Saturday, 1 February 2020

KATIBU TAWALA SINGIDA AANZA MWAKA 2020 NA SEKTA YA AFYA


Na John Mapepele

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Mageni Lutambi amesema Serikali haitamfumbia macho mdau yoyote wa utoaji wa huduma ya afya ambaye atafanya kazi kwa mazoea bila kuzingatia sheria na taratibu za utoaji huduma na kwamba kuanzia sasa Serikali itakaa na kupanga kwa pamoja ili kuwapatia wananchi huduma bora wakati wote kwa wananchi wa Mkoa wa Singida na taifa kwa ujumla.

Dkt. Lutambi amesema wakati akifungua mkutano wa maandalizi ya mpango kabambe wa afya, ustawi wa jamii na lishe Mkoa wa Singida ambapo kwa sasa kwenye Mkoa wa Singida umekuwa na wadau wengi wanaotoa huduma za afya kutokana na Serikali kuweka mazingira wezeshi lakini changamoto kubwa ni kuwa hakuna uelewa wa pamoja wa mdau gani anafanya nini katika eneo moja la utoaji wa huduma za afya.

Amesema Mkoa wa Singida ni kitovu cha nchi yetu ambapo watu kutoka sehemu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi hufika na kupita hivyo ni muhimu huduma inayotolewa katika mkoa huu kuwa katika kiwango cha kimataifa.

Aidha, amesema Mkoa wa Singida kuwa jirani na makao makuu ya nchi ni lazima uwe mkoa wa mfano katika utoaji wa huduma za afya ambapo amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida kuboresha huduma ili ifanane na hali halisi ya sasa.

Alisema ili kutekeleza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na John Pombe Magufuli kufikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo 2025 lazima sekta afya iratibiwe vizuri na wadau wote washirikiane na kupata namna ya utoaji wa huduma za afya ili wananchi waweze kupata afya bora.

“Ni kwa sababu hii ndiyo maana Serikali imeamua kuwakutanisha ili kujua namna bora ya kufanya shughuli hizo kwa manufaa ya taifa” alisema Katibu Tawala.

Alisema baada ya mkutano huu kila mdau atafahamu jinsi bora ya kufanya kazi baina yake na mwingine ambapo pia Serikali itatambua na kupanga ushiriki mzuri baina ya Serikali na wadau wote wa afya katika Mkoa wa Singida.

Dkt. Lutambi alisisitiza kuwa mpango huu ni nyenzo inayotumiwa na Timu ya uendeshaji wa afya mkoani Singida katika kupanga, kutekeleza, kusimamia na kutathmini shughuli mbalimbali za afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika Halmashauri zote na vituo vya kutolea huduma za afya na katika ngazi ya Jamii kila mwaka.

Akizungumzia ya baadhi ya mafanikio ya mpango huo kwa mwaka 2019, Mratibu wa ubia baina ya Serikali na Sekta Binafsi kwenye upande wa Afya Mkoa wa Singida, Dkt. Abdallah Balla alisema kumekuwa na kuongeza kiwango cha wajawazito kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Afya kutoka 86% (2018) hadi 99% (2019) kulingana na takwimu za NBS,kuongezeka kwa wateja wapya wa njia za kisasa za uzazi wa Mpango kutoka 27.4% (2018) hadi 32% (2019).

Dkt. Balla alisema kumekuwa na kupungua kwenye kiwango cha udumavu kutoka 34% (2014) hadi 29% (2018) Kuongeza kiwango cha uchanjaji kutoka 106% (2018) hadi 117% (2019).

Aidha, upimaji wa virusi vya UKIMWI ngazi ya jamii, kwa mwaka 2019 jumla ya wananchi 35,973 walipimwa na kati yao wateja 602 (46%) ya wagonjwa wapya waligundulika kuwa na maambukizi ya VVU na kuunganishwa na vituo vya kutolea huduma.

Aliongeza kuwa huduma ya tohara kinga kwa wanaumie ilitolewa kwa wanaume 31008 sawa na 94% ya lengo la mwaka, ikihusisha Halmashauri zote za Mkoa wa Singida.

Naye Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Singida Victorina Ludovick alimshukuru Dkt. Lutambi na kumhakikishia kuwa ataendelea kusimamia kikamilifu utolewaji wa huduma bora za afya katika Mkoa wa Singida.


Share:

Training Manager Job Vacancy at WASSHA

Position: Training Manager Job Summary Wassha is looking to employ a Training Manager with outstanding written, verbal and interpersonal communication skills. Minimum Qualification: Bachelor Experience Level: Mid level Experience Length: 2 years Job Description A Training Manager is expected to be a strategic thinker with fantastic organizational and time management skills. To ensure success, Training Manager should understand the… Read More »

The post Training Manager Job Vacancy at WASSHA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

ASSISTANT QUALITY ASSURANCE ANALYST Job at WASSHA

JOB TITLE: ASSISTANT QUALITY ASSURANCE ANALYST Job Summary We looking for Assistant Quality Assurance Analyst who be assisting in managing our call center. REPORTING TO: QUALITY ASSURANCE ANALYST DUTY STATION: DAR ES SALAAM Assistant Quality Assurance Analyst is responsible for  assessing the quality of the performance of our customer services officers who deal with our existing and potential customers… Read More »

The post ASSISTANT QUALITY ASSURANCE ANALYST Job at WASSHA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

36 Assistant Tutors & Tutors Jobs in Arusha February 2020

Overview An upcoming college in Arusha invites applications from suitable candidates with relevant qualifications and experience to apply for the following vacant positions to its Diploma and Certificate programmes in CLINICAL MEDICINE, NURSING AND MIDWIFERY, MEDICAL LABOROTORY SCIENCE, PHARMACY and COMPUTER SCIENCE. Job Title: Assistant Tutors (20 Posts) Qualifications: Diploma in Clinical Medicine (4 posts) Diploma in Nursing and Midwifery… Read More »

The post 36 Assistant Tutors & Tutors Jobs in Arusha February 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Non-Executive Director Job vacancy at DCB Commercial Bank Plc

Vacancy title: Non-Executive Director Deadline of this Job: 14 February 2020 Duty Station: Within Tanzania , Dar es Salaam , East Africa JOB DETAILS: DCB Commercial Bank Plc is one of the leading commercial banks in Tanzania. Established in 2002 The Board of Directors of DCB Commercial Bank Plc would like to invite applications from suitable candidates for the… Read More »

The post Non-Executive Director Job vacancy at DCB Commercial Bank Plc appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Independent Non-Executive Director Job vacancy at DCB Commercial Bank Plc

Vacancy title: Independent Non-Executive Director Deadline of this Job: 14 February 2020 Duty Station: Within Tanzania , Dar es Salaam , East Africa JOB DETAILS: DCB Commercial Bank Plc is one of the leading commercial banks in Tanzania. Established in 2002 The Board of Directors of DCB Commercial Bank Plc would like to invite applications from suitable candidates for… Read More »

The post Independent Non-Executive Director Job vacancy at DCB Commercial Bank Plc appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Processing Shift Coordinator Job at Alliance One

Company: At Alliance One our purpose is to transform people’s lives so that together we can grow a better world. We are the trusted provider of certified, sustainable and traceable agricultural products and ingredients to businesses and customers. We have 150 years of experience as a leading independent leaf tobacco merchant; serving the worlds multinational cigarette manufacturers. Our… Read More »

The post Processing Shift Coordinator Job at Alliance One appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Green Storage Supervisor Job at Alliance One

Company: At Alliance One our purpose is to transform people’s lives so that together we can grow a better world. We are the trusted provider of certified, sustainable and traceable agricultural products and ingredients to businesses and customers. We have 150 years of experience as a leading independent leaf tobacco merchant; serving the worlds multinational cigarette manufacturers. Our… Read More »

The post Green Storage Supervisor Job at Alliance One appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

 Leaf Accounts Coordinator Job at Alliance One

Company: At Alliance One our purpose is to transform people’s lives so that together we can grow a better world. We are the trusted provider of certified, sustainable and traceable agricultural products and ingredients to businesses and customers. We have 150 years of experience as a leading independent leaf tobacco merchant; serving the worlds multinational cigarette manufacturers. Our… Read More »

The post  Leaf Accounts Coordinator Job at Alliance One appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Assistant Lecturer (5 Post) Jobs at Muslim University of Morogoro (MUM)

Assistant Lecturer (5 Post) Muslim University of Morogoro (MUM) is a private higher learning institution owned by Muslim Development Foundation (MDF) with a vision of a higher education centre of excellence with cutting edge programs, responsive to the needs of the individual and the nation in a globalized world under the guidance of Islamic moral values. Application are invited… Read More »

The post Assistant Lecturer (5 Post) Jobs at Muslim University of Morogoro (MUM) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RC TELACK : MWAKA HUU TUNAINGIA MIKATABA YA KAZI NA WALIMU


Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela akizungumza na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa Mhe. Zainab Telack, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama Annamringi Macha na kulia ni Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza na Maafisa Elimu kata, Watendaji wa kata na Wakuu wa shule za msingi na sekondari(hawapo pichani) wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu, ambaye ni Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga Bw. Mohamed Kahundi akitoa mwongozo wa Wizara ya Elimu kuhusu upangaji wa vipindi shuleni katika kikao hicho
Baadhi ya washiriki wa kikao hicho wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa katika kikao hicho
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiwa darasani katika shule ya msingi Ukune, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu akifuatilia ufundishaji na ujifunzaji wa wanafunzi, kulia ni Katibu Tawala Mkoa Bw. Albert Msovela
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiagiza kukarabatiwa kwa viti na meza katika shule ya sekondari Ukune, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu 
***
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amesema mwaka huu 2020 ataingia mkataba wa kazi na Waratibu wa Elimu kata ili kuweka mikakati ya kuhakikisha ufaulu mzuri katika mitihani ya Taifa ya darasa la saba na kidato cha nne.

Akizungumza katika kikao cha pamoja na Watendaji wa kata, Waratibu Elimu kata na Wakuu wa shule za msingi na sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Wilaya ya Kahama jana tarehe 31/01/2020, Mhe. Telack amesema lengo la mikataba ni kuhakikisha kuwa kila mmoja anasimamia Elimu kikamilifu kwenye eneo lake ili kuongeza ufaulu.

"Mimi mwenyewe nitasaini Mikataba moja kwa moja na Waratibu Elimu kata nao watasaini na Wakuu wa shule pamoja na walimu, nataka kuona watoto wanatoka darasa la kwanza wanajua kusoma na kuandika, mjipangie mikakati ya kuondoa sifuri" amesema Telack.

Ili kufanikisha mkakati huo, Mhe. Telack amewataka Waratibu wa Elimu kata kuwasilisha kila mwezi taarifa ya maendeleo ya taaluma kwenye kila shule.

Aidha, amesema kuwa kuanzia mwezi Machi mwaka huu kila baada ya miezi miwili ifanyike mitihani ya kuwapima wanafunzi ili kubaini changamoto na kuzifanyia kazi.

Amesisitiza pia ni lazima kuhakikisha mitaala inakamilishwa ili wanafunzi wapate nafasi ya kufanya marudio kabla ya mtihani.

Telack amekemea tabia ya baadhi ya walimu kuwaachia wanafunzi kujisimamia ikiwemo kufuatlia mahudhurio yao wakati walimu wa madarasa wapo. "Walimu tumefikia pabaya, walimu wa madarasa hawafanyi kazi yao, sitaki kusikia"

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Elimu ambaye ni Afisa Elimu Mkoa, Bw. Mohamed Kahundi amewataka wasimamizi wote Elimu Mkoani hapa kufuata miongozo na maelekezo ya Wizara ya Elimu katika kuandaa ratiba za vipindi ili kukamilisha mitaala.

"Tusibadilishe miongozo na melekezo ya Wizara katika kuandaa vipindi" ,amesema Kahundi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewapa siku tatu Wakuu wote wa shule za msingi na sekondari Mkoani hapa kukarabati madawati, viti na meza kwa fedha ya ukarabati inayoletwa na Serikali kila mwezi.


Share:

SERIKALI IMEBORESHA KANUNI ZA USIMAMIZI ELEKEZI WA MAZINGIRA


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima amesema Serikali imeboresha Kanuni za Usimamizi Elekezi wa Mazingira ili kurahisisha na kuharakisha utoaji wa vibali vya tathmini ya mazingira.

Sima ametoa kauli hiyo jana bungeni jijini Dodoma wakati akichangia taarifa ya Kamati ya Viwanda, Biashara na Viwanda ya kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 ambayo pamoja na mambo mengine ilizungumzia urasimu wa kutoa vibali.

Alisema kuwa kupitia maboresho hayo sasa wataalamu hao wanaotambuliwa na Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) sasa utendaji kazi wao utaboreka kwakuwa kipengele cha kanuni hizo kitawabana wafanyde kazi kwa ueledi zaidi.

“Hili jambo tumelichukua kama lilivyo ili sasa twende tukakae na wataalamu wetu tukaweke njia sahihi kuondoa urasimu na tunatambua tumebadilisha kanuni lakini pia tunatambua katika suala la vibali leo tunatoa vibali vya muda mfupi ndani ya siku saba mtu anapata kibali wakati anasubiri kibali cha tatmnini ya mazingira ambacho kinachukua muda mrefu na ndio maana inawezekana wawekezaji wanaona kama kuna urasimu,” alisema.

Kwa upande mwingine kuhusu udhibiti wa biashara ya vyuma chakavu Naibu waziri aliwaondoa hofu wafanyabishara wa vyuma chakavu kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Wizara za Fedha na Mipango, Viwanda na Biashara pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha tunalinda miundombinu isiharibiwe.

Hata hivyo Naibu Waziri Sima alikiri kuwa ipo changamoto ya uelewa mdogo wa masuala ya mazingira miongoni mwa baadhi ya wananchi ambapo alisema Ofisi hiyo imeendelea kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari na semina ili kulipa uelewa kundi hilo la watu.


Share:

Taarifa Kwa Umma: Kusitishwa Kwa Matumizi ya Passport za Zamani




Share:

Naibu Katibu mkuu Wizara ya mambo ya ndani Ramadhan Kailima Awasili TAKUKURU Kuhojiwa

Naibu Katibu mkuu Wizara ya mambo ya ndani Ramadhan Kailima amewasili  TAKUKURU Makao Dodoma  majira ya saa 8:50 asubuhi  kwa ajili ya kuhojiwa akiwa na gari ya  Land cruiser T.830 DNL
 
Kailima alikwepa kuingilia lango kubwa la mapokezi akaingilia lango dogo la moja kwa moja hadi chumba cha mahojiano ili kukwepa kamera za wanahabari.

Naibu  waziri wa Mambo ya ndani Hamad Masauni atawasili saa sita mchana


Share:

Uingereza yajitoa rasmi Umoja wa Ulaya

Uingereza imeondoka rasmi katika Umoja wa Ulaya saa sita usiku tarehe 31 Januari 2020 kwa saa za Brussels, Ubelgiji kwa mujibu wa makubaliano, na imekuwa ni nchi ya kwanza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya katika historia ya umoja huo.

Mchakato wa kujitoa kwenye umoja huo uliodumu kwa miaka mitatu na nusu umekamilika jana, ambapo pia utakuwa ni mwanzo wa uhusiano wa aina mpya kati ya Uingereza na Umoja wa Ulaya katika siku za mbele.

Baada ya kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya, Uingereza itakuwa na kipindi cha mpito cha miezi 11 hadi tarehe 31 Desemba 2020. Katika kipindi hicho, pande hizo mbili zitafanya mazungumzo kuhusu uhusiano baina yao, ambapo ajenda kubwa itakuwa ni kufikia makubaliano ya biashara huria.

Hata hivyo muda wa miezi 11 ni mfupi kuweza kukamilisha mazungumzo hayo, na matokeo yake yatajulikana baadaye. Uingereza ilijiunga kama mwanachama mwaka 1973.


Share:

Makonda apigwa marufuku kuingia Marekani

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amepigwa marufuku kuingia Marekani.

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani jana  Ijumaa, Januari 31 2020 marufuku hiyo pia inamhusisha mke wa Makonda Bi Mary Felix Massenge.




Share:

Naibu Waziri Shonza: Wazazi Ndiyo Walezi Wa Kwanza Wa Mtoto

Na Anitha Jonas – WHUSM
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza amewataka wazazi na familia kuwa walezi wa kwanza kwenye jukumu la kumlea mtoto.

Mheshimiwa Shonza ametoa kauli hiyo jana  Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe.Mgeni Jadi Kadika (CUF) lilikokuwa likisema serikali haioni sasa ni wakati muafaka kwa vijana wetu kuwekewa umri maalumu wa kutumia mitandao ili kupunguza mmomonyoko wa maadili.

Akijibu swali hilo la msingi Mhe.Shonza alisema kuwa ni kweli utandawazi umechangia sana katika kuleta mmomonyoko wa maadili kwa kiasi kikubwa kwa jamii zetu hususani vijana kupitia intaneti,mitandao ya kijamii na maudhui ya nje kupitia muziki na filamu na ndiyo maana serikali ilileta Sheria ya Makosa ya Mtandao (Cybercrime Act) ya Mwaka 2015 pamoja na Kanuni za Maudhui ya Mtandao na Maudhui ya Redio na Runinga za Mwaka 2018.

‘’Serikali iliiona changamoto hii mmomonyoko wa maadili na ndiyo maana ikaunda Sheria hiyo ambayo ilipigiwa sana kelele ndani na nje ya nchi kuwa ibana uhuru ,‘’alisema Shonza.

Mhe.Shonza akiendeleza kuzungumza wakati ajibu swali la hilo alisisitiza kuwa familia na wazazi ndiyo wenye jukumu la ujumla la kumlea mtoto na taasisi za elimu ya awali,Msingi,Sekondari hadi Elimu ya Juu ambao huwaelimisha kwa maneno na vitendo watoto na vijana kuhusu utambuzi wa mambo mema na mabaya yanayofaa na yasiyofaa, na baada ya hatua hizo ndipo wajibu mkubwa wa serikali unapojitokeza.

Akiendelea kujibu swali la nyongeza la mbunge huyo lilihoji je, serikali haioni haja kufanya kama nchi zilizoendelea kuzuia watoto kuingia katika mitandao na kuangalia picha chafu katika mitandao,Naibu Waziri huyo alijibu kwa kusema kuwa serikali imekwisha fanya kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuunda sheria zinazosimamia masuala hayo, hivyo alitoa wito kwa viongozi kuwa wakwanza kuzisimamia sheria hizo na alisisitiza kuwa suala la malezi ya watoto siyo la serikali peke yake bali ni pamoja na wazazi.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger