Sunday 28 March 2021

RIPOTI YA CAG YABAINI DOSARI YA MATUMIZI YA FEDHA YANAYOFANYWA NA VYAMA VYA SIASA, TAASISI NA MASHIRIKA YA UMMA

...

 


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Tanzania, Charles Kichere

Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kicheere imeendelea kubaini dosari ya matumizi ya fedha yanayofanywa na taasisi na mashirika ya umma pamoja na vyama vya siasa.

CAG amesema kati ya hati 900 alizozikagua, hati 800 sawa na asilimia 87 zinaridhisha huku hati 81 zikiwa na mashaka na mbaya ni 10.

Kichere ameyasema hayo leo Jumapili, Machi 28, 2021 wakati akikabidhi ripoti aliyoifanya kwa taasisi za Serikali Kuu, mamlaka ya serikali za mitaa, mashirika ya umma, miradi ya maendeleo na vyama vya siasa kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ulioishia Juni 30, 2020.

“Tumeongeza mashirika 10 ambayo tunayakagua na nimeshirikiana na makampuni mengine binafsi kuhakikisha tunakagua ipasavyo pia tumefanya kaguzi za kitaalamu SGR, miundombinu mabasi yaendayo haraka, barabara kuu Morogoro, Kibaha, miradi ya maji wilaya ya Same na Korogwe,” amesema.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger