Friday, 23 July 2021

Mfanyabiashara Tabora Atiwa Mbaroni Kwa Kukutwa Akiuza Vifaa Tiba na Dawa Ambazo ni Mali ya Serikali


Na Lucas Raphael,Tabora  -TDMA
Mamlaka ya dawa na vifaa tiba kanda ya magharibi imefanikiwa kumkamata mfanyabiashara Zakayo Bagomwa aneyemiliki Duka la Dawa  muhumu ilinaloitwa Maliza na Yesu  akiuuza dawa za kifua kikuu TB ,kadi za kliniki za Kina mama Wajawazito, kutoa huduma za matibabu ndani ya duka , vifaa tiba mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kenya vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 4,869,900.

Akizugumza na waandishi wa habari leo Kaimu meneja wa Mamlaka ya hiyo kanda ya magharibi Christopher Migoha alisema kwamba tukio hilo litokea julai 20 mwaka huu mara baada ukaguzi maalumu wa duka la dawa katika Kijiji cha Kanindo, Kata ya Kanindo, Tarafa ya Ulyankulu, Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Mkoa wa Tabora.

Alisema kwamba katika duka hilo  walikuta  Dawa za Serikali ya Tanzania zikiwa zimetunzwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kuuzwa kinyume cha Kifungu cha 312(1) cha Kanuni ya Adhabu Sura 16.

Alisema kuwa walikuta Vitendanishi vya kupima UKIMWI pamoja na Vitendanishi vya kupima Malaria ambavyo ni Mali ya Serikali ya Tanzania vikiwa vimehifadhiwa na kutunzwa kwa ajili ya kuuzwa kinyume cha Sheria.

Aidha kaimu meneja huyo alisema kwamba kwenye duka hilo kulikuwa na  Dawa zisizosajiliwa kutumika nchini zikiwa zimehifadhiwa na kuuzwa kinyume cha Sheria 

Migoha aliendelea kusema kwamba ndani duka  walikuta dawa mali ya Serikali ya Kenya zikiwa zimetunzwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kuuzwa  .

Alisema kwamba ndani ya duka hilo walikuta dawa zisizoruhusiwa kuuzwa katika maduka ya dawa muhimu na kukuta  dawa zikiwa zimetunzwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kuuzwa kinyume cha kanuni ya 63 ya Makundi ya Dawa ya Mwaka 2015.

Hata hivyo meneja huyo wa kanda ya magharibu alisema kwamba walikuta  dawa zilizokwisha muda wake wa matumizi zikiwa zimetunzwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kuuzwa kinyume cha Kifungu cha 75(1) cha Sheria ya Dawa na Vifaa Tiba Sura 219.

Alisema kwamba mmiliki hyo hakuweza kuwasilisha risiti za manunuzi wala mauzo ya dawa zote alizokutwa nazo kinyume cha  Kanuni za Uendeshaji wa Biashara ya Dawa za Binadamu.

Migoha aliendelea kusema kwamba kulikutwa Vifaa Tiba ambavyo ni Seti ya  kufanyia tohara vikiwa vimetunzwa kinyume cha Sheria pamoja na dawa za wangojwa wa kifuu kikuu ambazo hazikustahili kuwepo ndani ya duka hilo wala kuunzwa kwenye maduka ya dawa muhimu.

Aidha aliwataka wadau  wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA) na  Wafanyabiashara wote wa bidhaa za Dawa, Vifaa tiba na Vitendanishi kufanya biashara zao kwa kuzingatia Sheria ya Dawa na Vifaa tiba Sura 219 pamoja na Sheria zingine    .


Share:

Wakulima 99,468 Bariadi kunufaika na mfumo mpya wa kilimo cha pamba


Samirah Yusuph.
Bariadi. Bodi ya pamba Tanzania (TCB)  imewafikia wakulima 99,468 waliopo wilaya ya Bariadi katika kampeni ya kitaifa ya kuongeza tija ya kilimo cha pamba nchini .

Kampeni hiyo iliyozinduliwa wilayani hapo juma lililopita ikilenga kuwawezesha wakulima kupata uelewa wa vipimo sahihi na vyenye tija katika maandalizi ya kilimo cha pamba pamoja na upandaji wa mbegu.

Akizungumza na watendaji wa vijiji,kata, maafisa kilimo na ugani pamoja na wakuu wa idara katika wilaya ya Bariadi baada ya kukamilisha mafunzo barozi wa kilimo cha pamba nchini Agrey Mwanri amesisitiza kuendelea kutoa mafunzo ya mfumo bora wa kilimo cha pamba kwa wakati ili msimu wa kilimo unapo anza kila mkulima awe na uelewa wa kutosha.

Mwanri amesema kuwa ili kila mkulima tumie mfumo wa kisasa wa sentimita 60 kwa 30 ni lazima viongozi wote katika wilaya washiriki kikamilifu katika kutoa elimu kwa kuonyesha tija iliyopo iwapo mkulima atatumia mfumo huu wa vipimo pamoja na manufaa yake katika uzalishaji.

"Shirikiana na mkulima tangu hatua za awali muelimishe namna ya kuweka mbolea msimamie hadi mavuno na yeye akiwa anaona shamba lako la lake yote yapo sawa sio unaenda kumpangia masharti tayari anakaribia mavuno, tuanze nao tangu mwanzo".

Ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha mkulima anajikwamua kiuchumi na kuona thamani ya kilimo, hivyo kwa watendaji watakaokuwa wazembe na kufanya kinyume itakuwa ni ukaidi wa sera ya kitaifa katika kilimo.

Kwa upande wake Renatus Luneja Mkaguzi wa kutoka bodi ya  Pamba alieleza kuwa pamoja na kuhamasisha matumizi ya samadi na mbolea za viwandani pia viongozi wananwajibu wa kuhakikisha wakulima wote wanakuwa katika vyama vya ushirika.
 

"Ni rahisi kuwafikia wakulima wanapokuwa Katika vyama vya ushirika hamasisheni wajiunge katika ushirika huku mkiendelea kuwapa elimu ili tija ya kilimo ionekane".
 
Kampeni ya kuongeza tija ya kilimo cha pamba nchini imelenga kuwafikia wakulima zaidi ya laki tano katika mkoa wa Simiyu ambapo hadi sasa zaidi ya wakulima laki moja wa wilaya ya Busega na Bariadi tayari wamefikiwa.



Share:

KUTANA NA FAMILIA YA AJABU YA WATU 9, WOTE WAMEZALIWA TAREHE MOJA



Mwalimu mmoja nchini Pakistan kwa jina Amir Ali, amevunja rekodi ya dunia kwa kuwa na familia yenye watu wengi waliozaliwa katika tarehe moja –ya Agost mosi baada ya watu tisa wa familia moja kuzaliwa tarehe hiyo.

Rekodi ya awali ilikuwa imeshikiliwa na familia kutoka Caymans kwa miaka tisa ambapo watoto watano walikuwa wamezaliwa tarehe 5 mwezi Februari lakini miaka tofauti.

Amir, mkazi wa Larakana , alisema alizaliwa tarehe 1 mwezi Agosti ,Mke wake alizaliwa tarehe moja mwezi Agosti , Binti yake wa kwanza Sindh alizaliwa mwanawe wa kiume wa pili Amber na wanae pacha Ammar na Ahmar, wote walizaliwa tarehe 1 Agosti.

Amir Ali anaamini katika elimu ya nyota- nyota yake ni Asad au Zmarai na inaelezwa kuwa namba ya kwanza ya bahati, wakati alipoanza kazi tarehe 1 mwezi Agosti na kuoa tarehe 1 mwezi Agosti.

Amir anasema familia yake yote inasheherekea siku ya kuzaliwa kwao siku moja. Bw. Amir pia anaamini katika unajimu na kuandika ushairi. Ana shahada ya uzamili kwenye masomo kadhaa, ikiwemo sayansi ya jamii, mahusiano ya kimataifa na uchumi.

Tarehe 1 mwezi Agosti, familia yote husheherekea kwa pamoja, Bw. Amiri anasema. Anaongeza kuwa watoto wote wamezaliwa nyumbani kisha wakasajiliwa na mamlaka za manispaa. Aliongeza kuwa kwa ushauri wa rafiki yake, alituma maombi ya usajili kwa ajili ya kuwekwa rekodi kwenye Guiness Book of World Records.
Share:

TRENI YENYE KASI ZAIDI DUNIANI YAZINDULIWA




Treni yenye uwezo wa kusafiri kwa kasi ya kilomita 600 kwa saa imezinduliwa katika eneo la Qingdao nchini China. Treni hiyo ya mfumo wa Magliev iliotengenezwa na shirika la reli nchini China ndiyo treni yenye kasi zaidi duniani CRRC kwa sasa.

‘’Magliev ni neno kwa ufupi lenye maana ya Magnetic Levitation’’. Treni hiyo inaonekana kuelea angani kutokana na nguvu za umeme zinazoifanya kuonekana kuwa juu ya barabara ya reli.
Liang Jianying, naibu meneja na muhandisi mkuu wa shirika la CRRC Sifang, aliambia vyombo vya habari nchini humo kwamba mbali na kasi yake , treni hiyo haina kelele na inahitaji uangalizi mdogo ikilinganishwa na treni zengine zenye kasi ya juu. Mfano wa treni kama hiyo ulifichuliwa kwa vyombo vya habari mwaka 2019.

Mwaka huohuo, China ilitangaza mipango yake ya kuanzisha uchukuzi wa saa 3 katika katika miji yake mikuu. Reli yenye kasi ya juu nchini China ni kipaumbele , ikiwa na lengo la kuunganisha miji yake mikuu kwa treni ili kupunguza muda na gharama za usafiri ndani ya taifa hilo lenye idadi kubwa ya watu duniani.
Kwa sasa , wastani wa kasi ya treni nchini humo ni kilomita 350 kwa saa, huku ndege zikiendeshwa katika kasi ya kati ya kilomita 800 hadi 900 kwa saa. Treni kama hiyo iliozinduliwa Qingdao inaweza kujaza pengo muhimu lililopo katikati. Hatahivyo kuna kitu kimoja muhimu ambacho ni kizuizi katika ufanisi wake ukosefu wa reli za magliev ambazo hazijakamilishwa.

Kwa sasa China ina reli moja pekee ya mfumo wa Magliev inayotumika kibiashara, na inaunganisha uwanja wa ndege wa Pudong huko Shanghai na kituo cha barabarani cha Longyang mjini humo. Safari hiyo ya kilomita 30 huchukua takriban dakika saba na nusu huku treni hiyo ikisafiri kwa kasi ya kilomita 430 kwa saa moja.
Share:

CORONA YAUA WATU 29 TANZANIA, WAZIRI ASEMA "UGONJWA UPO NA WATU WANAKUFA..WATU WACHUKUE TAHADHARI"

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima amesema hadi sasa jumla ya watu 29 wamefariki dunia kutokana na wimbi la tatu la Covid-19 huku jana Julai 22,2021 pekee kulikuwa na jumla ya wagonjwa wapya 176.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 23,2021 Dkt. Dorothy amesema takwimu hizo ni alizopata jana hivyo upo uwezekano vifo zaidi vikawa vimetokea.

“Itoshe kuwaambia kuwa ugonjwa upo na watu wanakufa, tusingependa kupeana hizi taarifa za vifo tuchukue tahadhari, kila mmoja wetu ajiulize unapofanya mambo kinyume na kuchukua tahadhari unalenga kumtesa nani,” amesema Dkt. Gwajima.

Idadi hiyo inafikisha Tanzania kuwa na jumla ya wagonjwa 858 wa Covid-19.
Share:

SPIKA JOB NDUGAI : TOZO ZA MIAMALA YA SIMU NI HALALI, FEDHA ZITACHAGIZA MAENDELEO


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai

Na Dotto Kwilasa, Dodoma.

Baada ya mijadala mingi kuhusiana na tozo ya miamala ya simu hususani kwenye mitandao ya kijamii ,Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai ameibuka na kudai kuwa tozo hizo ni halali na kwamba fedha hizo zitachagiza masuala ya maendeleo ikiwemo huduma za kijamii kama vile shule,hospitali na maji.

Hatua hiyo imekuja kufuatia baadhi ya wananchi kulalamika kwamba kumekuwa na tozo kubwa katika miamala ya simu huku akipigilia msumari kwenye tozo hizo kwa kudai kuwa Bunge ndio limepitisha na kwamba wanaopinga wanatakiwa kutoa mawazo mbadala nini kifanyike huku akisisitiza lengo ni ifikapo 2025 Tanzania iwe Taifa tofauti katika suala la Maendeleo.

Akizungumza mapema leo Julai 23,2021,katika kikao kazi kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,Spika Ndugai amesema "Sisi kama Bunge tulikaa kwa pamoja na kujadiliana kisha tukaamua kuwa na tozo katika miamala ya simu kwa sababu fedha zitakakazopatikana zitaenda katika mfuko Maalum ambao utawasaidia wananchi,"amesema na kuongeza;


"Tumepitisha na tukatunga sheria , tunataka kuliona hilo,sasa wewe ambaye unapinga tupe njia mbadala tutapata wapi fedha, tunafikaje 2025, kwa hiyo maamuzi ni hayo tumeyafanya, kwa nia njema kabisa kwamba 2025 tuwe tumetoka, tuwe ni taifa la Tanzania ambalo ni tofaut,CCM hoyee,nimemaliza,"amesema Spika huyo.


Pamoja na hayo amezungumzia kuhusu maendeleo ya mkoa wa Dodoma na kuwataka watendaji wa mkoa wa huu kujitathimini katika utekelezaji wa majukumu yao kwani serikali imekuwa ikitimiza wajibu wake kwa kuleta fedha kwa wakati lakini tatizo lipo kwa watendaji.

"Naomba nitolee mfano kwa mkuu wa mkoa wa huu Antony Mtaka ,alimetoka Simuyu kule alifanya kazi nzuri, hivyo hapa akishindwa kufanya vizuri tujue kabisa tatizo lipo kwetu na sio kwake,tukishirikiana nae vizuri ataacha alama kubwa kwenye Mkoa wetu,"amesisitiza Ndugai.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka amebainisha vipaumbele vinne ambavyo atavisimamia katika mkoa wa Dodoma na kusema kuwa kama watafanikiwa, Jiji la Dodoma litakuwa la kiuchúmi zaidi.

Amevitaja vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na Elimu, migigoro ya Ardhi, kilimo na ufugaji venye tija na huduma bora za sekta za afya huku akitangaza alizeti kuwa zao la biashara katika mkoa huo.

Akizungumzia katika kikao hicho ametaja lengo la kikao hicho kuwa ni kuweka mikakati ya pamoja ili kwenda pamoja kama timu katika kutekeleza mambo yanayohusu maendeleo.

"Ukitaka kufanikiwa nenda na wenzako,nawasii tuwe na lugha ya pamoja yapo Mambo mazuri wenzetu wameyafanya hivyo lazima tuyaendeleze, sisi Dodoma tunautofauti tunabeba haiba ya makao makuu ya nchi hivyo ni lazima tuwe na matarajio makubwa,"amesema.

Licha ya hayo Mtaka amezungumzia kiwango cha elimu Mkoa wa Dodoma kuwa kipo katika hali mbaya, katika ngazi zote ikiwemo mitihani ya mock kwa mkoa haujafanya vizuri hivyo zinahitajika nguvu za ziada kuhakikisha mkoa unafanya vizuri katika sekta ya elimu na kuondokana na aibu iliyopo.

"Halmashauri zote nane za mkoa wa Dodoma mnatakiwa kuwa na ubunifu wa vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitatuingizia fedha za kutosha kuendesha miradi mbalimbali,na kuufanya Mkoa wetu kuwa wa mfano,"amesisitiza Mtaka.

Amesema Jiji la Dodoma limekusanya sh.bilioni 70 kutokana na mauzo ya viwanja sasa wapo kiwango cha sh.bilioni 30 hivyo lazima watafute vyanzo vipya vya mapato na anatamani kuona ubunifu katika suala hilo.

"Natamani kuona kila kaya zikipanda miti mingi kwa ajili ya Utunzaji wa mazingira pamoja na kuweka Mipango mizuri ya Utunzaji wa mazingira katika mkoa huu,"amesemà.

Mtaka pia amesisitiza kuwa "Lazima niseme ukweli kwamba ili tufanikiwe Katika yote haya tuukatae uchonganishi na unafki,Wapo Watumishi waongo na wachonganishi siwapendi, watu wanachonganisha watu, hasa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, tumekutanishwa na kazi tufanye kazi tuheshimiane kiongozi haongozwi,".

Akitilia mkazo suala hilo amesemà ikitikea watumishe waongo na wachonganishi wakiendelwa kumtumia meseji atawataja hadharani ili kuepusha maneno na vikwazo katika uongozi wake.
Share:

MTANGAZAJI MAARUFU JOSEPHINE CHARLES ASHEREHEKEA 'BIRTHDAY' YAKE

Leo Julai 23,2021 Mwandishi wa Habari na Mtangazaji maarufu wa Kituo cha Matangazo Radio Faraja Fm Stereo, Josephine Charles anasherehekea siku yake ya kuzaliwa. Malunde 1 blog inaungana na Wasikilizaji na wadau wa Josephine Charles akisherehekea miaka kadhaa tangu kuzaliwa kwake.

Happy Birthday Josephine Charles
Share:

Nafasi 23 za Kazi BRELA, Mwisho wa Kutuma ni Tarehe 6/08/2021


 BRELA  Wametangaza Nafasi 23 za Kazi( Transfer) kama ifuatavyo;

1.Senior Legal Officer- 

2.Legal Officer II

3.Procurement Officer II

4. Senior ICT Officer (ICT System security)

5. ICT Officer I (Database Administrator)

6.Licensing Officer II

7.Registration Officer II

8.Internal auditor II

9.Planning Officer II

10.Senior Records Officer

11.Executive Assistance II

12. Office Management Secretary II

13.Personal Secretary II

14.Records Management Assistance II

15. Senior Receptionist

16. Receptionist II

17. Driver II

18. Office Assistance II

 

==>>Kujua Zaidi Pamoja na Kutuma Maombi <<BOFYA HAPA>>

__________________



Share:

WAZIRI AKERWA NA MRUNDIKANO WA BODABODA VITUO VYA POLISI


Na Abubakari Akida,MOHA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo amesikitishwa na uwepo wa idadi kubwa ya bodaboda katika Vituo mbalimbali vya Polisi nchini huku akiwaasa wananchi ambao mashauri yao yanasikilizika wafike katika vituo hivyo ili kuondoa msongamano wa vyombo hivyo.

Ameyasema hayo leo Visiwani Zanzibar baada ya kupata maelezo na kutembelea karakana ya kuhifadhia vidhibiti hivyo katika Kituo cha Polisi Madema ambapo amesikitishwa na wingi wa bodaboda kituoni hapo.

“Nchi yetu inataka kupiga hatua za kmaendeleo na uchumi, kwa namna hii ya mrundikano wa bodaboda katika vituo vya polisi maana yake shughuli nyingi huko za vijana zimesimama, naelewa kuna vidhibiti kwa ajili ya kesi maalumu ambazo nyingine ziko mahakamani hivyo haviwezi kuachiwa lakini kwa vile ambavyo kanuni na sheria inaweza kuviruhusu basi viondoke, natoa wito kwa wananchi kufika vituo vyote vya polisi nchi nzima na kufanya mazungumzo na wakuu wa vituo ili tuondoe mrundikano huu,kila mkoa ninaotembelea nakuta vituoni kuna mrundikano wa bodaboda,wananchi njooni muonane na wakuu wa vituo mchukue vyombo vyenu”, alisema Naibu Waziri Chilo.

Akizunguma katika ziara hiyo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Unguja, Awadh Juma Haji amesema vyombo vingi vilivyopo kituoni ni kutokana na waliovitendea makosa kutofika vituoni kwa wahusika wakuu hali inayopelekea uwepo wake hapo ambapo alikiri imekua ni kero kwa jeshi la polisi.

“Mheshimiwa Naibu Waziri hapa vyombo vilivyopo ambavyo tunavishikilia hatuwezi kuvitoa ni vile ambavyo mashauri yake bado yapo mahakamani lakini kuna vingine watuhumiwa wake wamekimbia tangu vikamatwe bado awajajitokeza tunachofanya tunasubiri ule muda wa kisheria wa miezi sita ili taratibu za utaifishaji zifanyike hapa tuna magari ya wizi,bodaboda nyingine zimeshiriki katika makosa ya usalama barabarani nyingine zimehusika kwenye uporaji na tatizo linguine wahusika hawaji vituoni kuonana na wakuu wa vituo kuchukua vyombo vyao hali hiyo upelekea mrundikano huu”,alisema RPC Awadh.

Akitoa hali ya ulinzi na usalama katika Kipindi hiki cha Sikukuu Kamanda Awadh amesema Sikukuu ya Eid imesheherekewa vizuri pasipo kuwepo matukio makubwa ya uhalifu huku Jeshi la Polisi likiendelea na doria zake za kawaida katika kuhakikisha amani na usalama vinakuwepo katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

Share:

J FLANI AREJEA KIVINGINE BAADA YA KUFANYA KAZI NA PRODUCER DEEY CLASSIC

Share:

RC MTAKA AKIPONGEZA CHUO CHA DODOMA VOCATIONAL TRAINING CENTRE KWA KUTOA UJUZI

 

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka akizungumza na wahitimu katika Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,akisisitiza jambo kwa wahitimu wakati akizungumza nao katika Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

Mkuu wa Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre,Jemima Nchimbi,akisoma risali wakati wa Mahafali ya tano ya chuo hicho kilichopo jijini Dodoma.

Baadhi ya wahitimu wakifatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati akizungumza katika Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka akikata keki wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka akilishwa keki na Mkuu wa Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre,Jemima Nchimbi wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

Mkuu wa Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre,Jemima Nchimbi akiwa katika meza kuu na baadhi ya viongozi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,akiwa na Mkuu wa Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre,Jemima Nchimbi pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa meza Kuu wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,akimsikiliza Kiongozi wa Wazee Bw.Ezekiel Chadwanga wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma.

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,akisimikwa Wazee Bw.Ezekiel Chadwanga kuwa kiongozi wao wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre kilichopo jijini Dodoma

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,akipokea zawadi ya Mbuzi kutoka katika uongozi wa Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre mara baada ya kuhudhuria Mahafali ya tano ya chuo hicho kilichopo jijini Dodoma

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka akigawa vyeti kwa wahitimu mbalimbali kulia kwake ni Mkuu wa Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre,Jemima Nchimbi wakati wa Mahafali ya tano ya Chuo hicho kilichopo jijini Dodoma.

..........................................................................................

Na Alex Sonna,Dodoma

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka amewataka vijana wa Mkoa wa Dodoma kuhakikisha wanakuwa na ujuzi ili kwendana na kasi ya Mkoa huo kuwa Makao Makuu ya Nchi.

Akizungumza leo,Julai 22,2021,katika mahafali ya tano ya Chuo cha Dodoma,Vocational Training Centre(Dodoma VCT)Mkuu huyo wa Mkoa amewataka vijana wa Mkoa huo kuwa na ujuzi ili kuzikimbilia fursa mbalimbali ambazo zitapatikana kutokana na Mkoa huo kuwa Makao Makuu ya Nchi.

“Wito wangu kwa vijana wa Mkoa wa Dodoma niwatake kuwa na ujuzi katika Makao Makuu ya Nchi niwatake kila mmoja apate ujuzi tumieni vyuo vya kati wazazi niwaombe watoto wapate ujuzi kama hajafaulu apate nafasi ya kusoma ujuzi wowote, Dodoma na Dunia tunayoiendea itakuwa na fursa nyingi lakini kama huna ujuzi utapishana na fursa

“Mtu anaenda Garage anakuwa ni msafisha vioo lakini baadae anajifunza umakenika baadae anajifunza udereva anakuwa dereva,vijana wengi ni bodaboda wewe (wahitimu) kuwa fundi bodaboda utakuwa umepata ajira lazima vijana mhakikishe mna ujuzi na kuna kozi zingine ni fupi tu,”amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

“Dodoma ni Makao Makuu hivyo mnafaida mjiandae miradi inayokuja ikukute una ujuzi hapa ujenzi ni mkubwa sana kama unakaa nyumbani hakuna kibarua ni wewe tu,tumia fursa.Tunajenga hapo Msalato likiwanja likubwa kabisa wakikuuliza una ujuzi wewe upo tu tafuta ujuzi.

“Kama unakaa hapa usidhani unapoteza muda kuna siku utamkumbuka huyu mama wazazi viombeeni hivi vyuo vya ujuzi kama kuna mtu anakudanganya fundi amekosa ajira huyo anakudanganya.Kama unasoma ujuzi shikilia hivyo ninyi hamjapoteza na wazazi mliopo nyumbani usikae na mototo ambaye hana ujuzi.

“Nakuombea Madame kazi zote duniani tunaanzia chini kazi moja tu ndio unaanzia juu kwenda chini kazi hiyo ni kuchimba kaburi na hapa tumeanza.Endelea kusoma mazingira kozi gani utaziongeza ili washindane na tembelea vyuo vingine uone ambavyo wanavyo wewe huna na mitaala pamoja na walimu,”amesema

Mkuu huyo wa Mkoa pia amekitaka Chuo hicho kuongeza ubunifu pamoja na kozi mbalimbali ili watu wengi waweze kupata ujuzi ambao utasaidia kuondokona na changamoto ya ajira.

“Madame nakushauru sana ongeza kozi tujitahidi tuweke matangazo kwamba Chuo kinafundisha kozi hizi na hizi local radio zungumza uwaokoe watoto wa Dodoma,tukitaka vijana wa Mkoa huu wawe washindani tuwapeleke kwenye elimu zote ya darasani,ufundi,elimu dunia aghera.Dunia tunayoiendea tunahitaji maeneo ya namna hiyo nimeona kozi zako ongeza kozi ili watu wajifunze kuwe na ujuzi”amesema.

Pia,amewataka wanafunzi licha ya kujifunza masomo mbalimbali pia wanatakiwa kuwa wabunifu ili wanapomaliza masomo yao waweze kuajirika kirahisi.

“Mjifunze vyote ujuzi na ubunifu ukienda mahali kutafuta vibarua unakuwa umekamilika kwa kila kitu,tunapeleka umeme vijiji vyote vya Tanzania kule vijijini hakuna mafundi maana yake fundi ni wewe.Tunapeleka umeme na maji katika vituo vya afya bomba likiharibika au kuziba wewe ndio fundi,”amesema.

Kuhusiana na changamoto ya eneo la ardhi la chuo hicho,RC Mtaka ameutaka uongozi wa Chuo kwenda makao makuu ya kata ili kukutana na timu ambayo inazunguka Mkoa wa Dodoma kumaliza changamoto za migogoro ya ardhi.

“Nikuombe kama utatumia nafasi vizuri,wanalalamikiana waende makao makuu ya Kata ili waweze kulitatua.Nakuomba uwezekutumia nafasi hiyo kupata muafaka katika siku hizo 10 ambazo tumeziongeza kwani tulitenga siku 10 na tuliongeza siku 10 zingine,”amesema RC Mtaka.

Awali akisoma risala Mkuu wa Chuo hicho,Jemima Nchimbi amesema wanakabiliwa na changamoto kukosa eneo la kujenga chuo kutokakana na eneo walilolipata kukabiliwa na mgogoro.

Amezitaja changamoro zingine ni vijana kutokupata mikopo kwa kozi za ufundi stadi,uelewa mdogo wa wazazi kutambua kozi zote ni kwa ajili ya jinsia zote.

Amesema mafanikio ambayo wameyapata ni pamoja na kufundisha vijana 679 wa kozi fupi,kufundisha vijana wa kike na wa kiume kwa kozi ndefu zaidi ya 333 ambapo vijana 1002 wameweza kupata mafunzo ambapo asilimia 75 wameajiriwa na asilimia 25 wamejiajiri.

Vilevile,amesema wamefanikiwa wamefanikiwa kutoa mafunzo kwa kina mama zaidi ya 197 kwa kozi za ujasiriamali na baadhi yao wamefungua maduka na kuuza bidhaa walizojifunza kutengeneza.

Share:

PROF : CHAGGU: MATUMIZI YA MAKAA YA MAWE HUPUNGUZA UKATAJI MITI OVYO


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mhandisi Prof. Esnat Chaggu (aliyesimama), akitoa salamu ya utambulisho kwa uongozi wa Mgodi wa Tancoal baada ya kuwasili katika Mgodi huo.
Mtaalam wa Miamba Bwa. Matiko Paul akitoa ufafanuzi kwa Bodi ya Wakurugenzi wa NEMC juu ya namna wanavyofanya shughuli zao katika Mgodi wa Ngaka.

Mkurugwnzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Mhandisi Dkt. Samuel Gwamaka (aliyenyanyua mkono), akizungumza jambo kwa Bodi ya Wakurugenzi ya NEMC wakati walipokuwa wakikagua Mgodi.




Sehemu ya Miamba inayotumika kutolea makaa ya mawe katika Mgodi wa Ngaka uliopo kijiji cha Ruanda Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma.

********************

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mhandisi Prof. Esnat Chaggu amesema kuwa, matumizi ya makaa ya mawe ni nishati mbadala ambayo inasaidia kupunguza matumizi ya mkaa na kuni hivyo kupelekea kupungua kwa kiasi kikubwa cha ukataji miti.

Ameyasema hayo alipokuwa katika Mgodi wa makaa ya mawe ya Ngaka uliopo kijiji cha Ruanda Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma, unaomilikiwa na Kampuni ya Tancoal Energy Limited, amesema kuwa makaa ya mawe ni muhimu sana kwa ajili ya nishati mbadala kama inavyofahamika kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani mwaka huu Mhe. Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amesisitiza kutumia nishati Mbadala kuepuka ukataji miti hovyo.

Aidha Prof Chaggu ameeleza kuwa makaa ya mawe yanaweza kutumika katika Taasisi mbalimbali ikiwemo shule, jeshi na hata majumbani kama nishati mbadala kwa ajili ya kupikia.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NEMC Prof. Hussein Sosovere amesema kuwa, Bodi imetembelea mradi huu kuona shughuli za uchimbaji wa madini kama zinazingatia matakwa ya sheria ya mazingira ya mwaka 2004. Amesema kuwa mradi huu unafaida lakini kunachangamoto nyingi za kimazingira kama haujazingatiwa ipasavyo, changamoto hizo ikiwemo uchafuzi katika vyanzo vya maji, kelele na vumbi.

“Hivyo tunawahimiza kampuni hii na NEMC kwa pamoja kushirikiana katika kuhakikisha vyanzo vya maji havichafuliwi, ili kuweza kuepusha uchafuzi wa mazingira na afya za binadamu kuwa salama” Prof Sosovere

Naye Meneja wa NEMC Kanda ya Kusini Bwa.Jamal Baruti amesema kuwa, kila shughuli inayofanywa na binadamu inaathari kwa mazingira, hivyo ni jukumu la Baraza na jamii kuhakikisha uwekezaji wowote unafanyika bila ya kuathiri mazingira.

“Sisi kama Baraza ikiwa kama jicho katika kusimamia mazingira, tumeweza kutoa ushauri na maelekezo katika suala la udhibiti wa vumbi na maji machafu ya mgodi ambayo yanaweza kusababisha uchafuzi katika vyanzo vya maji. Hivyo nitoe wito kwa makampuni mengine yanayohusika na uchimbaji wa makaa ya mawe wahakikishe wanatekeleza maelekezo yote waliyoelekezwa ili kulinda mazingira.” Bwana Baruti

kwa upande wake Meneja wa Mazingira na Usalama wa Tancoal Bwa. Fericks Bida amesema Kampuni inazingatia maelekezo wanayopewa na Baraza kwa kuhakikisha ulipuaji wa miamba unakuwa katika viwango vinavyokubalika isizidi mitetemo itakayoleta madhara kwa watu waliokaribu na mgodi. Kwa upande wa maji yanayotoka kwenye mgodi wanahifadhi katika mabwawa yaliyochimbwa kwenye mgodi ili kuepusha yasisambae na kwenda kwenye vyanzo vya maji.

Vile vile Bodi ya NEMC imetembelea Mto Luhuhu unaotenganisha Mkoa wa Ruvuma na Njombe, katika ziara hiyo Bodi imebaini uchafuzi mkubwa wa mto huo na kupelekea mto kujaa udongo na kina cha mto kupungua pamoja na maji ya mto kubadilika rangi kuwa mekundu. Bodi ya Wakurugenzi ya NEMC ipo kwenye ziara katika Kanda ya Kusini kukagua utunzaji na uhifadhi wa mazingira.
Share:

Tanzania Yairudisha Selous Kwenye Urithi Wa Dunia


Happy Lazaro,Arusha
Arusha.Katibu Mkuu wa Wizara ya maliasili na utalii Dk.Allan Kijazi amesema serikali kwa kushirikiana na wataalamu wa shirika la umoja wa mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni (UNESCO) waliopo hapa nchini wamefanikiwa kuirudisha Poli la akiba la selous ili iendelee kuwepo kwenye orodha ya maeneo ya urithi wa dunia .


Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi kilichoendeshwa kwa njia ya mtandao na kuhudhuriwa na nchi wanachama  21  Dk Kijazi amesema taarifa zilizokuwa zimetumika kutaka selous iondolewa kwenye orodha zilikuwa sio sahihi kwakuwa zilikuwa zimetegemea  kusikia na sio kupata taarifa kamili kutoka kwa nchi husika.


“Kama ambavyo tuliripoti wakati  wa mkutano wa unesco ulipoanza kulikuwa na mapendekezo ya selous kuondolewa kwenye  orodha ya maeneo ya urithi wa dunia  sisi na wataalamu tumekaa na kuona taarifa zilizotumika si sahihi na zilikuwa na uongo mwingi  “amesema .


Dk Kijazi ameongeza kuwa, mapendekezo ambayo yalikuwa yametolewa na IUCN pamoja na World heritage cental ambayo yalitumika  kuishauri UNESCO kuiondoa selous yalikuwa hayajafuata utaratibu kwa kuwa walikuwa hawajashirikishwa  kitu ambacho ni tofauti na miongozo walikubaliana kwenye kuchagua na kusimamia maeneo hayo .

 
“Wataalamu wamefanya kazi kubwa kueleza ukweli kuhusu hali ilivyo na kuziambia nchi  wanachama ishirini na moja ambazo zinapiga kula kuwa utaratibu umekosea na taarifa zilizotolewa sio sahihi   kwahiyo selous iendelee kubaki na kuwaomba IUCN pamoja na world heritage cental kukusanya taarifa zenye usahihi na sio za kupotosha dunia” ameongeza .


Kwa upande wake Profesa Hamisi Malebo ambaye ni  Katibu mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO  kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema taarifa iliyokuwa imetolewa ilikuwa imetiwa chumvi kwakuwa walikuwa wamesema selous ilikuwa imepoteza sifa kwa kuwa wamefyeka miti yote na kusababisha uharibifu kitu ambacho sio kweli kwakuwa eneo lililokuwa limefyekwa ni dogo sana .


“Walisema tumefyeka miti yote kwaajili ya kujenga bwawa akati ni sehemu chache sana iliyofyekwa miti  na pia walise  tembo wamepungua wakati tukiangalia tembo wamezaliana sana katika pori hili kwaiyo tunashukuru kuwa tumeweza kuionesha dunia ukweli wote ambao ulipindishwa na mataifa wameelewa na kupingana na IUCN katika taarifa waliyokuwa wameotoa” amesema 


Malebo ameongeza kuwa ,kazi ya kitaalamu huwa ni kuchambua vile vitu ambavyo sio vya kweli kwa kuwa IUCN ni wataalamu washauri wa unesco ni rahisi kukukandamiza usipokuwa makini kwa kuchambua vitu ambavyo ni muhimu .


Naye Evelin Swai ambaye ni Mratibu wa masuala ya unesco kutoka wizarani amewashukuru wataalamu wote waliosaidia kuitetea selous kurudishwa kwenye maeneo ya urithi wa dunia na kusema kuwa ujenzi wa bwawa haukuwa tishio kwenye hifadhi hiyo na kuahidi kuendelea kuishauri serikali ili kuendelea kuhifadi vizuri maeneo ya urithi.


Edward Ishengoma ni Kaimu kamishina wa wizara ya nishati amesema wao kama wahusika wakuu katika kusimamia mradi wa bwawa la Mwalimu Nyerere ambao unayekelezwa na serikali waliamua kuanzisha mradi huo ili uweze kuisadia nchi kwakuwa unafaida nyingi  tofauti la IUCN walivyokuwa wameishauri unesco .


“Mradi huu una manufaa makubwa sana tofauti na wao wanavyodhani kwa kuwa una manufaa kwanza  kimazingira ,kupata nishati , kuzuia mafuriko  na mengine mengi na hatutarudi nyuma “



Share:

Waziri Mkuu Aitaka Bodi Ya Korosho Kutafuta Masoko Ya Uhakika

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameiagiza Bodi ya Korosho Tanzania ihakikishe inatafuta masoko ya uhakika ya zao hilo na yatakayotoa bei nzuri na kuwanufaisha wakulima.

Pia, Waziri Mkuu ameitaka bodi hiyo isimamie mwenendo wa ujenzi wa viwanda vidogo na vikubwa vya kubangulia korosho katika maeneo yote yanayolima zao hilo ili kuondokana na uuzwaji wa korosho ghafi.

Mheshimiwa Majaliwa ametoa maagizo hayo jana (Alhamisi, Julai 22, 2021) wakati akizungumza na Wakuu wa mikoa ya Lindi, Pwani, Mtwara na Ruvuma, Mrajisi wa Ushirika, Viongozi wa vyama Vikuu vya Ushirika wa Korosho katika kikao kilichohusu upatikanaji wa pembejeo za korosho kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa mkoani wa Lindi.

Amesema lazima bodi hiyo ambayo ameizindua lazima iwajibike ipasavyo katika kuhakikisha inaongeza uzalishaji wa zao hilo na iwapo itashindwa Serikali haitosita kuivunja.

“Lazima mfuatilie na kuufahamu mwenendo wa zao mnalolisimamia na mjue mfumo unaotumika katika mauzo yake. Pia muwe na takwimu za wakulima na ukubwa wa mashamba yao ili kuweza kuwahudumia kwa urahisi.”

Waziri Mkuu amesema bodi hiyo inatakiwa iandae kalenda maalumu inayoonesha hatua zote zinazopaswa kufuatwa katika kilimo cha zao hilo kuanzia hatua za uandaaji wa shamba hadi mavuno kwa kuzingatia hali ya hewa ya eneo husika na ipelekwe kwa wakulima.

Amesisiza kwamba utaalamu lazima ufuatwe na uzingatiwe katika kilimo hilo kwa lengo la kuongeza tija kwa wakulima. Pia, Waziri Mkuu ameitaka bodi hiyo ihakikishe pembejeo ikiwemo miche bora na viuatilifu vinapatikana kwa urahisi.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameigiza bodi ya korosho iweke mkakati wa utoaji wa elimu kwa wakulima kuhusu kilimo cha zao hilo ikiwa ni pamoja na faida ya kulima zao la korosho. “Tumieni magari maalumu kwa ajili ya kwenda kuwafuata wakulima katika maeneo yao na kuwapa elimu.”

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema tayari mchakato wa kuviwezesha vyama vya wakulima kuanza ubanguaji wa korosho umeanza ambapo katika msimu wa mwaka huu TANECU imepata mkopo kutoka CRDB na itaanza kubangua tani 2,500.

Amesema vyama vingine vitakavyofuata utaratibu huo baada ya TANECU ni TAMCU, MAMCU na RUNALI ambavyo vyote vinampango wa kuanzisha viwanda vyenye uwezo wa kuchakata tani 2,5000 za korosho kwa mwaka.

Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho, Brigedia Jenerali Mstaafu Aloyce Mwanjile amesema wamepokea maelekezo na maagizo yote kwamba watayafanyia kazi kwa kusirikiana na wajumbe wa bodi hiyo na Menejimenti na kwamba hawatafanyakazi kwa mazoea.


Share:

Makamu Wa Rais Kuanza Ziara Ya Kikazi Mtwara


 Makamu wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango, leo Julai 23, 2021 anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tano mkoani Mtwara.

Makamu wa Rais akiwa mkoani Mtwara anatarajiwa kushiriki misa ya kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha hayati Rais wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa katika Kijiji cha Lupaso Wilaya ya Masasi.

Aidha Makamu wa Rais anatarajiwa kuzindua  stendi ya mabasi Wilaya ya Nanyumbu, soko la kisasa la matunda na mbogamboga la Jidah wilayani Masasi, kuzindua kiwanda cha kubangua korosho Wilaya ya Newala pamoja na kuzungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali atakayotembelea.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais anatarajiwa kuweka jiwe la msingi Hospitali ya Kanda ya kusini iliopo Wilaya ya Mtwara na baadaye kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya sabasaba Mtwara mjini.


Share:

PROF. LIPUMBA APATA CHANJO YA COVID-19





Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba akitoka katika hospitali ya Sali International iliyopo mkoani Dar es Salaam leo mara baada ya kupata chanjo.
**
Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba amepata chanjo ya kwanza ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya COVID-19 katika Hospitali ya Sali International iliyopo mkoani Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kupata chanjo hiyo aina ya AstraZeneca, Prof. Lipumba amesema kuna umuhimu kwa Watanzania wengi kupata chanjo hiyo ya hiari ili kujikinga na janga hilo linalosumbua ulimwenguni na taifa la Tanzania kwa ujumla.

“Nakumbuka Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani na Mwakilishi wa Mfalme wa Abu Dhabi kuhusu upatikanaji wa chanjo, naamini Serikali yetu itatumia fursa hiyo ya kupata chanjo kwa msaada wa nchi hizo”, amesema Prof. Lipumba.

Ametoa wito kwa Serikali ya Tanzania kukubali chanjo hizo zilizopitishwa na kukubaliwa na Jumuiya za Umoja wa Mataifa sambamba na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) kutokana na usalama wake kwa Wananchi.

“Mimi binafsi nimepata fursa hii kutokana na Mke wangu kufanya kazi katika Umoja wa Mataifa (UN), Bangladesh katika Shirika la UNICEF, wao wanatakiwa kupata chanjo na Familia zao hivyo nililetewa Fomu ya kujaza ili kupata chanjo hii katika Hospitali hii ya Sali International hapa Dar es Salaam.” ameeleza Prof. Lipumba.

“Nashauri pia kwa Serikali kutoa mafunzo na Elimu kwa Wahudumu wa Afya na Wananchi kwa ujumla kuhusu kujikinga na janga hili sambamba na matumizi ya chanjo hiyo ya hiari.”
Share:

LORI LAGONGA TRENI MOROGORO, MMOJA AFARIKI , KADHAA WAJERUHIWA




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger