Friday 30 August 2019

SANAMU TATA YA TRUMP YAZUA GUMZO

Sanamu ya mbao ya Donald Trump, iliyotengenezwa na Tomaz Schlegl, ilisimamishwa wiki kadhaa baada ya sanamu ya Melania Trump

Sanamu ya mbao ya rais wa Marekani imejengwa katika nchi alikozaliwa mkewe ya Slovenia, imeibua maoni tofauti.

Ikiwa na urefu wa karibu futi 26, sanamu hiyo ilijengwa katika ardhi ya kibinafsi na inamuonyesha Donald Trump akiwa na kichwa cha muundo wa mraba na kidevu huku akiwa anyenyenyua kichwa juu.

Msanii aliyeitengeneza amekiambia shirika la habari la AFP kuwa alitaka iwe kama kielelezo cha maoni ya kisasa ya wanaohisi kuwa watawala wa kisiasa hawawajali.

Sanamu hii imewekwa baada ya ile ya mke wa trump, Melania inayomuonyesha akiwa na ulimi uliojaa ndani ya mashabu.

Sanamu ya Melania, iliyochongwa ndani ya mti viungani mwa mji alikozaliwa wa Sevnica, inamuonyesha akiwa amevalia koti la rangi ya blu huku mkno wake ukionyesha angani. baadhi ya wakazi wanaichukulia kama ''aibu'', na wanasema inaonekana zaidi kama katuni kuliko mke wa rais wa Marekani.Mnara huu wa Trump unaripotiwa kujengw ana msanii wa Slovenia Tomaz Schlegl


Sanamu mpya ya rais wa Marekani ilijengwa katika kijiji cha Sela pri Kamniku, yapata kilomita 30 kusini -mashariki mwa mji mkuu wa Slovania -Ljubljana.

Mbunifu wake, Tomaz Schleglameliambia shirika la habari la AFP kwamba alilenga kutoa maoni ya wengi kupitia sanamu.

"Kwa mara ya kwanza ttangu Vita ya II ya dunia ndio mara ya kwanzamaoni ya wengi yanajitokeza kupinga utawala uliopo : Mtazame waziri mkuu wa Uingere za Boris Johnson, tazama Trump, rais wetu au waziri mkuu wa Hungary Viktor Orban. Dunia hii inaelekea wapi ?," alisema. "Tunataka kufungua macho ya watu kuelewa demokrasia ni nini ."
sanamu ya Bwana Trump inamuonyesha akiwa amevalia shati la blu na tai nyekundu, huku akiwa amesimama mithili ya mnara wa uhuru wa New York.

Bwana Schlegl anasema muundo wa ndani ya sanamu ya mbao unairuhusu kubadilika kutoka "sura ya urafiki mnamo siku za kazi za wiki na kuwa na sura ya kutisha sana katika siku za wikendi ", ikiwa ni sihara ya unafiki wa wanasiasa wanaotaka kuonyesha kuwa wanawajali wale wanaohisi kuwa wamesahaulika.

Lakini mnara huu umeibua maoni tofauti . Shirika la habari la AFP ililishuhudia mkazi mwenye hasira akiendesha gari lake la trekta na kugonga mnara huo wa sanamu wiki hii wakati maandalizi ya kuufungua rasmi Jumamosi yakiendelea.

Baadhi ya wakosoaji wa sanamu hiyo wamelalamikia juu ya "uharibifu wa mbao " na wakasema isingepaswa kujengwa .

"Majirani zetu wanadai sanamu hii ina sura mbaya na kwamba haifai katika eneo letu hili zuri tambalale ," Alisema Bwana Mr SchleglMnara huu wa Trump unaripotiwa kujengwa na msanii wa Slovenia Tomaz Schlegl

Watu wa Slovania wana maoni tofauti kumuhusu Rais wa Marekani . Mji anakotoka mkewe Mellania umekuwa ni kitovu cha utalii tangu alipochaguliwa mwaka 2016.

Huku wageni wakija kupata taswira ya mahali alikozaliwa na kuishi enzi za utoto wake , wakazi wametengeneza bidhaa zenye nembo ya melania zikiwemo kandambili, keki na baga zenye sura ya Trump na zilizopambwa na jibini iliyotengenezwa kama " nyweli" za Trump.

Japokuwa sanamu ya Mke wa rais ikiibua ukosoaji mwezi uliopita , mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameliambia shirika la habari la AFP n kwamba kazi ya sanaa kuihusu lilikuwa ni " wazo zuri".

"Melania ni shujaa wa Slovenian , amefikia mafanikio ya juu nchini Marekani ," alisema Katarina, mwenye umri wa miaka 66.
Chanzo - BBC
Share:

RAIS MAGUFULI AKERWA NA CHANGAMOTO ZA UMASKINI BARA LA AFRIKA

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia Mkutano wa Sita Jukwaa la Uongozi la Afrika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam, Tanzania.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Rais John Magufuli wa Tanzania amesema masalia ya fikra za kikoloni walizonazo Waafrika wengi ni miongoni mwa sababu zinazofanya Bara la Afrika kushindwa kusimamia rasilimali zake ili kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.

Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akihutubia kongamano la viongozi la 2019 akisema dhana ya uhuru haiwezi kutenganishwa na kujitegemea.

“Kama hujitegemei huwezi kuwa huru, kwani uhuru wako utakuwa mikononi mwa unayemtegemea.”

“Maana hasa ya kupigania uhuru ni kurejesha rasilimali zetu na hasa rasilimali zetu, lakini pia kuwa na uamuzi kamili wa namna ya kuzisimamia na kuzitumia wa kuzitumia ili kuleta ukombozi wa kiuchumi,” amesema Rais Magufuli.

Amesema kutokana na kutoelewa dhana kamili ya uhuru, nchi za Afrika zinadhani watawala wa zamani ndiyo wenye uwezo wa kusimamia na kusaidia na kuendeleza rasilimali.

Ametaja pia sababu ya kushindwa kusimamia rasilimali na kuleta mageuzi ya kiuchumi, akisema fedha siyo msingi wa rasilimali.

“Fedha ni matokeo ya mwisho kabisa ya matumizi ya rasilimali zetu na siyo msingi wa maendeleo. Hata hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Hakutaja pesa, alijua itakuja tu kama yale tutayatimiza,” amesema.

Ametaja pia ukosefu wa ubunifu na teknolojia ya viwanda akisema Afrika haitaweza kusimamia na kutumia rasilimali zake kiuendelevu bila kuwa na viwanda.

Mbali na viwanda, ametaja kukithiri kwa migogoro na hali tete ya siasa barani Afrika akisema inasababishwa na mabeberu wanaotaka kuendelea kutumia maliasili za Afrika kwa manufaa yao.

“Wakati sisi tunapigana wao wanakula na kamwe hawatataka tuwe na amani, kwani migogoro ndiyo mtaji wao,” amesema.

Ameendelea kutaja pia tatizo la mikataba na makubaliano yanayoingiwa na wawekezaji katika kutumia rasilimali akisema, “Na hapa nchi yetu imeliwa sana kutokana na mikataba mibovu na hasa kwenye madini.”

Kuhusu uharibifu wa mazingira, Rais Magufuli amesema unasababishwa na ukataji hovyo wa msitu kwa ajili ya nishati ya majumbani kutokana na gharama kubwa za umeme na gesi asilia.

“Chanzo kingine ni uchafuzi wa mazingira unaofanywa na mataifa mengine yaliyoendelea na yenye viwanda vingi, lakini Afrika ndiyo inayoathirika zaidi a machafuko hayo,” amesema.

Akizungumzia hatua zilizochukuliwa na Serikali, Rais Magufuli amesema imetungwa sheria ya kulinda utajiri na rasilimali na maliasili ya 2017 na kupitiwa upya na kurekebisha mikataba ya uchimbaji na madini isiyo na manufaa kwa Taifa.

“Tumeweka msukumo mkubwa kwenye ujenzi wa viwanda na ukuzaji wa teknolojia ya viwanda ili mazao yanayotokana na rasilimali zetu yasindikwe kwanza kabla ya kuuzwa nje,” amesema

Alitaja pia uanzishwaji wa mradi wa bwawa la Nyerere utakaozalisha MW 2115 kwenye bonde la mto Rufiji kama njia ya kutunza mazingira, kudhibiti nidhamu za watumishi wa umma na kupamba na rushwa na ufisadi.

Wageni maarufu waliohudhuria mkutano huo walikuwa marais wastaafu kutoka baadhi ya nchi za Afrika akiwemo Thabo Mbeki wa Afrika Kusini, Olusegun Obasanjo wa Nigeria, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete wa Tanzania.
Share:

KAMPUNI ZA JAPAN ZENYE UZOEFU KWENYE MIRADI YA GESI ASILIA ZAONESHA NIA YA KUWEKEZA TANZANIA


Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dkt. James Mataragio akipeana mkono na Mtendaji Mkuu wa Chiyoda Corporation Ndg. Ken Nagao baada ya kikao baina ya ujumbe wa Tanzania na Kampuni ya Chiyoda. Wengine pichani kutoka kushoto ni Ndg. Pius Gasper (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Mhandisi Innocent Luoga, Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu (Wizara ya Nishati), Ndg. Katsuo Nagasaka (Chiyoda) na Ndg. Koji Nishita (Chiyoda).
Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika kikao na Kampuni ya JGC kilichofanyika sambamba na kilele cha Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD7). Upande wa kushoto ni Ndg. Kenji Yamamoto (JGC), Ndg. Masayuki Sato (JGC), Ndg. Yanamaka (JGC) na Ndg. Taketoshi Shogenji (JGC). Upande wa Kulia ni Mhandisi Innocent Luoga, Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu (Wizara ya Nishati), Dkt. James Mataragio, Mkurugenzi Mtendaji (TPDC) na Ndg. Pius Gasper (Tanesco).
***
Yokohama, Japan.

Kampuni kubwa za Japan zenye uzoefu wa miaka mingi katika miradi ya gesi asilia zimeonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania hususan katika mradi mkubwa wa kusindika gesi asilia (Liquefied Natural Gas-LNG). Kampuni za JGC na Chiyoda zenye uzoefu wa miaka mingi katika kazi za uhandisi, manunuzi na ukandarasi (EPC) hususan katika kutekeleza miradi ya LNG duniani zimekutana na ujumbe wa Tanzania uliohudhuria kilele cha Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD7) zikionyesha nia ya kushiriki katika mradi wa ujenzi wa mitambo ya kusindika gesi asilia (LNG).

Katika kikao hicho kilichofanyika sambamba na TICAD7, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Dkt. James Mataragio alisema “katika kipindi cha muongo mmoja, Tanzania imepiga hatua kubwa katika sekta ya mafuta na gesi asilia ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu mikubwa ya kusambaza gesi kwa ajili ya umeme, viwanda na majumbani”.

Dkt. Mataragio pia alieleza nia ya Serikali ya Tanzania kuwekeza katika utekelezaji wa mradi wa kimkakati unaokadiriwa kugharimu dola za marekani bilioni 30 na utahusisha uendelezaji wa kiasi kikubwa cha gesi asilia kilichogunduliwa katika kina kirefu cha bahari.

Dkt. Mataragio alieleza kwamba kwa sasa Serikali iko katika hatua za majadiliano ya vipengele muhimu vya mkataba wa Serikali mwenyeji (Host Government Agreemet-HGA) na kampuni za kimataifa zilizogundua gesi asilia katika kitalu namba 1, 2 na 4. Kitalu namba 1 na 4 vinaendeshwa na Kampuni ya Shell ikishirikiana na Ophir Energy na Pavilion wakati kitalu namba 2 kinaendeshwa na Kampuni ya Equinor ikishirikiana na ExxonMobil.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Chiyoda Corporation, Ndg. Ken Nagao alisema “Kwa miaka kadhaa sasa tumeshirikiana na Tanzania katika kuendeleza sekta ya gesi asilia na tunadhani tunaweza kushirikiana zaidi katika kutoa uzoefu tulionao wa zaidi ya miaka 50 katika ujenzi wa mitambo ya LNG”.

Kampuni ya Chiyoda imehusika katika ujenzi wa miradi mikubwa ya LNG ikiwemo Australia, Nigeria, Qatar na nchi nyingine nyingi ikiwa na pato ghafi la takribani Trilioni 7.2. Nae Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya JGC, Ndg. Masayuki Sato alieleza nia ya kampuni yake kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha Wananchi wake wanafaidika na rasilimali ya gesi asilia kwa kujenga mitambo ya LNG itakayowezesha uvunaji wa gesi asilia iliyogunduliwa katika kina kirefu cha bahari ya Hindi.

Akizungumza katika kikao hicho, Ndg. Sato alisema “Tumeshirikiana na Tanzania katika maandalizi ya mpango kabambe wa matumizi ya gesi asilia (NGUMP) na tusingependa kuishia hapo kwani tunadhani Tanzania ina fursa ya kuwa kituo kikubwa cha kuzalisha na kusambaza gesi asilia kwa nchi zenye mahitaji makubwa ya nishati na hivyo kukuza uchumi na pato la Taifa”.

JGC ni miongoni mwa kampuni kubwa katika ujenzi wa mitambo ya LNG na ujenzi wa miundombinu mingine katika mnyororo wa thamani wa gesi asilia, alifafanua zaidi Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa JGC.

Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga nae alieleza nia ya Wizara ya Nishati kuhakikisha gesi asilia inatumika katika kukuza uchumi wa ndani kwa kuisambaza kwa viwanda vingi zaidi ili kuchochea ajenda ya uchumi wa viwanda itakayosaidia Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Mpango kabambe wa matumizi ya gesi asilia unaainisha wazi kwamba tutatumia gesi yetu kusaidia kukuza uchumi na kunyanyua sekta nyingine kama vile viwanda, kilimo, uvuvi, usafirishaji na nyinginezo ili kubadilisha uchumi wa Taifa na watu wetu” alisema Mhandisi Luoga.
Share:

MTOTO MWINGINE ALIYEANGUKIWA NA BOMBA LA MAJI AFARIKI DUNIA


Mfano wa Bomba lililomwangukia mtoto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora ACP Brnabas Mwakalukwa, amesema kuwa mtoto aliyeangukiwa na bomba kubwa la maji mkoani humo, amefariki dunia wakati akipelekwa hospitali ya Bugando kwa ajili ya matibabu.

Mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya msingi Kiyungi iliyopo Manispaa ya Tabora, alipata majeraha siku ya Agosti 28 baada ya kuangukiwa na bomba kubwa la kupitisha maji, walipokuwa wakicheza na wenzao hali iliyopelekea mtoto mwenzake kufariki muda huo huo.

''Yule mtoto aliyelazwa ICU walifanya utaratibu wa kumpeleka Bugando lakini bahati mbaya akafariki njiani maeneo ya Nzega, na daktari akathibitisha kufariki kwake'' amesema ACP Mwakalukwa.

Mabomba yaliyosababisha madhira hayo ni ya mradi mpya wa usambazaji wa maji mkoani humo kutoka Ziwa Victoria, yaliyokuwa yamehifadhiwa kwenye kiwanja cha shule hiyo.
Share:

Job opportunities at I&M Bank

Information Security Officer l&M Bank (T) Ltd, a subsidiary of l&M Group which has presence in Kenya, Tanzania, Rwanda and Mauritius invites applications from suitably qualified candidates to fill the following available positions. JOB TITLE:  INFORMATION SECURITY OFFICER REPORTS TO:  HEAD OF RISK JOB PURPOSE: Protecting organization’s computers, networks and data against threats, such as security breaches, computer viruses… Read More »

The post Job opportunities at I&M Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nafasi za kazi TADEPA- Jobs at TADEPA August 2019

Information about TADEPA Tanzania Development and AIDS Prevention Association (TADEPA) is a Tanzanian Nongovernmental organization (NGO) currently offices in Kagera, Geita, Shinyanga and Dodoma regions. Was formed and registered in 1997 and acquired mandated to work in all regions of Tanzania mainland. The main purpose of TADEPA is to promote development in totality through and fight against public… Read More »

The post Nafasi za kazi TADEPA- Jobs at TADEPA August 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at Vodacom, Head of Revenue Assurance

Head of Revenue Assurance   Role purpose: The key purpose of the Head of Revenue Assurance is to ensure completeness and accuracy of the company revenue streams across CBU, EBU and M-Pesa Units. In addition to checking on the integrity of systems in place, the position requires an inclination towards continuous improvements in revenue chain, proactive design and implementation… Read More »

The post Job Opportunity at Vodacom, Head of Revenue Assurance appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at NETIS Tanzania, Project Sheq officer

JOB TITLE: Project Sheq officer INDUSTRY: Telecommunication LOCATION: Dar es Salaam. ROLE PURPOSE To ensure that NETIS’s Quality, Safety, Health, Social, Security, Cultural, Environmental and Risk Management systems are defined, implemented, maintained and adhered to according to best practice standards at all levels of the organisation within Tanzania. KEY PEFORMANCE AREAS Document and communicate all SHERQ manuals and policies… Read More »

The post Job Opportunity at NETIS Tanzania, Project Sheq officer appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

11 Job Vacancies at BAK-AID Tanzania

EXCITING CAREER OPPORTUNITIES OVERVIEW BAKWATA NATIONAL HIV/AIDS PROGRAM (BAK-AIDS) is a Faith Based Organization (FBO) implementing HIV programs to support Tanzania Government efforts to reduce the rate of HIV pandemic in Tanzania. Since inception, BAK-AIDS has played a big role in supporting Tanzania’s social development initiatives by implementing health programs which include HIV and AIDS education and other… Read More »

The post 11 Job Vacancies at BAK-AID Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Wizara ya elimu (MOE): Commonwealth scholarships tenable in the United Kingdom 2020

Wizara ya elimu (MOE): Commonwealth scholarships tenable in the United Kingdom 2020: scholarships for tanzanians to study in tanzania, how to apply for commonwealth scholarship, commonwealth scholarship 2019/2020, tanzania scholarship 2019, how to apply for commonwealth scholarship 2019, what is commonwealth scholarship, commonwealth scholarship 2020, commonwealth scholarship application portal. The Ministry of Education, Science, and Technology as a… Read More »

The post Wizara ya elimu (MOE): Commonwealth scholarships tenable in the United Kingdom 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ardhi University- How to confirm selection 2020- Maelekezo jinsi ya kuthibitisha udahili kwa waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja

Ardhi University- How to confirm selection 2020- Maelekezo jinsi ya kuthibitisha udahili kwa waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja- Ardhi University (ARU) 2019. The Ardhi University (ARU) was established after transforming the former University College of Lands and Architectural Studies (UCLAS) which was then a constituent college of the University of Dar es Salaam from 1st July 1996. The… Read More »

The post Ardhi University- How to confirm selection 2020- Maelekezo jinsi ya kuthibitisha udahili kwa waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Ardhi University 2nd Round selection release date

Ardhi University 2nd Round selection release date 2019 The Ardhi University (ARU) was established after transforming the former University College of Lands and Architectural Studies (UCLAS) which was then a constituent college of the University of Dar es Salaam from 1st July 1996. The history of Ardhi University, however, dates back to 1956 when the then Surveying Training… Read More »

The post Ardhi University 2nd Round selection release date appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nafasi 61 za kazi Muhimbili National Hospital

Job opportunities at Muhimbili National Hospita (MNH) VACANCIES ANNOUNCEMENT AT MNH On behalf of the Muhimbili National Hospital (MNH), Public Service Recruitment Secretariat invites qualified Tanzanians to fill 61 vacant posts as mentioned below. A tertiary specialised and super specialist Hospital in Tanzania organized into nine directorates with bed capacity of 2,178 out of which 1,570 beds are… Read More »

The post Nafasi 61 za kazi Muhimbili National Hospital appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WAUMINI WASUSIA IBADA WAKIDAI PASTA MGENI BADO MBICHI HAJAOA 'ATAHARIBU BINTI ZAO'

Kisanga cha aina yake kimezuka katika kanisa moja la Gachororo, kaunti ya Kiambu nchini Kenya baada ya washirika kukosa kuhudhuria ibada wakidai pasta mgeni aliyetumwa kuwahudumia hakuwa na mke. 

Kondoo hao walisema kwamba, mtumishi alikuwa barobaro mwenye umri mdogo na kudai huenda alikuwa na njama fiche kanisani humo. 

Kwa mujibu wa Taifa Leo, washirika hao walianza kuondoka kanisani mmoja baada ya mwingine pindi tu mtumishi huyo aliposimama na kujitambulisha. 

Penyenye zinaarifu kwamba washirika hao walielezea wasiwasi wao kuhusu umri mdogo wa pasta kwani walihofia huenda akawa tishio kwa mabinti zao.

"Hata hajaoa. Mabinti zetu wataponea kweli. Huyu hapana. Huyu ni pasta hatari," washirika walisikika wakiteta.

 Inasemekana, pasta alijaribu kuwatuliza washirika hao na kuwaambia nia yake pale ilikuwa ni kueneza ijili ya Bwana na wala sio mambo mengine.

"Hayo hayawezekani. Nyinyi ni kama mnafanya biashara na kanisa. Rudi kwenu ukomae kwanza," mshirika mmoja alimfokea mchungaji. 

Duru zinaarifu kwamba, mtumishi huyo alikuwa amepewa uhamisho hadi tawi la kanisa hilo na kutoka alikokuwa akihubiri. 

Jaribilo la wazee wa kanisa kutuliza hali lilizua mzozo mkali huku waumini wakiwafokea na kuwataka kumshauri barobaro huyo kutafuta kazi nyingine ya kufanya na wala sio kuchunga kondoo. 

Penyenye zinaarifu kwamba, washiriki hao walimpa pasta muda wa siku mbili kusanya virago na kurejea alikotoka mara moja. 

 "Sisi hapa hatutaki kesi na wewe. Wasichana wetu wangali shuleni. Damu yako jinsi tunavyoiona ingali moto. Jipange uende kuhubiri kanisa lingine," waumini walizidi kumuonya pasta.

 Inadaiwa wazee walinza kuondoka mmoja baada ya mwingine na kumwacha pasta pekee yake baada ya kushindwa kudhibiti hali kanisani.
Share:

WADAU WA NAFAKA WAKUTANA DAR KUJADILI FURSA


 Wadau wa mazao ya nafaka, wakimsikiliza Waziri wa Kilimo Mhe. Japhate Hasunga wakati akihutubia mkutano wa siku mbili wa Wafanyabiashara wa Nafaka Ndani na Nje ya Nchi  kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam 
 Mhe. Waziri Hasunga.
 Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga akihutubia mkutano huo.
 Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF)Dkt.Hoseana Lunogelo, akiwasilisha mada kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses).
 Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF)Dkt.Hoseana Lunogelo, akiwasilisha mada kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storagefacilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses).
 Bi. Margareth Nzuki (katikati), akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF akifuatilia kwa makini mada iliyokuwa inawasilishwa na Dkt. Bunogelo kuhusu utafiti ambao ulifanywa na Taasisi hiyo kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage
facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses)
.

 Mkuurgenzi Mtednaji wa Benki ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw.Japhet Justine akipiga makofi wakati mkutano huo ukiendelea.
 Mjumbe akifuatilia kwa makini mkutano huo.
  Mjumbe akifuatilia kwa makini mkutano huo.
 Bi.Margareth Nzuki (kushoto), kutoka ESRF akibadilishana mawazo na Bi. Vumilia L. Zikankuba kutoka Wizara ya Kilimo wakati wa mkutano huo.
 Mshiriki akitoa maoni yake.
 Oswald Mashindani (kushoto), kutoka ESRF akizunhumza jambo mbele ya Katibu Mkuu (mstaafu) Wizxara ya Fedha, Bw. Paniel Lyimo (katikati) wakati wa mkutano huo.
 Mhe. Hadsunga (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na manaibu waziri makatibu wakuu na Mwenyekiti wa TPSF.
 Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo unaofikia kilele leo Agosti 30, 2019.
 Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo unaofikia kilele leo Agosti 30, 2019.
Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo unaofikia kilele leo Agosti 30, 2019.
***
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

MKUTANO wa siku mbili wa Wafanyabiashara wa Nafaka Ndani na Nje ya Nchi umefunguliwa na Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo Agosti 29, 2019.

Mkutano huo ambao umewajumuisha wasindikaji, wasafirishaji na wamiliki wa maghala ya nafaka Lengo lake ni kuangalia fursa zilizopo kwenye tasnia ya nafaka na jinsi ya kuzifikia ikiwa ni pamoja na masoko.

Akizungumza na washiriki wa mkutano huo uliowakutanisha wadau kutoka mikoa mbalimbali  nchini, Mhe. Hasunga ambaye alifuatana na Manaibu wake, Mhe. Husein Bashe, na Mhe. Omary Mgumba alisema mkutano huo utatoa fursa kwa wajumbe kuelimishwa kuhusu fursa ya biashara ya mazao ya nafaka katika soko la Afrika, uwezo wa Tanzania kuzalisha na nafasi ya wafanyabiashara kushiriki kikamilifu lakini pia washiriki watapata fursa ya kujifunza athari za upotevu wa mazao ya nafaka baada yamavuno na mkakati wa serikali kudhibidi hali hiyo.

“Kitaalamu wanasema utafiti uliofanyika Tanzania na  nchi nyingi za Kusini asilimia 40 ya mazao yote yakiwemo ya nafaka yanapotea baada ya mavuno kwa kuharibika na matatizo mengine, hii haikubaliki mkulima amewekeza, amevuna halavu mazao yake yanaharibika, lazima tuwe na mkakati wa kuzuia hali hii.” Alitoa hakikisho Mhe. Waziri Hasunga na kuongeza.

Kulingana na uzalishaji uliopo, nafaka nyingi kama mahindi mtama na nafaka nyingine huhifadhiwa katika kiwango kisichoridhisha hali hii huchangia kupoteza ubora wa nafaka na hatimaye huchangia kuzorota kwa ustawi wa afya zetu, alifafanua zaidi Mheshimiwa Waziri.

Alisema Agosti 1, mwaka huu kwenye sherehe za Nanenane kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muunganow a Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alizindua mkakati wa namna ya kupambana na kudhibiti upotevu wa mazao baada ya mavuno.

Katika utafiti wake ilioufanya hivi karibuni Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) chini ya Mradi wa Rapid Response Implementation Support to the Ministry of Agriculture and Agriculture Sector Lead Ministry (RARIS) unaofadhiliwa na Taasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation umebaini kuwa hali ya maghala mengi ya watu binafsi hayatoi taarifa serikalini na hii ni kutokana na mfumo wa sasa wa maghala.

Akitoa mada kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses), Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Dkt.Hoseana Lunogelo alisema ESRF ilifanya utafiti wa hali (status) ya maghala nchini na kubaini kuwa maghala ya watu binafsi hayalazimiki kisheria kutoa taarifa serikalini kuhusu nini kimehifadhiwa na kiasi gani cha nafaka kilichohifadhiwa ndani ya maghala hayo na hali hii serikali inategemea tu maghala ya Serikali yaani (Public Storage Facilities ) kupitia Werehouse Reseat Regulatory Board ili kujua takwimu za hali ya chakula nchini.

“Kwa sasa kuna maghala 3,430 yaliyopo kati ya hayo ni 185 tu ndiyo kuna uhakika wa kupata tawimu endapo zitahitajika lakini yaliyosalia huwezi kupata takwimu hizo kwa sababu hakuna sheria inayowalazimisha kufanya hivyo.” Alifafanua Dkt. Lunogelo.

Alisema hii ni changamoto kubwa, kama serikali inapata taarifa kutoka kwenye maghala machache sana nchini na yale mengi haipati taarifa zake, maana yake Serikali haiwezi kufanya maamuzi sahihi kuhusiana na upatikanaji wa chakula nchini na hiyo ina athari mbaya kwenye usalama wa chakula na pia ina athari mbaya pia kwenye biashara.” Alsiema Dkt. Lunogelo.
Share:

AMUOMBA MSAMAHA MAGUFULI BAADA KUUA MKEWE KWA KUMCHOMA VISU KISHA KUJIUA KWA KUJIKATA KOROMEO


Jovither Kaijage, Ukerewe
Mkazi wa Kijiji cha Kagera wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, Celestin Masatu (39) amejichoma kisu tumboni, kujikata kolomeo na kufa baada ya kumfanyia ukatili mkewe Jenifa Julias (30) wa kumchanachana mwilini na kisu, huku akiacha ujumbe akiomba msamaha kwa Rais John Magufuli kwa kitendo alichokifanya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi, saa 7.15 usiku, katika nyumba ya kulala wageni ya Emma iliyoko eneo la kata ya Nakatungulu mjini Nansio.

Alisema baada ya kumchoma visu mkewe na baadaye kujichoma kisu na kujikata koromeo, majeruhi hao wote walikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya mjini Nansio usiku huo huo ili kupatiwa matibabu lakini Masatu alipoteza maisha asubuhi siku iliyofuata wakati mkewe akihamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

Kamanda huyo alisema kabla ya kujidhuru kwa kujichoma na kisu tumboni, kisha kukatakata utumbo wake na baadaye kolomeo, Masatu alimchoma visu tumboni na shingoni mkewe na kusababisha utumbo na mfuko wa kizazi uliokuwa na mtoto mchanga wa miezi miwili kutoka nje.

Alisema wawili hao, awali waliwahi kuishi pamoja kama mme na mke na walijaliwa kupata watoto wawili kabla ya mwanamke kuamua kuondoka na vifaa vya nyumbani na kwenda kuishi peke yake katika kijiji cha Bukongo.

Alisema hata hivyo katika siku za hivi karibuni walirejesha mahusiano yao ya ndoa na hadi siku hiyo ya tukio walikubaliana wakutane lakini kumbe mwanaume alikuwa na mpango wa kumdhuru mwenzake kwa sababu ya wivu wa mapenzi.

Baada ya Polisi kufanya upekuzi kwenye chumba walichofikia, mbali ya kupata kisu kilichotumika kuwadhuru na vitu vyao vingine kama nguo na viatu, pia lilipatikana daftari lenye maandishi yanayosadikika kuandikwa na Masatu akiomba msahama kwa Rais Magufuli kwa kosa alilolifanya na mgawanyo wa mali zake.

“Sehemu ya barua hiyo imeandikwa hivi, nanuku: ‘Naomba radhi kwa serikali inayoongozwa na Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli kwa kitendo nilitakachofanya kwa hiari yangu.’ Mmiliki wa nyumba ya kulala wageni ya Emma, Musiba Mayunga alisema alishitushwa na kelele za mwanamke akiomba msaada usiku wa manane na alipowataka wafungue mlango, mwanaume alikataa ndipo aliomba msaada wa uongozi wa kitongoji na Polisi.

Alisema kelele hizo ziliwaamusha wageni wengine waliofikia kwenye nyumba yake na ndio waliofanikiwa kuvunja mlango wa chumba na kuwatoa wanandoa hao wakiwa na majeraha.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Sokoni, Kata ya Nakatungulu, Celestin Mangwesa alisema baada ya kujulishwa na kufika eneo la tukio, alishuhudia mwanamke akitoka nje ya chumba utumbo ukiwa nje. Alisema mwanaume aligoma kutoka hadi Polisi walipowasili na kuamua kuingia ndani ndipo akatolewa akiwa amepoteza fahamu kutokana na majeraha makubwa aliyokuwanayo.
Share:

MAHAKAMA YAELEZWA MWANDISHI WA HABARI ERICK KABENDERA KAPOOZA MGUU,ANA SHIDA YA KUPUMUA

Upande wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera, wameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kulielekeza Jeshi la Magereza mteja wao kwenda kupimwa katika hospitali ya Serikali.

Wakili wa utetezi, Jebra Kambole amedai leo Ijumaa Agosti 30, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Janeth Mtega baada ya Wakili Mwandamizi wa Serikali Wankyo Saimon kueleza upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Wakili Kambole amedai usiku wa kuamkia Agosti 2, 2019 mteja wake akiwa gerezani alianza kuumwa na hadi leo ana shida ya kupumua.

"Nilienda kumuona nikakuta amepooza mguu na kushindwa kutembea kwa siku mbili pamoja na kuishiwa nguvu, sisi kama mawakili na ndugu hatujui nini anachoumwa."

"Kwa kuwa mteja wetu hajapata vipimo ambavyo vinastahili tunaomba Mahakama ielekeze Jeshi la Magereza mteja wetu akapimwe katika hospitali yoyote ya serikali ikiwemo Muhimbili penye vipimo vya uhakika," amedai Wakili Kambole

Wakili Wakyo amedai swala la ugonjwa hakuna mtu anayeweza kupingana nalo lakini huwezi kulielekeza Jeshi la Magereza kwenda kumpima katika hospitali fulani.

"Mahakama yako haiwezi kuamuru kupelekwa hospitali fulani kwa kuwa hajawahi kuwasilisha maombi akakataliwa lakini sheria inasema makosa ya uhujumu uchumi yanasikilizwa na Mahakama Kuu hivyo Mahakama hii haina uwezo wa kutoa uamuzi wowote" ameeleza Wakili Wankyo

Via Mwananchi
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger