AMA kweli
dunia ina mambo na mambo yenyewe ndiyo haya! Katika hali ya kushangaza,
mwanaume aliyefahamika kwa jina la Ramadhan Ally, mkazi wa Kata ya
Mbuyuni Manispaa ya Morogoro amewashangaza wengi kufuatia uamuzi wake wa
kukodi ngoma ya asili kwa lengo la kwenda kumfumania mkewe
aliyejulikana kwa jina moja la Asha.
Tukio
hilo lililofunga mtaa lilijiri asubuhi ya saa 3:14 Jumatatu iliyopita
eneo maarufu kwa jina la Sultani baada ya mwanaume huyo kutonywa kuwa,
mke wake alikuwa amelala kwa rafiki yake kipenzi, Abdallah Elias.
Baadhi
ya wananchi waliobahatika kuwasili katika eneo la tukio walishuhudia
mwenye mali akiwashushia kichapo kikali ‘wasaliti’ hao ambapo vurugu
zikapamba moto.