Sunday, 17 April 2016

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL TAREHE 17.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
20160417_042648
20160417_042704
20160417_042728
20160417_042742MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL TAREHE 17/4/2016
20160417_042755
20160417_042815
20160417_042832
20160417_042844
20160417_042857
20160417_042907
MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL 17 2016
20160417_042907
20160417_042921
20160417_042934
20160417_042948
20160417_042959
20160417_043012
20160417_043021
20160417_043036
20160417_043047MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL TAREHE 17-4-2016
20160417_043100
20160417_043108
20160417_043120
20160417_043133
20160417_043216
20160417_043228
Share:

Saturday, 16 April 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAISI::YAHUSU TAARIFA YA KUZIMWA KWA DATA KWENYE MAKAMPUNI YA SIMU

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 
Share:

Takukuru kukata rufaa hukumu ya Mhando wa Tanesco

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Siku moja baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kumwachia huru aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, William Mhando, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inaandaa utaratibu wa kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo. 
Aprili 14, mwaka huu Mahakama hiyo ilimwachia huru Mhando na wenzake wanne akiwamo mkewe, Eva na maofisa watatu wa Tanesco; Francis Mchalange, Sophia Misida na Naftali Kisinga waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka ya matumizi mabaya ya fedha. 
Mashtaka mengine yaliyokuwa yakiwakabili ni kughushi  na kuwasilisha nyaraka za uongo kwa mamlaka za Serikali. 
Hata hivyo, washtakiwa hao waliibwaga Takukuru baada ya mahakama kuona kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha tuhuma hizo.
 Akisoma hukumu hiyo kwa niaba ya Hakimu Mkazi Mkuu, Kwey Rusema, Hakimu Hellen Riwa alisema kwa mujibu wa ushahidi, suala la msingi lilikuwa ni mkataba kati ya kampuni ya Santa Clara Supply Limited na Tanesco. 
Alisema katika mkataba, Mhando alikuwa mshtakiwa wa kwanza, akituhumiwa kutumia madaraka yake vibaya kwa kushindwa kutangaza masilahi yake kwa kampuni ya Santa Clara inayomilikiwa na Eva ambaye ni mkewe.
 “Suala la msingi ni kujiuliza ni vipi mshtakiwa huyo alihusika katika utoaji wa zabuni na nani aliyekuwa na uamuzi wa mwisho,” alisema. 
 Taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Tunu Mley ilisema imefikia uamuzi huo baada ya wadau wengi kuhitaji kujua hatua zitakazochukuliwa na chombo hicho baada ya hukumu hiyo. 
“Takukuru inawataka wadau na wananchi kwa ujumla kutambua kwamba ni utaratibu wa kisheria kwamba upande mmoja usioridhika na hukumu iliyotolewa kukata rufaa katika mahakama ya juu,” ilieleza taarifa hiyo.
Baada ya hukumu hiyo juzi, Wakili wa Takukuru, Leonard Swai aliomba Mahakama kuingilia kati.
Share:

Rais Magufuli Aweka jiwe la Msingi ujenzi wa Barabara ya Juu katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela jijini Dar leo

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale akitoa maelezo kwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi ujwenzi wa Barabara ya Juu (FlyOver) kwenye makutano ya Barabara ya Mandela na Nyerere, eneo la Tazara, Jijini Dar es salaam leo.
Share:

MAHAFALI YA KIDATO CHA SITA 2016 SHULE YA TUSIIME SECONDARI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


 WANAFUNZI 469 wa kidato cha Sita Sekondari ya Tusiime ya Tabata jijini Dar es Salaam leo wamehitimu kidato cha Sita katika mahafali yaliyo fanyika shuleni hapo. Pichani ni wahitimu mbali wa kidato cha sita wakiwa katika kusanyiko la mahafali.


 Meza kuu ya mgeni rasmi.
 Wazazi nao wapo wanafuatilia vitu mbalimbali 

Share:

MECHI ZA LEO JUMAMOSI LIGI KUU YA UINGEREZA-EPL APRIL 16 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Tangazo la Kazi Mohammed Enterprises Tanzania limited

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mohammed Enterprises Tanzania limited, agriculture division is now hiring for the below positions. The requirements and criteria for applications are as below:

Assistant Managers and Managers
Field Officers

Graduate in Agriculture with 5 to 8 years of experience working on the farms
Must have strong man management skills
Must be confident, positively aggressive and a hands on person
Must have good communication and interpersonal skills
Must have dealt with unions

Personnel officers :
Graduate in HR with 3-5 years of experience in operational HR role
Must have dealt with CMA and Unions and should be well aware of disciplinary procedures
Computer savvy with communication and translation skills (English)

APPLICATION INSTRUCTIONS:

We are looking for candidates who are ready to work and stay on our agriculture farms.
Interested candidates may send their CV only through recruitment@metl.net 
Female candidates are encouraged to apply.
Only shortlisted candidates will be contacted.
Share:

Manispaa ya Kinondoni Inayoongozwa na UKAWA Yasema Itawalipia Wananchi wake Wote Bima za Afya

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Manispaa  ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, inayoongozwa na Chama cha Demkrasia na Maendeleo (Chadema), chini ya Ukawa imeanza kazi kwa staili ya aina yake baada ya kutangaza neema ya bima ya afya kwa wananchi wa Manispaa hiyo.

Imeahidi kuanzisha mpango maalum ambao kila mwananchi wa Manispaa hiyo atachangia Sh. 40,000 kwa mwaka ili aunganishwe na mpango wa matibabu wa bima ya afya ambao utawawezesha kupata matibabu ya bure katika hospitali mbalimbali.

Mpango huo utaanza kutekelezwa mwezi Juni mwaka huu, huku bajeti ya Manispaa hiyo ikiongezeka kwa asilimia 59 kutokana na kukua kwa mapato ya ndani.

Wazee wa Manispaa hiyo nao wametangaziwa neema ya matibabu bure kwani watapewa kadi maalum zitakazowawezesha kutibiwa hospitali za umma.

Mapato hayo yametokana na ukusanyaji madhubuti katika kodi za majengo, mabango, leseni za biashara, huduma za kuegesha magari, hoteli na ruzuku ya serikali kuu.

Bajeti ya mwaka 2016/2017 katika Manispaa hiyo inafikia Sh. Bilioni 248.47 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka jana ambayo ilikuwa ya Sh. Bilioni 156.24.

Katika bajeti ya mwaka huu kuna ongezeko la Sh. zaidi ya bilioni 92.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob aliwasilisha bajeti hiyo jana jijini Dar es Salaam katika kikao cha Baraza la Madiwani.

Baada ya kuwasilisha bajeti hiyo, Madiwani wote wakiwamo wa upinzani na Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliipitisha kwa kauli moja ili ianze kuwahudumia wananchi.

Akisoma bajeti hiyo, Jacob alitaja ukusanyaji wa mapato ya ndani umeingiza Sh. bilioni 64.28 na kwamba imeongezeka kutoka Sh. bilioni 56.6 za mwaka jana.

Licha ya bajeti ya mwaka huu kulenga kugharamia huduma za matibabu, lakini imelenga kujenga shule ya bweni katika Kata ya Goba kwa gharama ya Sh. milioni 250, ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule, kujenga vyumba vya madarasa na ununuzi wa madawati 30,000.

Kazi nyingine zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa Barabara kuelekea kituo cha daladala cha ya Simu 2000 na Barabara ya Akachube ambazo zimetengewa Sh. bilioni 50.

Kuhusu suala la usafi, Meya Jacob alisema kila Kata itakuwa na gari lake la kuzolea takataka na Manipaa imetenga Sh. 2.2b .
 
Manispaa hiyo ina jumla ya Kata 25 na Sh. bilioni 3.6 zimetengwa kwa ajili ya gharama za kusafirisha takataka.

Aidha, katika bajeti hiyo, Manispaa inatarajia kununua Trekta lenye kijiko kwa ajili ya kutengeneza barabara na zimetengwa Sh. bilioni 1 kwa ajili ya kazi hiyo.

Kazi nyingine za fedha hizo ni kuweka sakafu ngumu katika masoko yote ya manispaa, ili kuondoa adha ya uchafu na matope katika msimu wa mvua na zimetengwa Sh. bilioni 1.65.

Kuhusu vijana na wanawake Manispaa hiyo imetenga Sh. bilioni 4.7 kwa ajili ya kuwakopesha na kila Kata itapata Sh. milioni 200.
Share:

BIBI KIZEE ABAKWA MKOANI SINGIDA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Pichani ni Bibi kizee mwenye umri wa miaka 84 na mkazi wa Kijiji cha Chungu, tarafa ya Ihanja, wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida akiwa amebebwa na mmoja wa ndugu zake wakati akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya mjini Singida kutoa ushahidi katika kesi inayomkabili kijana mmoja mwenye umri wa miaka 32 (jina lake halikupatikana) anayetuhumiwa kumbaka bibi kizee huyo kwa mara ya tatu sasa ndipo walipofanikiwa kumkamata. (Picha Na Jumbe Ismailly)
Share:

BUNGE LATOA UFAFANUZI KUHUSU MKATABA WA LUGUMI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Kumekuwa na taarifa zinazoendelea kupotosha umma na baadhi ya vyombo vya Habari kuwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ilipokuwa ikitekeleza majukumu yake tarehe 5 Aprili, 2016 ililitaka Jeshi la Polisi kuwasilisha Mkataba ulioingiwa Kati ya Jeshi hilo na Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd kuhusu mradi wa Utambuzi wa Alama za Vidole AFIS (Automated Fingerprint Identification System).

Ofisi ya Bunge inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu jambo hili kwamba, taarifa hizo si za kweli na zina lengo la kupotosha umma kutokana na kile kilicho amuliwa na kamati hiyo. 
Ukweli kuhusu jambo hili ni kwamba tarehe 5 Aprili, 2016, kamati hiyo ilikutana na kujadili Taarifa ya Ukaguzi wa hesabu zilizokaguliwa za fungu 28, Jeshi la Polisi kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2014 ambapo kamati pamoja na mambo mengine ilibaini dosari katika utekelezaji wa mkataba huo.

Kutokana na dosari hizo, kamati iliomba Afisa Masuhuli ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuwasilisha maelezo ya kina kwa maandishi kuhusu utekelezaji wa mradi huo kwa Ofisi ya Katibu wa Bunge ili kamati iweze kuchambua na kujadili maelezo hayo kabla ya kupendekeza kwa Bunge hatua zaidi za kuchukua. 
Kufuatia agizo hilo, kamati ilimwandikia pia Katibu wa Bunge taarifa kuhusu agizo hilo tarehe 12 Aprili, 2016 ili kupatiwa maelezo hayo kutoka kwa Afisa Masuhuli.

Aidha, Ofisi ya Bunge ilimwandikia barua Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani tarehe 12 Aprili, 2016 kuwasilsha Taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Kamati Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyotokana na kikao hicho cha tarehe 5 Aprili 2016 kabla ya tarehe 18 Aprili, 2018 kama ilivyoshauriwa na kamati . 
Hivyo ni vyema Umma ukafahamu kuwa kilichoombwa na Kamati ni Maelezo ya utekelezaji wa Mkataba huo na sio Mkataba kama inavyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya Habari ambapo Ofisi ya Bunge iliomba maelezo hayo yawasilishwe kabla ya tarehe 18 Aprili, 2016.
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano Ofisi ya Bunge
DAR ES SALAAM 15 Aprili, 2016.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL TAREHE 16.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
20160416_042203
20160416_042221
20160416_042631
20160416_042657
20160416_042238
20160416_042251
20160416_042310
20160416_042323
20160416_042337
20160416_042348
20160416_042413
20160416_042427
20160416_042439
20160416_042450
20160416_042505
20160416_042517
MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 16,2016
20160416_042535
20160416_042545
20160416_042557
20160416_042607
20160416_042715
20160416_042726
20160416_042738
MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 16 2016
20160416_042747
20160416_042821
20160416_042833
20160416_042927
20160416_042938
MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL TAREHE 16-4-2016
20160416_043000
20160416_043013
MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL TAREHE 16/4/2016
Share:

Friday, 15 April 2016

UEFA UEFA Champions League SEMI FINAL DRAW

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
RATIBA YA UEFA NUSU FAINALI 2016


MAN CITY vs REAL MADRID, ATLETICO vs BAYERN MUNICH
Ratiba ya Nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imepanga na inavyoonekana shughuli itakuwa pevu.
Matajiri wa Jiji la Manchester, Manchester City wanatarajiwa kukipiga dhidi ya Real Madrid wakati wabishi wa Jiji la Madrid, Atletico Madrid watawavaa Bayern Munich.
Mechi za kwanza za hatua hiyo zinatarajiwa kuchezwa Aprili 26 na 27, mwaka huu kisha kurudiana Mei 3 na 4 ikiwa ni katika mchakato wa kuelekea kwenye fainali ya michuano hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa San Siro jijini Milan nchini Italia mnamo Mei 28, mwaka huu.
 
Share:

MAOMBI YA KUJIUNGA NA MASOMO KATIKA NGAZI YA ASTASHAHADA/STASHAHADA CHUO CHA MADINI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

MAOMBI YA KUJIUNGA NA MASOMO KATIKA NGAZI YA 
ASTASHAHADA/STASHAHADA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

CALL FOR APPLICATION INTO CERTIFICATE/DIPLOMA
 PROGRAMMES FOR YEAR 2016/17
Share:

Taarifa Ya Jeshi La Polisi kwa vyombo vya habari Kuhusu Utapeli Wa AJIRA Katika Taasisi Mbalimbali

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Katika siku za hivi karibuni katika maeneo mbalimbali hapa nchini, kumejitokeza makundi ya watu ama mtu binafsi kutumia mwamvuri wa taasisi fulani kujipatia kipato kwa njia za udanganyifu (utapeli) kwa kuwaahidi vijana kwamba watawapatia ajira katika taasisi hizo.

Makundi haya ya kihalifu imebainika kwamba yapo katika maeneo mbalimbali, hivyo, ni suala ambalo linahitaji ushirikiano mkubwa kutoka kwa wananchi ili kukomesha vitendo hivyo. 
Juhudi za makusudi zinaendelea kufanyika na jeshi la polisi ili kuwatia mbaroni watu wote wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kitapeli.

Aidha, kufuatia kuibuka kwa vitendo hivyo, tayari Jeshi la Polisi limewakamata matapeli wawili wakiwa wamekusanya vijana katika mikoa ya Kilimanjaro na Mbeya, uchunguzi dhidi yao unaendelea na pindi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabiri.

Jeshi la Polisi likishirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama, kimsingi, kazi yetu kubwa ni kuhakikisha Tanzania inakuwa na Ulinzi na Usalama imara. 
Tutaendelea  kupambana na makundi haya ya kihalifu na utapeli ili nchi yetu iendelee kuwa salama.

Tunawasihi wananchi kufuatilia taarifa kwenye vyanzo sahihi juu ya jambo lolote wanalotaka kulifanya ili kuepuka utapeli unaoweza kufanywa na baadhi ya watu kwa lengo la kujipatia vipato. 
Aidha, wananchi watoe taarifa kwenye vyombo vya usalama kuhusu tabia na mienendo yoyote wanayoitilia mashaka. 
Jeshi la Polisi na vyombo vingine vyote  vya Ulinzi na Usalama viko imara, makundi ya kiuhalifu na wahalifu wote wajue hawana pa kukimbilia, watakamatwa.

Imetolewa na:
Advera John Bulimba – SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi,
Makao Makuu ya Polisi.
Share:

RAIS MAGUFULI AMPIGA CHINI MHARIRI MKUU WA MAGAZETI YA SERIKALI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali (TSN) Bw. Gabriel Nderumaki.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 14 Aprili, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, imeeleza kuwa Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kuanzia tarehe 18 Machi, 2016.

Kufuatia kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua Bi. Tuma Abdallah kukaimu
nafasi hiyo.

Bi. Tuma Abdallah ni Mhariri Mtendaji Msaidizi wa Magazeti ya Serikali (TSN)

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam-14 Aprili, 2016
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger