Monday, 6 April 2020

Takukuru Dodoma Yaokoa Tsh.297,115,474 Na Kushikilia Magari Matatu




Share:

Sekta mbalimbali zinavyoshirikiana katika kupambana na Coronavirus

Wote kote duniani hivi sasa wanapambana na tatizo la ugonjwa wa Coronavirus. Serikali zote barani Afrika kwa namna mbalimbali zinapambana kuhakikisha maambukizi hayasambai.

Tanzania nako hali ni hiyo hiyo. Hatua mbalimbali zimechukuliwa kupunguza mikusanyiko mfano kufunga mashule na kuzuia mikutano ya hadhara na michezo. Hata watu binafsi nao wanabadili mwenendo wao wa maisha kuwa kupunguza idadi ya watu wanaokutana nao.

Sekta ya biashara nayo vivyo hivyo. Baadhi ya hoteli zimesimamisha huduma kwa muda kupunguza uwezekano wa maambukizi huku sekta ya kilimo ikizidisha nguvu kuhakikisha chakula kinapatikana. Ama kwa hakika, ugonjwa huu umeonyesha namna sekta mbalimbali zimejiunga pamoja kukabiliana na adui na uzoefu huu utasaidia sana ziku zijazo hasa katika kufanya maamuzi ya kijamii na kibiashara.

Kwa mfano inafahamika wazi kwamba kampuni ya Tigo nchini Tanzania iko katika hatua za kuorodhesha hisa zake katika Soko la Hisa la Dar es Salaam baadaye mwaka huu jambo ambalo lingewezesha umma kununua hisa hizo, swali linabaki kwamba, mlipuko huu wa ugonjwa huu utalazimu kuchelewa kwa hatua hiyo chanya kwa sekta ya mawasiliano ya simu nchini Tanzania?

Wataalamu wa uchumi na biashara wanaeleza kuwa zoezi hilo huleta pamoja wadau katika mikutano mingi kulijadili kabla ya kukamilisha na kuongeza iwapo litacheleweshwa kutokana na janga hili vikao vya wadau kukutana uso kwa uso havitakuwepo msimu huu.

Nyakati hizi za sintofahamu tunapata faraja kwa habari chanya kuhusu tunapoelekea kama nchi na dunia nzima. Hata hivyo ni wakati sahihi pia wa kutofanya yale ambayo yanaweza kusubiri mpaka wakati sahihi lakini lengo iwe ni kusaidia umma.


Share:

Applications For admission into higher degrees academic year-2020/2021

Applications For admission into higher degrees academic year-2020/2021 Applications are hereby invited for admission into Higher Degrees at Sokoine University of Agriculture (SUA) for the academic year 2020/2021. Candidates for Postgraduate Diploma, Master and PhD Degree programmes with course work are admitted and registered  once every year for an academic year that starts in October of each year. Candidates for Master… Read More »

The post Applications For admission into higher degrees academic year-2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Vacancies at Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC) and Marine Services  Company Limited (MSCL)

Job Vacancies at Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC) and Marine Services  Company Limited (MSCL)   PRESIDENT’S OFFICE  PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT  Ref.No.EA.7/96/01/K/180 31st March, 2020  VACANCIES ANNOUNCEMENT- RE-ADVERTISED On behalf of Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC) and Marine Services Company Limited (MSCL), Public Service Recruitment Secretariat invites dynamic and  suitably qualified Tanzanians to fill 3 vacant posts.    1.0… Read More »

The post Job Vacancies at Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC) and Marine Services  Company Limited (MSCL) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TANGAZO: JE,UNAHITAJ PESA CHAP CHAP..,JIUNGE NA FREEMASON BILA KAFARA




KARIBU FREEMASONS.
Freemasons ni chama huru kinachotoa utajiri bila masharti ya kumwaga damu wala kutoa kafala.
Jiunge nasi upate upate Mali na umaarufu kaitka nyanja zifuatazo.
1.Katika kilimo na ufugaji
2Biashara ya aina yoyote
3.Masomo (Ngazi zote)
4.Music
5.Sanaa n.k
Watu wengi wamefanikiwa unasubiri jiunge leo ubadilishe maisha yako.
Wasiliana na wakala wetu MKUU kwa namba ..
+255 762 206 804
Popote ulipo.
Share:

TANGAZO: KUTANA NA SHEIKH NASORO ,AMBAE ANATATUA NA KUTIBU MATATIZO YAKO YOTE



SHEIKH NASSORO

GASERA Dawa ya MVUTO wa Mapenzi,  humvuta mke/mke , mchumba alie kuacha atarudi ndani ya masaa *MATATU* *TU*

Atatekeleza ahadi aliyokuahidi,  mfunge mpenzi wako asiwe na mtu mwingine kama alikuahidi kukupa pesa, kukufungulia biashara,  kukunulia gari,  kama alikuahidi kukuoa atatimiza haraka sana .

 *SHEIKH* *NASSORO* . Hutoa pete ya BAHATI,  kusafisha nyota,  kutafsri ndoto, kupata pete ya bahati na utajiri usiokuwa na mashariti ,  kurudisha mali iliyopotea/Kuibiwa au kudhulumiwa,  kurudishwa kazini na kupata kazi kwa haraka,  mfanye boss wako akuamini kwa kila jambo. Katika ofisi unayofanyia kazi.


 *H5* *POWER* Ni dawa bora ya nguvu za kiume,  huimalisha misuli iliyolegea dawa ni mchanganyiko wa dawa za Congo na Tanzania,  huongeza maumbile kwa wakati itakufanya itakufanya urudie tena la ndoa mara nne bila kuchoka/Hamu kuisha.
Tumia uone mafanikio kwa haraka.


 *HUDUMA HII UTAIPATA POPOTE *ULIPO NDANI* NA NJE YA NCHI* .
Kwa msaada zaidi wasiliana na SHEIKH NASSORO..
Call/whatassap *+255 759 402 128* ANAPATIKANA *BAGAMOYO* HUDUMA HII UTAIPATA POPOTE ULIPO.
Share:

Waziri Mkuu wa mpito nchini Libya, Mahmoud Jibril Aliyemng'oa Muammar Gaddafi Afariki Dunia Kwa CORONA

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa mpito nchini Libya, Mahmoud Jibril,  amefariki dunia baada ya kupata maambukizi ya virusi vya Corona.

Imeelezwa kuwa kiongozi huyo wa zamani aliyeongoza mapinduzi yaliyomtoa madarakani marehemu Muammar Gaddafi mwaka 2011 alilazwa hospitali baada ya kupata mshtuko wa moyo na siku tatu baadaye, aligundulika kuwa na ugonjwa wa COVID-19 na kuwekwa karantini.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Ganzouri iliyopo mjini Cairo, Hisham Wagdy, amesema Jibril alifikishwa hospitalini hapo Machi 21, 2020,  na alithibitishwa kuwa na virusi hivyo siku chache baadaye.

Ameeleza kuwa kiongozi huyo alikuwa akiendelea vizuri lakini hali yake ilibadilika ghafla na kusababisha kifo chake.


Share:

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yakabidhiwa Magari 12 Kwa Ajili ya Maandalizi Ya Uchaguzi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama amekabidhi magari 12 kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ambayo ni sehemu ya magari 20 yalionunuliwa na tume ikiwa ni maandalizi ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi magari hayo, Aprili 4,2020 Mhagama amesema Serikali itahakikisha kwamba NEC inawezeshwa kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba na Sheria ili iweze kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki.

“Kwetu sisi kama Serikali wajibu wetu wa kwanza ni kuhakikisha kwamba Tume haikwami katika kutekeleza majukumu yake, hata fedha zinazohitajika katika shughuli zote za uchaguzi zinatengwa kwenye mfuko mkuu wa Serikali,” amesema Mhagama.

Mhagama ameipongeza NEC kwa weledi katika utendaji kazi na kusema kwamba msingi wa uhuru wa Tume uliowekwa na Ibara ya 74 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 utaendelea kuheshimiwa na Serikali.

“Nchi kama Malawi na nchi nyingine zinakuja kujifunza kwenye Tume hii, nakupongeza sana Mwenyekiti (wa Tume) na wafanyakazi wote. Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ametamka kwamba mwaka huu tuna uchaguzi na ametamka kwamba uchaguzi huo lazima uwe huru na haki. Magari haya 12 mmepata, mtapata magari mengine nane (8) na sio magari tu bali vifaa vyote vya uchaguzi vimeshafikia hatua nzuri ya manunuzi, fedha zimeshatengwa,” amesema Mhagama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa (NEC) Jaji Semistocles Kaijage ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuweka mazingira mazuri kwa Tume ili iweze kutekeleza majukumu yake ya Kikatiba na Kisheria.



Share:

Madson property limited, Inakuletea mkopo nafuu kabisa wa viwanja na mashamba usio kuwa na riba wala dhamana yoyote ile

Madson property limited, Inakuletea mkopo nafuu kabisa wa viwanja na mashamba usio kuwa na riba wala dhamana yoyote ile.
 
*Viwanja vyetu vipo maeneo yafuatayo;

-Kigamboni Gezaulole bei 15,000 kwa Sqm

-Kigamboni mwembe mdogo bei 12,000 kwa Sqm

-Mapinga bei 14,000 kwa Sqm

-Goba njia nne bei 30,000 kwa Sqm

-Goba kulangwa bei 35,000 kwa Sqm

-Goba Mtambani bei 37,000 kwa Sqm

-Goba mpakani bei 32,000 kwa Sqm

-Madale Atlas bei 35,000 kwa Sqm

-Madale flamingo bei 40,000 kwa Sqm

-Bunju "B" njia ya mabwepande bei 25,000 kwa Sqm

-Mabwepande center bei 20,000 kwa Sqm

-Vigwaza mashamba bei 2,000,000 kwa heka moja

NB: Viwanja vyetu vyote vimepimwa kwa usahihi kabisa, Mteja atakabidhiwa hati miliki ya kiwanja chake husika mara tu baada ya kukamilisha malipo husika.

*Ofisi zetu zipo Mwenge tower ghorofa ya tano (5th floor) tupo opposite na Mlimani city mall
 .
Tupigie: 0767358229


Share:

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Jonhson alazwa hospitali akionyesha dalili za virusi vya corona

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amelazwa hospitalini ili kufanyiwa vipimo vya virusi vya corona, siku 10 baada ya kukutwa na virusi vya ugonjwa huo, ofisi yake ya Downing Street imesema.

Alikimbizwa katika hospitali moja ya mjini London siku ya Jumapili akionyesha dalili za virusi hivyo ikiwemo kiwango cha juu cha joto mwilini. Imedaiwa kuwa hatua hiyo ya tahadhari ilichukuliwa kutokana na ushauri wa daktari wake.

Waziri mkuu bado ndie msimamizi wa serikali, lakini waziri wa maswala ya kigeni nchini humo anatarajiwa kuongoza mkutano wa virusi vya corona siku ya Jumatatu.

Hatua hiyo inajiri baada ya malkia Elizabeth kulihutubia taifa akisema kwamba Uingereza itafanikiwa katika vita vyake dhidi ya mlipuko wa virusi hivyo.

Katika hotuba isio ya kawaida , mfalme huyo aliwashukuru raia kwa kufuata maelezo ya serikali kusalia nyumbani huku akiwapongeza wale waliojitolea kuwasaidia wengine.

Pia aliwashukuru wafanyakazi muhimu akisema kuwa kila saa la kazi linazidi kuirejesha Uingereza katika hali yake ya kawaida.

Hotuba hiyo inajiri huku idadi ya watu waliofariki kutokana na virusi hivyo nchini Uingereza ikipanda na kufikia 4,934.

Akizungumza katika jumba la kifalme la Windsor, malkia huyo alisema kwamba tumekumbwa na changamoto nyingi katika siku za nyuma lakini hii ni tofauti.

Aliongezea kwamba wakati huu tutaungana na mataifa mengine duniani kwa kutumia hatua za kisayansi zilizopigwa ili kujiponya. tutafanikiwa na kwamba ufanisi huo utakuwa wa kila mtu.

-BBC


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu April 6























Share:

Sunday, 5 April 2020

Wenye Virusi vya Corona Nchini Kenya Wafika 142

Kenya imethibitisha kuwa na wagonjwa wapya 16 wa corona, baada ya kuwafanyia vipimo watu 530.

Hadi sasa Kenya imefikisha idadi ya watu 142 wenye maambukizi ya Corona.

Wizara ya afya nchini Kenya imetaarifu kuwa katika visa vipya 16, raia wa Kenya ni 15 na mmoja anatokea Nigeria.

Raia 11 kati ya hao wana historia ya kusafiri nje ya nchi ilihali 5 ni raia wa eneo.

Watu 12 ni kutoka mji mkuu wa Kenya Nairobi, wengine watatu wanaishi Mombasa 3 na mmoja kutoka Kilifi.

Waliokutwa na maambukizi mapya ni wennye umri kati ya miaka 22 na 66, wanaume ni tisa na wanawake saba.

Kati ya waliothibitishwa, tisa walikuwa kwenye karantini tayari.

Wizara ya afya pia imeweka wazi kwamba inatengeneza barakoa ambazo zitasambazwa kwa wananchi hivi karibuni.

Wizara ya afya imeeleza kuwa watu watakaokufa kutokana na virusi vya Corona watazikwa ndani ya saa 24 huku watu wa karibu wa familia wasiozidi 15 wakiruhusiwa kuhudhuria mazishi hayo yatakayoandaliwa na Serikali.

-BBC


Share:

Wagonjwa wawili wa corona waongezeka Zanzibar, Sasa Wamefika 7

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetangaza uwepo wa wagonjwa wawili wapya wenye maambukizi ya virusi vya corona visiwani humo na sasa jumla wamefikia saba.

Taarifa ya Waziri Afya Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed imeeleza kuwa wagonjwa hao ni raia wa Tanzania ambao kwa nyakati tofauti waliingia visiwani Zanzibar kutokea mkoani Tanga.

Mohamed amesema watu hao waliingia kupitia bandari ya Mkokotoni mmoja ni mwanaume mwalimu wa shule wa mkoani Tanga aliingia Machi 18 na mwingine ni mfanyakazi wa hoteli (27) alienda Tanga Februari na kurudi Machi 13.

“Wagonjwa wote wanaendelea na matibabu katika kituo cha matibabu ya corona cha Kidimni na hali zao zinaendelea vizuri” imeeleza taarifa ya Mohamed


Share:

Sudan Kusini yathibitisha kisa cha kwanza cha Virusi vya Corona

Sudan Kusini imeripoti kisa chake cha kwanza cha virusi vya Corona. 

Nchi hiyo ni moja ya nchi za mwisho za Afrika kuthibitisha uwepo wa ugonjwa wa COVID 19 ndani ya mipaka yake. 

Akizungumza na waandishi habari mjini Juba makamu wa rais Riek Machar amesema mtu wa kwanza alieambukizwa virusi hivyo ni mwanamke aliye na miaka 29 aliyeingia Sudan Kusini akitokea Uholanzi kupitia Ethiopia tarehe 28 Februari. Bado uraia wake haujatajwa. 

Taarifa kutoka kikosi cha amani cha Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS zinasema mwanamke huyo ni mtumishi wake. 

Machar amesema Wizara ya afya kwa kushirikiana na shirika la afya duniani WHO pamoja na shirika la kudhibiti magonjwa ya kuambukiza wanawafuatilia wote waliokaribiana na mwanamke huyo.

 Sudan Kusini tayari imefunga migawaha, vilabu vya usiku na maduka isipokuwa yale yanayouza vyakula na kuwahimiza watu kuzingatia kanuni za kujitenga.


Share:

Wasafiri kutoka nje ya nchi kupelekwa karantini Hosteli za Magufuli

Serikali imetangaza rasmi kuwa wasafiri wote kutoka nchi zilizoathirika na ugonjwa wa virusi vya Corona, watalazimika kukaa Karantini kwa muda wa siku 14 katika hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es  Salaam maarufu hosteli za Magufuli.

Akizungumza katika hosteli za Magufuli, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema wasafiri hao watafikia katika hosteli za Magufuli ambazo zipo katika eneo la Ubungo Jijini Dar es Salaam.

“Lengo ni kuhakikisha tunadhibiti mienendo ya wasafiri hawa.Tumeona taarifa ambazo zimetoka kule Iringa, kuna baadhi ya wasafiri tuliwaweka hotelini wakatoroka sasa ili kudhibiti mienendo ya wasafiri hawa na kuwalinda Watanzania wengi tumeona kuna ulazima wa kuwaweka sehemu moja ambako kutakuwa na ulinzi wa saa 24 na mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam,Bw. Paul Makonda atasimamia kwa karibu chini ya Wizara ya Afya,” amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy Mwalimu amewataka wananchi kufahamu kuwa wasafiri hao si wagonjwa, bali ni kwa sababu wanatoka kwenye nchi zenye maambukizi yenye virusi vya Corona (Covid-19), hivyo hawapaswi kuchukuliwa kama ni wagonjwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameishukuru Wizara ya Afya kwa namna ambavyo imekuwa ikipambana kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa Corona nchini. "sisi kama mkoa tumejipanga kuhakikisha kwamba watu wote wanaokuja na ambao wapo wanakuwa na afya njema kwa ajili ya kujenga uchumi wa mkoa wetu na Taifa kwa ujumla".

Makonda amewataka Watanzania kufanya kazi na kwamba kuanzia Jumatatu, Aprili 6 atawakamata wazururaji wote wanaozunguka mjini bila kuwa na kazi maalumu watakamatwa kwa kuwa wanasababisha mikusanyiko isiyokuwa na tija.


Share:

FULL POWER , ZATI 50 SULUHISHO LA KUDUMU NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Zati 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Wataalamu Kutoka Wizara Nne Yawasili kwa Mzee Kisangani

Na Issa Mtuwa – Ludewa
Timu ya Wataalamu Tisa kutoka Wizara Nne kwa ajili ya kwenda kumkwamua Mjasiriamali Rueben Mtitu maarufu Mzee Kisangani imewasili mkoani Njombe na kuripoti kwa Katibu Tawala wa Mkoa huo na baadae kuelekea wilayani Ludewa na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya (DC) hiyo
Andrea Tsere.

Ujumbe huo uliwasili mkoani Njombe juzi Aprili 03, 2020 wakitokea maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dodoma, Dar es Salaam na Mbeya.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Prof. Silvester Mpanduji ambae ni Mkurugenzi Mkuu wa SIDO alimueleza DC kuwa Kamati yake ikiwa kwenye eneo la Mradi wa Mzee Kisangani itaainisha masuala mbalimbali ya Kiuchumi, Kibiashara, Kimazingira na Kijamii, huku ikibainisha viashiria hatarishi vinavyoweza kutokea kwenye mradi huo na namna ya kutatua.

Aliongeza kuwa wataalamu hao wako katika maeneo ya fani mbalimbali zitakazo kidhi kumkwamua Mzee Kisangani katika mradi wake kama serikali inavyokusudiwa. Kamati hiyo itaainisha masuala mbalimbali yanayohitaji katika kumsaidia Mzee Kisangani katika upanuzi wa mradi
wake.

Kila mjumbe anajukumu la kufanya na mara baada ya kazi hiyo ripoti ya kazi hiyo itawasilishwa kwa Waziri wa Madini Doto Biteko kwa hatua zaidi.

Kamati hiyo inatekeleza hadidu za rejea zilizotolewa na kikao cha mawaziri kilichokaliwa Machi 30, 2020 katika utekelezaji wa mpango kazi.

Uthubutu na ubunifu wa Mzee Kisangani umepelekea kumshawishi Waziri wa Madini Doto Biteko kuamsha hari ya kumsaidia Mzee Kisangani kutoka hali aliyonayo kibiashara na kufikia ndoto kubwa ya kuwa mfanyabiashara mkubwa huku akibainisha wizara yake kufanya kila linalowezekana kumwezesha kuwa mfanyabiashara mkubwa kupitia zana zake zinazotengenezwa na Madini ya Chuma.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Andrea Tsere, amemshukuru Waziri wa Madini Doto Biteko, kwa maamuzi ya kuundwa kwa timu hii huku akiwapongeza wataalamu hao kwa kuteuliwa kumsaidia Mzee Kisangani.

Ameongeza kuwa wilaya ya Ludewa ina Raslimali Madini za aina mbalimbali yakiwemo Chuma na Makaa ya Mawe huku kilio chake kikiwa ukosefu wa leseni za wachimbaji wadogo huku maeneo makubwa ya uchimbaji yakiwa yanamilikiwa na Shirika la Maendeo ya Taifa (NDC) huku akiwasilisha kilio hicho kwa mmoja wa Wajumbe kutoka (NDC) Dkt. Yohana Mtoni.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger