Sunday 30 December 2018

KAYA MASKINI WAELEZA WALIVYONUFAIKA NA FEDHA ZA TASAF, WABORESHA MAKAZI.

  Na Dinna Maningo,Tarime. Baadhi ya kaya maskini Wilayani Tarime mkoani Mara wameeleza kunufaika na fedha zitolewazo na mfuko wa maendeleo ya Jamii(TASAF) lengo likiwa kuwasaidia ili wajikwamue kimaisha katika kujiongezea kipato. Wakizungumza wakati wakipokea fedha za miezi miwili ya Novemba na Desemba katika viunga vya shule ya msingi Buhemba kata Bomani wamesema kuwa tangu waingizwe kwenye mpango wakunusuru kaya maskini wameweza kununua mifugo na fedha zingine zimewasaidia kujikimu kimaisha. Alex Muhagama miaka (73) mkazi wa mtaa wa Buhemba ambaye upokea sh.20,000 alisema kuwa kulingana na umri wake hana uwezo…

Source

Share:

BIDHAA ZENYE KILEVI KUTOZWA USHURU KIELEKTRONIKI


Bidhaa zinazostahili kutozwa ushuru wa bidhaa kama vile sigara, mvinyo, pombe kali pamoja na bia zitaanza kutumia rasmi stempu za kielektroniki Januari, 2019 katika Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Shinyanga na Mbeya ambapo mfumo wa stempu hizo umeshafungwa kwenye mitambo ya uzalishaji.
Akizungumza mara baada ya kumaliza kukagua ufungaji wa mfumo huo katika Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) na Kiwanda cha kutengeneza vinywaji vikali cha Nyati Spirit Tanzania jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kichere alisema kuwa mfumo huo mpya unaondoa mfumo wa zamani wa stempu za karatasi.

“Nimekuja kufanya ziara katika viwanda hivi ili kujiridhisha kama kweli mfumo huu wa stepu za kielektroniki umefungwa na nimejionea mwenyewe mfumo tayari umefungwa katika viwanda vyote nilivyotembelea. Hivyo, tunaachana na mfumo wa zamani wa stempu za karatasi na kwa sasa tunaendelea kufunga mfumo huu mpya wa stempu za kielektroniki kwenye mikoa mingine ambayo haitaanza katika awamu hii”, alisema Kichere.

Kichere alisema kuwa lengo la kuweka stempu za kielektroniki kwenye bidhaa hizo ni kupata idadi halisi ya uzalishaji wa bidhaa ili kutoza kodi stahiki na kuondoa dhana ya kusema kwamba TRA inawaonea wafanyabiashara wanaozalisha bidhaa hizo kwa kutoza kodi isiyoendana na uzalishaji.

“Lengo la kuweka stempu hizi za kielektroniki ni kupata kiasi halisi cha uzalishaji wa bidhaa hizi ili kila upande uridhike yaani mzalishaji alipe kodi sahihi na sisi TRA tutoze kodi stahiki bila kupingana wala kugombana na wateja wetu”, alisema Kichere.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha kutengeneza vinywaji vikali cha Nyati Spirit Tanzania Rupa Suchak amesema kuwa amefurahishwa na kitendo cha serikali kufunga mfumo huo wa stempu za kielektroniki kwa sababu serikali itaongeza mapato na wafanyabiashara wataongeza uhiari wa kulipa kodi.

“Ninaishukuru sana serikali yetu kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kuleta mfumo huu mpya ambao utaongeza mapato na kupanua wigo wa kodi lakini pia kwetu sisi wafanyabiashara tutaongeza uhiari wa kulipa kodi”, alisema Rupa.

Uwekwaji wa stempu za kielektroniki katika bidhaa nyingine kama vile juisi, maji ya chupa, bidhaa za muziki na filamu (CD\DVD\Tape) zitafuata kwa tarehe ambayo itatangazwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania hapo badae.
Share:

SERIKALI KUSAJILI WAKULIMA WOTE NCHINI

Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga (Mb) amewaagiza Wakurugenzi wa Bodi za Mazao kuanza mara moja zoezi la kuwatambua na kuwasajili wakulima wa mazao yote nchini lengo likiwa kuwatambua ili kupanga mipango sahihi yenye kuongeza tija na uzalishaji katika mazao yote.


Mhe Hasunga amesema hayo Jumamosi 29 Disemba 2018 wakati akizungumza na Wenyeviti wa Bodi za Mazao pamoja na Wakurugenzi wa Bodi hizo za Mazao Jijini Dodoma ambapo amesisitiza kuwa ili kuongeza tija na uzalishaji katika Sekta ya kilimo na kuandaa mipango madhubuti ya kuendeleza mazao yote ni vyema kuwatambua Wakulima wote nchini.

Agizo hilo limekuja baada ya takribani wiki tatu kupita tangu Waziri Hasunga alipotoa agizo kwa Bodi ya Korosho kuandaa daftali maalumu la kuwatambua wakulima wa korosho nchi nzima, ambapo moja ya taarifa ambazo zitajumuishwa katika daftali hilo ni pamoja na jina kamili la Mkulima, Mkoa, Wilaya, Kata na Tarafa anayotoka.

Mambo mengine yanayojumuishwa ni pamoja na Kitongoji, Mtaa au Jina la Kijijini anapotoka, mahali lilipo shamba pamoja na ukubwa wa shamba lake.

“Tumepata changamoto kadhaa wakati wa kuwahakiki wakulima wa korosho katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Ruvuma na kama Bodi ya Korosho ingekuwa makini kuandaa daftari la Wakulima zoezi la uhakiki lingekuwa rahisi, kwa ajili hiyo niliwaagiza Bodi ya Korosho kukamilisha zoezi hili mpaka Mwezi Machi, 2019 na Bodi za Mazao zilizobaki ukiacha Bodi ya Tumbaku ambao wao tayari walishafanya hivyo, kukamilisha Mwezi June, 2019,” amesema Mhe Hasunga.

Waziri Hasunga ameongeza kuwa mipango sahihi ya kuwaendeleza Wakulima kuanzia kwenye kilimo chenyewe hadi kufikia katika hatua ya kuvuna, kuhifadhi na kulifikia soko ni vyema kuwa na mfumo maalumu wa kanzi data (Database) ya kuwafahamu ili kushughulikia mahitaji yao kisasa na kwa haraka zaidi.

Bodi za Mazao zilizoshiriki mkutano huo ni pamoja na Bodi ya Korosho, Bodi ya Pamba, Bodi ya Mkonge, Bodi ya Pareto, Bodi ya Chai, Bodi ya Kahawa, Bodi ya Tumbaku, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko na Bodi ya Sukari.

Wakala zilizoshiriki ni pamoja na Wakala wa Taifa wa Mbolea (ASA) Wakala wa Wakulima Wadogo wa Chai (TSHTDA).

Taasisi nyingine za Wizara ya Kilimo zilizoshiriki ni pamoja na Taasisi ya Udhibiti wa Mbegu (TOSCI), Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO), Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya Ukanda wa Kitropiki (TPRI), Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (AGITF), Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA), Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI), Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Kampuni ya Taifa ya Mbolea (TFC) na Bodi ya Leseni za Maghala.

Chanzo:Eatv
Share:

Picha:RAIS MAGUFULI AMTEMBELEA MAMA YAKE MZAZI ANAYETIBIWA JIJIN DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Wasaidizi wake wakimuombea Mama yake Mzazi Bibi. Suzana Magufuli anayepatiwa Matibabu Jijini Dar es Salaam Desemba 30, 2018. Bibi Suzana Magufuli anasumbuliwa na ugonjwa wa Kiharusi ambapo amekuwa akipatiwa matibabu kwa takribani miezi mitatu sasa.




Picha na Ikulu
Share:

POLISI WAUA MAGAIDI 40 WALIOPANGA KULIPUA MAKANISA


Jeshi la polisi nchini Misri limesema kuwa limeua wapiganaji 40 wa makundi ya kigaidi waliokuwa wanapanga mashambulizi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani, polisi waliwavamia magaidi hao katika maficho yao yaliyokuwa Giza na Sinai Kaskazini, jana alfajiri.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa magaidi hao walikuwa wamepanga kushambulia makanisa, askari pamoja na maeneo yenye watalii wengi.

Juzi, wapiganaji wa makundi ya kigaidi walitekeleza shambulizi la bomu katika eneo la Giza kwenye basi la watalii. Hakuna kundi lolote lililojitokeza kudai kutekeleza tukio hilo ambalo lilisababisha vifo vya watalii kutoka Vietnam pamoja na waongozaji wa watalii hao

Imeelezwa kuwa polisi waliwaua watu 30 katika mashambulizi mawili ya kushtukiza kwenye eneo la Giza, na wengine 10 waliuawa katika eneo la El-Arish ambao ni makao makuu ya jimbo la Sinai Kaskazin

“Makundi ya magaidi yalikuwa yanapanga kutekeleza mashambulizi katika maeneo ya makanisa na sehemu ambazo wakristo walikuwa wanaabudia. Pia, walipanga kulenga maeneo ya utalii pamoja maeneo mengine ya kiuchumi,” imeeleza taarifa ya Wizara.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, polisi wamekamata vifaa vya kutengenezea mabomu pamoja na idadi kubwa ya silaha.
Share:

TAKUKURU KUINGILIA KATI SAKATA LA RUSHWA YA NGONO VYUO VIKUU

Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) imeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuongeza jitihada zaidi za kuwajengea uwezo 
wanafunzi na wahadhiri juu ya masuala ya rushwa hasa ya ngono kwa lengo la kupunguza au kumaliza kabisa tatizo hilo vyuoni.

TSNP umesema kuwa rushwa ya ngono kwa sasa imeshamiri katika vyuo mbalimbali nchini hivyo inapaswa kukemea kwani inaharibu maisha ya wanafunzi ambao wanategemewa kuwa viongozi wa baadae.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Katibu wa TSNP, Joseph Marekela alisema rushwa ya ngono vyuoni ni changamoto kubwa hasa kwa wanafunzi wa kike hivyo jitihada za makusudi zinahitajika ili kuhakikisha kuwa 
hakuna mtu anayepoteza haki yake ya msingi kwa kukataa kutoa rushwa hiyo ambayo si tu inapoteza utu wa mtu bali ni kinyume na haki za binadamu.

Alisema mfumo wa upimaji uwezo uliyopo sasa umempa mamlaka makubwa mhadhiri ya kuamua hatma ya mwanafunzi kitaaluma jambo ambalo lina
sababisha uwepo wa mianya ya rushwa ya ngono kwa wahadhiri wasio na maadili ambao wanatumia nafasi yao kuminya haki ya mwanafunzi.

“Kwakuwa tatizo hili ni kubwa na limeathiri wanafunzi wengi chuoni tunatoa wito kwa Takukuru waongoze jitihada zaidi kwa kuwajengea uwezo taasisi za 
Takukuru vyuoni ili kupambana na tatizo hili kikamilifu, pia vituo vya jinsia na Serikali za wanafunzi ziwajibike ipasavyo ili kuhakikisha kuwa hakuna anaepoteza haki yake ya msingi kwa kukataa kutoa rushwa hiyo ya ngono,” alisema.

Hata hivyo mtandao huo umesema kuwa ukosefu wa taulo za kujisitiri wanafunzi wa kike hasa wa vijijini kipindi cha hedhi inaathiri maendeleo ya wanafunzi 
hao kitaaluma.

Kutokana na hali hiyo, Marekela alisema wanatoa wito kwa Serikali kupitiaWizara yenye dhamana kulitazama upya suala kwa kugawa bure taulo hizo kwa 
wanafunzi wa kike hasa waliopo maeneo ya vijijini ili kunusuru ndoto zao walizojiwekea.

Aidha alisema suala la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu bado ni changamoto kwani wengi wao wameshindwa kuendelea na masomo kwa kukosa mikopo hiyo
Share:

CHADEMA WAZUIWA KUFANYA MKUTANO JIMBONI KWA MBOWE

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimezuiwa kufanya mkutano pamoja na ziara ya viongozi wa chama hicho kitaifa, wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.

Hayo yamebainishwa kupitia barua iliyotumwa kwa Katibu wa CHADEMA wilayani Hai, ambayo imesainiwa na Katibu tawala wa wilaya hiyo, Said Omary iliyoelekeza kusitisha kibali cha kufanya mkutano wilayani humo.

"Nimeagizwa na Mkuu wa Wilaya ambae ni mwenyekiti wa kamati ya usalama ya Hai. Nikuandikie kukutaka kusitisha mkutano na ziara ya viongozi wako kitaifa, tarehe 29/12/2018 na kuendelea", imesema barua hiyo.

Baada ya zuio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amethibitisha kukamatwa kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji pamoja na viongozi wengine watatu kwa makosa ya kufanya kusanyiko bila kibali.

Share:

Good News : Pakua Upya App ya Malunde 1 blog ...Imeboreshwa Kukupa Raha zaidi ...Bonyeza HAPA SASA

Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog

NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Share:

DC MBONEKO AWAONYA POLISI WANAOTUMIWA NA VIONGOZI KUONEA WANANCHI,CHUKI ZA DIWANI ZATAJWA

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Jasinta Mboneko amewaonya baadhi ya askari wa Kituo cha Polisi Kata ya Salawe kutumiwa na viongozi kwenda kuvuruga amani kwa wananchi, kinyume cha maadili ya kazi yao inayowataka kulinda usalama wa raia na mali zao.


Inadaiwa diwani wa kata hiyo, Joseph Buyugu anawatumia baadhi ya askari kuonea wananchi hasa wanaofichua maovu kwenye mikutano ya hadhara ya viongozi wakuu kwa kuwapiga na kisha kuwatia mbaroni.

DC Mboneko ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama alitoa onyo hilo juzi wakati alipofanya mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua kwenye kata hiyo, ambapo hivi karibuni kulitaka kutokea machafuko ya amani kwenye eneo hilo.

 Alisema amesikitishwa na viongozi wa maeneo hayo kulitumia Jeshi la Polisi vibaya kutaka kuvuruga amani ya nchi na kujichukulia mamlaka ambayo yapo nje ya utawala wao kwa kuwapiga wale ambao wamekuwa wakifichukua maovu yao pamoja na kuwavunjia nyumba wananchi na kuharibu mali zao.

“Jeshi la Polisi nawaonya msitumiwe na viongozi kuvuruga amani ya nchi ninyi kazi yenu ni kudumisha amani na kulinda usalama wa raia na mali zao na si vinginevyo, acheni kutumika kuonea wananchi pamoja na kuwaomba rushwa, kama mnaona mishahara yenu haitoshi acheni kazi,” alisema Mboneko. 

“Na nyie viongozi msiwe chanzo cha machafuko ya kuvuruga amani kwa wananchi, kazi yenu ni kuwatumikia na kutatua kero zao pamoja na kuwa hamasisha kwenye masuala ya maendeleo, na siyo kugeuka miungu watu na kuanza kuwaonea huku mkiwapiga, kuwavunjia nyumba zao, na kisha kuwasweka rumande,” aliongeza.

Awali baadhi ya wananchi wa kata hiyo ya Salawe wakiwakilisha kero zao kwa mkuu huyo wa wilaya akiwamo Seke Nyeke na Dumila Hamis, alisema malalamiko yao mengi yalikuwa ni viongozi wa maeneo hayo akiwamo na diwani wamekuwa wakishirikiana na askari Polisi kuwaonea na ili kutoka rumande, lazima watoe kitu kidogo.

Kwa upande wake, diwani Buyugu alikana tuhuma hizo za kulitumia Jeshi la Polisi kuvuruga amani huku Kamanda wa Polisi Wilaya ya Shinyanga, Claud Kanyolota akiwaonya askari hao kutorudia tabia hiyo na kubainisha malalamiko hayo atayafanyia kazi ili wachukuliwe hatua za kinidhamu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Ngassa Mboje alisikitishwa na kitendo cha diwani wa Salawe aliyechaguliwa na wananchi na matokeo yake kuwakandamiza huku tatizo hilo limeonekana analifanya kwa wale ambao ana chuki nao, jambo ambalo halifai na ni hatari alimuomba aache tabia hiyo ili wananchi waishi kwa amani.



Share:

Serikali Yakaribisha Wafanyabishara Wanaotaka Kubangua Korosho

SERIKALI  kupitia kwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda imewakaribisha wafanyabiashara kununua korosho na kuzibangua.
 
Mbali na uamuzi huo, Waziri Kakunda amesema Serikali  bado inaendelea kuingia mikataba na wabanguaji ili kupunguza mzigo wa korosho.

Kakunda ametoa kauli hiyo wakati taarifa ya timu ya pamoja ya wataalamu kuhusu hali ya utekelezaji wa operesheni korosho iliyotolewa Novemba 27 ikionyesha kuwa itachukua muda mrefu  kubangua korosho za msimu huu.
 
Novemba 12, Rais John Magufuli alitangaza Serikali kununua korosho yote kutoka kwa wakulima msimu huu kwa bei ya Sh3,300 kwa kilo.
 
Licha ya Waziri Kakunda kusema haina shida kwa ubanguaji kuchukua muda mrefu, amewataka wafanyabiashara wanaoweza kubangua wenyewe wakae meza moja na Serikali ili wauziwe korosho.
 
“Kama mtu anatokea popote iwe ndani au nje akasema mimi nataka ninunue korosho nikabangue mwenyewe, labda ana bei nzuri aje tuzungumze. Ije mvua, lije jua korosho ziko kwenye maghala, kuna tatizo hapo? Zitabanguliwa tu muda wowote,” alisema.
 
Alisema ubanguaji unaendelea baada ya Serikali kuingia mkataba na baadhi ya kampuni.
 
“Leo (juzi) ilikuwa niende kuzindua ubanguaji wa kule Mtwara, kwa hiyo siyo tumekaa tunasubiri wateja, tunaendelea kubangua.
 
“Sido (Shirika la Viwanda Vidogo) ambao ni wabanguaji wadogo, wameshabangua tani sita. Bado kuna viwanda tulikuwa tunaingia navyo mkataba, hadi jana (juzi) tumeingia mikataba minne na bado tutaingia mingine zaidi ya 12,” alisema.
 
Inaelezwa kuwa kuna jumla ya viwanda 23 vya kubangua korosho na ambavyo uwezo wake uliosimikwa sasa ni kubangua jumla ya tani 42,200. Hata hivyo, uwezo wa mashine kwa kiwanda kimoja ni tani 11,142 kwa mwaka sawa na asilimia 26 tu ya uwezo uliosimikwa wa viwanda hivyo.
 
Taarifa hiyo ya timu ya pamoja ya wataalamu inaonyesha matarajio ya uvunaji wa korosho kwa msimu wa mwaka 2018/19 kufikia jumla ya tani 275,191 na kama viwanda vinane vinavyofanyakazi vingebangua korosho kwa kiwango kinachotakiwa cha tani 127,200 kwa mwaka, kazi hiyo itafanyika kwa miaka miwili.
 


from MPEKUZI http://bit.ly/2LHBEZl
Share:

Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally Atoa Maagizo MAZITO Kwa Naibu Waziri wa Kilimo

Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amemwagiza Naibu Waziri wa Kilimo, Innocent Bashungwa kutafuta fedha za kuwalipa wakulima wa zao la kahawa mkoani Kagera kwa bei inayoridhisha kulingana na gharama watumiazo katika uzalishaji.
 
Dk Bashiru alitoa agizo hilo juzi mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa huo wanaotoka wilaya za Ngara Kyerwa na Karagwe alipokutana nao mjini hapa.
 
Katibu mkuu huyo wa CCM alitoa agizo kwa Bashungwa ambaye ni Mbunge wa Karagwe (CCM) aliyekuwapo kwenye
kikao hicho kwenda kuhakikisha bei inaboreshwa ili kuwavutia wakulima wa zao hilo.
 
Alisema licha ya Serikali kuzuia magendo ya kahawa kutoka Kagera kuingia Uganda lakini inanunuliwa kwa kificho kisha inasafirishwa na kuwekwa katika kasha au kopo la robo kilo hadi nje ya nchi ikiwa na thamani kubwa hasa China.
 
“Waganda wananunua kahawa kwa magendo wanaikaanga na kuifunga kwa kuweka picha ya mwanamke mrembo wa Kiganda, wanaisafirisha hadi China kupitia bandari yetu inauzwa kakopo Sh40,000 iweje mkulima apatiwe Sh1,000?” alihoji Dk Bashiru.
 
Pia alimuagiza Mkurugenzi Halmashauri ya Ngara, Aidan Bahama kutowanyang’anya wananchi ardhi kwa madai ya kuwagawia wawekezaji kutoka Korea Kusini.
 
“Nilikupigia simu kukuzuia sasa nakupa ‘live’ sitaki kusikia wawekezaji wa nje wanapewa ardhi bila kufuata utaratibu wa kuridhiwa kwanza na mkutano mkuu wa vijiji,” alisema.
 
Mkuu Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali, Marco Gaguti alisema katika kupambana na biashara ya magendo ya kahawa wilaya ya Misenyi imekamata magari 12 yenye tani zaidi ya 60 na pikipiki zilizokuwa zikisafirisha Uganda.


from MPEKUZI http://bit.ly/2Qc1023
Share:

Lugola Atoa ONYO Kwa Wanaotumia Misikiti na Makanisa Kuvuruga Amani ya Nchi

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema Serikali haitawavumilia wanaotumia taasisi za dini ikiwamo misikiti na makanisa kuvuruga amani.
 
Alisema hayo juzi kwa niaba ya Rais John Magufuli wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kamati ya Amani ikiwa ni kusheherekea Sikukuu ya Krismasi.
 
Waziri huyo alisema bado kuna viashiria vya mtu mmoja mmoja na vikundi vya watu wanaotaka kuvuruga amani, vitendo ambavyo Serikali haitavivumilia.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salum alisema ni mara ya kwanza kwa Waislamu kualikwa na kukaa pamoja katika kusheherekea Sikukuu ya Krismasi.
 
“Pamoja na kuwapo kwa mahusiano mazuri kati ya Wakristo na Waislamu nchini bado kumekuwa na shida kwa baadhi ya watu pale tunapokaa pamoja katika sikukuu hizi na kushindwa kutofautisha kusherehekea na kutambua,” alisema.
 
Naye Askofu wa Kanisa la Ufufuo, Paul Bendera alisema siku zote amani inatoka kwenye moyo wa mtu. 

“Haiwezekani tunakakaa pamoja akatokea mtu akatugawa, ili kuendeleza amani iliyopo tunapaswa kuthamini viongozi wetu na kutii mamlaka zao.”


from MPEKUZI http://bit.ly/2SxGtat
Share:

Saturday 29 December 2018

KIJANA INITIATIVE KUWAINUA WAJASIRIAMALI NA WASIOJIWEZA MOROGORO

Taasisi ya Kijana Initiative Foundation imeungana na familia mia moja (100) zinazoishi katika mazingira magumu wakiwemo wajane pamoja na wanawake wajasiriamali wadogo,ili kubadilishana mawazo na kula chakula cha pamoja katika ukumbi wa Chuo Kikuu Cha Jordan mkoani Morogoro. Hafla hiyo imefanyika Leo 29 Desemba 2018 na kujumuisha Viongozi mbalimbali akiwemo Ndg Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro ambaye alikuwa mgeni rasmi, pamoja na Ndg Said Said Nguya mdau wa maendeleo na wanawake wajasiriamali pamoja na familia zinazoishi katika mazingira magumu ambazo zimeonesha furaha ya wazi kwa msaada…

Source

Share:

TAMASHA KUBWA LA MKESHA WA MWAKA MPYA KUFANYIKA UWANJA WA TAIFA,KIINGILIO BURE


Tamasha kubwa la mkesha wa kufunga 2018 na kufungua mwaka 2019 linatarajiwa kufanyika Desema 31 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mkesha huo utakaokuwa wa aina yake unatarajia kumdondosha Mwanamuziki wa nyimbo za injili kutoka nchini Nigeria anaejulikana kwa jina la Chris Shalom, anayetamba na wimbo wake maarufu uitwao 'my beautifier' na nyingine nyingi.

Pamoja Na Chris Shalom pia waimbaji wengine mbalimbali mahiri kutoka hapa nchini akiwemo Jesica Honore, Goodluck Gosbert, Joel Lwaga Na John Lisu wanatarajiwa kutumbuiza katika mkesha huo.

Mkesha wa mwaka 2019 umeandaliwa na Nabii (prophet) Clear Malisa wa Passion Java ministry, kutoka ubungo kibangu jijini Dar es Salaam.Waigizaji/wachekeshaji na watu maarufu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania wanatarajiwa pia kuwepo akiwemo Pastor Kuria kutoka show ya churchchill nchini Kenya.

Katika tamasha hilo hakuna kiingilio na usafiri utatolewa kwa watu wote katika vituo vyote vikubwa vya usafiri Dar es Salaam.Mkesha wa mwaka 2019, umedhaminiwa Na Clouds media group, Elishadai shopping center Na Fair Travel adventures.


Share:

SIMBA WAILAZA SINGIDA UNITED 3 -0 , KICHUYA BALAA MTUPU

Kiungo mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya ameamua kumtumia salamu kocha Mkuu, Patrick Ausems baada ya kuonyesha ufundi wa kucheka na nyavu leo katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara uliochezwa uwanja wa Taifa kutokana na kuanzia benchi mara nyingi.

Kichuya aliwanyanyua mashabiki kwa kutoa pasi ya bao la kwanza dakika ya 17 lililofungwa na John Bocco ambaye kwa sasa anafikisha bao la tatu kwenye Ligi.

Dakika ya 49 Kichuya alifunga bao la pili akiwa ndani ya 18 kwa mguu wa kulia lililomshinda mlinda mlango wa Singida United kabla ya kulazimisha kuingia ndani ya 18 na kufunga bao la tatu dakika ya 54 kwa mguu wake wa kulia akimalizia pasi za Clytous Chama.

Licha ya kufungwa mabao hayo bado Singida United walijitahidi kufanya mashambulizi kwa kushtukiza lango la Simba hali iloyomfanya mlinda mlango Aishi Manula kuwa katika kazi nzito kuokoa jahazi la Simba na kufanikiwa.
Share:

AFISA UHAMIAJI AFARIKI BAADA KUNYWA POMBE KUPITA KIASI


Na John Walter-Babati
Afisa uhamiaji Mkoani Manyara aliyefahamika kwa jina la Peter Kambanga (35- 40) amepoteza maisha usiku wa alhamisi Disemba 27 kwa kile kinachoelezwa kunywa pombe kupita kiasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Agustino Senga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi hilo lilifika katika chumba alichopanga marehemu, mjini Babati na kukuta kimefungwa kwa ndani na kuwalazimu kuvunja ndipo walipoukuta mwili huo.

Kamanda Senga amesema kuwa chanzo cha kifo hicho ni unywaji wa pombe kupindukia na kukosa hewa na kuongeza kuwa alikuwa akiishi mwenyewe katika chumba alichokuwa amepanga.

Aidha Senga amesema mwili wa Marehemu umesafirishwa leo Jumamosi Disemba 29,2018 kwenda wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma kwa ajili ya taratibu za Mazishi.

Kamanda Senga ametoa wito kwa wakazi wa Manyara kuishi pamoja na ndugu au familia zao pindi wanapokuwa mbali kikazi.

Sambamba na hilo jeshi la polisi mkoani Manyara limewasishi wananchi kunywa pombe kistaarabu na kuendesha magari kwa uangalifu huku likizidi kuimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya mkoa huu katika kipindi hiki cha siku kuu za mwisho wa mwaka.

Share:

Utabiri Uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Kuanzia Usiku Huu




from MPEKUZI http://bit.ly/2rYaGnn
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger