Thursday 30 May 2019

Picha : DC MBONEKO AFUNGA MASHINDANO YA UMISSETA MKOANI SHINYANGA... ASISITIZA VIJANA KUBEBA MAKOMBE KITAIFA




Na Marco Maduhu - Malunde1 blog 

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, amefunga rasmi mashindano ya michezo kwa shule za Sekondari (UMISSETA 2019) Mkoani Shinyanga, na kuwataka washindi watakaoungana na kuwa timu moja ya mkoa, wakashiri kikamilifu katika mashindano hayo ngazi ya kitaifa huko Mtwara, na kupata ushindi wa makombe mengi.


Mashindano hayo ya (UMISSETA) yalifunguliwa na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack Mei 27, 2019 ambapo yamefungwa leo Mei 30 na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, kwenye viwanja vya CCM Kambarage mjini humo, ambapo washindi wamepewa zawadi  za makombe.

Mashindano yalishirikisha timu mbalimbali kutoka halmashauri ya Kahama Mji, Msalala, Ushetu, Kishapu, Shinyanga na Manispaa ya Shinyanga  kwa kuchezwa mpira wa miguu, kikapu, pete,tenesi, wavu, riadha, kucheza ngoma, pamoja na kuimba kwaya.

Akizungumza wakati akifunga mashindano hayo,Mboneko  amewataka washiriki ambao watachaguliwa kuwa timu moja za kwenda kushiriki (UMISSETA) ngazi ya kitaifa, wawe kitu kimoja na kutobaguana kuwa huyo anatoka halmashauri nyingine, bali washindane kama timu moja ambayo inatoka mkoani Shinyanga na hatimaye kuibuka na ushindi.

“Nawapongeza wanafunzi wote mlioshiriki kwenye mashindano haya ya (UMISSETA) ambapo mmeonyesha vipaji vyenu na wote ni washindi, lakini hamtaweza wote wanafunzi 704 kwenda kushiriki ngazi ya kitaifa, bali tutachagua wanafunzi 120 ili wakatuwakilishe na tunataka mrudi na makombe mengi,” amesema Mboneko.

“Na mtakapokuwa kambini muwe timu moja na kutobaguana kuwa huyu anatoka halmashauri hii, sitaki kitu kama hicho bali nataka muwe ndugu kwani nyie wote mnatoka Shinyanga, na mkashindane kweli kweli kwa kuonyesha vipaji vyenu na kuupatia sifa mkoa wetu,”ameongeza.

Pia amewataka washindi ambao watachaguliwa kwenda kushiriki mashindano hayo ngazi ya kitaifa, wakaonyeshe nidhamu ya hali ya juu na siyo kwenda kuchafua sifa ya mkoa.

Naye Afisa Elimu mkoa wa Shinyanga Mohamed Kahundi, amewataka wanafunzi hao pindi watakapokuwa huko Mtwara, waonyeshe vipaji vyao ikiwa michezo ni ajira kwa sasa.

Aidha washindi waliopatikana kwenye mashindano hayo ya (UMISSETA) Mwaka 2019 mkoani Shinyanga, mpira wa miguu wavulana ni halmashauri ya Msalala, wasichana halmashauri ya Shinyanga, mpira wa mikono (Handball) wavulana  Manispaa ya Shinyanga, wasichana Kishapu, Volleyball  Manispaa ya Shinyanga, wasichana halmashauri ya Shinyanga.

Kwa upande wa mpira wa kikapu wavulana na wasichana washindi ni kutoka halmashuri hya Shinyanga, mpira wa pete Kahama Mji, Tenesi mshindi wavulana na wasichana ni Halmashauri ya Shinyanga , riadha wavulana Shinyanga, wasichana Kishapu, ngoma kutoka Ushetu, kwaya Kahama Mji, usafi na nidhamu wavulana Kahama Mji, wasichana Shinyanga.

Hata hivyo katika mashindano hayo ya UMISSETA (2019) Mshindi wa jumla alitoka halmashauri ya Shinyanga , huku kauli mbiu ya mwaka huu inasema ‘MICHEZO NA SANAA KWA ELIMU BORA NA AJIRA.’

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akifunga rasmi mashindano ya michezo ya UMISSETA 2019 na kuwataka washindi ambao wamechaguliwa kushiriki ngazi ya kitaifa wakawe kitu kimoja na kupata ushindi wa makombe mengi. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Afisa elimu mkoa wa Shinyanga Mohamed Kahundi akiwataka wanafunzi ambao wamechaguliwa kwenda Mtwara kwenye mashindano hayo ya (UMISSETA) wakaonyeshe nidhamu ya hali ya juu.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akifungua fainali ya mashindano ya (UMISSETA 2019) kati ya timu ya mpira wa miguu Kahama Mji na Msalala huku kwa upande wa wasichana ni Kahama Mji na Shinyanga , na kuwataka wacheze kwa nidhamu kwa kuonyesha vipaji vyao.

Fainali ikiendelea kuchezwa kati ya timu ya Kahama Mji wenye jezi ya njano pamoja na Msalala wenye jezi nyekundu, ambapo hadi dakika 90 zinakamilika walitoka sare ya kufungana goli moja kwa moja na hatimaye kwenda kwenye matuta ili mshindi aweze kupatikana.

Penati/Matuta yakipigwa ambapo Msalala waliibuka na ushindi wa magoli 4 kwa matatu dhidi ya Kahama Mji na hatimaye kuwa mabingwa rasmi kwa mpira wa miguu katika UMISSETA Mwaka (2019) Mkoani Shinyanga.

Mchezo wa Fainali wa mpira wa miguu ukichezwa kati timu ya wasichana ya Shinyanga wenye Jezi ya Lightblue, na Kahama Mjini wenye Orange, ambapo Shinyanga waliibuka na ushindi wa goli moja na kuwa mabingwa.

Wanafunzi kutoka halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama wakiangalia fainali ya michezo ya mpira wa miguu kwa wasichana na wavulana kwenye hitimisho la mashindano ya (UMISSETA) 2019 Mkoani Shinyanga.

Wanafunzi kutoka halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama wakiangalia fainali ya michezo ya mpira wa miguu kwa wasichana na wavulana kwenye hitimisho la mashindano ya (UMISSETA) 2019 Mkoani Shinyanga.

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali mkoani Shinyanga pamoja na walimu wao wakiwa wanaangalia fainali ya mpira wa miguu ya wasichana na wavulana kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya (UMISSETA) mkoani Shinyanga.

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali mkoani Shinyanga pamoja na walimu wao wakiwa wanaangalia fainali ya mpira wa miguu ya wasichana na wavulana kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya (UMISSETA) mkoani Shinyanga.

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali mkoani Shinyanga pamoja na walimu wao wakiwa wanaangalia fainali ya mpira wa miguu ya wasichana na wavulana kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya (UMISSETA) mkoani Shinyanga na kusubiri washindi kupewa makombe yao.

Wadau wakishuhudia fainali ya mashindano ya UMISSETA.

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali mkoani Shinyanga wakiwa wanaangalia fainali ya mpira wa miguu ya wasichana na wavulana kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya (UMISSETA).

Hamasa zikitolewa uwanjani.

Wanafunzi kutoka Ushetu wakitoa burudani ya ngoma.

Awali mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akisalimiana na wachezaji wa timu ya Msalala kabla ya kuanza kucheza fainali na timu ya Kahama Mji, kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya UMISSETA Mkoani Shinyanga mwaka 2019 kwenye uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga Mjini.

Awali mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akisalimiana na wachezaji wa timu ya Kahama Mji, kabla ya kuanza kucheza fainali na timu ya Msalala kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya UMISSETA Mkoani Shinyanga mwaka 2019 kwenye uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga Mjini.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akikabidhi Kombe kwa mshindi wa mpira wa miguu kutoka halmashauri ya Msalala.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akikabidhi kombe kwa washindi wa mpira wa miguu kwa upande wa wasichana kutoka halmashauri ya Shinyanga.

Ukabidhiwaji wa makombe kwa washindi ukiendelea kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya UMISSETA mkoani Shinyanga mwaka 2019.

Ukabidhiwaji wa makombe kwa washindi ukiendelea kwenye hitimisho la mashindano ya michezo ya UMISSETA Mkoani Shinyanga mwaka 2019.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akikabidhi Kombe kwa mshindi wa jumla kwenye hitimisho la mashindano hayo ya michezo ya UMISSETA Kutoka halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Awali makombe yakiandaliwa tayari kwa kukabidhiwa washindi wa mashindano ya michezo ya UMISSETA mkoani Shinyanga mwaka 2019.

Waamuzi nao wakiwa kwenye picha ya pamoja.

Awali mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akiwasili kwenye uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga Mjini kwa ajili ya kufunga Rasmi mashindano ya michezo ya UMISSETA Mkoani Shinyanga Mwaka 2019.

Na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:

KAMPUNI YA JATU KUFANYA MKUTANO MKUU WA WANAHISA WAKE JUMAMOSI,JUNI MOSI JIJINI DAR


Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare
***
Mkutano mkuu wa Kampuni ya Umma ya Jenga Afya, Teketeza Umaskini (Jatu TLC) umepangwa kufanyika Jumamosi June Mosi, katika Ukumbi wa Mgulani jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, wanachama wa Kampuni hiyo watachagua viongozi wapya wa bodi ambao watakua na jukumu la kuingiza kampuni hiyo kwenye soko la hisa ( DSE)

Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare alisema kuwa kampuni hiyo itaingia rasmi kwenye soko la hisa mapema mwezi August kwa mtaji wa Shilingi Bilion 7.5

Akizungumzia kampuni hiyo alisema ilianzishwa na vijana 2015 kuhusiana na masuala ya afya na lishe na haki za binadamu, watu wengi wanapata changamoto kwenye masuala mbali mbali, "Wengi ni maskini wanashindwa kumudu gharama za maisha na kusababisha migogoro kwenye jamii,"alisema na kuongeza

"Tuwe na afya lakini tuweze kujitegemea na kuwa na afya nzuri, tumejikita kwenye kilimo, masoko na bima ya afya, watu wengi wanahitaji kuwekeza katika biashara na kuhitaji mikopo.

Alisema kampuni hiyo ya umma imesajiliwa mwaka 2016 na imefanikiwa katika Kilimo cha Mpunga Kilombero, Manyara kilimo cha Alizeti na Mahindi, Tanga kulimo cha Maharage.

"Tunawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao watawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

"Igima kiwanda cha kukoboa mchele, Kibaigwa kiwanda cha mahindi na alizeti, tunaunganisha kilimo na viwanda, na soko tumelitengeneza wenyewe."

Alisema Jatu unaponunua chochote kama chakula, ni rahisi kukuza faida Kwani kuna mfumo rasmi wa kugawa faida, mteja akinunua bidhaa anapata bonasi ambapo gawio analipata mwisho wa mwezi.

Alisema kampuni hiyo imekuwa inawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao wanawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

“Kilimo kinalipa ukikitilia manani, Jatu tuna watu zaidi ya 13,000 ambao wanafanya kilimo na biashara, kama kampuni tunanufaika pia na kupata mazao moja kwa moja kutoka kwa mkulima bila kupitia kwa madalali wa kati.” alisema 


Alisemaunaweza kujiunga kwa kuuza bidhaa upata mgao kila mwezi au ujiunge kwenye kilimo, au kununua hisa kupata gawiwo ukapata faida kutokana na faida ya kampuni.
Share:

Picha : WOMEN FUND TANZANIA YATAMBULISHA MRADI WA KUWEZESHA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KITAIFA WA KUZUIA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO SHINYANGA

Shirika lisilo la kiserikali la Women Fund Tanzania linalofanya shugghuli za utetezi wa haki za wanawake na ujenzi wa tapo ya wanawake Tanzania lenye makao yake jijini Dar es salaam limetambulisha rasmi Mradi wa Kuwezesha Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Mradi huo wa “Support for the implementation Fund for National Plan of Action to End Violence Against Women and Children” umezinduliwa na kutambulishwa rasmi leo Alhamis Mei 30,2019 wakati wa Kikao cha Wadau wa Haki za Wanawake na Watoto na upingaji wa ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wilaya ya Shinyanga kilichofanyika katika Ukumbi wa Karena Hoteli Mjini Shinyanga.

Akizindua Mradi huo,Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga,Boniface Chambi kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo,alisema mradi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

“Tunawashukuru sana Women Fund Tanzania kwa kutuletea mradi huu katika halmashauri yetu,ninachoweza kusema huu ni mfuko wezeshi kwa jamii,sisi kama serikali tutatoa ushirikiano,kinachotakiwa sasa ni kuwa na mawasiliano kati ya Women Fund Tanzania na wadau watakaowezeshwa/ watakaopata ruzuku,toeni taarifa serikalini”,alisema Chambi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania, Carol Francis Mango alisema mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu kama majaribio katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

“Tumeichagua halmashauri hii iwe ya mfano kwa sababu kuna matukio mengi ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto,ili kufanikisha mradi huu tutatoa ruzuku kwa mashirika ya wanawake na wasichana kwa ajili ya utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya ukombozi wa mwanamke na msichana”,alieleza Mango.

“Miongoni mwa Watekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na ambao ndio walengwa wa mradi huo ni Halmashauri,Mashirika,taasisi na asasi zisizo za kiserikali ‘NGOs’,mabaraza ya watoto na jamii kwa ujumla”,aliongeza.

Aidha alisema lengo la WFT ni kuchangia harakati za kutetea haki za wanawake,kuwawezesha na kuendeleza mikakati ya ujenzi wa vuguvugu la utetezi wa nguvu za pamoja ili kukuza haki na usawa wa wanawake kimapinduzi nchini.

“Sisi ni mfuko wa kwanza na pekee unaolenga kutoa ruzuku kwa ajili ya kuendeza shughuli za utetezi wa haki za wanawake hususani waliopo kwenye ngazi ya jamii.Tunataka kuchangia katika kujenga tapo la wanawake imara nchini Tanzania kwa kufadhili na kuimarisha uwezo wa wanawake kwa njia ya kuendeleza mikakati ya kuunganisha nguvu za pamoja na kutafuta rasilimali”,aliongeza.

Aidha alisema shirika hilo liko mbioni kufungua ofisi mkoani Shinyanga ili kurahisisha uratibu wa shughuli za mradi huo mkoani Shinyanga.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga, Boniface Chambi akitambulisha na kuzindua Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Kijamii la Women Fund Tanzania. Kushoto ni Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango,kulia ni Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,Deus Mhoja . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Sehemu ya Wadau wa Haki za Wanawake na Watoto wilaya ya Shinyanga wakiwa katika Ukumbi wa Karena Hoteli Mjini Shinyanga.
Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga,Boniface Chambi akitambulisha na kuzindua Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akitoa wasilisho la Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akielezea kuhusu Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Wadau wakimsikiliza Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akiendelea kufafanua kuhusu mradi huo.
Mratibu wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akielezea malengo ya kikao cha wadau wa haki za wanawake na watoto.
Mratibu wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia  akizungumza ukumbini.
Wadau wakiwa ukumbini.
Afisa kutoka Women Fund Tanzania,Neema Msangi akifafanua jambo ukumbini.
Mdau, Kassabrankahr Herman kutoka shirika la AGPAHI akiuliza swali wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Afisa Mabadiliko ya tabia,mawasiliano na jinsia - Mradi wa Sauti shirika la Engender Health Tanzania,Matilda Nombo akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Mkurugenzi wa shirika la TVMC,Musa Jonas Ngangala akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Mkurugenzi wa shirika la Agape ACP, John Myola akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Wadau wakifuatilia matukio ukumbini.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,Ngasa Mboje akilishukuru shirika la Women Fund Tanzania kupeleka mradi katika halmashauri yao na kuahidi kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa mradi.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Dkt. Rashid Mfaume akitoa neno la shukrani kwa Women Fund Tanzania na kueleza kuwa uongozi wa mkoa wa Shinyanga umepokea mradi huo na wapo tayari kutoa ushirikiano wote kufanikisha malengo ya mradi huo unaolenga kuwakomboa wanawake na watoto.
Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Mhoja akiwahamasisha wadau wa haki za wanawake na watoto kuchangamkia fursa ili kuhakikisha jamii inaondokana na mambo maovu.
Mkuu wa Progamu kutoka Women Fund Tanzania,Carol Francis Mango akiwaomba wadau wa haki za wanawake na watoto kushirikiana na WFT kutetea haki za wanawake na watoto.
MC wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto, Elizabeth Mweyo akitoa maelekezo ukumbini,
Picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa Mradi wa Kusaidia Utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kuzuia Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.
Picha ya pamoja.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Share:

Naibu Waziri Nditiye Awataka Watanzania Kusoma Kwanza Maelekezo Ya Tiketi Kabla Ya Kukata Tiketi Ili Kuondoa Migogoro.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye amewataka watanzania  Kuwa na desturi ya kusoma kwanza maelekezo yaliyopo kwenye tiketi  ya kusafiria  pindi wanapotaka kusafiri ili kuondoa migongano na migogoro baina yao na Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri. 

Mhe.Nditiye ameyasema hayo Mei 30,2019 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa ShauriMoyo  Mhe.Mattar Ali Salum  aliyehoji juu ya  baadhi ya kampuni za usafiri hususan Usafiri wa Majini kwa njia ya Boti  kuuza tiketi kwa abiria  kwa ajili ya Safari  lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo  huwa haitumiki  na hivyo kusababisha hasara na usumbufu kwa abiria . 

Katika Majibu yake Mhe.Nditiye amesema tiketi ni moja ya mkataba kati ya abiria na mmiliki wa chombo cha usafiri hivyo abiria  anatakiwa kusoma kwanza maelekezo yaliyo kwenye tiketi na kama hatoridhika na maelekezo hayo ana ruksa ya kusitisha kukata tiketi ili kuondoa usumbufu.

Hata hivyo,Mhe.Nditiye amesema ufuatiliaji wa Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano  kupitia TASAC Umebaini kuhusu changamoto hizo na serikali inalifanyia uchunguzi.


Share:

Msemaji wa Serikali: Maono Na Mtazamo Wa Rais Magufuli Yazidi Kupaisha Makusanyo Ya Mapato Ya Madini

Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
SERIKALI imesema maono na mtazamo yakinifu wa Rais Dkt. John Magufuli katika usimamizi na ufuatiliaji wa sekta ya madini, umewezesha ongezeko maradufu la makusanyo ya mapato ya sekta hiyo kutoka Tsh Bilioni 210 mwaka 2015/16 hadi kufikia Tsh Bilioni 302 kwa mwaka 2018/19 na kuifanya Tanzania kuzidi kujijenga Kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari leo Alhamisi (Mei 30, 2019) Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, alisema Serikali ya Awamu ya Tano inafanya kazi kisayansi na itahakikisha rasilimali za nchi zinaendelea kulindwa ili ziweze kuleta manufaa kwa Watanzania wote.

Dkt. Abbasi alisema mara baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani Novemba 2015, ilifanya mageuzi mbalmbali katika usimamizi na ufuatiliaji wa rasilimali za madini, kwani huko nyuma Serikali ilikuwa ikipoteza kiasi kikubwa cha fedha na kuamua kuchukua hatua stahiki ikiwemo kufanya mabadiliko katika Sheria ya Madini ya mwaka 2010.

“Tulipofanya marekebisho katika sheria yetu ya madini mwaka 2017, matokeo tumeanza kuyaona kwani tumedhibiti mianya yote ya upotevu wa mapato yetu na kuanza kusimamia kwa umakini mkubwa utoroshaji mkubwa wa madini ambapo ilisababisha Serikali kupoteza kiasi kikubwa cha mapato” alisema Dkt. Abbasi.

Akitolea mfano Dkt. Abbasi alisema kufuatia agizo la Rais Dkt. John Magufuli la kuanzishwa kwa masoko ya madini ambayo ni utekelezaji wa sheria ya madini ya mwaka 2017, hadi sasa kuna jumla ya masoko 24 ambayo yamekuwa yakithibiti ubora, thamani na takwimu za madini nchini, ambapo soko la kwanza lilianzishwa Mkoani Geita, mwezi Machi mwaka huu.

Aidha Dkt. Abbasi alisema Takwimu za jumla za uzalishaji wa dhahabu katika kipindi cha miezi miwili , mkoani Geita kuanzia mwezi Machi hadi Mei, mwaka huu zinaonyesha kuwa uzalishaji umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufikia kilo 312.65 za dhahabu ukilinganisha na uzalishaji wa dhahabu  kilo 259.12 zilizokuwa zikizalishwa kabla ya masoko hayo.

“Mwezi April, pekee uliweka rekodi ya Geita kwa kuzalisha kilo 200 ambazo hazijapata kufikiwa mkoani humo kwa wachimbaji wadogo na wa kati na kwa Takwimu za Mei mwezi mwaka huu zinazidi kuthibitisha kuwa Watanzania wanapaswa kuendelea kumuombea na kumuunga mkono Rais Magufuli” alisema Dkt Abbasi.

Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema eneo lingine la mageuzi yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika sekta ya madini ni pamoja na maamuzi iliyochukua ya kujenga ukuta kuzunguka eneo la wachimbaji wa Madini ya Tanzanite Mkoani Manyara ambao Serikali iliweka mifumo ya masoko na ukaguzi, na hivyo kuchangia ongezeko la mapato ya wachimbaji wadogo na Serikali kwa ujumla.

Akifafanua zaidi Dkt. Abbasi alisema uzalishaji wa madini ya Tanzanite kutoka kwa wachimbaji wadogo ulioripotiwa kwa mwaka 2016 ulikuwa kilo 164.6 na kilo 147 kwa mwaka 2017, ambapo Serikali iliweka kukusanya kiasi cha Tsh Milioni 71 (2016) na Tsh Milioni 166 (2017), lakini uzalishaji huo uliongezeka maradufu mara baada ya Serikali kujenga ukuta huo.

“Uzalishaji uliongeza sana mara baada ya ujenzi wa ukuta kwani Kilo 781.2 zilizalishwa mwaka 2018 na kuiingizia Serikali mapato ya Tsh Bilioni 1.43 na uzalishaji kwa mwaka 2019 katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Mei ulikuwa kilo 1086.05 zenye thamani ya Tsh Bilioni 1.422” alisema Dkt. Abbasi.

Aliongeza kuwa mabadiliko hayo yameanza kuleta faida kwa nchi ambapo kwa sasa nchi nyingi za Afrika zimeanza kuiga mageuzi yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ikiwemo kupitia upya mikataba na wawekezaji na pia watafiti mbalimbali wanairejea Tanzania inayogeuza “laana” ya madini kuwa “Baraka” ya Madini.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger