Thursday, 15 December 2016

Kauli ya CHADEMA kufuatia kutoweka kwa kada wao Bwana Ben Sanane

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hadi sasa hakijui alipo msaidizi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Ben Saanane.

Kimevitaka vyombo vya dola, kuchukua hatua za haraka kuhakikisha msaidizi huyo anapatikana haraka. 
Saanane inadaiwa alitoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 18, mwaka huu. Juhudi za kumtafuta katika vituo vya polisi, hospitalini na vyumba vya kuhifadhia maiti, zimefanyika bila mafanikio.

Kauli hiyo imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Saanane ambaye hajulikani aliko. 
Alisema hata wao hawajui alipo, hawafahamu kama yuko hai au ameshikiliwa mahali. Kwamba wanachokijua ni kwamba hawajui aliko.

“Katika mazingira haya, tunaiomba serikali na vyombo vyake vya ulinzi, ituambie kama imemkamata na inamshikilia Ben Saanane tuanzie hapo…lakini kama hawajamkamata na hawamshikilii, serikali na vyombo vyake watueleze mawasiliano yake ya mwisho yalikuwa lini, na nani, wapi na yalihusu nini,” alisema.

Alisema kwa kuwa serikali ndiyo yenye udhibiti wa mipaka yote nchini, iwaeleze kama kuna rekodi yoyote inayoonesha Ben aliondoka nchini kwa kupitia mipaka hiyo, kama ni mipaka ya nchi kavu, majini au viwanja vya ndege.

Katika hatua nyingine, alisema pamoja na majibu hayo, lakini pia wanaitaka serikali pamoja na vyombo vyake vya dola, kufukua miili ya watu waliokufa katika mto Ruvu na ifanyiwe uchunguzi ili wajulikane watu hao ni akina nani, ili isije kuwa miongoni mwa watu hao ni Saanane.

Lissu alisema kuwa mawasiliano ya mwisho kati ya Saanane na Mbowe, yalikuwa ni Novemba 14, mwaka huu wakati Saanane akiwa Dar es Salaam na mwenyekiti huyo akiwa Dodoma.

“Alimwambia mwenyekiti uko wapi, akamwambia nakwenda kwenye maziko ya Samuel Sitta, mawasiliano ya mwisho ni ya tarehe 14 Novemba,” alisema Lissu.

Alisema pamoja na kwamba Saanane alikuwa ni msaidizi wa Mbowe katika masuala ya kisiasa na kijamii, lakini hakuwa akitembea na mwenyekiti huyo na kwamba shughuli zake alikuwa akifanyia katika Makao Makuu ya chama hicho.

Lissu alisema kuwa wapo watu wanahoji inawezekanaje Mwenyekiti hajui mahali alipo msaidizi wake, lakini wanapaswa kufahamu kuwa Mbowe hakuwa akitembea na Saanane.

Alisema baada ya maziko ya Sitta, viongozi wote wa chama hicho walikuwa wakizunguka katika mikoa mbalimbali kwa ajili ya kufanya shughuli za chama, lakini katika kipindi chote hicho, mwenyekiti huyo hakuwa na msaidizi wake huyo, kwa kuwa hatembei naye na si jambo la ajabu.

“Baada ya hizi ziara, tulienda nchi za nje…katika kipindi chote hiki Mwenyekiti hakuwa na Ben na vilevile nataka niweke hii vizuri, Mwenyekiti hakupata wasaa wa kusema Ben yuko wapi, kwa sababu hatembei naye, hayuko naye muda wote.”
 “Sasa kuna watu wanaosema Mwenyekiti ndiye anayejua, atuambie yuko wapi, Mwenyekiti hajui, mimi sifahamu aliko Ben, tungekuwa tunafahamu tungeshasema,” alisema.

Alisema kwa mara ya kwanza alipigiwa simu na mdogo wake Ben, aliyemtaja kwa jina la Dorice Desemba 4, lakini hakumpata na alimtumia ujumbe kumwambia kuwa kaka yao Ben amepotea, hawajui aliko na alikuwa akitaka ushauri ambapo alimjibu waliripoti jambo hilo polisi na kwenye vyombo vya habari.

Alisema si kwamba wamenyamaza kimya, kwa kuwa wanajua alipo msaidizi huyo na kwamba watu wanaodai hivyo si sahihi. 
Alitaka mtu yeyote mwenye taarifa kuhusu Saanane alipo, azitoe taarifa hizo hadharani, polisi, kwenye chama, vyombo vya habari au kwa ndugu zake.
Share:

Wednesday, 14 December 2016

TAARIFA MUHIMU KUTOKA JKT KWA WANAFUNZI WA FORM 6 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA JKT AWAMU YA PILI 2016



TAARIFA KWA UMMA
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linapenda kutoa ufafanuzi kwa umma, juu ya vijana waliohitimu kidato cha sita mwezi Mei mwaka 2016 na kutakiwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria Opereshani Magufuli awamu ya pili.
Share:

BREAKING NEWS:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO MWAKA WA MASOMO 2016/2017

 Image result for HESLB.GO.TZ
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu wametangaza majina ZAIDI YA 20000 ya wanafunzi waliopata mkopo 2016/2017.

Kama utahitaji kuangaliziwa jina lako kwa "usahihi" na "kasi ya ajabu" (ambapo utajibiwa ndani ya dk 1 tu) kama limepata mkopo tafadhali fanya yafuatayo;

1.TUMA EXAM NAMBA YAKO YA FORM 4 NA MWAKA
   ULIOMALIZA  MFANO:S3409.0012.2013-HESLB  KWENDA
   NAMBA
0652740927

2.HUDUMA HII UTATOZWA TSHS 1000 TU(KWA AJILI YA
    KUISUPORT MASWAYETU   BLOG)


3.TUMA PESA KWENDA 0768260834-MPESA
                                               0652740927-TIGO PESA
                                                                     &AIRTEL MONEY

    
                                                                  


  


4.UTAJIBIWA NDANI YA DK 1 TU.

5.TUMA PESA KWANZA,NDIO UTAJIBIWA SMS YAKO

KUONA MAJINA HAYO ;

<<BONYEZA HAPA>> 
Share:

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - KIKAO CHA NEC


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO DECEMBER TAREHE 14.12.2016

Share:

Hashim Rungwe kumtetea ‘Ndama mtoto wa ng’ombe’,Kesi yake Yaahirishwa Hadi Disemba 27

Share:

Lowassa adai T.B Joshua ameitabiria Chadema ushindi


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa amesema ataingia Ikulu baada ya miaka minne ijayo na rafiki yake T.B Joshua amemtabiria kuwa Serikali ijayo itaongozwa na Chadema. 

Lowassa, ambaye alishika nafasi ya pili katika kinyang’anyiro cha urais mwaka jana, ameshaonyesha nia ya kuingia tena kwenye mpambano huo wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. 

Akizungumza na viongozi na wanachama wa Chadema mkoani Tabora, waziri huyo mkuu wa zamani alisema ana uhakika wa kuingia Ikulu bila ya umwagaji wa damu. 

Huku akishangiliwa, Lowassa ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, aliwashukuru wana Tabora na Watanzania kwa ujumla kwa kura walizompa katika uchaguzi mkuu uliopita. 

Lowassa aliwaeleza wanachama na viongozi wa chama hicho kuhusu utabiri wa T.B.Joshua na angalizo alilompa. 

Alisema muhubiri huyo maarufu barani Afrika anayefanya shughuli zake nchini Nigeria na ambaye alikuja nchini mara baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita, alimpa angalizo kuwa ili washinde ni lazima wawe wamoja, washikamane na kuwa majasiri.

 “Najua waandishi wa habari wataandika, lakini sijali rafiki yangu Joshua ametabiri Serikali ijayo ya Tanzania itaongozwa na Chadema,” alisema. 

Lowassa amekuwa akienda Lagos, Nigeria kuhudhuria ibada za T.B Joshua anayeongoza kanisa la The Synagogue Church of All Nations na ambaye amekuwa akitabiri matukio makubwa kutokea sehemu mbalimbali duniani. 

Katika kudhihirisha urafiki wake na T.B Joshua, Lowassa alisema katika mahafali ya wanafunzi wa vyuo vikuu ambao ni wanachama wa Chadema yaliyofanyika jijini Dar es Salaam katikati ya mwaka, kuwa CCM ilimuita nabii huyo nchini baada ya uchaguzi ili amshawishi akubali matokeo. 

Lowassa aliwaambia wanafunzi hao kuwa alimweleza T.B Joshua matukio yote yaliyotokea wakati wa uchaguzi na hivyo kumfanya nabii huyo aamue kutohudhuria sherehe za kuapishwa.

 Hata hivyo mwenyewe T.B Joshua hajathibitisha kauli hiyo ya Lowassa. Kuhusu Tabora, Lowassa alisema ni mkoa wa kihistoria na ndio kitovu cha siasa nchini kwa kuwa ndiko kulikoanza vuguvugu la mapambano ya kudai uhuru na kwamba una heshima yake kisiasa. 

Aliwataka viongozi na wanachama wa Chadema kuhakikisha wanalinda heshima hiyo kwa kuifanya Chadema kuongoza nchi. 

Lowassa, ambaye aliwahi kuwa Waziri Mkuu, aliwaeleza wanachama na viongozi kuwa ruzuku ni fimbo ya kuwagombanisha wanachama katika vyama vya siasa. 

Aliwataka wanachama na viongozi kuhakikisha hawagawanywi na ruzuku na kwamba waulinde Ukawa na wakatae kuvurugwa. 

“Vyama vingi nchi za Afrika hugawanywa kwa fedha za Serikali zilizopo madarakani, jambo ambalo sisi tulikatae,” alisema. 

Aliwaleza wanachama hao ruzuku inatolewa ili wanachama wabaki wakigombana na kushindwa kufanya mambo ya msingi. 

Akiizungumzia elimu, Lowassa alisema CCM inapata ushindi katika maeneo ambayo yapo nyuma kielimu na kuitaja mikoa ya Singida, Mtwara, Lindi, Dodoma na Tabora. 

Alieleza kuwa mikoa iliyo nyuma kielimu ndio ngome ya chama tawala na kwamba ndio maana anaposisitiza elimu itolewe bure, anajua anachomaanisha. 

Mbunge huyo wa zamani wa Monduli aliambatana na mjumbe mwingine wa Kamati Kuu ya Chadema, Mwita Waitara, ambaye katika hotuba yake alisisitizia suala la tume huru ya uchaguzi. 

Waitara, ambaye ni mbunge wa Jimbo la Ukonga aliwataka wanachama wa Chadema kusimama imara kudai tume huru. 

Awali, mratibu wa Chadema wa Kanda ya Magharibi, General Kaduma alisema watu watakaojaribu kuwagawa wanachama, watawekwa pembeni ili wawaache wengine waendelee kuongoza chama. 

Alisema madhumuni ya mikutano ya ndani ya chama hicho inayoendelea nchi nzima ni kupanga mambo yanayohusu ujenzi wa chama chao na kuwakumbusha viongozi mambo ya msingi ya chama.
Share:

Watumishi TRA Wafikishwa Mahakamani kwa Rushwa ya Milioni 66

Share:

Kamanda Sirro: Aliyetishwa na kauli ya Mzee wa Upako afungue kesi

Share:

Rais Dkt Magufuli ateua Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.

Share:

Polisi Dar yawatia mbaroni watu 22 kwa kosa la uporaji katika magari

Share:

Tuesday, 13 December 2016

Humphey Polepole ateuliwa kuwa katibu wa halmashauri kuu itikadi na uenezi

[​IMG]
Share:

Mwanzilishi wa JamiiForums, Maxence Melo akamatwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.
Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Kosa ni kuwanyima Polisi taarifa binafsi za wateja wa mtandao wa JamiiForums zilipohitajika. Maxence ameendelea kushikilia msimamo kuwa ni uvunjwaji wa sheria na haki za wananchi kufanya hivyo.

Taarifa zaidi baadaye
Share:

Official VIDEO | Vanessa Mdee & Jux - Juu | Watch/Download



Share:

CCM Dimani yapitisha 3 mchujo wa awali ubunge


 
WAGOMBEA watatu wa nafasi ya kinyang’anyiro cha ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani Zanzibar, wamepitishwa katika hatua ya awali na mkutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jimbo hilo.
Katibu wa CCM Wilaya ya Mjini Magharibi, Yahya Saleh alithibitisha kupitishwa kwa majina hayo, ambayo yatapelekwa mbele ya Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa kwa ajili ya uchambuzi zaidi na kupigiwa kura.
Majina ya wanachama waliopitishwa kugombea nafasi ya ubunge Dimani katika hatua ya tatu bora ni Juma Ali Juma, Hussein Migoda Mataka pamoja na aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Hafidh Ali Tahir ambaye nafasi yake ilichukuwa katika uchaguzi wa mwaka jana, Abdalla Sheria.
“Tumepitisha majina matatu ya wagombea wa nafasi ya ubunge Jimbo la Dimani katika hatua ya awali na majina hayo yatapelekwa mbele ya Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa kwa uchambuzi zaidi,” alisema.
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Magharibi kichama, Yussuf Mohamed aliwataka viongozi kujenga mshikamano huku wakiweka mbele mikakati na malengo ya kuhakikisha chama cha Mapinduzi kinashinda katika uchaguzi huo.
Alisema wagombea wote waliojitokeza kuchukua fomu wana sifa na vigezo vya kuongoza, lakini katika utaratibu wa awali lazima wapungue ili kupata idadi inayohitajika na hatimaye mtu mmoja atakayepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi huo.
“Tulikuwa na wagombea 16, lakini sasa tunao watatu ambao tutakwenda na hatimaye kupata jina la mtu mmoja tu ambaye ndiye atakayepeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi huo,” alieleza mweneyekiti huyo.
Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani utafanyika Januari 22, mwakani, kujaza nafasi ya Hafidh Ali Tahir aliyefariki ghafla mkoani Dodoma mwezi uliopita wakati akihudhuria vikao vya Bunge.
Share:

Uhuru wa kuabudu kutochezewa


WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu kwa kila Mtanzania na haitamvumilia mtu wala kikundi chochote kitakachofanya mambo yanayotishia usalama na amani ya nchi.
Aidha, ametaka migogoro katika nyumba za ibada, ikiwemo misikiti imalizwe ndani kwa kutumia mabaraza badala ya kutoka nje kwa jamii kwani inaashiria sura mbaya ya kiimani na haina tija.
Majaliwa aliyasema hayo jana alipozungumza katika Baraza la Maulid ya kumbukizi ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) lililofanyika kitaifa kijijini Shelui wilayani Iramba, mkoani Singida na kurushwa hewani na televisheni ya TBC1.
Maulid ilisomwa juzi usiku na mapumziko pamoja na Baraza la Maulid ilikuwa jana.
Kabla ya kuzungumzia ujumbe huo kuhusu amani ya nchi, Majaliwa alimshukuru Rais John Magufuli kwa kusitisha kikao cha Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) isiendelee hadi jana ili kumwezesha kuhudhuria Baraza hilo la Maulid.
Waziri Mkuu alisema serikali haitayumba katika kusimamia usalama wa nchi na kuhakikisha hakuna nafasi kwa kikundi chochote kitakachoipeleka nchi pabaya na kuwataka viongozi wa dini kuwahakikisha waumini wao hawaenezi chuki dhidi ya imani nyingine.
“Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kila mwananchi kuabudu kile anachoona kinafaa. Serikali itafanya kila liwezekanalo kusimamia na kuhakikisha hakuna kikundi kinahatarisha usalama wa nchi na hatutayumba katika hilo,” alisema Waziri Mkuu na kuongeza: “Mara nyingi huwa napenda kurejea kauli ya Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere) aliyosema kuwa: Nchi haina dini bali watu wake wana dini, na kusimamia hilo kwamba tutaendelea kuwezesha uhuru wa kuabudu.”
Hata hivyo, alionya kuwa pamoja na serikali kusimamia uhuru wa kuabudu, haitawavumilia watakaotoa mahubiri yasiyozingatia misingi ya sheria na kanuni za nchi na yenye kumuumiza mtu wa imani nyingine.
Pamoja na hayo, alisema mpaka sasa dini zote nchini zinafanya vizuri katika kuhubiri imani zao na amani ya nchi, jambo linaloendelea kuifanya Tanzania kuwa kimbilio kwa wananchi wa mataifa yenye mapigano. “Bado Tanzania imeendelea kuwa kimbilio kwa wanaopigana, sisi hatuna mahali pa kwenda, kama wao wanakuja hapa kwetu sisi tutakwenda wapi? Ukitafakari hilo utadumisha amani,” alisema Majaliwa.
Akijibu risala iliyosomwa kwake ikielezea mambo kadhaa ikiwemo tishio la ugaidi, watu kubambikiziwa kesi kwa chuki, kuundwa kwa kamati ya kitaifa ya Kiislamu kushughulikia maadili na uanzishwaji wa chombo cha maarifa (Daruu/Nyumba ya Maarifa), Waziri Mkuu alisema ni masuala ambayo serikali inayachukulia kwa uzito wake.
Alisema serikali inatambua uwepo wa matishio ya ugaidi sehemu mbalimbali na pamoja na kwamba ipo imara, inahitaji nguvu ya pamoja ya wananchi kukabiliana na vitendo hivyo na matendo maovu yote.
Kuhusu migogoro katika nyumba za ibada, Waziri Mkuu Majaliwa alisema kumekuwa na ugomvi na migogoro katika maeneo ya ibada ya watu kugombea madaraka na uongozi na kuleta taswira mbaya.
Akielezea upande wa misikiti, majaliwa alisema ugomvi na migogoro katika misikiti ni sura mbaya, haina tija na inapaswa kumalizwa ndani na si kutoka nje.
“Tutumie mabaraza yetu kutatua migogoro ndani ya misikiti yetu,” alieleza na kusisitiza kuwa serikali itaendelea kutegemea dini kuimarisha amani nchini, na kuwataka pia waumini wa dini hiyo na viongozi kutokukaa bila kufanya kazi kwani hata vitabu vingine vya Mungu ikiwemo Biblia Takatifu, vinaeleza wazi kuwa, asiyefanya kazi na asile.
Waziri Mkuu pia alizungumzia kuhusu uwajibikaji wa watumishi wa umma na kusema kuwa hatua ambazo serikali inachukua kwa watumishi wake ni sahihi na kamwe haitarudi nyuma katika kusimamia haki za Watanzania bila kujali dini, rangi wala kabila.
Alizungumzia pia suala la maadili kwa vijana na jamii kwa ujumla na kutaka viongozi wa dini ya Kiislamu kuwalea vijana katika malezi ya kiislamu kwa ajili ya kuwaandaa kuwa viongozi wema wa sasa na baadaye kwa dini na taifa.
Alitumia fursa hiyo pia kuwatakia Wakristo kote nchini sikukuu njema ya kuzaliwa Yesu Kristo Desemba 25 na pia aliwatakia Watanzania wote sherehe njema za kuupokea Mwaka Mpya 2017.
Kauli ya Mwigulu Mbunge wa Iramba Magharibi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akizungumza katika baraza hilo, alisema wizara yake inasimamia taasisi zote za kiimani na kutaka viongozi wa dini wasaidie kuwafichua wanaofanya uovu kwa kisingizio cha dini.
Alisema mtu akifanya kosa asihukumiwe kwa dini au imani yake, bali liwe kosa la mtu husika ili kuendelea kuifanya nchi kuwa ya dini mbalimbali na yenye uhuru wa kuabudu.
“Ikitokea Idd hata kule bungeni huwa tunashiriki, hii suti si ya jana, hivyo tusaidiane kuwafichua wanaofanya uovu na kusababisha makosa, lawama na taswira ziende kwenye taasisi zilizotukuka na taasisi tukufu,” alisema Mwigulu.
Aidha, alitoa mabati 1,500 mwaka juzi na mwaka huu kwa ajili ya misikiti iliyofikia hatua ya kupauliwa na kama bado ipo kwenye misingi, aliahidi kutoa saruji.
Pia alisema alikutana na viongozi wa Kiislamu mjini Dodoma na kuzungumza suala la usafiri na kuahidi kuwapatia gari kwa shughuli za Bakwata wilayani Iramba. “Sasa niwaambie jambo hilo limekamilika baada ya wiki mbili tumeni dereva tumepata Noah kwa ajili ya Bakwata yetu ya wilaya ya Iramba,” alieleza Mwigulu.
Mufti ahimiza amani, furaha Kwa upande wake, Mufti Shehe Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeiri alisema kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) na maisha yake kwa ujumla yalilenga furaha, amani na umoja wa kuishi kindugu baina ya Waislamu, wasio waislamu na jamii nzima.
Mufti alitaka Waislamu wamuenzi Mtume Muhammad kwa kuacha majungu, fitina na kuishi kwa upendo.
“Umma huu siku hizi kila mtu shehe, si kweli, na si kila shehe anafaa, anayefaa si shehe wa fitina, asiyejua neno gani aliseme wapi, kwenye harusi anatia neno la msiba,” alisema Mufti akizungumzia viongozi kujitathimini kauli zao na kutii mamlaka zilizopo madarakani kwa kuwa kila zama zina namna yake ya uongozi.
Akizungumzia uchumi, aliagiza viongozi wa Kiislamu kufanya kazi badala ya kujificha katika imani akisisitiza mtu akikaa tu bila kazi hapaswi kulalamika hana kitu.
“Mbingu hainyeshi mvua ya dhahabu wala ya fedha, ukiweka mikono juu, Mungu nipe nipe, akupeje umekaa tu,” alieleza. “Fanya kazi usiduseduse tu katika majumba ya watu, unasalimia, fanyakazi acha kula vyakula vya watu kwa kigezo cha kumcha Mungu,” alisema Mufti.
Aliitaka misikiti na madrasa ianzishe vyanzo vya mapato kuepuka kutegemea wafadhili ili kupata mashehe wazuri wenye elimu ya dini na ya dunia badala ya kujingamba kuwa wewe si mtu wa mchezo kumbe hakuna lolote.
Share:

Magufuli kuongoza kikao cha NEC leo

 

KIKAO cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinakutana leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni kikao cha kwanza kuongozwa na Rais John Magufuli tangu achaguliwe kukiongoza chama hicho tawala Julai mwaka huu.

Juzi, Rais Magufuli aliongoza kikao cha Kamati Kuu ambacho kilipaswa kuwa cha siku mbili, lakini kikamaliza kazi zake juzi.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye aliwaambia waandishi wa habari juzi baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu kwamba mapendekezo au hoja zote zilizoibuliwa na wajumbe katika kikao hicho zitawasilishwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kitafanyika jijini Dar es Salaam.

Nape hakueleza hoja na mapendekezo hayo yanayopelekwa NEC, lakini kwa ujumla kikao hicho ndicho chenye uamuzi wa kubariki mapendekezo yanayotoka katika kikao cha Kamati Kuu hivyo inatarajiwa kuwa itafanya maamuzi mbalimbali.

Miongoni mwa hayo ni uteuzi wa mgombea wa ubunge wa Jimbo la Dimani Zanzibar, lakini pia huenda NEC ikabariki uteuzi wa wajumbe wa Sekretarieti ya chama hicho kama yatawasilishwa kwao na Mwenyekiti kutokana na nafasi mbalimbali kuwa wazi.

Naibu Katibu Mkuu Bara, Rajab Luhavi na aliyekuwa Kaimu Katibu wa NEC wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk Pindi Chana hivi karibuni wameteuliwa kuwa mabalozi wakati Nape pia anashikilia wadhifa wa uwaziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo.

Aidha, aliyekuwa Msemaji wa chama, Christopher ole Sendeka mwishoni mwa wiki aliteuliwa na kuapishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, hali inayoashiria kuwa mabadiliko katika Sekretarieti hayaepukiki. 
Aidha, Nape aliwaambia waandishi juzi kuwa ajenda kuu katika kikao hicho cha Kamati Kuu ilikuwa ni tathimini ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Alisema tathimini hiyo ilikuwa ni pana na imefanyika kwa kipindi cha karibu mwaka mmoja ambayo ilifanyika kwa ngazi ya mikoa, wilaya na kata na wamemaliza tathimini na kuipeleka makao makuu ya chama ili kupitiwa na vikao vya maandalizi vya sekretarieti na vikao vingine kisha ikawasilishwa kamati kuu kwa ajili ya kujadiliwa.

Alisema baada ya tathimini hiyo kujadiliwa Kamati Kuu itapelekwa katika kikao cha Halmashauri Kuu leo ambacho ndio chenye maamuzi na kitapitia na kuangalia endapo kuna mambo yaliyopendekezwa na hatua za kuchukua kama mabadiliko na vitu vingine.

“Huu ni utaratibu wa kawaida katika chama chetu kila uchaguzi huwa inafanyika tathimini ambazo hutusaidia sana, kujua wapi tulifanya vizuri na wapi hatukufanya vizuri na mengineyo yote yaliyokuwa sehemu ya ushiriki wa chama katika Uchaguzi Mkuu, na tumekuwa tukifanya hivi katika chaguzi zote hali ambayo imeifanya CCM kuimarika zaidi,” alieleza Nape.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger