Tuesday, 6 January 2026

RAIS MSTAAFU WA DKT. KIKWETE, AZINDUA JENGO LA AFISI YA UHAMIAJI NA MAKAZI YA ASKARI MICHEWENI, MKOA WA KASKAZINI PEMBA


Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(wapili kulia) akipiga makofi pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene(wapili kushoto),Kamishna Jenerali wa Uhamiaji.Dkt.Anna Makakala(wakwanza kulia) na wakwanza kushoto ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar,Hassan Ali Hassan, wakati wa Uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari,wilayani Micheweni,mkoa wa Kaskazini Pemba ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Naibu Kamishna wa Uhamiaji,Tatu Burhani kabla ya uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari,wilaya ya Micheweni,mkoa wa Kaskazini Pemba ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Watatu kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene na wakwanza kulia ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar,Hassan Ali Hassan.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari lililopo wilayani Micheweni, mkoa wa Kaskazini Pemba, watano kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene,watatu kulia ni Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais(SMZ),Hamza Hassan Juma na wanne kulia ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala.Uzinduzi huo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene(wakwanza kushoto) na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dkt. Anna Makakala(watatu kushoto), baada ya kutembelea Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari lililopo wilayani Micheweni,mkoa wa Kaskazini Pemba. Uzinduzi huo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Share:

RAIS MSTAAFU WA DKT. KIKWETE, AZINDUA JENGO LA AFISI YA UHAMIAJI NA MAKAZI YA ASKARI MICHEWENI, MKOA WA KASKAZINI PEMBA


Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(wapili kulia) akipiga makofi pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene(wapili kushoto),Kamishna Jenerali wa Uhamiaji.Dkt.Anna Makakala(wakwanza kulia) na wakwanza kushoto ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar,Hassan Ali Hassan, wakati wa Uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari,wilayani Micheweni,mkoa wa Kaskazini Pemba ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Naibu Kamishna wa Uhamiaji,Tatu Burhani kabla ya uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari,wilaya ya Micheweni,mkoa wa Kaskazini Pemba ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Watatu kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene na wakwanza kulia ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar,Hassan Ali Hassan.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari lililopo wilayani Micheweni, mkoa wa Kaskazini Pemba, watano kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene,watatu kulia ni Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais(SMZ),Hamza Hassan Juma na wanne kulia ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala.Uzinduzi huo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene(wakwanza kushoto) na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dkt. Anna Makakala(watatu kushoto), baada ya kutembelea Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari lililopo wilayani Micheweni,mkoa wa Kaskazini Pemba. Uzinduzi huo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Share:

Monday, 5 January 2026

CHADEMA WAJIFUNZE KUTOKA KITABU CHA HESABU: KUKIRI MAMLAKA SI UDHAIFU, NI HEKIMA INAYOEPUSHA ADHABU NA MAANGAMIZI

Katika kipindi ambacho jamii inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kimaadili na kimfumo, somo la kale kutoka Kitabu cha Hesabu Sura ya 16 limeibuka kuwa dira muhimu kwa Watanzania. Uchambuzi wa tukio la kihistoria la uasi wa Kora, Dathani, na Abiramu unatoa onyo kali: Kukataa mamlaka zilizopo si tu kukiuka utaratibu wa nchi, bali ni kualika hukumu ya kimungu na maangamizi.

Kitabu cha Hesabu kinaelezea kwa kina jinsi Kora na wenzake walivyojitokeza kupinga uongozi wa Musa na Haruni. Kwa nje, walionekana kana kwamba wanatetea haki na usawa wa jamii, wakidai kuwa kila mtu ni mtakatifu. Hata hivyo, maandiko yanabainisha kuwa ndani yao kulikuwa na sumu ya kiburi na kiu ya madaraka yasiyo ya halali.

"Uasi huu haukuwa tu dhidi ya binadamu, ulikuwa ni uasi dhidi ya 'God’s Order' (Utaratibu wa Mungu). Mungu ni Mungu wa mpangilio, na anapoweka mamlaka, anategemea nidhamu na utii ili kulinda amani ya wengi," anasema mchambuzi wa maandiko.

Moja ya mambo ya kusikitisha katika simulizi hiyo ni pale Musa alipojaribu kuwaita wapinzani wake (Dathani na Abiramu) ili wazungumze kwenye meza moja ya maridhiano. Kwa dharau, walijibu: "Hatuji!" Msimamo huu wa kukataa mazungumzo na kudharau mamlaka ndio uliopasua mlango wa hukumu. Matokeo yake, ardhi ilipasuka na kuwameza wote waliohusika na uasi huo. 

Hii ni fundisho kwa Watanzania wa leo; kwamba kukaa kwenye meza ya mazungumzo na kukiri mamlaka si udhaifu, bali ni hekima ya kiroho inayookoa taifa dhidi ya machafuko.

Ili taifa liendelee, ni lazima kuwe na msingi wa kuheshimiana kati ya viongozi na wananchi: Kukiri mamlaka kunajenga nidhamu na kuzuia "hukumu ya pamoja" inayoweza kuikumba jamii pale uasi unapotawala. Ni lazima kutofautisha kati ya kutoa maoni kwa staha na kufanya uasi kwa nia ya kubomoa. Hayo yanatokana na ukweli kuwa Mfumo wa Mungu unamtaka kiongozi kuwa na moyo kama wa Musa—moyo wa unyenyekevu na utayari wa kusikiliza malalamiko ya watu kabla hayajazaa chuki.

Ukisoma kitabu hicho unang'amua kwamba amani, uwajibikaji, na haki haviwezi kupatikana kupitia mivutano na uasi. Badala yake, vinapatikana pale kila mmoja anapokubali mfumo sahihi uliowekwa na Mungu na sheria za nchi.

"Tunahitaji umoja zaidi ya hapo awali. Unapokataa mamlaka, unachallenge msingi wa utulivu wa taifa. Hukumu ya uasi si lazima iwe ardhi kupasuka, inaweza kuwa kupotea kwa amani, kusimama kwa maendeleo, na kuvunjika kwa misingi ya kijamii," anaongeza mchambuzi huyo.

Watanzania wanahimizwa kuachana na kiburi cha moyoni kinachochochea uasi.  Kukiri mamlaka ni ukomavu. Ni ujasiri wa kutambua kuwa sote tunahitajiana chini ya mwavuli mmoja wa uongozi ili kufikia nchi ya ahadi. Tuwe na hekima, tuepuke uasi, na tuchague meza ya mazungumzo kwa ajili ya mustakabali wa taifa letu. Kwa kufanya hivyo, tunaepuka laana ya maangamizi na kuvuta baraka za Mungu juu ya nchi yetu.

"Hekima ya kweli ni kujua kuwa uasi una mwisho wa mauti, lakini utii na maridhiano huleta uzima."

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 5,2026



Magazeti






















Share:

Sunday, 4 January 2026

SH MILIONI 500 ZA RAIS SAMIA KWA TAIFA STARS NI UWEKEZAJI, SI MATUMIZI

Hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa zawadi ya Shilingi milioni 500 kwa timu ya Taifa, Taifa Stars, baada ya kufuzu hatua ya 16 bora ya AFCON, imeibua mijadala mipana miongoni mwa wananchi. Wakati baadhi wakitazama zawadi hiyo kama matumizi ya ziada, uchambuzi wa kina wa kiuchumi na kijamii unaonesha kuwa huu ni uwekezaji muhimu katika kugeuza mpira wa miguu kuwa ajira rasmi badala ya kuishia kuwa burudani ya msimu pekee.

Dunia ya sasa inaitazama michezo kama sekta ya uzalishaji inayochangia kwa kiasi kikubwa katika Pato la Taifa kupitia mnyororo wa thamani. 

Zawadi hii ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatuma ujumbe mzito kwa vijana nchi nzima kuwa soka ni taaluma inayoweza kumhakikishia mchezaji kipato na heshima, sawa na udaktari au uhandisi. 

Kwa kuwapa wachezaji uhakika wa kipato, tunajenga mazingira ya wao kuanza kuishi kama wataalamu (professionals), jambo ambalo ndilo msingi wa mataifa makubwa ya soka duniani kama Senegal na Nigeria ambapo wachezaji wao ni bidhaa zenye thamani ya mamilioni ya dola katika soko la kimataifa.

Katika upande wa diplomasia ya michezo, mafanikio ya Taifa Stars yanaitangaza Tanzania kwa kasi kuliko kampeni nyingine yoyote ya masoko. Kila mara timu yetu inapoingia uwanjani katika michuano ya kimataifa, bendera ya nchi inapepea mbele ya mabilioni ya watazamaji, jambo ambalo ni tangazo la bure kwa utalii na fursa za uwekezaji nchini.

Thamani ya matangazo hayo (Global Exposure) ni kubwa mara dufu kuliko kiasi kilichotolewa, kwani inajenga taswira ya taifa lenye ushindani na linaloinukia kiuchumi.

Vilevile, uwekezaji huu unaongeza thamani ya wachezaji wetu katika soko la usajili. Wachezaji wanapofanya vizuri na kupata hamasa, wanavutia maskauti wa klabu kubwa duniani, jambo ambalo linamaanisha kuongezeka kwa fedha za kigeni zinazoingia nchini kupitia mikataba yao. Hali hii inapunguza mzigo wa serikali katika kutengeneza ajira rasmi, kwani sekta ya michezo inaanza kufyonza maelfu ya vijana wenye vipaji kuanzia ngazi ya vijiji hadi taifa.

Pia ni muhimu kutambua kuwa fedha hizi zinachochea hamasa kwa kizazi kijacho. Mtoto aliyepo kijijini akiona juhudi za wachezaji zinatambuliwa na Mkuu wa Nchi, anapata ari ya kufanya mazoezi kwa bidii ili na yeye aifikie hatua hiyo. Huu ni uwekezaji katika rasilimali watu unaolenga kutengeneza "Kiwanda cha Vipaji" ambacho miaka ijayo kitachangia kukuza mzunguko wa fedha kupitia mauzo ya vifaa vya michezo, huduma za tiba za wanamichezo,  biashara za habari na uchambuzi.

Kwa kuhitimisha, wakati serikali ikiendelea na miradi ya kimkakati kama barabara, elimu, na afya kupitia bajeti yake kuu, kutenga kiasi hiki kwa ajili ya Taifa Stars ni sehemu ya mikakati ya kukuza sekta binafsi na kuliingiza taifa katika uchumi wa kisasa wa michezo. Hii si kuchezea fedha, bali ni kuweka mbegu itakayozalisha matunda ya kiuchumi, kidiplomasia, na kijamii kwa miaka mingi ijayo, huku ikiondoa dhana ya soka kuwa jambo la bahati nasibu na kulifanya kuwa biashara kamili na ajira ya kudumu.

Share:

TAHADHARI: ‘UTANDAWAZI NI CHUI’, TUJILINDE NA UTEKAJI WA AKILI NA FIKRA

 

Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na mjadala mzito kwenye mitandao ya kijamii nchini, ambapo baadhi ya watu wameonekana kushabikia vitendo vya mataifa makubwa, hususan Marekani, kuvamia mataifa mengine huru na kuwaondoa madarakani viongozi waliochaguliwa na wananchi wao. 

Hali hii imeibua maswali mazito kuhusu uzalendo wa baadhi ya Watanzania na uelewa wao wa siasa za kimataifa (Geopolitics), huku ikionekana wazi kuwa uvamizi huo mara nyingi hulenga kulinda maslahi ya taifa mvamizi na si demokrasia kama inavyodaiwa.

Wachambuzi wa mambo wameonya kuwa, kutoa sapoti kwa mataifa makubwa yanapovunja sheria za kimataifa ni ishara ya "kutekwa kiakili." Katika muktadha huu, msanii na mshairi wa kisasa, Lwaga Mwambande, ameibuka na shairi lenye tahadhari nzito kwa jamii, akisisitiza kuwa utandawazi na teknolojia vimekuwa silaha mpya zinazotumiwa na "adui" kuteka fikra za watu bila wao wenyewe kujua.

Sanaa ya Mwambande na Utekaji wa Akili

Kupitia shairi lake maarufu la “Tunatekwa Hatujui”, Mwambande anatumia lugha ya picha kuonya jinsi ambavyo binadamu wa sasa anavyopoteza uwezo wa kufanya maamuzi huru. Anasema:

“Tunatekwa hatujui, tunategwa hatujui, tunashikwa hatujui, akili ituingie.”

Mshairi huyu anaufananisha utandawazi na "chui" mwenye makucha ya "buibui," akimaanisha kuwa ni mfumo uliotengenezwa kwa ufundi mkubwa wa kunasa akili za watu kupitia runinga, vishikwambi, na simu janja. Kwa mujibu wa Mwambande, wakati watu wakisherehekea picha, vichekesho, na michezo ya kubashiri (kubeti) kwenye mitandao, wanashindwa kutambua kuwa muda wao na uwezo wao wa kufikiri unateketezwa.

Jiopolitiki na Maslahi ya Mataifa Makubwa

Kushabikia uvamizi wa taifa huru kwa kisingizio cha kuleta mabadiliko ni kukosa uelewa wa historia. Wanataaluma wanabainisha kuwa uvamizi wa kijeshi na kuingilia siasa za mataifa mengine mara nyingi hufuatiwa na uporaji wa rasilimali na kudhoofisha uhuru wa kiuchumi.

Mwambande anatoa tahadhari kuwa "adui" huja kwa namna ambayo hatumtambui, tukijiona hatuugui wakati akili zetu zimeshazidiwa. Katika beti zake, anauliza:

“Kaenda huko adui, ajua hatutambui, twaona hatuugui, akili ituingie.”

Hii ni sawia na wale wanaoshangilia machafuko yanayopandikizwa na mataifa ya nje, wakidhani ni ukombozi, kumbe ni mtego wa kutawaliwa upya kiakili na kiuchumi.

Wito wa Uzalendo na Fikra Huru

Ili kukabiliana na changamoto hizi, makala za wanataaluma na mashairi ya Mwambande yanapendekeza kuimarisha elimu ya fikra huru. Ni lazima Watanzania wajifunze kulinda maslahi ya ndani na kuhifadhi tamaduni zao badala ya kuwa mashabiki wa kila kinachotoka nje, hata kama kina madhara kwa amani ya dunia.

Mwambande anahitimisha kwa uchungu akisema kuwa tunacheka na vichekesho visivyotatua shida zetu, na kusoma vitabu hatutaki, jambo linalotufanya tubaki tukiwa "hatukui."

Ni wazi kuwa, katika ulimwengu huu wa utandawazi, silaha kubwa ya kujilinda si bunduki pekee, bali ni "Akili." Kama taifa, tunapaswa kuwa macho na wale wanaotaka kutugawa na kutufanya tushabikie uharibifu wa mataifa mengine, kwani gharama ya kupoteza amani na uhuru ni kubwa, na mara nyingi huanza kwa kutekwa kwa akili.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 4,2025


 GG
Share:

Saturday, 3 January 2026

SHAMRASHAMRA ZA MWAKA MPYA 2026: AMANI YA TANZANIA YASHINDA CHOKOCHOKO NA MAANDAMANO

Watanzania wameuanza mwaka mpya wa 2026 kwa kishindo cha furaha na amani ya kipekee ikiwa ni kielelezo cha wazi kuwa taifa hili ni kisiwa cha utulivu kisichoweza kutikiswa na chokochoko za kisiasa wala shinikizo la maandamano yasiyo na tija kupitia mitandao. 

Katika kila kona ya nchi kuanzia fukwe za Coco Beach jijini Dar es Salaam hadi viwanja vya Mwanga Community Center mkoani Kigoma na Nyerere Square jijini Dodoma wananchi wameonekana kuburudika kwa tabasamu na upendo wakidhihirisha ushindi dhidi ya mipango ya vurugu iliyokuwa ikipigiwa upatu hapo awali na watanzania wanaoishi na kula bata ughaibuni kupitia machafuko nchini Tanzania. 

Hatua hii ya wananchi kudharau na kubeza shinikizo la maandamano imetoa ujumbe mzito kuwa watanzania wa leo wanathamini amani kuliko mizozo na wameamua kushirikiana na serikali yao kuhakikisha hali inabaki kuwa shwari ili waendelee kufurahia matunda ya uwekezaji na ukuaji wa uchumi wa nchi yao.

Serikali imedhamiria kwa dhati na inaendelea kutekeleza wajibu wake wa kimsingi wa kulinda usalama wa raia na mali zao huku wananchi nao wakitekeleza wajibu wao wa kizalendo kwa kukataa kujiingiza katika mitego ya chuki na ukatili wa kisiasa mitandaoni. 

Taswira iliyojitokeza katika fukwe za Coco Beach inadhihirisha mshikamano wa hali ya juu ambapo wakazi wa Dar es Salaam na viunga vyake walijumuika kwa wingi pasipo hofu yoyote wakithibitisha kuwa Tanzania salama inasonga mbele kwa kasi ya ajabu. Hali kadhalika mkoani Mwanza na Kagera wananchi wameupokea mwaka kwa umoja na nidhamu huku wakazi wa Geita wakionyesha kuwa sehemu ya amani ya Tanzania kwa kuukaribisha mwaka mpya kwa utulivu uliopitiliza jambo linaloongeza imani kwa wawekezaji na watalii kuwa nchi hii ni sehemu salama zaidi duniani.

Ni vyema ikaeleweka kuwa amani tunayoiona si jambo la bahati mbaya bali ni matokeo ya utawala bora na umakini wa viongozi katika kusimamia haki na maslahi ya wote jambo ambalo limejenga imani kubwa kwa wananchi. 

Pamoja na furaha hiyo bado kuna haja ya kuimarisha maeneo ya starehe kama fukwe za Coco Beach kwa kuongeza mazingira ya kisasa ikiwemo maeneo ya watoto na huduma za mtandao ili kukuza zaidi utamaduni huu wa amani na utulivu. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuendelea kuwa mlinzi wa amani ya mwenzake na kuepuka ukatili wa kisiasa mitandaoni ambao unalenga kupandikiza chuki kati ya vijana wasanii na makundi mbalimbali ya kijamii kwani umoja wetu ndiyo fahari ya kizazi cha sasa na urithi wa vizazi vijavyo.

Kusherehekea mwaka mpya kwa amani kumezima kabisa sauti za wachache waliotaka kurudisha nyuma maendeleo ya taifa kupitia machafuko na badala yake kumeleta matumaini mapya ya ustawi wa jamii katika mwaka mzima wa 2026. 

Kwa utulivu huu wananchi wametoa onyo kwa wale wote wanaoendelea kupandikiza mbegu ya chuki mtandaoni kuwa watanzania wameshashtuka na hawatakuwa tayari kufuata mkumbo wa kuvunja amani kwa kisingizio chochote. 

Hakika mwaka huu uwe ni wa upendo na mshikamano ambapo kila tone la furaha lililoonekana katika sherehe hizi liwe ni chachu ya kufanya kazi kwa bidii huku tukilinda amani yetu ambayo ni ngao ya usalama na dira ya kuelekea Tanzania yenye mafanikio makubwa zaidi kimataifa.

Share:

CHIKAMBO AKAGUA MIUNDOMBINU KOROFI MASONYA TARURA YATOA AHADI YA SULUHISHO LA HARAKA

Mbunge viti maalum Tunduru Sikudhani Yassin Chikambo akiwa na meneja wa TARURA Wilaya ya Tunduru Mhandisi Kweka wakiwa wanakagua kivuko cha Masonya chenye changamoto kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo 

Na Regina Ndumbaro Tunduru-Ruvuma 

Mbunge wa viti maalumu kutoka Wilaya ya Tunduru, mheshimiwa Sikudhani Yassin Chikambo amefanya ziara ya kukagua miundombinu korofi katika kata ya Masonya akiwa ameongozana na meneja wa TARURA Wilaya ya Tunduru, Mhandisi Kweka. 

Ziara hiyo imelenga kujionea changamoto zinazowakabili wananchi, hususani katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha mara kwa mara wilayani humo.

Katika ziara hiyo  Sikudhani Chikambo ametembelea kivuko cha Masonya ambacho kimekuwa kero kubwa kwa wakazi na wakulima wa kata hiyo. 

Kivuko hicho kimeripotiwa kusababisha madhara makubwa kwa wananchi, hasa wakati wa mvua nyingi, hali inayokwaza shughuli za kiuchumi na usafiri wa wakazi wa eneo hilo.

Aidha, pia Chikambo ametembelea kijiji cha Nakayaya Mashariki (Misufini) ambako kuna changamoto kubwa ya barabara inayokatiza katika bonde hatarishi. 

Bonde hilo limeendelea kupanuka kutokana na mvua za mara kwa mara, hali inayohatarisha usalama wa wananchi na kuathiri mawasiliano ya barabara katika eneo hilo.

Chikambo ameambatana na katibu wa siasa na uenezi wa CCM wilaya ya Tunduru, Komredi Yanini Stambuli, pamoja na diwani wa kata ya Masonya, Saidi Bwanali. 

Kwa upande wake, meneja wa TARURA, Mhandisi Kweka, amesema amejionea changamoto hizo na kusisitiza kuwa ofisi yake itaanza kuchukua hatua mara moja ili kuboresha miundombinu hiyo na kuchagiza maendeleo ya wananchi wanaoathirika moja kwa moja na hali ya barabara na vivuko hivyo.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger