Sunday 1 August 2021

Picha : BITEKO AFUNGA MAONESHO YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA....ATANGAZA KUZINGUA WALIOSHIKILIA LESENI ZA UCHIMBAJI

...

Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko akizungumza wakati akifunga Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko leo Jumapili Agosti 1,2021 amefunga Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yaliyoanza Julai 23,2021 katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga yakiongozwa na kauli mbiu “Uwekezaji wa Madini na Viwanda Shinyanga kwa Uchumi Endelevu”.

Akizungumza wakati wa kufunga Maonesho hayo, Biteko amewataka Wawekezaji walioshikilia leseni za uchimbaji madini kuendeleza na kuwazuia wananchi wenye uwezo wa kuchimba kuendeleza maeneo hayo na kwamba Serikali imewapa siku 60 baada ya hapo itafuta leseni hizo.

Amesema kumekuwapo na tatizo kwa baadhi ya wawekezaji wa madini kuhodhi lesseni kwa muda mrefu na kutozitumia na pale yanapovumbuliwa madini na wachimbaji wadogo ndipo hujitokeza na kudai eneo hilo ni lao.

Kufuatia hali hiyo, Biteko amesema wametoa siku 60 za kutaifisha leseni za uchimbaji wa madini zilizohodhiwa na wawekezaji kwa muda mrefu bila kuzitumia akibainisha kuwa Serikali imedhamiria kuinua Sekta ya Madini, pamoja na kumaliza migogoro yote ambayo hujitokeza baina ya wachimbaji wadogo na wakubwa.

"Naomba mfikishe salamu kwa wawekezaji wa madini ambao wana leseni za uchimbaji na hawazitumii, tumetoa siku 60 tu zianze kutumika, zaidi ya hapo tunazitaifisha na kutoza gharama ambazo Serikali imeingia kutokana kutolipiwa kodi kwa muda mrefu na kusababisha Serikali kukosa mapato  na fedha hizi lazima zilipwe hatutakuwa na msalia mtume, hatutaki migogoro ya uchimbaji madini," amesema Biteko.

Biteko pia amewataka wachimbaji wenye Leseni walipe kodi na waepuke vitendo vya utoroshaji madini akibainisha kuwa atakayetorosha madini atakuwa anachoma madini kwa tochi hivyo akikamatwa hatabaki salama.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini mkoa wa Shinyanga 'Shinyanga Region Miners Association – SHIREMA', Hamza Tandiko amezishukuru Taasisi za Kifedha kwa kuanza kuwapatia mikopo Wachimbaji wa Madini huku akiomba serikali kupeleka Umeme wenye nguvu ya kuendesha mitambo kwenye maeneo ya machimbo kwani umeme uliopo sasa ni kwa ajili ya mwanga tu.

Kwa upande wake, Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Said Pamui ambao ni miongoni mwa Wadhamini wakuu wa Maonesho hayo, amesema taasisi za kifedha ikiwemo Benki ya CRDB zimeanza kuwezesha mikopo vikundi vya Wachimbaji wa Madini na Wajasirimali hivyo kuwakaribisha kupata huduma katika Benki yao ambayo pia inatoa Bima za aina mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Philemon Sengati amesema maonesho hayo yamesaidia kuutangaza Mkoa huo na kuonyesha fursa za biashara hasa katika sekta ya madini. 

Amesema wataendelea kuboresha maonesho na kuwaunganisha wafanyabiashara na wajasirimali akiongeza kuwa Maonesho hayo ni muhimu kwa sababu mkoa wa Shinyanga una madini mengi na una madini ya pekee ya Almasi ambayo yanaendelea kuchochea ukuaji wa uchumi taifa.

"Kupitia maonesho haya washiriki wamepata fursa ya kutambulisha biashara zao, kuuza bidhaa na kujifunza teknolojia ya kisasa na kujua wapi wapate mitaji",amesema.

Hata hivyo amesema atakuwa mkali kwa watu wanaotorosha madini na atakayekamatwa atafirisika hivyo kuwataka wachimbaji madini kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

Tazama picha hapa chini
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko akizungumza wakati akifunga Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yaliyoanza Julai 23,2021 katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga leo Jumapili Agosti 1,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko akizungumza wakati akifunga Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yaliyoanza Julai 23,2021 katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga leo Jumapili Agosti 1,2021.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Prof. Idris Kikula akizungumza wakati wa ufungaji Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza wakati wa ufungaji Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko akiwapongeza Wanakwaya wa AICT Shinyanga wakitoa burudani kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Zuwena Omary na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga , Jasinta Mboneko wakicheza na Wanakwaya wa AICT Shinyanga kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yaliyoanza Julai 23,2021
Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Meshack Kulwa akizungumza wakati akifunga Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yaliyoanza Julai 23,2021.
Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini mkoa wa Shinyanga ‘Shinyanga Region Miners Association – SHIREMA', Hamza Tandiko akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Dk. Emmanuel Joseph Makala akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Said Pamui akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Zuwena Omary akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Katibu wa CCM mkoa wa Shinyanga, Donald Magesa akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Mwakilishi wa Mkoa wa Mwanza akizungumza wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Said Pamui ambao ni miongoni mwa Wadhamini wakuu wa Maonesho hayo akionesha zawadi aliyopewa na Kamati ya Maonesho wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Mwakilishi wa Kampuni ya Barrick ambao ni miongoni mwa Wadhamini wakuu wa Maonesho hayo akionesha zawadi aliyopewa na Kamati ya Maonesho wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Wanafunzi wa shule za Little Treasures wakitoa burudani wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Kikundi cha Ngoma cha Mabulo ya Jeshi kikitoa burudani wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Wadau wakifuatilia matukio wakati wa kufunga Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Wanafunzi wa Shule za Hope wakitoa burudani wakati wa ufungaji wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (katikati) akiwa katika Banda la Tume ya Madini Mkoa wa Shinyanga kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yaliyoanza Julai 23,2021 katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (katikati) akiangalia madini ya Almasi katika Banda la Tume ya Madini Mkoa wa Shinyanga kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (katikati) akiwa katika Banda la Wachimbaji Wadogo wa Madini Mgodi wa Mwakitolyo kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Waundaji wa Miundo Michundo ' Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga. Kushoto ni Mwenyekiti wa Shinyanga Best Iron, Kashi Salula akimuomba Waziri Biteko serikali ipeleke umeme wenye nguvu ya kuwasha mitambo kwenye maeneo ya machimbo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini mkoa wa Shinyanga ‘Shinyanga Region Miners Association – SHIREMA', Hamza Tandiko akizungumza wakati Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (katikati) akiwa katika banda la SHIREMA kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini mkoa wa Shinyanga ‘Shinyanga Region Miners Association – SHIREMA', Hamza Tandiko akizungumza wakati Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko akiwa katika banda la SHIREMA kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Mgodi wa Williamson 'Mgodi wa Mwadui' kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (wa tatu kulia) akiwa katika Banda la Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Barrick kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Kampuni ya Barrick kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Mgodi wa ZEMD kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Stamigold kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko na msafara wake wakielekea katika mabanda mbalimbali kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kushoto) akiwa katika Banda la SIDO kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola akielezea huduma zinazotolewa na SHUWASA.
Kushoto ni Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddi akimwelezea Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko huduma zinazotolewa na Benki ya CRDB ambayo sasa ina Akaunti ya HODARI isiyo na makato kwa ajili ya Wajasiriamali kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Kulia ni Meneja wa Benki ya NMB tawi la Manonga, Sebastian Kayaga akimwelezea Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko huduma zinazotolewa na Benki ya NMB alipotembelea banda la NMB kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Kulia ni Meneja wa Benki ya NBC tawi la Shinyanga, Joyce Chagonja akimwelezea Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko huduma zinazotolewa na Benki ya NBC alipotembelea banda la NBC kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la shule za Hope kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kushoto) akiwa katika Banda la TANESCO kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko (kulia) akiwa katika Banda la Kampuni ya Uzalishaji na Uuzaji wa dawa za asili maarufu Faraja Natural Herb Kigoma kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga. Kushoto ni Dkt. Faraja Peter akionesha dawa inayotibu matatizo ya upumuaji.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger