Saturday, 12 February 2022

WAZIRI MCHENGERWA-RAIS SAMIA AWEKA BILIONI 1 KWENYE MFUKO WA MAENDELEO YA SANAA NA UTAMADUNI

Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na wadau wa Filamu nchini na kufafanua mafanikio ya Serikali kwenye tasnia hiyo.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt.Hassan Abbas akizungumza na wadau wa Filamu nchini na kufafanua mafanikio ya Serikali kwenye tasnia hiyo.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam Wadau mbalimbali wa sanaa wakifuatilia mkutano na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Mohamed Mchengerwa pamoja na viongozi mbalimbali wa tasnia hiyo.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam *************************** NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa ameweka wazi kuwa Serikali ya awamu ya sita ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu ana dhamira ya kuboresha na kunyanyua kazi za Sanaa nchini na ameongeza Fedha Kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni. Akizungumza na wadau wa kazi za Sanaa nchini Waziri Mchengerwa amesema Serikali ya Tanzania inatambua Mchango wa kazi za Sanaa nchini na awamu ya 6 imedhamiria kuboresha Miundombinu ya kazi za Sanaa na kwa kuanza Rais ameweka billion 1 kwa Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni. "Dhamira yangu ni kuona Sekta ninazo simamia kuona zinapiga hatua kubwa tunahitaji kufanya Mapinduzi nakuona Maendeleo ya Sanaa ya Filamu nchini hivyo Serikali Ina dhamira pia ya kuhakikisha kazi za Sanaa zinafika mbali na zinakuwa zenye viwango na Mama Samia ameongeza takribani bilioni 1 na kufikia bilioni 2.5 katika Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa hivyo Wasanii wajitokeze kukopa Fedha hizo ." Hata hivyo Mchengerwa ameeleza kuwa Wasanii Wizara itahakikisha wanachapa kazi na hakuna kazi ya Sanaa itakayosimama Kwa kisingizio cha Fedha kwani Milango ipo wazi Kwa wadau wa Filamu kukopesheka Kwa Fedha hizo Ili kuona Kwa namna gani watayarishaji wanatengeneza kazi zenye viwango na Bora zenye kutambulisha Utamaduni wa Taifa la Tanzania. "Ule mkamwo wa kusitasita kutengeneza Filamu zenye uhalisia Sasa basi tayari Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa una shilingi Bilioni 2.5 ni Fedha Kwa ajili ya kazi za Sanaa ambapo Mtayarishaji atakopeshwa Fedha hizo bila malipo ya riba hivyo tunategemea kazi za Sanaa nzuri zitazalishwa Kwa wingi na zenye ubora Ili kufikia Masoko ya nje." Aidha, Mchengerwa ameeleza dhamira nyingine ya wizara yake kuweka Mkakati wa wizara kuwa na televisheni na radio Ili kuweza kuonyesha kazi za Sanaa Kwa masaa 24 na kuwapa fursa Wasanii wanaochipukia kuonekana Pamoja Mkakati wa wizara kuwa na Vyombo vya kisasa vya kuandaa Filamu ambavyo vitakuwa vikikodishwa . Pamoja na hayo Waziri Mchengerwa amewaomba Wasanii kuonyesha ushirikiano na wizara husika na kuahidi kushikamana na wasanii bega Kwa bega na Wasanii kuhakikisha kazi zinajitangaza na kuwaleta watu wenye Mchango katika Sekta ya Filamu kidunia Ili kusaidia kiwanda cha Filamu nchini kinakua na wigo mpana . Mchengerwa ameongeza kuwa Wizara Ina Mkakati wa kujenga nyumba Kwa Wasanii zenye hadhi kwani Serikali inatambua Mchango wa Sanaa nchini katika kutangaza Utamaduni. Kwa upande wake Katibu Mkuu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Dkt.Kiagho Kilonzo amebainisha changamoto na Mafanikio mbalimbali yaliyopatikana kupitia vikao vilivo fanyika Kwa kushirikisha viongozi,Wasanii na wadau wa Filamu na vyama vya Wasanii. "Katika Mafanikio yaliyopatikana kupitia Serikali ya Jamhuri wa Tanzania Kwa kushirikiana na bodi ya Filamu nchini tuliweza kushirikisha vyama vya Wasanii , Wasanii na wadau na tukagundua vitu mbalimbali ikiwemo swala la kupatiwa Tuzo kama kielelezo Cha kutambua Mchango wa kazi za Sanaa na 2021 tuliweza kufanikiwa kuwepo Kwa Tuzo za Sanaa". Aidha Dkt.Kilonzo ameongeza kuwa mbali na kuwepo Kwa Tuzo kulihitajika Mitaji Kwa ajili ya kuongeza ubora wa kazi zao pamoja na changamoto ya Kodi na tozo Kwa Filamu. Pia amebainisha baadhi ya Mafanikio yaliyopatikana ikiwemo Filamu mbili "Vuta nikuvute" na Filamu ya "Binti" kushinda Tuzo pamoja na Kuonyeshwa katika Mtandao wa Kimataifa wa kuonyesha Filamu Netflix.
Share:

MATUKIO KATIKA PICHA - KAMPENI YA ELIMU KWA MLIPAKODI MLANGO KWA MLANGO SIRARI - MARA


Kaimu Meneja Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mara Bw. Robert Busumabu akichangia hoja wakati wa semina kuhusu taratibu za forodha zinazotumika kuwahudumia wafanyabiashara wa kati na wadogo wanaotumia Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Semina hiyo imefanyika kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.

Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Edwin Iwato akitoa elimu ya taratibu za forodha zinazotumika kuwahudumia wafanyabiashara wa kati na wadogo wanaotumia Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Elimu hiyo imetolewa kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.

Afisa Msimamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Lameck Ndinda akitoa mafunzo ya huduma bora kwa wateja kwa watumishi wanaofanya kazi katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Mafunzo hayo yametolewa kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.

Afisa Uhusiano kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi Salome Mwandalanga akimsikiliza kwa makini mfanyabiashara wa Sirari Bw. Joseph Mokare wakati wa kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea katika Wilaya ya Tarime mkoani Mara.

Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Abdallah Seif akitoa elimu ya kodi kwa mfanyabiashara wa Sirari Bw. Jumanne Omari wakati wa kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea katika Wilaya ya Tarime mkoani Mara. (PICHA ZOTE NA TRA).
Share:

KIKWETE KUZINDUA KITABU CHA MAISHA YAKE



Rais mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kuzindua kitabu cha maisha yake alichokiita kwa kimombo “From a barefoot student to President” tafsiri yake kwa Lugha ni Kiswahili ni “Kutoka Mwanafunzi Aliyetembea Peku Hadi Kuwa Rais.”

Kitabu hicho kinachosubiriwa kwa hamu ni muendelezo wa utamaduni mzuri wa marais wastaafu wa Tanzania kuandika vitabu vya kumbukumbu ya maisha yao ya kawaida na uongozi.
Share:

ZAIDI YA WANAFUNZI 2,000 WAFIKIWA NA KAMPENI YA "MKINGE MWANAFUNZI NA AJALI ZA BARABARANI"

Meneja Miradi wa PESACO Bw.Abel Swai akitoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Al-haramain iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, Elimu hiyo ni mwendelezo wa Kampeni ya Mkinge Mwanafunzi Dhidi ya Ajali za Barabarani. Mwenyekiti wa PESACO Bw.Mfaume Hassani akitoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Al-haramain iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, Elimu hiyo ni mwendelezo wa Kampeni ya Mkinge Mwanafunzi Dhidi ya Ajali za Barabarani. Katibu wa PASACO Bw.Fransisco Peter akitoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Al-haramain iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, Elimu hiyo ni mwendelezo wa Kampeni ya Mkinge Mwanafunzi Dhidi ya Ajali za Barabarani. Wanafunzi wa shule ya Sekondari Al-haramain iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, wakiwasikiliza wataalamu kutoka Taasisi ya PESACO wakitoa elimu ya Usalama barabarani ambapo ni mwendelezo wa Kampeni ya Mkinge Mwanafunzi Dhidi ya Ajali za Barabarani.

*****************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Shirika lisilo la Kiserikali linalojihusisha na utoaji elimu ya Usalama barabarani (PESACO) limeendelea na kampeni yake ya "Mkinge Mwanafunzi Dhidi ya Ajali za Barabarani" kwa kutoa elimu ya usalama barabarani katika shule za Msingi na Sekondari nchini.

Akizungumza katika zoezi hilo lililofanyika katika shule ya Sekondari Al-haramain iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa PESACO Bw.Mfaume Hassani amesema ajali za barabarani zimezidi kua miongoni mwa vyanzo vikubwa vinavyo chukua uhai wa watu wengi na kusababisha majeraha na ulemavu kwa maelfu ya watu.

Amesema Umoja wa mataifa na shirika la afya duniani wanakadiria kuwa watu zaidi ya milioni 1.3 hupoteza maisha kila mwaka, idaidi hii ikiwa ni mara mbili ya vifo vinavyosababishwa na Malaria na UKIMWI. Vifo vingi na majeraha hutokea zaidi katika nchi za uchumi wa kati na zinazoendelea kama Tanzania.

"Ili kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani PESACO imejizatiti kuunga mkono jitihada za serikali na vyombo vyake katika kuhakikisha tunafikia Tanzania isio na ajali. Tukitumia nyenzo ya elimu PESACO inayafikia makundi yote sita ya watumia barabara, kuwapa elimu stahiki itakayowasaidia kudumisha uwiano wa matumizi salama ya barabara ili kuepukana na ajali". Amesema Bw.Hassani.

Pamoja na hayo Bw.Hassani amesema zoezi hilo ni endelevu kwani mpaka sasa wameshawafikia wanafunzi zaidi ya elfu mbili (2,000) ambapo kwa hakika elimu walioitoa itasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani.

Share:

WAZIRI BASHUNGWA APENDEZWA NA CWT KINAVYOCHOCHEA UBORA WA ELIMU NCHINI, ASIFU MPANGO WA ELIMU BURE

Na Dotto Kwilasa Malunde 1 blog-DODOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)imesema imepeleka jumla ya shilingi trilioni 1.43, kwa ajili ya kugharamia Mpango wa elimu msingi bila Malipo ulioanza kutekelezwa 2015 na kuleta fursa ya upatikanaji wa elimu kwa kuongeza uandikishaji wa wanafunzi, kutokana na kuondolewa kwa vikwazo. 

Hayo yameelezwa na Waziri wa TAMISEMI Innocent Bashungwa Februari 11,2022 jijini hapa katika hafla ya  utoaji tuzo  za ubora wa taaluma kwa walimu,wanafunzi , Shule, Halmashauri na mikoa yote  iliyofanya vizuri kwenye matokeo  ya mitihani ya Mwaka 2021 ya kumaliza elimu ya msingi, kidato cha nne na kidato cha sita.

Amesema katika mwaka 2016, jumla ya wanafunzi 2,670,125 waliandikishwa, kati ya hao wanafunzi 917,137 wa elimu ya awali, 1,386,592 wa darasa la kwanza na wanafunzi 366,396 wa kidato cha kwanza.

Waziri Bashungwa ameeleza mwaka 2022, jumla ya wanafunzi 3,046,919 wameandikishwa, kati ya hao wanafunzi 1,123,800 ni wa Elimu ya Awali sawa na asilimia 82, wakiwemo wenye mahitaji maalum 2,352, wanafunzi 1,454,544 ni wa darasa la kwanza sawa asilimia 91, huku wanafunzi 664,698 wakiwemo wenye mahitaji maalum ni 2,747.

"Wanafunzi 664,698 wa kidato cha kwanza wameripoti shuleni, sawa na asilimia 73.2 ya wanafunzi waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza Mwaka 2022, wakiwemo wanafunzi 679 wenye mahitaji maalum,"amesema.

Amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na walimu nchini katika kuboresha taaluma, hivyo ni dhamira ya Serikali kuendelea na ujenzi wa nyumba za walimu kulingana na bajeti.

"Serikali ya awamu ya Sita imeendelea kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji katika Shule za Msingi na Sekondari Nchini,kwa Mwaka 2021 ufaulu katika mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi umefikia asilimia 81.97, mtihani wa kumaliza kidato cha nne umefikia asilimia 87.30 na kidato cha sita asilimia 99.62.

“Ninawapongeza walimu kupitia CWT kwa kuongeza na kuimarisha ufaulu,hata hivyo nina wahimiza kuongeza usimamizi wa shughuli za Elimu na kuondoa changamoto zinazosababisha baadhi ya shule kutofanya vizuri”amesisitiza Waziri huyo.

Katika kuimarisha utendaji kazi, Bashungwa ameeleza kuwa mipango madhubuti imewekwa ili kuhakikisha walimu, wakuu wa shule, Maafisa Elimu wa Kata, Wilaya na Mikoa wanaendelea kupata mafunzo mbalimbali ya kuwajengea uwezo katika ufundishaji na usimamizi wa Sekta ya Elimu.

Amefafanua kuwa katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya walimu 1,817 wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum ya ujifunzaji, wamejengewa uwezo wa kutumia mbinu za kufundishia na kujifunzia. 

Vilevile walimu Wakuu 8,096 walipata mafunzo juu ya matumizi ya Kiunzi cha Uthibiti Ubora wa Shule ili kuhakikisha Uthibiti wa Ubora wa Shule unakuwa na matokeo mazuri, kuanzia katika ngazi ya Shule na kwamba mafunzo kama hayo yataendelea kutolewa kila mwaka ili kutimiza lengo la kumarisha utendaji kazi.

Pamoja na hayo amezielekeza Taasisi za elimu nchini kuhakikisha wanafuata sheria, miongozo na taratibu katika usimamizi wa sekta ya Elimu ili kufikia malengo ya Serikali ikiwa ni pamoja na kusimamia vizuri miradi yote, inayotekelezwa katika maeneo yao, ili kuwa na miradi yenye viwango vinavyoendana  na thamani ya fedha.

Vile vile amesema Serikali itaendelea kutoa Elimumsingi bila malipo, kuboresha miundombinu, na kusambaza vifaa vya kufundishia na kujifunzia.

Kwa upande wake Katibu mkuu wa Chama Cha Walimu  Tanzanaia (CWT )Mwalimu  Deus Seif amesema Chama hicho kinatambua  jitihada  kubwa zinazofanywa na walimu nchini katika kuhakikisha wanafunzi wanapata ufaulu mzuri.

Kutokana na hayo Katibu huyo kupitia CWT ameahidi kushirikiana na Serikali kuendelea kutatua kero zinazowakabili walimu ili kuwapa ari ya kufanya kazi katika mazingira mazuri.

“Tunatambua Serikali inaendelea kutujali kupitia upandishwaji wa madaraja na  urekebishwaji wa mishahara kwa walimu, pamoja na malimbikizo ya madeni  yasiyo ya mishahara,hivyo na sisi Kwa nafasi yetu tutaendelea kushirikiana Katika kutatua kero nyingine ”amesema Mwl Seif.

Amezitaja changamoto za walimu nchini  kuwa ni uhaba  wa nyumba za walimu, madai mbalimbali  ya walimu  bado yapo katika halmashauri  pamoja na ajira  kwa walimu huku akiwatoa hofu kuwa madai yote hayo Serikali kwa kushirikiana na CWT yatapatiwa ufumbuzi.

Naye  Kaimu rais wa CWT, Dina Mathamani amesema wao kama walimu wanaipongeza Serikali kwa kuona  umuhimu wa kutoa tuzo na pongezi kwa walimu waliofanya vizuri na kuwafanikisha wanafunzi kufaulu vizuri.

“Ni jambo jema ambalo kila mtu angependa lifanyike,kupitia motisha hii ufaulu unaendelea kupanda siku hadi siku taaluma inapanda na mazingira ya walimu yataendelea kuboreshwa zaidi na kusaidia kila mtu kusimama kwenye nafasi yake,

Kwa niaba ya Chama hiki,naahidi  tutafanya kazi usiku na mchana ,kwa weledi mkubwa  ili kuhakikisha ufaulu wa watoto wetu wapendwa unaongezeka,kupitia hili tutapata wataalamu wabobezi na wajuzi na hatimaye kuwa juu kiuchumi,"amesema.



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 12, 2022


Magazetini leo Jumamosi February 12 2022







Share:

Friday, 11 February 2022

SABABU KIFO CHA MWELE MALECELA


BAADA ya kusambaa kwa taarifa za kusikitisha kuhusu aliyekuwa Mkurugenzi wa Udhibiti w a Magonjwa Yasiyopewa Kipaumbele, Dk. Mwele Ntuli Malecela kufariki dunia, jana Alhamisi, Februari 10, 2022, Geneva mchini Uswisi, familia ya marehemu imetaja chanzo cha kifo hicho.

Kaka wa Marehemu William Malecela maarufu kama Lemutuz amesema kifo cha dada yake kimesababishwa na kansa.

“Ni kweli amefariki leo Hospitalini Geneva, Switzerland alikua anasumbuliwa na Kansa, msiba utakuwa Dodoma,” amesema Lemutuz.

Mwele Ntuli Malecela alizaliwa tarehe 26 Machi 1963, alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Tafiti za Kiafya Tanzania (NIMRI). Aliwania nafasi ya mgombea wa uraisi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.



Kuanzia Aprili 2017 Mwele Malecela alikua akifanya kazi na Shirika la Afya Duniani (WHO) ambapo alikua Mkurugenzi wa Udhibiti w a Magonjwa Yasiyopewa Kipaumbele.



Mwele Ntuli Malecela alizaliwa tarehe 26 Machi 1963, alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Tafiti za kiafya Tanzania (NIMRI). Aliwania nafasi ya mgombea wa uraisi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Kuanzia Aprili 2017 Mwele Malecela alikua akifanya kazi na Shirika la Afya Duniani (WHO) ambapo alikua Mkurugenzi wa Udhibiti w a Magonjwa Yasiyopewa Kipaumbele.
Share:

NABII Dkt. JOSHUA AITISHA MAOMBI YA SIKU 121 KUMUOMBEA RAIS SAMIA, KUTOKOMEZA MAUAJI


Kiongozi Mkuu wa Huduma ya Sauti ya Uponyaji Tanzania, Nabii Dkt.Joshua Aram Mwantyala

NA GODFREY NNKO

KIONGOZI Mkuu wa Huduma ya Sauti ya Uponyaji Tanzania, Nabii Dkt.Joshua Aram Mwantyala ameitisha maombi ya siku 121 kwa ajili ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na kutokomeza roho ya mauaji ambayo imekuwa ikishamiri kwa kasi nchini.

Nabii Dkt.Joshua ameyasema hayo leo Februari 11, 2022 makao makuu ya Huduma ya Sauti ya Uponyaji Tanzania yaliyopo Yespa, Kihonda mjini Morogoro wakati akitoa taarifa rasmi ya ujumbe ambao amepewa na Mungu katika Taifa letu kuhusu mauaji ambayo yanaendelea kwenye Taifa letu tangu Januari hadi Februari, 2022.


"Huu ni ujumbe ambao Mungu amenipa kwa ajili ya kuliponya Taifa letu na kuliokoa dhidi ya mauaji ambayo yametikisa nchini, na yamekuja kwa tabia ambayo haijazoeleka katika jamii na nchi yetu, Mungu amenionesha kwamba, katika ulimwengu wa roho, ibilisi tayari ameweka ajenda yake ndani ya nchi yetu.

"Na anapelekea kusambaza roho ya mauaji ambayo baadaye itakuja kuingia katika ajenda za kisiasa. Lakini asili yake itaanzia kwenye makundi fulani ya kijamii. Kuna kabila kubwa katika nchi yetu, ambalo mimi ninasema ni kundi fulani katika la kijamii, litapandikiziwa roho ya chuki binafsi dhidi ya Rais wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na wanasiasa watakapogundua hicho kitu watatumia hiyo nafasi kujenga chuki dhidi ya Serikali kwa ajili ya Uchaguzi wa mwaka 2025.

"Kwa hiyo, hiyo roho itasambaa, watu wataanza kulipa visasi na kuleta vurugu itakayosababisha mauaji makubwa sana 2025 ili kutia dosari katika uongozi wa Mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan. Hii inawezekana, kwa sababu Biblia inasema kisha shetani akamuingia Yuda, halafu Yuda akapata tamaa ya kumsaliti Yesu ili auawe,"amesema.

Nabii Dkt. Joshua amesema kuwa,Yuda hakuwa hivyo asili yake, lakini shetani alimuingia,halafu alivyomuingia Mafarisayo waliokuwa wanamchukia Bwana Yesu,wakamtumia Yuda kumsaliti, akasaliti ili wampate kwa sababu wasingempata bila msaliti wake.

"Kwa hiyo katika ulimwengu wa roho hii nguvu itaendelea na watatokea watu ambao wanaaminiwa zaidi na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, watamsaliti.

"Kwa hiyo mifumo ya kiusalama na siasa za nchi zitavurugika kwa wakati huo na watu wabaya watatumiwa sana na ibilisi, kwa sababu ibilisi sasa hivi anatafuta watu wa kuwaingia ambao wana ushawishi katika nchi. Ikishaingia hiyo roho, itajenga sasa mpasuko ambao utatengeneza chuki, vikundi vya uhalifu vitaungwa mkono kufanya mauaji makubwa kwa ajili ya kuua ndoto za Mheshimiwa Rais Samia,"amesema.

Kwa mujibu wa Biliblia takatifu kitabu cha Mathayo 26:14-27:38, Nabii Dkt.Joshua alinukuu maandiko akionesha namna amabvyo Yuda alikubali kumsaliti Yesu.

"Kisha mmojawapo wa wale wanafunzi kumi na wawili aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa kuhani mkuu akamwambia. Mtanilipa kiasi gani nikimtoa kwenu? Wakamlipa vipande thelathini vya fedha. Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.

"Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate isiotiwa chachu wale wanafunzi walikuja kwa Yesu wakamwuliza? Ungependa tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?. Akajibu, nendeni kwa mtu fulani huko mjini mkamwambie, Bwana anasema hivi, saa yangu imekaribia, napenda kula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu nyumbani kwako.’

"Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaambia, wakaandaa Pasaka. Ilipofika jioni, Yesu aliketi mezani pamoja na wanafunzi wake. Walipokuwa wakila akawaambia. Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.Wakasikitika sana, wakaanza kumuuliza mmoja mmoja. Ni mimi, Bwana? Yesu akawaambia, yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami, ndiye atakayenisaliti.

"Mimi Mwana wa Adamu sina budi kufa kama ilivyoandikwa katika maandiko, lakini ole wake mtu yule atakayenisaliti. Ingalikuwa nafuu kwake kama hakuzaliwa. Kisha Yuda, yule ambaye alimsaliti akasema, “Ni mimi, Bwana? Yesu akamjibu,umetamka mwenyewe. Bwana? Yesu akamjibu, umetamka mwenyewe.

"Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, chukueni mle, huu ni mwili wangu.Kisha akachukua kikombe, akashukuru, akawapa akisema. Kunyweni nyote katika kikombe hiki. Hii ni damu yangu ya agano ambayo inamwagika kwa ajili ya wengi ili wasamehewe dhambi.

"Ninawahakikishia kuwa sitakunywa tena maji ya mzabibu mpaka siku nitakapoyanywa pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu. Walipokwisha kuimba wimbo walikwenda kwenye mlima wa Mizeituni. Kisha Yesu akawaambia, Usiku wa leo kila mmoja wenu atanikimbia kwa maana maandiko yanasema, nitampiga mchungaji, na kondoo wote wa kundi lake watatawanyika.Lakini baada ya kufufuka, nitawatangulia kwenda Galilaya.

"Petro akasema, hata kama wote watakuacha, mimi sitaku acha. Yesu akamjibu,ninakuambia kweli, usiku huu huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu. Lakini Petro akasema,hata kama itabidi nife pamoja na wewe, sitakukana. Na wana funzi wote wakasema hivyo hivyo.

"Kisha Yesu akaenda nao mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane. Akawaambia, kaeni hapa, mimi ninakwenda mbele zaidi kuomba.Akamchukua Petro, pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kufadhaika na kuhuzunika.Kisha Yesu akawaambia,moyo wangu umejaa majonzi karibu ya kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami,"amefafanua Nabii Dkt. Joshua kwa kunukuu maandiko matakatifu.


Pongezi

Aidha,Nabii Dkt.Joshua amempongeza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mhadisi Hamad Masauni kwa kazi nzuri ambayo anafanya, ingawa amesema juhudi zake zinatatizwa kwa kukosa watu sahihi.

"Ni kweli vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinafanya kazi kubwa sana. Hasa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (Mhandisi Hamad Masauni) tumemuona anawajibika sana,na kwa kweli Mungu ambariki na Mungu ambariki Mama kwa kuona kuwa anaweza kumsaidia.

"Lakini amekosa watu sahihi, wa kumtia moyo na kumuunga mkono katika kazi anayoifanya. Jukumu letu sasa, mimi kama Nabii, Mungu ameniambia kuwa, nichukue hatua ya kulitahadharisha Taifa, kwanza viongozi wenye dhamana waanze kumtafuta Mungu kila mtu binafsi kwenye dhamiri yake, kwa sababu mamlaka hizi zinawekwa na Mungu,"ameongeza Nabii Dkt.Joshua.

Amefafanua kuwa, "Daudi alipoona hali mbaya ya Kitaifa alimlilia Mungu na Mungu alilipona nchi yake, kwa hiyo rai yangu ya kwanza ni viongozi wenye mamlaka kumlilia Mungu kwa sababu ni na hakika ni wazalendo. Na kazi kubwa ambayo mama yetu anafanya ni tishio kubwa kwa watu wengi ambao wana uchu wa madaraka.

"Kwa hiyo, sisi watumishi wa Mungu tutasimama, mimi binafsi na kanisa langu tumeitisha maombi ya siku 121 kwa ajili ya kutokomeza hii roho ili isistawi kwenye Taifa kiasi cha kuwafikia watu wabaya na kuwaletea maslahi maovu kwenye Taifa letu.

"Tunayo maombi ya siku 121 kwa ajili ya kumuinua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ili Mungu ampiganie na kuweza kumpa nguvu na kuweza kutimiza majukumu yake, halafu pili Mungu aweze kumuondolea watu ambao si sahihi wanaomzunguka ambao wanasubiri siku moja wamsaliti. Na maombi yetu nina hakika kuwa yatafanikiwa.

"Lakini ni muhimu wajibu huu uwafikie viongozi wenye dhamana ya Taifa letu, kumtafuta Mungu kwa sababu nchi yetu imejengwa katika msingi wa bila dini, lakini katika hofu ya Mungu,"amesema Nabii Dkt. Joshua.
Share:

NYUKI NUSURA WAWAUWE MATAPELI WALIONIPORA SHAMBA LANGU

Nilinunua shamba kwa matapeli Kenya kule Kitemgela. Nililipa kiasi kikubwa mno cha hela nikijua nitaanza kujenga hivi nyumba yangu hivi karibuni kumbe walikuwa wamenipangia. 


Mimi natoka Tanzania lakini mke wangu ni wa Mkenya kutoka Ukambani na alipenda tuishi kule Kenya alikozoea. Nilikubali nikamfuata kisha tukaanza kutafuta kipande cha ardhi tulichopata pale Kitengela.

 Nilikuwa na pesa nyingi za mkopo wa benki kama milioni sita unusu. Nililipa milioni mbili nikamaliza nikaanza kuweka ua kando ya ardhi hiyo. Nilipomaliza kuzingira shamba lile, fujo ikaanza na nikafurushwa bila kurejeshewa chochote. 

Maisha yangu yakagonga mwaba karibu nijitie kitanzi. Bibi Yangu alinitia moyo akaniambia nisijali. Sikumsikiza hata nikafikiria yeye ni mmoja wao walinipangia. Asubuhi Ijumaa iliyofuata, bibi yangu alinisihi tuende tutemebee mahali. Sikufahamu ni wapi alitaka kunipeleka lakini vile alivyokuwa akiiongea alitaka mno nisiikose.

 Nilifunga safari naye hadi kwa Daktari mmoja wa miti shamba anayeitwa Kiwanga. Alimsimulia yote yaliyojiri kwa maisha yetu kule Kitemgela. Daktari alicheka na akatuonyesha kioo na pisha ya majangili wale wote.


 Tulimuambia ni hao kabisa! Ilikuwa mshangao. Kachakea na kutuambi kwa muda wa takribani saa mbili hivi shamba letu la Kitengela litakuwa limerudi. Tulitoka kuruidi makwetu huku nikifikia hiyo ni utapeli tu bibi yangu ameamua kunimaliza kabisa sababu mimi ni Mtanzania. Sikutaka kumuuliza maswali sababu yalikwua yashaa fanyika. 

Ningefanya jambo mbaya hivyo nikazuia kabisa sababu ya sheria. Tulipofika nyumbani, jioni hiyo, simu ikapigwa. Aliyekuwa amepiga simu hiyo alikuwa analia kuwa nyuki zimemvamia zinamuua.

 Alinisihi niende haraka anipatie pesa zangu hataki kifo cha mapema. Nikamuuliza pesa zipi akaniambia za shamba la Kitengela. Nikamtumia account number azipeleke benki.

 Kwa kweli aliweka pesa zote takribani milioni mbili walizokuwa wamenitapeli. Kiwanga Doctors ni matata kweli. Nina furaha sana. Pia Kiwanga wanashughulikia shida kama uwezo wa kurudishisha mpenzi aliyekuwacha, Nyota ya biashara, kupata cheo kazini na kupata kazi kwa haraka. 

Wasiliana na Kiwanga Doctors kwa nambari +254 769404965 kwa WhatsApp ipo pia au tembelea Website yao: www.kiwangadoctors.com Unaweza kuandika barua pepe yaani Email kwa: kiwangadoctors @gmail.com.

Share:

Video Mpyaaa!!! NTEMI OMABALA - MAJUNGU


Hii hapa ngoma mpya ya Msanii Ntemi Omabala inaitwa Majungu..




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger