Sunday, 13 January 2019

RATIBA YA LIGI KUU BARA YAPANGULIWA


Ratiba ya ligi kuu soka Tanzania bara, imepanguliwa kwa mchezo mmoja kusogezwa mbele.

Mchezo huo ni namba 220 ambao ulikuwa unazikutanisha timu za KMC ya Kinondoni dhidi ya Coastal Union ya Tanga.

Awali ulipangwa kuchezwa Jumatano Januari 16, 2019 lakini sasa utapigwa Alhamis Januari 16, 2019 kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Ligi kuu hiyo ipo kwenye raundi ya pili mechi za 20 kwa baadhi ya timu huku Simba ndio ikiwa timu yenye viporo vingi zaidi ambapo imecheza mechi 14 pekee.

Msimamo unaongozwa na Yanga wenye alama 50 katika mechi 18 huku Tanzania Prison ikiwa na alama 12 katika nafasi ya 20 ikiwa imecheza mechi 19.
Share:

AZAM FC MABINGWA KOMBE LA MAPINDUZI...WAMECHINJA MNYAMA SIMBA 2 -1


Azam FC wameichapa Simba SC 2-1 katika mechi kali ya  fainali ya kombe la Mapinduzi ndani ya Uwanja wa Gombani uliopo Pemba, Zanzibar jioni hii.

Goli la kutangulia la Azam limefungwa kwa mkwaju mkali wa Mudathir Yahya dakika ya 44.

Simba wamesawazisha kupitia kichwa cha Yusuph Mlipili akimalizia kona ya Shiza Kichuya dakika ya 63.

Obrey Chirwa akaifungia Azam FC bao la pili akimalizia kwa kichwa krosi ya Nickolas Wadada dakika ya 72.

Kwa matokeo haya Azam FC ndiyo bingwa mpya wa kombe la Mapinduzi kwa mwaka 2019.

Kikosi cha Azam Fc kilichoua Simba SC

1-Razak Abalora
2-Nickolas Wadada
3-Bruce Kangwa
4-Agrey Moris
5-Yakubu Mohamed
6-Stephan Kingue Mpondo
7-Salum Abubakar Sure Boy
8-Mudathir Yahya
9-Obrey Chirwa
10-Tafadzwa Kutinyu
11-Enock Agyei Atta

SUBs
-Mwadini Ally
-Hassan Mwasapili
-Lusajo Mwaikenda
-Salimin Hoza
-Ramadhani Singano
-Daniel Lyanga
-Donald Ngoma
Share:

SPIKA WA BUNGE KUSHITAKIWA

Zitto Kabwe na wabunge wengine wanne wanatarajia kufungua kesi ya kikatiba Mahakama Kuu ili kupata tafsiri ya kisheria, juu ya mipaka ya kinga ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na mamlaka ya Spika kumshtaki mwananchi bila kuathiri uhuru wa maoni ya kikatiba. Zitto kabwe mbunge wa kigoma mjini act-wazalendo, picha mtandao Zitto Kabwe na wabunge wengine wanne wanatarajia kufungua kesi ya kikatiba Mahakama Kuu ili kupata tafsiri ya kisheria, juu ya mipaka ya kinga ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na mamlaka…

Source

Share:

MILIONI 433.46 KULIPA WAKANDARASI WA MIRADI YA MAJI NGARA

Na Mwandishi wetu, Ngara. Naibu waziri wa maji,Juma Aweso ameahidi wizara yake kuwalipa wakandarasi wa miradi ya maji inayofadhiliwa na benki ya dunia katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera kiasi cha Sh433.46 milioni baada ya kucheleweshewa fedha hizo kutoka serikalini tangu mwaka 2014. Naibu waziri huyo pia amepongeza uongozi wa wilaya hiyo kwa kusimamia miradi ya maji katika vijiji inayofadhiliwa na benki ya dunia na kwamba halmashauri hiyo imedhibiti matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazoelekezwa kwa wananchi kupata maji safi na salama. Aweso ametoa pongezi hizo Januari 13, 2019…

Source

Share:

WABUNGE WATANO WATAKAO FUNGUA KESI KUITAKA MAHAKAMA ITAFSIRI MIPAKA YA CAG NA SPIKA WABAINIKA

Wabunge watano wanatarajia kufungua kesi ya kikatiba kuiomba Mahakama Kuu ya Tanzania kutoa tafsiri ya kisheria juu ya mipaka ya kinga ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na mamlaka ya Spika wa Bunge. Wabunge hao ni Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), Salome Makamba (Viti Maalumu), Hamidu Bobali (Mchinga), Saed Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini). Akizungumza na waandishi wa habari leo, Zitto amesema wamemuagiza Wakili wao Fatma Karume kuisajili kesi hiyo chini ya hati ya dharura. “Tutaenda Mahakamani ili kupata tafsiri ya kisheria kuhusu ni wakati…

Source

Share:

KOCHA JS SOURA AWATUPIA LAWAMA KINA ‘SHAFII DAUDA’ KIPIGO CHA GOLI TATU

Ligi ya mabingwa Afrika (CAFCL) hatua ya makundi (16 bora) imeanza rasmi siku ya Jumamosi tarehe 12-01-2019 ambapo vilabu mbalimbali vilijitupa katika viwanja tofauti kutafuta pointi 3 muhimu.Wawakilishi pekee ukanda wa Afrika Mashariki Simba sports Club (SSC) wao walikuwa na kibarua kigumu katika ardhi ya nyumbani walipowakaribisha waarabu klabu ya JS SOURA anayoitumikia pia mtanzania Thomas Ulimwengu katika uwanja wa Taifa(kwa mchina) Mechi hiyo iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka nchini nan chi jirani ulimalizika kwa matokeo ya kufurahisha na kutia moyo kwa Wekundu wa msimbazi Simba kuibuka…

Source

Share:

SHAFII DAUDA,YANGA SC WAUNDA KAMATI NZITO,KUIPA SIMBA UBINGWA WA AFRIKA

Ligi ya mabingwa Afrika rasmi ilianza jana kwa michezo mbalimbali ambpo kundi D linaloundwa na Vilabu vya Al Ahly ya Misri,Simba SC ya Tanzania,AS Victor ya DRC na JS Soura ya Algeria vilitupa karata zao za kwanza na kushuhudiwa wenyeji (Simba sc na Al Ahly) kwa mechi za mzunguko wa kwanza zikishinda michezo yao,Hapa Tanzania mnyama Simba aliibugi JS Soura mabao 3-0 na kule Misri Al Ahly wakiibuka na ushindi wa goli 2-0 hivyo kufanya kundi hilo kuongozwa na Simba mpaka sasa kwa pointi tatu na magoli matatu Kikosi cha…

Source

Share:

WAZEE 25499 KUTIBIWA BURE MAGU

Na Shushu Joel Halmashauri ya wilaya ya Magu mkoani Mwanza imefanikiwa kuwakabidhi wazee 25499 vitambulisho kwa ajili ya kupata matibabu bure. Akikabidhi vitambulisho hivyo kwa wazee hao mkuu wa wilaya hiyo Dr Philemon Sengati alisema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Raisi Magufuli imejipanga kuhakikisha wazee wote nchini wanapata matibabu bila malipo kama walivyoahidiwa mwaka 2015 wakati wa kampeni. Aidha aliongeza kuwa mbali na kuwakabidhi vitambulisho wazee hao, pia limetengwa dirisha maalum kwa ajili ya utoaji wa huduma kwa wazee ili kurahisisha kufikia huduma bila kupanga foreni kutokana…

Source

Share:

CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU YA ELIMU YAPUNGUZWA USHETU

Na Maiko Luoga Ili kupambana na changamoto zinazoikabili sekta ya elimu katika maeneo mbalimbali nchini hatimae Mh Elias Kwandikwa Mbunge wa Ushetu na Naibu waziri wa ujenzi amefanya ziara ya kikazi katika kata ya Igwamanoni Jimboni kwake ili kuona changamoto mbalimbali zinazoikabili secta ya Elimu Sekondari na msingi na kuzitafutia ufumbuzi. Katika ziara hiyo Mh Mbunge alipata fursa ya kukagua shule ya sekondari Igwamanoni, shule ya msingi Luhaga na Shule ya msingi Iramba ambapo alibaini upungufu wa madarasa ya Shule ya sekondari Igwamanoni hali iliyomlazimu Mh Kwandikwa kutoa pesa kiasi…

Source

Share:

NAIBU WAZIRI MAJI AWASHUKIA WANANCHI WANAOHUJUMU MIRADI YA MAJI

Na Allawi Kaboyo-Kagera. Naibu waziri wa maji Juma Aweso akiwa mkoani Kagera ametangaza kiama kwa wananchi wanaojihusisha na hujuma za miundombinu ya maji na kupelekea wanachi kukosa huduma ya maji Aweso ametoa tamko hilo alipokuwa akiendelea na ziara yake katika wilaya ya Ngara ambapo imesemekena miradi mingi ya maji inahujumiwa na wananchi wachache wasioitakia mema nchi yao na kuahidi kuwashugulikia bila kujali wala kuangalia nafasi zao. “Haiwezekani serikali tutoe pesa nyingi ili kutekeleza miradi hii alafu watokee majangili wachache waanze kuhujumu jitihada hizi, hatutakubali tutawashugulikia hatakama wanamapembe makubwa kiasi gani…

Source

Share:

KIGWANGALLA,FATMA KARUME WATISHANA KWENYE MNUSO

Share:

NYOTA WA SOKA AFRIKA AFARIKI DUNIA

Share:

WACHEZAJI AZAM,SIMBA WAPAA KWA NDEGE MAALUMU KUKIPIGA FAINALI PEMBA



Kamati ya maandalizi ya michuano ya Mapinduzi mwaka 2019, inayofikia tamati leo, imeeleza kuwa timu za Azam FC na Simba zimesafiri leo kwa ndege kutoka Unguja kwenda Pemba tayari kwa mchezo wa fainali.

Kamati hiyo kupitia kwa Mwenyekiti wake imeeleza kuwa timu hizo ambazo zimecheza mechi za makundi na nusu fainali katika visiwa vya Unguja imebidi zisafiri kwa ndege ya kukodi ili kwenda kumaliza fainali leo.

''Maandalizi yote kwaajili ya mchezo wa fainali yamekamilika na timu zimesafiri kwa ndege leo, hivyo mchezo utafanyika muda uliopangwa kwenye uwanja wa Gombani ambao una ubora wa kutosha'', amesema.

Azam FC inacheza fainali yake ya tatu mfululizo huku ikiwa tayari imeshachukua ubingwa huo katika fainali zote mbili zilizopita ikiwemo ile ya mwaka jana (2018) ambayo waliwafunga Simba.

Kwa upande wa Simba wachezaji Haruna Niyonzima, Shiza Kichuya na Rashid Juma tayari wamewasili visiwani Pemba kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Simba ambacho kina wachezaji wengi wa kikosi B.
Share:

DOGO JANJA AMPIGA CHINI UWOYA...HUYU HAPA MPENZI WAKE MPYA


Dogo Janja akiwa na mwanamke anayedaiwa kuwa mpenzi wake mpya

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Abdulaziz Chende maarufu 'Dogo Janja' ameonekana akiwa kwenye mapozi yenye utata na mwanamke ambaye anadaiwa kuwa ndiye mrithi wa Irene Uwoya.

Picha pamoja na video zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha Janjaro akiwa na mwanamke asiyefahamika jina na wengi kudai kuwa Irene Uwoya amepinduliwa kwa Dogo Janja, ikiwa mpaka sasa wawili hao hawajaweka wazi kuachana.

Uwoya na Dogo Janja walianza kurushiana maneno ya mafumbo katika mtandao wa Instagram Januari 07, hali ambayo ilitafsiriwa kuwa ni wazi kuwa ndoa yao itakuwa imevunjika.

Baada ya sakata hilo, baba mlezi wa Dogo Janja, Madee Ali 'Seneda' ameingilia kati suala hilo na kuwaonya kutorushiana maneno mitandaoni.
Share:

TFDA YAJIVUNIA KUIPAISHA TANZANIA KWA KUWA NA MIFUMO BORA YA UDHIBITI WA BIDHAA

NA WAMJW-Dar es Salaam
Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imesema katika kipindi Cha Miaka mitatu imeweza kufanya mambo mbalimbali ya udhibiti wa usalama, ubora na usalama wa bidhaa za ndani na nje ya Nchi ikiwemo kutambulika kimataifa kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya ISO 9001: 2015.


Hii ni kutokana na mafanikio ya miaka mitatu ya utekelezaji wa kazi chini ya Serikali ya Awamu ya Tano, kwa kufikia na kuvuka malengo iliyojiwekea katika udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendanishi ili kulinda afya ya jamii nchini.


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Adam Fimbo amebainisha hayo wakati akitoa ripoti ya miaka mitatu ya Mamlaka hiyo wakati wa ziara maalum ya Maafisa Mawasiliano na habari wa Wizara ya Afya na taasisi zake katika kampeni maalum ya ‘Tumeboresha Sekta ya Afya’ inayolenga kueleza mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli.


“Kutokana na kuwa na mifumo thabiti ya udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa dawa, mnamo Mwezi Desemba 2018, TFDA imetambulika kufikia ngazi ya tatu (Maturity Level 3) ya Shirika la Afya Duniani (WHO) ya ubora wa mfumo wa udhibiti wa dawa, vifaa tiba na vipodozi, ambapo hatua hii imeifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kufikia hatua hii


Fimbo ameeleza kuwa, TFDA katika mikakati yake hiyo imeweka mifumo na taratibu za ndani za utoaji huduma na utendaji bora ili kukidhi mahitaji na matarajio ya wateja kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya ISO 9001:2015 kwa huduma za kawaida na ISO 17025:2005 kwa huduma za maabara.


Aidha, ameongeza kuwa huduma za TFDA hutolewa kwa kuzingatia viwango vya Mkataba wa Huduma Wateja kama ulivyorejewa mwaka 2016.


“Mfumo wa usajili wa bidhaa umeendelea kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo idadi ya bidhaa za chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendanishi vilizosajiliwa imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka, katika kipindi cha 2015/16 hadi 2017/18.


Pia tumesajili jumla ya bidhaa 14,345 kutoka bidhaa 8,866 zilizokuwa zimesajiliwa mwaka 2015/16 ambapo ni sawa na ongezeko la 62%. Hii imetokana na kuongezeka kwa uelewa wa matakwa ya sheria miongoni mwa wafanyabiashara na kukua kwa biashara.” Ameeleza Fimbo.


Aidha, Fimbo ameongeza kuwa TFDA imekuwa ikifanya tathmini na usajili wa bidhaa kwa lengo la kuhakiki endapo bidhaa zinakidhi vigezo vya usalama, ubora na ufanisi kabla ya kuruhusiwa katika soko.


“Kuwepo kwa bidhaa nyingi zilizosajiliwa katika soko ni uthibitisho kuwa walaji wanapata bidhaa zilizo salama, zenye ubora na ufanisi.


Pia tumeweza kusajili maeneo ya biashara za bidhaa za chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendanishi kwa lengo la kutambua maeneo ambayo bidhaa hizo zinazalishwa, kuhifadhiwa, kusambazwa na kuuzwa. Mfumo huu husaidia kuhakikisha kuwa maeneo husika yanakidhi vigezo ili kutoathiri usalama, ubora na ufanisi wa bidhaa”. Alieleza Fimbo.


Aidha ameongeza kuwa, TFDA katika kipindi cha miaka mitatu (2015/16 – 2017/18), imeweza kusajili jumla ya maeneo 25,630 ya biashara za bidhaa zinazodhibitiwa ikiwa ni pamoja na maeneo 9,000 yaliyosajiliwa mwaka 2016/17 na maeneo 5,606 mwaka 2015/16, hii ikiwa ni sawa na ongezeko la 60.5%.


Aidha, katika kipindi hiki, TFDA imeendelea kushuhudia kufikiwa kwa dira yake ya kuwa taasisi ya mfano barani Afrika katika udhibiti wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendanishi na hivyo kuvutia nchi mbalimbali kuja kujifunza mifumo iliyopo na kwenda kuitekeleza nchini kwao.


(mfano nchi za Zimbabwe, Rwanda, Kenya, Uganda, Ethiopia, Sudan Kusini, Botswana, Mauritius, Lesotho na Bangladesh zinekuja kujifunza TFDA).


“Katika kipindi cha mwaka 2015/16 – 2017/18, Mamlaka imefanikiwa kufikia na kuvuka malengo iliyojiwekea katika utekelezaji wa mipango kazi yake.

Mamlaka katika kipindi cha 2017/18 itaendelea kutoa kipaumbele katika utekelezaji kwa ufanisi wa malengo mahususi nane (8) yaliyomo katika Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano (5) yaani 2017/18 – 2021/22, ili kulinda afya ya jamii.” Alieleza Fimbo.


Mafanikio mengine ni pamoja na kukamilika kwa jengo la Maabara na kufungwa kwa vifaa vya kisasa vya uchunguzi jijini Mwanza jambo ambalo limesaidia kusogeza huduma zaidi kwa jamii .
Share:

WAZIRI WA KILIMO AKUTANA NA WADAU WA MRADI WA KUENDELEZA TASNIA YA MBEGU NCHINI

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) tarehe 12 Januari 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na wadau wa kuendeleza tasnia ya mbegu nchini.

Katika Kikao kazi hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Kilimo maarufu kama Kilimo I Jijini Dar es salaam pamoja na wadau kutoka Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), Taasisi ya kudhibiti ubora wa mbegu (TOSCI), na Taasisi ya utafiti Tanzania (TARI), vilevile walialikwa wadau kutoka Bill & Melinda Gates kupitia kampuni ya ushauri ya mradi wa AGRI Experience.

Akizungumza katika kikao kazi hicho Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga alisisitiza kuwa serikali imedhamiria kuleta mapinduzi ya kilimo kwa kuongeza tija katika uzalishaji kwa kuongeza matumizi ya teknolojia ikiwemo mbegu bora.

Alisema pamoja na mambo mengine serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt John Pombe Magufuli imjidhartiti katika kuhakikisha kuwa nchi inajitosheleza kwa mafuta ya kula na hivyo serikali inataka mradi huo kuondoa chanagmoto katika sekta ya mbegu kwa kuzalisha mbegu za mafuta hasa za alizeti na michikichi.

Mhe Hasunga amewapongeza wadau kutoka Bill & Melinda Gates kupitia kampuni ya ushauri ya mradi wa AGRI Experience kwa ushirikiano na serikali ya Tanzania kutekeleza mradi huo.
Share:

KAULI YA JPM YA 'KUCHINJWA NA KUTUPWA BAHARINI' YAWAIBUA WAPINZANI


Wakati Rais John Magufuli akieleza sababu zinazomzuia kukutana na wanasiasa, viongozi wa vyama vya upinzani wamemtaka asiwe na hofu kukutana nao na kwamba pengine mtu aliyetishia kumchinja, alikuwa na maana ya “kuchinjwa kisiasa”.


Akizungumzia ushauri uliotolewa na Askofu Zachary Kakobe wa Kanisa la FGBF kutaka wanasiasa wakutane kama walivyofanya viongozi wa kidini, Rais alisema amekuwa akisita kwa sababu baadhi ya wanasiasa wanamtukana na wengine wametishia kumchinja na kumtupa baharini ndio maana ameamua awaache peke yao.

Hata hivyo, alisema yuko tayari kukutana nao.

Hayo yalitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati wa mapokezi ya ndege mpya ya Serikali aina ya Airbus A220-300, ambako viongozi kadhaa wa kidini walipewa nafasi ya kufanya sala, akiwemo Askofu Kakobe, ambaye kabla ya sala aliomba aseme neno.

“Nimeusikia wito wa Mzee Kakobe kuwa walipokutana na wao (viongozi wa dini) kule, basi na sisi wanasiasa tuwe tunakutana,” alisema Rais.

“Mimi nimekubali sana, lakini tatizo ni kuwa huwezi kukutana na mtu anayekutana na kukuambia siku uchinjwe, utupwe baharini. Je, siku ukikutana naye iwe ndiyo siku ya kuchinjwa?”

Kauli hiyo ilimfanya mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, John Shibuda aombe radhi kama kiongozi wa wadau wa siasa na kwa niaba ya vyama vyote iwapo kuna kauli zimewahi kutolewa zenye mbomoko wa maadili.

“Nampongeza kwa kutambulisha utashi wake wa kutaka kukutana na viongozi wa vyama vya siasa. Hivyo kama kuna kauli ambayo imewahi kumkwaza atusamehe sisi wadau wa siasa kama ambavyo amekuwa akisamehe wafungwa ili na sisi tutoke kifungoni. Adhabu ya miaka mitatu inatosha,” alisema.

Alisema Rais anapaswa kuwapangia fursa ya kukutana nao ili awaeleze hisia zake na wao waeleze zao ili kudumisha utamaduni mzuri wa siasa kwa kuwa Tanzania ina deni la kuwa kielelezo cha siasa bora ya demokrasia ya vyama vingi.

Rais hakumtaja mtu aliyetoa tishio hilo la kuchinja, lakini wanasiasa wengi waliotoa lugha iliyotafsiriwa kuwa haifai, wamefikishwa mahakamani na baadhi kama mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi wameshatumikia adhabu ya kifungo.

Naye mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), James Mbatia alisema bado msimamo wake ni meza ya mazungumzo na kwamba hata alipokutana na Rais Ikulu, Novemba 13 mwaka jana alimsisitiza jambo hilo.

“Kauli ya mtu mmoja asiichukulie vibaya. Anatakiwa kujua kuwa yeye ni jalala,” alisema mwenyekiti huyo wa NCCR-Mageuzi akirejea msemo maarufu wa “ukubwa ni jalala”.

“Awe na moyo wa uvumilivu, aweke kipaumbele cha taifa mbele kwa kuwa nchi ni kubwa zaidi ya mtu yeyote.”

Alisema Watanzania wote wanapaswa kutunza nguzo ya hekima, umoja na amani kwa kuwa jamii yoyote yenye migogoro haiwezi kustawi.

Mbatia alitoa mfano wa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mpinzani wake mkuu, Raila Odinga ambao siku za hivi karibuni walishikana mikono kumaliza tofauti zao na wamekuwa wakionekana pamoja katika shughuli za kitaifa, kijamii na kiserikali.

Mbatia anaungwa mkono na kiongozi wa ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe ambaye alisema Rais Magufuli hakupaswa kutoa kauli kama hiyo ya “kuchinjwa na kutupwa baharini” kwa kuwa ana cheo cha Rais na amiri jeshi mkuu, lakini akasisitiza kuwa wamekuwa wakiomba kukutana naye kwa mwaka wa pili sasa.

“TCD wamemuandikia barua ya kutaka kuonana naye huu ni mwaka wa pili, lakini majibu yake ndio kama hayo unayoyaona. Hata juzi Mwenyekiti Mbatia alisema kuwa alipokutana naye alimkumbusha,” alisema Zitto

Naye naibu katibu mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salumu Mwalimu alisema kauli ya Rais Magufuli ilikuwa na utata kwa kuwa hakueleza ni kuchinjana kwa namna gani wala ni nani aliyewahi kuahidi kumchinja.

“Kuna vyama vya upinzani 18 yeye hajasema nani anataka kumchinja. Kama kuchinjana kisiasa ni sawa tu kwa kuwa tafsiri yake ni kuchuana, lakini kama ni kuchinjana kwa tafsiri nyingine sio kauli nzuri ina utata ndani yake maana kuchinjana si Utanzania,” alisema Mwalimu.

Kuhusu suala la kukutana na Rais Magufuili, Mwalimu alisema ustaarabu wa siasa ni pamoja na viongozi wa vyama kukutana na kujadili pamoja mambo ya kitaifa, kukosoana kwa heshima na kuruhusu hoja mbadala na hicho ndicho kimekuwa kikifanywa na viongozi waliopita, ndiyo maana siasa za taifa hili zimekuwa zikisifika.

“Siasa zetu zinapaswa kuwa upinzani na ushindani kama ilivyo kwa Simba na Yanga na si uadui. Tukiwa katika majukwaa tunachuana lakini tukishuka chini tunakunywa chai pamoja.

“Tunaoleana na tunashirikishana na kushauriana katika mambo mbalimbali wakati wa tatizo na wakati wa amani. Jambo hilo linarekebisha tabia hata za wafuasi wetu,” alisema Mwalimu.

Alisema Chadema haijawahi kuombwa kukutana na Rais ikakataa, wala haijawahi kusema haitaki kuonana na Rais. Alisema chama hicho kimekuwa kikikutana na marais wote hata Rais aliyepita walikutana naye mara kadhaa kwa kuwa alikuwa na siasa za kistaarabu.

“Hapa nchini kuna Rais mmoja tu, naye ana nafasi ya kutoa mwelekeo wa siasa za nchi. Kama kweli anataka kukutana na viongozi wa siasa ajiamini, aseme wala asiogope.”

Na Ephrahim Bahemu, Mwananchi 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger