Monday, 8 July 2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 8 July























Share:

Sunday, 7 July 2019

Isikupite Hii! 👉Naitwa Chief Karim Wa Sultan.....Ni Bingwa Na Mtabiri Wa Nyota

Isikupite hii! 👉Naitwa CHIEF KARIM WA SULTAN Kutoka- TANGA - TANZANIA: Ni Bingwa, Mnajimu na Mtabiri wa Nyota na Matatizo yote ya ndoa/mahusiano.

Natabiri nyota yako, Kung'alisha nyota, Kufungua nyota zako za mafanikio zilizo fungwa  na kusababisha usifanikiwe katika maisha yako, au unajikuta unafanya kazi/biashara unapata hela lakini pesa yako haikai yaani inapita tu katika mikono yako.

Nawezesha  NYOTA, ni UTAJIRI usio na kafara yoyote na ni UTAJIRI unaoendana na nyota yako tu.

Hakika watu wengi wanazidi kufanikiwa na kutimiza ndoto zao , Kulipwa haraka haki zako unazodai, Mvuto wa mapenzi, kumrudisha mpenzi, mme au mke aliyekuacha/kukutelekeza.

 Je unapata wapenzi/wachumba lakini wanakuacha bila kujua sababu? Nitakusaidia!

Kufungua kizazi chako kilichofungwa na kusababisha usipate mimba/mtoto au unashika mimba zinatoka/kuharibika na maumivu makali ya tumbo/chango.

 👉KWA TATIZO LOLOTE  LA KINYOTA WASILIANA NAMI 👉WhatsApp : 0763 103 527
au
👉PIGA SIMU  : 0716 681 318
👉 0688 745 790


NB 👉(KWA MWANAUME YOYOTE MWENYE TATIZO LA KUISHIWA AU KUPUNGUKIWA NGUVU ZA KIUME AU KAMA UMEATHIRIKA NA TATIZO LA KUPIGA PUNYETO TUWASILIANE POPOTE ULIPO)*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾ ✨WABILLAHHI TAWFIQ ASALLAM  ALAIKUM✨ 


Share:

WANACHAMA PSSSF WAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUFUATILIA TAARIFA ZA MICHANGO YAO


Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi  (SACP), David Misiime ambaye ni  mwanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), akipitia taarifa ya michango yake huku akipata usaidizi kutoka Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa Umma wa Mfuko huo, Bi. Eunice Chiume  Julai 7, 2019 wakati alipotembelea banda la PSSSF  kwenye viwanja vya Julius Nyerere (Sabasaba) wakati wa maonesho ya 43 ya biashara ya Kimata ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye viwanja hivyo. 
 Afisa Mwandamizi wa Malipo, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma,(PSSSF), Bi.Nyangi Masalu (kushoto), akimuhudumia mwananchi aliyetembelea banda la PSSSF Julai 7, 2019.
 Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Ftma Elhady, na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo Bw. Abdul Njaidi, wakiwasilkiliza wananchi waliotembelea banda la Mfuko huo Julai 7, 2019.
 Hakika mama ni mama: Afisa Mwandamizi wa Malipo, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF), Bi.Nyangi Masalu (kulia), akimbembeleza kichanga huyu huku mama yake akiwa karibu wakayi Nyangi alipomalzia kumuhudumia mume wa mama huyo aliyetembeela banda la PSSSF.
 Afisa Mwandamizi wa Malipo, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma,(PSSSF), Bi.Nyangi Masalu (kulia), akimsikilzia Mwanachama aliyetembelea banda la Mfuko huo
 Mwnaachama wa PSSSF akimsikliza Afisa wa PSSSF wakati alipofika kwenye banda la Mfuko huo ili kuhudumiwa.
 Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Ftma Elhady, akimsikiliza mwanachama huyu aliyetembelea banda la PSSSF Julai 7, 2019.
Afisa Michango PSSSF Bi. Getrude Athanas (kulia), akimsikiliza mwanachama huyu aliyefika na familia yake kupata taarifa za michango yake
Afisa Mafao PSSSF, Bw. Salvatory Athanas akimsikiliza mwanachama huyu aliyefika kuhudumiwa.
***
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WASTAAFU watarajiwa wa  Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi  wa Umma (PSSSF) wameaswa kujenga utamaduni wa kufuatilia  taarifa za michango yao mara kwa mara ili kujipanga vema wakati wa kustaafu unapowadia, Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa Umma (CMPR), wa Mfuko huo, Bi. Eunice Chiume amesema.

Bi Chiume ameyasema hayo Julai 7, 2019 wakati akiungana na watumishi wenzake wa Mfuko kuhudumia wanachama wanaofika kupata huduma kwenye banda la PSSSF kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam ambapo watu wengi hususan wale wanaotarajia kustaafu wamekuwa wakijitokeza ili kujua taarifa za michango yao.

Wanachama na wananchi wanahamasishwa kutembela banda hilo ili kupata huduma na taarifa mbalimbali kuhusu shughuli za Mfuko ambao umeundwa baada ya kuunganishwa kwa Mifuko minne ya Hifadhi ya Jamii ya GEPF, PSPF, LAPF
na PPF.

Huduma zitolewazo na PSSSF kwenye banda hilo namba 13 ambalo pia linatumiwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), ni pamoja na taarifa za Uhakiki wa wastaafu, taarifa za Pensheni ya Uzee, taarifa za Mafao ya kukosa Ajira, taarifa za Mafao ya Uzazi, taarifa za Dhamana ya Mikopo ya Nyumba na na taarifa za Uwekezaji. Maonesho hayo yaliyoanza Juni 28, 2019 yanatarajiwa kufikia kilele Julai 13, 2019 ambapo Kauli mbiu ya mwaka huu ni "Usindikaji wa Mazao ya Kilimo kwa Maendeleo Endelevu ya Viwanda." 
Share:

SHIRIKA LA RELI TANZANIA TRC KUFUNGA NJIA ZA RELI KWA SAA 72 ILI KUKARABATI RELI YA KATI


Na Grace Semfuko,MAELEZO
Shirika la Reli Tanzania TRC limeanza kukarabati njia ya Reli ya kati ya kutoka Dar Es Salaam mpaka Isaka iliyopo Wilaya ya Kahama Mkoa wa Shinyanga takribani kilomita 970 ili kuimarisha reli hiyo yenye kiwango cha Mitagauge zoezi ambalo lilianza Juni mwaka huu na kutarajia kukamilika mwaka 2020.

Katika Utakabati huo Shirika hilo linatarajia kufunga njia za reli hiyo kwa saa 72 kwa wiki ikiwa ni sawa na siku tatu kwa Wiki kwa muda wa miezi mitano kuanzia Julai hadi Novemba 2019, zoezi zoezi ambalo  kukamilika kwake kutaingiza faida mara dufu ya usafiri huo.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Shirika hilo Masanja Kadogosa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam na kubainisha kuwa kukamilika kwa Reli hiyo kutaongeza mapato ya usafirishaji wa Reli kwa asilimia mia moja.

“Waandishi wa Habari na Watanzania kwa ujumla, TRC sasa tunakuja kuimarisha miundombinu yenu ya Reli, tunafanya hivi kwa kuwa tunafahamu mnahitaji huduma hizi, tunaomba mtuvumilie kwa siku ambazo tutafunga njia hizi”alisema Kadogosa.

Alisema kwa treni za kawaida za mjini (Cummuter Train) za kutoka Kamata kwenda Ubungo na Pugu zitafanya kazi siku za jumatatu hadi Ijumaa huku Treni za kawaida (Ordinary Train) za kutoka Dar Es Salaam kwenda Kigoma, Mwanza na Mpanda zitafanya kazi siku za Jumatatu na Jumatano saa tisa alasiri tu na treni za Deluxe ya kutoka Dar kwenda Kigoma zitakuwepo siku ya Jumanne pekee.

Alibainisha kuwa ukarabati mwingine wa njia ya Reli kutoka Tanga kwenda  Arusha ulianza mapema mwaka huu ambapo njia hiyo itaanza kutumika mwezi Desemba mwaka huu.

“Ndugu zangu wa mikoa ya Kaskazini mtaanza kunufaika na usafiri wa treni ya Abiria kuanzia Desemba mwaka huu, yaani Sikukuu zaKrismas na Mwaka mpya mtaenda nyumbani na Treni ya Abiria ya TRCälisema Kadogosa.

Akizungumzia ujenzi wa Reli ya Standard Gauge inayoendelea kujengwa Nchini Kadogosa alisema kwa awamu ya kwanza kutoka Dar Es Salaam kwenda Morogoro ujenzi huo umefikia asilimia 56.
 


Share:

Viongozi wa dini Watakiwa Kusimamia malezi ya Vijana ili kuhakikisha Taifa linakuwa na watu waliostarabika na kuwa na hofu ya Mungu.

NA SALVATORI NTANDU
Vijana hapa nchini wametakiwa kubadilika na  kuachana na vitendo vinavyomchukiza Mwenyezi Mungu ambavyo ni pamoja matumizi ya dawa za kulevya, wizi, na uasherati,  ambavyo vinaweza kubabisha wakapoteza mwelekeo na kutotimiza malengo yao

Kauli hiyo imetolewa leo  na kiongozi wa Vijana wa Kitaifa wa Jumuiya ya Waislam wa (Ahmadiya) Shekh, Ramadhani Hassani Nauja katika kongamano la siku tatu lijulikanalo kama Ijtemaa ya Khuddam kanda ya kaskazini la mwaka 2019 linalojumuisha washiriki kutoka mikoa saba lililofanyika katika wilaya ya kahama mkoani Shinyanga.

Amesema ipo haja kwa viongozi wa dini kuhakikisha wanawalea vijana katika misingi ya kiimani ambayo itawasaidia kupata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu pamoja na kuwa raia wema katika maeneo wanayoishi.

Amesema vijana ndio nguvu kazi ya taifa hivyo ni budi kwa viongozi wa Dini wakawajengea misingi mizuri ya kumjua Mwenyezi Mungu na kuondokana na vitendo viovu kwani ndio kundi pekee ambalo lipo katika hatari kubwa ya kukumbwa na vishawishi katika ulimwengu huu.

Nae shekeh Musa Issa kutoka visiwani Zanzibar amesema viongozi wadini wapaswa kujikita kutoa elimu ya dini kwa wananchi waliopo vijijini ili kuwasaidia kumjua mungu na kuondokana na matukio ya mauaji  ya vikongongwe na ulawiti na watu wenye ualibo.

Kwa upande wake Shekhe Yusuph Mgeleka kutoka Kahama amesema Kongamano hilo litaweza kuwabadili vijana kifikra na kuwa raia wema kwa kufanya kazi halali ambazo zitaweza kuwapatia vipato na kuongeza nguvu kazi katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Mahdilah Issa na Musa Saidi ni miongoni mwawashiriki  Mafunzo hayo kutoka mikoa ya Tabora na Kagera wamesema mafunzo waliyoyapata yatawawezesha kuwa mabalozi kwa vijana wenzao katika maeneo yao wanayoishi ili kutoa fursa ya vijana wengine.

kongamano hilo limejumuisha vijana zaidi ya 200 kutoka katika mikoa ya Tabora, Mwanza, Kagera, Geita, Simiyu na Mara limeenda sambamba na mashindano ya Kusoma Quan tukufu,mashindano ya mpira wa miguu na shughuli mbalimbali za kijamii katika mji wa kahama na lilianza rasimi siku ya ijumaa na limehitimishwa hii leo.


Share:

VIJANA ZAIDI YA 200 KUTOKA MIKOA SABA TANZANIA WAKUTANA SHINYANGA KWENYE KONGAMANO LA JUMUIYA YA WAISLAM WA AHMADIYYA

Vijana hapa nchini wametakiwa kubadilika na kuachana na vitendo vinavyomchukiza Mwenyezi Mungu ambavyo ni pamoja matumizi ya dawa za kulevya, wizi, na uasherati, ambavyo vinaweza kubabisha wakapoteza mwelekeo na kutotimiza malengo yao.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumapili Julai 7,2019 na Kiongozi wa Vijana wa Kitaifa wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya, Sheikh Ramadhan Hassan Nauja katika kongamano la siku tatu lijulikanalo kama Ijtemaa ya Khuddam Kanda ya Kaskazini la Mwaka 2019 linalojumuisha washiriki kutoka mikoa saba lililofanyika katika wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Sheikh Nauja amesema ipo haja kwa viongozi wa dini kuhakikisha wanawalea vijana katika misingi ya kiimani ambayo itawasaidia kupata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu pamoja na kuwa raia wema katika maeneo wanayoishi.

Amesema vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa hivyo ni budi kwa viongozi wa dini wakawajengea misingi mizuri ya kumjua Mwenyezi Mungu na kuondokana na vitendo viovu kwani ndiyo kundi pekee ambalo lipo katika hatari kubwa ya kukumbwa na vishawishi katika ulimwengu huu.

Naye Sheikh Musa Issa kutoka Visiwani Zanzibar amesema viongozi wa dini wanapaswa kujikita kutoa elimu ya dini kwa wananchi waliopo vijijini ili kuwasaidia kumjua Mungu na kuondokana na matukio ya mauaji ya vikongwe na ulawiti na watu wenye ualbino.

Kwa upande wake, Sheikh Yusuph Mgeleka kutoka Kahama amesema Kongamano hilo litasaidia  kuwabadili vijana kifikra na kuwa raia wema kwa kufanya kazi halali ambazo zitaweza kuwapatia vipato na kuongeza nguvu kazi katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Mahdilah Issa na Musa Saidi ambao ni miongoni mwa washiriki  kongamano hilo kutoka mikoa ya Tabora na Kagera,wamesema mafunzo waliyoyapata yatawawezesha kuwa mabalozi kwa vijana wenzao katika maeneo yao wanayoishi ili kutoa fursa ya vijana wengine.

Kongamano hilo limejumuisha vijana zaidi ya 200 kutoka katika mikoa ya Tabora, Mwanza, Kagera, Geita, Simiyu na Mara limeenda sambamba na mashindano ya Kusoma Quran Tukufu,mashindano ya mpira wa miguu na shughuli mbalimbali za kijamii katika mji wa kahama na lilianza rasimi siku ya Ijumaa na limehitimishwa leo Jumapili.
Na Salvatori Cevin - Malunde1 blog
ANGALIA PICHA
Viongozi wa kitaifa wa Jumuiya ya kiislama ya Ahmadiya wakiomba dua kabla ya kuanza kwa kongamano hilo. Picha zote na Salvatori Cevin - Malunde1 blog
Kiongozi wa Vijana wa Kitaifa wa Jumuiya ya Waislam wa (Ahmadiya) Shekh, Ramadhan Hassani Nauja kushoto akisoma dua katikati ni Sheikh, Musa Issa kutoka Visiwani Zanzibar kulia ni Sheikh Yusuph Mgeleka.
Viongozi mbalimbali wa Kongamano hilo wakiwa wanasikiliza kwa makini mada zinavyowasilishwa.
Shekh Yusuph Mgeleka akiwasilisha mada mbalimbali katika kongamano hilo.
Shekh, Musa Issa kutoka Zanzibar akisoma Quan Tukufu katika kongamano hilo ambalo lilikuwa na mashindano ya kusoma kitabu hicho.
Washiriki wa kongamano hilo la siku tatu liliofanyika mjini Kahama.
Viongozi mbalimbali wa jumuiya ya kiislam ya ahmadiya kutoka mkoa wa shinyanga wakiwa na viogozi wa kitaifa wa jumuiya hiyo.

Share:

Watanzania wamekuwa na mwamko mkubwa katika Michezo; Dkt.Mwakyembe.

Na Shamimu Nyaki –WHUSM
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe ametoa pongezi kwa watanzania kwa kuwa na mwamko mkubwa wa kupenda michezo kuanzia kushiriki,kushangilia pamoja na uhamasishaji ambao umechangia kwa kiasi kikubwa  mafanikio na  maendeleo ya michezo hapa nchini na uwakilishi mzuri nje ya nchi. 

Dkt.Mwakyembe ameyasema hayo leo Jijini Dodoma alipokuwa anamuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluh Hassan katika mashindano ya riadha ya Capital City Marathon ambapo amesema kuwa kwa sasa nchi yetu imeanza kurudi katika ramani ya michezo kutokana na watanzania kushriki kwa wingi katika michezo mbalimbali. 

“Nawapongeza sana Watanzania wamekuwa na ari kubwa sana ya kushirikiki michezo hasa riadha ambayo imetutangaza vyema nje ya nchi,ni matuamini yangu mtaendelea kufanya vizuri zaidi lakini pia na michezo mingine vijana endeleeni kuchezakwa bidii zaidi  kwakua michezo sasa ni chanzo kikubwa cha kipato”amesema Dkt.Mwakyembe. 

Aidha Dkt.Mwakyembe ameongeza kuwa Taifa limekuwa na uwakilishi mzuri katika mchezo wa Soka kwani limepata nafasi ya kushiriki AFCON 2019,kuongezeka kwa timu zitakazoshiriki Klabu Bingwa Afrika ambayo ni Simba na Yanga pamoja na Klabu Mbili zitakazoshiriki Kombe la Shirikisho ambazo ni Azam FC na KMC. 

Katika hatua nyingine Mhe.Waziri Mwakyembe ameiagiza Idara ya Maendeleo ya Michezo kushirikiana na wadau kuwa na utaratibu wa kuandaa orodha ya wadhamini  wanaojitokeza na namna wanavyodhamini mashindano mbalimbali ili kuweka kumbukumbuku vizuri na kutoa ushauri panapowezekana katika kuimarisha Sekta hiyo. 

Kwa upande wake Mratibu wa Mbio hizo Bw.Nsolo Mlozi mbali na kuishukuru Serikali kwa ushirikiano iliyotoa pamoja na washiriki waliojitokeza  ameishauri jamii kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi na kushiriki mashindano mbalimbali ya riadha ili kujenga miili yao kwa kuimarisha afya lakini pia kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza ambayo kwa sasa yamekuwa yakiwatesa wananchi wengi. 

Vilevile Bw.Nsolo ameongeza kuwa Capital City Marathon ilianza na kuwa na idadi ndogo ya washiriki  lakini mwaka huu idadi imeongezeka na kufikia washiriki 2,200 ambao kulingana na miundombinu imara ya Jiji la Dodoma wameweza kukimbia bila kupata changamoto yoyote.

Naye mshindi wa km 21 kwa upande wa wanaume  Bw.Emmanuel Giniki amesema kuwa mchezo wa riadha ni mchezo ambao unahitaji kuwa na mazoezi ya mara kwa mara ili kuweza kufanya vizuri ambapo amewashauri vijana wengi kujitokeza katika mashindano mbalimbali ya riadha yanayotokea ili kupata kipato pamoja na kupata ajira. 

Mbio za Capital City Marathon zinafanyika kwa mara ya pili Jijini Dodoma ambapo mwaka huu zimehusisha mbio za KM 22 Baiskeli,km.21wanawake na wanaume,km 10 wanawake na wanaume pamoja na km 5.


Share:

Rais Magufuli ampa Rais Kenyatta tausi wanne

Rais Magufuli amemzawadia Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ndege aina ya tausi kama kumbukumbu ya uhusiano, urafiki na ujirani mwema baina ya nchi hizo mbili.

Magufuli ametoa zawadi hiyo  Jumamosi Julai 6, 2019 wilayani Chato mkoani Geita na kumpatia Kenyatta aliyekuwa nchini Tanzania kwa ziara binafsi ya siku mbili.

“Nimeguswa sijawahi kugawa tausi kwenye nchi yoyote kwa sababu wana historia ya nchi yetu. Kwa  heshima kubwa na mahusiano  yaliyopo kati ya Tanzania na Kenya, nimekubali na hili nataka kulisema wazi.

“Najua watu wataandika lakini hili limenigusa kutoka moyoni, nitatoa tausi wanne watapelekwa Kenya kwa Kenyatta,” alisema Magufuli huku akitabasamu.



Share:

Serikali Yaikabidhi Mwauwasa Ujenzi Wa Mradi Wa Maji Kwimba

Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa amekabidhi ujenzi wa mradi wa maji wa Shilima Wilayani Kwimba kwa Mamlaka ya Maji Mwanza (MWAUWASA) baada ya Mkandarasi Kampuni ya Palemon Construction Ltd ya Mwanza kushindwa kukamilisha kwa wakati.

Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Shilima na kushuhudiwa na watendaji mbalimbali wa Serikali na mamia ya wananchi wa Shilima na maeneo ya vijiji vya jirani.

Akizungumza kabla ya kukabidhi mradi, Waziri Mbarawa alieleza kwamba ujenzi wake ulianza tangu mwaka 2013 na kwamba ulipaswa kukamilika ndani ya miezi sita lakini hadi sasa mradi huo haujakamilika.

Alisema Serikali iliamua kusitisha mkataba na Mkandarasi ambaye alishindwa kutekeleza ujenzi wa mradi kama ilivyo kwenye makubaliano.

Mara baada ya kuukabidhi mradi huo, Profesa Mbarawa aliiagiza MWAUWASA kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ujenzi unakamilika ndani ya Siku 60 ili kuwaondolea mateso ya muda mrefu wanachi wa maeneo hayo hasa ikizingatiwa kwamba mradi ulipaswa kukamilika tangu mwaka 2013.

“Tunataka wataalam hawa wafanye kazi usiku na mchana na baada ya miezi miwili wananchi wapate maji safi na salama, uwezo tunao, tunaweza kumaliza tatizo la maji hapa kwa muda mfupi sana,” alisema Profesa Mbarawa.

Aliongeza kuwa kuna miradi ipatayo 88 kote nchini ambayo ujenzi wake ulianza kati ya Mwaka 2010 hadi 2015 ambayo ilipaswa kuwa imekwisha kamilika lakini hadi hivi sasa bado inasuasua na huku akiutolea mfano mradi huo wa Shilima.

Alibainisha kwamba Serikali kupitia Wizara ya Maji imeamua kuwa na utaratibu mpya wa kuzikabidhi Mamlaka za Maji miradi ambayo ujenzi wake una changamoto inayosababisha isikamilike kwa wakati.

“Tumeamua kubadilisha utendaji wa Sekta ya Maji, kila mahala tatizo ni maji, hili halikubaliki, tumejipanga na tunadhamira ya dhati kuhakikisha kero hii inakuwa historia kote nchini,” alisema Waziri Mbarawa.

Kuhusu utaratibu huo mpya, Profesa Mbarawa alibainisha kuwa ni wa nchi nzima na kwamba wakandarasi wanaoshindwa kutekeleza miradi waliyokabidhiwa kwa wakati hawatovumiliwa na watanyanganywa na itakabidhiwa kwa Mamlaka za maji kwenye maeneo husika.

“Tumeamua miradi yote yenye changamoto tutaisimamia wenyewe na tutahakikisha inafanya kazi. Wananchi wamechoka kuendelea kuisubiri miradi hii ikamilke, fedha nyingi zinapotea, Serikali haitokubaliana na Mkandarasi anaechelewesha ujenzi wa mradi tayari tumefanya hivi Rungwe na sasa tumefanya hapa Shilima,” alisema Profesa Mbarawa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Anthony Sanga alisema wamepokea agizo hilo la kutekeleza mradi huo ambao umesuasua kwa kipindi kirefu na kwamba wataukamilisha kwa wakati kama ilivyoagizwa.

“Tunaahidi hadi kufikia Septemba 3, 2019 tutakuwa tumeukamilisha mradi kwani itakuwa tayari ni Siku 60 na wananchi wataanza kupata majisafi na salama kutoka Ziwa Victoria,” alisema Mhandisi Sanga.

Aidha, kwa mujibu wa Mhandisi wa Maji, Wakala wa Maji Vijijini Wilaya ya Kwimba, Mhandisi Boaz Pius ni kwamba mradi huo utakapokamilika utahudumia wakazi 16,675 kutoka vijiji vinne ambavyo ni Shilima chenye wakazi 7,526, Mhande chenye wakazi 1,967, Kasang’wa wakazi 2,730 na Kijiji cha Izizimba “A” chenye wakazi wapatao 4,452.

Mhandisi Boas aliongeza kwamba kukamilika kwa mradi huo pia kutaweza kuhudumia vijiji vya Sangu, Gurumwa, Mwalubungwe na Kikubiji, ambapo bomba kuu linapita.


Share:

FILAMU YA 'MIMI SIYO MWEHU' KUTIKISA ZAIDI YA 'LAANA YA MKE'


Unaikumbuka ile Filamu ya Laana ya Mke iliyoigizwa na wasanii kutoka mkoa wa Shinyanga ambayo hivi karibuni ilifanikiwa kushinda Tuzo ya Heshima Filamu Bora yenye maudhui ya kitaifa Kanda ya Ziwa???.

Sasa ni hivi?!! Baada ya Filamu ya Laana ya Mke kutikisa....Wasanii wa Filamu mkoa wa Shinyanga wanakuletea filamu nyingine kali imepewa jina la " MIMI SIYO MWEHU".... Ndiyo!!  Mimi siyo Mwehu ni bonge la filamu yenye tungo zenye manufaa katika jamii zenye kuelimisha, kuonya,kuburudisha zilizojaa mafunzo ya uhalisia wa maisha halisi katika jamii za Kiafrika.

Mwandaaji wa Filamu hiyo, Ibrahim Juma Songoro maarufu 'Songoro Gadafi' ambaye ni Mwenyekiti wa Bongo Movie Shinyanga ameiambia Malunde1 blog kuwa filamu ya 'Mimi Siyo Mwehu' inalenga kuelimisha jamii inayowachukulia watu wasio na kipato,waliochoka kimaisha, kiuchumi na kiafya mawazo yao au ushauri wao haustahili bali ni wendawazimu.

"Mimi Sio Mwehu ni filamu iliyosheheni Misemo ya hekima itakayomfanya mtazamaji asichoke kuitazama katika maisha yake, washiriki wakuu kwenye filamu hii iliyoongozwa na Director Dave Skerah ni Juma Ibrahim Songoro, Goodness Mndeme na Fadhili Mungi".

"Naapa kurudisha heshima ya tasnia ya Filamu Tanzania kwa kuwaletea Filamu zenye tungo zenye manufaa katika jamii kwa lengo la kuelimisha, kuonya na kuburudisha kwa kuangalia uhalisia wa maisha ya jamii zetu za Kiafrika",amesema Songoro.

Amesema Filamu ya 'Mimi Siyo Mwehu' itazinduliwa hivi karibuni na kuwaomba mashabiki wa filamu kujiandaa kupokea Filmu hii yenye ubora wa hali ya juu.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Songoro

Goodness 
Share:

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AWATAKA WANANCHI KUTUNZA VYANZO VYA MAJI,ARIDHISHWA NA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA VYANZO VYA MAJI MUHEZA

MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mark Yona

 KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally akivishwa skafu na vijana wa skauti mara baada ya kuwasili wilayani Muheza.
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo katikati akiwa na viongozi mbalimbali mara baada ya mwenge kuwasili kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Muheza Like Gugu na Mbunge wa Jimbo la Muheza( CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto ni  KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akihamasisha kushiriki kuimba kwa pamoja nyingi mbalimbali za mwenge wakati wakiiusubiri
 MMOJA kati ya wakimbiza Mwenge Kitaifa akiweka mwenge mara baada ya kukimbizwa kwenye miradi mbalimbali
 Mwenge wa Uhuru 2019 ukikimbizwa wilayani Muheza
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kulia akiteta jambo na Mwenyekiti wa Halmashauri Bakari Mhando
 KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally katikati akionyeshwa namna ya utunzaji wa mazingira unavyoifanyika wakati alipotembelea na kukagua mradi wa shughuli za uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji Kijiji cha Shembekeza.
 KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally kushoto akimkabidhi cheki ya Sh.Milioni moja Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbaramo Mussa Salimu ikiwa ni mchango uliotoka Halmashauri kuunga mkono ujenzi wa Hosteli kwenye shule ya Msingi Mbaramo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalumu anayeshuhudia katikati ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia akiwakabidhi zawadi mbalimbali wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2019

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally amewataka wananchi wanaoishi karibu na vyanzo vya maji wilayani Muheza mkoani Tanga kuhakikisha wanavitunza ili viweze kuwa endelevu.

Alitoa kauli hiyo mara baada ya Mwenge wa Uhuru kukagua mradi wa shughuli za uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji ikiwemo kukagua mabanda ya wadau wa mazingira na kupanda miti eneo maalumu lillotengwa Kijiji cha Shembekeza.

Akiwa kwenye eneo hilo kiongozi huyo alionyeshwa kuridhishwa na namna mradi wa uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji ambao umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uharibifu wa vyanzo vya maji.

Alisema kwani Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kutekeleza miradi hiyo kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji hivyo ni muhimu kulindwa na kuendelezwa kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kiongozi huyo alisema suala la upatikanaji wa maji limekubwa na changamoto nyingi ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za serikali huku baadhi ya waka ndarasi wamekuwa wakichukua muda mrefu kukamilika miradi hiyo na hata wengine kukamilisha chini ya kiwango.

“Lakini pia niwaambie kwamba sio jambo jema kufanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji ikiwemo ukulima, ufugaji na kujenga karibu na vyanzo hivyo tushirikiane kuhakikiha tunatunza vyanzo vya maji ili vielendee kumudu kwqa vizazi vya sasa na vijazo”Alisema Kiongozi huyo.

Awali amkizungumza wakati akisoma taarifa ya miradi itakayozinduliwa na mwenge ikiwemo kukaguliwa Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo alisema kwamba miradi yenye thamani ya Bilioni 29.471.7 huku akieleza kwamba mwenge huo umekimbizwa kwenye miradi na shughuli mbalimbali.

Alisema wakati wa mkesha wa mwenge huo huduma mbalimbali zilitolewa ikiwemo upimaji vvu ambapo walipimwa watu 448 ambapo kati yao wanaume 307 na wanawake 141 na waliokutwa na maambukizi ni wanaume wawili na wanawake wawili

Wakati huo huo Mpiga picha wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Muka Sabuni amepongeza na viongozi wa mbio hizo kutokana na namna aliyoweza kutengeneza mabango yenye picha zao wakati ulipoongia wilayani Muheza.

Hatua ya mmoja ya wakimbiza Mwenge ni kushangazwa na ubinfu uliotumiwa na mpiga picha huyo kwa kuweka picha zao kwenye mabango yaliyokuwa yamebeba ujumbe wa mwenge wilayani humo.

Kutokana na hali hiyo mmoja wa wakimbiza Mwenge hao Kenon alitumia muda wa makabidhiano baina ya Muheza na Pangani ndipo aliposimama na kumtambulisha huku akionyeshwa kufurahishwa na utendaji wake na kuiwataka viongozi wa wilaya hiyo kuendelea kumtumia kwenye shughuli mbalimbali. 
Mwisho 
Share:

HALMASHAURI TARIME YAPATA HATI SAFI...BILIONI 1.5 ZAVUKA MWAKA BILA KUTUMIKA


Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima akizungumza kwenye kikao cha madiwani

Na Dinna Maningo,Tarime.
Zaidi ya shilingi Bilioni 1.5 zinadaiwa kuvuka mwaka pasipo kutumika katika Halmashauri ya wilaya ya Tarime jambo linalodaiwa kukwamisha uendeshaji na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime ambaye pia ni Diwani kata ya Nyamwaga Misiwa Yomami kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime cha kujadili Taarifa ya mpango kazi na majibu ya Menejimenti kuhusu hoja za ukaguzi zilizoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali kwa mwaka unaoishia Juni 30,2018.

Yomami alisema pamoja na Halmashauri hiyo kupata hati safi ,kuna fedha Bilioni 1.5 zimevuka mwaka bila kutumika kutokana na kucheleweshwa.

"Tunaomba Serikali itatue hii ni changamoto inayokwamisha utendaji pesa zote hizo zinavuka mwaka bila kutumika zingekuja kwa wakati zingesaidia kukamilisha masuala mbalimbali kwa wakati ,lakini pamoja na changamoto zinazojitokeza naipongeza Halmashauri kwa kupata hati safi",alisema Yomami.

Akisoma Taarifa ya mpango kazi kuhusu hoja za Ukaguzi Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Apoo Tindwa alitaja hati halmashauri ilizopata katika kipindi cha mwaka 2013-2018 ,ambapo mwaka 2013/2014 Halmashari ilipata Hati safi,2014/2015 Hati yenye shaka,2015/2016 Hati Safi,2016/2017 Hati safi na 2017/2018 Hati safi,na katika Miradi ya Maendeleo kwa kipindi cha miaka hiyo imepata Hati safi ikiwemo miradi ya TASAF,ASDP, na HBF.

Tindwa aliongeza kuwa katika kutekeleza mkakati kwa ajili ya kuzuia hoja, kuna changamoto ambazo Halmashauri inahitaji kuzitatua ili kufikia lengo la kuondoa hoja ikiwemo fedha za maendeleo na matumizi ya kawaida kutopokelewa kwa wakati kutoka hazina,tatizo la kukatika kwa mtandao wa mawasiliano na upungufu wa Watumishi katika Idara za Halmashauri.

Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima aliwataka Madiwani kushikamana ikiwa ni pamoja na kujadili,kuangalia mapungufu na kuzifanyia kazi hoja za CAG ili kusiwepo na hoja nyingi za ukaguzi.

January 2019 Halmashauri hiyo iliingia katika tuhuma nzito ambapo mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima akiongea na Madiwani aliihituhumu Halmashauri kwa matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo ambazo ni mapato ya ndani Bilioni 9.5 kutoka Mgodi wa Dhahabu wa ACACIA uliopo Nyamongo tangu mwaka 2015-2018.

Malima aliunda Tume ya uchunguzi wa fedha hizo ikiongozwa na Katibu wake Mwita Chacha iliyoanza kazi Januari 28,2019 na kukamilisha uchunguzi Febuari 25,2019 na mwezi Aprili 2019 Tume hiyo mbele ya Madiwani na RC Malima ilieleza na kukiri uwepo wa ubadhilifu wa matumizi mabaya ya fedha ya Bilioni 15 kati ya hizo Bilioni 9.4 ni mapato ya Mgodi.

Kupitia tume hiyo aliiagiza Taasisi ya Kupambana na Rushwa Takukuru kumchungunza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Apoo Tindwa huku Watumishi wengine 4 wakisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger