Saturday, 18 January 2020

International Entrance Scholarship In Canada

Scholarship Description: International Entrance Scholarship in Canada is open for International Students The scholarship allows Bachelor level programm(s) in the field of All Subjects taught at University of Regina The deadline of the scholarhip is 15 Mar 2020. Degree Level: International Entrance Scholarship in Canada is available to undertake Bachelor level programs at University of Regina. Available Subjects:… Read More »

The post International Entrance Scholarship In Canada appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Uclan Asia Pacific Institute Scholarship

Scholarship Description: Uclan Asia Pacific Institute Scholarship is open for International Students The scholarship allows level programm(s) in the field of Asia Pacific Studies, North Korean Studies taught at University of Central Lancashire(UCLAN), UK Universities The deadline of the scholarhip is 16 Feb 2020. Degree Level: Uclan Asia Pacific Institute Scholarship is available to undertake level programs at… Read More »

The post Uclan Asia Pacific Institute Scholarship appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi January 18

















Share:

Erling-Persson International Awards (Masters In Public Health, Umea University)

Scholarship Description: Erling-Persson international awards (Masters in Public Health, Umea University) is open for International Students (all nationalities) The scholarship allows Masters level programm(s) in the field of Public Health taught at UmeÃ¥ University The deadline of the scholarhip is 01 Mar 2020. Degree Level: Erling-Persson international awards (Masters in Public Health, Umea University) is available to undertake… Read More »

The post Erling-Persson International Awards (Masters In Public Health, Umea University) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Friday, 17 January 2020

Baba amuua mwanaye kwa kumchoma moto makalioni

Na Silvia Mchuruza.
Jeshi la polisi mkoani Kagera linamshikilia Juma Daniel, mkazi wa Kijiji cha Kazingati kata ya Keza wilayani Ngara, kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa kumzaa, mwenye umri wa miaka miwili.
 
Daniel anadaiwa kumuuwa mwanaye huyo kwa kumchoma moto usoni na makalioni na kumjeruhi kwa kitu chenye ncha kali sehemu za haja kubwa, baada ya mtoto huyo kujisaidia haja kubwa kitandani wakati wamelala.
 
Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Revocatus Malimi, amesema kuwa Baba huyo alikwishatengana na mama mzazi wa mtoto huyo na kuoa mke mwingine. 
 
Aidha Kamanda Malimi alilitaja jina la mtoto huyo kuwa ni Bahati Juma, na kwamba alifanyiwa kitendo hicho cha kikatili Disemba 27, 2019 na hakupelekwa hospitali badala yake alianza kumtibu kienyeji nyumbani, na baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya baba huyo alitoroka.


Share:

Rais Vladimir Putin wa Urusi Ateua Waziri Mkuu Mpya Baada ya Baraza Zima la Mawaziri Kujizulu

Rais Vladimir Putin wa Urusi amemteua Mikhail Mishustin kuwa waziri mkuu mpya wa Russia. Mapema jana baraza la chini la bunge la Russia lilipitisha uteuzi huo kupitia upigaji wa kura.

Baada ya kuteuliwa Bw. Mishustin alitoa hotuba kwenye baraza la chini la bunge, na kuwashukuru rais Putin na baraza hilo kwa uungaji mkono wao, pia amesema ataripoti sera za serikali mpya kwa baraza la chini mnamo mwezi Aprili mwaka huu.

Vilevile amewaambia waandishi wa habari kuwa atakabidhi orodha ya mawaziri kwa rais Putin hivi karibuni.

Waziri mkuu wa zamani wa Russia Dmitry Medvedev ameteuliwa kuwa naibu mwenyekiti wa Baraza la usalama la Urusi.


Share:

Rwanda Yajiweka Kwenye Tahadhari Kubwa Kukabiliana na Nzige....Hadi sasa Wametafuna Hekta 70,000 za Mashamba Kenya, Somalia na Ethiopia

Rwanda iko kwenye tahadhari ya hali ya juu kufuatia uvamizi wa nzige unaoweza kutokea ambao kwa sasa wameonekana katika nchi kadhaa za Afrika Mashariki, zikiwemo Ethiopia, Kenya na Somalia. 

Waziri wa kilimo na rasilimali ya wanyama wa Rwanda Bibi Geraldine Mukeshimana amesema, wizara yake iko tayari kukabiliana na uvamizi huo wa nzige. 

Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa limesema, nzige wameharibu karibu hekta 70,000 za mashamba nchini Somali na Ethiopia, na kutishia utoaji wa chakula katika nchi hizo.


Share:

Tahadhari Ya Mvua Kubwa na Upepo kwa Siku 5

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya mvua kubwa na upepo mkali katika baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Lindi, Mtwara, Dar es Salaam, Zanzibar na Pwani kwa muda wa siku tano kuanzia jana.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, kuanzia jana hadi Jumapili, kunatarajiwa kuwapo upepo mkali na mawimbi makubwa kwa baadhi ya maeneo ya Pwani ya Bahari ya Hindi, hivyo kusababisha shida kwenye uvuvi na usafiri wa baharini.

"Kiwango cha mvua na upepo ni cha wastani, hivyo wananchi wachukue tahadhari katika shughuli zao," TMA ilieleza katika taarifa yake hiyo.

Ilisema athari huenda zikajitokeza kutokana na kusimama kwa shughuli za binadamu, kuharibika kwa miundombinu na makazi kuzingirwa na maji, hivyo kuna haja kuchukua tahadhari.

Mamlaka hiyo ilisema mvua inayonyesha sasa ni mwendelezo wa utabiri wa mvua za vuli ilioutoa kipindi cha nyuma na katika baadhi ya maeneo itaendelea hadi mwezi ujao.




Share:

7 Watiwa Mbaroni Kwa Kuwaua Kwa Mapanga Wanandoa Wawili

Watu  saba wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kagera, wakituhumiwa kuwaua wanandoa wawili kwa kuwakata sehemu mbalimbali za miili yao, chanzo kikidaiwa kuwa ni mgogoro wa ardhi.

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Revocatus Malimi, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea Januari 14 mwaka huu saa saba usiku katika Kijiji cha Mabale, Kata ya Nyakahura wilayani Biharamulo.

Alisema kuwa wakati wanandoa hao wakiwa wamelala, mlango wa nyumba yao ulivunjwa na kuvamiwa na kundi la watu ambao hawakufahamika na kuanza kuwakata kwa kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za miili yao na kusababisha kupoteza maisha papo hapo.

Aliwataja waliouawa katika tukio hilo kuwa ni Elizeus Rubanie (35) na mke wake, Juliana Joseph (28).

"Kabla ya tukio hilo, kulikuwa na mgogoro wa ardhi kati ya marehemu na baadhi ya wanaukoo kwa muda mrefu, uliotokana na kuachiwa eneo alilokuwa akiishi na babu yake, aliyehama kwa shinikizo la wanajamii waliomtuhumu kuwa ni mwizi," alidai.

Kamanda Malimi alidai kuwa baada ya babu huyo kuhama na kumwachia eneo hilo mjukuu wake, baadhi ya wanajamii waliungana na baadhi ya ndugu kwenye ukoo huo, hasa shangazi wawili wa marehemu, na kuanza kumsakama marehemu na familia yake na kumtolea vitisho.

Aliwataja wanaoshikiliwa kuwa ni Sophia Joseph (45), Joseph Magambo (47), Alphonce Karoli (37), Martine Makabe (36), Alex Leopord (44), Salvatory Mwiliza (38) na Aloyce Leopord (45).

Kamanda Malimi alidai upelelezi bado unaendelea ili kubaini watu wote waliohusika na tukio hilo, na kuwa watuhumiwa watafikishwa mahakamani wakati wowote baada ya upelelezi kukamilika.



Share:

Marekani Yakiri Wanajeshi Wake 11 Walijeruhiwa na Makombora Ya Iran

Licha ya Marekani  hapo awali kudai kuwa hakuna askari wake  aliyeuawa au kujeruhiwa katika mashambulizi 22 ya Makombora ya  Iran dhidi ya kambi mbili za kijeshi za nchi hiyo huko Iraq, lakini hivi sasa imefichuka kuwa, wanajeshi kadhaa wa Marekani  walijeruhiwa vibaya na wakupelekwa kwa usafiri wa ndege katika nchi za Ujerumani na Kuwait kwa ajili ya matibabu.

Hapo jana, maafisa wa Marekani walilazimika kukiri juu ya kujeruhiwa wanajeshi wa nchi hiyo na makombora ya Iran, licha ya hapo awali kukataa  kuwa kulikuwepo na majeruhi katika shambulizi hilo

Masaa machache baada ya Iran kuvurumisha makombora na kupiga kambi mbili za Marekani nchini Iraq, Rais Donald Trump alijitokeza na kudai kuwa, "Ni furaha kuwatangazia Wamarekani kuwa hakuna askari wetu hata mmoja aliyeuawa au kujeruhiwa katika shambulizi la makombora la Iran nchini Iraq."


Share:

Kamwelwe: Muda Wa Kusajili Laini Za Simu Hautaongezwa

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema serikali haitaongeza muda wa kusajili laini za simu kwa alama za vidole, huku akitahadharisha kuwa katika siku zilizosalia, kasi ya wizi wa kimtandao kupitia simu za mkononi imeongezeka.

Amesema hayo jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu siku zilizobaki kabla ukomo wa siku 20 alizotoa Rais John Magufuli, haujawadia. Mwisho wa usajili ni Januari 20 mwaka huu.

“Kumejitokeza wizi wa kimtandao; wananchi tuwe macho sana tunapomalizia hizi siku zilizosalia kabla laini ambazo hazijasaliwa hazijazimwa. Watu wanatumia siku chache zilizosalia kuibia watu kwa kiwango cha juu; bila kuwa makini, watu tutaibiwa sana,” alihadharisha Waziri Kamwelwe.

Waandishi wa habari walipotaka kujua kama siku za usajili huo kwa alama za vidole zitaongezwa, waziri alisema: “Hakuna siku kuongezwa; siku za usajili hazitaongezwa.”


Share:

Facilitator, Financial Literacy Life Skills Club at Room to Read

Facilitator, Financial Literacy Life Skills Club at Room to Read Position Overview: The Life Skills Clubs Facilitator will be responsible for organizing and implementing the life skills club sessions and activities that are part of Room to Read’s larger Girls’ Education Program (GEP) in Bagamoyo, Chalinze and Kibaha Districts. The Life Skills Clubs have a primary focus on… Read More »

The post Facilitator, Financial Literacy Life Skills Club at Room to Read appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Marketing and Communications Fellow at Small Things

Marketing and Communications Fellow at Small Things Small Things Dar es Salaam Descriptions The Small Things, a small grassroots non-profit located in Nkoaranga, Arusha, Tanzania is looking for a qualified Marketing and Communications Coordinator. The Small Things strives to keep vulnerable and orphaned children in the Meru District of Tanzania in their families by creating sustainable, participatory and… Read More »

The post Marketing and Communications Fellow at Small Things appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Payables Bookkeeper Job Opportunity at Sokowatch

Payables Bookkeeper  Company Description:  Sokowatch is transforming communities across Africa by revolutionizing access to essential goods and services. By connecting small shops to the digital economy, we fix inefficient supply chains and provide services that were previously unavailable. Sokowatch aims to provide everything a retailer needs, no wholesalers or banks necessary. Thousands of retailers across Kenya, Tanzania, and… Read More »

The post Payables Bookkeeper Job Opportunity at Sokowatch appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Warehouse Manager Job Opportunity at SOKOWATCH

Warehouse Manager  Dar es Salaam About Us:  Sokowatch is transforming communities across Africa by revolutionizing access to essential goods and services. By connecting small shops to the digital economy, we fix inefficient supply chains and provide services that were previously unavailable. Sokowatch aims to provide everything a retailer needs, no wholesalers or banks necessary. Our Vision Dominate the… Read More »

The post Warehouse Manager Job Opportunity at SOKOWATCH appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Kesi Ya Kumuondoa Trump Madarakani: Maseneta 100 Waapishwa

Maseneta 100 wa Marekani wameapishwa Alhamisi kama baraza la mahakama litakaloshughulikia kesi inayomkabili Rais Donald Trump.

Hakimu mkuu wa mahakama ya juu zaidi John Roberts aliapisha maseneta kuhakikisha wanatenda haki bila upendeleo.

Wiki zijazo, maseneta wataamua iwapo Trump anastahili kuondolewa madarakani kwa makosa yaliyowasilishwa na Bunge la Wawakilishi. Kesi hiyo imepangiwa kuanza kusikilizwa Januari 21.

Hakimu Roberts aliwauliza maseneta, " Je mnaapa ya kwamba katika kesi inayomkabili Donald Trump, Rais wa Marekani, ambayo inayongoja kusikilizwa, mutatenda haki bila upendeleo kulingana na katiba, Mungu awasaidie?"

Wabunge wakajibu "Ndio" kabla ya kila mmoja wao kusaini kitabu walichochukulia kiapo. Kiongozi wa waliowengi wa Republican Mitch McConnell, kisha akaahirisha kikao cha kutathmini iwapo Donald Trump ana kesi ya kujibu na kutangaza kwanza kesi hiyo itaanza kusikilizwa Jumanne, 13:00 EST (18:00 GMT).

Bwana Trump anashtumiwa kwa kutumia vibaya madaraka na kuingilia bunge. Hata hivyo amekanusha kutekeleza makosa hayo na kusema kwamba kesi dhidi yake ni madai dhidi yake ni ya uongo

BBC



Share:

Key Account Manager at Yara International January 2020

Key Account Manager at Yara International January 2020 Job description Key Account Manager YARA BRASIL · Chemical and pharmaceutical Dar es Salaam, Dar es Salaam Region, Tanzania From January 14, 2020 to February 14, 2020 In Yara Full time · Salary to negotiate Requirements Entry level No Education Salary to negotiate Dar es Salaam Description About the Unit… Read More »

The post Key Account Manager at Yara International January 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger