Friday 2 September 2016

New AUDIO | Chadala X Ney Wamitego - Niweje | Download

Share:

MPYA NACTE:MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VYA UALIMU,AFYA,KILIMO,MIFUGO NK. CHETI NA DIPLOMA AWAMU YA PILI 2016/2017 KUTANGAZWA RASMI TAREHE 5 SEPTEMBER 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTEUZI WA PILI NA KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI KATIKA KOZI ZA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwaarifu wote walioomba kudahiliwa katika kozi za cheti na diploma na Umma kwa ujumla kuwa lilifunga dirisha la maombi mnamo tarehe 13 Agosti 2016 ili kuruhusu uteuzi wa awamu ya pili kwa waombaji wa kozi hizo. Uteuzi wa awamu ya pili kwa waombaji wa cheti na diploma ulitarajiwa kutangazwa tarehe 31 Agosti 2016 lakini kwa sababu zilizo nje wa uwezo wetu umesogezwa mbele mpaka tarehe 5 Septemba 2016.

Baraza pia linapenda kutoa taarifa  kuwa Mfumo wa Pamoja wa Udahili (CAS) kwa waombaji wa cheti na diploma utafunguliwa tena tarehe 5 Septemba 2016 hadi tarehe 15 Septemba 2016 ili kujaza nafasi za udahili zitakazokuwa wazi baada ya uchaguzi wa awamu ya pili. Hatua hii itawezesha kuruhusu machaguo mapya kwa wale ambao hawakuchaguliwa katika kozi walizoomba pamoja na  kuruhusu waombaji wapya ambao kwa njia moja au nyingine hawakuomba udahili hapo awali.

Baraza linaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo.

Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE
Tarehe: 02 September, 2016
Share:

MPYA:SCHORALSHIP KWA FORM SIX KWENDA OMAN 2016/2017

Share:

MPYA:SCHORALSHIP KWA FORM SIX KWENDA EGYPT 2016/17

Share:

HIZI HAPA FORM FIVE JOINING INSTRUCTION 2016/2017 PDF - Joining Instruction Kidato cha Tano 2016/2017 -SECOND SELECTION

FORM FIVE JOINING INSTRUCTION 2016/2017 PDF - Joining Instruction Kidato cha Tano 2016/2017

PATA JOINING INSTRUCTION FORM FIVE 2016/2017


DOWNLOAD JOINING INSTRUCTION  FORM FIVE 2016/2017/MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO 2016/2017


JOINING INSTRUCTION FORM FIVE 2016/2017 1ST SELECTION


SECOND SELECTION FORM FIVE 2016/2017 JOINING INSTRUCTIONS


MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SEKONDARI KIDATO CHA TANO 2016


Chagua Mkoa
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI SECOND SELECTION KIDATO CHA 5 2016 ,WANAFUNZI WENYE UMRI ZAIDI YA MIAKA 25 HAKUNA KUINGIA FORM 5


ndalichako 




TANGAZO MUHIMU!


MUDA WA KURIPOTI (REPORTING TIME) KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2016 wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili (31-AUG-2016.) atakuwa amepoteza nafasi h

>>bonyeza hapa kuona majina ya Waliochaguliwa kidato cha tano awamu ya pili 2016, Form Five Second Selection 2016 - TAMISEMI - New Update


ii.
Share:

breaking news:haya hapa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga form 5 awamu ya pili (second selection) 2016

 Image result for serikali ya tanzania

TAARIFA KWA UMMA





OR-TAMISEMI inatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya Pili (Second Selection) kwa mwaka 2016. Jumla ya wanafunzi 3,918 wakiwemo wasichana 2,413 na wavulana 1,505 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi na wanafunzi ambao hawakuripoti awamu ya kwanza.
Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 1,864 wakiwemo wasichana 1,099 na wavulana 765 sawa na asilimia 47.58 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 2,054 wakiwemo wasichana 1,314 na wavulana 740 sawa na asilimia 52.42 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara.
Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2015 wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili atakuwa amepoteza nafasi hii.
Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2016 inapatikana kwenye tovuti ya OR-TAMISEMI ya www.tamisemi.go.tz
Imetolewa na Katibu Mkuu,
OR-TAMISEMI


>>bonyeza hapa kuona majina ya Waliochaguliwa kidato cha tano awamu ya pili 2016, Form Five Second Selection 2016 - TAMISEMI - New Update

Tumia link hii kupata matokeo : >> Waliochaguliwa kidato cha tano awamu ya pili 2016
Link ya Matokeo ya awali : >> Waliochaguliwa kidato cha tano na vyuo vya ufundi 2016
Share:

Rais Magufuli amuapisha Bw. Doto M. James kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,  tarehe 01 Septemba, 2016 amemuapisha Bw. Doto M. James kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 
Bw. Doto M. James aliteuliwa kushika wadhifa huo jana tarehe 31 Agosti, 2016 na amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Servacius Likwelile ambaye atapangiwa kazi nyingine.
 
Kabla ya uteuzi huo, Bw. Doto M. James alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera).
 
Hafla ya kuapishwa kwa Bw. Doto M. James imehudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.
 
Aidha, Bw. Doto M. James amekula kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma, zoezi ambalo limeongozwa na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Salome Kaganda.

 Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es salaam
01 Septemba, 2016
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Septemba 2

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger