



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akitoa maelekezo kwa viongozi wa kiwanda cha Quaim Steel Mills limited mara baada ya kutembelea kiwanda hicho katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akisikiliza maelekezo kutoka kwa baadhi ya viongozi wa kiwanda cha Kamel Steel Industry kinachozalisha nondo katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akikagua baadhi ya nyaya zilizotengenezwa na madini ya kopa kwenye kiwanda cha OK Plast Limited katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akisikiliza maelekezo kutoka kwa mmoja wa viongozi wa kiwanda cha OK Plast limited kinachotengeneza nyaya za umeme kwa kutumia madini ya kopa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akizungumza na uongozi wa kiwanda cha OK Plast limited kinachotengeneza nyaya za umeme kwa kutumia madini ya kopa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam.
(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)
**************************
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Selemani Jafo amekiagiza kiwanda cha Quaim Steel Mills limited kuhakikisha kufikia miezi miwili kiwe kimejitengenezea mkakati wa kuhakikisha moshi wa kiwanda hicho hautoki na kusambaa kusababisha uchafuzi wa mazingira.
Ameyasema hayo leo Mhe.Jafo mara baada ya kutembelea kiwanda hicho katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika viwanda vinavyozalisha nondo Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika ziara hiyo Waziri Jafo amewaagiza wenye kiwanda hicho kuhakikisha wanakifanyia marekebisho kiwanda hicho kwaajili ya kulinda afya za wananchi hususani ajenda ya utiririshaji wa moshi hivyo amewataka NEMC baada ya miezi miwili kufika katika kiwanda hicho na kukagua kama kimeshafanyiwa marekebisho.
"Kiwanda cha Quaim Steel Mills limited nimewapa miezi miwili waweze kufanya marekebisho makubwa katika kiwanda chao kwa lengo la kukidhi sheria ya mazingira no.20ya mwaka 2004". Amesema Waziri Jafo.
Aidha Waziri Jafo mewataka wenye viwanda nchini kuhakikisha wanazingatia afya za wananchi kwa kuhakikisha viwanda hivyo havitirirshi moshi ama maji taka ambayo yataenda kuathiri watanzania.
Hata hivyo Waziri Jafo amesema atakaa na kuzungumza na Wizara ya Viwanda na Biashara kuhakikisha wanavisaidia viwanda vya ndani viweze kufanya kazi vizuri na kuhakikisha mazingira yanatunzwa na vijana wa kiktanzania kupata ajira kupitia viwanda hivyo.
Na Mwandishi Wetu
Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) umezindua mpango maalum wa kuwasajili na kuwahudumia wajasiriamali wadogo kupitia ukaguzi wa sehemu za kazi, kuwapa mafunzo na ushauri wa kitaalam kuhusiana na masuala ya usalama na afya mahali pa kazi.
Mpango huo umezinduliwa rasmi katika maonesho ya wajasiriamali na wawekezaji yaliyohitimishwa mwishoni mwa wiki katika kituo cha uwezeshaji wananchi kiuchumi mjini Kahama mkoani Shinyanga.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda, amesema mpango huo mahsusi umeandaliwa na Taasisi yake baada ya kuendesha programu ya mafunzo kwa wajasiriamali wadogo kwa miaka mitano na kubainisha ombwe katika usimamizi wa usalama na afya miongoni mwa kundi hilo muhimu.
“Tumekuwa na programu ya mafunzo kwa wajasiriamali wadogo kwa zaidi ya miaka mitano lakini hivi karibuni tulifanya tathmini ya mpango husika na tukabaini kwamba tunahitaji kuwa na utaratibu mzuri na rahisi zaidi kwa ajili ya kundi la wajasiriamali wadogo kuweza kukidhi viwango vya usalama na afya mahali pa kazi. Hivyo, tukaone tutengeneza mfumo wa kieletroniki utakaotuwezesha kuwasajili na kisha kuwafikia katika maeneo yao ili kuwaelimisha pamoja na kushauri namna bora ya kuboresha mazingira yao ya kazi,” alisema Mwenda.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa GS1 Tanzania ambao ndio waratibu wa maonesho hayo kwa kushirikiana na kituo cha uwezeshaji wananchi kiuchumi Kahama, Fatma Kange, amesema Taasisi yake inashirikiana na OSHA katika kuwawezesha wajasiriamali kukuza biashara zao pamoja na kuwapa miongozo ya kuboresha mazingira yao ya kazi.
“Miaka kumi ijayo tunaanza kazi na OSHA na ndio maana unaona katika maonesho haya OSHA amekuwa mdhamini muhimu sana kwa lengo la kuja kuelimisha wajasiriamali wetu ili wafanye uzalishaji kwa kuzingatia afya na usalama wao. Kama tunavyofahamu OSHA wana wajibu mkubwa wa kulinda rasilimali uhai na afya ya kila mtanzania. Hivyo, tunataka wazalishaji wetu watambue nafasi ya afya katika shughuli zao za kila siku” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa GS1 Tanzania",alisema.
Baadhi ya wajasiriamali walioshiriki katika maonesho hayo na kupata fursa ya kusajili maeneo yao ya kazi pamoja na kupatiwa mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi wameeleza jinsi walivyoupokea mpango huo pamoja na mafunzo waliyoyapata.
“Kupitia maonesho haya kuna mafunzo mbali mbali na miongoni mwa mafunzo hayo ni mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na OSHA. Kwakweli mafunzo haya nimeyafurahia sana kwasababu yametupatia nyenzo za kujikinga zaidi katika kazi zetu ili kujiepusha na madhara tunayoweza kuyapata tukiwa kazini au baada ya kustaafu,” alisema Amina Madeleka, Mjasiriamali aliyeshiriki maonesho na mafunzo yaliyotolewa na OSHA.
OSHA ni taasisi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu ambayo husimamia utekelezaji wa Sheria Na. 5 ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Majukumu yake ya msingi ni pamoja na kusajili maeneo ya kazi, kufanya kaguzi za usalama na afya mahali pa kazi, kuchunguza afya za wafanyakazi, kufanya tafiti na kuishauri serikali kuhusu masuala ya usalama na afya mahali pa kazi.
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job no: 535233 Contract type: Fixed Term Appointment Level: NO-4 Location: Tanzania,Uni.Re Categories: WASH (Water, Sanitation and Hygiene), NO-4 UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged children in order to save their lives, defend their rights and to help them fulfill their potential. Across 190 countries and territories, we work for every […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
At Vodacom, we’re working hard to build a better future. A more connected, inclusive and sustainable world. As a dynamic global community, it’s our human spirit, together with technology, that empowers us to achieve this. We challenge and innovate in order to connect people, businesses, and communities across the world. Delighting our customers and earning […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Title Assistant Facilities Supervisor Reports to: Facilities/Site Supervisor Department: Operations Start date: June, 2021 IST Foundational Documents IST Mission Challenging, inspiring and supporting all our students to fulfil their potential and improve the world IST Vision IST will be a global leader in the education of internationally-mobile young people. All students, regardless of their starting […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Title Library Assistant Category (cf Policy 5.101) Teaching Assistance Reports to: Elementary School Principal Department: Elementary School Job Holder Start date: 1 August 2021 IST Foundational Documents IST Mission Challenging, inspiring and supporting all our students to fulfill their potential and improve the world IST Vision IST will be a global […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
A LITTLE ABOUT US Founded in 1951, the Nature Conservancy (TNC) is a global conservation organization dedicated to conserving the lands and waters on which all life depends. Guided by science, we create innovative, on-the-ground and scalable solutions to our world’s toughest challenges so that nature and people can thrive together. This decade is critical […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details