Thursday 3 January 2019

AMUACHA MUMEWE KITANDANI KISHA KUTOKA NJE NA KUJIUA KWA MTANDIO



Mkazi wa mtaa wa Nakayaya wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, Awetu Makunula (44) amejinyonga hadi kufa kwa kutumia mtandio jirani na nyumbani kwa wazazi wake.

Mume wa marehemu Awetu, Salum Namtikwe, amesema usiku walilala wote na kabla ya tukio hilo mkewe aliamka saa 11 alfajiri na kumuaga kuwa anatoka nje kwa ajili ya kufagia nje ya nyumba yao.

Amesema baada ya kupewa maelezo hayo yeye aliendelea kulala lakini baadaye alishangaa kupata taarifa za mkewe kukutwa akiwa amejinyonga hadi kufa kwa kujining’iniza katika mti uliopo jirani na nyumbani kwa wazazi wake.

“Baada ya kupatiwa taarifa hizo niliamka na kwenda eneo la tukio na kumtambua marehemu mke wangu, baadaye tulitoa taarifa kwa viongozi wa serikali kwa ajili ya taratibu za kuuondoa mwili huo katika eneo hilo,” amesema mume wa marehemu.

Akisimulia maisha ya mkewe, Namtikwe amefunguka kuwa hajawahi kugombana naye lakini alikuwa mgonjwa wa homa za mara kwa mara licha ya kwamba siku aliyojinyonga hakulalamika kuumwa.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, ASCP Gemin Mushy amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema polisi inaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo chake.

Chanzo- Eatv
Share:

AKAMATWA AKISAFIRISHA WAHAMIAJI HARAMU KWA GARI LA LAKE OIL

Dereva wa lori la mafuta mali ya Kampuni ya Lake Oil, Christopher Kikwete (42) mkazi wa Kibamba Jijini Dar es Salaam anashikiliwa na polisi mkoani Songwe kwa tuhuma za kusafirisha wahamiaji haramu 10 raia wa Ethiopia kinyume cha sheria.

Kamanda wa Polisi mkoani huo, Mathias Nyange amesema hayo jana Jumatano Januari 02, 2019 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Amesema dereva huyo alikamatwa Desemba 31, 2018 katika stendi ya mabasi ya Makaburini mjini Vwawa wilayani Mbozi saa 4 asubuhi wakati polisi kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji wakiwa katika doria walilisimamisha lori hilo na kukuta limejaza wahamiaji hao katika kitanda kilichopo nyuma ya kiti cha dereva.

Kamanda huyo amesema lori hilo lenye namba T 500 DFJ na tera lenye namba T 833 CMN aina ya Scania ni tanki lililokuwa limebeba mafuta ya petroli kutoka Dar es Salaam kwenda nchini Zambia nalo linashikiliwa na jeshi hilo.
Share:

MAWAKILI WA 'MPEMBA WA MAGUFULI' WAIANGUKIA MAHAKAMA

Upande wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Yusuf Ali maarufu kama ‘Mpemba wa Magufuli' na wenzake, umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Da es Salaam kuchoshwa na maelezo ya upande wa mashtaka kuwa jalada la kesi hiyo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).


Wakili wa utetezi, Hassan Kiangio, ameieleza mahakama hiyo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Wanjah Hamza, baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa jalada la kesi hiyo lipo kwa DPP kwa ajili ya kutolewa maamuzi.


Yusuf na wenzake watano, wanakabiliwa na mashtaka manne, likiwamo la kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo yenye thamani ya Sh. milioni 785.6.


Washtakiwa hao wamekaa rumande kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokukamilika.


Washtakiwa hao walifikishwa Kisutu kwa mara ya kwanza, Novemba 17, 2016 kujibu mashtaka yanayowakabili.


“Kesi hii ni ya muda mrefu, wateja wangu wanaendelea kusota rumande bila kujua hatima yao, tumechoshwa na hizi kauli za upande wa mashtaka kuwa jalada lipo kwa DPP linafanyiwa kazi, tunataka wenzetu wa upande wa mashtaka watuambie wamefikia wapi juu ya upelelezi wa kesi hii,” Kiangio aliiambia mahakama hiyo.


Akitolea ufafanuzi wa hoja hizo, Wakili wa Serikali, Elia Athanas, alidai kuwa kesi hiyo iliitishwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba jalada halisi la kesi hiyo lipo kwa DPP, hivyo wanasubiri uamuzi wake.


Novemba 15, mwaka jana, Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, aliieleza mahakama kuwa wapo katika hatua za mwisho za uandaaji wa nyaraka ili kuipeleka kesi hiyo katika hatua nyingine.


Hakimu Mkazi, Hamza baada ya kusikiliza hoja za pande zote, aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 15, 2019 itakapotajwa na kusema kuwa hoja za upande wa utetezi zitafanyiwa kazi na Hakimu anayesikiliza shauri hilo, Thomas Simba, atakaporejea kutoka likizo.
Share:

SHEPU YA HAMISA MOBETTO YAWA GUMZO MTAANI

SHEPU YA HAMISA MOBETO GUMZO MTAANI Mwaka 2018 ulikuwa ni mwaka ambao kulikuwa na mgawanyiko mkubwa katika mafanikio ya kimaisha ambapo watu wengi walionekana kutoufurahia kwa malalamiko ya vyuma kukaza wakimaanisha ugumu wa maisha kupitiliza tofauti na miaka mingine Kwa upande wa mastaa wa kiwanda cha Burudani hapa Tanzania kuna waliofanikiwa na kuna waliofeli katika mahangaiko yao.Ukiachilia mbali waliofeli kabisa Hamisa Mobeto ni miungoni mwa wasanii ambao walipitia vipindi vyote(kipindi kigumu na kipindi cha mafanikio) Kwa upande wa matukio yaliyomuumiza na kumvunja moyo bila shaka itakuwa ni kupoteza penzi lake…

Source

Share:

MHE. MABULA ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA TENK NNE ZA MAJI ZENYE UWEZO WA KUHIFADHI LITA 3,300,000 NYAMAGANA.

  Haya yanebainishwa na Mbunge Jimbo la Nyamagana Mhe. Stanslaus Mabula katika ziara yake MWAUWASA Mwanza Urbun Water Supply Supply and Sanitation Authority, Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Jijini Mwanza katika ukaguzi wa ujenzi wa tank nne za kuhifadhia maji zenye uwezo wa kuhifadhi Lita 3,300,000 zitakazo hudumia wakazi takribani 105,649. Mhe. Mabula amesema ukamilishwaji wa ujenzi tank hizi zilizopo Kata tatu za Halmashauri ya Jiji la Mwanza ikiwemo Kata ya Isamiro lilipo tank la Mji la Mwema lenye uwezo wa kubeba maji Lita 1,200,000, tank la maji…

Source

Share:

WANAWAKE TUMUOGOPE MUNGU,KUZAA MTOTO NA KUMTELEKEZA NI KUHATARISHA MAISHA YAKE.

  NGARA. Na Mwandishi wetu, Wanawake wameshauriwa kumuogopa mungu na sheria za nchi kwa kuepuka vitendo vya ukatili dhidi ya watoto baada ya kuwapata kwa kuwazaa kisha kuwaua au kuwatelekeza wakiwaacha mazingira hatarishi. Ushauri huo umetolewa na mmoja wa wafanyakazi wa benki ya NMB tawi la Ngara mkoani Kagera Witness Mwanga baada ya kuungana na wenzake kutembelea watoto yatima wa kituo ANGEL’S HOME kilichopo Kanisa katoliki la Rulenge wilayani Ngara. Witness Mwanga amesema kuzaa mtoto ni baraka hivyo mtoto anahitaji malezi, matunzo na kupewa haki zake za msingi kuliko kutupa…

Source

Share:

TUNDU LISSU AMALIZA MATIBABU...KUACHIA WARAKA MZITO


Tundu Lissu amehitimisha matibabu yaliyomchukua siku 480 baada ya kuondolewa vyuma vilivyokuwa katika mguu wake wa kulia ambavyo aliwekewa Julai 9, mwaka jana ili kuunganisha mifupa.

Baada ya kuhitimisha matibabu hayo yaliyotokana na majeraha aliyopata baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana mwaka juzi, mbunge huyo wa Singida Mashariki, amesema anatarajia kutoa waraka alioeleza umebeba ujumbe mzito juu ya masuala mbalimbali likiwamo tukio hilo na hali ya kisiasa nchini.

Akizungumza na Mwananchi jana, Lissu alisema alifanyiwa upasuaji wa mwisho wa kuondoa vyuma hivyo Jumatatu iliyopita mchana.

“(Upasuaji) ulichukua kama saa moja na nusu. Niliingia chumba cha upasuaji saa 6:30 mchana na nikatoka huko saa nane mchana.Baada ya hapo nilipelekwa chumba cha mapumziko kwa saa mbili za uangalizi halafu nikarudishwa chumbani kwangu saa 10:30 jioni.”

Lissu alishambuliwa mchana wa Septemba 7, 2017 akiwa ndani ya gari, nje ya makazi yake Area D, mjini Dodoma wakati akitoka kuhudhuria mkutano wa Bunge. Alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma kwa matibabu ya awali na siku hiyohiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi, Kenya.

Alipata matibabu katika hospitali hiyo hadi Januari 6, mwaka jana alipohamishiwa Ubelgiji.

Hivyo, tangu Septemba 7, 2017 hadi Desemba 31, 2018, mwanasheria huyo mkuu wa Chadema ametibiwa kwa kipindi cha siku 480 sawa na mwaka mmoja, miezi mitatu na siku 24.

Akizungumzia hatua hiyo, mke wa Lissu, Alicia Magabe alisema, “Namshukuru sana Mungu kwa hatua hii na tunaanza kuona si muda mrefu tunarudi nyumbani ni furaha sana. Tumekuwa ugenini tangu Septemba 7 (2017) sasa tunapenda kurudi kuishi nyumbani kwa amani na kujumuika na ndugu, jamaa na marafiki.”

Pia, kaka wa Lissu, Alute Mughwai alisema familia inamshukuru Mungu na, “Tunawashukuru sana Watanzania kwa jinsi walivyokuwa na sisi katika maombezi, michango ya hali na mali hadi sasa anapofikia hatua za mwisho za matibabu yake kwa kusimama mwenyewe.

“Lakini nawashukuru zaidi Hospitali ya Dodoma, Nairobi na Ubelgiji kwa jinsi walivyomhudumia,” alisema.

Alisema kwa kutambua mchango ulioonyeshwa na Hospitali ya Dodoma, familia ya Lissu imepanga kwenda kutoa shukrani maalumu.

Alipoulizwa kama familia hiyo itafanya hivyo katika hospitali nyingine alikolazwa, Alute aliyekuwa akizungumza kwa furaha alisema, “Tunaanzia nyumbani kwanza, ujue bila Hospitali ya Dodoma, Lissu asingefika Nairobi.”

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma, Ernest Ibenzi alipokea shukrani hizo za Alute na kusema ilikuwa moja ya kazi yao kuhakikisha wanaokoa maisha ya mgonjwa.

“Timu iliyomhudumia ilitekeleza wajibu wake ipasavyo hasa ikizingatiwa hali aliyokuwa nayo, kwa hiyo tunashukuru na wakiwa tayari tunawakaribisha,” alisema Dk Ibenzi.

Alipoulizwa maoni yake kuhusu kauli ya Lissu kuhusu utayari wake wa kugombea urais mwaka 2020 iwapo vyama vya upinzani vitampitisha, Alute alisema familia haina tatizo na kwamba jambo la msingi kwao ni kuona ndugu yao anapona na anarejea nchini salama.

Aidha, Alicia ambaye kitaaluma ni mwanasheria alizungumzia nia ya mumewe kugombea urais alisema suala hilo ni litategemea mchakato ndani ya taasisi na ikiwa atapitishwa litakuwa jambo la heshima.

“Ni heshima na sifa na mimi nitamuunga mkono nikiwa mke wake, ubavu wake, msaidizi wake wa karibu sana kwa ngazi ya familia, mimi ni nani hadi nisimuunge mkono ikiwa taasisi zitamwamini? Nitamuunga mkono bega kwa bega,” alisema.

Desemba 26, mwaka jana, Lissu akizungumza na Mwananchi kuhusu ndoto zake za kuwania urais iwapo atapitishwa na vyama vya upinzani alisema, “Wakikaa katika vikao na kunipa bendera, nitakubali kubeba msalaba huo mzito kwa mikono miwili.”

Via Mwananchi

Share:

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI JAN,3 2019, OZIL KUBAKI ARSENAL


Christian Eriksen anagoma kutia saini mkataba mpya Tottenham, huku mkataba wa sasa wa kiungo huyo wa kati wa Denmark mwenye miaka 26 ukitarajiwa kufikia kikomo baada ya miezi 18. (Evening Standard)

Juventus wamethibitisha kwamba wameonyesha nia ya kumtaka kiungo wa kati wa Arsenal Aaron Ramsey, 28, bila kulipa ada yoyote baada ya mkataba wake kumalizika mwisho wa msimu. (Sky Sports) 

Wolves wamewasilisha ofa ya £18m kumtaka mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham, 21, ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo katika klabu ya Aston Villa inayocheza ligi ya Championship. (Sun)

Tammy Abraham
Mesut Ozil, 30, amesisitiza kwamba mustakabali wake bado upo Arsenal licha ya kutafutwa na Real Madrid na Inter Milan. (Goal) 

Watford hawataki kumuuzaAbdoulaye Doucoure, 26, ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa £50m kwa Paris St-Germain wakati wa dirisha la uhamisho wa wachezaji la Januari. (Evening Standard)

Bayern Munich wameimarisha ofa yao hadi £30m wakitaka kumnunua winga wa Chelsea Callum Hudson-Odoi, 18, baada ya ofa yao ya awali ya £20m kukataliwa. (Sun)

Callum Hudson-Odoi alijiunga na Chelsea mwaka 2007

Everton wanamtaka winga wa Barcelona Malcom, ambaye amekuwa hachezeshwi sana kikosi cha kwanza tangu ajiunge na Barca kutoka Bordeaux mwanzoni mwa msimu. (Marca)

Lakini Toffees wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa klabu ya Guangzhou Evergrande inayocheza Ligi Kuu ya Uchina, ambao wametoa ofay a euro 50m (£45m) kumtaka Mbrazil huyo. (Goal) 

Bournemouth watamruhusu mshambuliaji wa England Jermain Defoe kuondoka klabu hiyo Januari. Mchezaji huyo wa miaka 36 amechezeshwa mara nne pekee kama nguvu mpya ligini msimu huu. (Sky Sports)

Chelsea wanapanga kuendelea kuimarisha kikosi chao mwezi huu hata baada ya kumnunua Christian Pulisic. The Blues bado wanamtaka mshambuliaji wa Bournemouth Callum Wilson, 26, na pia wanamtafuta beki mpya. (Mirror)

Liverpool wanapanga kumpa mshambuliaji wa wao Daniel Sturridge, 29, mkataba mpya. (Mail)

Arsenal wamewasilisha ofay a euro 16m (£14m) kumtaka kipa wa Real Madrid kutoka Costa Rica Keylor Navas, 32. (Sport)

Kipa wa Costa Rica Keylor Navas

Newcastle wanatarajiwa kuwasilisha ofa kumtaka beki wa AC Milan kutoka Uruguay Diego Laxalt, 25, ambaye hucheza kama beki wa kushoto mwezi huu. (Calciomercato)


Manchester City hawatatafuta mchezaji wa kujaza pengo lililoachwa na kiungo wao wa kati mkabaji Fernandinho, 33, wakati wa dirisha la kuhama wachezaji Januari. (ESPN) 

Burnley na Cardiff wanang'ang'ania kupata saini ya kiungo wa kati wa Scotland Matt Phillips, 27, kutoka klabu ya West Brom inayocheza ligi ya Championship. (Mirror)

Meneja wa Monaco Thierry Henry anamtaka beki wa kati anayechezea Crystal Palace Mamadou Sakho, 28, pamoja na kiungo wa kati wa Chelsea Cesc Fabregas, 31, mwezi huu. (Independent)

Cesc Fabregas

Kiungo wa kati wa Leicester City Vicente Iborra, 30, anasema huenda akaihama klabu hiyo na kujiunga na Villarreal mwezi Januari. (RNE, via Leicester Mercury)

Mshambuliaji wa Italia Manolo Gabbiadini, 27, anataka kuihama Southampton mwezi huu, na tayari AC Milan wanamtaka. (Calciomercato)

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez hataki kumwacha winga Jacob Murphy, 23, aondoke kwa mkopo hadi klabu hiyo itakapokuwa imepiga hatua katika kuwanunua wachezaji wengine Januari. (Chronicle)


Liverpool waliamua hawamtaki tena Christian Pulisic aliyenunuliwa na Chelsea kutoka Borussia Dortmund baada yao kumnunua Xherdan Shaqiri, 27, kutoka Stoke mwanzoni mwa msimu. (Liverpool Echo) 

Diego Godin na Atletico Madrid wanazozana kuhusu mkataba mpya na raia huyo wa Uruguay mwenye miaka 32 ambaye ni mkabaji wa kati huenda akaihama klabu hiyo mkataba wake wa sasa utakapomalizika mwisho wa msimu. (Marca)

Diego Godin

Real Madrid wanamtaka kiungo mshambuliaji wa Sevilla Pablo Sarabia, 26, ambaye amesalia na miezi 18 pekee katika mkataba wake wa sasa. (AS)
Share:

LUGOLA – ASKARI WANAOCHAFUA JESHI LA POLISI, WAKATAFUTE KAZI NYINGINE.

  Na Allawi Kaboyo – Bukoba Kagera. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Kangi Lugola, ameanza Rasmi ziara yake Mkoani Kagera ambapo amekutana na idara pamoja na taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo, na kisha kufanya Mkutano wa hadhara katika viwanja vya mayunga mjini Bukoba sambamba na kusikiliza kero za wananchi. Mhe.Lugola katika hotuba yake iliyojaa ufafanuzi wa Utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya ccm unaofanywa na Mh. Rais John Pombe Magufuli, katika Kusimamia amani ya nchi na watanzania kwa ujumla, na kuwa Mh. Rais hapendi kusikia mwananchi…

Source

Share:

Wednesday 2 January 2019

MBUNGE NA WANANCHI NGARA WATOFAUTIANA KUHUSU ARDHI WAMTAKA WAZIRI KUINGILIA KATI

Na Mwandishi wetu Mbunge wa jimbo la Ngara mkoani Kagera Alex Gashaza (CCM) amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Kazingati katika jimbo hilo chini ya vyombo vya ulinzi na usalama, baada ya kuwepo malalamiko ya kwamba anapinga wawekezaji kupata ardhi kijijini humo Mbunge huyo Gashaza amefanya mkutano huo hii leo ikiwa ni siku chache Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi ngazi ya Taifa kuagiza uongozi wa wilaya ya Ngara kuacha mara moja mipango ya kugawa ardhi kwa mwekezaji kutoka korea Kusini Wawekezaji wa nchi hiyo wanahitaji ardhi…

Source

Share:

ZANZIBAR YAJIDHATITI NA UOKOAJI DHIDI YA AJALI ZA MAJI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejidhatiti kuwaokoa wananchi wake kutokana na ajali zinazotokea baharini kwa kununua vifaa vya kisasa vinavyokwenda na wakati uliopo. Dk. Shein alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kujiimarisha kwa kukipa vifaa vya kisasa vya uzamiaji na uokozi kikosi cha KMKM, ili kukabiliana na ajali zinazotokea baharini sambamba na kuimarisha usalama katika miji ya Unguja na Pemba. Dk Shein aliyasema hayo, katika uzinduzi wa Vituo vya Uokozi vya KMKM kwa…

Source

Share:

SERIKALI YAWATAKA WACHIMBAJI WADOGO KUWA WAZALENDO  KWA KULIPA KODI NA TOZO ZINAZOTAKIWA.

Hayo yamesemwa leo January 02, 2019 na Naibu Waziri wa Madini Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko alipokuwa akifungua mafunzo ya uchimbaji wenye tija kwa wachimbaji wadogo wilaya ya Bukombe mkoani Geita. Akihutubia wachimbaji hao, Mheahimiwa Biteko ameendelea kuweka wazi nia ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dr. John Pombe Magufuli ya kuhakikisha wachimbaji wadogo wanasaidiwa na kifikia uchimbaji wa kati ambapo jumla ya fedha taslimu shilingi Bilioni nane na milioni mia tano zimetengwa kwa ajili ya utafiti wa Madini wenye lengo la kuboresha uchimbaji wa wachimbaji wadogo. Fedha…

Source

Share:

MRADI WA UJENZI VYO BORA KUTOKA MWAUWASA WAZINUFAISHA SHULE,ZAHANATI NA SOKO NYAMAGANA

Wilaya ya Nyamagana ni miongoni mwa wilaya mbili Mkoani Mwanza zinazonufaika na Mradi wa usafi wa Mazingira unaotekelezwa na shirika la Maji safi na maji taka MWAUWASA Mwanza Urban water Supply and Sanitation Authority, Kwa ujenzi wa Vyoo bora na Vya Kisasa katika shule 14, Zahanati moja ya Mkolani pamoja na Soko la Igogo. Akiongea katika ziara maalum MWAUWASA Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo la Nyamagana kukagua mradi wa usafi wa mazingira shule ya Msingi Mlimani, amesikitishwa na hali chafu ya mazingira ya vyoo vipya na kuwataka watendaji wa serikali…

Source

Share:

MAAFANDE WA JKT TANZANIA WAPIGISHWA KWATA NA WAPIGA DEBE WA STAND SHINYANGA

Wapiga debe wa Stand,timu ya stand united al maarufu kwa jina la chama la wana imemaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka tanzania bara msimu wa 2018/19 kwa kuwapigisha kwata maafande wa jkt tanzania kwa kuwachapa bao 1-0 


Mchezo huo wa ligi kuu soka Tanzania bara umepigwa leo Januari 2  2019 katika uwanja wa CCM kambarage mjini Shinyanga mchezo ambao haukuwa na kasi wala mvuto wowote kwa watazamaji katika kipindi cha kwanza kutokana na wachezaji kukosa utulivu uwanjani (butua butua) kwa wachezaji kushindwa kumiliki mpira hata kuchungulia nyavu zao. 

Lakini kipindi cha pili baada ya mabadiliko ya baadhi ya wachezaji kutoka timu zote mchezo ulishika kasi na wapiga debe wakafanikiwa kuwapigisha kwata maafande wa jkt tanzani kupitia mchezaji wake moris mahela mnamo dakika ya 77 bao ambalo limedumu na kuwaibua vifua mbele wapiga debe haona kufikisha jumla ya alama 22. 

Bakari Shime ni kocha wa JKT Tanzania amesema makosa yaliyojitokeza katika nafasi ya ushambuliaji ndio yamesababisha kukosa alama tatu na kwamba watajipanga katika mzunguko wa lala salama. 

"Kimsingi wachezaji wameshindwa kutumia nafasi tulizopata,ambapo wenzetu wamepata nafasi moja na kuitumia kupata alama tatu,sisi tunaendelea kujipanga na michezo mingine ili kupata matokeo mazuri uwanjani" Alisema Shime.

Upande wapili kwa wapiga debe huku ni hoya hoya kwani chama la wana limekuwa likisuasua kupata matokeo mazuri katika dimba la kambarage kocha Athuman Bilal amesema kazi imeanza na timu ipo tayari kuleta ushindani katika mzunguko wa pili. 

Na Malaki Philipo, Malunde 1 blog.
Share:

MBOWE NA VIGOGO WENGINE 13 KUPISHANA MAHAKAMA YA KISUTU KESHO

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na vigogo wengine 13 kesho Alhamisi Januari 3, 2019 watafika katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusikiliza kesi zinazowakabili.

Miongoni mwa kesi hizo ni za kufanya mikusanyiko isivyo halali inayowakabili viongozi tisa wa Chadema.

Kati ya vigogo hao wa Chadema, Mbowe na mhazini wa Baraza la Wanawake la chama hicho (Bawacha), Esther Matiko ndio wapo gerezani tangu Novemba 23, 2018 baada ya kufutiwa dhamana na hakimu mkazi mkuu wa mahakama hiyo, Wilbard Mashauri.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya jinai namba 112 ya 2018 ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa; mbunge wa Kibamba, John Mnyika; Katibu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji na mbunge wa Bunda, Ester Bulaya.

Wengine ni naibu katibu mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu; mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari Mosi na 16, 2018.

Kesho pia itasikilizwa kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Harbinder Seth na mfanyabiashara James Rugemalira.

Kesi nyingine itakayosikilizwa ni kesi ya mauaji ya aliyekuwa mjumbe wa tume ya mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi.

Na Hadija Jumanne, Mwananchi 
Share:

NGULI WA SOKA MAKELELE : PAUL POGBA ANA DHARAU WAPINZANI


Wachezaji wakongwe mbalimbali (kwenye duala jeusi ni Claude Makélélé.

Kiungo wa zamani wa klabu ya Chelsea na timu ya taifa ya Ufaransa, Claude Makelele amesema mtindo wa ushangiliaji mabao wa kiungo wa Manchester United Paul Pogba ni kutoheshimu wapinzani wake.

Makelele ameeleza kuwa Pogba hastahili kufanya hivyo mbele ya wapinzani wake kwani sio jambo la busara kimichezo.

"Kumfunga mpinzani wako goli 4 kisha unacheza mbele yake baada ya mchezo sio jambo la hekima kwa mpinzani hata kidogo. Huko ni kudharau wapinzani wake aliowafunga", ameeleza Makelele.

Makelele amesisitiza kuwa kila mchezaji huwa anafurahi anapopata ushindi au kufunga bao lakini mambo kama hayo ayafanye kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.

Tangu kuondoka kwa Jose Mourinho na kuteuliwa kwa Ole Gunnar Solskjær Pogba amekuwa kwenye wakati mzuri akifunga mabao 4 na kusaidia matatu kwenye mechi 3 walizocheza mpaka sasa.
Share:

KESI YA JAMAL MALINZI NA WENZAKE KUSIKILIZWA SIKU TATU MFULULIZO

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kusikiliza ushahidi wa kesi ya Utakatishaji fedha inayomkabili aliyekuwa Rais wa (TFF) Jamal Malinzi na wenzake kwa siku tatu mfululizo.

Hayo yameelezwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya kesi hiyo kuitishwa leo kwa ajili ya kutajwa.

Katika kesi hiyo iliyofikia shahidi wa 10, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi January 16, 17 na 21, 2019 kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.

Baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, Malinzi na wenzake waliwatakiwa kheri ya mwaka mpya, ndugu, jamaa na rafiki waliofika katika kesi yao.

Washitakiwa wengine ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Nsiande Mwanga ambao wakikabiliwa na mashitaka 28, ikiwemo ya utakatishaji fedha ambazo ni Dola za Marekani, 375,418.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger