Friday, 6 December 2019

Rais Dkt. Magufuli apata tuzo kwa kuimarisha Diplomasia ya Uchumi wa nchini.

Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dar es Salaam
Shirika lisilo la Kiserikali la Kuinua Diplomasia ya Uchumi Tanzania (TEDEF) limetambua juhudi na kuthamini kazi anazofanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Dkt. John Pombe Magufuli kuhakikisha azma ya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025 inafikiwa.  

TEDEF imemtunuku tuzo Rais Dkt. Magufuli  na kuwa miongoni mwa Watanzania 10 waliofanya vizuri kwa kutoa mchango wao katika kuimarisha Diplomasia ya Uchumi wa nchini. 

Akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Rais Dkt. Magufuli na kuwakabidhi tuzo hizo watanzania wengine waliomstari wa mbele kuinua diplomasia ya uchumi nchini Desemba 5, 2019 katika ukumbi wa Karimjee uliopo jijini Dar es salaam, Naibu Waziri Wa Habari, Utamaduni, Sanaa Na Michezo Juliana Shonza ameishukuru TEDEF kwa uamuzi wao wa  kushirikiana  na  Serikali  katika kuimarisha diplomasia ya Uchumi nchini. 

 “Diplomasia  ya  Uchumi  ni  Muhimu  kwa  ustawi  wa  Taifa.  Mataifa yote makubwa duniani yameupa umuhimu wa kwanza Diplomasia ya Uchumi ambao umekuwa ni muhimili wa kukuza mataifa hayo. Nanyi TEDEF mmekuwa wazalendo kwa kutambua na kuthamini mchango wa viongozi na wananchi mbalimbali katika kuhakikisha nchi yetu inafikia azma yake ya kuwa nchi ya uchumi wa kati” alisema Naibu Waziri Shonza. 

Miongoni mwa kazi zilizomfanya Rais Dkt. Magufuli kupewa tuzo hiyo mchango wake katika kujenga miundombinu ya kufanikisha  Diplomasia ya Uchumi Tanzania ikiwemo miradi ya reli  ya  kisasa (SGR), kuimarisha shirika la  ndege, ujenzi wa barabara na madaraja mbalimbali nchini  pamoja na  Mradi  wa  umeme Bwawa la Nyerere.    

Watanzania wengine waliopata tuzo za kushiriki kujenga diplomasia ya uchumi ni mawaziri wawili ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi kwa kuongoza  majadiliano ya Biashara ya Kimataifa baina  ya Tanzania na Kampuni  ya  Madini  ya Barrick kwa mafanikio makubwa kwa Tanzania pamoja na Wiziri wa Mambo ya Ndani nchi  Kangi Lugora ambaye anasimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao kwa kutambua amani iliyojengeka ni muhimu kwa kufanikisha Diplomasia ya Biashara na Diplomasia ya Uchumi.      

Tuzo hizo pia zimeenda kwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi ambao nao wametambuliwa kwa mchano wao katika kujenga diplomasia ya uchumi; Ubalozi wa Tanzania Nchini Rwanda ukiongozwa na Balozi Ernest Mangu ambao umeongoza kwa mauzo ya nje katika nchi za Afrika Mashariki, Ubalozi wa Tanzania nchini China ukiongozwa na Balozi Mbelwa Kairuki kwa kwa kuongoza katika uwekezaji mitaji nchini pamoja na Ubalozi wa Tanzania Nchini Marekani ukiongozwa na Balozi Wilson Masilingi ambao umeongoza kwa kuleta watalii nchini. 

Mbali na viongozi hao, Mkoa wa Dar es Salaam ambao unaongozwa na Mkuu wa mkoa huo Paul Makonda nao umepata tuzo hiyo kwa kuongoza kwa miradi  ya uwekezaji ambapo takribani miradi 109 imesajiliwa. 

Aidha, Watanzania wengine ambao wametambuliwa kwa mchango wao katika kushiriki katika kuitangaza Tanzania kimataifa katika diplomasia ya uchumi na kupewa tuzo hiyo ni mchezaji wa mpira wa miguu Mbwana Samata kupitia sekta ya michezo, mwanamuziki Nasibu Abdul (Diamond) kupitia sekta ya muziki pamoja na mtangazaji wa TBC Elisha Elia anayetangaza kipindi cha Kishindo cha Awamu ya Tano  na  kusaidia  kutangaza miundombinu ya Diplomasia ya Biashara na Diplomasia ya Uchumi kupitia sekta ya habari.      
  
Kwa upande wake Mkurugenzi na Makamu Mwenyekiti Bodi ya TADEF Dkt. Wilbroad Mtabuzi ameyataja baadhi ya majukumu ya msingi ya shirika hilo kuwa ni pamoja  na  kuvutia uwekezaji hasa kwenye viwanda, Kuhamasisha biashara ya kimataifa kuhamasisha utalii, kutangaza sifa njema za nchi yetu ambayo  ni amani, utulivu na  umoja wa Kitaifa ambapo majukumu hayo yatasaidia kuchangia kasi yakuufikia uchumi wa kati. 

Dkt. Mutabuzi amesema kuwa TEDEF imefanikiwa kuunda vyama vya ushirika kwa wahimitimu wa elimu ya juu nchini ambao wamejiajiri katika katika sekta ya kilimo-biashara  kwenye  mikoa  ya  mikoa  ya  Dare  es  salaam,  Pwani, Dodoma,  Kigoma,  Mbeya  na  Mwanza.   

Wahitimu hao wamefanikiwa kuanzisha vikundi vya ufugaji samaki kibiashara katika mkoa wa Pwani eneo la Ruvu wilayani Bagamoyo pamoja na kuwasaidia wakulima zaidi ya 2000 wanaojishughulisha na kilimo wamenufaika na huduma za TEDEF nchini. 

Sera ya Diplomasia ya Uchumi Mwaka 2001 nchini ilianza kutekeleza kufuatia idhini ya Rais wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa mwaka 2000 ikitambua kuwa Diplomasia ya Uchumi ni Ustawi ambapo ushiriki wa TEDEF katika diplomasia hiyo una mchango katika kuleta ustawi katika nchini.
-Mwisho-


Share:

Waziri Lukuvi Awapa Kibarua Wakuu Wa Mikoa

NA. MWANDISHI WETU
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ametoa wito kwa wakuu wa mikoa kuhakikisha  wanawalinda wamiliki wa ardhi ambao wapo kisheria.

Waziri Lukuvi alitoa agizo hilo jana Desemba 05, 2019 wakati wa mkutano wa mashauriano kati ya Serikali, wafanyabiashara na wawekezaji  uliofanyika mjini Kibaha na  kuongozwa na Waziri  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Mhe. Angellah Kairuki.

Wawekezaji na wafanyabiashara walipata nafasi kufikisha malalamiko yao ambayo ni kikwazo katika shughuli zao.

Waziri Lukuvi alibainisha kuwa  Mkoa wa Pwani unaongoza kwa uvamizi ambapo Wilaya ya Bagamoyo inatajwa kuwa kinara.

Lukuvi alisema, wakuu hao wa mikoa wana askari wanaweza kuwaondoa waliojimilikisha  ardhi kinyume cha sheria.

“Tumieni mabaraza ya ardhi yaliyoundwa kisheria kuondoa wavamizi kwenye maeneo ambayo yanamilikiwa kisheria" alisema.

Naye Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga aliwahimiza wawekezaji kuwekeza kwenye kilimo cha alizeti na michikichi kwa ajili ya mafuta ya kupikia.

Waziri Hasunga alisema, kuna uhitaji wa mafuta ya kula tani 650 ambazo kiasi cha shilingi billion 675 zimekuwa zikitumika kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi.

Alisema, upande wa mafuta wawekezaji ni wachache, hivyo wakipatikana wawekezaji wengi wataokoa fedha ambazo zinaenda nje ya nchi zibaki hapa nchini.

Aidha kuhusiana na mikopo kwa wakulima alisema, kwa anayetaka kulima awasiliane na mfuko wa pembejeo pamoja na benki ya kilimo kupata taratibu.

Akihitimisha mkutano huo Waziri Kairuki amewahahakikishia kuwa majibu yote ambayo hayajapatikana papo hapo wizara inaandaa bango kitita ambalo malalamiko na changamoto zote zitajumuishwa na kupelekwa ngazi zote akiwemo Mhe.  Rais na Waziri Mkuu.

Amewapongeza wawekezaji wazao ambao wameweza kusajili miradi zaidi ya 70 kwa mwaka huu pekee huku akizitaka taasisi za kibenki kuondoa urasimu katika kutoa mikopo kwa wawekezaji wazawa badala yake waweke mazingira rafiki.

Mkutano huo wa mashauriano wa siku moja ulihudhuriwa na mawaziri watatu pamoja na manaibu Mawaziri tisa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angellah Kairuki, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William  Lukuvi , Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mussa Sima, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu ,Naibu  Waziri wa Mambo wa Ndani ya Nchi,Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Antony Mavunde  (Kazi, Vijana na Ajira), Naibu Waziri Ofisi ya Rais  Tamisemi, Josephat Kandege.

Pia ulihudhuriwa na Taasisi wezeshi, mwenyekiti wa wafanyabiashara Mkoa wa Pwani, mwenyekiti wa wafanyabiashara ndogondogo machinga, wawekezaji pamoja na viongozi wengine kutoka Halmashauri na Mkoa.

=MWISHO=


Share:

Waziri wa Kilimo Atishia kuifuta Bodi ya Wakala wa Mbegu (ASA)

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Morogoro
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ametangaza kuifuta Bodi ya Wakala wa Mbegu (ASA) endapo itashindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuzalisha mbegu za kilimo zipatazo Tani 5000 katika msimu wa kilimo wa mwaka 2019/2020.

Ametoa kauli hiyo juzi tarehe 4 Disemba 2019 wakati akizungumza na watumishi wa Taasisi hiyo mara baada ya kutembelea Mkoani Morogoro akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja ambapo amesema kuwa tishio hilo litahusisha pia Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu.

Amesema kuwa pamoja na ASA kuongeza eneo la uzalishaji wa mbegu kutoka hekta 9890 mpaka kufikia hekta 10,115.2 lakini bado uzalishaji ni mdogo kwani ASA inazalisha Tani 1440 pekee huku zaidi ya asilimia 85 ya watanzania wanaojihusiaha na kilimo wakiwa na uhitaji wa mbegu.

Waziri Hasunga amesema kuwa matrekta matatu mapya yaliyonunuliwa na ASA pamoja na zana zake kama vile Boom Spayer, majembe matatu mapya na Planter tatu mpya yanapaswa kutumika ipasavyo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mbegu bora.

“Sisi kama nchi tunahitaji Tani 100,086 za mbegu na mpaka sasa hivi uwezo wetu wa kuzalisha ndani na kuagiza nje hauzidi Tani 57,000 sasa mahitaji ni makubwa watu wanataka mbegu bora lakini uzalishaji bado upo chini” Amesisitiza Mhe Hasunga

Waziri Hasunga amesema kuwa mbegu bora ndio msingi na muhimili wa kilimo hivyo ili kubadilisha kilimo kutoka kujikimu na kuwa kilimo chenye tija na cha kibiashara ni lazima kuwa na uzalishaji mkubwa wa ndani ya nchi.

Aliongeza kuwa serikali itaiwezasha ASA kuongeza vituo vya usambazaji wa mbegu kutoka vitano ambavyo vinatumika sasa mpaka kuwa vituo 10 ili kuwarahisishia wakulima kupata mbegu katika maeneo yao.

Kadhalika, waziri Hasunga amemtaka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu (ASA) kuhakikisha kuwa anatatua changamoto alizozibainisha kwenye taarifa yake ikiwemo ukosefu wa mtaji wa kutosha, kutokuwa na hifadhi ya mbegu ya Taifa, ukosefu wa miundombinu ya umwagiliaji, upungufu wa vitendea kazi na uhaba wa vituo vya kusambaza mbegu.

Changamoto zingine ni upungufu wa magari ya kusambaza mbegu, uchakavu wa mitambo ya kuchakata mbegu, na upungufu na uchakavu wa maghala ya kuhifadhia mbegu.

Wakala wa Mbegu (ASA) ulianzishwa chini ya sheria ya wakala za serikali sura ya 245 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2009 na kuzinduliwa rasmi tarehe 23 Juni, 2006 ikiwa ni Taasisi inayounganisha sekta ya umma na binafsi katika mfumo wa uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora.

MWISHO


Share:

Swahili Speakers – Remote Voice Artists  Job Opportunity at TransPerfect

Swahili Speakers – Remote Voice Artists  Job description Voice Artist We are looking for speakers of several languages to join us in a new series of innovative and interesting voice related tasks to improve Artificial Intelligence (i.e. as speech or text recognition, input methods, keyboard/swipe technology or other areas of human-machine interaction related to languages). As Voice Actress/Actor… Read More »

The post Swahili Speakers – Remote Voice Artists  Job Opportunity at TransPerfect appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at Tanzania Cricket Association, Chief Executive Officer (CEO)

Chief Executive Officer (CEO)  TANZANIA CRICKET ASSOCIATION PO.BOX 918 DAR ES SALAAM TANZANIA. APPLICATION FOR THE POST OF CHIEF EXECUTIVE OFFICER (CEO) TCA is a Registered Sports Association with the National Sports Council of Tanzania and an associated member of INTERNATIONAL CRICKET COUNCIL (ICC) a sole representative body in charge of running cricket as a sport in Tanzania,… Read More »

The post Job Opportunity at Tanzania Cricket Association, Chief Executive Officer (CEO) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Sales & Reservations Manager Job Opportunity at Mwiba Holdings

Sales & Reservations Manager – (1 Post) Mwiba Holdings Limited is registered Tanzanian Company under Companies Ordinance (Cap. 212) and a leading Hospitality company with its Operations in Arusha, Meatu-Simiyu and Mara Regions. We are currently looking for Sales A Reservations Manager to be part of our team and provide support to all our tourist facilities and enhance Photographic… Read More »

The post Sales & Reservations Manager Job Opportunity at Mwiba Holdings appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

IT Systems/Network Administrator Job Opportunity at Mwiba Holdings

IT SYSTEMS/NETWORK ADMINISTRATOR – (1 POST) Ker & Downey Safaris Tanzania Limited is registered Tanzanian Company under Companies Ordinance (Cap. 212) and a leading Hospitality company with its Operations in Arusha, Tabora Region, Shinyanga Region, Kigoma Region, Meatu-Simiyu and Mara Regions. We are seeking a well-rounded, full time IT Systems\Network Administrator with at least 3yrs experience to join our… Read More »

The post IT Systems/Network Administrator Job Opportunity at Mwiba Holdings appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Halima Mdee Akana Kushiriki Maandamano

Mbunge wa jimbo la Kawe, Halima Mdee amekana kushiriki katika mkusanyiko usio halali unaodaiwa kufanyika katika maeneo tofauti ya Buibui, Mwananyamala na barabara ya Kawawa Februari 16 mwaka jana kama inavyodaiwa na upande wa mashtaka.

Mdee ameeleza hayo jana Alhamisi Desemba 5, 2019 wakati akitoa ushahidi katika kesi ya jinai namba 112/2018 yenye mashtaka 13 yakiwemo ya uchochezi inayomkabili pamoja na wenzake.

Akiongozwa na wakili  wa utetezi, Peter Kibatala alidai kuwa Februari 16, 2018 kabla ya mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi wa marudio jimbo la kinondoni alikuwa bungeni Dodoma.

Amedai  kuwa siku hiyo afya yake haikuwa nzuri na alishiriki mkutano huo kuonyesha mshikamano na upendo kwa mgombea na baada ya kushuka  jukwaani aliondoka.

Akijitetea mbele ya  Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, mbunge huyo amesema alikamatwa na askari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akiwa anatokea Afrika Kusini kwenye matibabu.


Share:

Job Opportunity at Ker & Downey Safaris

IT Systems/Network Administrator  – (1 POST) Ker & Downey Safaris Tanzania Limited is registered Tanzanian Company under Companies Ordinance (Cap. 212) and a leading Hospitality company with its Operations in Arusha, Tabora Region, Shinyanga Region, Kigoma Region, Meatu-Simiyu and Mara Regions. We are seeking a well-rounded, full time IT Systems\Network Administrator with at least 3yrs experience to join… Read More »

The post Job Opportunity at Ker & Downey Safaris appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at Precision Air – December 2019

AVSEC Officer – Operations, Investigation And Protection Precision Air Services Plc is a fast growing private Tanzanian airline which operates in Partnership with Kenya Airways, with its strategies to expand wings beyond East Africa and Africa. In order to keep our services at a higher level and meet our customers’ maximum satisfaction. We wish to invite applications from… Read More »

The post Job Opportunity at Precision Air – December 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

UTAFITI WABAINI KUKU WENGI WANAOUZWA MTAANI WAKIDAIWA NI WA KIENYEJI KUMBE SI KWELI


Mtaalamu wa masuala ya kutetea Haki na Ustawi wa Wanyama kutoka shirika la World Anima Protection ,Dkt Victor Yamo akizungumza na Waandishi wa habari leo jijini Dar,alipokuwa akiwasilisha ripoti ya utafiti uliyofanywa katika nchi nne Tanzania ikiwamo, kuhusu kubainika kwa kuku wengi wanaouzwa katika maeneo mbalimbali nchini wakidaiwa kuwa ni wa kienyeji kumbe si wa kienyeji kama inavyosemwa.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza mtaalamu huyo wa Haki na Ustawi wa Wanyama kutoka shirika la World Anima Protection ,Dkt Victor Yamo alipokuwa akiendelea kufafanua mambo mbalimbali yahusuy haki na ustawi wa Wanyama nchini Tanzania 
Mtaalamu wa masuala ya kutetea Haki na Ustawi wa Wanyama kutoka shirika la World Anima Protection ,Dkt Victor Yamo akifafanua jambo kwa msisitizo mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar,alipokuwa akiwasilisha ripoti ya utafiti uliyofanywa katika nchi nne Tanzania ikiwamo, kuhusu kubainika kwa kuku wengi wanaouzwa katika maeneo mbalimbali nchini wakidaiwa kuwa ni wa kienyeji kumbe si wa kienyeji kama inavyosemwa.
***

UTAFITI uliyofanywa na Shirika linalohusika na usalama na Ustawi wa wanyama Duniani (World Animal Protection) umebaini kuwa kuku wengi wanaouzwa katika maeneo mbalimbali nchini wakidaiwa kuwa ni wa kienyeji si wa kienyeji kama inavyosemwa.

Utafiti huo umebaini kuku hao si wa kienyeji bali ni kuku wa kisasa maarufu kama kuku wa kizungu wanaofugwa majumbani kwa kupewa majani pamoja na dawa mbalimbali za kuwakuza na kuwafanya kuwa wagumu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati akiwasilisha ripoti ya utafiti huo uliyofanywa katika nchi nne Tanzania ikiwamo, Msemaji Mkuu wa Shirika hilo, Victor Yamo alisema utafiti huo ambao ulifanywa Juni hadi Julai mwaka huu katika mikoa ya Arusha na Dar es Salaam umebaini jambo hilo hivyo watumiaji wanapaswa kuwa makini.

Yamo amesema kuku wengi wanauzwa katika mikoa hiyo wamekuwa wakupewa dawa za kuwakuza ambazo zina madhara kwa binadamu pindi wanapotafuna mifupo yao

"Wakati watu wetu wakitembelea kwenye masoko mbalimbali kuulizia bei ya kuku na wakabaini uwepo wa kuku wa kisasa wengi na mwananchi huuziwa kwa kuambiwa kuwa ni wa kienyeji jambo ambalo ni uongo," alisema.

Amesema utafiti huo ulifanyika kwa lengo la kujua walaji wananunua nyama za aina gani, kutoka wapi pamoja na kuangalia kama wanafahamu ubora wa chakula na matumizi ya dawa za wanyama.

"Tunaamini kuwa mteja ataelewa nyama anayotaka kununua au kula inaubora au tatizo kiasi gani itakuwa rahisi kujiepusha nayo na kutafuta kitu kingine mbadala cha kula," alisema

Aidha Yamo amesema kwa sasa Shirika lao linafanya jitihada kubwa kuhakikisha linaimarisha ustawi na haki za wanyama na sheria za kuwalinda wanyama hao zinapitishwa na serikali husika katika kila nchi.

Amesema pamoja na kuyafanya hao wanatoa wito kwa watanzania waanze kuelewa kuwa kama watashindwa kuangalia ustawi wa wanyama hasa wanaoliwa kuna hatari kubwa ya kupotea.

"Ni ukweli uliyowazi kuwa ustawi wa wanyama ni muhimu sana na kwa kutambua hilo tumekuwa tukienda mashuleni kufundisha jambo hilo na masuala ya usalama wa chakula na ubora wa dawa," alisema.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa December 6



















Share:

Thursday, 5 December 2019

HR Officer (Tanzania) at Smollan Tanzania

Smollan is recruiting for an HR Officer, to provide a full generalist HR functions to the relevant business unit(s), including recruitment, performance management, training and development, IR and general HR administration and reporting Key Responsibilities and Deliverables: Effective recruitment, selection and on-boarding Identify recruitment need and what the business is looking for and create and load advertisement on… Read More »

The post HR Officer (Tanzania) at Smollan Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Android APP developer at KOPAGAS – Dar Tanzania

You will report to the Head of Engineering and collaborate cross-functionally with Kopa teams.   Responsibilities: Build, own, and maintain android applications. Develop unit-testing code for robustness, including edge cases, usability, and general reliability Review design documents, perform code reviews and contribute to implementation decisions. Support and collaborate with cross-functional teams (Product, Operations and Services) to ship excellent… Read More »

The post Android APP developer at KOPAGAS – Dar Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Small and Medium Business Adviser – Remote at VSO

Role Overview The ideal Candidate will be providing technical support to microfinance institution (s) to improve their capacity to strengthen loan scheme systems targeting smallholder farmers in Zanzibar Island, Tanzania. Liaise with Small Business advisors to advise CBOs / Parents to set up appropriate income generation activities. Skills, Knowledge And Experience Skills, qualifications and experience Minimum of 8… Read More »

The post Small and Medium Business Adviser – Remote at VSO appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Partner Help Desk Coordinator at Airtel Tanzania PLC

Airtel Tanzania PLC is looking for a suitable Tanzanian candidate  for the Partner Help Desk  Coordinator Position. The incumbent will assist in enhancing partner satisfaction and ensure timely release of payments to the partners. Key deliverables; Handle all partner queries and resolve them accordingly Educate partners on process flow and update them on invoice status Invoice Management Timely payment follow… Read More »

The post Partner Help Desk Coordinator at Airtel Tanzania PLC appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Software Developer at NMB Bank Plc December 2019

Job Purpose To build, test and implement in-house well designed new business applications or modify/upgrade existing business software applications to meet key business goals. Main Responsibilities Integrate technical and application components to meet business requirements Code and test program modules that meet design specifications Maintain, tune and repair applications in order to keep them performing according to technical… Read More »

The post Software Developer at NMB Bank Plc December 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger