Saturday, 1 February 2020

Naibu Waziri Shonza: Wazazi Ndiyo Walezi Wa Kwanza Wa Mtoto

Na Anitha Jonas – WHUSM
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza amewataka wazazi na familia kuwa walezi wa kwanza kwenye jukumu la kumlea mtoto.

Mheshimiwa Shonza ametoa kauli hiyo jana  Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe.Mgeni Jadi Kadika (CUF) lilikokuwa likisema serikali haioni sasa ni wakati muafaka kwa vijana wetu kuwekewa umri maalumu wa kutumia mitandao ili kupunguza mmomonyoko wa maadili.

Akijibu swali hilo la msingi Mhe.Shonza alisema kuwa ni kweli utandawazi umechangia sana katika kuleta mmomonyoko wa maadili kwa kiasi kikubwa kwa jamii zetu hususani vijana kupitia intaneti,mitandao ya kijamii na maudhui ya nje kupitia muziki na filamu na ndiyo maana serikali ilileta Sheria ya Makosa ya Mtandao (Cybercrime Act) ya Mwaka 2015 pamoja na Kanuni za Maudhui ya Mtandao na Maudhui ya Redio na Runinga za Mwaka 2018.

‘’Serikali iliiona changamoto hii mmomonyoko wa maadili na ndiyo maana ikaunda Sheria hiyo ambayo ilipigiwa sana kelele ndani na nje ya nchi kuwa ibana uhuru ,‘’alisema Shonza.

Mhe.Shonza akiendeleza kuzungumza wakati ajibu swali la hilo alisisitiza kuwa familia na wazazi ndiyo wenye jukumu la ujumla la kumlea mtoto na taasisi za elimu ya awali,Msingi,Sekondari hadi Elimu ya Juu ambao huwaelimisha kwa maneno na vitendo watoto na vijana kuhusu utambuzi wa mambo mema na mabaya yanayofaa na yasiyofaa, na baada ya hatua hizo ndipo wajibu mkubwa wa serikali unapojitokeza.

Akiendelea kujibu swali la nyongeza la mbunge huyo lilihoji je, serikali haioni haja kufanya kama nchi zilizoendelea kuzuia watoto kuingia katika mitandao na kuangalia picha chafu katika mitandao,Naibu Waziri huyo alijibu kwa kusema kuwa serikali imekwisha fanya kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuunda sheria zinazosimamia masuala hayo, hivyo alitoa wito kwa viongozi kuwa wakwanza kuzisimamia sheria hizo na alisisitiza kuwa suala la malezi ya watoto siyo la serikali peke yake bali ni pamoja na wazazi.


Share:

Mahakama Kenya yazuia wananchi kusajiliwa kwa alama za vidole

Mahakama Kuu Kenya imesitisha kutekelezwa kwa mfumo wa usajili wa wananchi kwa njia ya alama za vidole hadi hapo sheria ya kulinda taarifa itakapopitishwa.

Mbali na kuzuia utekelezaji huo, mahakama imesema kuwa kukusanya taarifa za eneo (GPS) na vinasaba (DNA) ni kinyume na katiba ya nchi.

Serikali ya Kenya imekuwa ikikusanya taarifa mbalimbali katika usajili huo ikiwa ni pamoja na alama za vidole, taarifa za familia, na eneo kamili mtu analoishi.

Wakati wa zoezi hilo ambalo serikali ilisema ni la lazima wale wote ambao hawatojiandikisha hawatopata huduma za msingi za serikali kama vile pasi ya kusafiria (passport), na cheti cha kuzaliwa.

Mahakama imezuia zoezi hilo kwa kile ilichoeleza kwamba wananchi wanaweza kujikuta katika hatari isiyorekebishika endapo taarifa zilizokusanywa zitatumiwa vibaya.

Majaji watatu wa mahakama hiyo waliamuru kusitishwa kwa mpango huo unaofahamika kama Huduma Namba hadi sheria ya kina ya kulinda taarifa zinazotolewa na wananchi upitishwe.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi February 1


















Share:

Friday, 31 January 2020

PICHA: Aliyekuwa Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani balozi Jacob kingu Naye Awasili TAKUKURU Kuhojiwa

Aliyekuwa Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi, balozi Jacob kingu amefika ofisi za Takukuru jijini hapa kwa ajili was mahojiano kufuatia agizo la Rais John Magufuli kuhusu mkataba tata wa Tsh trilioni 1 wa ununuzi wa vifaa vya zimamoto.  


Kingu ametanguliwa na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Kangi Lugola


Share:

Intern Opportunity at Tegeta Branch NBC

Intern Tegeta Branch NBC NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Description No role profile available as this role has no assigned corporate grade: This role should not be used to create new positions.… Read More »

The post Intern Opportunity at Tegeta Branch NBC appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rais Magufuli ateua wenyeviti watatu wa bodi.




Share:

Packaging Engineer at SBL Dar es Salaam

Packaging Engineer SBL Dar es Salaam, Tanzania Job Description : Context/Scope: Serengeti Breweries Ltd (SBL), a subsidiary of East Africa Breweries Ltd (EABL) operates exclusively in Tanzania and is the 2nd largest beer company. The company is an integrated demand/supply business with 3 operational breweries in Dar Es Salaam, Mwanza, and Moshi. SBL’s flagship brand is Serengeti Premium… Read More »

The post Packaging Engineer at SBL Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Head of Corporate & Investment Banking at NBC Head Office

Head of Corporate & Investment Banking Head Office NBC NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Description Commercial/Business Leadership:: Enterprise leadership of a banking product or function; Coordinates activities at a product or functional… Read More »

The post Head of Corporate & Investment Banking at NBC Head Office appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HR Manager at SICPA Tanzania

HR Manager Req ID: 15868 Posted on: 30-Jan-2020 Location: Dar Es Salaam (TZ10), Tanzania Department: ID-Human Resources & General Administration (50007 Job Family: Human Resources HUMAN RESOURCES MANAGER Fundamental Purpose: Responsible for staffing the needs of SICPA Tanzania, this will involve an active recruitment across Tanzania within short time frame, focus on integration and retention of employees and… Read More »

The post HR Manager at SICPA Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WHO yatangaza virusi vya corona kuwa hali ya dharura

Shirika la Afya UIimwenguni - WHO limetangaza mlipuko wa virusi vipya vya corona nchini China ambavyo vimesambaa katika nchi nyingine kadhaa kuwa hali ya dharura ya kimataifa. 

Hii ni baada ya visa vya maambukizi ya virusi hivyo kusambaa kwa kasi katika kipindi cha wiki moja, ikiwemo idadi ya vifo vya watu 24 viliyotokea katika saa 24 leo Ijumaa. 

China imeripoti wagonjwa 9,692 waliothibitishwa kuambukizwa huku idadi ya vifo ikifikia 214. Nyingi ya visa hivyo vimeripotiwa katika mkoa wa Hubei na mji mkuu wake Wuhan, ambao ndio kitovu cha mlipuko huo. 

Hakuna vifo vilivyoripotiwa nje ya China. Akizungumza na wanahabari mjini Geneva, Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus ametaja hofu iliyopo ya kusambaa kwa virusi hivyo miongoni mwa watu nje ya China.

 Amesema tangazo hilo la hali ya dharura sio la kura ya kutokuwa na imani na China. Badala yake, WHO inaendelea kuwa na imani na uwezo wa China kuudhibiti mripuko huo.


Share:

Spika Ndugai Asema Wanamsubiri Zitto Kabwe awaeleze kwanini aliandika barua kwa benki ya dunia kuzuia mkopo kwa ajili ya elimu nchini

Spika wa Bunge, Job Ndugai Leo Ijumaa Januari 31, 2020 amesema wanamsubiri Mbunge Zitto Kabwe awaeleze kwanini aliandika barua kwa benki ya dunia kuzuia mkopo kwa ajili ya elimu nchini 

Fedha za mkopo huo ambazo ni zaidi ya Sh1.2 Trilioni zingeelekezwa katika programu za shughuli za elimu.

Kikao hicho kilipangwa kufanyika Jumanne Januari 28, 2020  kwa ajili ya kuidhinisha mkopo huo, lakini kikaahirishwa dakika za mwisho kutokana na kile kilichoripotiwa na vyombo vya habari vya nje kuwa ni ombi la taasisi ya kijamii ambayo ina wanachama wake Tanzania.

“Mtu unaweza kuwa na tofauti na sera au mtazamo kati ya wewe mbunge au upande wa Serikali na kadhalika, lakini kufikia mahali pa ‘kublock’ Tanzania isipate fursa fulani nadhani ni kwenda mbali mno.

“Kwa sababu watoto watakaokosa fursa hiyo ni watoto wa Tanzania ni walimu wa Tanzania ni miundombinu ya elimu ya Tanzania, sijui katika hilo kama mbunge unanufaika nini maana kama ni suala la utofauti la kisera haya ni mambo ya kujadiliana tu,” amesema Spika Ndugai.

Katika kusisitiza hilo, Spika Ndugai amesema, “ningependa kutoa ushauri wa ujumla tu kwamba ni vema kutumia fursa yetu kama wawakilishi wa wananchi tukaelimishana tukaelezana kuliko kuwakosesha Watanzania fursa wakati baadhi yetu watoto wetu wapo Feza Boys, wapo Marian Girls halafu unablock msaada kwa watoto walio wengi wa wapiga kura wetu jambo ambalo halifai kabisa.”


Share:

Waziri Mkuu: Serikali Haiwezi Kufuta uchaguzi wote wa Serikali za Mitaa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema licha ya kuwepo kwa ugatuaji wa madaraka (D by D), Serikali za Mitaa bado zina wajibu wa kuwahudumia wananchi kwa sababu ziko karibu nao zaidi kuliko Serikali Kuu.

Ametoa kauli hiyo jana (Alhamisi, Januari 30, 2020) bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Bi. Ruth Mollel, kwenye kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu bungeni. Mbunge huyo alisema dhana ya ugatuaji wa madaraka inakinzana na hali halisi kwani utekelezaji wake haujaenda sawasawa kwa vile Serikali inakusanya fedha kutoka kwenye vyanzo vya mapato vya Halmashauri kama vile kodi ya majengo na mabango.

“Wajibu wa kumhudumia mwananchi ni wa Serikali za Mitaa kwa sababu iko karibu nao zaidi. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kuwa tunashirikiana na Serikali za Mitaa kumhudumia mwananchi lakini hatujaondoa wajibu wa Serikali za Mitaa kuwahudumia wananchi,” amesisitiza.

Amesema Serikali Kuu bado inalo jukumu la kusimamia mapato na imeamua kudhibiti ukusanyaji wa mapato na imekuwa ikihakikisha mapato haya yarudi tena kwa wananchi. “Tunaporudisha kwa wananchi, tunawapelekea hao hao Serikali ya Mitaa kwa mahitaji yao ili watekeleze hilo jambo, hatujawaondolea mamlaka ya kusema tunahitaji darasa, tunahitaji kituo cha afya, tunahitaji uboreshaji wa miundombinu.”

“Tumeongeza hata taasisi kwa kuunda TARURA ili isimamie miundombinu; sasa hivi tunaenda kwenye maji, kutakuwa na taasisi ya kusimamia utoaji wa maji. Pale ambapo kuna mahitaji, Mamlaka ya Serikali za Mitaa iseme inahitaji shilingi ngapi, kwa ajili ya nini, nasi tunawapelekea, ndiyo kwa sababu leo tunaona huduma zinatekelezwa mpaka vijijini. Hii ni kwa sababu tunashirikiana na Serikali za Mitaa katika kuratibu.”

“Ule udhaifu wa usimamizi wa makusanyo, na udhaifu wa usimamizi wa matumizi ambao ulikuwa umejitokeza sasa tunaendelea kuutibu na ndiyo kwa sababu unaona wakati wote tunapokwenda huko kwenye ziara, kwanza tunauliza ukusanyaji na kama makusanyo yoyote yamehifadhiwa na matumizi yake yako sawa, na pale ambapo matumizi yanakuwa si sahihi tunachukua hatua,” amesema.

Amesema kutokana na muundo uliopo, zipo Serikali za Mitaa ambazo zina majukumu yake yaliyoainishwa rasmi na kuna Serikali Kuu ambayo pia inawajibika kuzihudumia Serikali za Mitaa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema haitaleta maana endapo Serikali italazimika kutengua matokeo ya uchaguzi wote wa Serikali za Mitaa wakati wagombea ambao hawakuridhishwa na matokeo hayo walikuwa na fursa ya kukata rufaa.

“Chaguzi zote nchini zinatawaliwa na kanuni na sheria zake. Kila mmoja aliyeshiriki kama aliona kuna ukiukwaji wowote, alikuwa na fursa ya kukata rufaa na kama hajaridhika, alikuwa na fursa ya kwenda mahakamani,” alisema.

Alisema chaguzi zote zina sheria zake na kanuni zake na hata wakati wa kuandaa kanuni za Serikali za Mitaa, vyama vyote vya siasa vilishirikishwa katika kutengeneza kanuni zao na moja kati ya kanuni hizo ni pale ambapo inatoa fursa kwa yeyote ambaye hajaridhika huko anakogombea, anaweza kukata rufaa na atakapoona rufaa hiyo kwenye ngazi inayofuata haikutenda haki, aende mahakamani.

“Kwa hiyo kulichukua hili kwa ujumla ujumla, inaweza isiwe sahihi sana kwa sababu kila mmoja kule alipo, alikuwa na mamlaka yake inayoratibu na anayo fursa ya kwenda kwenye mamlaka kukatia rufaa pale ambapo hajaridhika na utekelezaji wa jambo hilo. Na vyama vyote vilishiriki kwenye hii kanuni ya kukata rufaa, kwa hiyo ni wajibu wa huyo mgombea kwenye eneo hilo kwenda kukata rufaa,” alisema.

Alikuwa akijibu swali la mbunge wa Mbozi, Bw. Pascal Haonga, aliyetaka kujua kama Serikali iko tayari kurudia uchaguzi wa Serikali za Mitaa wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu kwa sababu ule uliopita uligubikwa na dosari nyingi.

“Mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019, uligubikwa na dosari nyingi sana zikiwemo za wagombea kutoka vyama vya upinzani kunyimwa fomu, ofisi kufungwa kwa muda wote, hivyo kupelekea baadhi ya wagombea hasa wa upinzani kushindwa kupata fursa za kugombea. Serikali haioni kwamba ni vema uchaguzi wa Serikali za Mitaa uweze kurudiwa sambamba na uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu?” alihoji.


Share:

Tanzanian Consultant to Manage HIV Data Collection

Tanzanian Consultant to Manage HIV Data Collection Company Overview: Palladium is a global leader in the design, development and delivery of Positive Impact – the intentional creation of enduring social and economic value. We work with foundations, investors, governments, corporations, communities and civil society to formulate strategies and implement solutions that generate lasting social, environmental and financial benefits. … Read More »

The post Tanzanian Consultant to Manage HIV Data Collection appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Madini na Viwanda Vyaleta Mageuzi ya Uchumi Nchini

Na. Immaculate Makilika – MAELEZO
Mauzo ya bidhaa nje ya nchi zisizo kuwa za kawaida yameongezeka kwa asilimia 41.9 kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mwezi  Novemba, mwaka jana.

Hayo yamesemwa jana Jijini Dodoma  na Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari .

Dkt. Abbasi amesema kuwa kupitia jitihada mbalimbali zinazochagizwa na Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli zimesaidia kuongeza ukusanyaji wa mapato, kuongeza mauzo ya bidhaa muhimu kwenda nje na ukuaji wa viwanda nchini  ikiwa ni sehemu muhimu ya  mageuzi ya uchumi nchini.
 
 “Wote mnafahamu kuwa Serikali imechukua hatua kubwa kuanzisha masoko ya madini na kuzuia uuzaji holela na utoroshaji wa madini. Matokeo yake tumeanza kufaidi. Hadi Novemba, 2019, mauzo ya dhahabu nje ambayo ni asilimia 51.4 ya mauzo yote ya bidhaa nje ya nchi yaani bidhaa zisizo za kawaida, yaliongezeka kwa asilimia 41.9 kufikia kiasi cha Dola Bilioni 2.1”, alisema Dkt. Abbasi
 
Aidha, aliongeza kuwa  “sera ya kuchagiza ujenzi wa viwanda nayo imezidi kulipa, ambapo  mauzo ya bidhaa za viwandani nje ya nchi  yameongezeka kwa asilimia 28.4 kufikia Dola milioni 996.0 ikichangiwa zaidi na bidhaa za chuma na mabati, vioo, tumbaku, katani na mbolea. 
 
Jitihada hizo za Serikali zimeendelea kusaidia kuongeza ajira kwa watanzania, sambamba na kuwa vyanzo vipya vya mapato huku vikitazamiwa kusaida uboreshaji wa huduma za kijamii.
 
Mwisho


Share:

Serikali Yasema Mkopo wa Benki ya Dunia wa Dola za Marekani Milioni 500 kwa nchi ya Tanzania haujasitishwa bali majadiliano yanaendelea.

Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Dk Hassan Abbasi amewatoa hofu Watanzania kuhusu madai kuwa Benki ya Dunia (WB) imesitisha kutoa mkopo wa masharti nafuu wa Dola 500 milioni za Kimarekani kwa Tanzania, akibainisha kuwa bado wapo kwenye mazungumzo.

Ameeleza hayo jana Alhamisi Januari 30, 2020 katika mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma.

Dk Abbasi ameeleza hayo baada ya kikao cha bodi ya utendaji ya Benki ya Dunia ambacho kingetoa uamuzi kuhusu kuruhusu mkopo huo kuripotiwa kuahirishwa.
 
Kikao hicho kilipangwa kufanyika Jumanne Januari 28, 2020  kwa ajili ya kuidhinisha mkopo huo, lakini kikaahirishwa dakika za mwisho kutokana na kile kilichoripotiwa na vyombo vya habari vya nje kuwa ni ombi la taasisi ya kijamii ambayo ina wanachama wake Tanzania.

Kabla ya kuahirishwa kwa kikao hicho, mkurugenzi anayehusika na haki za watoto wa taasisi ya kimataifa inayojishughulisha na haki za binadamu ya Human Rights Watch (HRW), Zama Neff aliiomba WB kuchelewesha fedha hizo hadi suala la wasichana wanaopata mimba shuleni litakapopatiwa ufumbuzi kuhusu mustakabali wa elimu yao.

Katika maelezo yake , Dk Abbasi amesema, “walipanga kukutana siku fulani, mmoja wa wawakilishi wao aliomba wakutane leo,  mtu anatoka hapo mishipa imekutoka eti mkopo umesitishwa,sio kweli.... kukopa unaweza kuomba benki moja ukakosa nyingine ikakubali kwa hiyo ni majadiliano yanaendelea.”

==>>Msikilize hapo chini


Share:

Uchumi wa Tanzania Wazidi Kukua na Kuimarika

Na Immaculate Makilika - MAELEZO
Hali ya uchumi wa Tanzania imezidi kuimarika na kukua  kwa asilimia 6.9 ikiwa ni  takwimu za hadi mwezi Septemba 2019, huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 7.0% na 7.1% .

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) Januari 20 mwaka huu, inaonesha  kuwa uchumi wa dunia utakua kidogo kutoka asilimia 2.9 hadi asilimia 3.3 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2019/20.

Akizungumza na waandishi wa habari, jana jijini Dodoma, kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Serikali, Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alisema kuwa, huu ni ukuaji mkubwa katika nchi za Afrika Mashariki nyuma ya Rwanda pekee na bado Tanzania ni miongoni mwa nchi za juu kwenye ukanda wa  Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Afrika kwa ujumla.

Dkt. Abbasi alisema kuwa sekta inayoongoza kwa ukuaji wa uchumi ni ujenzi ambayo inachangia asilimia 16, uchimbaji madini na mawe asilimia 13.7, habari na mawasiliano 10.7, maji asilimia 9.1, na usafirishaji na uhifadhi wa mizigo asilimia 9.1.

Aidha, Dkt. Abbasi alisema kuwa, katika kipindi cha miaka mitatu Serikali ya Awamu ya Tano imefanikiwa katika ongezeko la ukusanyaji wa mapato kwa mwezi kutoka shilingi bilioni 850 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi trilioni 1.3.

“Leo ninayo furaha kulitangazia rasmi taifa kuwa kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato na Idara nyingine za Serikali, wastani wa mapato ya kodi kwa mwezi kati ya Julai hadi Disemba, mwaka 2019, umepanda na sasa ni shilingi trilioni 1.5 kwa mwezi. Hii kwa sasa ndio rekodi mpya, na ndio habari mpya ya mjini”, alisisitiza Dkt. Abbasi.

Ukusanyaji wa mapato ni moja ya vipaumbele muhimu vya Serikali ya Awamu ya Tano. Huku ikitazamia kujenga uwezo wa ndani wa kujitegemea kifedha na kupunguza kwa kadri inavyowezekana utegemezi kutoka kwa Wadau wa Maendeleo na kuhakikisha kwamba mipango ya kukuza uchumi na kupunguza umaskini inatekelezwa bila kukwama kwa sababu ya ukosefu wa fedha.

 Aidha, azma ya Serikali ya kuifanya Tanzania nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, haiwezi kufikiwa endapo Serikali haitokuwa na uwezo wa kifedha wa kugharamia shughuli mbali mbali za maendeleo.


Share:

IT Support Associate Job Opportunity at Sokowatch

IT Support Associate About Us: Sokowatch is transforming communities across Africa by revolutionizing access to essential goods and services. By connecting small shops to the digital economy, we fix inefficient supply chains and provide services that were previously unavailable. Sokowatch aims to provide everything a retailer needs, no wholesalers or banks necessary. Reporting To: Support Manager Location: Dar… Read More »

The post IT Support Associate Job Opportunity at Sokowatch appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger