Tuesday, 19 January 2021

SKAUTI MBEYA WATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KATA YA KALOBE

 

Muathirika wa mafuriko Bibi, Tamali Mwalukunga Mkazi wa Kata ya Kalobe jijini Mbeya akiwashukuru Vijana  wa Skauti baada ya kumjengea choo kilicho sombwa na mafuriko. Wa pili kushoto ni Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock  Ntole na kulia ni Mratibu wa Majanga wa  chama hicho mkoani humo, Lusajo Exaud Sanga.
Vijana wa Skauti wakizibua mtaro.
Diwani wa Kata ya Kalobe, akiwapongeza vijana wa Skauti kwa kazi hiyo.
Vijana wa Skauti wakiwa katika picha ya pamoja.
Kazi ya uchimbaji choo cha Bibi Tamari Mwalukunga ikiendelea.
Choo cha Bibi Tamari Mwalukunga kikichimbwa.
Kazi ikiendelea.
Kazi ikiendelea..

Na Dotto Mwaibale.

CHAMA cha Skauti Mkoa wa Mbeya kimetoa msaada kwa kuwasaidia waathirika wa mafuriko katika Kata ya Kalobe jijini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Kamishna wa Skauti wa mkoa huo Mratibu wa Majanga wa  chama hicho mkoani humo, Lusajo Sanga alisema eneo lililoathiriwa zaidi na mafuriko hayo ni Mtaa wa Maendeleo A katika kata hiyo.

Alisema mafuriko hayo yalitokea Januari 8 mwaka huu kufuata mvua kubwa iliyonyesha.

" Eneo hilo liliathiriwa zaidi na mafuriko hayo kutokana na mifereji ya maji kuziba hivyo maji ya mvua kukosa muelekeo na kwenda kwenye makazi ya watu" alisema Sanga.

Alisema baada ya kutokea mafuriko hayo walisaidia na Kamishna wa Skauti Mkoa huo, Sadock Ntole, kuratibu namna ya kwenda eneo la tukio kutoa msaada wa kibinadamu kwa waathirika ikiwa ni pamoja na kuchimba vyoo vilivyosombwa na maji, kuzibua mitaro na kuwafariji waathirika kwa kushirikiana na diwani wa kata hiyo na viongozi wengine. 

Sanga alisema mafuriko hayo yaliathiri nyumba tano katika mtaa huo ambapo nyumba ya mkazi mmoja wa eneo hilo  aliyefahamika kwa jina la Mama Muro na Bibi Tamali Mwalukunga ziliathiriwa zaidi  kwani sehemu ya nyumba yake na choo  vilibomoka ambapo walilazimika kumjengea choo kingine cha muda.

Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock  Ntole alisema wao kama skauti wamekuwa wakitoa msaada kwa jamii pale yanapotokea majanga ya namna hiyo hivyo baada ya kutokea mafuriko hayo walienda eneo la tukio kutoa msaada huo. 

Share:

WANAWAKE IKUNGI WAOMBA HATUA KALI ZICHUKULIWE KWENYE KESI ZA UKATILI

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Justice Kijazi, akizungumza kwenye kikao kazi cha tathmini ya hali ya matukio ya ukatili kwa wanawake na watoto wilayani humo jana kilichoshirikisha wanawake 120 waliokutanishwa na Shirika la SPRF chini ya ufadhili wa FCS ili kujadili namna bora ya kutokomeza matukio hayo kwa mujibu wa sheria.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) Dkt. Suleiman Muttani  akizungumza kwenye mkutano huo ulioshirikisha wanawake 120 kutoka vijiji 12 kuzunguka wilaya ya Ikungi, Singida. 

Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada mbalimbali zilizojikita katika kuwajengea uwezo na kuwaimarisha katika mapambano dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia wilayani humo.

Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada mbalimbali zilizojikita katika kuwajengea uwezo na kuwaimarisha katika mapambano dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia wilayani humo.

Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada mbalimbali zilizojikita katika kuwajengea uwezo na kuwaimarisha katika mapambano dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia wilayani humo.

Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada mbalimbali zilizojikita katika kuwajengea uwezo na kuwaimarisha katika mapambano dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia wilayani humo.

Kikao kazi cha vikundi vya uhamasishaji kwa Sauti Ya Mwanamke na Sauti ya Mwanafunzi  kikiendelea.

Maafisa Watendaji wa Shirika la SPRF wakifuatilia matukio yanayoendelea kwenye kikao hicho.

Jeshi la Polisi likishiriki ipasavyo kikao hicho.

Mmoja wa waratibu wa mradi wa Aware, Bernard Maira akizungumza kwenye kikao hicho.

Mwenyekiti wa Sauti ya Mwanamke kwenye moja ya makundi ya uhamasishaji akizungumza.

Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ikungi, Beatrice Maeda akizungumza.

Kikao kikiendelea.
Moja ya kikundi cha Uhamasishaji cha Sauti ya Mwanamke wilayani  Ikungi  wakieleza moja ya tukio la ukatili wa kijinsia walilofanikiwa kuliibua.

Na Dotto Mwaibale, Singida

SHIRIKA lisilo la Kiserikali linalojikita zaidi katika mlengo wa shughuli za kupunguza umaskini kwa afya na ustawi nchini (SPRF) kupitia mradi wake wa  ‘Aware’ jana limewakutanisha wanawake 120 kutoka vijiji 12 vya wilaya ya Ikungi, mkoani hapa kwa lengo la kuwaimarisha kuweza kukabiliana ipasavyo na  matukio ya ukatili.

 Jumla ya matukio ya ukatili wa kijinsia 104 yameripotiwa kufanyika ndani ya Wilaya ya Ikungi  kwa kipindi cha kati ya Julai 2019 hadi Novemba 2020, ambapo kati ya matukio hayo 56 yalijitokeza katika kipindi cha Julai 2019 hadi Februari 2020, huku matukio mengine 48 ya aina hiyo hiyo yakijitokeza  kipindi cha Machi hadi Novemba 2020.

Kwa mujibu wa SPRF chini ya ufadhili wa Shirika la Foundation for Civil Society (FCS) imebainika kuwa kati ya matukio hayo 56 yaliyoripotiwa kutoka vijiji 12 vya mradi huo kwa kipindi hicho cha Julai 2019 hadi Februari 2020 ni kesi 2 ndizo zilizofikishwa kwenye ngazi ya mahakama, na kati ya hizo kesi moja pekee ndiyo iliyotolewa hukumu.

Matukio mengine 7 ya ukatili yaliyoripotiwa yaliishia kwenye Kituo cha Polisi Ikungi kutokana na kukosa vielelezo na ushahidi shawishi, huku kesi 4 zikikomea kwenye vituo vidogo vya polisi, 7 kwenye ngazi za kata, 16 ngazi ya vijiji, 5 ngazi ya vitongoji na 14 zikiishia kutatuliwa kindugu kwenye ngazi ya familia.

Aidha, kwa upande wa matukio 48 yaliyojitokeza  kwenye kipindi cha Machi hadi Novemba 2020 ni kesi 2 pekee ndizo zilizofikishwa na kuamriwa kwenye ngazi ya mahakama, huku matukio mengine 11 yakiishia Kituo cha Polisi Ikungi, 5 vituo vidogo vya polisi kwenye maeneo hayo, 1 ngazi ya kata, 12 vijiji, 6 Ustawi wa Jmii Wilaya, 2 Vitongoji na  7 zikiishia kutatuliwa kindugu kwenye ngazi ya familia.

Wakichangia ripoti hiyo kabla ya kufikia maazimio, baadhi ya wanawake kutoka kwenye majukwaa ya Sauti za wanawake na Sauti za Wanafunzi wilayani hapo walisema bado kuna udhaifu mkubwa katika kushughulikia utekelezaji wa sheria zinazopinga  vitendo vya ukatili.

“Suala hili limeendelea kuwa sugu na linalochochea  ongezeko la matukio ya kufedhehesha, undugu, ujamaa na urafiki ndio chanzo kikubwa kinachoathiri mwenendo wa mashauri haya ya ubakaji, ndoa za utotoni na mimba za umri mdogo hasa pale tunaporuhusu yamalizwe kwenye ngazi za familia,” alisema mmoja wa washiriki wa mkutano huo, Anna Heneriko.

Mwingine Pili Hussein alisema kesi nyingi zimekuwa zikimalizwa kwenye ngazi ya vituo vya polisi na kwa maaafisa watendaji. Lakini kubwa zaidi kuna uvujishaji mkubwa wa siri kwa watoa taarifa jambo ambalo linafifisha hamasa ya mapambano dhidi ya vitendo hivyo. 

Kupitia mkutano huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Justice Kijazi aliwataka maafisa wa ustawi wa Jamii na Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria katika kuhakikisha mashauri yote yanayoripotiwa yanafikishwa kwenye ngazi za utatuzi wa kisheria.

“Niwahakikishieni mama zangu wote mliopo hapa serikali yenu chini ya Rais John Pombe Magufuli ni sikivu sana, na inakwazwa sana na aina yoyote ya uhalifu na uvunjifu wa sheria kwa makusudi. Nimeguswa sana na matukio haya yanayofedhehesha mama zetu na watoto wetu…chukueni namba zangu za simu ili yeyote kati yenu atakayeona tukio lolote la ukatili likitendeka anijulishe,” alisema Kijazi

Aidha, Kijazi aliwataka aliwataka maafisa Ustawi wa Jamii na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanashughulikia kikamilifu kesi za matukio yote ya ukatili yanaripotiwa kwa utimilifu unaozingatia matakwa ya kisheria kwa minajiri ya kutokomeza kabisa vitendo hivyo, sambamba na kuwezesha haki kuonekana kutendeka.

 Hata hivyo, Jeshi la Polisi Ikungi kupitia mkutano huo liliwataka wananchi wa wilaya hiyo kutoa ushirikiano wa kutosha pindi matukio hayo yanapojitokeza, na hasa kutoharibu wala kuwashawishi wahanga kuficha ushahidi ili hatua stahiki za kisheria zichukuliwe pindi matukio hayo yanapojitokeza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa SPRF, Dkt. Suleiman Muttani  alisema lengo la kikao hicho ni kutaka kuyaimarisha kiutendaji majukwaa ya vikundi vyote vya uhamasishaji dhidi ya matukio ya ukatili, ikiwemo kundi la Sauti ya Mwanamke katika kuendelea kushirikiana na majukwaa mengine kutetea haki za wanawake na watoto.

“Azma ya mradi huu wa ‘Aware’ ni kuona mifumo ya serikali za mitaa imeimarika kwa kupokea na kuitikia kwa haraka utekelezaji wa mahitaji ya jamii hasa matakwa ya wanawake, watoto na makundi mengine athirika kuona wanatambua suala la ukeketaji, ndoa za utotoni, ukatili kwa wanawake na unyanyasaji kwa watoto haukubaliki,” alisema Muttani 

mpaka sasa kati ya matukio yote hayo yaliyoibuliwa kwa ushirikiano wa majukwaa yake mbalimbali ikiwemo Sauti ya Mwanamke, Sauti ya Mwanafunzi, Kamati za Mtakuwa na Wanaume Washawishi ndani ya Vitongoji na Vijiji ni kesi 48 pekee ndizo zilizofika kwenye ngazi za utatuzi huku nyingine utatuzi wake ukiishia kwenye ngazi za familia.

Share:

MVUA YALETA MADHARA SONGEA


Mvua mkubwa iliyoambatana na upepo imesababisha maafa ya kuezuliwa paa katika madarasa matano, ofisi mbili na stoo moja kwenye shule ya msingi ya Mfaranyaki iliyopo manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma, – Simon Maigwa amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa tisa mchana, ambapo mvua hiyo ilidumu kwa takribani dakika 30.

Kamanda Maigwa amesema licha ya kuezua paa katika madarasa hayo matano, mvua hiyo pia imesababisha madhara kwa kaya tisa ambapo saba ni katika mtaa wa CCM kata ya Mjini na nyumba nyingine mbili za familia za polisi katika kituo kikuu nazo zimeezuliwa paa.

Amesema mvua hiyo pia imeezua paa katika baadhi ya vibanda vya biashara kwenye soko kuu la Songea huku tathmini ya madhara hayo ikiendelea kufanyika.

Diwani wa kata ya Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)katika Manispaa ya Songea Mathew Ngalimanayo amesema hakuna kifo chochote kilichoripotiwa kufuatia mvua hizo.


Share:

TAIFA STARS KUANZA NA ZAMBIA LEO MICHUANO YA CHAN


Kuelekea kwenye mchezo huo, kocha wa Taifa Stars, Mrundi Etienne Ndayiragije amesema “maandalizi yameenda vizuri, wachezaji wapo sawa. Kuhusu korona wamechekiwa wote wako sawa, tuko vizuri. Tunaendeelea kujiandaa kwenye vile ambavyo tunaamini vitakuwa vya msaada kwetu”.

Kuhusu nafasi ya Stars kwenye mchezo huo, Ndayiragije amesema “ morali na hali ya kujiamini kuko juu kwenye kambi, wachezaji wapo tayari kwa mchezo, nimewaambia tutatcheza ili tushinde maana najua ushindi utainua ari kwenye kikosi na kupelekea tufanye vizuri kwenye michezo inayofuata”.

Etienne amesema ari imeongezeka baada ya kocha msaidizi Selemani Matola kujiunga na kikosi hicho  baada ya kumaliza majukumu ya kuiongoza kikosi cha Simba kwenye michuano ya Mapinduzi viswani Zanzibar na Erasto Nyoni akijiunga na timu baada ya kumaliza matatizo ya kifamilia.

Ushiriki wa Taifa Stars kwenye michuano ya CHAN umekuja baada ya miaka takribani 11 tokea ushiriki wao mwaka 2009 michuano hiyo ulipoanzishwa na ndiyo msimu ambapo Zambia walishiriki kwa mara ya kwanza na kushika nafasi ya 3 ikiwa ndiyo ya juu zaidi kwa upande wao kwenye CHAN.

Huu utakuwa mchezo wa 18 wawili hao kukutana, kwenye michezo 8 ya mwisho ambayo Stars imekutana na Zambia kwenye michuano tofauti kukiwa na mchanganyiko wa wachezaji wao wakigeni kwenye vikosi vyao, Zambia imeshinda mara 4, sare 3 wakati Stars imeshinda mara 1 pekee.

Ili Taifa Stars iweke hai matumaini ya kufuzu hatua inayofuata ya robo fainali, inahitaji ipate ushindi michezo yote mitatu ya makundi watakayocheza au kuwa na matokeo yatakayomfany awe na alama nyingi kuliko wote kwenye kundi D au alama nyingi zitakazomfanya ashike wapili kwenye kundi.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 19,2021


















Share:

Monday, 18 January 2021

BABU WA MIAKA 80 AFARIKI HOTELINI AKIWA NA MPENZI WAKE WA MIAKA 33 DAR

 

Picha ya kitanda

Na Mwandishi wa Malunde 1 blog Dar es salaam

Mwanaume aliyejulikana kwa jina la David Makerege Mluli (80) amekutwa amefariki dunia ndani ya Hoteli ya Mbezi Garden iliyopo Mbezi jijini Dar es salaam akiwa na mpenzi wake aliyejitambulisha kwa jina la Neema Kibaya (33).

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni ACP Ramadhan Kingai amesema tukio hilo limetokea Januari 16,2021 majira ya saa 9 alasiri katika eneo la Mbezi Beach ambapo Jeshi la polisi lilipokea taarifa kutoka kwa Meneja wa Hoteli ya Mbezi Beach Garden, Newton Mkonda kuwa katika hoteli hiyo kuna mteja amefariki dunia.

"Baada ya taarifa hiyo kupokelewa, Jeshi la polisi lilifika katika hoteli hiyo chumba namba 22 na kubaini uwepo wa maiti ya mwanaume ambaye baada ya kupekua katika nguo zake vilikutwa vitambulisho vyenye majina ya David Makerege Mluli (80) mkazi wa Goba aliyekuwa amekodi chumba hicho",ameeleza

"Pia katika chumba hicho alikutwa mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Neema Kibaya (33) mkazi wa Goba ambaye katika maelezo yake alieleza kuwa marehemu alikuwa mpenzi wake", ameongeza Kamanda Kingai.

Kamanda Kingai amesema uchunguzi wa awali ulifanyika na kubaini kuwa mwili wa marehemu hauna jeraha lolote na kuchukuliwa na askari polisi kupelekwa katika hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya uchunguzi na hifadhi.

Aidha amesema mwanamke huyo aliyekutwa chumbani ambamo mwili wa marehemu ulikuwemo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Share:

Communications & Resource Mobilization Manager at SAT

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Communications & Resource Mobilization Manager    Sustainable Agriculture Tanzania (SAT) is a grassroots organization with registration number 00NGO/R/0833. SAT works closely with small scale farmers on organic farming and stakeholders like universities, companies and governmental extension officers. Its holistic approach is built on the four pillars dissemination, research, application and networking. An exciting opportunity with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Assistant Communications Manager at SAT

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Assistant Communications Manager     Sustainable Agriculture Tanzania (SAT) is a non-for-profit organization with registration number 00NGO/R/0833. SAT works closely with small scale farmers on organic farming and stakeholders like universities, companies and governmental extension officers. Its holistic approach establishes an Innovation Accelerator, which is built on the four pillars dissemination, research, application and networking. An […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Director of Operations at APHFTA

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Position Title:  Director of Operations   Reports to:  Chief Executive Officer-APHFTA Department: Programs Supervisory role: All Project Heads and Departmental Heads Location: Dar es Salaam APHFTA is an umbrella organization of the private (self-sustaining) health sector in Tanzania established in 1994, as a Non-State organization. It serves as a public forum for the private health sector and provides […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Technical Director at APHFTA

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Position Title: Technical Director   Reports to: Chief of Party-SAFE VMMC Project Department: Programs Supervisory role: 4 Deputy Directors (Deputy Director Clinical services, Demand Creation, Project Coordination and Monitoring and Evaluation Location: Dar es Salaam APHFTA is an umbrella organization of the private (self-sustaining) health sector in Tanzania established in 1994, as a Non-State organization. It serves as a […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Branch Coordinators at Tunakopesha Company Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Position: Branch Coordinators   TKL, a Micro Finance, loan provider for government institutions and private sectors is looking for dynamic Branch Coordinators. Locations: Dar es salaam, Shinyanga, Iringa, Mbeya & Singida. ( 5 post ) OVERVIEW OF ROLE Plan, direct and implement Sales strategies and programs to achieve or exceed the sales objectives for the region. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Graphic Designers at AA TANCH holding company ltd

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job title: GRAPHIC DESIGNERS (2 position)   Location: ARUSHA, Head office Reports to: Managing director Projects: SOKOKUUONLINE AND TANCH EXPRESS APP SUMMARY: AA TANCH holding company ltd is a private limited company established in 2018.It focused on connecting buyers to seller, dedicated in providing easy, reliable and secure trades as well as shipment and delivery of products […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MCHUNGAJI WA KANISA LA 'YESU NAKUPENDA UMEOKOKA' AUAWA KWA KUCHOMWA KISU


Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Rose Jacob - Mwanza
Mchungai wa Kanisa la Yesu Nakupenda Umeokoka, Beneth Karange (66) na binti yake Renatha Beneth (42), wilayani Nyamagana, jijini Mwanza wameuawa kikatili kwa kuchomwa kisu na mtoto wake wa kiume ambaye naye alifariki baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira.

Anayedaiwa kutekeleza mauaji hayo ni kijana wake wa kiume, Richmond Beneth, ambaye naye alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa hospitali ya Sekouture, kutokana na kupigwa na wananchi wenye hasira.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Murilo Jumanne, alisema  tukio hilo limetoke juzi saa tisa alasiri ambapo Richmond (32), alikuwa akisoma Chuo Kikuu cha Kampala kilichopo jijini Dar es Salaam.

Kamanda Muliro alisema, kijana huyo ambaye naye aliuawa, aliwachoma kisu baba na dada yake sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha vifo vyao papo hapo.

Muliro alisema kijana huyo aliyesababisha mauaji hayo, alirudi nyumbani kutoka chuoni kwa kukosa ada.

Share:

Picha : RAIS MAGUFULI NA BAADHI YA VIONGOZI LEO BUKOBA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba Methodius Kilaini, Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi Dkt. Abednego Keshomshahara, Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba Desiderius Rwoma, Shehe wa Bukoba Mubarak Juma pamoja na Padre Revocatus Mwehuzi muda mfupi mara baada ya kupata chakula cha Mchana katika Ikulu ndogo ya Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 18 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Balozi wa Uingereza hapa nchini David Concar pamoja na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke muda mfupi mara baada ya kupata chakula cha mchana katika Ikulu ndogo ya Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 18 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amewashika mikono Balozi wa Uingereza hapa nchini David Concar pamoja na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke muda mfupi baada ya kupata chakula cha Mchana katika Ikulu ndogo ya Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 18 Januari 2021.
Share:

SPIKA NDUGAI AFANYA UTEUZI KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE



Taarifa Kuhusu Uteuzi wa Wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge




Share:

NAIBU WAZIRI KIPANGA ATOA WITO KAMATI YA USIMAMIZI WA MRADI WA UJENZI WA CHUO CHA VETA KOROGWE KUHAKIKISHA UNAKAMILIKA KWA WAKATI

Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga akisisistiza jambo  wakati wa ziara yake ya siku moja ya kukagua ujenzi wa Chuo cha Veta wilayani Korigwe mkoani Tanga mradi unaojengwa chini ya Usimamizi wa Chuo cha Veta Kihonda mkoani Morogroro wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Kissa Gwakisa wa kwanza kushoto (aliyevaa tisheti nyeupe) ni Mkuu wa Chuo cha Veta  Kihonda Morogoro na Msimamizi wa Mradi huo Maganga Kashinde

Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga akisisistiza jambo  wakati wa ziara yake ya siku moja ya kukagua ujenzi wa Chuo cha Veta wilayani Korigwe mkoani Tanga mradi unaojengwa chini ya Usimamizi wa Chuo cha Veta Kihonda mkoani Morogroro wa pili kulia Mkuu wa Chuo cha Veta  Kihonda Morogoro na Msimamizi wa Mradi huo Maganga Kashinde
Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga katikati akikagua ujenzi wa chuo cha Veta wilayani Korogwe wakati wa ziara yake kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Kissa Gwakisa

Muonekano wa ujenzi wa baadhi ya majengo ya Chuo cha Veta wilayanu Korogwe
Fundi akiendelea na ujenzi kwenye Chuo cha Veta wilayani Korogwe kama alivyokutwa




Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Kipanga amefanya ziara ya kutembelea Chuo cha Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) wilayani Korogwe Mkoani Tanga huku akitoa wito kwa kamati inayosimamia mradi wa ujenzi huo kuhakikisha unakamilika kwa wakati uliopangwa.

Akiwa katika katika ziara ya kukagua mradi huo ambao unasimamiwa na chuo cha VETA Kihonda cha mkoani Morogoro alionesha kuridhishwa na hatua iliyofikiwa na kushauri matumizi ya jeshi la akiba kama vibarua ili kuharakisha utekelezaji wa mradi huo.

Kipanga alisema kwamba amekagua mradi huo na kuridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa hadi sasa na kuwaagiza wasimamizi wa mradi kuhakikisha unakamilika kwa wakati uliopangwa ikiwemo kuwashauri kutumia vibarua kutoka Jeshi la Akiba kwa kuwa wapo wengi ambao wanaweza kufanya kazi hizo.

Hata hivyo Naibu Waziri huyo alitoa wito kwa wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha vifaa vya upauaji vinapatikana mapema ili ujenzi uweze kukamilika kwa muda uliopangwa.

“Kwa kuwa majengo karibu yote yamefikia hatua ya upauaji, nitoe rai kuwa vifaa vya upauaji vipatikane mapema ili ujenzi uendelee na kukamilika kwa wakati,” amesisitiza Mhe. Kipanga.

Awali Akisoma taarifa ya ujenzi wa chuo hicho, Mkuu wa chuo cha VETA Kihonda, Kashindye Maganga amesema ujenzi wa mradi huo unagharimu kiasi cha Bilioni 1.6 huku kiasi ambacho walikwisha kupokea ni Tsh.Milioni 940.2 na hadi sasa wametumia kiasi cha Tsh.Milioni 917.9 na kiasi kilichobakia ni milioni 22.2 hivyo fedha ambazo imetumika ni sawa na asilimia 57.37 ya fdha ya mradi wote.

Alisema mpaka sasa mradi huo umefikia 34 ya kazi zote na kazi iliyobakia kwa sasa ni kumalizia kufunga lenta,kupaua na kazi ya umaliziaji ambapo tayari walikwisha kuomba fedha kwa ajili ya kumalizia kazi hizo na wanategemea kukamilisha kazi ya mradi huo ifikapo Machi 31 mwaka huu endapo fedha walizoomba watapatiwa mapema.



Naye Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Kissa Gwakisa akizungumza katika ziara hiyo alionyeshwa kufurahishwa na hatua ya Serikali kujenga chuo hicho katika Wilaya yao na kwamba anaamini chuo hicho kikikamilika kitatoa vijana mahiri watakaotumika kiuzalishaji katika viwanda mbalimbali nchini .

Mkuu huyo wa wilaya aliahidi kushirikiana na Kamati ya ujenzi kuhakikisha vijana wa jeshi la akiba wanapatikana haraka ili kuweza kukamilisha ujenzi huo kwa wakati uliopangwa.

 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger