Friday, 23 August 2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 23 August























Share:

Thursday, 22 August 2019

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598


Share:

SERIKALI YA MAREKANI YAAHIDI KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UGONJWA WA SELI MUNDU (SICKLE CELL) NCHINI


Na WAJMW-Brazzaville
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amekutana na Waziri wa Afya wa Marekani Amiral Brett Giroir na kufanya mazungumzo na kuona namna gani nchi hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kupambana na ugonjwa wa Sickle Cell (Seli Mundu) hasa kwa watoto wachanga na wale walio chini ya miaka mitano.
Waziri Ummy amemueleza Waziri huyo kuwa watoto wapatao 11,000 wanazaliwa na ugonjwa huo Tanzania na wengi hupoteza maisha kwa sababu ya kuchelewa kufanyiwa vipimo na kugundulika mapema.
Waziri Ummy amemueleza kuwa muelekeo wa nchi sasa ni kuhakikisha kuwa kila mtoto anayezaliwa anapimwa Sickle Cell na watakaogundulika matibabu yaanze mapema ili kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Mawaziri hao wamekubaliana kwa pamoja kushirikiana katika kudhibiti vifo vinavyoweza kutokea kwa sababu ya ugonjwa huo huku Waziri Amiral akiahidi kuimarisha upatikanaji wa vipimo, pamoja na matibabu kwa watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kuanzia ngazi ya zahanati na vituo vyote vya kutoa huduma za afya ya msingi nchini.
“Ni muhimu huduma hizi zikatolewa katika ngazi ya afya ya msingi mpaka taifa ili kuwapa huduma stahiki wananchi, hii ikiwa ni utekelezaji wa afya kwa wote. Suala la upimaji wa Seli Mundu, elimu kwa jamii na pia suala la matibabu katika ngazi zote za utoaji huduma ni muhimu vikapewa kipaumbele”. Aliongeza Waziri Ummy.
Hivi sasa huduma hii hapa nchini inapatikana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Hospitali za Rufa za Mikoa za Amana na Temeke pekee kwa nchi nzima.
Kwa upande wake Waziri Brett amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kujenga viwanda vya dawa nchini ikiwa ni pamoja na za Sickle Cell. Pia ameahidi kutembelea Tanzania kuona na kujadiliana zaidi namna nchi hizi mbili zitavyoshirikiana katika kushughulikia ugonjwa huu nchini.
Mawaziri hao wanahudhuria mkutano wa 69 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaojumuisha Mawaziri wa Afya toka nchi mbalimbali za Afrika unaoendelea jijini Brazzaville nchini Jamhuri ya Kongo.
Share:

RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WANAOIWAKILISHA TANZANIA KATIKA NCHI MBALIMBALI ZA NJE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika Kikao na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje mara baada ya kikao chao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Brazil Emanuel Nchimbi mara baada ya Kikao na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri wa Mambo ya Nje Profesa Palamagamba Kabudi watano kutoka (kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Damas Ndumbaro watano kutoka (kulia) pamoja na baadhi ya Mabalozi Wanawake wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
Share:

WAFANYAKAZI TBL WATOA MSAADA WA VIFAA VYA KUSITIRI WASICHANA WAKATI WA HEDHI MASHULENI

Meneja Ugavi wa TBL, Poul Canute akikabidhi vifaa vilivyotolewa na wafanyakazi kwa Afisa Mwandamizi kutoka taasisi ya Her Africa, Asnath Ndosi Wakati wa hafla hiyo,wengine pichani ni wafanyakazi wa TBL
 Meneja wa masuala Endelevu wa TBL,Irene Mutiganzi (wa tatu kushoto) Akiongea Wakati wa hafla hiyo.
 Maofisa wa taasisi ya Her Africa wakifurahia msaada huo wa kusaidia wasichana kukabiliana na changamoto ya hedhi wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo. Na Cathbert kajuna - Kajunason/MMG.

 Wafanyakazi wa kampuni yak Bia Tanzania (TBL Group), chini ya kampuni mama ya kimataifa ya AB InBev, wametoa msaada wa taulo za kike kwa ajili ya kuwasitiri wasichana wanafunzi wanaosoma shule za sekondari kupitia mradi wa kukabiliana na changamoto za hedhi unaoendeshwa na taasisi ya Her Africa. 

 Hafla ya kukabidhi msaada huo ilifanyika katika ofisi za makao makuu ya TBL zilizopo Ilala jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wafanyakazi maofisa kutoka taasisi ya Her Africa na wafanyakazi wa TBL.

 Akiongea wakati wa hafla hiyo, Meneja wa Masuala Endelevu wa TBL, Irene Mutiganzi, alisema kuwa msaada huo umetolewa kutokana na michango ya wafanyakazi baada ya kuguswa na changamoto ya vifaa vya hedhi mashuleni kwa wasichana, hususani wanaotoka kwenye familia zenye vipato vidogo na kuwapunguzia uwezo wao wa kufaulu vizuri kutokana na wengine kutohudhuria masomo wanapokuwa kwenye vipindi hivyo. 

 “TBL tunayo sera ya kujenga ulimwengu maridhawa ambayo inatekelezwa pia na wafanyakazi, ambapo mara nyingi wamekuwa wakijitoa kukabiliana na changamoto za kijamii na sio kwa kutoa pesa tu bali pia wamekuwa wakitoa hata muda wao kushiriki katika kazi za kijamii kama ambavyo wamefanikisha kutoa mchango huu” alisema Mutiganzi. 

 Kwa upande wake Mwanzilishi mwenza wa taasisi ya Her Africa nchini, Salha Kibwana, alishukuru wafanyakazi wa TBL kwa kulipa kuipa umuhimu changamoto ya vifaa vya Watoto wa kike wa sekondari kujisitiri wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi mashuleni, kwa kutoa msaada huo na amewahakikishia kuwa utawafikia walengwa 

“Nawashukuru kwa kujitoa na nina imani tukizidi kuunganisha nguvu tutafanikiwa kusaidia wanafunzi wengi zaidi hususani maeneo ya vijijini” alisema.
Share:

MPC YAKANUSHA UZUSHI WA TAARIFA YA WAANDISHI WA HABARI KUNUNULIWA BEI YA MAJI MWANZA

TAARIFA  KWA    VYOMBO   VYA HABARI  JUU YA TUHUMA ZA WAANDISHI WA HABARI

Klabu  ya  Waandishi  wa    habari    ya  Mkoa  wa  Mwanza  (MPC)  imepokea  kwa  masikitiko  makubwa    taarifa   zinazosambaa   kwenye    mitandao  ya  kijamii    juu    ya  waandishi  wa  habari  wa  Mkoa    wa  Mwanza kununuliwa    na  MWAUWASA  ili    kutoandika    habari    za  ongezeko  la  bei  za  maji  Jijini    Mwanza.


MPC  inawataka    wadau    kuzipuuza    taarifa    hizo    kwani    zina    lengo  la    kuzichafua    taasisi    zetu    mbili, MWAUWASA    NA  MPC  pamoja      na  waandishi  wa  habari  wa    Mkoa  wa  Mwanza,    kupitia    kwa  watu wachache    wasio    na  nia    njema    na  taasisi    hizo  na     wenye    uelewa    mdogo    wa  sayansi    ya    mahusiano   na  uandishi  wa  habari.   

Ifahamike  kuwa,  MPC    ndio    iliyoingia  kwenye    fungate  na  MWAUWASA  kuandaa    ziara    ya  waandishi  wa habari  wa  Mkoa  wa  Mwanza  kuitembelea    miradi  ya  maji  inayosimamiwa  na    MWAUWASA  kwa  lengo    la kujenga    ufahamu  wa  miradi  hiyo  kwa  waandishi  wa  habari  wa  Mkoa  wa  Mwanza  ,  hivyo  MPC    ndiyo  iliyoalika  waandishi  mia  moja(100)  kwenda    ziara    hiyo  na  sio  sabini    kama    inavyoelezwa  na  msambazaji wa  taarifa    hiyo,  ambaye    anaonyesha  kutofahamu  hata    takwimu    halisi.

Ndugu    Waandishi  wa  habari    ifahamike    kuwa,  ziara  za  waandishi  wa  habari   kwenda    kwenye    taasisi   fulani    kukagua  shughuli    zinazofanywa  na  taasisi    hiyo    siyo  suala    geni    hapa    Nchini,  jambo  hili   linafanywa    kila    siku,   mfano    ziara  za  waandishi  kutembelea    mradi  wa  reli  ya  kisasa  (SGR),  waandishi   kutembelea    Mbuga    za  wanyama,  waandishi  kutembelea    TBL  na  miradi  mingine,  msingi  wa  jambo  hili  ni kujenga  mahusiano   na  kuwarahisishia    waandishi    kuzifahamu    taasisi    husika    kwa  upana.

 Ikumbukwe    kuwa,  suala    la  kupanda    kwa  bei    za  maji    haikuwa    ajenda    ya    MPC    kwenye    kutembelea miradi  ya  MWAUWASA  ,  kwani      jambo  hilo  ni  jambo  la  kisheria    na  ikumbukwe  kuwa    MPC  haihusiki  kutengeneza  maudhui    ya    habari  kwa  vyombo  vya  habari,  hivyo  maamuzi  ya    kufuatilia  ongezeko  la    bei za  maji  yalibaki    kwa    vyombo    vya  habari    na  sio    ziara    ya  waandishi. 

  Pia    MWAUWASA  ilitoa  nafasi    ya    kila    Mwandishi    kuuliza    swali    lolote   alilokuwa    nalo  na  waandishi   walifanya  hivyo    na    habari    ziliandikwa  juu    ya    sababu    za  kupanda    kwa  bei  za  maji,  hivyo    waandishi walitekeleza    wajibu  wao  kwa  kufanya    uzania  kwa  pande  zote  mbili. 

Ndugu    waandishi,   mwandishi    anayesambaza  taarifa    hizo      ameshindwa    kuhoji    MPC,  MWAUWASA  na   hata    Mwandishi    mmoja    kati    ya  hao  sabini  aliowataja,  hii    inayoonyesha    udhaifu    mkubwa  wa  hoja   zake  pamoja  na  kutofahamu    msingi  wa  uandishi  wa  habari  na  sheria  mama    ya  taaluma.(MSA  Act,2016). 

Mwisho  MPC  tunaahidi    kuendelea    kufanya    kazi    na  MWAUWASA  ,  waandishi  wa  habari  na  wadau  wengine    wote    kwa  nia    ya  kuchakata      maendeleo    ya    Mkoa  wa  Mwanza.  
  
Edwin    Soko
Mwenyekiti- MPC
Share:

Picha : TACCEO YAENDESHA MAFUNZO YA UCHAGUZI KWA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA ZIWA



Mwezeshaji kwenye mafunzo ya waandishi wa habari za uchaguzi wakili wa kutoka kampuni ya TIFLD Gelina Fuko akizungumza kwenye mafunzo hayo. 


Na Marco Maduhu - Malunde1 blog


Mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia uchaguzi Tanzania (TACCEO), chini ya kituo cha Sheria za haki za Binadamu (LHRC), umeendesha mafunzo kwa waandishi wa habari Kanda ya Ziwa Victoria wakikusudia kuongeza tija katika kazi za uandishi ili kutoa elimu kwa umma ikiwemo elimu ya uchaguzi.

Mafunzo hayo yameanza leo Alhamsi Agosti 22,2019 ambayo yatadumu kwa muda wa siku tatu hadi Agost 24,2019  katika ukumbi wa mikutano Belmont Hotel Jijini Mwanza, yameshirikisha waandishi wa habari kutoka mikoa ya Shinyanga,Simiyu, Geita, Mara, Kagera, Kigoma na Mwanza.


Mratibu wa mafunzo hayo, Joseph Moses Oleshaghai kutoka kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC), amesema wanatoa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari, wakiamini kuwa waandishi wa habari ni wadau muhimu wa kufikisha elimu kwa umma ikiwemo elimu ya kiraia na uchaguzi.


“Tunatoa mafunzo haya kwa waandishi wa habari ili kuwaongezea tija kwenye kuandika habari za uchaguzi na kuwapatia wananchi ujumbe sahihi, ambao una husu masuala ya elimu ya uraia na uchaguzi, pamoja na kuwa hamasisha kujitokeza kugombea uongozi, kujiandikisha, pamoja na kupiga kura,”amesema Oleshaghai.


Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo wakili kutoka Kampuni ya (TIFLD) Jijini Dar es salaam Gelina Fuko, amewataka waandishi wa habari pale wanapokuwa wakiandika habari zao kwenye kipindi hiki cha uchaguzi, wazingatie kupaza sauti za makundi mbalimbali wakiwamo watu wenye uhitaji, walemavu, wanawake, na wazee ili waweze kupata haki zao kwenye uchaguzi.


Amesema kwenye kipindi cha uchaguzi makundi hayo maalumu ya mekuwa yakisahaurika kupaziwa sauti, na hivyo kuendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali kwenye uchaguzi, ikiwamo kunyimwa haki ya kugombea, kubaguliwa, ambapo msaada wao ni waandishi wa habari.


TAZAMA PICHA HAPA CHINI

Mratibu wa mafunzo ya habari za uchaguzi kwa waandishi wa habari Joseph Moses Oleshaghai kutoka kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC),akielezea dhumuni wa mafunzo kuhusu masuala ya uchaguzi kwa waandishi wa habari wa Kanda ya Ziwa leo. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Mwezeshaji kwenye mafunzo ya waandishi wa habari za uchaguzi wakili wa kutoka kampuni ya Tangible Initiatives for Local Development Tanzania (TIFLD) Gelina Fuko, akiwataka wanahabari kupaza pia sauti za watu wenye uhitaji kwenye kipindi hiki cha uchaguzi ili waweze kupata haki zao.

Mwandishi wa habari Nashoni Kenedy kutoka Gazeti la Daily News Jijini Mwanza, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari jinsi ya kuandika habari za uchaguzi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.

Mwandishi wa habari Moshi Ndugulile kutoka Radio Faraja Mkoani Shinyanga ,akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.

Mwandishi wa habari Salma Mrisho kutoka STARTV Mkoani Geita, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma yao na kutokwenda kinyume na sheria za uchaguzi.

Mwandishi wa habari za mitandaoni Fedrick Chibuga kutoka BMG Online TV Jijini Mwanza, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wana habari kutoka Kanda ya Ziwa juu ya kuandika habari za uchaguzi.

Mwandishi wa habari za mitandaoni Salvatory Ntandu kutoka Mpekuzi Blog, akichangia mada kwenye mafunzo hayo ya wanahabari kutoka Kanda ya Ziwa namna ya kuandika kwa usahihi habari za uchaguzi.

Mwandishi wa habari Joel Maduka kutoka Radio Storm FM Mkoani Geita naye akichangia mada kwenye mafunzo hayo wana habari Kanda ya ziwa namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi na kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi kupitia vyombo vyao vya habari.

Waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mafunzo Jijini Mwanza namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi, pamoja na kutumia vyombo vyao kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi.

Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi.

Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi na kuhabarisha umma kupitia vyombo vyao vya habari.

Mafunzo yakiendelea namna ya kuandika habari za uchaguzi kwa usahihi pamoja na kuzingatia maadili ya taaluma ya habari na sheria za uchaguzi.

Waandishi wa habari kutoka Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mafunzo Jijini Mwanza  namna ya kuandika habari sahihi za uchaguzi, pamoja na kutumia vyombo  vyao kutoa elimu ya uraia na uchaguzi kwa wananchi.

Na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:

WADAU WAKUTANA DODOMA KUJADILI USAWA WA KIJINSIA KUFIKIA 50% KWA 50% KWENYE UONGOZI


Serikali imesema imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa wanawake wanashirikishwa katika nafasi mbalimbali za uongozi ya 50 kwa 50 kufikia mwaka 2025.

Mkakati huo ni kufuatia serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuridhia kutekeleza malengo endelevu ya dunia likiwemo lengo namba 5 linalohusu usawa wa kijinsia ifikapo mwaka 2030.

Akizungumza katika kongamano la kuwaleta pamoja wadau katika kuzungumzia usawa wa kijinsia hasa katika kuwashirikisha wanawake na wasichana katika ngazi mbalimbali za uongozi na maamuzi,lililofanyika leo jijini Dodoma, mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk. Benelith Mahenge amesema kongamano limedhihirisha wananchi wanakusudia kufikia mikakati ya 2025 na malengo endelevu ya 2030.

Awali mbunge wa viti maalum Mkoa wa Dodoma Fatma Taufiq ambaye pia ni Mwenyekiti wa shirika la Achieve SDG5 Coalition in Tanzania,amesema lengo la kongamano hilo ni kuhakikisha vikwazo vinavyowakumba wanawake kushindwa kufikia lengo namba 5 katika malengo endelevu ya dunia vinapatiwa ufumbuzi.

Amesema kuwa kutokana na kuwa wafanyakazi wa ndani ni wanawake wanapata stahiki zao za malipo sambamba na ushiriki wao wa kupata nafasi za uongozi na kutoa maamuzi.

Hata hivyo baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema moja ya vikwazo violivyokuwa vinawakumba wanawake ni pamoja na rushwa katika maeneo ya kazi.

Kongamano hilo limeambatana na ujumbe usemao “Lengo namba tano la malengo endelevu litafikiwa kwa kuwawezesha wanawake na wasichana kushiriki kikamilifu katika ngazi zote za uongozi na maamuzi, Kufikia asilimia 50 % kwa 50% inawezekana.

Share:

LAAC Yaiagiza Ofisi ya CAG Kufanya Ukaguzi Nyang’hwale Ndani Ya Miezi 3 Baada Ya Kubainika Ubadhilifu Wa Zaidi Ya Tsh.bilioni 3.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Kamati ya Bunge ya  kudumu ya Hesabu za serikali za Mitaa [LAAC]imeipa   muda wa  miezi 3 ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali [C.AG] Kwenda kufanya ukaguzi Maalum katika halmashauri ya  wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita baada Ya Kubainika Ubadhilifu wa zaidi ya Tsh.Bilioni 3.
Akizungumza  Mbele ya kamati hiyo leo  Agosti 22,2019  Bungeni Jiji Dodoma  ,iliyokutanisha  watumishi wa halmshauri ya  Nyang’hwale,watumishi  wa CAG ,Makamu Mwenyekiti wa LAAC , Abdallah Chikota amesema ofisi ya CAG imetoa hati mbaya kwa halmashauri  hiyo . 

Mhe.Chikota amesema katika halmashauri ya Wilaya Ya Nyang’hwale amesema baada ya ofisi ya CAG Kufanya ukaguzi wa ndani katika halmashauri hiyo kuna upotevu wa Zaidi ya Tsh.Bilioni 3,vitabu 50 vya ukusanyaji mapato havikuwasilishwa Kwa Mkaguzi  wa CAG,Kuna hati za Malipo [Voucher] zenye thamani ya Tsh.Bilioni 1,milioni 49, laki 1,40 elfu na 91  pamoja na uhamisho wa fedha Bilioni 1 na milioni 700 bila kuonesha shughuli zinakokwenda. 

Aidha Makamu Mwenyekiti huyo wa kamati amefafanua kuwa kuna zaidi ya Tsh.Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya hazipo na kituo cha Afya hakijajengwa  huku kukiwa na Fedha za P4R  kwa Shule za Sekondari  Milioni  576 zikitumiwa nje ya Malengo yaliyokusudiwa ,Mradi wa Maji kulikuwa na salio la Tsh.Milioni 74.1 lakini benki inaonesha milioni 71.1 haipo  na hati za malipo kwenye mradi wa Maji  zenye thamani ya Tsh. Milioni  134.5 hazikuwasilishwa kwa wakaguzi. 

Naibu  Waziri wa TAMISEMI Mwita Waitara amesema jambo la ubadhilifu huo wao kama serikali limewafedhehesha sana huku akitoa wito kwa watendaji wapya kuwa waaminifu katika kuwahudumia Watanzania . 

Naye katibu tawala Mkoa Wa Geita Denis  Bandisa amesema ukaguzi  maalum wa CAG utaenda kuonesha utendaji kazi kwa halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale hata kwa viongozi wa sasa huku akibainisha kuwa wapo tayari kuipokea kamati ya CAG Kufanya ukaguzi huo.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger