Friday, 15 January 2021

Cluster Marketing Implementer at Puma Energy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Cluster Marketing Implementer   Puma Energy Dar es Salaam, Tanzania Objectives Works in partnership with and manages the implementation of all brand and marketing campaigns for respective clusters within Retail COE, Corporate Affairs, Brand & Marketing Teams in support of Lines of business – Commercial, Retail, Lubricants, Aviation and Future Energies across markets of choice. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Branch Manager at WATU Credit Africa ARUSHA

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About WATU: WATU is a focus driven, customer-centric company that believes everyone deserves the opportunity to be an entrepreneur and achieve their ambitious goals in life. As Africa’s fastest growing Asset Finance company, we see the continent’s bright and prosperous future and want to be part of making it a reality. Our vision is to […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

NECTA YAFUTA MATOKEO YA WATAHINIWA 215 KIDATO CHA NNE 2020...YAZUIA MATOKEO YA WATAHINIWA 252

Share:

MSICHANA ALIYESHIKA NAFASI YA KWANZA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2020 AFUNGUKA


Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Canossa aliyeshika nafasi ya kwanza kwa wasichana katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2020 Justina Gerald (15) amesema anataka kuwa mhandisi wa mafuta.

Mbali na kuwa wa kwanza kwa wasichana katika mtihani huo, Justine aliyesema siri ya kufaulu ni kumtanguliza Mungu na kuweka malengo katika masomo, ameshika nafasi ya pili katika orodha ya wanafunzi 10 bora kitaifa.

“Nataka kuwa mhandisi wa mafuta ya petroli kwa sababu nchi zinazoendelea kama Tanzania ndiyo zinategemea kukuza uchumi wake,” amesema Justina.

Share:

ALIYESHIKA NAFASI YA KWANZA KITAIFA MATOKEO KIDATO CHA NNE 2020 ANATOKA FAMILIA YA WASOMI

Mwanafunzi aliyeshika nafasi ya kwanza kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2020, Paul Luziga aliyekuwa akisoma shule ya sekondari Panda Hill ya jijini Mbeya anatoka familia ya wasomi.

Paul ni mtoto wa tano katika familia ya Luziga na ndugu zake wawili wamehitimu chuo kikuu na wengine wawili wanasoma katika vyuo vikuu mbalimbali nchini.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Ijumaa Januari 15, 2021 mama mzazi wa mwanafunzi huyo, Lucy Mwogela amesema siri ya watoto wake kufanya vizuri shuleni ni kumwamini Mungu.

Watoto hao wote wamefika chuo kikuu wakisomea fani mbalimbali.

“Mtoto wa kwanza alimaliza shahada ya kwanza yuko Dar es Salaam anafanya kazi. Wa pili ni wa kike amemaliza shahada ya uzamili, watatu na wa nne ni mapacha wapo chuo kikuu na huyu Paul ndiyo wa mwisho.”

“Siri ni kumwamini Mungu tu, hakuna ujanja wowote ninaoweza kufanya,” amesema Lucy.

CHANZO - MWANANCHI

Share:

HATIMAYE MAMA DANGOTE AMTAJA BABA MZAZI WA MSANII DIAMOND PLATNUMZ


Sanura Kassim maarufu mama Dangote ambaye ni mama mzazi wa msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz amesema baba halisi wa mwanaye ni Salum Iddi Nyange na si Abdul Juma ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifahamika kama baba wa mkali huyo wa Bongofleva.

Mama Dangote ameeleza hayo leo Ijumaa Januari 15, 2021 baada ya kupigiwa simu na Dida, mtangazaji wa kipindi cha Mashamsham kinachorushwa na redio ya Wasafi kueleza kuhusu uhusiano kati ya Diamond na Ricardo Momo aliyekuwa akihojiwa na redio hiyo.

Katika majibu yake, mama Dangote amesema Ricardo na Diamond ni ndugu na baba yao ni Nyange ambaye kwa sasa ni marehemu.

Chanzo - Mwananchi

Share:

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI, MHANDISI KASEKENYA AIPONGEZA TMA


Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (katikati) akizungumza na uongozi na menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA) katika ziara yake kuitembelea taasisi hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Dkt. Buruhani Nyenzi pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi (kulia).
Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi (kulia) akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (katikati) katika ziara yake kuitembelea taasisi hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Dkt. Buruhani Nyenzi. 
Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi (kulia) akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya akitembelea shughuli anuai za taasisi hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Dkt. Buruhani Nyenzi. 
Meneja Kituo Kikuu cha Utabiri – TMA, Bw. Samwel Mbuya akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya akitembelea shughuli za TMA.
Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA, Dk. Hamza Kabelwa (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (katikati) alipofanya ziara ofisi za TMA. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi.
Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi wa TMA, Dk. Ladislaus Chang'a (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (kulia) alipotembelea TMA.
Sehemu ya menejimenti ya TMA wakifuatilia maelekezo ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya.
***

NAIBU Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA) kwa ufanisi na utendaji mzuri wa kazi zao kiasi ambacho taifa linatambuliwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na shughuli zake kutegemewa na nchi za jirani.

Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema hayo jana katika ziara yake alipotembelea na kujionea shughuli na majukumu ya TMA ofisi kuu za mamlaka hiyo zilizopo Jengo la Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam, kupokea taarifa ya utendaji na kuzungumza na menejimenti ya TMA. 

"...Kwanza niwapongeze sana kwa kazi nzuri mnayoifanya, sasa endeleeni kuboresha zaidi. Kimsingi nimefarijika sana kusikia Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi pia ni Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) hii ni hatua kubwa. Kutambulika kwa Dkt. Kijazi kimataifa ni sifa kwa taifa letu hivyo nawapongeza sana.

"Nimesikia pia Tanzania, imepewa jukumu na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kusaidia mataifa takribani matano jirani zetu upande wa hali ya hewa hii pia ni sifa kwa taifa letu na kukubalika," alisema Naibu Waziri Mhandisi Godfrey Kasekenya alipokuwa akizungumza na uongozi wa TMA. 

Aliitaka TMA kutambua mchango wa wafanyakazi wanaofanya vizuri na hata kuwapongeza na wale wasiowajibika kuwajibishwa ili kuongeza ari ya utendaji ndani ya mamlaka. Aidha ameitaka TMA kuhakikisha taarifa zao zinasaidia katika ujenzi wa miundombinu nchini na pia kuwa na utaratibu mzuri wa kuziifadhi kisasa ili ziendelee kulisaidia taifa leo na hata hapo baadae zitakapo hitajika.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Kasekenya ameviomba vyombo vyote vya habari nchini kusaidia kusambaza taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA kwa wananchi ili ziweze kuwasaidia wananchi kujua na kufuata ushauri wa mamlaka. Alisema licha ya mamlaka hiyo kuchakata taarifa nzuri za hali ya hewa itakuwa kazi bure kama hazitawafikia wananchi mapema na ama kujihami au kujipanga kulingana na ushauri wa wataalam hao.

Awali akitoa taarifa kwa Naibu Waziri, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi alisema viwango vya utoaji wa taarifa sahihi vya TMA vimeendelea kuboreshwa mwaka hadi mwaka na kuishukuru Serikali kuongeza vifaa na wataalam pamoja na kuwaongezea ujuzi kielimu mara kwa mara.

"...Tunaishukuru Serikali kwa kutuwezesha kuanzia vifaa vya kisasa, wafanyakazi pamoja na kutuongezea ujuzi kielimu hii yote ni kutuwezesha kufanya kazi zetu vizuri zaidi. Tuna kuhakikishia tutaendelea kufanya kazi kiufanisi zaidi na kuzingatia maelekezo ya Serikali ili kulisaidia taifa," alisema Dkt. Agness Kijazi.

Share:

UZINDUZI KIJANISHA WILAYA YA IKUNGI-SINGIDA YASHIKA KASI

 

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo akiongoza zoezi la maadhimisho ya uzinduzi wa upandaji miti kitaifa kwa ngazi ya wilaya mkoani Singida hivi karibuni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi akishiriki zoezi hilo kikamilifu.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo (kulia)na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi kwa pamoja wakiwajibika kwenye maadhimisho hayo.

Mkuu wa Idara ya Usafishaji na Mazingira, Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Onesmo Rwehumbiza akipanda mti.

Mtendaji wa Kata ya Dung’unyi Yahaya Njiku na Kamanda wa Jeshi la Akiba wilaya ya Ikungi Massawe wakishiriki zoezi hilo.
Askari wa Jeshi la Akiba wakisikiliza hotuba ya DC Mpogolo kabla ya kuanza zoezi la kupanda miti kwenye maadhimisho hayo.
Watumishi wa Vitengo na Idara mbalimbali wakisikiliza hotuba ya DC Mpogolo kabla ya kuanza zoezi la kupanda miti kwenye maadhimisho hayo .
Maadhimisho ya uzinduzi wa upandaji miti yakiendelea.
Maadhimisho ya uzinduzi wa upandaji miti yakiendelea.
Maadhimisho ya uzinduzi wa upandaji miti yakiendelea.
Kazi ikiendelea.
Kazi ikiendelea.
Afisa Tawala wa Wilaya ya Ikungi akishiriki ipasavyo zoezi hilo..
Mhifadhi Misitu wa TFS kutoka Wilaya ya Ikungi, Wilson Pikoloti akishiriki maadhimisho hayo.

Mwonekano wa mradi wa ujenzi unaoendelea wa Majengo ya itakayokuwa Hospitali ya Wilaya ya Ikungi.

Afisa Tarafa wa Ikungi, Josephina Kadaso, akishiriki kupanda miti.

Na Dotto Mwaibale, Singida

MKUU wa Wilaya ya Ikungi mkoani hapa, Edward Mpogolo ameongoza mamia ya watumishi katika maadhimisho ya uzinduzi wa upandaji miti kiwilaya, ikiwa ni safari ya mwendelezo wa shabaha iliyopo ya hitaji la kufikisha idadi ya miti isiyopungua 709,000, huku kila kaya ikitarajia kupanda miti 10 kwa msimu wa 2020/2021.

Katika uzinduzi huo uliofanyika hivi karibuni, jumla ya miche ya miti 400 ilipandwa eneo la kijiji cha Muungano, mahali unapotekelezwa mradi wa ujenzi wa majengo ya itakayokuwa hospitali ya Wilaya ya Ikungi, huku miti mingine takribani elfu 30 inayozalishwa na TFS ikitarajiwa kusambazwa na kupandwa kwenye taasisi nyingine zote ndani ya wilaya hiyo.

“Shabaha yetu kwa mwaka huu kwanza ni kupanda zaidi ya miche laki saba lakini pia tunatarajia kupanda zaidi ya miche ya korosho milioni moja. Na kuhusu miche ya korosho tayari Jeshi la Kujenga Taifa hapa wilayani wameshazalisha zaidi ya miche laki 3…kikubwa tuendelee kuhamasishana,” alisema Mpogolo

Aidha, aliwataka wakazi wanaoishi ndani ya wilaya hiyo kuhakikisha idadi iliyopangwa ya kupanda miti 10 kwa kila kaya inatekelezwa kikamilifu kwa kiwango cha kuchanganya aina mbalimbali za miti ikiwemo ile ya mbao, lakini bila kusahau kupanda nje ya nyumba zao miti ya kivuli, miembe, korosho na palachichi.

Hata hivyo, aliwataka TFS kuongeza idadi ya uzalishaji miche kutoka elfu 30 iliyopo kwa sasa na kufikia angalau elfu 50 ili kukidhi hitaji la miti hiyo kwa kuzingatia jiografia ya ukubwa wa maeneo yanayozunguka wilaya hiyo ikiwa ni kubariki jitihada zinazoendelea katika kukabiliana na ukame.

“Kwa mwaka huu sitarajii tena kuona kuna upotevu wa miti, nikuombe Mkurugenzi tusimamie kikamilifu sheria zetu ndogondogo ili kutunza hii miti ambayo tumeanza kuipanda leo na tutakayoendelea kuipanda kwa mwaka mzima. Msiruhusu mifugo iwe sababu ya upotevu wa miti yetu,” alisema Mpogolo na kuongeza:

“Tumeamua kufanya uzinduzi huu kwenye hospitali hii sababu tunataka wagonjwa wetu wanapofika hapa wapumzike vizuri na wapate kivuli na hewa safi. Rais John Magufuli ametupatia jumla ya shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa majengo haya ya hospitali yetu ya wilaya…tunataka siku akija kuizindua basi akute kuna mazingira rafiki na uoto wa miti ya kutosha.”

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya aliagiza kuhakikisha wale wote waliovamia maeneo ya misitu ya Minyughe na Mlilii wanaondoka mara moja ili kuokoa bionuai za misitu hiyo iliyopo ndani ya wilaya ya Ikungi, ambayo siku hadi siku imeendelea kuathiriwa na uvamizi huo unaenda sambamba na shughuli za kibinadamu.

“Kwa bahati nzuri TFS kwa kushirikiana na Halmashauri wameanza kutenga baadhi ya maeneo na tumeshaanza kuangalia athari zilizojitokeza kwenye misitu hiyo ili kukamilisha taratibu zote kuwezesha msitu kupimwa na kupata GN ili tuweze kuumiliki kisheria,” alisema.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ikungi Justice Kijazi alisema uoto wan chi yetu ni kitu muhimu na ili tuweze kurithisha uoto huo kwenye kizazi kinachokuja tunapaswa kutengeneza mazingira mazuri ya upandaji miti kama zoezi endelevu kwa mfano wa tukio la uzinduzi huo.

Alisema kwa Halmashauri ya Ikungi kuanzia mwaka 2016/2020 imefanikiwa kupanda miti 1,385,900 lakini kati ya hiyo iliyopona mpaka sasa ni 145,860 sawa na asilimia 63.

“Tatizo kubwa linalosababisha uharibifu wa miti inayopandwa ni mifugo inayozunguka kwenye maeneo yetu. Natambua mifugo ni neema lakini wengi wetu tunaifuga kiholela,” alisema Kijazi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Usafishaji na Mazingira, Halmashauri ya Ikungi, Onesmo Rwehumbiza, alimweleza Mkuu wa Wilaya kwamba kuna misitu miwili ya asili ya Hifadhi, yaani Miili na Minyughe, lakini misitu hii kwa sasa imevamiwa na watu zaidi ya 1200 kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya wilaya ya ikungi.

“Pamoja na halmashauri ya wilaya kujitahidi kuweka mabango ya kukataza mtu yeyote kuingia kwenye hifadhi hizo lakini bado wananchi wanakaidi agizo hilo kwa kuendelea kuingia hifadhini na kufanya uharibifu mkubwa kwenye misitu hiyo ya asili,” alisema Rwehumbiza.


Share:

Breaking News : ANGALIA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA PILI, DARASA LA NNE, KIDATO CHA NNE NA MAARIFA 2020

Share:

KUWA WA KWANZA KUPOKEA HABARI UKIWA NA APP YA MALUNDE 1 BLOG...PAKUA HAPA IMEBORESHWA 2021

Share:

HII HAPA ORODHA YA WANAFUNZI 10 BORA KITAIFA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2020


Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya kidato cha nne huku wavulana wakiongoza katika orodha ya wanafunzi 10 bora.

Katika orodha ya wanafunzi 10 bora, wavulana wapo saba na wasichana watatu.

Matokeo hayo yametangazwa leo Ijumaa Januari 15, 2021 na katibu mtendaji wa baraza hilo, Dk Charles Msonde.

Shule ya sekondari Cannosa ndiyo iliyong'ara zaidi kwa kuingiza wanafunzi watatu kwenye 10 bora.

Kulingana na orodha hiyo, Paul Luziga wa Panda Hill ameshika nafasi ya kwanza akifuatiwa na msichana Justina Gerald wa Canossa.

Mwanafunzi wa tatu ni Timothy Segu wa (Mzumbe), Isaya Rukamya(Feza Boys), Ashraf Ally (Ilboru), Samson Mwakabage (Jude), Derick Mushi (Ilboru).


Wengine walioingia kumi bora ni Layla Atokwete (Canossa), Innocent Joseph (Mzumbe) na nafasi ya 10 ikishikwa na Lunargrace Celestine wa Canossa.

Bofya Link kuona

πŸ‘‰MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020

Share:

Breaking : MATOKEO YA KIDATO CHA PILI, DARASA LA NNE, KIDATO CHA NNE NA MAARIFA 2020 KUTANGAZWA



MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE NA MAARIFA, UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI NA DARASA LA NNE KWA MWAKA 2020 YANATARAJIWA KUTANGAZWA HIVI PUNDE.






Share:

Equipment Control Executives at Inchcape Shipping Services

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Equipment control executives     Inchcape shipping services is a global organization providing a services through a connected world in which our customers trade successfully and make better decision in every port. We are expanding our Linear business in Tanzania and are inviting ambitious capable candidates with experience in the shipping and marine industry to apply […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Customer Services Imports/Exports at Inchcape Shipping Services

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Customer services imports/exports     Inchcape shipping services is a global organization providing a services through a connected world in which our customers trade successfully and make better decision in every port. We are expanding our Linear business in Tanzania and are inviting ambitious capable candidates with experience in the shipping and marine industry to apply […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MAENEO YENYE MIFUMUKO YA MADINI LAZIMA YARASIMISHWE - PROF. MANYA

Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akingumza jambo na baadhi ya wadau wa Madini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu.

 Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya katikati, kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka na kulia ni Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula  wakiwa kwenye kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo

Baadhi ya wadau wa Sekta ya Madini wakifuatilia kikao cha Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya.
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akitoa ufafanuzi mara baada ya kikao baina yake na wadau wa madini.
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akitoa ufafanuzi mara baada ya kikao baina yake na wadau wa madini.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula akizungumza jambo katika kikao cha Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya, kushoto ni Naibu Waziri wa Madini Prof. Manya

Jengo la Kituo cha Umahiri la Mkoa wa Simiyu

Na Tito Mselem Simiyu,

Imeelezwa kuwa mfumuko wa madini (Rush) ni dharura tu, lazima sehemu zote zenye mifumuko ya madini zirasimishwe ili maeneo hayo yaweze kuchangia maduhuli ya Serikali.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya kwenye kikao baina yake na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo.

Prof. Manya amesema mfumuko wa madini ni kitu cha mpito hakitaachiwa kiendelee kwa muda mrefu na badala yake kirasimishwe ili kisadie kwenye ushirikishwaji wa watanzania kwenye rasilimali ya madini ambayo watanzania wote wanatakiwa kunufaika nayo.

“Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alisema wachimbaji wadogo watafutiwe maeneo ya kuchimba ila lazima wazingatie taratibu na sheria ikiwa ni pamoja na kuwa na leseni ya uchimbaji madini husika”, alisema Prof. Manya.

Prof. Manya aliongeza kuwa, Mkoa wa Simiyu umebarikiwa kuwa na madini mbalimbali ikiwemo madini ya metali kama dhahabu, shaba na nikeli, madini ya ujenzi kama mawe, kokoto, moramu na mchanga, madini ya vito kama amethyst na madini ya viwandani kama chokaa na chumvi.

Aidha, Prof. Manya amesema baadhi ya wachimbaji na wadau wengine wa shughuli za madini hawaelewi vyema Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na Marekebisho yake ya mwaka 2017 kuhusu haki ya leseni ya madini na haki ya ardhi hivyo kupelekea wamiliki wa ardhi kutowaruhusu waliopewa haki ya leseni madini kutofanya makubaliano ya fidia katika maeneo yao na kupelekea shughuli za uchimbaji kutofanyika katika maeneo yaliyotolewa leseni.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula amesema Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini imeshafanya mazungumzo na baadhi ya mabenki ili wapatiwe mikopo wachimbaji wadogo wa madini na kuwatoa hofu ya kwamba wachimbaji wadogo hawakopesheki.

“Tuliziambia taasisi za kibenki kwamba wale ambao wana leseni hai wakopeshwe, hivyo wachimbaji wanapaswa kujiunga ili wapatiwe leseni na waondokane na mfumo walionao wa mifumuko ya madini ambapo wanachimba bila leseni, lazima leseni zitolewe na Rush zikome mara moja”, alisema Prof. Kikula.

Naye, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Yahya Samamba, amewataka wachimbaji wa mkoa wa Simiyu kupendana na kuachana na wivu, majungu, chuki na fitina na badala yake wachimbe kwa kushirikiana ili walete tija kwenye shughuli zao.

Pia Mhandisi Samamba amewapongeza watumishi wa Ofisi ya Madini ya Mkoa wa Simiyu kwa kuvuka lengo la makusanyo ya maduhuli ya Serikali ambapo walipangiwa wakusanye kiasi Tsh milioni 250 na badala yake wamekusanya Tsh bilioni 2.3 ambapo wamevuka lengo kwa zaidi ya asilimia 1700 ndani ya miezi sita.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger