwamba swala zima la kumpenda Evans litakuja hapo baade akiwa amesha weka kila kitu sawa. Mtanange wa wakati huu hakuwa wa kinyonge,  Nabii Sanga alizidi kuchanganyikiwa na kupagawa na penzi bichi kabisa la Magreth.
“Nitakupa kila utakacho kitaka Mage”
Nabii Sanga
“Kweli?”
“Haki ya Mungu vile, sijawahi kupata penzi tamu kama lako.”
“Uta nilinda dhidi ya mke wako?”
“Ndio baby, hawezi kukugusa”
“Niahidi”
“Nakuahidi, haki ya Mungu vile”
Magreth alifanya mahojiano hayo huku akijituma vzr. Kuokoka kwake hakukumfanya ashindwe kumpagawisha nabii Sanga. Hadi mzunguko una kwisha kila mmoja akajikuta akiwa ameridhika

“Niambie nini una hitaji nikufanyie?”
“Aahaa…kuna yule mgonjwa wangu kule hospitalini. Nilikuwa nina ombi moja”
“Ombi gani baby”
“Nimezungumza naye na amenieleza shida alizo pitia. Siku ile aliyo niokoa aliweza kuibiwa vyeti vyake vya kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu na siku ile aliondoka kwa rafiki yake na hakuwa na pakuishi. Nina omba nitakaopo hamia kwenye ile nyumba kigamboni, niweze kuishi naye”
Magreth alizungumza huku akiwa amejilaza kifuani mwa nabii Sanga
“Ahaha. Una muamini?”
“Kama aliweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yangu. Nina muamini kwa maana wale Panya road siku zile wange nibaka na sijui ningekuwa kwenye maisha gani. Inawezekana ningekuwa nimesha kufa sasa”
“Nimekuelewa mke wangu. Basi akitoka hospitalini, utaishi naye. Ila hakikisha kwamba huni saliti”
“Kwa nini nikusaliti mpenzi wangu, ikiwa usichana wangu wewe ndio ume bahatika kuutoa. Au huniamini?
“Nakuamini tena sana kwa maana nime jionea jinsi gani ulivyo ”
“Nashukuru mume wangu”
“Leo usiku nitarudi kwangu, ila hakikisha kesho una kwenda kununua asset zote za ndani kisha zinapelekwa kwenye hiyo nyumba mpya.”
“Sawa mpenzi”
“Kuna rafiki yangu mmoja ana kampuni ya magari. Nitamuambia kesho akutafutie gari zuri na lenye hadthi na wewe”
“Asante sana mpenzi wangu, ila mimi siwezi kuendesha gari?”
“Ohoo usijali katika siku hizi ambazo nita kuwa hapa Tanzania, nitakufundisha gari, hadi nina ondoka nina imani utakuwa umesha mudu kuendesha”
“Sawa sawa mume wangu”


                                **********
‘Kama porini hakuweza kuonekana na majambazi tumewakuta wao wenyewe, je watakuwa wamemuaa? Hapana hajauwawa au wamemuachia?’
RPC aliwaza kichwani mwake huku akijaribu kujiongeza kutokana na mazungumzo ya Tomas.
‘Kama wamemuachia ata kuwa amekwenda wapi? Au ame fahamu kwamba mke wake ndio msaliti?’
‘Ila kama aliamua kumnunulia mwanamke nyumba ya milioni mia tano na kuhitaji kumfungulia mgahawa, nina imani kwamba atakuwa ana muamini sana huyo mwanamke na kumpenda’
‘Magreth…..Yaa Magreth anaweza kufahamu ni wapi alipo nabii Sanga. Ni lazima tumpate huyu msichna’
RPC baada ya kupata mwanga katika swala la kuto kumpata nabii Sanga, akanyanyuka kwa haraka na kuelekea mahabusu alipo fungiwa Tomas.
“Nileteeni mtu wa kuchora”
RPC alimuagiza bodyguard wake huku akimtazama Tomas ambaye amejikunyata kwenye kona ya chumba hicho.
“Nahitaji utuelezee sifa za Magreth. Si una mkumbuka kwa sura?”
“Ndio nina mkumbuka”
Polisi mwenye taaluma ya kuchora akafika eneo hilo. Tomas akaanza kuelezea muonekano wa Magreth.
“Ana sura nyembaba kiasi iliyo chongoka kwenye kidevu chake. Ana macho yaliyo kaa muundo kama wa yai, ila si makubwa. Ana pua ndogo ndogo kiasi na lipsi zake pia ni ndogo kiasi. Ni mrefu kama futi sita kasoro kidogo. Ana rangi ya chocolate fulani hivi.”
Kila alicho kieleza Tomas ndicho anacho kifanya mchoraji. Baada ya muda mfupi sura halisi ya Magreth ikapatikana kwenye karatasi ya mchoraji.
“Imekamilika?”
“Ndio mkuu”
RPC akaitazama picha hiyo ya Magreth, kweli ni mwanamke mzuri sana na anaye vutia. RPC akamgeuzia Tomas picha hiyo.
“Ndio huyu?”
“Ndio ndio huyo huyo wala hujakosea”
Tomas alizungumza wa kubabaika.
“Vijana wako hawakukuambia ni wapi walipeleleza hadi wakatambua anapo ishi?”
“Hapana hawakunijulisha kwani lengo lao kubwa ilikuwa ni nabii Sanga na waliweza kumfwatilia nabii Sanga alipo kuwa ana rudi kwake ndio waka mvamia na kumteka.”
RPC akaikunja vizuri karatasi hiyo yenye picha ya Magreth. Akaeleka kwenye kitengo cha askari wanao dili namitandano.
“Scan hii picha na unitafutie huyu binti”
“Sawa mkuu”
Kijana huyo aka iscan picha hiyo na kuiingiza kwenye computer yake na kuanza kutafuta picha hiyo ya Magreth kwenye mtandao. Haikuchukua muda maelezo yote kuhusiana na Magreth yakatokea katika computer hiyo. Imekuwa ni rahisi sana kwa askari hao kuipata kwani Magreth ni miongoni mwa  walio jisajili kwenye kitambulisho cha taifa hivyo taarifa zote zinazo muhusu yeye zipo hapo.
“Magreth Jonas Asinga”
RPC alisoma maelezo yanayo onekana kuhusiana na Magreth.
“Hembu tuma maelezo hayo kwenye mitando ya simu watupatie information za binti huyo. Nina imani mtandoa mmoja wapo utakuwa na information zake za mawasiliano.”
“Sawa mkuu”
Kijana huyo akaandika email kwa mitandoa mikubwa mmine ya mawasiliano , huku email hiyo ikwia huku ikiwa na wito wa kuomba data za mteja Magreth Jonas Asnga, ikiwemo namba yake ya simu. Baada ya dakika tano kijana hiyo akajibiwa email yake na mtandao wa simu ambao Magreth ana utumia.
“Waombe simu zote zilizo pigwa jana na leo watutumie”
Maombi hayo hayakuweza kukataliwa kwa maana yana tokea makao makuu ya polisi. Wakaanza kuorozesha audio za mazungumzo yote aliyo yafanya Magreth kwa siku ya jana na leo. Wakaanza kusikiliza mazungumzo hayo ambayo yanamuhusisha Magreth na nabii Sanga ambaye alimpa maelekezo ya kwenda kuchukua pesa ofisini kwake. Wakazidi kuendelea kusikiliza mazungumzo hayo hadi jinsi MagreLth aivyo wasiliana na majambazi hao na kuwajulisha amefika Mkinga.
    Mazungumzo ya siku ya leo kati ya nabii Sanga na muhasibu wake akimuomba amfwate sehemu alipo, ikampa picha RPC ya kuweza kufahamu kwamba nabii Sanga yupo sehemu gani na yupo sehemu salama. Ila kutokana ni ahadi ambayo alitoa kwa wananchi kwamba jeshi la polisi lita hakikisha kwamba lina mrudisha nabii Sanga salama salmini mikononi mwa familia yake. Ikamlazimu RPC kuandaa kikosi cha vijana wake wanne na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwa Magreth, huku zoezi hilo likifanyika kwa siri sana pasipo askari wengine kuweza kufahamu ni kipi RPC wao ame kigundua.


 ==>>SIN -Sehemu ya 13  
“Huu ndio mtaa anao ishia huyo binti?”
RPC aliwaambia vijana wake huku wakitazama mtaa huu wa uswahilini wenye mchanaganyiko wa watu wa kila aina.
“Msichana mwenyewe anafanania hivi?”
RPC alizungumza huku akiwaonyesha picha ya Magreth iliyo chorwa kwenye karatasi hiyo.
“Huyu ame fanya kosa gani mkuu?”
“Ina sadikika huyu ndio yupo na babii Sanga?”
“Mkuu unataka kuniambia kwamba huyu binti ndio alite mteka nabii Sanga?”
“Hapana, hapa inaonekana nabii Sanga alisha achiwa na watekaji, ila akaamua kuelekea kwa kimada wake kujificha”
“Mmm!! Sasa kwa nini asiende kwake au kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi?”
“Hilo ni swali ambalo tutalipata mara baada ya kuwapata wote wawili. Hembu waulize hao watoto juu ya picha hiyo”
“Sawa”
Askari mmoja aliye valia nguo za kirai. Akashuka kwenye gari hilo na kuwasogelea watoto wanao cheza pembezoni mwa barabara hiyo ya vumbi.
“Mambo”
“Poa shikamoo”
“Marahaba. Nina swali nahitaji kuwaliza”
“Uliza tu?
“Muma mfahamu dada huyu?”
Askari huyo aliwaonyesha watoto hao picha ya Magreth, wenye miaka kati ya sita hadi kumi.
“Ndio tuna mfahamu ana itwa dada Mage”
“Ana ishi wapi?”
Watoto hawa wakatazamana, kisha mmoja wao akaonyesha ishara ya kuhitaji kupewa pesa. Askari huyu akatoa noti ya shilingi elfu tano mfukoni mwake na kuwakabidhi. Mtoto huyo mwenye kimo kirefu kuliko wezake wote, akaipokea pesa hiyo.
“Ana kaa pale kwa bi Ngedere. Ile nyumba yenye kibaraza mbele na ngazi?”
“Ile nyumba yenye matairi mbele na wale wamama walio kaa??”
“Ndio”
“Sawa asanteni”
Askari huyo akarudi kwenye gari.
“Daa kweli kazi ipo bosi, yaani hadi watoto wameanichomoa pesa ya kuelekezwa tu”
“Hahaahaa, ni wapi alipo sema?”
Askari huyo akawaonyesha wezake nyumba hiyo. Taratibu wakaegesha gari hilo kwenye hiyo nyumba na wakashuka askari wawili ambao wote wamevalia nguo za kiraia. Gari hilo iana ya Toyota VX V8 likawastua sana wapangaji wa nyumba hiyo walio kuwa wamekaa kibarazani.
“Habari zenu?”
“Salama”
“Tume mkuta Magreth?”
Wapangaji hawa wkatazamana, katika siku mbili tatu hizi Magreth amekuwa akiletwa na magari ya kifahari jambo ambalo lime zua maswali mengi kwa wamama hao wanne.
“Ndio yupo”
“Ahaa muna weza kutusaidia kutuonyesha chumba chake?”
“Mmm shosti yetu amekuja kufumaniwa nini?”
Mama Boka aliwanong’oneza kwa sauti ndogo wezake hao kwa maana wana sikia sauti ya mwanaume katika chumba cha Magreth ila hawajamuona mwanaume ambaye yupo ndani humo.
“Ahaa ingieni humo ndani, chumba cha pili, mkono wa kulia ndio chumba chake”
“Tuna shukuru”
“Ila nyinyi ni kina nani?”
“Ni watu wema kabisa musiwe na mashaka”
“Mmmm haya”
Askari hao wakaingia ndani humo, wakasimama kwenye mlango wa Magreth na kusikilizia miguno ya kimahaba inayo tokea ndani humo.
“Gonga mbona una shangaa?”
“Wapo kwenye starehe zao bwana”
“Sisi tupo kazini. Ngoja nigonge”
Askari huyo akaanza kugonga kwa nguvu hadi Magreth na nabii Sanga ambao wapo katikati ya mapenzi mazito wakastuka.
“Nani huyo?”
Nabii Sanga aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka.
“Atakuwa ni mama mwenye nyumba. Kwani sauti yangu ina sikika hadi huko nje?”
“Sijajua, ila mbona naona ina sikika hapa hapa”
“Ngoja”
Magreth akajichomoa ,. Akashuka kitandani, akajifunga tenge na kufungua mlango huo huku akiwa na jazba kubwa, na amepania kama ni mama mwenye nyumba basi ata mpatia jibu litakalo mtingisha mwana mama huyo mwenye maneno mengi. Magreth akastuka sana mara baada ya kukutana na sura za wanaume ambao haja wahi kuwaona hata siku moja.
“Wewe ndio Magreth?”
“Ndio ni mimi. Ny….i….nyi ni kina nani?”
Magreth aliuliza huku woga ukiwa umemtawala. Mahojiano hayo yakamfanya nabii Sanga kutafuta suruali yake nakuivaa kwa haraka huku kichwani mwake akihisi kwamba watu hao ni majambazi.
“Tume mkuta nabii Sanga?”
Swali hilo lika wachanganya kabisa, nabii Sanga na Magreth kwani watu hao hawajajitambulisha hadi sasa hivi.
“Ahaa nyingi ni kina nani?”
Ikamlazimu Magreth kuuliza swali hilo kabla ya kujibu swali alilo ulizwa.
“Sisi ni maofisa wa polisi kutoka kituo cha kati”
“Waache waingie”
Nabii Sanga alimuambia Magreth na kumfanya ageuke na wakatazamaana huku Magreth akiwa na mshangao mkubwa sana.
“Waache wapite”
“Karibuni”
Askari hao wakaingia na kumkuta nabii Sanga akiwa ana vaa shati lake
“Habari yako mzee”
“Salama. Tumekuja kukuchukua na kukuweka mikono salama”
“Hapa pia ni mikono salama. Ila nina elewa nini munataka kufanya. Sasa hivi ni saa kumi na mbili, acheni kigiza kiweze kuingia nami nitatoka ndani humu”
“Ila muheshimiwa, tupo hapa na mkuu wetu na ametoa agizo la sisi kukuchukua na kukupeleka kwenye gari lake lipo hapo nje”
“Nendeni mukamuite mkuu wenu”
“Ahaa kwa nini?”
“Nyinyi nendeni mukamuite yeye, ndio nahitaji kuzungumza naye”
Askari mmoja akatoka ndani humo na kurudi kwenye gari. Akamueleza RPC nini anacho hitaji nabii Sanga.
“Waondoeni hao wamama hapo barazani, sihitaji wafahamu juu ya uwepo wangu mtaani hapa?”
“Sasa tuta fanya nini mkuu”
“Fanyeni chochote.  Nyinyi ni askari hakikisheni kwamba wana ondoka eneo hilo”
Askari hao watatu wakajishauri na kushuka kwenye gari hilo. Wakawasogelea wana mama hao wanao endelea kutazama kila kinacho endelea na kila mmoja ana hamu ya kufahamu ni nini kinacho endelea kwa mpangaji mwenzao.
“Sisi ni maofisa polisi. Muna ishi humu ndani?”
Wamama hao wakastuka kidogo huku wakiwatazama askari hao.
“Ndio”
“Basi kila mmoja aingie chumbani kwake na asidhubutu mtu kuchungulia”
“Kwani kuna nini?”
“Mama hatuna muda wa kutangaza au kukueleza kuna nini. Ingieni ndani”
Askari mmojaa alizungumza kwa ukali sana na kuwafanya mama Boka na wezake wanyanyuke huku wakikunja mkeka walio kuwa wameukalia. Wakaingia ndani huku wakiwa na hofu kubwa. Askari walipo hakikisha kwamba hali imekuwa shwari, bodyguard wake akamfungulia mlango na akashuka kwenye gari hilo na kuingia ndani. Nabii Sanga aka simama na kuepeana mkono na RPC kwani ni watu wanao fahamiana kwa muda mrefu na pia wana heshimiana.
“Naomba mutupishe”
RPC alizungumza na vijana wake wakatoka na kusimama kwenye kordo hiyo kuimarisha ulinzi.
“Huyu ni Mage, binti ambaye aliweza kujitolea kunipa msaada wa kipesa kipindi nilipo kuwa nimewekwa kizuizini na majambazi”
“Ahaa sawa mzee. Nina litambua hilo kwa maana tume fwatilia mazungumzo ya simu ya binti. Hayo mazungumzo ndio yameweza kutusaidia sisi kuweza kufika hapa”
“Sawa sawa”
“Tumekuja kwa jambo moja tu. Tunahitaji tukupeleke nyumbani kwako kwa maana sehemu hii sio salama kabisa.”
“Sawa hilo halina shaka. Ila nahitaji huyu msichana asi sumbuliwe kwa chochote na wala asiweze kuitwa kituoni kwa mahojiano”
“Sawa sawa”
“Mage kuwa na amani na kesho hakikisha kwamba una fanya ule utaratibu nilio kuagiza uweze kuufanya”
“Sawa baba”
“Kwa heri”
Nabii Sanga na RPC pamoja na vijana wake wakatoka ndani hapo na moja kwa moja wakaeleka katika gari na kuondoka. Magreth akashusha pumzi na kujitupa kitandani, kwani uwepo wa maaskari hao umemfanya awe katika wakati wa mashaka. Ila alipo kumbuka kwamba ana kiasi kikubwa cha pesa benki, basi mawazo na matatizo hayo ya polisi yakamuondoka kabisa kichwani mwake.
“Sasa mimi ni tajiri”
Magreth alizungumza kwa furaha. Mlango wake ukagongwa na akasikia sauti ya mama Boka ikimuita.
“Nakuja”
Magreth alizungumza huku akishuka kitandani. Akajifunga tenge lake vizuri na kufungua mlango.
“Ehee upo salama wewe?”
“Ndio kwa nini?”
“Hawa polisi wamekuja kufanya nini hapa?”
“Hahaa mbona muna mashaka hivyo au mume hisi nime tekwa na watu ?”
“Weee!! Mwanzo tulihisi kwamba ume kuja kufumaniwa. Ila walipo tuambia tuingia ndani na kujifungia, hapo ndipo matumbo yalipo tupata moto”
“Kweli shosti yetu tulijawa na wasiwasi mwingi sana. Haya tuambie ni nini kinacho endelea?”
Mama Amina naye aliuliza.
“Ngoja kwanza niwashukuru majirani zangu kwa kuishi nami kwa amani japo tulikwaruzana katika maswala ya zamu za usafi na ununuzi wa luku, ila yote katika yote. Mungu yeye pekee ndio anaye fahamu nini tunacho pitia kwenye haya maisha”
“Mbona una ongea hivyo?”
Mama mwenye nyumba aliuliza huku akitokea mlango wa uwani na kuwafanya wapangaji hao walio simama kwenye mlango wa Magreth kumshangaa.
“Kesho nina hamia Kigamboni. Kuna nyumba yangu nimenunua kule”
Magreth aliwadanganya wezake hao katika swala zimala kununua nyumba.
“Mage ume nunua nyumba!!?”
“Ndio mbona muna shangaa au sina hadhi ya kununua nyumba?”
“Mmmm kwa kazi gani ulio kuwa nayo? Hembu acha kuwaongopea wezako na wewe”
Mama mwenye nyumba alizungumza kwa kejeli.
“Hahaa, wewe baki hapo hapo kwenye hili banda lako la kuku”
“Hahaaa!! Banda la kuku, ulitumwa kujakukaa hapa kupanga?”
Bi Ngedere alizungumza kwa hasira kwani hakupenda nyumba yake iweze kudharauliwa namna hiyo.
“Mage hembu achana naye. Tupe siri ya mafanikio yako kwa maana siku mbili hizi tumekuona una shushwa kwenye magari ya kifahari na wala hatukuoni jikoni ukijumuika nasi katika swala zima la kuchoma maandazi”
“Ni kweli jamani, kesho mimi nina hama. Haya yaliyo tokea humu ndani kwangu sinto weza kuwaambia. Leo mumesha pika?”
Magreth alibadili mada kwa kuwaliza maswali.
“Mimi nimepika toka mchana”
“Mimi nasubiri saa mbili mbili nisonge ugali nile na wanangu”
“Mimi nita nunua maandazi tu ninywe na chai.”
“Mimi bado sijapika”
“Bi Ngedere na wewe?”
“Na mimi nini, una pesa ya kunipa nikanunue chakula?”
“Ahaa…maneno yote ya nini mama angu. Hivi wewe mama una shindwa kuwa na kinywa kizuri cha kuzungumza?”
“Babuu weweee nikiwa na kinywa kizuri nita faidika na nini?”
“Haya nisamehe mimi. Jamani nisubirini”
Magreth akaingia ndani na kuchukua laki moja na nusu na kutoka nayo nje. Akawapa wapangaji wezake wanne kila mmoja elfu thelethini.
“Jamani hizo mutanunua mukipendacho usiku huu”
Wapangaji hao wakajawa na furaha sana, huku wengine wakimuona Magreth ndio mkombozi wao kwani baadhi yao tayari wamesha anaza kuwakimbia vijumbe wa michezo yao wanayo cheza kila siku kwa kukosa pesa za kutoa.
“Wewe mama utakula jeuri yako. Hata mia sikupi na kesho nitakagwa vitu vyangu vyote vya ndani na hata kijiko sikupi. Muangalie ndio maana Mungu alikunyima kimo kirefu ndio maana akili zako zipo kama kimo chako”
Maneno ya Magreth yakawafanya wapangaji wezake hao kucheka kwa dharau huku wakigongeana mikono na kumfanya mama mwenye nyumba ajisikie vibaya sana.
                                ***
“Kile mulicho kiona pale nyumbani kwa yule binti musi mueleze mtu yoyote”
Nabii Sanga alizungumza huku gari hilo la RPC likizidi kuchanja bunga kueleka nyumbani kwake.
“Hatuto mueleza mtu”
RPC alijibu huku akiwa amekaa siti ya mbele, pembeni kabisa ya dereva.
“Nashukuru kusikia hivyo.”
“Upo salama lakini?”
“Ndio nipo salama”
Wakafika nyumbani kwa nabii Sanga. Wakaelekea moja kwa moja sebleni na kumfanya mtoto wa nabii Sanga kumkimbilia baba yake na kumkumbatia kwa nguvu. Mfanyakazi wake wa ndani naye akafanya hivyo alivyo fanya binti huyo. Kelele za furaha zinazo sikika sebleni zikamfaya mrs Sanga kukurupuka ndani kwake na kukimbilia sebeeni. Mapigo ya moyo yakamstuka mara baada ya kukutanisha macho yake uso kwa uso na mume wake ambaye hajaonyesha sura yoyote ya kumchangamkia. RCP akaingiza mkono wake mfukoni na kutoa pingu huku akimtazama mrs Sanga anaye shuka kwenye ngazi huku akilazimisha tabasamu la kinafki kwani shida zote zilizo tokea katika siku mbili hizi yeye ndio chanzo.
                                                                                                ITAENDELEA
Haya sasa, Nabii Sanga amesha rudi nyumbani kwake, moyoni mwake ana ufahamu ukweli kwamba mke wake ndio adui namba moja. RPC ana toa pingua mfukoni je ata mfunga mrs Sanga na kuondoka naye kama mtuhumiwa? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 14.

 


Share:

Relationship Manager (Chinese Portfolio)

Relationship Manager (Chinese Portfolio) Job Purpose To evaluate Chinese portfolio credit risks associated with lending at the client interface, with the primary objective to contain credit risk within acceptable parameters. Main Responsibilities Provision of direct credit evaluation services at the customer interface. Identify credit and risk management requirements at the source of the deal negotiation/ business proposal. Conduct credit… Read More »

The post Relationship Manager (Chinese Portfolio) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunities at DUCE – Various Posts

Overview The Dar es Salaam University College of Education (DUCE) is a Constituent College of the University of Dar es Salaam established in 2005.The main functions of the College as stipulated in the Dar es Salaam University College of Education Charter and the Rules of 2010, are to provide integrated teaching, research and public service. The College invites… Read More »

The post Job Opportunities at DUCE – Various Posts appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WAZIRI WA MADINI AIMWAGIA SIFA GGML KUWEKEZA KIMKAKATI GEITA



Waziri wa Madini, Dotto Biteko akielekea kukagua soko kuu la Geita huku akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Josephat Maganga (kulia) pamoja na maofisa wengine wa mji wa Geita.
Waziri wa Madini, Dotto Biteko akitoa pongezi za serikali kwa GGML baada ya kutembelea miradi hiyo. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Josephat Maganga wakati kushoto ni baadhi ya maofisa wa mji wa Geita. 
Waziri wa Madini, Dotto Biteko akitoa pongezi za serikali kwa GGML baada ya kutembelea miradi hiyo.



Makamu wa Rais anayeshughulikia Maendeleo Endelevu katika Kampuni ya GGML, Simon Shayo akizungumza katika ziara ya Waziri wa Madini, Dotto Biteko aliyetembelea miradi ya kampuni hiyo inayotekelezwa chini ya mpango wa kusaidia jamii (CSR) mkoani Geita.


****
Na Mwandishi wetu - Geita

Waziri wa Madini, Dotto Biteko ameipongeza Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu - Geita (GGML) kwa kuwa mdau wa mfano katika kuchangia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Geita.

Biteko ametoa kauli hiyo jana katika ziara fupi aliyoifanya mkoani Geita na kukagua miradi inayotekelezwa na Kampuni ya GGML chini ya mpango wake wa kusaidia jamii (Corporate Social Responsibility) katika Mji wa Geita.

Aidha, alisema lengo la Serikali ni kuona maisha ya watu katika maeneo yote yenye rasilimali madini, ikiwemo Geita yanabadilika kiuchumi.

“Nimefurahishwa na namna ambavyo Serikali katika Mkoa wa Geita inavyosimamia ukusanyaji wa mapato kutoka kwenye sekta ya madini. Tayari tumeshafikia lengo la kukusanya zaidi ya Sh bilioni 400 kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 2020 kutoka kwenye sekta hii, na sehemu kubwa ya makusanyo haya imetoka Geita, hususan GGML. 

“Inatia moyo sana kuona kwamba sekta hii sasa inachangia zaidi ya asilimia 5 ya uchumi wa nchi yetu. Lengo ni kuhakikisha kwamba sekta ya madini inachangia asilimia 10 ifikapo mwaka 2025,’’ alisema Biteko.

Mojawapo ya miradi ambayo ilikaguliwa na waziri huyo katika ziara yake ni ujenzi wa Kanda maalumu ya uwekezaji 'Special Economic Investment Zone' ambao utasimamiwa na Mamlaka ya ukanda maalumu wa Uwekezaji (EPZA) na Halmashauri ya Mji wa Geita.

Pia alitembelea miradi mingine ya kimkakati inayofadhiliwa na GGML, ikiwemo ujenzi wa Soko Kuu la Geita Mjini na soko la Katundu. 

Aidha, Makamu wa Rais anayeshughulikia Maendeleo Endelevu katika Kampuni ya GGML, Simon Shayo alisema utekelezaji wa miradi ambayo imetembelewa na waziri Biteko ni sehemu ya mpango wa mwaka 2018/19 unaoenda sambamba na mojawapo ya tunu za kampuni hiyo inayoelekeza kwamba jamii inayozunguka shughuli zake sharti ifaidike kwa uwepo wake.

Alisema GGML ambayo ni sawa na kampuni-raia inawajibika ipasavyo kwa jamii kwani hutumia Sh bilioni 9.2 kila mwaka kugharimia miradi ya jamii katika mkoa wa Geita na kuifanya kampuni hiyo kuwa ya kipekee kutokana na mchango mkubwa inayotoa kusaidia jamii.

“Kama Kampuni-raia ndani ya Tanzania, GGML iliyoko chini ya AngloGold Ashanti itaendelea kuunga mkono na kusaidia jamii zinazotuzunguka. Utekelezaji wa miradi ya CSR na shughuli zingine kama hizo ni ushahidi wa wazi kwamba kampuni, serikali na jamii zikifanya kazi pamoja zinaweza kuboresha maisha ya watu kupitia uwekezaji endelevu katika miundomuni ya biashara na huduma.

“Tunataka kuona maisha ya mtu wa kawaida katika jamii yetu yakiwa bora zaidi kupitia uwekezaji endelevu wa Kampuni yetu”, alisema.

Alisema katika kipindi cha mwaka 2018, GGML iliwezesha utekelezwaji wa miradi kadhaa kupitia mpango wake wa kuwekeza katika jamii. 

“Miradi hii inajumuisha; uwekaji wa taa za barabarani katika mji wa Geita, ujenzi wa kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti, ujenzi wa soko la kisasa Geita mjini, umaliziaji wa majengo zaidi ya 600 ya afya na elimu na ujenzi kamili wa shule tatu mpya na vituo vya afya vinne.

“Pia GGML imetenga kiasi cha Sh bilioni 18 kwa ajili ya miradi mingine kama hiyo katika kipindi cha kati ya mwaka 2019/20 na 2020/21.
Share:

Jobs at AMREF Health Africa Tanzania – Various Posts MBEYA and DSM

Overview Amref Health Africa is an independent, non-profit, non-governmental organization (NGO) whose mission is “to improve the health of people by partnering with and empowering communities and strengthening health systems”. Amref Health Africa has over 1000 employees throughout Africa with its headquarters in Nairobi, Kenya. Amref Health Africa has offices in Tanzania, Ethiopia, Kenya, Uganda, and South Africa,… Read More »

The post Jobs at AMREF Health Africa Tanzania – Various Posts MBEYA and DSM appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

BODI YA MAZIWA NA WADAU KUWEKA MIKAKATI YA KUZALISHA MAZIWA YA KUTOSHA NCHINI


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Luhaga Mpina akizungumza na wandishi wa habari na wadau wa maziwa wakati wa kilele cha wiki ya maziwa jijini Dodoma.
Sehemu ya Wadau wa maziwa wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Luhaga Mpina wakati wa kujadili mambo mbalimbali ya sekta ya maziwa katika wiki ya maziwa ambayo kitaifa imefanyika jijini Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe Patrobas Katambi,aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma akizungumza na wadau wa maziwa wakati wa kilele cha wiki ya maziwa jijini Dodoma.
Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa, Dk Sophia Mrote akizungumza na wadau wa bodi ya maziwa wakati wa ufungaji wa kilele cha siku wiki ya maziwa.
Mwenyekiti wa Baraza la wadau ni Bi.Catherine Dangat,akizungumza na wadau wa maziwa wakati wa kilele cha wiki ya maziwa jijini Dodoma.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (wa pili kushoto) akinywa maziwa kuashiria kufunga wiki ya maziwa nchini sambamba na Viongozi wengine akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi (wa tatu kutoka kushoto) na Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa, Dk Sophia Mrote (katikati).
..............................................................................................
Na. Mwandishi wetu, Dodoma
SERIKALI imeitaka Bodi ya Maziwa na Wadau wote wa maziwa kuweka mkakati wa pamoja wa kuhakikisha ndani ya miaka miwili ijayo Tanzania inazalisha maziwa ya kutosha ili kusiwe na haja ya kuagiza maziwa nje Nchi.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina leo jijini Dodoma wakati akihitimisha wiki ya Maziwa duniani ambapo ametumia nafasi hiyo kuwataka wenye viwanda vya kusindika maziwa kuongeza uzalishaji zaidi.

Mhe. Mpina amesema kiwango cha kunywa maziwa kwa watanzania kinapaswa kuwa Tani 200 lakini hadi sasa kiwango kinachonyweka ni tani 54 hivyo kuwataka watanzania kuongeza unywaji wa maziwa kwani husaidia kuboresha kinga za mwili na kukuza ubongo.

Mhe. Mpina amesema kuwa ili kuhakikisha uzalishaji wa maziwa unaongeza serikali imewaunganisha wawekezaji wa maziwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) ili waweze kupatiwa mifugo sambamba pia na kutoa msamaha wa kodi kwenye sekta hiyo.

" Ndugu zangu ni muda sasa wa kuhamasisha unywaji wa maziwa nchini kwani Maziwa ni mlo kamili hasa katika kuimarisha mifupa na kuweka ubongo sawa, na yana viini lishe vya kuimarisha pia kinga za mwili”, amesisitiza Mhe. Mpina.

Aidha Mhe. Mpina ameweka wazi kuwa Tanzania ni Nchi ya pili kwa kuwa na Ng'ombe wengi nyuma ya Ethiopia kuwa Tanzania ina Ng'ombe Milioni 33 lakini Ng'ombe wanaozalisha maziwa ni Milioni 1.9 na kiwango cha maziwa kinachozalishwa ni Bilioni tatu ambacho ni kidogo kulinga na mifugo tuliyinayo.

Mhe. Mpina amesema kwa sasa kuna programu ya kuhamasisha unywaji wa maziwa mashuleni kwa baadhi ya mikoa na kusisitiza sasa ni wakati wa kila mkoa kuweka mkakati wa kuhimiza unywaji wa maziwa kwenye kila shule ndani ya mikoa yao.

Pia Mhe. Mpina ametoa wito kwa wawekezaji nchini kutumia fursa ya kuwekeza kwenye usindikaji wa maziwa kwani viwanda vilivyopo kwa sasa vinazalisha asilimia 23 tu ya maziwa na vipo 99.

Mhe. Mpina amehitimisha kwa kuelekeza Halmashauri zote nchini kuzingatia bei elekezi ya chanjo ya mifugo na atakayekaidi hatua kali za kisheria na kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake

Naye Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa, Dk Sophia Mrote amesema wiki ya Maziwa imekua ya manufaa sana kwani wiki hii waligawa Lita 1650 kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma.

Dkt. Mrote amesema kuwa ndani ya wiki hiyo ya maziwa walikutana wadau wote wa maziwa na kujadili mambo mbalimbali yatakayoweza kuivusha sekta hiyo ili kufikia hatua ya kuzalisha maziwa mengi na kukuza soko hilo hadi nje ya mipaka ya Nchi.


Share:

NCCR Mageuzi kutoa ratiba ya uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Madiwani Wiki Ijayo

Baada ya CHADEMA kuwataka watangaza nia ya kugombea nafasi ya Urais ndani ya chama hicho wajitokeze, NCCR Mageuzi nao wamesema kuwa wanatarajia kutoa ratiba ya uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Madiwani wiki ijayo, na kuiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutenda haki katika uchaguzi ujao.

Pia, chama hicho kimefungua milango kwa chama chochote cha siasa nchini, ambacho kipo tayari kushirikiana ili kuiondoa Serikali ya Chama cha Mapinduzi madarakani.

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alibainisha hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma.

Mbatia alisema, tayari ameshamwagiza Katibu Mkuu wa chama hicho kutoa ratiba ya uteuzi wa wagombea ndani ya chama mapema wiki ijayo.

“Nitoe wito kwa vijana na wale wote wenye sifa, kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali, katika uchaguzi huu, nafasi za urais Tanzania bara na Zanzibar, ubunge, wawakilishi pamoja na zile za udiwani,” alifafanua Mbatia.

Alisema, katika uchaguzi mkuu mwaka huu, chama hicho kipo tayari kushirikiana na vyama vingine vya siasa kwa maslahi ya taifa.
 
“Sisi tupo tayari kushirikiana na chama chochote kile cha siasa kwa maslahi ya mama Tanzania, kwani hata salamu yetu inasema kwa pamoja tutashinda,” alisema Mbatia.


Share:

Kinana amuomba radhi Rais Magufuli kutokana na kauli zake

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Abdulrahaman Kinana, amemwomba msamaha hadharani Mwenyekiti wa CCM, Taifa, Dk. John Magufuli.

Kiongozi huyo ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa CCM wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne, alitangaza hadharani kuomba msamaha huo kwa makosa aliyoyatenda kipindi chake cha uongozi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana, Kinana alisema akiwa kiongozi anaamini kuwa yapo mambo aliyoyafanya ambayo yaliwakwaza viongozi wengine akiwamo Mwenyekiti wa CCM, Dk. John Magufuli, ambaye ni Rais wa Tanzania na anaamini atamsamehe.

“Naamini ilifika wakati nikakereka na kusema maneno ambayo yanaweza kuwa siyo mazuri, nimekaa na kutafakari sasa, namuomba radhi Mwenyekiti wa CCM, Magufuli,” alisema Kinana na kuongeza:

“Kama kiongozi ni kweli naamini ilifikia hatua nikatofautiana na wenzangu ama niliwakera wenzangu na pia, hata kiongozi wangu, Mwenyekiti wa Chama, kiukweli ninamwomba radhi.”

Akiwa Arusha, Kinana pia alikutana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Zelote Steven na Katibu wa Mkoa wa huo, Mussa Matoroka na kuwaeleza kuwa pamoja na kustaafu, ataendelea kutoa ushirikiano wa hali na mali ndani na nje ya chama chake.

“Mimi kwa sasa nimestaafu uongozi, ninamshukuru Mungu na ninaendelea kujifunza, kusoma vitabu na kufanya mazoezi na niko tayari kuendelea kutoa mchango wangu wa hali na mali ndani na nje ya chama,” alisema.

Desemba 13, mwaka jana, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), iliagiza makada watatu wa chama hicho akiwamo Kinana, waitwe na wahojiwe na Kamati ya Maadili na Usalama, baada ya kutuhumiwa kwa makosa ya kufanya mambo kinyume na taratibu za chama.

Kamati Kuu, iliwaadhibu viongozi hao na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Memba, kufukuzwa uanachama kwa kukiuka maadili ya chama hicho.

Kadhalika, Makamba alisamehewa huku Kinana akipewa barua ya onyo ikiwamo kuwa chini ya uangalizi kwa miezi 18 na kuzuiliwa kujihusisha kugombea nafasi yoyote ndani ya chama hicho.


Share:

LIVE: Rais Magufuli Mgeni Rasmi Katika Mkutano Mkuu Wa Uchaguzi Wa Chama Cha Walimu Tanzania

LIVE:  Rais Magufuli Mgeni Rasmi Katika Mkutano Mkuu Wa Uchaguzi Wa Chama Cha Walimu Tanzania


Share:

Trump ashtakiwa kuhusiana na mashambulizi ya polisi dhidi ya waandamanaji

Makundi ya kutetea haki za binadamu nchini Marekani yamewasilisha kesi dhidi ya rais Donald Trump baada ya vikosi vya usalama kuwarushia mabomu ya moshi waandamanaji waliokuwa wakiandamana kwa amani nje ya Ikulu ya White House. 

Umoja wa Uhuru wa Raia wa Marekani, ACLU pamoja na makundi mengine, yalimshtumu rais huyo na maafisa wakuu serikalini kwa kukiuka haki za waandamanaji hao waliokuwa wakiendesha kampeni inayojulikana kama maisha ya watu weusi ni muhimu pamoja na waandamanaji wengine wa kibinafsi.

 Mkurugenzi wa masuala ya kisheria katika umoja huo wa ACLU Scott Michelman amesema kuwa matamshi ya ''kiuhalifu'' ya Trump dhidi ya waandamanaji hao kwasababu anatofautiana na maoni yao yanatikisa msingi wa mpangilio wa kikatiba nchini humo. 

Waandamanaji hao wamekuwa wakifanya maandamano nchini humo katika siku za hivi karibuni kuelezea kughadhabishwa kwao na kifo cha Mmarekani mweusi George Floyd mikononi mwa polisi katika jimbo la Minnesota.

-DW


Share:

Aliyekuwa Mtendaji Mkuu Wa MSD Na Mwenzake Kufikishwa Mahakamani Leo




Share:

Tufanye mambo gani ili tuweze kunufaika na maendeleo ya kiteknolojia?

Nchini Tanzania, kama ilivyo katika maeneo mengine duniani teknolojia imeleta maendeleo na mabadiliko makubwa kwenye jamii.

Hakuna shaka yoyote kwamba teknolojia imebadili namna na kasi ya mawasiliano yetu ambayo yamepitia hatua mbalimbali kuanzia barua posta, simu za mezani na sasa kidijitali.

Katika miezi ya karibuni gonjwa la korona limewavuta watu wengi zaidi kutumia mbinu za kidijitali si tu kuwasiliana bali hata kwenye kufanya malipo na kupata burudani.

Tukitazama mbele yapo mambo mbalimbali tunayoweza kufanya kuhakikisha kwamba sote tunafaidi matunda ya teknolojia na uchumi wa kidijitali.

Jambo mojawapo ni kuhakikisha huduma ya fedha kidijitali inapatikana kwa watu wengi zaidi.

Huduma ya namna hii ni muhimu katika kukuza uchumi, kupanua wigo wa mfumo rasmi wa fedha na ni njia rahisi kufanya malipo, kutuma na kupokea fedha.

Kampuni za simu nchini Tanzania zimechangia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha tunanufaika na teknolojia. Kampuni kama Tigo Tanzania kupitia huduma yake ya Tigo Pesa ni moja ya wadau wanaohakikisha hilo.

Ubunifu pia ni muhimu kadiri mahitaji na teknolojia inavyobadilika. Ubunifu kama huduma ya Ujanja Ni kutoka Tigo kwa mfano inawapa wateja wake vifurushi vya intaneti na dakika katika bei wanazomudu.

Tuendelee kuwa wabunifu katika zama hizi za teknolojia ili tuzidi kuvuna matunda yake.




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa June 5



















Share:

Tumefanya Maboresho Kwenye App Yetu ya Mpekuzi Ili Kukuwezesha Kupata Habari zetu Haraka hasa Wakati huu wa janga la Corona

Tumefanya maboresho katika App yetu ya MPEKUZI ili kuendana na changamoto ya sasa ya janga la Corona inayoikumba dunia Nzima

Usikubali kupitwa na taarifa muhimu zinazoendelea hapa nchini na Duniani  kwa Ujumla . Tumejipanga vizuri sana kukupatia taarifa sahihi na kwa wakati.

👉1. Tumebadili muonekano na kuufanya kuwa mzuri zaidi
👉2. Kila habari tunayoweka kuanzia sasa utapata notification kwenye simu yako 
👉3. Habari zote kwa sasa zinafika kwa haraka kwenye simu yako kuliko ilivyokuwa hapo awali

KUMBUKA: App yetu ni BURE. Unachotakiwa kukifanya ni kuingia Playstore na kupakua MPEKUZI APP

Kama tayari unayo, basi Ingia Playstore kwa ajili ya kupata UPDATE hii ya Toleo Jipya

Tumekurahisishia, Unaweza pia ...<<KU BOFYA HAPA>> Kupata toleo hili Bure Kabisa


Share:

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.


Share:

Thursday, 4 June 2020

HATIMAYE KINANA AMUOMBA RADHI MAGUFULI



Baada ya kimya cha muda mrefu hatimaye katibu mkuu mstaafu wa chama cha mapinduzi Comrade Abdulrahaman Kinana amejitokeza hadharani na kumuomba radhi Mwenyekiti wa Chama ChaMapinduzi taifa Dkt. John Pombe Magufuli kwa matukio mbalimbali yaliyojitokeza baada ya kung’atuka katika uongozi chama hicho.

Kinana pia amewaomba radhi Watanzania na wanachama wa CCM aliowakwaza kwa kitendo kilichotokea.

Awali akizungumzia adhabu aliyopewa na Chama Kinana amekiri kutokea kwa jambo hilo na kudai kuwa kama binadamu alighafilika na kudai kuwa akiwa ni mkongwe katika chama hicho adhabu ni utaratibu uliopo katika chama chochote kwa kiongozi au mwanachama anapokosea.

Wakati huo huo Komrade Kinana ametembea ofisi za CCM mkoa wa Arusha na kuzungumza na mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Arusha Zelothe Stephen Zelothe.

Kinana akiwa na baadhi ya viongozi wakongwe wa chama hicho walipewa adhabu hiyo baada ya mazungumzo yao ya simu kunaswa wakimteta rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii hali iliyosababisha uongozi wa CCM kuwaita na kuwahoji, viongozi hao wakiwemo wastaafu na waliopo madarakani.

Tangu sakata hilo litokee Katibu mkuu huyo mstaafu wa CCM Abdulrahamani Kinana hakuwahi kusikika katika vyombo vya habari wala mitandao ya kijamii kuzungumzia sakata hilo.
Share:

DC Mwanga Aongoza Mazishi Ya aliyekuwa Mpigapicha wa Waziri Mkuu Chris Mfinanga

MKUU wa Wilaya ya Mwanga, Bw. Tom Apson ameongoza mazishi ya aliyekuwa Mpigapicha wa Waziri Mkuu, Bw. Chris Mfinanga yaliyofanyika kwenya kijiji cha Mangio, Vuchama, wilayani humo.

Akizungumza na waombolezaji kijijini hapo jana (Jumatano, Juni 3, 2020), Mkuu huyo wa Wilaya ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bibi Anna Mgwira alisema Chris Mfinanga alikuwa mtu aliyejaa upendo ndiyo maana wengi wanahuzunishwa na kifo chake.

“Chris alikuwa mtu mcheshi na mwenye upendo, alisaidia wengi lakini tusisahau kwamba Mungu ndiye mtoa riziki. Msikate tamaa kwa sababu Mungu yupo na alimwezesha Chris na ndiyo maana aliweza kuwasaidia wengine na hata kuwasomesha watoto wenu.”

“Ninawasihi muamini kuwa Yesu yupo na kwake kuna faraja. Amini Yesu yupo na usiamini katika mganga wa kienyeji au ushirikina. Tuache ramli, tumtegemee Mungu nasi tutapata faraja,” alisisitiza.

Mapema, akiongoza ibada hiyo, Mchungaji Kiongozi wa KKKT Usharika wa Vuchama, Bill Graham Msangi aliwataka waombolezaji waweke mambo yao sawa na Mungu wao pamoja na majirani wanaoishi nao.

Akitoa mahubiri kutoka kitabu cha Ufunuo wa Yohana (14:13), Mchungaji Msangi alisema watu wanaomwamini Kristo wana heri kwa sababu wanapoaga dunia ni sawa na watu wanaoenda kupumzika baada ya taabu zao hapa duniani. “Wanaokufa katika Bwana wanaenda kupumzika baada ya taabu zao. Wana heri sababu matendo yao yanafuatana nao.”

“Kama wewe ni mchawi au mpiga ramli na kazi yako ni kuchonganisha watu, au wewe ni kibaka au mfitini, je hayo matendo yako utaenda nayo wapi? Kule kwenye pumziko siyo kwao watu wa aina hiyo,” alisema.

“Neno la Mungu limesema; bali wao wasioamini, waongo wote, wachukiao na wezi wote na waabuduo sanamu, sehemu yao ni kwenye ziwa la moto ambao hata mende hawaungui. Hata uwe tajiri kiasi gani, au uwe mzuri kiasi gani au uwe baunsa, hautaweza kuzuia kuingia kwenye jehanamu ya moto eti kwa sababu ya ubaunsa wako.”

“Tunapaswa tujiandae kwa sababu siku ikifika, Mungu haatangalia uzuri ulionao. Yeye Mungu ni mzuri kuliko huo uzuri wako. Shetani alikuwa mzuri sana lakini alipoasi alifukuzwa.”

Aliwasihi wafiwa na wakazi wa kijiji hicho hao wawe na umoja ili amani iweze kutawala.   “Umoja ukae miongoni mwa familia, ukae miongoni mwa kaya nyingine na wanavijiji wote. Tukiishi kwa namna hiyo, amani itatawala kwa sehemu kubwa.”

Naye Padre Japhet Njaule wa Parokia ya Vuchama ambaye aliongoza mazishi ya Baba yake Chris Mei 21, 2020, aliwataka waombolezaji wamtumaini Mungu na waishi kwa kujiandaa na kuwa tayari wakati wote.

“Sisi sote ni mali ya Bwana. Tuishi leo na sasa kana kwamba ni saa hii tunaondoka na wala tusiwaze kuhusu kesho yetu. Tukumbuke kuwa Mungu ana mpango na maisha ya kila mmoja wetu,” alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Fadhili Liwaka aliwataka wanafamilia wapate faraja kutoka kwa Mung una wala wasiumizwe na msiba wa Chris. “Tusione ajabu ya msiba huu kwa sababu hili ni jaribu la moto na Mungu anatukumbusha juu ya kuzaliwa, kuishi na kufa. Hakuna binadamu ambaye anaweza kukwepa kifo na hakuna mahali mapenzi ya mwanadamu yanaweza kuzuia kifo cha yule unayempenda.”

Alisema: “Msiba unapotokea, unatukumbusha kuwa tutarejea kwa Mungu, pia utakuja kutuunganisha kama ndugu na kutujulisha kuwa hii neema ya Mungu na si jambo la kibinadamu na tatu unatukumbusha juu ya kujenga, amani, utulivu na kukubaliana na matokeo.”

Naye Baba mdogo wa marehemu, Alhaj Mzee Yusufu Mfinanga aliwashukuru madaktari na wauguzi waliomhudumia Chris wakati akipatiwa matibabu. Pia aliwashukuru ndugu, jamaa, marafiki, majirani na wafanyakazi wenzake kwa ushirikiano mkubwa waliounesha. “Ushirikiano huo ni dalili tosha kwamba Chris alikuwa akiishi vizuri na watu.”

(mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger