Saturday, 30 August 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 30,2025




Magazeti


Share:

Friday, 29 August 2025

NABII RABIEL KUFANYA MAOMBI YA TAIFA

 


Nabii Rabiel Akyoo wa Kanisa la Ukombozi akiongea na waandishi wa habari 


Na Woinde Shizza Arusha Arusha

Nabii Rabiel Akyoo wa Kanisa la Ukombozi anatarajiwa kuongoza maombi ya kitaifa kesho jijini Arusha kwa lengo la kuliombea taifa kudumisha amani na mshikamano wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu.


Akizungumza na waandishi wa habari Nabii Akyoo alisema maombi hayo yatakusanya waumini kutoka maeneo mbalimbali nchini na yatakuwa na ajenda kuu ya kuombea utulivu na mshikikano wa taifa.


“Ni wajibu wa kila Mtanzania kulinda amani Ikitoweka, hakuna kazi, hakuna kipato, na maisha yatakuwa magumu kwa kila mmoja wetu,” alisema.


Sambamba na maombi hayo, kutafanyika harambee ya kuchangia kituo kipya cha habari cha kanisa hicho, kitakachojumuisha televisheni na redio, huku sera yake ikizinduliwa rasmi.


Katika siku hiyo pia kutakuwa na burudani ya nyimbo za injili kutoka kwa waimbaji mbalimbali maarufu akiwemo Upendo Nkone, anayetarajiwa kupamba maombi kwa nyimbo zake za kumsifu Mungu.


Waumini na wananchi wataungana kushiriki ibada ya Meza ya Bwana, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mshikamano wa kiroho na taifa kwa ujumla.


Nabii Akyoo aliwaasa Watanzania kujitokeza siku ya kupiga kura kwa amani na utulivu, akisisitiza kuwa kura ni sauti ya kila raia, lakini amani ya taifa ni urithi wa kudumu.


“Kura yako ni sauti yako, lakini zaidi ya yote, amani ya taifa letu ndiyo urithi mkubwa tunaopaswa kuudumisha,” alisema Nabii huyo.


Maombi hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na waumini wa madhehebu mbalimbali, viongozi wa dini na wananchi kutoka mikoa tofauti, huku Arusha ikitarajiwa kuwa kitovu cha ibada kubwa ya taifa

Share:

Thursday, 28 August 2025

SHEHENA YA MAGARI INAYOPITA BANDARI YA TANGA INAHUDUMIWA KWA UMAKINI MKUBWA

 


Na Oscar Assenga,TANGA

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA)  Bandari ya Tanga  imesema kwamba wanatumia umakini mkubwa na ufanisi katika kuhudumia shehena  mbalimbali zinazopita kwenye Bandari hiyo ikiwemo ya magari ambayo imekuwa ikiongezeka kila mara

Hayo yalisemwa na Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga  Bw. Peter Millanzi alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya taarifa zilizosambaa kwa baadhi ya mitandao kuwa  uwepo wa wizi wa baadhi ya vifaa kwenye magari ambayo yanapitia katika Bandari hiyo jambo ambalo limewashangaza kutokana na umakini wao katika kuhudumia shehena hiyo.


Millanzi alisema kwamba , shehena ya mzigo unaopita wanaouchukulia kwa umakini zaidi ambayo watu wengi wana masilahi yao  binafsi  ambapo wametengeneza utaratibu wa kuhakikisha mizigo yote inayoingia na kutoka  bandarini hapo  ipo salama na inafika kwa wateja ikiwa salama.

“Kwa hiyo katika kuhudumia shehena hizo ikiwemo magari kwa tunatengeneza utaratibu ambapo meli inapotia nanga bandarini lazima kuwepo na taasisi mbalimbali ikiwemo Wakala wa Meli (TASAC),Survey, na TPA kwa hiyo magari yanapoteremka yanakaguliwa na  kurekodiwa taarifa zake kwenye fomu maalumu inayoitwa  “VDITT”inaonyesha hali halisi ya gari lilivyopokelewa bandari hapo  na kuna maeneo mbalimbali yanawekwa alama ya vema kuonyesha vifaa ambavyo vilivyoanishwa havijanyofolewa” Aliongeza Millanzi 



“Lakini pia yapo magari tunayapokea yakiwa yamenyofolewa na yenyewe tunaonyeshwa kwenye ile fomu na hao wote waliotajwa wanashuhudia kile kilichojazwa  na yapo makubaliano baada ya kujaza jinsi hali halisi gari lilivyopokelewa kwenye bandari na kutiliana saini ya makubaliano  na hilo gari linapelekwa eneo la kuhifadhi” Alisema Millanzi 

Aidha alisema kwamba katika eneo la kuhifadhi kuna watu wanapokea wa ulinzi na makarani kisha kusaini  ili kuonyesha kwamba magari waliopokea ni sawa na vile walivyojaza na magari yanapokuja kuchukuliwa na mteja anasaini baada ya kulikagua gari lake na wakijiridhisha wanatoa ushuhuda gari lake amelipokea kama lilivyopokelewa  bandarini hapo.


“Baada ya hapo anasaini na kulichukua kwenda zake kiujumla kipindi chote  hatujawahi kupokea tukio lolote la malalamiko kwamba gari limenyofolewa  au kuharibiwa likiwa  mikononi  mwa bandari.”Alisema Kaimu Meneja huyo wa Bandari ya Tanga.

katika hatua nyingine Milanzi alisema kwamba hivi sasa wameongeza ufanisi mkubwa katika kuhudumia shehena hususani Magari kutokana na uwepo wa maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali kwa kutumia kiasi cha Sh.Bilioni 429.1 na hivyo tokea walipoanza kuhudumia magari imepita mwaka mmoja


Millanzi alisema kwamba, kutokana na uwekezaji huo shehena ya Magari imekuwa ikiongezeka mwezi hadi mwezi kutokana kuongezeka kwa ufanisi katika  kuhudumia shehena mbalimbali na hivyo wenye meli na wateja wameamua kupitisha mizigo yao katika Bandari ya Tanga na  magari yalianza kupitia bandari hiyo mwezi Agosti mwaka 2024 .


Alisema kwamba na takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa kuanzia mwezi Agosti,  2024 hadi  mwezi Julai , 2025 wameweza kuhudumia meli 45 zilizokuwa zimebeba shehena ya magari na magari yaliyohudumiwa ni magari 9,665 na wamepata bahati ya kupata wateja na mawakala mbalimbali ambao wameamua kupitisha shehena ya magari katika bandari hiyo.


“Shehena hizo za magari yanapita hapa nchini na mengine nje ya nchi kama unavyojua Tanzania imepakana na nchi nyingi ambazo hazipakani na bahari kama vile Rwanda,Burundi,Kongo,Uganda ,Malawi,Zambia na nchi nyengine iliyopo mbali zaidi lakini kutokana na kuwepo huduma bora imeamua kupitisha mizigo yake ni  Zimbambwe  “ Alisema Millanzi


Alieleza pia wamekuwa na vikao mbalimbali na wadau ili kuweza kuona kama kuna changamoto wanakutana nazo ili kuzipatia ufumbuzi kwa kufikia viwango vya juu na meli zinapofika Bandarini kupeleka shehena ya mbalimbali ikiwemo magari zinahudumiwa kwa muda wa saa 72 iwapo mteja amekamilisha taratibu zote za kiforodha mara gari linapopokelewa anayofursa ya kuchukua gari lake.


 -

Share:

ASKARI AVUA SARE KAZI BAADA YA KUPATA HABARI MKEWE ANAISHI NA MCHUNGAJI


Askari mmoja wa kituo cha polisi aliibua mshangao baada ya kuamua kuvua sare hadharani na kutangaza kuacha kazi mara moja. Tendo hilo lililotokea karibu na kituo cha polisi mchana wa saa saba liliwashangaza wengi, huku wakazi wakijitokeza kwa wingi kushuhudia. Wengi walidhani huenda askari huyo alipata mshtuko wa akili, lakini muda si mrefu ukweli wa kusikitisha ulifichuka.
Share:

Wednesday, 27 August 2025

DC MASINDI AWATAKA WAGOMBEA KUTUMIA JUKWAA KUFANYA SIASA ZA HESHIMA NA SIO MATUSI


Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi Tarafa ya Mondo Agosti 27,2025

Na Sumai Salum-Kishapu

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga, Mhe. Peter Masindi amewataka wagombea wote wa Jimbo la Kishapu wanaoelekea kuanza kampeni za uchaguzi kutumia lugha ya heshima na sera zenye kujenga badala ya matusi au kejeli wanapokuwa jukwaani.

Akizungumza Agosti 27, 2025 katika ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Tarafa ya Mondo,Masindi amesema siasa za matusi hazina tija, na kuwakumbusha wagombea kwamba kuna maisha baada ya uchaguzi, hivyo hakuna sababu ya kuchochea uhasama.

“Wananchi wanataka kusikia sera zinazogusa maisha yao na namna mtakavyoboresha huduma za kijamii. Huu sio muda wa matusi wala kejeli. Tufanye siasa zenye heshima na staha,” amesema Masindi.

Aidha, amewataka wananchi kusikiliza kwa makini sera za wagombea na kufanya maamuzi sahihi ifikapo Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa msingi wa maendeleo upo mikononi mwao. Vilevile, Masindi amewahimiza wananchi kuendelea kuchangamkia fursa za kiuchumi, kufanya kazi kwa bidii, kuishi kwa nidhamu na kumtanguliza Mungu katika kila jambo.


Afisa Tarafa ya Mondo Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Atka Faki akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi Agosti 27,2025

Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wazazi pia kuhakikisha wanalea watoto wao kwenye maadili, nidhamu na ujasiri ili wawe nguzo ya maendeleo ya jamii.

Katika wito wake kwa jamii, amewahimiza kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo ikiwemo uanzishaji wa maboma ya madarasa, nyumba za walimu, vituo vya afya pamoja na kulinda miundombinu ya maji na umeme iliyowekwa kwa manufaa ya wananchi.

Mbali na hayo, amewahimiza watendaji wa Halmashauri na wakuu wa taasisi zingine za Umma na za fedha kuhakikisha wanafanya kazi kwa maslahi ya wananchi na kuwasogezea huduma muhimu ambazo serikali imekusudia kuwafikishia.

Aidha, wananchi wameelimishwa kuhusu huduma za mikopo zinazotolewa na Halmashauri na Taasisi ya Kifedha (CRDB), huku wakihimizwa kuchangamkia fursa hizo ili kuepuka kuingia kwenye mikopo isiyo rasmi inayochochea migogoro ya kifamilia.

Mhe.Masindi amehitimisha ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika tarafa ya Mondo Vijiji vya Nyasamba Kata ya Bubiki, Mwajiningu Kata ya Busongwa,Itongoitale Kata ya Mwasubi pamoja na Kijiji cha Idukilo Kata ya Idukilo.




Afisa wa taasisi ya fedha CRDB tawi la Maganzo Benjamini Sheka akitoa elimu ya fedha na mikopo kwenye mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi wa kupokea na kutatua kero za wananchi Agosti 27,2028

















Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwajiningu Kata ya Busangwa Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga James Daniel akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi Agosti 27,2025

Mwenyekiti wa Kijiji chaItongoitale Kata ya MwasubiWilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Furahisha Jilinga akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi Agosti 27,2025

Mwenyekiti wa Kijiji cha Idukilo Kata ya Idukilo Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Patrick Kapela Mabala akifuatilia mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi Agosti 27,2025




Share:

SIMON SONGE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA BUSEGA KUPITIA CCM


Mgombea Mbunge wa Jimbo la Busega, Simon Songe akichukuwa fomu ya kugombea ubunge katika Jimbo hilo

Na Woinde Shizza , Busega

Mbunge wa Jimbo la Busega, Simon Songe ameibua matumaini mapya kwa wananchi wa jimbo hilo baada ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea tena nafasi ya ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, mbunge huyo aliwashukuru viongozi wa chama hicho kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuendelea kulitumikia jimbo hilo kupitia tiketi ya CCM Aidha, alimshukuru Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan, pamoja na Kamati Kuu ya chama hicho kwa mwongozo na maono yao ya kuliletea taifa maendeleo.

“Naishukuru sana Kamati Kuu ya CCM ikiongozwa na Mwenyekiti wetu, Mama Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi imara unaoendelea kuimarisha chama na kuwaletea Watanzania matumaini Nimechukua fomu hii nikiwa na dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa Busengo kwa uaminifu na mshikamanio wa kweli,” alisema.
Mbunge huyo aliahidi kuendelea kushirikiana bega kwa bega na wananchi wa Busengo katika kuhakikisha changamoto mbalimbali zinazowakabili zinatatuliwa, ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama, huduma za umeme vijijini, pamoja na kuboresha sekta ya elimu.
Aliongeza kuwa maendeleo ya Jimbo la Busega ni jukumu la pamoja, hivyo ataendelea kusimama mstari wa mbele kushirikiana na wananchi, serikali na wadau wengine ili kuhakikisha kila mwananchi ananufaika na matunda ya chama hicho.

Wananchi waliokusanyika kushuhudia tukio hilo walionyesha furaha na kuahidi kumpa ushirikiano wa dhati katika safari yake ya kuendeleza maendeleo ya jimbo hilo kupitia CCM.

Share:

DKT. SAMIA AREJESHA FOMU YA URAIS INEC



Na Dotto Kwilasa,Dodoma

MGOMBEA wa urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 27, 2027, amerejesha rasmi fomu ya kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), zilizopo Njedengwa, jijini Dodoma.

Dkt. Samia, ambaye pia ni Rais wa sasa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliwasili katika ofisi hizo saa 1:50 asubuhi akiwa ameongozana na mgombea mwenza wake, Dkt. Emmanuel Nchimbi, pamoja na viongozi waandamizi wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma, Alhaj Adamu Kimbisa.

Mara baada ya kuwasili, msafara wa Dkt. Samia ulipokelewa rasmi na Mkurugenzi wa INEC, Kailima Ramadhan, kabla ya kuelekea ofisini kwa ajili ya zoezi la urejeshaji wa fomu – hatua muhimu inayowezesha kuendelea kwake katika mchakato wa kugombea nafasi ya juu kabisa ya uongozi wa taifa.

Dkt. Samia alichukua fomu ya kugombea Urais mapema Agosti 9, 2027, na leo amerejesha rasmi ikiwa ni ishara ya kuhitimisha hatua muhimu katika maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Mbali na CCM, vyama vingine 17 vimeshachukua fomu za kuwania nafasi hiyo ya juu serikalini. Miongoni mwa vyama hivyo ni pamoja na ACT-Wazalendo, CUF, NCCR-Mageuzi, UDP, ADC, TLP, na vyama vingine kama NRA, UMD, CHAUUMA, AAFP, Chama Makini, NLD, UPDP, ADA-TADEA, CCK, DP na SAU.

Urejeshaji huu wa fomu unafungua ukurasa mpya kuelekea kuanza kwa kampeni rasmi, huku Watanzania wakisubiri kwa hamu kuona namna wagombea watawasilisha hoja na dira zao za kuiongoza Tanzania katika kipindi kijacho.



Share:

SHANGWE ZATAWALA KITUMBO AKIREJESHA FOMU UTEUZI KUWANIA UDIWANI KATA YA MJINI - SHINYANGA



Na Marco Maduhu,SHINYANGA

Salum Shabani Kitumbo amerudisha Fomu za uteuzi kugombea Udiwani Kata ya Mjini Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Amerudisha Fomu hizo leo Agosti 27,2025 kwa msimamizi msaidizi wa Uchaguzi (INEC) Kata ya Mjini Simon Mashishanga, huku akisindikizwa na wanachama wa CCM.


Kitumbo akizungumza mara baada ya kurudisha Fomu hizo,amesema anakishukuru Chama chake kwa kumuamini na kupitisha jina lake kugombea nafasi hiyo ya Udiwani Kata ya Shinyanga Mjini,na kuahidi ataitendea haki katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Aidha,ameomba makundi yote yaliyokuwepo wakati wa kura za maoni za kumtafuta mshindi mmoja wa kugombea nafasi hiyo ya udiwani,kwamba yavunjike na kuungana kuwa kitu kimoja na kutafuta kura za ushindi katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29,2025 kwa nafasi za Udiwani,Ubunge na kura nyingi za Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger