Wednesday 1 January 2020

Head; Business Banking at NMB Tanzania

Reporting Line: Chief, Retail Banking Job Purpose To builds an effective network of internal and external relationships, such as community and industry relationships, to actively acquire new clients and/or expand existing clients and enhance the client experience. Leverages reporting and sales tools to proactively identify and successfully convert sales opportunities To Manage risk/return and drives quality for new… Read More »

The post Head; Business Banking at NMB Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rais Magufuli apiga simu moja kwa moja stejini kwa ⁦ Diamond Platnumz ⁩ akiwa jukwaani.....Kigoma yageuka shangwe tupu.

Msanii wa kizazi kipya hapa nchini Naseeb Abdul maarufu kwa jina la  Diamond Platinumz usiku wa jana alikuwa akitumbuiza katika kusherekea miaka 10 katika muziki wa Bongo Fleva Mkoani Kigoma ambapo  akiwa jukwaani alipigiwa simu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dkt John Pombe Magufuli kisha kupongezwa kwa jitihada zake anazofanya katika sanaa na Taifa kwa ujumla.

Ilikuwa majira ya saa 7:54 usiku akiwa amemaliza kuimba wimbo wa Tetema na Rayvany, ambapo simu hiyo ilipelekwa jukwaani na Katibu Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole  akiongozana na meneja wake Babu Tale.

Baada ya kuipokea aliwatangazaia mashabiki waliofika uwanjani hapo kwamba ‘Wanakigoma nimewaambia kitu si nimewaambia leo mna bahati sana, kwenye simu tuko na Mheshimiwa Magufuli piga shangweeee, Mheshimiwa shikamooo.

Baada ya hapo akaweka sauti kubwa ambayo ilikuwa ikisikika kwenye spika, na kumwambia nakutakiwa wewe heri ya mwaka mpya pamoja na Wanakigoma wote, wakati huo mashabiki wakawa wanapiga kelele za babu!babu!babu!.

Kutokana na hali hiyo Diamond aliwatuliza, lakini bado hawakusikia na kuendelea kupiga kelele. Rais amesema alitamani na yeye angekuwepo hapo, lakini amemtuma Polepole na wengine waliokuja hapo.

Diamond alimjibu baba watu tunakupenda sana na tunakuhakikishia awamu inayokuja unapita kwa kishindo sana, tunapiga mia kwa mia, Magufuli oyeeee!CCM oyeee!.

==>>Tazama hapo chini


Share:

Government of India (ICCR) Scholarships for Africans to Study in India 2020-2021 (900 scholarships available)

Deadline: February 29, 2020 Applications are open for the Indian Council for Cultural Relations (ICCR) Scholarships. The Government of India through the ICCR is enhancing academic opportunities for students of African Countries in India by offering up to 900 scholarships for African students to pursue undergraduate/postgraduate and higher studies at Indian Institutions/Universities. This scholarship scheme was launched at the inaugural… Read More »

The post Government of India (ICCR) Scholarships for Africans to Study in India 2020-2021 (900 scholarships available) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

AEDX India International Internship 2020 on SDG, Art and Culture

Deadline: Ongoing Applications are open for the AEDX India International Internship 2020 on SDG, Art, and Culture. AEDX India is pleased to offer this internship for students who are passionate about traveling and learning in their chosen area of interest. The opportunity is based out of Chennai, India. India refers collectively to the thousands of diverse, yet unique cultures,… Read More »

The post AEDX India International Internship 2020 on SDG, Art and Culture appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

#IdeasChangeLives Global Innovation Challenge

#IdeasChangeLives Global Innovation Challenge Deadline: 10 January 2020 Open to: anyone and everyone across the world Benefits: funding, support and mentorship DESCRIPTION #IdeasChangeLives is a global innovation challenge to find digital solutions to some of the world’s greatest problems. They are looking for people with a fresh, entrepreneurial spirit and a big idea that has the potential to make a positive… Read More »

The post #IdeasChangeLives Global Innovation Challenge appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Apply for the French Government Challenge 2020 for young African Entrepreneurs(Fully-funded)

OVERVIEW Announced at the press conference presenting the 2020 Africa-France Summit held in Bordeaux on Tuesday 17 September 2019, the Challenge of 1.000 is a joint initiative of Digital Africa and the Summit. The State will invite 1.000  African entrepreneurs to come to Bordeaux to present their solutions at The City of Solutions, a show dedicated to projects and solutions… Read More »

The post Apply for the French Government Challenge 2020 for young African Entrepreneurs(Fully-funded) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

British Council Future News Worldwide Conference 2020 in London(Fully-Funded)

British Council Future News Worldwide Conference 2020 in London(Fully-Funded)   Are you the future of journalism? British Council is looking for 100 of the world’s most talented, motivated and passionate student journalists to attend an intensive media training programme. You’ll receive exclusive coaching from world-leading editors, broadcasters, writers and reporters, and see how publishers around the world are… Read More »

The post British Council Future News Worldwide Conference 2020 in London(Fully-Funded) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Reservation Agent Job Opportunity at Four Seasons

Reservation Agent Four Seasons – Serengeti Mara, Tanzania Reservations Agents sell the resort and provide information to prospective guests, capture sales from the incoming calls and coordinate details of each reservation. Employment type Full-time Job function Industries Marketing and Advertising Leisure, Travel & Tourism Hospitality CLICK HERE TO APPLY

The post Reservation Agent Job Opportunity at Four Seasons appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Teacher Training Program Coordinator Job opportunity at The Foundation For Tomorrow

Teacher Training Program Coordinator The Foundation For Tomorrow (TFFT)– Arusha Office TFFT is a high-energy and fast-growing non-governmental organization that focuses on addressing vulnerability through education. We offer individual orphaned and vulnerable children the opportunity to succeed through access to quality schooling, health and psycho-social support and life skills programs. Additionally, we work to improve the quality of… Read More »

The post Teacher Training Program Coordinator Job opportunity at The Foundation For Tomorrow appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Regional Sales Manager East Africa Job Opportunity at Lobo Management Services

Regional Sales Manager East Africa Job Opportunity at Lobo Management Services   Job Title: Regional Sales Manager East Africa Our client a reputed regional FMCG company within the personal care category is seeking a Regional Sales Manager to establish distribution and grow sales in eastern and central African countries. The role will be responsible for: Developing/Implementing route to market… Read More »

The post Regional Sales Manager East Africa Job Opportunity at Lobo Management Services appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Waziri Mkuu Aagiza Miundombinu Ya Shule Ikamilike Mapema....Asema Kama kuna wahusika walioko likizo warudishwe haraka

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema miradi yote ya ujenzi wa miundombinu ya shule ikamilike mapema na kama kuna watendaji walioko likizo warudi kwani Serikali inataka wanafunzi wote waanze masomo pamoja.

Ameyasema hayo jana (Jumanne, Desemba 31, 2019) wakati alipofanya ziara kukagua ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleoa wilayani Ruangwa. Amesisitiza ukamilishwaji wa miradi hiyo ili wananchi waanze kuitumia.

Waziri Mkuu amesema agizo alilolitoa kwa wakuu wa mikoa Desemba 29, 2019 kuhusu usimamizi wa miundimbinu ya shule ikiwemo ujenzi wa madarasa liko pale pale kwa sababu Serikali haitaki kuona wanafunzi wakipishana katika kuanza masomo.

Miradi ambayo Waziri Mkuu ameitembelea ni ujenzi wa shule ya msingi ya Ng’au ambayo ipo katika hatua za mwisho kukamilika, ujenzi wa chuo cha VETA, hospitali ya wilaya ya Ruangwa na shule ya sekondari ya Lucas Maria.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatoa fedha kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo hivyo ni lazima viongozi katika maeneo husika wahakikishe wanashirikiana katika kusimamia utekelezaji wake.

Amesema wanafunzi wanatakiwa kuanza masomo mwanzoni mwa mwezi Januari, 2020, hivyo ni lazima usimamizi ukaongezwa katika baadhi ya maeneo ambayo miundombinu yake bado haijakamilika ili kuwahi masomo.

Akiwa katika shule ya Sekondari ya Lucas Maria Waziri Mkuu amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Andrea Chezue ahakikishe mafundi wanafanya kazi usiku na mchana.

“Shule zinakaribia kufunguliwa na baadhi ya majengo kama bwalo, maabara, nyumba za walimu hayajakamilika mafundi hawapo eneo la ujenzi na Serikali imetoa fedha. Nataka kazi hii ikamilike mapema kwani hakuna sababu.”

Wakati huo huo, Wananchi wa Wilaya ya Ruangwa wamepongeza na kumshukuru Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Magufuli kutokana na miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Wananchi hao wakiwemo vijana wanaojenga chuo cha VETA walitoa pongezi na shukrani hizo mbele ya Waziri Mkuu baada ya kumaliza kukagua mradi wa ujenzi wa chuo hicho. Mafunzo yatakayotolewa chuoni hapo ni pamoja na ufundi uashi, seremala, magari, ushonaji nguo na Tehama.

Kadhalika, vijana hao wamewashauri vijana wenzao wajitokeze na kuchangamkia fursa za ajira zinazopatikana katika maeneo yao kupitia miradi mbalimbali inayotokelezwa na Serikali ili waweze kujikwamua kiuchumi.


Share:

Jeshi La Magereza Lajipanga Kimkakati Kuzalisha Chakula Cha Wafungwa Kwa Mwaka 2020

Na ASP Lucas Mboje, Dodoma
JESHI la Magereza limejipanga kwa mwaka 2020 kuendelea na utekelezaji wa jukumu la uzalishaji wa chakula cha kutosha cha wafungwa kwa kutumia rasilimali zilizopo katika Jeshi hilo ili kufikia adhma ya Serikali ya awamu ya tano kuhusu kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa magerezani.

Akizungumza na Maafisa na askari wa Jeshi hilo katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2019 na kuukaribisha mwaka mpya 2020 jana jijini Dodoma, Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike amesema kuwa Jeshi hilo tayari limejiwekea mkakati maalum wa kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa magerezani.

Katika kulifanyia kazi suala hilo, Kamishna Jenerali Kasike amesema kuwa mavuno yameongezeka katika msimu wa kilimo 2018/2019 ambapo Jeshi hilo limeweza kuzalisha chakula cha wafungwa katika magereza kumi(10) ya kimkakati(Songwe, Mollo, Ludewa, Arusha, Pawaga, Idete, Kitete, Isupilo, Kitai na Kitengule).

“Kupitia Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza(SHIMA), Jeshi limeweza kulisha unga wa mahindi kwa wahalifu magerezani kwa kipindi cha mwaka mzima katika mikoa ya Lindi, Ruvuma, Mtwara, Rukwa, Njombe na Katavi. Aidha, katika mikoa mingine Shirika limeweza kulisha unga kwa miezi mitatu hadi sita”, amesema Kamishna Jenerali Kasike.

Ameongeza kuwa kuna mkakati wa muda mrefu wa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia vyanzo vya maji vilivyopo katika maeneo mbalimbali ya magereza ambapo Jeshi hilo tayari limekamilisha andiko linalohusu mapindizi ya kilimo na tayari limewasilishwa serikalini katika hatua mbalimbali za ngazi ya maamuzi.

Akizungumzia mafanikio mengi ya kujivunia kwa mwaka 2019 Kamishna Jenerali Kasike amesema kuwa kumekuwa na mwitikio mkubwa miongoni mwa maafisa na askari katika kuishi na ajenda mahususi ya Jeshi hilo kuhusu umuhimu wa kubadilika kimtizamo, kifikra na utendaji kama nguzo ya mabadiliko katika Jeshi hilo.

“Naomba nisistize kuwa bado tuendelee kuishi na ajenda hii ya mabadiliko ya kimtizamo na kifikra katika mwaka mpya 2020 tunaoutarajia kuuanza muda mfupi ujao kwa kufanya kazi kwa weledi, ubunifu katika maeneo yetu ya kazi. Tradition die hard”, amesisitiza Kamishna Jenerali Kasike.

Mafanikio mengine aliyoyaainisha ni pamoja na utekelezaji wa agizo la Serikali kuhusu kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa, ujenzi wa nyumba za watumishi wa Jeshi hilo katika maeneo mbalimbali nchini kwa njia ya ubunifu, udhibiti wa uingizaji wa vitu visivyoruhusiwa magerezani kwa kufunga CCTV camera katika baadhi ya magereza. Aidha, katika kuhakikisha kuwa wafungwa waliopo magerezani wanafanya kazi, Jeshi kupitia Shirika lake limefanikiwa kupata  leseni ya usajili ya kuwatumia wafungwa katika kandarasi mbalimbali ikiwemo kufanya usafi katika Barabara zilizopo nchini na shughuli nyinginezo za kuweza kuliingizia faida Shirika hilo.

“Shirika la Magereza limefanikisha utaratibu wa kuingiza miradi yake yote katika mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali(GePG) na hivyo kuziba mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali. Pia, Shirika hilo limeweza kutoa mchango wake Serikalini kiasi cha Tsh. Milioni mia moja na therasini kwa mwaka 2019”, ameainisha Kamishna Jenerali Kasike.

Aidha, pamoja na mafanikio hayo Kamishna Jenerali Kasike amebainisha changamoto zinazolikabili Jeshi hilo ikiwemo ufinyu wa bajeti, uhaba wa vitendea kazi mbalimbali kama vile magari, vyombo vya mawasiliano, pia changamoto za makazi na uchache wa nguvu kazi ya maafisa na askari katika Jeshi hilo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike amehitimisha hotuba yake leo jijini Dodoma kwa kuwatakia heri ya mwaka mpya 2020 maafisa, askari pamoja na watumishi wote wa Jeshi hilo na amewataka kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi ya kazi, Dira na Dhima ya Jeshi hilo.


Share:

Trump apandwa na hasira Baada Ya Waandamanaji Kuuvamia ubalozi wa Marekani nchini Iraq na Kutaka Kuuchoma Moto

Rais Donald Trump wa Marekani ameonyesha kuchukizwa na  maandamano makubwa mbele ya ubalozi wa nchi hiyo huko Baghdad, mji mkuu wa Iraq lakini hata hivyo akaishia kusema anaamini  Iraq itatumia vikosi vyake vya usalama kuulinda ubaloz huo wa Marekani

Kauli hiyo ameitoa wakati ambapo anailaumu Iran kwa kuchochea vurugu hizo dhidi ya eneo lake. 

Wananchi wa Iraq ambao ni wafuasi wa wapiganaji wanaoungwa mkono na Iran waliandamana kwenye ubalozi wa Marekani siku ya Jumanne huku wakiimba nyimbo zinazosema ''Kifo cha Marekani,'' wakirusha mawe, wakivunja kamera za usalama pamoja na kulichoma moto eneo la mapokezi, wakilaani mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani.

Mashambulizi hayo yaliyofanyika Jumapili iliyopita yaliwaua wapiganaji wapatao 25 wa kundi la wanamgambo wa Kataeb Hezbollah. 

''Tunatarajia Iraq itavitumia vikosi vyake kuulinda ubalozi na tumearifiwa hivyo,'' ameandika Trump katika ukurasa wake wa Twitter. Trump amesema Iran itawajibika kikamilifu kwa machafuko hayo.


Mashambulizi ya Marekani yalikuwa ni kujibu shambulizi la roketi lililofanywa wiki iliyopita na kumuua mkandarasi mmoja wa Kimarekani katika kituo cha jeshi la Iraq, ambalo ni la karibuni kufnayika lililenga maslahi ya Marekani nchini Iraq. 

Hakuna kundi lolote lililodai kuhusika na shambulizi hilo, lakini vikosi vya usalama vya Marekani vimelishutumu kundi la Kataeb Hezbollah.
 
Trump amesema Marekani imejibu vikali shambulizi ambalo limemuua mkandarasi huyo na skwamba siku zote itafanya hivyo. 

Uhusiano kati ya Marekani na Iran umekuwa ukizorota tangu Marekani ilivyojiondoa kwenye mkataba wa kihistoria wa nyuklia wa Iran mwaka 2018 na kuweka vikwazo vipya.

Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka kadhaa kwa waandamanaji kufanikiwa kuufikia ubalozi wa Marekani mjini Baghdad, uliopo kwenye eneo lenye ulinzi mkali maarufu kama Green Zone. 

Vikosi vya usalama ndani ya ubalozi huo walifyatua mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji nje ya ubalozi huo. Imeripotiwa kuwa zaidi ya watu 20,000 walikusanyika nje ya ubalozi huo.


Share:

Waandamanaji wa Iraq wavamia ubalozi wa Marekani mjini Baghdad

Waombolezaji nchini Iraq wamekusanyika nje ya ubalozi wa Marekani mjini Baghdad kulaani mashambulio ya ndege za Marekani yaliyolenga vituo vya wanamgambo wa Kishia.

Waombolezaji hao walizingira ubalozi huo uliopo kwenye eneo lenye ulinzi mkali wakiwa wamebeba bendera za kundi la wanamgambo lenye ushawishi mkubwa.

Wakati huo huo, Saudi Arabia imewalaani wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran kwa kuyashambulia majeshi ya Marekani yaliyoko nchini Iraq ambapo mkandarasi mmoja wa Marekani aliuliwa.

Wanamgambo hao walifanya mashambulio hayo wiki iliyopita. Marekani ilijibu kwa kuwashambulia kwa ndege wanamgambo hao wa Kataib Hezbollah Jumapili iliyopita. 


Wanamgambo hao wa Hezbollah walikishambulia kituo cha kijeshi cha Marekani nchini Irak Ijumaa iliyopita.

Hata hivyo Waziri Mkuu wa Iraq, Adel Abdul Mahdi ameilaani pia Marekani kwa kufanya mashambilio ya ndege yaliyolenga vituo vya wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran. 


Amesema hatua ya Marekani inaweza kuitumbukiza zaidi Iraq katika vita vya kiwakala baina ya Marekani na Iran.


Share:

Rais Magufuli awatakia Watanzania heri ya mwaka Mpya 2020

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia Watanzania wote heri ya Mwaka mpya wa 2020 na kuwaomba waendelee kudumisha amani na upendo ili uwe mwaka wa maendeleo na ustawi kwa Taifa.

Mhe. Rais Magufuli ametoa salamu hizo jana  wakati akiagana na Maafisa na Askari Wanyamapori na Hifadhi ya Misitu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ambako alitembelea na kujionea vivutio vya utalii pamoja na wananchi wa Nyabugera na Muganza aliowasalimu wakati akiwa njiani kurejea nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amepokea salamu za heri ya Mwaka Mpya wa 2020 kutoka kwa wananchi, viongozi mbalimbali wakiwemo Marais Wastaafu, Maaskofu na Masheikh ambao wamempongeza kwa kazi nzuri ya kuongoza nchi kwa mafanikio makubwa na wamemuelezea matarajio yao ya kufanikiwa zaidi katika mwaka ujao.

“Mhe. Rais wangu, Dkt. Magufuli, Bwana Yesu Asifiwe. Ninakupa hongera sana kwa wajibu mzito ulionao. Kwa neema ya Mungu tumejaaliwa kufikia siku ya mwisho kwa mwaka huu wa 2019. Mimi nakupongeza kwa jitihada zako nyingi za kuleta maendeleo kwa nchi yetu. Ninakuombea na kukutakia Mwaka Mpya 2020 wa heri na mafanikio makubwa. Uso wa Bwana uende nawe popote utakapokuwa” amesema Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dkt. Frederick Shoo.

Kabla ya kuondoka katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo, Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Dkt. Allan Kijazi, Maafisa na Askari wote wa hifadhi hiyo kwa mapokezi mazuri na juhudi kubwa zilizowezesha hifadhi hiyo kuvutia na amewahakikishia kuwa pamoja na kutoa shilingi Bilioni 2 za ujenzi wa kivuko cha kwenda hifadhi ya Kisiwa cha Rubondo, Serikali itatoa shilingi Milioni 200 za kuboresha barabara za hifadhi hiyo.

Baada ya kuvuka ziwa Victoria kwa kivuko cha MV Chato, Mhe. Rais Magufuli amekutana na wananchi wa Kasenda na kuelezea kutoridhishwa kwake na ukusanyaji wa mapato ya soko la dagaa na samaki la Kasenda baada ya kuelezwa kuwa makusanyo ya mapato ya soko hilo ni shilingi laki 5 kwa siku licha kuwa soko kubwa namba 2 kwa kuuza dagaa katika ukanda wa Ziwa Victoria.

Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Chato, kufuatilia ukusanyaji wa mapato katika soko hili na kuchukua hatua za kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato itakayobainika ili Halmashauri ya Wilaya ya Chato iweze kupata fedha zitakazosaidia kutatua kero za wananchi ikiwemo kuboresha mazingira ya soko hilo na ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyabugera ambayo amechangia shilingi Milioni 5.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Bw. Eliud Mwaiteleke kutangaza zabuni ya ujenzi wa barabara ya Kasenda - Muganza yenye urefu wa kilometa 2.2 ili ijengwe kwa kiwango cha lami kama alivyoahidi, na kwamba Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara hiyo.

Mhe. Rais Magufuli pia amewasalimu wananchi wa Muganza, ambapo amewapongeza kwa maendeleo yaliyopatikana katika eneo hilo na amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma ili iendelee kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo yenye manufaa kwa wananchi.

“Nchi hii ilikuwa inaliwa sana na majizi na mpaka sasa bado wapo, namuomba Mwenyezi Mungu aendelee kunipa uhai ili katika mwaka 2020 niendelee kuwatumbua majizi wote na fedha tutakazopata tuzipeleke kwenye miradi ya maendeleo kama ambavyo tumenunua ndege 11, tunajenga reli (standard gauge), tunatoa elimu bure na mengine mengi” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli pia amemuonya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Bw. Eliud Mwaiteleke kwa matumizi mabaya ya fedha yanayofanywa na halmashauri hiyo na ametaka dosari hizo zirekebishwe mara moja. “Nataka ujirekebishe, wananchi hawa wanateseka sana” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato


Share:

WAZIRI KIGWANGALLA : KULETA KIBURI NA JEURI KWENYE MAZINGIRA HAYA NI UPUMBAVU


Baada ya Rais John Magufuli kuagiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Adolf Mkenda kumaliza tofauti zao vinginevyo atawaondoa, Kigwangalla ameibuka na kudai kuwa tayari walishamaliza tofauti zao na sasa hali ni shwari.

Kupitia akaunti yake ya Twitter na Instagram  amesema walishafanya kikao na Katibu Mkuu, Prof. Adolf Mkenda cha kumaliza tofauti zao.

“Kazi ya Urais ni ngumu sana, tulioteuliwa na Rais kumsaidia utendaji/usimamizi wa maeneo mbalimbali hatupaswi kumuongezea frustrations nyingine zaidi, sisi kwenye Wizara yetu, baada ya kikao na Chief Secretary tulimaliza tofauti zilizokuwepo na sasa hali ni shwari,” amesema Kigwangalla.

Ni imani na heshima kubwa sana kwako kuteuliwa kuwa Waziri kwenye nchi yako. Kwenye nchi ya watu milioni 60, kwa nini Hamisi KIGWANGALLA? Sijui. Ni neema na baraka za Mungu tu. Maana siyo kila mtu kwenye maisha yake atapata fursa ya kuhudumu kwenye serikali kama Waziri ama kama Katibu Mkuu kwenye serikali. Siibezi wala siwezi kuichezea fursa hii adhimu.

Ni kwa kuelewa ukweli huu na ushauri, mwongozo na maelekezo ya wakuu wa kazi, na watendaji wazoefu kwenye utumishi wa umma, kama Katibu Mkuu Kiongozi, tulikaa mimi na Katibu Mkuu wangu na kukubaliana kufungua ukurasa mpya wa mahusiano mazuri zaidi kwa manufaa ya nchi yetu.

Kuondolewa kwenye nafasi ya Uwaziri unaweza kuondolewa kwa sababu mbalimbali lakini kuondolewa kwa sababu watu wazima, tena viongozi, ambao mmepewa fursa ya kushauriwa, mmeshindwa kuelewana, ni upumbavu! Mimi siyo mpumbavu.

Kuleta kiburi na jeuri kwenye mazingira Haya ni upumbavu. Kwanza sisi waislam tunafundishwa kuwa wanyenyekevu, maana ‘kiburi’ ni sifa ya Mungu, siyo yetu wanadamu. Kufanya kiburi na jeuri ni upumbavu. Hekima ya Mungu ni kujishusha na kumshinda shetani.

Sina jeuri wala kiburi sababu nimelelewa vizuri na bibi yangu Mama Bagaile, na pia naogopa hasira za Mungu. Tumalizie haya masaa kwa amani! Happy New Year Good People. Nitaendelea kutoa darasa la mambo niliyojifunza 2019, na mipango yangu ya 2020.

Nipo jimboni nachunga ng’ombe wangu kidogo. Ningekuwa Dar ningemtembelea Prof. Mkenda kwa ajili ya picha tukigonga glass ili mjue tuko sawa 😀. Mhe. Rais yeye ana namna yake ya kupata taarifa zetu. Atazipata tu! 😀. Limeisha hilo au niongeze volume? 🤷🏾‍♂️ Wakatabahu Dkt. Hamisi KIGWANGALLA, MB., MNEC, WMU.
 


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano January 1, 2020





















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger