Wednesday 29 June 2016

CCM Yawalima Barua Wabunge Wake.....Sasa Watakiwa Kujieleza Kamati Kuu


Kamati Kuu ya CCM imeagiza Kamati ya Wabunge wa chama hicho kuwapa barua za kujieleza wabunge wao wasiohudhuria, wanaochelewa na wanaondoka kabla ya vikao vya Bunge kuahirishwa. 
Tayari maagizo hayo yamefanyiwa kazi na Katibu wa Wabunge wa CCM, Jasson Rweikiza ambaye amewalima barua wabunge hao. 

Katika barua yenye kichwa cha habari “Maagizo ya Kamati Kuu ya CCM” aliyopewa mmoja wa wabunge wa CCM inaonyesha wametakiwa kujieleza kwa nini siku nyingine walifika wamechelewa na mara kadhaa walitoka mapema kabla kuahirishwa kwa Bunge. 
“Mwenendo huu ni kukiuka kanuni za Kamati ya Wabunge wote wa CCM hasa kanuni ya 41. Tafadhali andika maelezo kwa nini Kamati Kuu isichukue hatua? Maelezo yanifikie  kabla ya Juni 25 mwaka huu,” ilisema sehemu ya barua ya mmoja wa wabunge walioandikiwa. 
Alipoulizwa Rweikiza kuhusiana na barua hiyo alisema haitambui na kwamba imeghushiwa. 

“Kanuni zipo zinazoongoza vikao vya Bunge, zipo pia zinazoongoza wabunge wa CCM. 

"Wakitaka kuondoa wabunge wa CCM wanazijua sana, isipokuwa hatujafikia hatua ya kufundishana kwa kuanza kuandikiana barua,”alisema. 
“Wanajua mbunge hawezi kuondoka bila kwenda kwa Spika na kuomba ruhusa au kujulisha kwenye chama kwamba anatoka, wanajua,” alisema Rweikiza na kusisitiza kwamba hata taarifa zinazoonyesha kuna wabunge wanaotakiwa kujieleza kwake ni majungu tu. 
Japokuwa Rweikiza ameikana barua hiyo, wabunge kadhaa wa CCM walioomba majina yao yasitajwe wamekiri kwamba barua hizo zimetolewa na kwamba wanabanwa kwa kutakiwa kujisajili mara mbili; kitabu cha Bunge na cha CCM. 
Katika ukurasa wake wa Facebook uliosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), alisema wabunge wa CCM wanalalamikia kulazimishwa kuingia bungeni kwa kuwa Bunge halina ladha. 
Pia, Msigwa alisema wabunge hao wa CCM wanadai Naibu Spika Dk Tulia Ackson hafuati kanuni na taratibu na kwamba wametakiwa kujieleza Kamati Kuu ya CCM. 
Aidha, baadhi ya wabunge wa CCM walionekana kukerwa na utaratibu wa kujisajili sehemu mbili yaani Bunge na CCM mara mbili kwa siku. 
“Kuna haja gani ya kutia dole (kusaini kwa utaratibu wa kieletroniki) halafu tena tuje tusaini kwenye makaratasi ya CCM?,” alihoji mmoja wa  wabunge. 
Alisema ili kusaini karatasi hizo inawapasa wabunge kwenda upande wa Kambi Rasmi ya Upinzani ambapo wabunge waliokabidhiwa kazi ya kuzitunza karatasi hizo hukaa kama kambi mbadala baada ya wabunge wa upinzani kususia vikao vinavyoendeshwa na Dk Tulia.
“Wengine tunaheshima zetu hatuwezi kwenda upande wa upinzani kufuata makaratasi ya kusaini. Kwanza Bunge lenyewe halina mvuto unakuja hapa watu wawili ndio wanapewa nafasi ya kuchangia mjadala na baada ya hapo wanapitisha,” alisema. 
Mbunge mwingine wa CCM alisema haoni haja ya kuwepo ndani ya Bunge kwa sababu hawapewi nafasi ya kutosha ya majadiliano na hivyo bora kutokuwepo ndani ya ukumbi muda wote. 
“Mimi saa hizi naingia ndani ya ukumbi wa Bunge nasaini natoka naenda zangu kantini (ya Bunge) kuangalia mpira maana hata nikikaa ndani sitopata nafasi ya kuchangia,” alisema mbunge huyo. 
Alisema haoni haja ya kusaini mara mbili kwa sababu CCM wanaweza kutumia usajili wa Bunge kufahamu wabunge waliopo na wasiohudhuria kwa wakati wanaouhitaji. 

Alisema orodha hiyo haina mashiko kwa sababu wanazo namba za wabunge wote kama kuna jambo ambalo wanahitaji basi wanaweza kuwataarifu. 
“Hata mimi nimepewa barua ya kujieleza lakini si kwamba ni mtoro bali tunakuwa na majukumu mengine ya kibunge nje ya Bunge,” alisema. 
Hatua hiyo inakuja wakati wabunge 118 wa vyama vinavyounda Ukawa, wakiwa wamesusia vikao vya Bunge vinavyoendeshwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kwa madai ya kuongoza vikao kibabe na kutofuata kanuni. 
Hii ni wiki ya nne tangu Dk Tulia aanze kuendesha vikao vya Bunge peke yake bila kupokewa na wenyekiti wa Bunge kama ilivyokuwa kabla hajatofautiana na kambi rasmi ya upinzani
Share:

Tuesday 28 June 2016

BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD FORM YA MKOPO/ KUOMBA MKOPO BODI YA MIKOPO 2016/2017

 

Share:

RASMI:Maombi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu Mwaka wa Masomo 2016 /2017 Yafunguliwa

 

MAOMBI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU 2016/2017

Kuanza kuomba Tafadhari 

<<BOFYA HAPA>>

Share:

VIDEO:GWAJIMA BADO ANATAFUTWA NA JESHI LA POLISI KWA UDI NA UVUMBA-SIMON SIRRO



Kamanda wa polisi jiji la Dar Simon Sirro amesema bado wanamtafuta sana askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Josephat Gwajima na wametumia mtandao wa polisi wa kimataifa Interpol lakini bado hawajapata majibu.

Amesema walipokea barua kutoka kwa wakii wake lakini wao hawafanyi kazi kwa taarifa hizo, amewataka waandishi wa habari na wananchi wasaidie kupatikana kwake.




Share:

MPYA:BODI YA MIKOPO YAFUNGUA APPLICATION ZA MIKOPO (KUANZIA JUNE 27 HADI JULY 31) KWA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU MWAKA WA MASOMO 2016/2017

 
Tokeo la picha la heslb

 

 GUIDELINES AND CRITERIA FOR ISSUANCE OF STUDENTS’ LOANS AND GRANTS FOR THE 2016/2017 ACADEMIC YEAR

 These Guidelines and Criteria are issued to prospective loan applicants and the public at large to guide the whole process of application and issuance of loans and grants for the academic year 2016/2017. 



Share:

MECHI YA YANGA VS TP MAZEMBE: Mashabiki Kuingia Uwanjani Bure Leo, Kikomo cha Mashabiki ni 40,000 Ukichelewa "Tazama Kwenye TV"

MASHABIKI wa Yanga leo watajazana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam bila kulipa hata senti tano kushuhudia mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Hata hivyo, kujazana kwao uwanjani hakutakuwa na maana iwapo kikosi hicho cha Kocha Hans van der Pluijm kitashindwa kuondoka na pointi tatu.
Katika mchezo wa kwanza wa mashindano hayo dhidi ya Mo Bejaia ya Algeria, Yanga ililala kwa bao 1-0, hivyo mechi ya leo kuwa na kila sababu ya kushinda hasa kwa kuzingatia itakuwa mbele ya mashabiki wake wengi.
Awali, kulikuwa na mvutano kati ya Yanga na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya klabu hiyo ya Jangwani kutangaza kuwa mashabiki wataingia bure.
Hata hivyo, makubaliano ya mwisho yaliyolishirikisha pia Shirikisho la Soka Afrika (Caf), mashabiki wasiozidi 40,000 ndiyo watakaoruhusiwa kuingia uwanjani kutokana na sababu za kiusalama, kwa mujibu Msemaji wa TFF, Alfred Lucas.
Lucas alisema kamisaa wa mchezo huo kutoka Zambia, Kidio Joseph alikuwa na shaka huenda uwanjani ungejaa kupia uwezo, hivyo kuhatarisha usalama.
"Hayo ni maelekezo tuliyoyapata kutoka CAF na Yanga wanazo taarifa hizi na ni lazima tufuate maelekezo hayo," alisema Lucas.
Aidha, alisema mashabiki wataruhusiwa kukaa kwenye jukwaa la mzunguko na majukwaa mengine watakaa watu maalum (Special Seat).
Aidha, kwa upande wa Yanga wamekubali maelekezo hayo ya CAF.
Afisa habari wa timu, Jerry Muro, alisema wamepata taarifa hiyo ya CAF na hawana pingamizi nayo.
Achana na habari hiyo, turudi kwenye mchezo wa Yanga na Mazembe.
Wawakilishi hao wa Tanzania, wataingia uwanjani wakiwa na dhamira moja tu ya ushindi, kwani hata matokeo ya sare dhidi ya timu hiyo ngumu hatawasaidia kujiweka kwenye nafasi nzuri.
Pluijm alisema wachezaji wake wanafahamu umuhimu wa ushindi kwenye mchezo huo, kinyume na ushindi basi vijana hao wa Jangwani watakuwa wamepotea njia.
"Kupoteza mchezo wa kesho (leo) itakuwa mbaya zaidi kwetu, kundi letu lina timu nne na kati ya hizo mbili zilipata ushindi kwenye mechi zao za kwanza," alisema Pluijm.
Pluijm, ambaye kikosi chake kiliweka kambi zaidi ya wiki mbili nchini Uturuki kujiandaa na michuano hiyo, ana matumaini wakubwa wachezaji wake watafuata maelekezo yake na kushinda mechi hiyo.
"Wachezaji wangu wako kwenye hali nzuri, wamejiandaa kikamilifu kwa mchezo huu. Ukimuondoka Msuva (Simon), wengine wako kwenye hali nzuri kimchezo," alisema na kuongeza:
"Tunahitaji kushinda leo mbele ya mashabiki wetu waliopata fursa ya kuingia uwanjani bila kulipa kiingilio. Haitakuwa na maana kupoteza mchezo huu, siyo tu kwa sababu mashabiki wetu wataingia uwanjani bura, bali matokeo ya kipigo yatatuweka kwenye wakati mgumu."
TP Mazembe wanashuka dimbani wakiwa na kumbukumbu ya ushindi baada ya kushinda mchezo wa kwanza, hivyo wamejipanga kikamilifu kuifunga Yanga nyumbani
Katikati ya wiki hii, mshambuliaji Mazembe, Thomas Ulimwengu alisema mchezo utakuwa mgumu kutokana na ukweli kwamba Yanga ni timu nzuri na hawatakubali kupoteza mchezo mwingine baada ya kushindwa kupata pointi kwenye mchezo wa kwanza.
"Tumejiandaa vizuri na mchezo huu, pamoja ya kuwa mpira una matokeo matatu lakini kwetu tunaamini kwenye ushindi," alisema Ulimwengu.
Share:

New AUDIO | Linex Ft. Christian bella - Hewala | Download

Share:

New AUDIO | Q Chief Ft. Mb Dog, Amour,Kadjanito & Meddy - SOHARD | Download

Share:

Official VIDEO | Yamoto Band Ft. Ruby - Su | Watch/Download


https://www.youtube.com/watch?v=7dkEhmEHdZ4
Share:

Magazeti ya Leo Jumanne ya June 28, 2016


Share:

Monday 27 June 2016

Afariki Dunia Baada ya Kunywa GONGO Kupita Kiasi


MKAZI wa Mondo katika Kijiji cha Kitumba wilayani Magu, Wilson Magola (45), amekufa baada ya kunywa pombe haramu ya gongo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoani Mwanza, Ahmed Msangi alisema jana kuwa, tukio hilo lilitokea Juni 23, mwaka huu, saa 8:00 mchana kitongojini humo.

Msangi alieleza kuwa, baada ya kufika nyumbani kwa Daudi Mtula anayeuza gongo kwa siri Magola alikunywa pombe hiyo kupita kiasi akaishiwa nguvu na kupoteza maisha.

“Mtu huyo pia alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifafa,” Kamanda Msangi alisema na kuongeza kuwa, baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alitoroka na kuuacha mwili wa marehemu nyumbani kwake.

Alisema kuwa Polisi inamtafuta kwa ajili ya kumchukulia hatua za kisheria. 
“Tulipata taarifa kutoka kwa raia mwema na tulipofika nyumbani kwa mtuhumiwa tuliupata mwili na tayari umekwishafanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa familia kwa ajili ya maziko,” alisema.

Alitoa wito kwa wananchi kuiunga Polisi mkono kudhibiti biashara ya pombe hiyo haramu.
Share:

Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo

Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo kuanzia jana. 
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa ikimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imesema Rais amemteua Dk Charles Mlingwa ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Siha kujaza nafasi hiyo. 
Mulongo anakuwa mkuu wa mkoa wa pili kutimuliwa kazi na Rais Magufuli baada ya Anne Kilango Malecela aliyekuwa Shinyanga.

Hata hivyo, tofauti na Kilango ambaye alitimuliwa kutokana na kutoa taarifa potofu kuhusu watumishi hewa mkoani mwake, Ikulu haikutoa sababu za kutenguliwa kwa uteuzi wa Mulongo.

Mulongo ameondolewa madarakani miezi sita baada ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Dk Faisal Issa baada ya kutofautiana na Mulongo wakati huo akiwa mkuu wa mkoa huo.

Baada ya kumwondoa Dk Issa na nafasi yake kujazwa na aliyekuwa Kamishna wa Polisi, Fedha na Utawala (CP) Clodwig Mtweve, miezi miwili baadaye Rais alimbadilisha Mulongo kituo cha kazi akimhamishia Mara.

Alipoulizwa jana jinsi alivyoipokea hatua hiyo iliyochukuliwa dhidi yake Mulongo alisema: “Sina taarifa rasmi.” 

Kabla kuhamishiwa Mara akitokea Mwanza, Mulongo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Alishika nafasi hiyo baada ya kupandishwa cheo akiwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo.
Share:

CHADEMA Watafakari Hatua za Kuchukua Baada ya Rais Magufuli Kutaka Siasa Zifanywe 2020 ( wakati wa Uchaguzi Mkuu ujao )


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Pwani kimesema kinatafakari hatua gani ya kuchukua baada ya Rais John Magufuli kutaka siasa za nguvu zifanywe wakati wa Uchaguzi Mkuu ujao, kauli inayotafsiriwa kuwa ni kupiga marufuku shughuli za kisiasa. 
Rais alitoa kauli hiyo mapema wiki iliyopita wakati akipokea taarifa ya Uchaguzi Mkuu kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kuisisitizia juzi wakati wa hafla ya kuzindua mpango wa polisi wa kuboresha huduma za usalama wa jamii. 
Akizungumza jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam, katibu wa Chadema wa kanda hiyo, Casmir Mabina alisema wamefikia azimio la kupinga unyanyasaji na ukandamizaji kwa vyama vya siasa unaofanywa na Serikali ya Dk Magufuli. 
Mabina alisema Rais Magufuli anavunja Katiba na Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 ambayo inaviruhusu vyama vya siasa kuendesha shughuli mbalimbali za kisiasa. 
Alisema vyama haviwezi kukaa kimya mpaka mwaka 2020 wakati kazi yao ni kukutana na wananchi. 

“Tunamshauri Rais Magufuli aache kutawala nchi kwa woga na ubabe ... afuate misingi ya Katiba na sheria, na kuwaongoza Watanzania badala ya kuwatawala,” alisema Mabina. 
 
Mabina aliongeza kuwa Jeshi la Polisi liache kutumiwa na Serikali kufinyanga sheria za nchi na kukandamiza upinzani kwa kutumia vibaya Sheria ya Jeshi la Polisi, kifungu cha 43 (3) kwa kusingizia habari za ‘kiintelijensia’ na ‘hali ya uvunjifu wa amani’. 
Mwenyekiti wa Chadema wa Kanda ya Dar es Salaam Kuu, Mwita Waitara alilalamikia kitendo cha mameya wa Dar es Salaam kunyimwa vibali vya kwenda nje ya nchi kutafuta fedha ili kusaidia maendeleo ya halmashauri zao. 
Alisema fedha za safari hizo zinatolewa na washirika wa maendeleo, lakini Serikali imekuwa ikizuia safari hizo kwa kisingizio cha kubana matumizi. 
Alisema safari nyingine za nje ni muhimu kwa sababu zinawawezesha mameya kukutana na wadau wa maendeleo ili kupata misaada. 

 “Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob alikuwa na safari ya kwenda Afrika Kusini kukutana na mameya wengine duniani, lakini alizuiliwa kwa maelekezo. 

"Hatuwezi kuendelea kama tutashindwa kukaa na wenzetu ili kujifunza mambo ya maendeleo,” alisema.

Mwita alidai kuwa huo ni mpango wa Serikali kudhoofidha halmashauri zinazoongozwa na upinzani ili wasiweze kufanya mambo makubwa ambayo hayajawahi kufanywa na CCM. 
Alisema yeye pia alizuiliwa kwenda Marekani akiwa mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii. 

Ushauri mwingine ulitolewa na mwenyekiti wa Kanda ya Ilala, Dk Makongoro Mahanga ambaye alimtaka Rais kufuata Katiba kwa sababu aliapa kuilinda na kuitetea kwa masilahi ya Taifa. 
Dk Mahanga alimtaka Rais akumbuke ahadi mbili alizozitoa wakati wa kampeni na wakati anaapishwa, ambazo ni kuilinda Katiba na kuwaletea wananchi maendeleo. 
“Kinachowaogopesha CCM ni upinzani kupata kura zaidi ya milioni sita wakati wa uchaguzi. Wanajua kwamba wanaweza kuchukua nchi, ndiyo maana wameanza kudhibiti vyama vya siasa ili visiwe na nguvu,” alisema Dk Makongoro ambaye aliwahi kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNE TAREHE 27.6.2016

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger