Thursday 28 April 2022

Picha : POLISI SHINYANGA, WAANDISHI WA HABARI WAENDESHA MDAHALO NAMNA YA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP George Kyando akizungumza kwenye mdahalo wa waandishi wa habari mkoani Shinyanga.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

KLABU ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga (SPC), wamefanya mdahalo na Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, katika kujadiliana namna ya kuimarisha mahusiano mazuri na Jeshi hilo hasa wanapokutana kwenye matukio na kila mmoja akitekeleza majukumu yake na kusiwepo na mifarakano pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama kwa pande zote.

Mdahalo huo umefanyika leo Aprili 28, 2022 kwa kukutanisha maofisa wa Jeshi la Polisi ngazi za juu mkoani Shinyanga, pamoja na waandishi wa habari mkoani humo.

 Akizungumza wakati wa kufungua Mdahalo huo,Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga Patrick Mabula, amesema Jeshi la Polisi na waandishi wa habari wanapaswa kuwa na mahusiano mazuri, kwa sababu wanategemeana katika utekelezaji wa majukumu hasa katika matukio ya kiharifu na ajali za barabarani.

“Lengo kubwa la mdahalo huu ni kuboresha mahusiano mazuri kati ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari hasa katika utekelezaji wa majukumu yetu,”amesema Mabula.

Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP George Kyando, amepongeza kufanyika kwa mdahalo huo na kueleza kuwa ni muhimu sana katika kuimarisha mahusiano mazuri baina ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari.

“Waandishi wa habari na Jeshi la Polisi wanafanya kazi sawa, sababu nyie mnategemea kupata taarifa za uhalifu kutoka Jeshi la Polisi na kwenda kuhabarisha umma, na kutusaidia sisi kupunguza uharifu au kuukomesha kabisa kupitia kalamu zenu,”amesema Kyando.

“Nawapongeza sana walioandaa mdahalo huu, ambao ni muhimu sana katika kuimarisha mahusiano mazuri baina ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari, kwa sababu nyie mnafanya kazi sawa na sisi hasa katika kuhabarisha umma juu ya matukio ya uhalifu na kuacha mara moja,”ameongeza.

Katika hatua nyingine Kamanda wa Jeshi la Polisi, amewataka waandishi wa habari mkoani humo, kujenga tabia ya kufika kwenye maeneo ya matukio hasa yale ya karibu, na siyo kutegemea kila kitu kutoka kwa Jeshi la Polisi na kushindwa kupata taarifa ya tukio kwa undani zaidi.

Amesema Jeshi la Polisi linapofika kwenye tukio, huwa halikusanyi taarifa za habari, bali wao huwa wanafika kukusanya ushahidi wa tukio, na kuwataka wabadilike katika utendaji wao kazi wa kukusanya taarifa na kuhabarisha umma.

“Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga tupo pamoja kushirikiana na ninyi waandishi wa habari katika utekelezaji wa majukumu yenu, lakini kwa kuzingatia taratibu na kazi zetu, na pia mbalansi habari zenu hasa za matukio,”amesema Kyando.

Naye Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Shinyanga (RTO) Debora Lukololo, amesema ili waandishi wa habari kuendelea kuwa na mahusiano mazuri na Jeshi la Polisi ni lazima wafanye kazi zao kwa weledi pamoja na kubalansi taarifa zao na kupata usahihi wa tukio na siyo kulirusha na kuleta taharuki.

Nao baadhi ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga, wamesema mdhahalo huo umesaidia kuendelea kuimarisha mahusiano mazuri baina ya waandishi wa habari na Jeshi la Polisi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP  George Kyando, akizungumza kwenye mdahalo huo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga George Kyando akizungumza kwenye mdahalo huo.

Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga Patrick Mabula, akizungumza kwenye mdahalo huo.

Mkuu wa kikosi cha usalama Barabarani mkoani Shinyanga Debora Lukololo akizungumza kwenye mdahalo huo.

Mrakibu msaidizi wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama Barabarani mkoani Shinyanga Analyse Kaika akizungumza kwenye mdahalo huo.

Katibu wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga Ally Litwayi, akizungumza kwenye mdahalo huo.

Mjumbe wa Kamati Tendaji Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga Marco Mipawa, akichokoza mada kwenye mdahalo huo.

Mjumbe wa Kamati Tendaji Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga Marco Mipawa akichangia mada kwenye mdahalo huo.

Mwandishi wa Habari AZAM TV Kosta Kasisi akichangia Mada kwenye mdahalo huo.

Mkurugenzi mtendaji wa Malunde 1 blog Kadama Malunde akichangia hoja kwenye mdahalo huo.

Mwandishi wa habari wa Gazeti la Nipashe wilayani Kahama Shabani Njia, akichangia hoja kwenye mdahalo huo.

Maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Mwandishi wa Nipashe wilayani Kahama Shabani Njia akiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakiwa kwenye mdahalo huo.

Viongozi na wajumbe wa Kamati Tendaji Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakipiga picha ya pamoja na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo George Kyando na maofisa wa Jeshi hilo mkoani Shinyanga.

Viongozi na wajumbe wa Kamati Tendaji Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakipiga picha ya pamoja na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo George Kyando na maofisa wa Jeshi hilo mkoani Shinyanga.

Waandishi wa habari mkoani Shinyanga wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mdahalo huo.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA.
Share:

Picha : VIONGOZI WA VYAMA VYA USHIRIKA SHINYANGA WAPATIWA MAFUNZO, RAS ATAKA WAWE WAAMINIFU, WAAJIRI WATENDAJI WENYE SIFA


Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga leo Alhamisi Aprili 28,2022 katika ukumbi wa SHIRECU Mjini Shinyanga. 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Serikali ya Mkoa wa Shinyanga imewataka viongozi wa Vyama vya Ushirika kuwa waaminifu katika kulipa wakulima bei stahiki na kujitahidi kudhibiti ubora wa mazao, usafi wa mazao na vipimo sahihi wakati wa kuuza mazao ili yaweze kupata bei nzuri.


Hayo yamesemwa leo Alhamisi Aprili 28,2022 na Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika (Madini, pamba na tumbaku) mkoa wa Shinyanga yenye lengo la kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya usimamizi wa Ushirika, kujiendesha kibiashara na Maadili ili waweze kufanya shughuli zao vizuri.


Omary ameshauri pia mazao yaliyopo kwenye Ushirika ambayo ni Pamba, Korosho,Mkonge na Tumbaku yapangwe katika madaraja sahihi ili kumrahisishia mnunuzi kutoa bei nzuri zaidi kuliko kuchanganya.

“Hivi sasa tunaelekea msimu wa masoko kwa mazao ya pamba na tumbaku. Niwaombe tujaribu kusimamia masoko yetu vizuri ili kuhakikisha changamoto za msimu uliopita hazijirudii.Tuweke mifumo mizuri ya uuzaji za ulipwaji wa pesa zetu hasa upande wa vyama vya pamba,tuachane na malipo ya pesa taslimu yatatuchelewesha maendeleo na kutusababishia migogoro ya upotevu na wizi wa pesa za pamba”,amesema Omary.

“Pia tuimarishe zaidi usimamizi wa vyama vya ushirika kwa kuajiri watendaji wenye sifa badala ya kuleana na kubebana. Hili naomba sana Mrajis Msaidizi wahimize Maafisa Ushirika wako wavielekeze vyama kuajiri watendaji wenye sifa ambao wana uwezo wa kutuvusha na kutufikisha mahali tunapopatarajia kufika la sivyo vyama hivi havitabadilika”,ameongeza.

Amebainisha kuwa serikali inahitaji kuona vyama vya ushirika vikijiendesha na kusimamiwa vizuri kwa misingi ya Ushirika badala ya kufanya mambo kwa mazoea.

Aidha amewahimiza wana ushirika kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kufanya kazi kwa bidii na kulima kilimo chenye tija na kilimo cha kisasa kuachana na kilimo cha mazoea kwani serikali inaendelea kutoa fursa mbalimbali za kumkomboa mkulima ikiwemo kutoa dawa na mbegu bure,kuboresha huduma za ugani kwa kugawa vitendea kazi kwa maafisa ugani nchi nzima na benki kupunguza riba kwenye kilimo.

Katika hatua nyingine amevitaka Vyama vya Ushirika kuhakikisha vinachagua viongozi wenye uwezo kwa kufanya kazi kwa misingi ya utawala bora badala ya kufanya kazi kwa mazoea huku akisisitiza kuwa viongozi hao wanatakiwa kuwa wenye maono,wabunifu na kuwea kuzitunza na kuzilinda mali za wana ushirika na siyo kuhujumu mali hizo.

“Kwa sasa mkoa wa Shinyanga una jumla ya maafisa ushirika 7 katika halmashauri sita lakini Ofisi ya Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa anayesimamia vyama 452 vya mkoa mzima hana hata afisa ushirika wa kumsaidia kakzi kwenye ofisi yake. Suala hili serikali kupitia Wizara ya Kilimo inaendelea kulitafutia ufumbuzi ili kuwa na idadi ya watumishi wanaotakiwa”,amesema.

“Jukumu la kuubadilisha ushirika wetu siyo la mtu mmoja ni letu sote. Jukumu hili siyo la Mrajis Msaidizi mkoa pekee lazima tusaidiane naye kuhakikisha mipango iliyowekwa na Tume ya maendeleo ya Ushirika pamoja na maono ya wana ushirika tunasaidiana kuyatekeleza kwa pamoja na kwa umoja wetu. Na huo ndiyo ushirika wenyewe na hiyo ndiyo dhana ya ushirika”,ameongeza Omary.


Naye Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace amesema mafunzo hayo kwa Wajumbe wa bodi yanatarajiwa kuleta tija kwa kuonesha mabadiliko chanya kwa viongozi wa vyama vya ushirika katika maeneo wanayoyasimamia.

“Mafunzo haya yana lengo la kukumbushana wajibu na mipaka ya vyama vya ushirika,kubadilishana mawazo,kuwakutanisha na wadau wa sekta ya kilimo ili kuonesha fursa zilizopo kwani tunataka vyama vya ushirika vinakuwa endelevu”,amesema Boniphace.

“Tunataka Ushirika uwe imara na ujiendeshe kibiashara. Tunashukuru viongozi wa vyama vya ushirika wamehudhuria mafunzo haya kwa wingi tofauti na matarajio yetu hii inaonesha ni kiasi gani wanataka mabadiliko katika kuboresha utendaji kazi wao”,amesema.


Mkoa wa Shinyanga una jumla ya vyama vya Ushirika vya Msingi 457 vyenye jumla ya wana ushirika 46,395. Pia kuna vyama vya Upili vitatu vinavyojumuisha Union mbili za SHIRECU LTD na KACU LTD vyenye jumla ya vyama wanachama na mkoa una jumla ya SACCOS 7 tu ambazo zimepata leseni kati ya SACCOS 20 zilizokuwepo hapo awali.


ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga leo Alhamisi Aprili 28,2022 katika ukumbi wa SHIRECU Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga leo Alhamisi Aprili 28,2022 katika ukumbi wa SHIRECU Mjini Shinyanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga leo Alhamisi Aprili 28,2022 katika ukumbi wa SHIRECU Mjini Shinyanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zuwena Omary wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga leo Alhamisi Aprili 28,2022 katika ukumbi wa SHIRECU Mjini Shinyanga.
Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace akizungumza kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace akizungumza kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace akizungumza kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace akizungumza kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace akizungumza kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Mwezeshaji Charles Malunde akitoa mada kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Mwezeshaji Charles Malunde akitoa mada kwenye mafunzo kwa Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

POLISI, MAHABUSU WAFARIKI KWA AJALI GEITA



Watu wanne ambao ni askari wa Jeshi la Polisi wawili na mahabusu wawili wamefariki dunia, kwenye ajali iliyotokea katika kijiji cha Ibanda mkoani Geita.

Ajali hiyo imetokea April 27 majira ya saa 10:00 jioni ikihusisha gari la Polisi namba PT 3798 Toyota Landcruiser lililokuwa likitokea Geita kusikiliza kesi mahakamani, kugongana na Lori aina ya Scania namba T 691 DBQ mali ya kampuni ya Nyanza lililokuwa likitokea mkoani Mwanza kuelekea mkoani Geita.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita Henry Mwaibambe ameeleza chanzo cha ajali hiyo kuwa ni gari la Polisi kupata hitilafu.

Mganga Mfawidhi hospitali ya rufaa mkoa wa Geita Dkt. Mfaume Salum amesema alipokea majeruhi watatu na wote wamepatiwa matibabu mmoja anaweza kuruhusiwa.
Share:

Dkt. FIMBO : MTUMIAJI WA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME ATAKUFA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Dkt. Adam Fimbo
**
Mkurugenzi Mkuu wa TMDA Dkt. Adam Fimbo, amesema kwamba watumiaji wa dawa za kuongeza nguvu za kiume wapo kwenye hatari zaidi ya kupoteza maisha kwa sababu dawa hizo hupanua mishipa ya damu.

Dkt. Fimbo, amesema kwamba dawa za kuongeza nguvu za kiume zinaongoza kwa sasa kwa kununuliwa zaidi kwenye maduka makubwa ya dawa nchini.

"Watumiaji wa dawa hizi watakufa kwa sababu zinapanua mishipa ya damu, mishipa ya kichwani ikishapanuka, itapasuka na hivyo mtumiaji wa dawa hizi atakufa tu,"amesema Dkt. Fimbo.

Chanzo - EATV
Share:

HAYA NDIYO MAHARAGE YANAYOONGEZA NGUVU ZA KIUME


Maharage aina ya Jesca

KUTOKANA na kuwa na ongezeko kubwa la wanaume wenye upungufu wa nguvu za kiume tafiti zimeonesha kuwa kuna aina ya maharage yanayopatikana jijini Arusha na Tanzania kwa ujumla ambayo ni suluhisho la tatizo hilo.


Maharage hayo yanafahamika kwa jina la Jesca ambalo kimsingi limetokana na muunganiko wa herufi za kwanza za majina ya vijana wanne ambao waliamua kuungana na kufanya utafiti pamoja na kufanya uzalishaji wa maharage hayo ambayo wanadai yanapatikana kote nchini tena kwa bei ambayo ni rafiki kwa mteja.
Maharage aina hii yanaongeza nguvu za kiume

Vijana hao ni John, Elizabeth, Sostenes, Clement na Alex.

Maharage hayo yameongezwa viini lishe vya madini ya zinki na chuma ambavyo vinasaidia kuongeza uzalishaji wa homoni aina ya testosteroni pamoja na kuongeza damu mwilini,


Licha ya kwamba maharage hayo yamekuwa yakipewa majina mbalimbali kutokana na maeneo husika mathalani majina kama Iringa au Punda, lakini jina halisi ambalo watafiti hao wameliweka wazi kama jina la Kampuni ni JESCA.


Naye mtaalamu kutoka Taasisi ya Lishe Celestin Mgoba amesema maharage ya Jesca yameongezewa kwa wingi madini chuma na madini ya zinki kwa njia ya kilimo ambayo amedai kwa madini chuma ni lazima iwe miligramu 74 hadi 92 kwa kilo moja na zinki iwe miligramu 26 hadi 43 kwa kilo moja.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger