Friday, 8 July 2016

Taarifa ya marekebisho katika majina ya Wakurugenzi yaliyotolewa leo Julai 7, 2016

...

Tunapenda kufanya marekebisho madogo katika majina yaliyopo kwenye orodha ya wakurugenzi wa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya ambapo Dkt. Leonard Moses Massale ametangazwa kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma.

Jina hilo limeingizwa katika Orodha ya Wakurugenzi wa halmashauri kwa makosa, na kwa sababu hiyo Dkt. Leonard Moses Massale anaendelea kuwa Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza.

Kufuatia marekebisho hayo, uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma utatangazwa baadaye.

AIDHA, tunapenda kutoa ufafanuzi kuwa makatibu tawala wa wilaya wote ambao majina yao yamejitokeza katika orodha ya wakurugenzi wa halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na wilaya, Mhe. Rais Magufuli ameamua kuwabadilishia majukumu na sasa watatumikia vyeo vyao vya ukurugenzi badala ya vyeo vya Ukatibu Tawala wa Wilaya.

Kufuatia mabadiliko hayo, nafasi za Makatibu Tawala wa Wilaya ambao wameteuliwa kuwa Wakurugenzi wa Halmshauri zitajazwa baadaye.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam

07 Julai, 2016
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger