Thursday 5 January 2017

Habari Zilizopo Katika Magaeti Ya Leo Alhamisi ya January 5




Share:

Jeshi la Polisi Laua Majambazi Watatu Dar es Salaam

Share:

Amuua Mkewe Kwa Visu na Kumnyonga Mtoto Baada ya Kuambiwa Ana Mchepuko Nje ya Ndoa

Mkazi  wa Bukene wilayani Nzega mkoani Tabora, amemuua mkewe pamoja na mtoto wake.
Share:

Wednesday 4 January 2017

PUBLIC NOTICE: Admission for March/April 2017 Intake through Central Admission System (CAS)

 
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
 
PUBLIC NOTICE
Admission for March/April 2017 Intake through Central Admission System (CAS)
The National Council for Technical Education (NACTE) is a statutory body established under the National Council for Technical Education Act, Cap. 129, to oversee and coordinate the provision of technical education and training in Tanzania.  Under the establishing Act, in order to attain and maintain the status of a training provider, all institutions are required to be registered, accredited and have their curricula approved by the Council. Institutions are not allowed to admit students and start offering any programme without the approval of the Council.

The Council has received requests from Technical Institutions offering Certificate and Diploma programmes to have March/April 2017 Intake for the academic year 2017/2018. The Council, has therefore decided to make a public notice to inform all Institutions offering Certificate and Diploma programmes  intending to have March/April 2017 Intake for the  academic year 2017/2018  to submit their intention. The March/April 2017 Intake is meant for Certificate and Diploma programmes only.
The request for having the March/April 2017 Intake should clearly specify:   

  • The number of students enrolled in the requested Certificate and/or Diploma  programme who are registered as first year for 2016/17 academic year;
  • Capacity of the institution in the requested  programme;
  • Empty slots that need to be filled in order for the institution to acquire full capacity; and
  • Whether the college has enough infrastructure and staff to manage two intakes.

Please be informed further that, Central Admission System will be open for applications from 23rd January 2017 to 6th March 2017.

The submission of notice of intention and commitment for having March/April 2017 Intake for the academic year 2018/2019 should reach the Council by 15th January 2017.


Issued by:
OFFICE OF THE EXECUTIVE SECRETARY
NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION (NACTE)
DATED: 4TH JANUARY 2017
Share:

New AUDIO | Rayvanny [Raymond] – Furaha | Download

Share:

Serikali kuajiri walimu 4000 wa masomo ya Sayansi na Hisabati

1
Serikali imesema ipo kwenye mchakato wa kuajiri walimu 4000 wa masomo ya Sayansi na Hisabati.
Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akiwa katika ziara yake ya kutembela wilaya mpya za jiji hilo, akianzia na Kigamboni siku ya leo.
Majaliwa amesema mchakato wa ajira hizo unaendelea chini ya Ofisi ya Rais Utumishi, na muda wowote kutoka sasa mchakato huo utakapokamilika, majina yatatolewa na walimu hao kuajiriwa.
Kuhusu walimu wa masomo mengine, Waziri Mkuu amesema walimu wa masomo mengine hususani ya sanaa wapo wa kutosha na kwamba wanapaswa kusubiri kwakuwa wao wako wengi zaidi na hakuna uhaba na uhitaji wa walimu hao wa masomo ya sanaa.
Hivi karibuni, Wizara ya Elimu iliwataka wahitimu wa ualimu katika masomo ya sayansi na hisabati kutuma taarifa (CV) zao ili izihakiki kabla ya ajira, mchakato ambao tayari umekamilika na majina yalitumwa katika wizara ya utumishi.
Naibu Waziri wa Elimu, Mhandisi Stella Manyanya wiki mbili zilizopita wakati akiongea na kituo cha EATV alisema kuwa kazi ya wizara yake ilikuwa ni kuhakiki taarifa za wahitimu hao, na si kuajiri, huku akibainisha kuwa zoezi hilo limekamilika na majina yako utumishi ambao ndiyo watahusika na kuajiri.
Pia alisisitiza kuwa kama wizara ya elimu waliomba kupewa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati haraka kwa kuwa uhitaji wao ni mkubwa zaidi na kuwataka wahitimu wote waliotuma taarifa zao, wasubiri watapata majibu muda si mrefu.
Chanzo: mpekuzi huru
Share:

Tuesday 3 January 2017

MAHAKAMA YAIAMURU SERIKALI KUREKEBISHA VIFUNGU VYA SHERIA YA MITANDAO

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameondolewa mamlaka ya kutoa adhabu isiyokatiwa rufaa kwa mshtakiwa anayekiri makosa ya kimtandao.

Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu,umeipa Serikali miezi 12 kukifanyia marekebisho kifungu cha 50 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao kilichobatilishwa.

Hata hivyo, mahakama hiyo imehalalisha vifungu vingine vyote vya sheria hiyo, ambavyo pia vimekuwa vikilalamikiwa na wadau wa matumizi ya mitandao na teknolojia ya habari.

Uamuzi huo umetokana na kesi ya kikatiba, iliyofunguliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)na mashirika mengine.

Katika hukumu iliyotolewa na majaji Profesa John Ruhangisa, Winfrida Korosso na Lugano Mwandambo, Mahakama ilibatilisha Kifungu cha 50 cha sheria hiyo, lakini ikaridhia vingine kuwa ni halali.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARY TAREHE 3.1.2017



Share:

MWENYEKITI WA CHADEMA NA WENZAKE 7 WAFIKISHWA MAHAKAMANI

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Karatu mkoani Arusha, Thomas Darabe na wenzake saba wamepandishwa kizimbani kujibu shitaka la kuharibu mali ya thamani ya zaidi ya sh milioni 75.4 na vitunguu.

Pamoja na Darabe, waliopandishwa jana katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha/ Arumeru ni Charles Lameck ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia maji ya ya vijiji saba vilivyoko katika wilaya ya Karatu na George Pius.

Wengine ni Baridi John, Christopher Lameck, Florian Tiofil, Daniel Ninida na Lazaro Emmanuel.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia maji alishitakiwa na mashitaka manne pekee yake ya thamani ya zaidi ya sh milioni 60 katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha na Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.

Akisomewa shitaka la kwanza na Mwendesha mashitaka wa serikali, Charles Gakirwa mbele ya Hakimu Mkazi Patricia Kisinda, alidai kuwa Desemba 28 mwaka huu mtuhumiwa alifanya uharibifu wa mali aina ya pampu ya maji ya thamani ya sh milioni tatu na bomba la maji la sh 448,000.

Shitaka la pili lililosomwa wakili wa serikali Gakirwa mbele ya hakimu mkazi wa wilaya ya Arusha , Devotha Msofe ilidaiwa kuwa Lameck alifanya uharibifu katika wa mfumo wa maji katika kijiji cha Quandet Karatu wa thamani ya zaidi ya sh milioni 1.6.

Mtuhumiwa alikana mashitaka yote na alipewa dhamana ya mtu mmoja na wadhamini wakifanikiwa kukidhi vigezo vyote katika mashitaka hayo. 
Katika mashitaka yaliyowahusu washitakiwa wote, akiwemo Darabe pamoja na Lameck ilidaiwa kuwa wote kwa pamoja walitenda kosa la uharibifu wa mali kwa kuchoma pampu ya maji ya thamani ya zaidi ya sh milioni tatu na injini ya maji ya thamani ya sh milioni 12.

Shitaka la tatu lililokuwa likiwakabili washitakiwa wote ni kuharibu mazao aina ya vitunguu ya thamani ya zaidi ya sh milioni 49 na pampu mbili za sh milioni sita. 
Washitakiwa wote walikana mashitaka hayo na dhamana zao zilikuwa wazi na upelelezi wa kesi hiyo ulikuwa bado haujakamilika na kesi hiyo itatajwa tena januari 16 mwaka huu.
Share:

MAJAMBAZI YAPORA MAMILIONI MBELE YA ASKARI POLISI DAR

Watu  wanaodaiwa majambazi wamepora kiasi cha fedha kinachokadiriwa kuwa zaidi ya shilingi milioni 25 katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere, eneo la Tazara, Dar es Salaam.

Tukio hilo lilitokea  jana saa 4 asubuhi wakati gari hilo likiwa kwenye foleni ya magari eneo hilo la taa za Tazara.

Watu hao wameporwa katika eneo ambalo huwa askari doria wametanda, lakini wakikamata pikipiki zinazotokea eneo la Buguruni.

Aidha taa za Tazara yaliko makutano ya barabara kutokea Buguruni, Temeke, Kariakoo/Posta na Gongo la Mboto ndilo eneo lenye askari wengi wakiwemo wa usalama barabarani.

Wakati tukio likifanyika kulikuwepo askari wenye magwanda maalumu ya askari doria zaidi ya watano wakivurumushana na waendesha pikipiki upande wa Barabara ya Mandela kutokesa Buguruni. Hata hivyo imeelezwa kuwa watu hao waliokuwa wakipeleka benki hawakuwa na ulinzi kama inavyoshauriwa na Jeshi la Polisi.

Majambazi hao waliokuwa watatu, walipora fedha hizo katika gari ndogo aina ya Toyota Rav4 yenye namba za usajili T 455 DFN mali ya kampuni ya kutengeneza mabati ya Sun Share iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aliyejitambulisha kwa jina la Richard Charles.

Kwenye gari pia alikuwepo mfanyakazi mwingine wa kampuni hiyo, mwenye asili ya China, aliyetambulika kwa jina la Cheng Deng.

Kwa mujibu wa dereva wa gari hiyo, Charles, walikuwa wakizipeleka fedha hizo benki eneo la Quality Centre na ndipo walipovamiwa na watu hao wakiwa na pikipiki aina ya boxer wakati magari yakiwa kwenye foleni wakisubiri taa ziwaruhusu kupita kutoka barabara ya Mandela.

Charles alisema majambazi hao walimwamrisha kufungua mlango na kuwapatia begi la fedha lililokuwa limewekwa katika kiti cha nyuma huku wakimtishia kwa bastola kabla ya kuvunja kioo cha nyuma cha gari hilo na kubeba fedha hizo na kutokomea nazo.

“Kwa kweli hata sielewi mpaka sasa hivi kilichotokea. Walikuja watu wawili mmoja upande wangu mwingine wa bosi wangu wakinitishia kwa bastola nifungue mlango niwape begi la fedha. Ghafla mtu mwingine akavunja kioo cha nyuma kwa kutumia kitako cha bastola na kubeba begi la fedha na kutokomea” alisema Richard.

Askari wenye silaha walifika katika eneo la tukio dakika 20 baada ya tukio hilo wakaishia kuhoji. Hata hivyo askari mmoja ambaye hakutaka kujitambulisha jina lake alilaumu tabia ya baadhi ya watu kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha pasipo kuomba ulinzi wa polisi jambo linalohatarisha usalama wao na mali zao.

“Kama walijua wanasafirisha kiasi kikubwa hicho cha fedha kwa nini wasingeomba hata ‘escort’ (kusindikizwa kwa ulinzi) ya polisi? Hili ni tatizo, hasa katika kipindi hiki kigumu cha upatikanaji wa fedha, watu wanatakiwa kuchukua tahadhari mapema.” alisema askari huyo.

Credit: Habari Leo
Share:

MOTO WATEKETEZA MADUKA 14 ARUSHA

Maduka 14 katika eneo la Mianzini jijini Arusha yameteketea kwa moto jana asubuhi na kusababisha hasara mbalimbali huku jeshi la polisi likiimarisha ulinzi na kusimamia shughuli za uokoaji wa mali zilizosalimika. 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme iliyoanzia kwenye baadhi ya majokofu yaliyokuwa katika baadhi ya maduka hayo. 
Kamanda Mkumbo alisema mara baada ya hitilafu hiyo, moto huo ulishika mitungi ya gesi iliyolipuka na kuanza kusambaa kwa kasi na kuunguza maduka hayo. 
Alisema wamefanikiwa kuokoa baadhi ya mali katika maduka tisa kati ya 14 kwa msaada wa wananchi na wasamaria wema waliokuwa katika eneo la tukio lakini ukubwa wa hasara bado haujajulikana.
 Mmiliki wa moja ya maduka yaliyoteketea, Zena Athuman alisema kabla ya kufungua biashara yake, alifika katika eneo la tukio na kukuta moto huo umeshaanza na hakufanikiwa kuokoa mali yoyote kwa kuwa moto huo ulikuwa ukisambaa kwa kasi ya ajabu. 
Shuhuda wa tukio hilo, Julius Sangeti alisema alifika katika eneo hilo saa 11:30 asubuhi na kushuhudia moto ukiwaka katika duka kubwa la Mianzini na kadri muda ulivyokuwa ukisonga, ndivyo ulivyokuwa ukihamia kwenye maduka mengine na kuteketeza mali.
Share:

RAIS JPM AZUIA CHAKULA CHA MSAADA MISENYI,ASEMA WANANCHI WACHAPE KAZI

Share:

Monday 2 January 2017

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA UDOM

  
KUISOMA
Share:

RAIS ATENGUA UTEZU WA MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 01 Januari, 2017 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Felchesmi Mramba.

Kufuatia kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua Dkt. Tito Esau Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Tito Esau Mwinuka alikuwa Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

Uteuzi wa Dkt. Tito Essau Mwinuka unaanza mara moja.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
01 Januari, 2017
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger