Friday, 23 August 2019
Thursday, 22 August 2019
Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85) Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45
SUNUPER; Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa , matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,
Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno
ONDOA MATATIZOYAKO YOTE ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe) kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, pete ya bahati, kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa
Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO 0759208637 / 0620510598
SERIKALI YA MAREKANI YAAHIDI KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UGONJWA WA SELI MUNDU (SICKLE CELL) NCHINI

Na WAJMW-Brazzaville
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amekutana na Waziri wa Afya wa Marekani Amiral Brett Giroir na kufanya mazungumzo na kuona namna gani nchi hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kupambana na ugonjwa wa Sickle Cell (Seli Mundu) hasa kwa watoto wachanga na wale walio chini ya miaka mitano.
Waziri Ummy amemueleza Waziri huyo kuwa watoto wapatao 11,000 wanazaliwa na ugonjwa huo Tanzania na wengi hupoteza maisha kwa sababu ya kuchelewa kufanyiwa vipimo na kugundulika mapema.
Waziri Ummy amemueleza kuwa muelekeo wa nchi sasa ni kuhakikisha kuwa kila mtoto anayezaliwa anapimwa Sickle Cell na watakaogundulika matibabu yaanze mapema ili kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Mawaziri hao wamekubaliana kwa pamoja kushirikiana katika kudhibiti vifo vinavyoweza kutokea kwa sababu ya ugonjwa huo huku Waziri Amiral akiahidi kuimarisha upatikanaji wa vipimo, pamoja na matibabu kwa watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kuanzia ngazi ya zahanati na vituo vyote vya kutoa huduma za afya ya msingi nchini.
“Ni muhimu huduma hizi zikatolewa katika ngazi ya afya ya msingi mpaka taifa ili kuwapa huduma stahiki wananchi, hii ikiwa ni utekelezaji wa afya kwa wote. Suala la upimaji wa Seli Mundu, elimu kwa jamii na pia suala la matibabu katika ngazi zote za utoaji huduma ni muhimu vikapewa kipaumbele”. Aliongeza Waziri Ummy.

Hivi sasa huduma hii hapa nchini inapatikana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Hospitali za Rufa za Mikoa za Amana na Temeke pekee kwa nchi nzima.
Kwa upande wake Waziri Brett amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kujenga viwanda vya dawa nchini ikiwa ni pamoja na za Sickle Cell. Pia ameahidi kutembelea Tanzania kuona na kujadiliana zaidi namna nchi hizi mbili zitavyoshirikiana katika kushughulikia ugonjwa huu nchini.
Mawaziri hao wanahudhuria mkutano wa 69 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaojumuisha Mawaziri wa Afya toka nchi mbalimbali za Afrika unaoendelea jijini Brazzaville nchini Jamhuri ya Kongo.
RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WANAOIWAKILISHA TANZANIA KATIKA NCHI MBALIMBALI ZA NJE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika Kikao na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje mara baada ya kikao chao Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Brazil Emanuel Nchimbi mara baada ya Kikao na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri wa Mambo ya Nje Profesa Palamagamba Kabudi watano kutoka (kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Damas Ndumbaro watano kutoka (kulia) pamoja na baadhi ya Mabalozi Wanawake wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
WAFANYAKAZI TBL WATOA MSAADA WA VIFAA VYA KUSITIRI WASICHANA WAKATI WA HEDHI MASHULENI
Meneja wa masuala Endelevu wa TBL,Irene Mutiganzi (wa tatu kushoto) Akiongea Wakati wa hafla hiyo.
Maofisa wa taasisi ya Her Africa wakifurahia msaada huo wa kusaidia wasichana kukabiliana na changamoto ya hedhi wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo. Na Cathbert kajuna - Kajunason/MMG.
Wafanyakazi wa kampuni yak Bia Tanzania (TBL Group), chini ya kampuni mama ya kimataifa ya AB InBev, wametoa msaada wa taulo za kike kwa ajili ya kuwasitiri wasichana wanafunzi wanaosoma shule za sekondari kupitia mradi wa kukabiliana na changamoto za hedhi unaoendeshwa na taasisi ya Her Africa.
Hafla ya kukabidhi msaada huo ilifanyika katika ofisi za makao makuu ya TBL zilizopo Ilala jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wafanyakazi maofisa kutoka taasisi ya Her Africa na wafanyakazi wa TBL.
Akiongea wakati wa hafla hiyo, Meneja wa Masuala Endelevu wa TBL, Irene Mutiganzi, alisema kuwa msaada huo umetolewa kutokana na michango ya wafanyakazi baada ya kuguswa na changamoto ya vifaa vya hedhi mashuleni kwa wasichana, hususani wanaotoka kwenye familia zenye vipato vidogo na kuwapunguzia uwezo wao wa kufaulu vizuri kutokana na wengine kutohudhuria masomo wanapokuwa kwenye vipindi hivyo.
“TBL tunayo sera ya kujenga ulimwengu maridhawa ambayo inatekelezwa pia na wafanyakazi, ambapo mara nyingi wamekuwa wakijitoa kukabiliana na changamoto za kijamii na sio kwa kutoa pesa tu bali pia wamekuwa wakitoa hata muda wao kushiriki katika kazi za kijamii kama ambavyo wamefanikisha kutoa mchango huu” alisema Mutiganzi.
Kwa upande wake Mwanzilishi mwenza wa taasisi ya Her Africa nchini, Salha Kibwana, alishukuru wafanyakazi wa TBL kwa kulipa kuipa umuhimu changamoto ya vifaa vya Watoto wa kike wa sekondari kujisitiri wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi mashuleni, kwa kutoa msaada huo na amewahakikishia kuwa utawafikia walengwa
“Nawashukuru kwa kujitoa na nina imani tukizidi kuunganisha nguvu tutafanikiwa kusaidia wanafunzi wengi zaidi hususani maeneo ya vijijini” alisema.
MPC YAKANUSHA UZUSHI WA TAARIFA YA WAANDISHI WA HABARI KUNUNULIWA BEI YA MAJI MWANZA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA TUHUMA ZA WAANDISHI WA HABARI
Klabu ya Waandishi wa habari ya Mkoa wa Mwanza (MPC) imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii juu ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Mwanza kununuliwa na MWAUWASA ili kutoandika habari za ongezeko la bei za maji Jijini Mwanza.
MPC inawataka wadau kuzipuuza taarifa hizo kwani zina lengo la kuzichafua taasisi zetu mbili, MWAUWASA NA MPC pamoja na waandishi wa habari wa Mkoa wa Mwanza, kupitia kwa watu wachache wasio na nia njema na taasisi hizo na wenye uelewa mdogo wa sayansi ya mahusiano na uandishi wa habari.
Ifahamike kuwa, MPC ndio iliyoingia kwenye fungate na MWAUWASA kuandaa ziara ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Mwanza kuitembelea miradi ya maji inayosimamiwa na MWAUWASA kwa lengo la kujenga ufahamu wa miradi hiyo kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Mwanza , hivyo MPC ndiyo iliyoalika waandishi mia moja(100) kwenda ziara hiyo na sio sabini kama inavyoelezwa na msambazaji wa taarifa hiyo, ambaye anaonyesha kutofahamu hata takwimu halisi.
Ndugu Waandishi wa habari ifahamike kuwa, ziara za waandishi wa habari kwenda kwenye taasisi fulani kukagua shughuli zinazofanywa na taasisi hiyo siyo suala geni hapa Nchini, jambo hili linafanywa kila siku, mfano ziara za waandishi kutembelea mradi wa reli ya kisasa (SGR), waandishi kutembelea Mbuga za wanyama, waandishi kutembelea TBL na miradi mingine, msingi wa jambo hili ni kujenga mahusiano na kuwarahisishia waandishi kuzifahamu taasisi husika kwa upana.
Ikumbukwe kuwa, suala la kupanda kwa bei za maji haikuwa ajenda ya MPC kwenye kutembelea miradi ya MWAUWASA , kwani jambo hilo ni jambo la kisheria na ikumbukwe kuwa MPC haihusiki kutengeneza maudhui ya habari kwa vyombo vya habari, hivyo maamuzi ya kufuatilia ongezeko la bei za maji yalibaki kwa vyombo vya habari na sio ziara ya waandishi.
Pia MWAUWASA ilitoa nafasi ya kila Mwandishi kuuliza swali lolote alilokuwa nalo na waandishi walifanya hivyo na habari ziliandikwa juu ya sababu za kupanda kwa bei za maji, hivyo waandishi walitekeleza wajibu wao kwa kufanya uzania kwa pande zote mbili.
Ndugu waandishi, mwandishi anayesambaza taarifa hizo ameshindwa kuhoji MPC, MWAUWASA na hata Mwandishi mmoja kati ya hao sabini aliowataja, hii inayoonyesha udhaifu mkubwa wa hoja zake pamoja na kutofahamu msingi wa uandishi wa habari na sheria mama ya taaluma.(MSA Act,2016).
Mwisho MPC tunaahidi kuendelea kufanya kazi na MWAUWASA , waandishi wa habari na wadau wengine wote kwa nia ya kuchakata maendeleo ya Mkoa wa Mwanza.
Edwin Soko
Mwenyekiti- MPC
Picha : TACCEO YAENDESHA MAFUNZO YA UCHAGUZI KWA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA ZIWA
Mwezeshaji kwenye mafunzo ya waandishi wa habari za uchaguzi wakili wa kutoka kampuni ya TIFLD Gelina Fuko akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Na Marco Maduhu - Malunde1 blog
Mafunzo hayo yameanza leo Alhamsi Agosti 22,2019 ambayo yatadumu kwa muda wa siku tatu hadi Agost 24,2019 katika ukumbi wa mikutano Belmont Hotel Jijini Mwanza, yameshirikisha waandishi wa habari kutoka mikoa ya Shinyanga,Simiyu, Geita, Mara, Kagera, Kigoma na Mwanza.
Mratibu wa mafunzo hayo, Joseph Moses Oleshaghai kutoka kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC), amesema wanatoa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari, wakiamini kuwa waandishi wa habari ni wadau muhimu wa kufikisha elimu kwa umma ikiwemo elimu ya kiraia na uchaguzi.
“Tunatoa mafunzo haya kwa waandishi wa habari ili kuwaongezea tija kwenye kuandika habari za uchaguzi na kuwapatia wananchi ujumbe sahihi, ambao una husu masuala ya elimu ya uraia na uchaguzi, pamoja na kuwa hamasisha kujitokeza kugombea uongozi, kujiandikisha, pamoja na kupiga kura,”amesema Oleshaghai.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo wakili kutoka Kampuni ya (TIFLD) Jijini Dar es salaam Gelina Fuko, amewataka waandishi wa habari pale wanapokuwa wakiandika habari zao kwenye kipindi hiki cha uchaguzi, wazingatie kupaza sauti za makundi mbalimbali wakiwamo watu wenye uhitaji, walemavu, wanawake, na wazee ili waweze kupata haki zao kwenye uchaguzi.
Amesema kwenye kipindi cha uchaguzi makundi hayo maalumu ya mekuwa yakisahaurika kupaziwa sauti, na hivyo kuendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali kwenye uchaguzi, ikiwamo kunyimwa haki ya kugombea, kubaguliwa, ambapo msaada wao ni waandishi wa habari.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI

Mratibu wa mafunzo hayo, Joseph Moses Oleshaghai kutoka kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC), amesema wanatoa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari, wakiamini kuwa waandishi wa habari ni wadau muhimu wa kufikisha elimu kwa umma ikiwemo elimu ya kiraia na uchaguzi.
“Tunatoa mafunzo haya kwa waandishi wa habari ili kuwaongezea tija kwenye kuandika habari za uchaguzi na kuwapatia wananchi ujumbe sahihi, ambao una husu masuala ya elimu ya uraia na uchaguzi, pamoja na kuwa hamasisha kujitokeza kugombea uongozi, kujiandikisha, pamoja na kupiga kura,”amesema Oleshaghai.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo wakili kutoka Kampuni ya (TIFLD) Jijini Dar es salaam Gelina Fuko, amewataka waandishi wa habari pale wanapokuwa wakiandika habari zao kwenye kipindi hiki cha uchaguzi, wazingatie kupaza sauti za makundi mbalimbali wakiwamo watu wenye uhitaji, walemavu, wanawake, na wazee ili waweze kupata haki zao kwenye uchaguzi.
Amesema kwenye kipindi cha uchaguzi makundi hayo maalumu ya mekuwa yakisahaurika kupaziwa sauti, na hivyo kuendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali kwenye uchaguzi, ikiwamo kunyimwa haki ya kugombea, kubaguliwa, ambapo msaada wao ni waandishi wa habari.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mratibu wa mafunzo ya habari za uchaguzi kwa waandishi wa habari Joseph Moses Oleshaghai kutoka kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC),akielezea dhumuni wa mafunzo kuhusu masuala ya uchaguzi kwa waandishi wa habari wa Kanda ya Ziwa leo. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Mwezeshaji kwenye mafunzo ya waandishi wa habari za uchaguzi wakili wa kutoka kampuni ya Tangible Initiatives for Local Development Tanzania (TIFLD) Gelina Fuko, akiwataka wanahabari kupaza pia sauti za watu wenye uhitaji kwenye kipindi hiki cha uchaguzi ili waweze kupata haki zao.

Mwandishi wa habari Nashoni Kenedy kutoka Gazeti la Daily News Jijini Mwanza, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari jinsi ya kuandika habari za uchaguzi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.

Mwandishi wa habari Moshi Ndugulile kutoka Radio Faraja Mkoani Shinyanga ,akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.

Mwandishi wa habari Salma Mrisho kutoka STARTV Mkoani Geita, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma yao na kutokwenda kinyume na sheria za uchaguzi.

Mwandishi wa habari za mitandaoni Fedrick Chibuga kutoka BMG Online TV Jijini Mwanza, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wana habari kutoka Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi.

Mwandishi wa habari za mitandaoni Salvatory Ntandu kutoka Mpekuzi Blog, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari kutoka Kanda ya Ziwa namna ya kuandika kwa usahihi habari za uchaguzi.

Mwandishi wa habari Joel Maduka kutoka Radio Storm FM Mkoani Geita naye akichangia mada kwenye mafunzo hayo wana habari Kanda ya ziwa namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi na kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi kupitia vyombo vyao vya habari.

Waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mafunzo Jijini Mwanza namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi, pamoja na kutumia vyombo vyao kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi.

Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi.

Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.

Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi.

Waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mafunzo Jijini Mwanza namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi, pamoja na kutumia vyombo vyao kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi.
Na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog
Mwezeshaji kwenye mafunzo ya waandishi wa habari za uchaguzi wakili wa kutoka kampuni ya Tangible Initiatives for Local Development Tanzania (TIFLD) Gelina Fuko, akiwataka wanahabari kupaza pia sauti za watu wenye uhitaji kwenye kipindi hiki cha uchaguzi ili waweze kupata haki zao.
Mwandishi wa habari Nashoni Kenedy kutoka Gazeti la Daily News Jijini Mwanza, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari jinsi ya kuandika habari za uchaguzi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.
Mwandishi wa habari Moshi Ndugulile kutoka Radio Faraja Mkoani Shinyanga ,akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.
Mwandishi wa habari Salma Mrisho kutoka STARTV Mkoani Geita, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma yao na kutokwenda kinyume na sheria za uchaguzi.
Mwandishi wa habari za mitandaoni Fedrick Chibuga kutoka BMG Online TV Jijini Mwanza, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wana habari kutoka Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi.
Mwandishi wa habari za mitandaoni Salvatory Ntandu kutoka Mpekuzi Blog, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari kutoka Kanda ya Ziwa namna ya kuandika kwa usahihi habari za uchaguzi.
Mwandishi wa habari Joel Maduka kutoka Radio Storm FM Mkoani Geita naye akichangia mada kwenye mafunzo hayo wana habari Kanda ya ziwa namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi na kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi kupitia vyombo vyao vya habari.
Waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mafunzo Jijini Mwanza namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi, pamoja na kutumia vyombo vyao kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi.
Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi.
Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.
Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi.
Waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mafunzo Jijini Mwanza namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi, pamoja na kutumia vyombo vyao kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi.
Na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog
WADAU WAKUTANA DODOMA KUJADILI USAWA WA KIJINSIA KUFIKIA 50% KWA 50% KWENYE UONGOZI
Serikali imesema imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa wanawake wanashirikishwa katika nafasi mbalimbali za uongozi ya 50 kwa 50 kufikia mwaka 2025.
Mkakati huo ni kufuatia serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuridhia kutekeleza malengo endelevu ya dunia likiwemo lengo namba 5 linalohusu usawa wa kijinsia ifikapo mwaka 2030.
Akizungumza katika kongamano la kuwaleta pamoja wadau katika kuzungumzia usawa wa kijinsia hasa katika kuwashirikisha wanawake na wasichana katika ngazi mbalimbali za uongozi na maamuzi,lililofanyika leo jijini Dodoma, mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk. Benelith Mahenge amesema kongamano limedhihirisha wananchi wanakusudia kufikia mikakati ya 2025 na malengo endelevu ya 2030.
Awali mbunge wa viti maalum Mkoa wa Dodoma Fatma Taufiq ambaye pia ni Mwenyekiti wa shirika la Achieve SDG5 Coalition in Tanzania,amesema lengo la kongamano hilo ni kuhakikisha vikwazo vinavyowakumba wanawake kushindwa kufikia lengo namba 5 katika malengo endelevu ya dunia vinapatiwa ufumbuzi.
Amesema kuwa kutokana na kuwa wafanyakazi wa ndani ni wanawake wanapata stahiki zao za malipo sambamba na ushiriki wao wa kupata nafasi za uongozi na kutoa maamuzi.
Hata hivyo baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema moja ya vikwazo violivyokuwa vinawakumba wanawake ni pamoja na rushwa katika maeneo ya kazi.
Kongamano hilo limeambatana na ujumbe usemao “Lengo namba tano la malengo endelevu litafikiwa kwa kuwawezesha wanawake na wasichana kushiriki kikamilifu katika ngazi zote za uongozi na maamuzi, Kufikia asilimia 50 % kwa 50% inawezekana.
LAAC Yaiagiza Ofisi ya CAG Kufanya Ukaguzi Nyang’hwale Ndani Ya Miezi 3 Baada Ya Kubainika Ubadhilifu Wa Zaidi Ya Tsh.bilioni 3.
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Kamati ya Bunge ya kudumu ya Hesabu za serikali za Mitaa [LAAC]imeipa muda wa miezi 3 ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali [C.AG] Kwenda kufanya ukaguzi Maalum katika halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita baada Ya Kubainika Ubadhilifu wa zaidi ya Tsh.Bilioni 3.
Akizungumza Mbele ya kamati hiyo leo Agosti 22,2019 Bungeni Jiji Dodoma ,iliyokutanisha watumishi wa halmshauri ya Nyang’hwale,watumishi wa CAG ,Makamu Mwenyekiti wa LAAC , Abdallah Chikota amesema ofisi ya CAG imetoa hati mbaya kwa halmashauri hiyo .
Kamati ya Bunge ya kudumu ya Hesabu za serikali za Mitaa [LAAC]imeipa muda wa miezi 3 ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali [C.AG] Kwenda kufanya ukaguzi Maalum katika halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita baada Ya Kubainika Ubadhilifu wa zaidi ya Tsh.Bilioni 3.
Akizungumza Mbele ya kamati hiyo leo Agosti 22,2019 Bungeni Jiji Dodoma ,iliyokutanisha watumishi wa halmshauri ya Nyang’hwale,watumishi wa CAG ,Makamu Mwenyekiti wa LAAC , Abdallah Chikota amesema ofisi ya CAG imetoa hati mbaya kwa halmashauri hiyo .
Mhe.Chikota amesema katika halmashauri ya Wilaya Ya Nyang’hwale amesema baada ya ofisi ya CAG Kufanya ukaguzi wa ndani katika halmashauri hiyo kuna upotevu wa Zaidi ya Tsh.Bilioni 3,vitabu 50 vya ukusanyaji mapato havikuwasilishwa Kwa Mkaguzi wa CAG,Kuna hati za Malipo [Voucher] zenye thamani ya Tsh.Bilioni 1,milioni 49, laki 1,40 elfu na 91 pamoja na uhamisho wa fedha Bilioni 1 na milioni 700 bila kuonesha shughuli zinakokwenda.
Aidha Makamu Mwenyekiti huyo wa kamati amefafanua kuwa kuna zaidi ya Tsh.Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya hazipo na kituo cha Afya hakijajengwa huku kukiwa na Fedha za P4R kwa Shule za Sekondari Milioni 576 zikitumiwa nje ya Malengo yaliyokusudiwa ,Mradi wa Maji kulikuwa na salio la Tsh.Milioni 74.1 lakini benki inaonesha milioni 71.1 haipo na hati za malipo kwenye mradi wa Maji zenye thamani ya Tsh. Milioni 134.5 hazikuwasilishwa kwa wakaguzi.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Mwita Waitara amesema jambo la ubadhilifu huo wao kama serikali limewafedhehesha sana huku akitoa wito kwa watendaji wapya kuwa waaminifu katika kuwahudumia Watanzania .
Naye katibu tawala Mkoa Wa Geita Denis Bandisa amesema ukaguzi maalum wa CAG utaenda kuonesha utendaji kazi kwa halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale hata kwa viongozi wa sasa huku akibainisha kuwa wapo tayari kuipokea kamati ya CAG Kufanya ukaguzi huo.





















