Monday 24 January 2022

WATAALAMU 422 WA TANZANIA BARA, ZANZIBAR WAPATIWA MAFUNZO YA ANWANI ZA MAKAZI


Muonekano picha ya vongozi na wataalam waliopo kwenye vituo vinne vya mikoa ya Mwanza, Mbeya, Tanga na Zanzibar wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jim Yonazi (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya anwani za makazi na postikodi kwa wataalam hao kwa njia ya mkutano mtandao wakati akiwa ofisi za TTCL, jijini Dodoma
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dorosela Rugaiyamu akizungumza kwa njia ya mkutano mtandao (video conference) na wataalam wa Halmashauri mbalimbali za Tanzania Bara na Zanzibar wakati Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Jim Yonazi (aliyeketi kulia)  akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu kwa ajili ya kutekeleza anwani za makazi katika mkutano uliofanyika leo ofisi za TTCL, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jim Yonazi akizungumza kwa njia ya mkutano mtandao (video conference) na wataalam kutoka Halmashauri mbalimbali za Tanzania Bara na Zanzibar wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu hao  ya utekelezaji wa anwani za makazi katika mkutano uliofanyika leo ofisi za TTCL, jijini Dodoma.

***
 
Na Dotto Kwilasa,Malunde 1 Blog, DODOMA.
KATIBU  Mkuu , Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jim Yonazi amefunga mafunzo ya utekelezaji wa anwani za makazi na postikodi huku akiwataka wataalamu hao kwenda kutekeleza mafunzo hayo kwa vitendo kwa kuweka namba za nyumba, majina ya mitaa na barabara kwenye halmashauri wanazotoka.

Dkt.Yonazi amezungumza hayo leo Jijini Dodoma kwenye  mkutano baina yake na wataalamu hao uliofanyika kwa njia ya mtandao(video conference) yaliyofanyika kwenye vituo vinne vya mkoa wa Mwanza, Mbeya, Tanga na Zanzibar na kuongeza kuwa zoezi hilo kinapaswa kutekelezwa nchi nzima na kukamilika ifikapo mwezi Mei mwaka huu.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa anwani za makazi na postikodi utasaidia kufungua kasi ya uchumi, utoaji wa huduma za kijamii kwa wananchi na kuifungua Tanzania kidijitali.

"Mkafanye kazi kwa ufanisi,ikiwa zoezi hili litafanikiwa mwananchi yeyote atatambulika duniani na anaweza kufikiwa na mteja kwa ajili ya kuuza bidhaa au huduma, hivyo kila mwananchi awiwe kuwa na namba ya nyumba, jina la barabara au mtaa anapoishi,” amesema 
 
Mbali na hayo  ametoa wito kwa kampuni, wadau mbali mbali na familia kuchangia utekelezaji wa anwani za makazi na postikodi na kila mmoja awe balozi wa anwani za makazi na wataalam watoe taarifa kwa viongozi wao na Wizara iko tayari kuendelea kushirikiana kutekeleza hili
 
Kwa upande wake  Mratibu wa Kitaifa wa Anwani za Makazi na Postikodi wa Wizara hiyo, Mhandisi Jampyion Mbugi, amesema kuwa wataalam waliopatiwa mafunzo hayo ni wataalam wawili kutoka kwenye kila halmashauri nchi nzima ambapo inahusisha wataalam wa TEHAMA, Ardhi, Mipango Miji na Ramani.

Amesema, wataalamu hao wamepatiwa mafunzo hayo kwa muda wa wiki moja
kuanzia  Januari 17 hadi Januari 23 mwaka huu yanayolenga  utekelezaji wa anwani za makazi na postikodi ikiwemo kuweka namba za nyumba, jina la mtaa au barabara na kuweka taarifa za maeneo hayo kwenye mfumo wa kielektroniki wa NAPA .

"Jambo hili ni muhimu sana kwa kuwa litawezesha  wananchi  kutoka eneo moja kwenda eneo lingine kwa kutumia simu ya mkononi au kompyuta na kutunza muda ,"amefafanua.
 
Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya wataalam wengine waliopatiwa mafunzo hayo, Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Kilindi, Tanga ndugu Anastius Biswalo Manumbu amesema wamepatiwa mafunzo hayo kwa vitendo na wataenda kuwafundisha wataalam wengine ili kuhakikisha kuwa anwani za makazi zinakamilika kwa wakati kuendana na azma ya Serikali .

"Tunawashukuru sana wawezeshaji kwani  tumeiva na sasa tupo tayari kutimiza wajibu wetu kwa vitendo na tutazingatia miongozo iliyopo ya uwekaji wa anwani za makazi na postikodi,"ameeleza.
 
Ufungaji huo wa mafunzo ya anwani za makazi na postikodi nchini, umehudhuriwa na viongozi mbali mbali wa vituo vinne ambapo mafunzo hayo yametolewa kwa kuwashirikisha  wawakilishi wa wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa mikoa ya Tanga, Mwanza, Mbeya na Zazibar ambapo kwa upande wa Zanzibar waliongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ndugu Amour Bakari

Aidha katika mafunzo hayo  jumla ya wataalam  422 wamepatiwa mafunzo ambapo wataalam 389 wametoka Tanzania Bara na 33 wametoka Zanzibar .

Share:

MAMA AJITOLEA KUMZALIA MTOTO MWANAE


MAPYA yaibuka! Pichani Maree Arnold (54) kutoka Australia ameamua kumbebea mimba mwanae huyo wa kumzaa Meagan (28) hivyo kumzaa mjukuu wake wa kiume mwenye afya njema tarehe 13 mwezi huu.

Imekuwaje? Meagan akiwa na miaka 17 aligundulika kuwa hana mfuko wa uzazi(uterus) hiyo ina maana kwamba hata period haingii kila mwezi na kamwe asingeweza kuja kubeba mimba na kuzaa, hata hivyo licha ya changamoto hiyo lakini madaktari waligundua bado ovaries zake zinafanya kazi hivyo baadaye akiamua bado anaweza kupata mtoto wake mwenyewe (biological child) ikiwa atatokea mwanamke mwingine wa kumsaidia kumbebea mimba.

2015 akakutana na jamaa pichani ambaye kwasasa ni mumewe, jamaa alipojua changamoto za mkewe wakakubaliana watafute mwanamke wa kuwasaidia kuwabebea mimba (surrogate) ambapo alipatikana nchini Canada kupitia agency flani, mimba ilibebwa na surrogate lakini mtoto akiwa na wiki 21 akafariki kisha janga la corona lilipoingia ndio kabisa Meagan akaanza kukata tamaa maana ilikuwa ngumu hata kusafiri nje ya nchi.

Maree alipoona binti yake huyo hana furaha muda mwingi sababu ya kuamini hatakuja kupata mtoto wake mwenyewe maishani, akafanya utafiti kidogo na kuambiwa licha ya kuwa tayari yeye ana miaka 54 na alishazaa watoto 5 lakini bado anaweza kumsaidia kumbebea mimba mwanae huyo wa kumzaa.

Maree alienda hospitali kupandikizwa embryo (kiinitete) kilichotokana na yai la mwanae na mkwe wake, alipandikizwa mara tatu lakini zote haikufua dafu ikashindikana kwa mara ya nne ndio ikakubali.

Kwa umri wake wa miaka 54 Maree tayari alikuwa hedhi imeshakoma(menopause) hivyo kabla ya kupandikizwa mimba hiyo ilibidi madaktari wampe dawa za ku-reverse process ya menopause na kujaribu kuuboresha mfuko wake wa uzazi uweze kubeba mtoto tena.

Maree akizungumza amesema mimba hii ilimfanya achoke zaidi kulinganisha na miaka 22 iliyopita alipobeba mimba ya mwisho ya mtoto wake halisi, lakini amesema amejisikia fahari kumsaidia mwnaae na kama muda ungekuwa unarudi nyuma basi angejitosa kumbebea mwanae mimba ya mtoto mwingine.

Kwa upande wa Meagan kwasasa furaha yake hailezeki baada ya kufanikiwa kuitwa mama kwa mtoto ambaye ni damu yake, aidha, pia amemshukuru sana mzazi wake kumbebea mimba.
Share:

MABASI YASIYO NA DEREVA KUANZA KUFANYA KAZI


NCHI ya Norway imesema inajiandaa kuanza majaribio ya mabasi ya abiria (ya umma) ambayo hayana dereva, kuanzia mweiz Aprili, mwaka huu.

Mabasi hayo ya umeme ambayo yametengenezwa na Kampuni ya nchini Uturuki ya Karsan yana uwezo wa kubeba abiria 50 na yana urefu wa mita 8, siti 21 na eneo kubwa la watu kusimama na kwa sasa yameanza majaribio katika eneo la Forus Business Park kabla ya maeneo mengine.

Wakati wa majaribio kutakuwa na madereva kwenye magari hayo kwa ajili ya kusimamia usalama na kusaidia kuweka vitu sawa kama kutakuwa na changamoto lakini baada ya muda wa majaribio yatakuwa yanasafirisha abiria bila kuwa dereva.

Majaribio hayo yatafanyika kwa muda wa miaka miwili katika majiji, miji na wilaya mbalimbali za nchi hiyo kabla ya kuanza kazi rasmi na kuiongezea Serikali ya nchi hiyo kipato huku ikitarajia kupunguza gharama za uendeshaji.

Majaribio hayo ya kwanza makubwa Barani Ulaya yatafanywa na Kampuni ya Vy kwa kushirikiana na Kampuni ya Kolumbus kwa kutumia teknolojia ya AI (Artificial Intelligence) na sensa kutoka Kampuni ya Adastec na teknolojia ya ufuatiliaji (monitoring technology) kutoka Kampuni ya Norway ya Applied Autonomy.
Share:

AKAA KWENYE MATAIRI YA NDEGE SAA 11 ANGANI


JESHI la Polisi wa Uholanzi wanasema wamempata mtu akiwa hai katika sehemu ya gurudumu la ndege iliyotua katika uwanja wa ndege wa Amsterdam wa Schiphol kutoka Afrika Kusini.

Safari za ndege kutoka Johannesburg hadi Amsterdam huchukua takriban saa 11, huku ndege ya mizigo ikiaminika kusimama mara moja, jijini Nairobi, Kenya.

Si jambo la kawaida sana kwa wanaopanda ndege kimagendo kuishi, kutokana na baridi na oksijeni kidogo kwenye miinuko ya juu. Umri na utaifa wa mwanaume huyo bado haujabainishwa, polisi wanasema.

“Mwanaume huyo alipatikana akiwa hai katika sehemu ya gurudumu upande wa pua ya ndege na alipelekwa hospitalini akiwa katika hali nzuri,” msemaji wa Polisi wa Kijeshi wa Uholanzi Joanna Helmonds aliambia shirika la habari la AFP.

“Inashangaza kwamba mtu huyo bado yuko hai,” alisema.

Kwa mujibu wa mtangazaji wa Uholanzi NOS, joto la mwili wa mtu huyo liliongezeka katika eneo la tukio na wakati gari la wagonjwa lilifika, aliweza kujibu maswali ya msingi.

Msemaji wa idara ya shehena ya mizigo Cargolux alithibitisha katika barua pepe kwa Reuters kwamba mtu huyo alikuwa kwenye ndege inayoendeshwa na Cargolux Italia.

Kulingana na data ya ndege, ndege pekee ya Cargolux ya mizigo kutoka Johannesburg hadi Schiphol Jumapili pia ilisimama Nairobi.

 Haijulikani iwapo mwanaume huyo alipanda ndege hiyo nchini Afrika Kusini au Kenya.
Share:

Sunday 23 January 2022

Video Mpya : NYANDA MADIRISHA OBHADO 'MALIGANYA' - BHUHANGWA


Ninakualika kutazama Video Mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado ' Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo kutoka Kahama mkoani Shinyanga inaitwa Bhuhangwa iliyotengenezwa na Director Manwell. 

Tazama Video hapa chini

Share:

WATOTO WATATU WAFARIKI KWA KULA UYOGA NZEGA



 Katika hali ya kustaajabisha, watoto watatu wa familia moja wamefariki dunia baada ya kudaiwa kula uyoga unaodhaniwa kuwa na sumu katika eneo la Igombanilo, Nzega Mkoani wa Tabora.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amesema waliokula chakula hicho ni mama na watoto wake ambapo mpaka sasa mama na mtoto mmoja wanaendelea vizuri na wameruhusiwa kutoka Hospitali.

Kamanda Abwao amewataja waliofariki dunia ni Happiness Greyson, Annastazia Greyson na Maria Greyson.
Share:

WATU WATANO WA FAMILIA MOJA WAUAWA DODOMA


Watu watano wa familia moja wamekutwa wakiwa wameuawa nyumbani kwao eneo la Zanka wilayani Bahi mkoani Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Onesmo Lyanga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Mkuu wa Mkoa Dodoma Antony Mtaka pamoja na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Dodoma, Onesmo Lyanga wamefika eneo la tukio usiku wa kuamkia leo ambapo miili ya watu hao imekutwa ikiwa ndani ya nyumba yao walimokuwa wanaishi ikiwa tayari imeharibika.

Waliouawa katika tukio hilo ni Baba, mama, watoto wawili na mjukuu mmoja.

Akizungumza mara baada ya kufika eneo la tukio, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka amelitaka Jeshi la Polisi mkoani humo kuanza uchunguzi mara moja ili kubaini watu waliohusika kufanya mauaji ya watu hao watano wa familia moja.


Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi kuhusu vifo hivyo, ikiwemo kubaini watekelezaji wa tukio hilo la kikatili.
Share:

Waziri Bashungwa: Wakandarasi Wazembe Kutopatiwa Kazi Za Tarura


Na. Angela Msimbira, Njombe
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Innocent Bashungwa amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Victor Seff kuwaorodhesha makandarasi wote ambao wako kwenye rekodi ya kutokufanya vizuri na wababaishaji kufutwa na kutofanya kazi za TARURA nchi nzima.

Ameyasema hayo mapema leo wakati akikagua barabara ya Igosi –Ujindile-Wangama yenye urefu wa kilometa 16.9 iliyopo kata ya Wangama katika Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe Mkoani Njombe ambayo inatarajiwa kujengwa kwa kiwango cha changarawe kutokana na Fedha za Tozo ya Mafuta.

Waziri Bashungwa amesema kuwa Makandarasi ambao hawafanyi vizuri wasiwe wanahamishwa kutoka sehemu moja hadi nyingine, badala yake wapewe kazi makandarasi ambao wanauwezo wa kufanya kazi kwa viwango na kasi inayotakiwa.

“Serikali ya Awamu ya Sita inataka kupeleka huduma kwa wananchi kwa kuboresha mawasiliano ya miundombinu ya barabara hasa vijijini, Rais wetu anataka kuiboresha TARURA ili iweze kuhudumia watanzania, Makandarasi wanaofanya kazi kwa mazoea hawahitajiki kwa sasa “, amesema Waziri Bashungwa

Waziri Bashungwa amesisitiza kuwa moja ya vitu ambavyo vitafanyika kwa Makampuni na Makandarasi wazembe na rekodi zinaonyesha ni wazembe ameelekeza apelekewe taarifa zao ili wasipatiwe kazi za TARURA kwani Serikali itafanya kazi na Makandarasi watakaofanya kazi kwa weledi na kukamilisha miradi kwa wakati na ameelekeza kuwepo kwa kanzidata kwa ajili ya Makampuni na Makandarasi ambayo yanafanya kazi vizuri ili waweze kupatiwa kazi za TARURA.

Amesisitiza kuwa lengo la kuanzishwa kwa TARURA nchini ni kuhakikisha inawasaidia wananchi wa vijijini katika Suala zima la ujenzi wa miundombinu ya barabara ili kuwasaidia watanzania ambao ni wakulima kuwafungulia fursa za kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi, hivyo ni wajibu kutumia makandarasi wanaofanya kazi kwa uaminifu na kuhakikisha miradi wanayopatiwa na Serikali inakamilika kwa wakati.

Akiwasilisha taarifa kuhusu ujenzi wa barabara hiyo, Meneja wa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe, Mhandisi Boniface Kasambo ameeleza kuwa barabara ya Igosi-Ujindile-Wangama ni muhimu kwa wanachi wa eneo hilo kwa kuwa inatumika kusafirisha mazao ya biashara ikiwemo parachichi, viazi na mbao kutoka mashambani Kata ya Wangama na Igosi kupeleka katika masoko ya Njombe Mji na Makambako kupitia barabara kuu ya Njombe -Makete.

Mhandisi Kasambo amesema ujenzi wa barabara hiyo unatarajiwa kuanza hivi karibuni, umeidhinishiwa zaidi ya shilingi milioni 400 na utajumuisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha changarawe, kuchimba mifereji na kujenga makalati.


Share:

Saturday 22 January 2022

SERIKALI INAENDELEA KUYABAINI MAENEO YA MACHIFU NA KUYATUNZA ILI YAWE VIVUTIO NCHINI-RAIS SAMIA


********************

NA EMMANUEL MBATILO, KILIMANJARO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu ameitaka Wizara ya Utamadunu,Sanaa na Michezo kuendelea taratibu,kuvikuza na kuviendeleza VIKUNDI vya burudani za kitamaduni ili vizalishe kazi za mikono za utamaduni.

Ameyasema hayo leo Rais Samia wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Utamaduni Kilimanjaro lililoandaliwa na uongozi wa machifu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Rais Samia amesema tayari Serikali imeanzisha kanzi data sahihi inayohusu machifu, na imeshaanza kuweka taarifa Sahihi za machifu na mchango wao katika kupamabana na ukoloni.

"Serikali inaendelea kuyabaini maeneo ya kichifu na kimila na kuyatunza ili yawe sehemu za vivutio vya nchi yetu na kuibua, kuimarisha na kuhifadhi majengo na zana za zamani ili zibaki kuwa vielelezo vya Utamaduni wetu ". Amesema Rais Samia.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Paulina Gekul amesema kuna umuhimu mkubwa kwa Watanzania kuendelea kutunza tamaduni zetu na kuachana na tamaduni potofu zinazofanywa na baadhi ya watu.

Amesema Serikali kupitia Wizara yake watandelea kutoa ushirikiano kwa machifu kutunza na kuenzi tamaduni zetu.
Share:

PAKUA APP MPYA YA MALUNDE 1 BLOG UPOKEE HABARI NA MATUKIO KWA URAHISI KWENYE SIMU YAKO


Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>
Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>
Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>

Habari Njema Wasomaji wa Malunde 1 blog !! Ili kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio  ya ukweli na uhakika kwa wakati yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla tunakushauri kupakua/ kudownload Aplikesheni ya Malunde 1 blog

Usikubali kupitwa na habari na Matukio yanayotokea… Pakua leo App ya Malunde 1 blog


Tembea na dunia kiganjani mwako kiulaini kabisa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. 


Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>



Share:

UKIPOTEZA MKEKA UNALIPWA: SOMA HAPA JINSI YA KUOMBA BONUS UKILOST MKEKA WAKO

Habari njema kwa wadau wa kubeti ambao hupoteza mikeka yao mara kwa mara hapa nitakueleza namna ya kuomba utumiwe bonus  kama malipo ya mikeka yako uliyopoteza

Ofa hii inapatikana ndani ya kampuni ya kubet ya 22bet

Masharti ya kupata bonus hii,

👉 Ni lazima uwe umejisajili na >>22bet>>

👉Uwe umepoteza angalau mikeka 20 mfululizo

👉Katika timu zote ulizopoteza  timu ziziwe na ods juu ya 3.0 maana kuna watu watachagua timu yenye ods 12 ili walost makusudi na kuomba bonus.

👉Mikeka yote uliyolost iwe imewekwa ndani ya siku 30 sio zaidi ya hapo.

👉 Kila mkeka uliolost  stake yake ianzie $2 sawa na kama 4700 

👉Kumbuka  unatakiwa kuomba bonus hii kwa account moja tu, ikiwa unamiliki zaidi ya account 1 hutopewa na watagundua kupitia IP adress

Does your series of losing bets meet all the requirements? Then email us at support@22bet.com  account number and putting "Series of losing bets" in the subject line.

Kama umetimiza vigezo hivyo tuma barua pepe, na sehemu ya subject jaza account namba yako  na idadi ya mikeka uliyopoteza  utapokea malipo yako ndani ya muda mfupi, kumbuka email itumwe   kwenda  support@22bet.com  

   kUJISAJILI NA 22BET BOFYA >>>HAPA>>


Share:

SIASA ZILINIPIGA CHENGA, NILIAMBULIA PATUPU LICHA YA KUMWAGA HELA


Ama kwa hakika siasa hapa nchini Kenya huwa na wenyewe jinsi watu wanavyosema. Kila mara nilipowaona wanasiasa wakishinda viti mbalimbali hapa nchini nilidhani ni swala rahisi tu bora kujieleza.

 Nilifikiria tu wakati unapofanya mkutano wa kisiasa na wakati mwingine umati mkubwa wa watu ujitokeze ilikuwa ishara tosha kwamba ungeshinda kiti kile lakini hii haikuwa kweli kwani umati labda ulikuwa umekuja kula hela zako ama kusikia ajenda zako na mara nyingi wao huwa na mtu wao ambao wangependa kumpigia kura. 


Ama kwa hakika ulikuwa ni mchezo mchafu na ulio na watu waliouelewa. Mwaka mmoja nilisimama kiti cha ubunge wa kaunti na nikaona maajabu. 

Nilikopa hela za kampeni na kuwamwagia vijana, wazee na watu mbalimbali kwa ajili ya umaarufu ile niibuke bigwa kwenye debe. Mambo yalienda mrama kwani niliibukia limbukeni na nikawa mkia kwenye kinyang’anyiro hicho.


 Sikuwa na chochote cha kujivunia kwani nilikuwa nimepoteza hela pamoja na muda wangu kwa wakati mmoja. Nilingojea miaka mitano baadae na nikajitoza kwenye kiwanja tayari kuonyesha makali yangu ana mara hii nilidhania eti kwa vile nilimaliza mkia wakati uliopita, raia wenye eneo wadi ile wangenihurumia na kunipa kura.


 Kampeni zilichacha na hapo nilifahamu fika kwamba mambo yalikuwa mazuri kwani vijana na akina mama waliniahidi uungwaji mkono. Kiongozi wa chama chetu mara hii alibnifadhili kwani ajenda zangu zilienda sambamba na manifesto ya chama.


 Kila nilipoenda mashinani, watoto kwa vijana kwa wanawake wote waliimba jina langu. Nilifahamu huu ulikuwa ni mwamko mpya kwenye shughuli zangu za kisiasa. Ama kwa hakika ilikuwa ni siku njema ilyoanza kuonekana mapema. Siku ya kupiga kura ilifika na hapo nilifurahishwa na idadi ya watu waliojitokeza. Wakati wa matokeo ulipofika, nilipigwa na butwaa kwani wakati huu pia nilikuwa wa mwisho. 


Aibu ilinikumba nisijue la kufanya. Kila mtu alinikejeli na kuniita majina matusi. Wengine walisema kuwa nilikuwa naharibu pesa zangu nikijitosa kwenye ulingo huu wa siasa. 


Atafutaye hachoki lakini kwa wakati huu nilikuwa nimefikia kwenye ukingo wa swala zima la siasa. Nilipatana na mbunge Flani ambaye jina lake nalibana. Nilimuuliza siri yake kwenye ulingo wa siasa na akanielezea kwamba daktari Kiwanga alimsaidia akashinda kiti hicho kwa mpigo. 


Siku iliyofuatia nilienda ofisini kwa daktari Kiwanga kwa ushauri na usaidizi kwani ilikuwa imebaki ni mwaka mwezi mmoja kabla ya uchaguzi mkuu. Nilirejea kutoka kwa daktari Kiwanga na kurejelea shuguli zangu za kampeni. Mara hii umati mkubwa ulijitokeza kunishangilia kwa kishindo. 


Jambo hili lilitia wapinzani wangu kiwewe kwani ilikuwa ni ishara tosha mambo yalikuwa yamebadilika kwa uwezo wa daktari Kiwanga. Mara nyingi wapinzani wangu walitafuta sababu za kuniharibia lakini kwa kweli wimbi nilikuwa nalo kwa wakati ule.

 Hela nilimwaga kama ilivyokuwa kawaida yangu ili kuwarai raia waweze kunipigia kura. Siku ya kupiga kura ilipowadia nilijihisi kama niliyekuwa na mwamko mpya maishani. Nilipiga kura yangu asubuhi na mapema na nikarejea nyumbani kupumzika huku nikongoja matokea na mara hii nilikuwa na matumaini kuwa ningeibukia mshindi. 


Wakati wa matokea uliwadia na nilikuwa nimeketi ukumbini nikiwa ange kujua yote yaliyojiri kwenye uchaguzi ule. Matokea yalianza na hapo nilitangazwa kama mshindi na mbunge wa wadi. Nilipokezwa cheti kwa mpigo. Hakuna yeyote aliyepeleka kesi mahakamani kupinga kuchaguliwa kwangu kama mbuge wa wadi ile kwa wakati wowote. 


Ama kwa hakika daktari Kiwanga alikuwa ameimarisha azma yangu ya kuwa mwanasiasa. Daktari Kiwanga ana uwezo wa kusuluhisha mizozo ya ndoa,biashara kunawiri, kushinda kesi kotini na mengineyo. Ana uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali kama vile kifua kikuu, kifafa, kifaduro na mengineyo kwa siku tatu pekee. Waweza kumpata Dkt. Kiwanga kupitia wavuti www.kiwangadoctors.com barua pepe kiwangadoctors@gmail.com au piga simu kwa nambari +254769404965.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 22,2022



Magazeti ya leo Jumamosi January 22,2022


Share:

Friday 21 January 2022

SERIKALI KUWABAINI WATU 200,000 WANAOISHI NA VVU BILA KUJUA



MCHAKATO wa kuwapata watu 200,000 waishio na virusi vya Ukimwi bila kujua ni mbinu mojawapo ambayo Wizara ya Afya imesema itaitumia ili kupunguza maambukizi mapya na kufikia malengo ya milenia mwaka 2030.

Pamoja na hayo Wizara imesema inakusudia kupunguza idadi ya watoto wachanga wanaozaliwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) kutoka 6000 wanaozaliwa kila mwaka kwa kuhakikisha inamfikia kila mwanamke mwenye ujauzito.


Hayo yamesemwa jana Alhamisi Januari 20, 2022 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu wakati alipokuwa akizindua mpango mkakati wa miaka mitano ya tafiti na mafunzo katika masuala ya afya ya jamii na lishe.

“Nchini Tanzania inakadiriwa watu milioni 1.7 wanaoishi na Virusi vya Ukimwi lakini wanaotambua hali zao za afya ni milioni 1.5 pekee, hii ni changamoto kwetu lazima tuwatafute hawa 200,000 kwani ndiyo wanaochangia maambukizi mapya bila kujua.

“Tutawapata hawa kwa kuwashauri na kuhamasisha ili wapime kupitia mtaa kwa mtaa, kata kwa kata, halmashauri kwa halmashauri lazima tuhakikishe tunamaliza ugonjwa huu Tanzania ifikapo mwaka 2030. Mpaka sasa wanaotambua hali zao ni asilimia 88, wanaotumia dawa ni asilimia 98 na waliofanikiwa kufubaza makali ya virusi ni asilimia 92,” amesema Waziri Ummy.

Amesema suala la mtoto kuzaliwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi halikubaliki. “Matamanio ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuona watoto wote wanazaliwa na afya njema pasipo virusi vya ukimwi, kaswende wala homa ya ini, hii ni changamoto kwetu lazima tuwatafute wote tuwapime na tukiwabaini tuwaingize kwenye dawa kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto,” amesema.

Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk Donald Wright amesema kati ya vipaumbele ambavyo ubalozi wa Marekani umewekeza ni kusaidia tafiti za masuala ya ukimwi kupitia Usaid na mafunzo pamoja na tafiti za masuala ya afya na lishe.

Chanzo - Global Publishers
Share:

HOSPITALI YABURUZWA MAHAKAMANI KWA KUMPA MGONJWA MAJIBU YA UONGO...MWENYEWE ADAI FIDIA MILIONI 40




Kituo kimoja cha kutolea huduma za matibabu kilichopo Mombasa Kenya kimetakiwa na Mahakama kulipa fidia ya Ksh. milioni 2 (Tsh. milioni 40) kwa Mgonjwa aitwaye Roberto Macri baada ya kumpa majibu ya uongo ya vipimo kuwa ana cancer wakati hana cancer.

Jaji wa Mahakama ya Malindi, Julie Oseku amesema Mgonjwa huyo alifika Kituoni hapo ‘Jamu Imaging Centre’ akiwa na changamoto ya kupata shida ya kumeza chakula na akaambiwa ana ‘Cancer Stage Four’ hali iliyomlazimu kusafiri hadi Italia ambako aliambiwa hana Cancer.

“Mgonjwa kama asingeambiwa ana Cancer asingelazimika kutumia gharama kwenda Italia baada ya kuwa na hofu, pia majibu yalimsababishia stress na maumivu zaidi ndio maana aliporudi tu kutoka Italia akafungua kesi,” amesema Jaji Oseku.
Share:

WAZALISHAJI WA BIDHAA ZA VIWANDANI WATUMA OMBI KWA SERIKALI NA TRA , KUSHUSHA GHARAMA ZA STEMPU ZA KODI ZA KIELEKTRONIKI (ETS)

 


 

Wazalishaji wa bidhaa zinazotozwa ushuru kwa kutumia Stempu za Kodo za Kielektroniki (Electronic Tax Stamps - ETS) wameiomba Wizara ya Fedha na Mipangopamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupunguza zaidi viwango vilivyotangazwa Jumatatu wiki hii kwa vile viwango vya sasa vya ushuru huo ni vikubwa sana.

Akizungumza na vyombo vya habari kwa niaba ya wazalishaji wanaotozwa ushuru huo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Bwana Leodegar Tenga amesema kwamba sekta binafsi inaunga mkono uanzishwaji na matumizi ya stempu za kodi za kielektroniki na kusisitiza kuwa kiwango cha gharama hizo kiwezeshe ukuaji wa viwanda nchini.

"Wenye viwanda wanaunga mkono mpango wa serikali kutekeleza matumizi ya ETS kwakuwa yanaleta usawa na ushindani sawia na kuboresha mazingira ya biashara kwa ajili yakuchochea ukuaji wa uchumi, Wanachama wa Shirikisho pia wanaunga mkono matumizi ya ETS kwa kuwa ETS inasaidia kuleta uwazi katika uendeshaji wa biashara na kupunguza undanganyifu kwenye biashara na kuondoa ongezeko la biashara haramu kwenye soko, lakini pia ushuru wa ETS unaotozwa sasa siyo tu kwamba unaongeza gharama za uzalishaji, vilevile unaathari kwenye maendeleo ya sekta ya viwanda na uchumi kwa ujumla, wenye viwanda wamewahi kuwa na majadiliano na TRA, na kuwasilisha kwa serikali  mfumo mbadala kama jawabu la kupunguza kiasi kikubwa cha viwango vya gharama vinavyotozwa kwenye ETS. Hata hivyo, maombi yetu ya kuomba viwango vya gharama za ETS upunguzwe hayakuchukuliwa kabisa kufuatia kutangazwa wiki hii kwa viwango vipya vyenye mabadaliko madogo sana” ,alisema Mkurugenzi Mtendaji wa CTI

Na kuongezea kuwa CTI kwa niaba ya wenye viwanda ilishawahi kupeleka mapendekezo ya wenye viwanda serikalini ambayo yalitarajiwa yazingatiwe katika kutoa maamuzi ya kuweka viwango vipya vya gharama za ETS kutokana na Vigezo ivyo tunaomba kupitia upya na kupunguza gharama za ETS ili kupunguza athari za viwanda ambavyo vinaendelea kulipa kodi mbalimbali, wazalishaji wakiwakilishwa na shirikisho kama wadau, washirikishwe katika mchakato wa kurekebisha mfumo mzima wa ETS , Mchakato wa kutafuta mzabuni uwe wa wazi na shindani, kuwepo mpango mahususi wa kutoa huduma ya ETS kwa kutumia mfumo unaoendeshwa na sisi wenyewe, Malipo ya Stempu za ETS yafanyike kwa shilingi za Kitanzania badala ya dola za kimarekani, na mwisho Tunaomba mchakato wa kutafuta mbadala wa ETS ufanyike kukidhi vigezo vya serikali na kupunguza mzigo wa gharama za viwanda",alisema Tenga.

Aidha wameipongeza Serikali kwa kuruhusu ulipaji wa gharama za ETS kwa fedha za Kitanzania na kukiri kuwa ukweli ni kwamba punguzo la gharama za ETS Haliwatii moyo wazalishaji hao wa Bidhaa za Viwandani.




Share:

SHILINGI BILIONI MBILI KUKARABATI MITAMBO YA UJENZI WA SKIMU ZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI


Picha Ikimuonesha Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Bw. Daudi Kaali alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari hawapo katika picha, kuhusu matengenezo ya Mitambo, katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagilijai Jijini Dodoma jana.
Picha ikionesha moja ya mtambo uliokarabatiwa unaotumika katika ujenzi wa skimu za kilimo cha umwagiliaji.
Mhandisi Hassan Dyali akizungumza na waandishi wa habari kuhuasiana na sehemu ya majukumu ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ya Ukarabati wa Mitambo inayotumika katika Ujenzi wa Skimu za Kilimo cha Umwagiliaji nchini.

**

Na Mwandishi Wetu – Dodoma

Kiasi cha fedha shilingi Bilioni Mbili za Kitanzania, zitatumika katika ukarabati na matengenezo ya mitambo inayotumika katika ujenzi wa miundombinu katika skimu za kilimo cha Umwagiliaji nchini.

Hayo yamesemwa jana jioni jijini Dodoma, na kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali alipokuwa akizungumza waandishi wa habari katika viunga vya ofisi za Tume hiyo wakati zoezi la ukabati wa mitambo hiyo ukiendelea.

Bw. Kaali alisema nchi nzima ina mitambo zaidi ya 53 na inayoweza kutengenezwa ni mitambo 44 na malengo yaliyowekwa na Tume hiyo ni kutengeneza mitambo 43 hadi kufikia mwakani 2023. “Tutaokoa fedha nyingi kwani kukodi mtambo mmoja siyo chini ya Sh. Milioni moja kwa siku moja na unaweka kukuta, skimu moja inaweza ikahitaji siku hata ishirini au theathini kwa ajili ya matengenezo , hivyo kwa mahesabu ya haraka utaona ni fedha nyingi sana zinahitaji kukodisha mtambo mmoja kwa siku”. Alisisitiza Kaali.

Aidha alifafanua kuwa, Tume hiyo imetenga wastani wa hekta laki mbili na hamsini kwa mwaka zinazoweza kuendelezwa, hivyo matengenezo ya mitambo hiyo yataweza kuongeza kasi ya kuweza kuendeleza eneo hilo. “Tukienda hivi baada ya miaka mitano tunaweza kuwa tumeongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji kufikia hekta milioni moja na laki mbili. Alisema.

Mhandisi Hassan Ndyali, ni Msimamizi wa kitengo cha mitambo hiyo anafafanua kuwa, pamoja na kuwa kazi ya kukarabati mitambo hiyo ni sehemu ya majukumu ya ofisi, alisema kuwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe “Ambaye alitamani sana kuona tunafanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa na kukamilisha kwa wakati ili mitambo hiyo iweze kuleta tija kwa Taifa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji”,alisisitiza Mhandisi Ndyali.

Mmoja wa fundi wa mitambo hiyo Bw. Raphael Kanuha, amewahakikishia wakulima kuwa mashine hizo zitakamilika ndani ya muda mfupi na zitaingia kazini na kufanya kazi kwa ufanisi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger