Tuesday, 9 July 2019

Tanzania Kuendelea Kunufaika Kiuchumi na SADC

Na Frank  Mvungi- MAELEZO- Morogoro
Katibu Mkuu Mstaafu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Mussa Uledi amesema kuwa Tanzania inanufaika kiuchumi  kama mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo  Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja na jumuiya nyingine ambazo Tanzania ni mwanachama.
 
Akizungumza wakati akiwasilisha mada leo mjini Morogoro ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo  kwa waandishi  wa habari ya kuwajengea uwezo wa kuandika na  kuripoti   habari za SADC, Bw. Uledi amesema kuwa  nchi yetu imenufaika na utekelezaji wa miradi ya miundomnbinu,  biashara, uwekezaji  na viwanda.
 
“ Mkakati wa maendeleo wa SADC unafafanana kwa kiwango kikubwa na ule wa Tanzania ambao pia unazingatia haja ya utekelezaji wa viwanda na miundombinu hapa nchini hali itakayochangia katika kuimarisha maendeleo na kukuza uchuni na ustawi wa wananchi” Alisisitiza Bw. Uledi
 
Akifafanua amesema kuwa vipaumbele vya Tanzania vimejikita katika upanuzi wa Mauzo nje na uongezaji wa michepuo yake lengo likiwa ni kukuza na kuendeleza biashara hali inayowezesha uendelezaji wa viwanda vya kuongeza thamani katika malighafi za ndani hususan mazao ya kilimo na madini.
 
Aliongeza kuwa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli  katika baadhi ya nchi wanachama wa SADC imeonesha kuwa Tanzania imejipanga vizuri kimkakati inaweza kuwa ghala la Chakula kwa kukuza zaidi uzalishaji kuendana na mahitaji katika soko la jumuiya hiyo na hata nje ya jumuiya.
 
 Alitaja vipaumbele vingine kuwa ni pamoja na  uendelezaji miundombinu kama barabara, reli, usafiri wa anga, uzalishaji na usambazaji huduma za umeme ambayo ni nyenzo muhimu sana katika kuyaunganisha masoko ya nchi wanachama wa SADC.
 
Aliongeza kuwa vipaumbele vingine ni utafutaji wa rasilimali na utekelezaji wa miradi ya Kikanda kwa kuundwa kwa kikosi kazi cha Mawaziri wenye dhamana ya Fedha na uendelezaji miundombinu, Amani na Usalama umeendelea kuimarika ndani ya SADC.
 
Tanzania inatarajiwa kuleta msukumo mpya kwa nchi wanachama wa SADC katika utekelezaji wa miradi na program za maendeleo za Jumuiya hiyo kwa kuwa itakuwa na dhamana kubwa ya kukidhi matarajio makubwa ya nchi wanachama wakati wote wa uenyekiti wake.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, Brigedi ya Magharibi ya Jeshi  la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania (JWTZ)  Kanali Wilbert  Ibuge akiwasilisha mada katika mafunzo hayo amesema kuwa  Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa Barani Afrika zilizotoa mchango mkubwa na kuratibu kuanzishwa kwa mtangamano wa  SADC.
 
“Hadi sasa hali ya amani na usalama imeendelea kuimarika katika SADC kama inavyojidhihirisha kwa takribani nchi zote za SADC  ambapo nchi wanachama ziliazimia kusimamia maendeleo ya kiuchumi ya Kanda kwa kuzingatia malengo ikiwemo kukuza uchumi, kuondoa umasikini, kuboresha hali ya maisha ya wananchi.
 
Msingi wa SADC ni kusimamia malengo yake ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii sambamba na yale ya ulinzi na usalama unabainishwa katika Ibara ya 2 ya mkataba wa SADC ( Article 2 of SADC Treaty).


Share:

TARURA Kuanza Kutumia Mfumo Mpya Wa Malipo Serikalini

Na. Geofrey Kazaula, TARURA, Morogoro
Mfumo wa Ulipaji Serikalini (MUSE) umeanzishwa na wataalamu wa ndani ili kuunganisha mifumo mingine iliyopo, lengo likiwa ni kupunguza gharama na kurahisisha upatikanaji wa taarifa za fedha.

Hayo yameelezwa na Mhasibu Mkuu wa Serikali, Bw. Francis Mwakapalila, ambaye alikuwa mgeni Rasmi katika ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo wa Ulipaji Serikalini- MUSE kwa wahasibu na wahandisi wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini- TARURA mkoani Morogoro.

Bwana Mwakapalila alisema kuwa mfumo huo umetengenezwa na wataalam wa ndani kutoka Wizara ya Fedha na Mipango na utaanza kutumiwa na TARURA kisha kutumiwa na Taasisi zote za Serikali pamoja na Wizara baada ya kujiridhisha na ufanisi wake.

 “Nitoe wito kwa washiriki wote wa mafunzo haya kuhakikisha wanauelewa vizuri mfumo na kuwa tayari kuutumia mara tu baada ya mafunzo kukamilika kwa kuwa mfumo huu ni muhimu kutoka na mabadiliko ya teknolojia katika mifumo ya fedha duniani”, alisema Bw. Mwakapalila .

Naye Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff, amewataka wataalam wa Wakala huo wanaoshiriki mafunzo, kutokuwa na mtazamo hasi kuhusu mfumo na badala yake changamoto watakazo kutana nazo waziwasilishe mahali husika ili kuweza kutafutiwa ufumbuzi kwa kuwa mfumo huo ndio suluhisho la matumizi bora ya fedha za Serikali.

Aidha ameeleza kuwa Wizara ya Fedha na Mipango imetoa wataalam wa kutosha ili kuhakikisha wahasibu wote wa TARURA wanapatiwa mafunzo na kuuelewa mfumo kwa kina.

Kwaupande wake Mkurugenzi wa Mifumo ya Fedha wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. John Sausi, alieleza kuwa mfumo huo utaiwezesha Serikali kuangalia malipo yanayofanyika Katika Taasisi, Kampuni na wadau wengine wanaotoa huduma Serikalini .

Alisema kuwa mfumo huo ulianza baada ya kukusanya mahitaji kutoka kwa wadau mbalimbali zikiwemo Taasisi Ishirini za Serikali na kwamba Taasisi ya TARURA itakuwa ya kwanza kutumia mfumo huo kupitia wahasibu wake na wahandisi watakao kuwa wakiidhinisha malipo.

Bwana Sausi, alisema mafunzo hayo yanawahusisha wahasibu na wahandisi wa TARURA nchi nzima kuanzia ngazi ya Halmashauri lengo likiwa ni kumwezesha Mtendaji Mkuu wa TARURA kuona malipo yote yanayofanyika na Wakala huo katika sehemu mbalimbali kwa wakati.

Wizara ya Fedha na Mipango imekuwa ikitumia Mifumo ya Fedha tangu miaka ya Sitini na kutokana na ukuaji wa teknolojia imeamua kufanya maboresho ya mifumo hiyo ili kuendana na mahitaji ya sasa na kurahisisha kupata hesabu sahihi za fedha kwa wakati.

Mwisho


Share:

Katazo La Mifuko Ya Plastiki Nchini Limesaidia Kuweka Mazingira Safi.

Na Faidha Jumanne-Maelezo.
Serikali kupitia Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, kwa kushirikiana na wadau wa masuala ya mazingira imefanikiwa kuboresha upatikanaji wa mifuko bora mbadala kwa wananchi. 

Hii imetokama na jitihada za serikali za kupiga marufuku mifuko hiyo, kuanzia tarehe 01 Juni 2019 na kupelekea kupatikana kwa mifuko mbadala,  kwa wananchi inayoimarisha afya zao kuongeza ajira na kupunguza uchafuzi wa mazingira. 

Akihojiwa na Idara ya Habari - MAELEZO, Afisa Habari Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, Lulu Musa, alianza kusifia juhudi zilizopatikana kwa muda mfupi, huku akirejea Siku ya Maazimisho ya Usafi Kitaifa Jijini Dodoma, yaliyofanyika Juni 5, 2019. 

``Tumetoa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki kwa wananchi, kazi hii inafanywa na Halmashauri za Serikali za Mitaa- TAMISEMI kwa kusimamia maeneo yao kwa kutotumia mifuko ya plastiki hakika wanastahili pongezi, nasema hongereni sana”. 

Uamuzi wa Serikali kuhusu kuondoa matumizi ya mifuko ya plastiki lengo lake ni kuboresha usafi wa mazingira na kuwaweka wananchi katika hali ya kuepuka magonjwa ya milipuko kama kipindupindu na kuhara damu. 

“Lengo ni kuimarisha afya.  Kadhalika, mazingira salama ambapo, sote tunatambua umuhimu wa mtu kuwa na mazingira mazuri na yenye usalama kiafya kwa kushiriki katika shughuli za kijamii na za kitaifa”. Amesisitiza Lulu. 

Ameongeza  serikali itaendelea kuwa macho kufuatilia mwitikio mzuri wa wananchi kutoendelea kutumia mifuko ya plastiki, na kutotegemea watu wengine kusimamia mazingira ya Watanzania, kadhalika akasema bali iwe ni zoezi la kawaida kwa wananchi.  

Lulu akazidi kufafanua kuwa, serikali itaendelea kutoa elimu kwa wananchi jinsi ya kutunza mazingira kwa lengo  la kuboresha afya zao na kufahamu kwa kina mifuko ya plastiki kwa kiasi gani imeleta madhara na kusababisha magonjwa ya aina mbalimbali yakiwemo nyemelezi,  kuteketeza uhai wa viumbe kama vile samaki na mifugo. 

Aidha, Tanzania ni nchi miongoni mwa nchi zilizoonekana katika orodha ya matumii makubwa ya mifuko uya plastiki. Hii ilitokana na kuongezeka kwa kasi kwa matumizi hayo kadiri siku zilivyozidi kwenda, amesema Lulu.  

Imeelezwa pia, Serikali kwa kushilikiana na wadau kama Shirika la Viwango Tanzania -TBS limeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo kwenye sekta ya afya na mazingira yenye lengo la kuboresha matumizi ya mifuko mbadala na kuimalisha afya za wananchi. 

Mfano, TBS imeweka viwango vya ujazo kwenye mifuko ya plastiki ambayo bado inatumika kama vifungashio kuepusha kuzagaa kwa mifuko ya plastiki na kusababisha uchafuzi wa mazingira. Pia, imebainisha  viwango vya mifuko ambayo imeruhusiwa kwa kutumika kwa kufungashia chakula pamoja na madawa ya kilimo kwa kuangalia uzito/ujazo wa bidhaa, aina za bidhaa ambazo zitatumia mifuko hiyo ili kuweza kusaidia katika utunzaji wa mazingira. 

Vilevile,  Lulu aliongezea kuwa shirika la viwango, TBS litakua na uwezo wa kuwasiliana na wananchi kwa njia yoyote ile hata ikiwa kimtandao kwa kuwapa taarifa ya matumizi ya mifuko iliyo bora na yenye viwango  ili kuweza kusaidia kutoa huduma bora kwa wanainchi. 

Akielezea mfumo wa matumizi ya kidigitali Lulu amesema kuwa, Tanzania ilishaingia mfumo wa matumizi ya kidigitali katika utoaji huduma kwenye maeneo mengi, na imekuwa msaada mkubwa katika shirika la viwango TBS. 

Hata hivyo Tanzania imekua na matumizi mazuri ya mfumo wa kidigitali kwa kutoa mawasiliano kwa wananchi katika mambo mbalimbali ya kijamii na kuleta mafanikio chanya katika mwitikio wa jambo kama hili la katazo ya mifuko ya pllastiki, Lulu akasema, “Kupitia mfumo huu wa kutoa mawasiliano katika mitandao ya kijamii utasaidia kuongeza uwingi wa watu katika kupata taarifa kwa uharaka na sisi kutupelekea ufanyaji kazi wetu kutoa taarifa haraka kwa umma”.
`` … tutaendelea kuwa na utaalamu wa hali ya juu kwa kuhakikisha taarifa tutakazo zitoa zitakuwa taarifa sahihi zenye viwango sahihi kwa kutoa msaada mkubwa sana kwa kuwa hizi taarifa ni za muhimu sana kwa wananchi’’.   

Akiongea mmoja wa wananchi waliohojiwa,  Hashim Chikwaya ambaye ni mkulima amesema, “  Kutokana na kusitishwa  kwa mifuko ya plasiki,  hakika hili ni jambo jema sana kwa wananchi kwa kuwa wananchi walikuwa wakitumia mifuko hiyo kwa kuhifadhia chakula ambacho chakula hicho ni chenye joto” alisema Chikwaya.  

Akaendelea Chikwaya ambaye anaonekana kuwa na uzoefu wa kujua athari za mifuko, kuwa Kutokana na joto la kwenye mfuko linasababisha kutoa mvuke wenye majimaji ya tindikali ambayo imetumika kutengenezea mfuko huo na kuingia kwenye chakula, iwapo chakula hicho kikiliwa na mtu, hupata athari kubwa za kiafya.   

Vilevile, akielezea zaidi adhari za kiafya Chikwaya alisema “Kulikuwa na matumizi mengine yasiyokuwa ya lazima pale mtu anapochukua mfuko wa plastiki kwa matumizi ya kuwashia moto, hususani jiko la mkaa, kitendo hicho kinapofanyika mtu huyo anavuta hewa ya mfuko unaoyeyuka na kumsababishia madhara ya kupata ugonjwa wa kansa”. 

Akimalizia, Chikwaya alisema, mbali na uchafuzi wa mazingira mara nyingi, mfano hospitali madaktari walikuwa wakishauri kuepukana na matumizi ya vifaa vya plastiki kuhifadhia chakula chenye joto na kusema kuwa plastiki hizo huchubuka zipatapo joto na kusababisha athari ya upatikanaji wa magojwa pinde ulapo chakula hicho, akaongeza, “hata hivyo si rahisi kuona michubuko hiyo kwa macho”.  

Zoezi la katazo la Mifuko ya Plastiki limeanza Juni mosi, 2019 ambapo mpaka sasa kwa tafiti imeonyesha mafanikio, mfano katika Jiji la Dar-es-salaam wengi waliohojiwa mitaa ya Kariakoo wamesema mitaa yao inaonekana safi kwa kuondolewa mifuko hiyo na hivyo wanaishukulu serikali.      


Share:

UWT MANISPAA YA IRINGA WANAWAKE KOPENI KWA MALENGO


Mwenyekiti wa umoja wa wanawake Manispaa ya Iringa (UWT) Ashura Jongo akizungumza wakati wa baraza la UWT manispaa ya Iringa akiwaasa wanawake kukopa kwa malengo.

Mwenyekiti wa CCM manispaa ya Iringa Said Rubeya akitoa neno kwa wanawake wa UWT manispaa ya Iringa. 


Na Fredy Mgunda,Iringa. 

Kukosekana kwa elimu ya matumizi bora ya mikopo kwa wanawake kumetajwa kuwa sababu ya wanawake wengi wa manispaa ya Iringa kushindwa kurudisha mikopo katika taasisi za kifedha.

Akizungumza kwenye baraza la UWT manispaa ya Iringa,mwenyekiti wa umoja huo Ashura Jongo  amesema kuwa wananwake wamekuwa wanakopa bila ya kuwa na elimu ndio maana wanashindwa kurejesha mikopo ambayo wamekopa kwenye taasisi za kifedha.

“Changamoto za wanawake kutokuaminika katika vyombo au taasisi za kifedha ni kutokana na hali ngumu,wanawake wanaweza wakakopa wakiwa na malengo lakini wakirudi nyumbani wanakutana na matatizo mengi yanahitaji matumizi ya fedha” aliema Jongo

Jongo alisema kuwa wanawake wanatakiwa kuendelea kuwawezesha kwa kuwa wanauwezo wa kutmia vizuri fedha ambazo zinapatikana hivyo ukimuwezesha mwanamke umewawezesha watu wengi kwa kuwa wanawake ndio nguzo ya familia hasa kwenye maswala ya kiuchumi.

Kwa upande wake mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi Rose Tweve amezitaka taasisi za kifedha kutoa elimu kwa wakopaji ili waweze kuzitumia vizuri fedha hizo.
“Shida moja wapo ya wanawake kushindwa kurudisha mikopo ni kutokana na kutokuwa naelimu ya matumizi ya fedha kwa kuwa pesa hiyo inahitaji nidhamu na matumizi bora ya fedha hizo za mikopo” alisema Tweve

Tweve alisema kuwa tasisi za kifedha zinatakiwa kutoa elimu kwanza kabla ya kutoa mikopo kwa wanawake ili waweze kuzirejesha kwa wakati kwa kuwa tayari ameshapata elimu ya matuzi bora ya mikopo waliyokopa.

“Pale wanapokopa lazima wajue matumizi ya hizo pesa la sivyo watazitumia bila nidhamu fedha hizo na kushindwa kuzirejesha na kujikuta wakiwa matatani kutokana na kushindwa kulipa mkopo huo” alisema Tweve

Naye mgeni rasmi kwenye baraza hilo mwenyekiti wa CCM manispaa ya Iringa Said Rubeya amewataka wanawake kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha ili kufikia malengo waliyojiwekea kabla ya kwenda kukopa.

“Kwa kwali wanawake wa CCM manispaa ya Iringa wengi mnakopa mikopo lakini hamrejeshi kwa wakati na hili ni bomu kubwa kwa chama hivyo mnatakiwa kuwa na nidhamu ya matumizi ya mikopo hiyo” alisema Rubeya
Share:

Live : RAIS MAGUFULI ANAZINDUA HIFADHI MPYA YA TAIFA YA BURIGI CHATO

LIVE:Rais Magufuli anazindua Hifadhi mpya ya Taifa ya Burigi Chato


Share:

Upandaji holela wa miti katika njia za umeme Kahama watajwa kusababisha nishati ya umeme kukatika.

NA SALVATORI NTANDU
Upandaji holela wa miti katika njia kuu za Umeme Wilayani kahama mkoani Shinyanga umetajwa kuchangia kusababisha Nishati hiyo kukatika mara kwa mara kutoka na miti hiyo kugusa nyanya za Umeme.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wilayani Kahama Mhandisi King Fokanya wakati akizungumza na waandishii wa habari ofini kwake kuhusiana namna walivyojipanga kutoa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji wa miundombinu ya umeme.

Amesema katika maeneo mengi wilayani humu wananchi wamepanda miti mikubwa katika karibu na nguzo za umeme jambo ambalo linaweza kuleta madhara makubwa pindi nguzo zinapo anguka ama kuguswa na miti hiyo.

Amefafanua kuwa pindi Shirika hilo linapotaka kuikata baadhi yao wamekuwa wakilaumu juu ya ukataji wa miti hiyo katika njia za umeme na watumishi wake katika oparesheni za kuhakikisha miundombinu hiyo inakuwa salama.

Katika Hatua nyingine Mhandisi Fokanya amesema katika mwaka wa fedha wa 2019/2020 Ofisi yake imepokea shilingi milioni 847 kwa ajili ya kupeleka huduma ya nishati ya umeme kwenye kata 10 ambazo hazina umeme zilizopo Halmashauri ya Mji wa Kahama na Msalala.

Amefafanua kuwa  shilingi Milioni 847 zimegawanya katika makundi mawili ambapo shilingi milioni 402 zitatumika kupeleka huduma ya nishati ya umeme kwenye kata 10 msalala na kahama mjini huku Milioni 445 zinatumika kwenye mategenezo ya kubadilisha nguzo,vikombe, maboresho ya Transfoma na vifaa vilivyoharibika.

Kata ambazo zinapelekewa huduma hiyo ni pamoja  kata ya Muhungula, Nyakato, Mbulu, Mhongolo, Nyashimbi, Nyihogo sekondari, Kagongwa, Mwendakulima Isaka na Kakola.

Mwisho.


Share:

Makamu Wa Rais Mhe. Samia Ahudhiria Mkutano Wa 12 Wa Dharura Wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika kuhusu Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan,  ameshiriki katika Mkutano wa 12 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) unaofanyika jijini Niamey nchini Niger.
 
Makamu wa Rais Mhe. Samia ameipongeza Serikali ya Ghana kwa kuchaguliwa kuwa Makao Makuu ya Sekretarieti ya AfCFTA na kuisihi Kamisheni ya Umoja wa Afrika kuharakisha ukamilishaji wa muundo, wa bajeti na mpango kazi  wa Sekretarieti hiyo ili ianze kufanya kazi haraka.
 
Mkutano huo wa Wakuu wa nchi na Serikali umepokea taarifa ya Mheshimiwa Mahamadou Issoufou, Rais wa Jamhuri ya Niger kuhusu utekelezaji wa AfCFTA ambayo imepokelewa na kupishwa na viongozi hao. Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) umeanza kazi rasmi tarehe 30 Mei, 2019 na unahusu uasili wa bidhaa zitakazouzwa katika soko la Afrika, kufungua biashara ya bidhaa kwa asilimia 97 na uanzishwaji wa Sekretarieti ya kusimamia utekelezaji wa Mkataba wa AfCFTA.
 
Aidha, alimpongeza Mheshimiwa Mahamadou Issoufou, Rais wa Jamhuri ya Niger kwa jitihada zake za kuhakikisha azma ya Umoja wa Afrika ya kuanzisha Soko Huru la pamoja la Afrika inafikiwa. 

Makamu wa Rais pia alizipongeza nchi 27 wanachama wa Umoja huo zilizoridhia mkataba wa uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) kati ya nchi 54 zilizotia saini mkataba huo na kuahidi kwamba Tanzania itaungana nao baada ya kukamilisha taratibu za ndani.
 
Kwenye mkutano huo Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambapo alitoa salam za Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Wakuu wa Nchi na Serikali waliohudhuria mkutano huo.
 
Wakati huo huo Waziri wa Fedha na Uchumi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa amesema kwa upande wa Afrika Mashariki  Tanzania imepiga hatua zaidi kutokana na kuwepo katika Jumuiya za Afrika Mashariki na SADC, hivyo Tanzania imefaidika sana kutokana na kupanuka kwa Soko hilo.
 
Nae Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro amesema Tanzania imenufaika na mkutano huo kutokana na kuendelea kujifunza zaidi kuhusiana na Biashara ya pamoja katika Afrika pamoja na kuweza kushiriki kuchagua Muwakilishi wa Bara la Afrika katika nafasi mbalimbali ndani ya Afrika na Duniani kote wakati Tanzania imepata nafasi moja ambapo Bethabina Seja Afisa wa Takukuru amechaguliwa katika Bodi ya kudhibiti Rushwa Barani Afrika.


Share:

Bunge la Tanzania kuwa mwenyeji wa vikao vya Kamati ya Uongozi na ya Bajeti za Chama cha Wabunge wa Nchi za Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika

Bunge la Tanzania linatarajia kuwa mwenyeji wa vikao vya Kamati ya Uongozi na ya Bajeti za Chama cha Wabunge wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika (CPA-AFRICA REGION) vitakavyofanyika tarehe 9 hadi 14, Julai, 2019 katika Ofisi Ndogo za Bunge la Tanzania, Jijini Dar es Salaam.

Kamati hizo zitakutanisha Wajumbe kutoka Mabunge zaidi ya Kumi (10) ya nchi za Afrika ambapo mbali na Wajumbe hao vikao hivyo pia vinatarajiwa kuhudhuriwa na Spika wa Bunge la Kenya Mhe. Justin Muturi, Spika wa Bunge la Sierra Leone Mhe. Dkt. Abbas Bundu, Spika wa Bunge la Uganda Mhe. Rebbeca Kadaga na Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Job Y. Ndugai ambaye ndiye mwenyeji wao.
 
Aidha, mbali na Maspika hao, vikao hivyo vitahudhuriwa na Naibu Spika wa Bunge la Cameroon Mhe. Emilia Lifaka, Naibu Spika wa Bunge la Namibia, Mhe. Bernard Sibalatani na pia Mnadhimu Mkuu wa Bunge la Ghana Mhe. Dkt. Osei Mensah Bonsu.
 
Mbali na vikao vya Kamati, kutakuwa pia na kikao cha Bodi ya Chama cha Wabunge wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola-Kanda ya Afrika ambacho kitafanyika tarehe 11 Julai, 2019.
 
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Job Y. Ndugai anatarajiwa kuhudhuria na kuongoza kikao cha Bodi ya Chama cha Wabunge wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika na pia kutoa hotuba ya ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Uongozi wa chama hicho.
 
Wajumbe wengine ambao ni Waheshimiwa Wabunge wanaotarajiwa kuhudhuria katika vikao hivyo wanatoka katika Mabunge ya nchi za Malawi, Kenya, Nigeria, Ghana, Sierra Leone, Afrika kusini, Uganda, Namibia, Zambia, Lesotho, Mauritius na wenyeji Tanzania. Kwa hivi sasa Bunge la Tanzania ndiyo Sekretarieti ya Chama Chama cha Wabunge wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola–Kanda ya Afrika.
 
Imetolewa na;
KATIBU WA CPA-KANDA YA AFRIKA
8 Julai, 2019


Share:

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE


Atletico Madrid imeanzisha mchakato wa kumuadhibu mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 28, ambaye anatarajiwa kuhamia Barcelona kwa dau la £107.5m . (Guardian)

Real Madrid inafikiri kumuuza mshambuliaji wake raia wa Colombia James Rodriguez, 27, ili kukusanya £150m kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba, 26. (Mail)

Napoli ina hamu ya kumsaini James kutoka Real Madrid, pamoja na mshambuliaji wa Argentina na Inter Milan Mauro Icardi, 26. (Goal.com)

Bayern Munich inataraji winga wa Ujerumani Leroy Sane, 23, kuamua wiki ijayo iwapo anataka kujiunga na mibabe hao wa Ujerumani kutoka Manchester City. (Mail)

Arsenal, Manchester United na Paris St-Germain wana hamu ya kumsaini kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 24, kutoka Chelsea. (RMC Sport - in French)

West Ham wanafikiria kulipa dau la £43.5m na kuishinda Valencia ili kumsajili mshambuliaji wa Celta Vigo na Uruguay 22. (Evening Standard)

Mshambuliaji wa Manchester United na Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, anatumai kuwa mchezaji wa Inter Milan kufikia wakati ambapo ataikabilia Man United tarehe 20 mwezi Julai.. (Mirror)

Aston Villa wamewasilisha ofa ya dau la £7m kumnunua kipa wa Burnley na Uingereza Tom Heaton, 33. (Sun)

Arsenal inakaribia kumsajili beki wa Saint-Etienne William Saliba, huku mchezaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 8 akidaiwa kugharimu £25m. (Evening Standard)

Beki wa kushoto wa Liverpool, 27, raia wa Uhispania Alberto Moreno anakaribia kuhamia Villarreal. (ESPN)
Gareth Bale alikuwepo wakati wachezaji wa Real Madrid waliporudi katika maandalizi ya msimu mpya siku ya Jumatatu , baada ya wachache kutomtarajia mshambuliaji huyo katika timu hiyo. (Marca)

Manchester City inakaribia kumsaini kinda wa Uingereza anayechezea timu ya Uingereza ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 Morgan Rogers kutoka West Brom, (Mail)

Everton inakaribia kuwasilisha ofa ya dau la £35m kumnunua mshambuliaji wa Barcelona na Brazil Malcom.
Arsenal pia inamnyatia mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23. (RMC Sport - in French)

Watford ina hamu ya kumsajili winga wa Ufaransa Allan Saint-Maximin, 22, kutoka klabu ya Nice kwa dau la rekodi la £25m. (Sky Sports)

Aston Villa ina hamu ya kusalia kwa mkopo beki wa Man United Axel Tuanzebe baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 kuhudumu msimu wake uliopita akichezea klabu hiyo. (Telegraph)

CHANZO.BBC SWAHILI
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 9 July























Share:

Monday, 8 July 2019

Waandishi wa Habari Waaswa Kuzingatia Uzalendo na Weledi Wanapotangaza Fursa Zilizopo SADC

Na Frank Mvungi- MAELEZO,  Morogoro
Waandishi wa Habari nchini wameaswa kuzingatia uzalendo na weledi  katika utekelezaji wa majukumu yao  wakati wote wa kuripoti habari zinazohusu fursa zilizopo katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  pamoja na mkutano wa wakuu wa nchi wanachama utakaofanyika Jijini Dar es Salaam Agosti 17 na 18, 2019. 

Akizungumza leo mjini Morogoro wakati akifungua awamu ya kwanza ya mafunzo yakuwajengea uwezo  waandishi wa habari ili waweze kuandika na kuripoti habari za Jumiya hiyo, Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza amesema  kuwa mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama unakuja na fursa nyingi zitakazowanufaisha wananchi wote. 

“  Tunawaomba Waandishi wa Habari kutekeleza jukumu la kutangaza habari zinazohusu SADC kwa uzalendo, weledi na kwa ufanisi ili watanzania waweze kushiriki kikamilifu kutokana na umuhimu wa Jumuiya hii na kutumia fursa za kiuchumi na biashara zinazopatikana kupitia wananchi takribani milioni 450 wa nchi zote za SADC”Alisisitiza Mhe Shonza 

Akifafanua Mhe Shonza amesema kuwa  kila mwandishi wa habari analo jukumu la kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafahamu fursa zilizopo katika Jumuiya hiyo na mamna zinavyoweza kuwanufaisha wananchi wote katika nyanja za kiuchumi na kijamii. 

Aliongeza kuwa  waandishi wa habari wa Tanzania kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na uelewa wa pamoja wakati wa mkutano huo  kwa kutambua kuwa wao ni daraja kati ya wananchi na Serikali pamoja na Jumuiya zote ambazo Tanzania ni mwanachama ikiwemo SADC. 

“Ni matumanini yangu kuwa baada ya mafunzo haya mtawaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa SADC kwa maendeleo ya kiuchumi ya nchi wanachama, fursa za kiuchumi, Namna nchi yetu inavyotekeleza mikakati mbalimbali ya SADC, Fursa za masoko ndani ya SADC kutokana na bidhaa na mazao ya kilimo yanayozalishwa katika nchi wanachama” Alisisitiza Mhe Shonza 

Katika kusisistiza umuhimu wa amani na utulivu Mhe. Shonza aliwaasa wanahabari kuwaelimisha wananchi umuhimu wa amani kipindi choche cha mkutano huo wa wakuu wa nchi wanachama na hata baada  ili kuendelea kujenga taswira nzuri ya Tanzania. 

Baadhi ya fursa zinazotokana na mkutano wa 39 wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo utakaofanyika mwezi ujao hapa nchini ni pamoja na usafiri na usafirishaji, malazi na utalii kwa wageni hao zaidi ya 1000 wanaotarajiwa kuja hapa nchini kutokana na mkutano huo. 

Aidha, Mheshimiwa Shonza aliwataka waandishi wote wa habari hapa nchini kutumia nafasi zao kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa amani iliyopo hapa nchini ambayo ni moja ya kivutio kikubwa kwa wageni kutoka mataifa mbalimbali kuja na kuwekeza hapa nchini. 

“ Sitarajii mwandishi wa habari wa Tanzania kutumia kalamu yake kuchafua taswira ya nchi yetu katika kipindi hiki cha mkutano huu mkubwa na hata baada ya  mkutano, matarajio ya Serikali ni kuendelea kuona mnatangaza mafanikio ya Jumuiya na fursa zilizopo ili ziweze kuwanufaisha wananchi” Alisisitiza Mhe. Shonza 

Katika kutekeleza jukumu hilo amewaasa waandishi hao kuzingatia kuwa jukumu la kutangaza fursa zilizopo katika Jumuiya hiyo ni la kila mwanahabari  ili kuwajengea uelewa wananchi  juu ya namna watakavyoweza kunufaika na idadi kubwa ya wananchi waliopo katika jumiya hiyo. 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) linalodhamini mafunzo hayo kwa kushirikiana na Sekretarieti ya SADC, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  Bw. Dagmore Tawonezvi amesema kuwa  mafunzo hayo yanatokana na maombi ya Serikali ya Tanzania na yatasaidia kujenga uelewa kuhusu fursa zilizopo na namna ya kuzitumia ili kuchochea maendeleo hapa nchini na katika nchi wanachama wa SADC. 

Aliongeza kuwa Shirika hilo litaendelea kushirikiana na nchi wanachama kujenga uwezo kwa waandishi wa habari ili waweze kutangaza na kuwaelimisha wananchi kuhusu jumuiya hiyo na manufaa yake katika kukuza uchumi. 

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi Agnes Kayola amesema kuwa mafunzo hayo yanafanyika kwa awamu mbili zitakazoshirikisha waandishi wa habari 30 kwa kila awamu. 

Mkutano huo utatanguliwa na maonesho ya wiki ya viwanda  yatakayotumika kutangaza bidhaa zinazozalishwa hapa nchinina nchi za SADC kwa madhumuni ya kuhamasisha ukuaji wa viwanda katika nchi za  SADC . 

Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo unafanyika Tanzania mwezi Ujao ambapo Tanzania inatarajiwa kupokea wageni zaidi ya 1000 kutoka nchi wanachama wa SADC, katika mkutano huo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe  Magufuli anatarajia kuwa mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Agosti 2019 hadi Agosti 2020. 

Mkutano  huo wa wakuu wa nchi wanachama utakuwa na kauli mbiu ”Mazingira wezeshi ya Kibiashara kwa Maendeleo Jumuishi na Endelevu ya Viwanda” utatanguliwa na vikao vya awali vya ngazi ya Makatibu Wakuu na Mawaziri wa SADC, Unatarajiwa kuhudhuriwa na wakuu wa    nchi 16 wanachama wa SADC .


Share:

Balozi Sokoine Afungua Mafunzo Ya Wawezeshaji Wa Mashamba Darasa

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine leo amefungua Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini (ldfs), katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro.

“Ni matumaini yangu kuwa elimu na ufahamu mtakauopata kupitia mafunzo haya, mtaitumia katika kufanikisha uanzishaji wa mashamba darasa katika maeneo ya mradi” alisema Balozi Sokoine.

Mafunzo hayo ya siku 5 yanalenga kujenga uwezo kwa washiriki katika uanzishaji wa mashamba darasa katika vijiji na shehia ambako mradi wa LDFS unatekelezwa.

Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wamekuwa wakitekeleza miradi inayolenga kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo kwa kusogeza karibu teknolojia kwa wakulima. Lengo likiwa ni kuongeza usalama wa chakula na kuongeza kipato cha jamii. Mradi wa LDFS ambao umeandaa mafunzo haya ni mfano wa juhudi hizo za Serikali. Juhudi hizi zinahusisha uingizaji na matumizi ya teknolojia mpya ikiwemo matumizi sahihi ya mbolea, mbegu zenye ubora; uboreshaji wa nyanda za malisho; utoaji wa huduma za ugani na mafunzo kupitia shamba darasa. Juhudi hizi zote zina lengo la urejesha ardhi iliyoharibika ili iweze kuendelea kuzalisha mazao ya kilimo, mifugo na misitu.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi huo wa LDFS Bw. Joseph Kihaule amesema mradi huo utajumuisha na uanzishwaji wa mashamba darasa 100.

Wawezeshaji wa mradi huo ni Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO), Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Wakala wa Taifa wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA) ambapo washiriki wa mafunzo hayo wametoka Wizara za Kilimo, Maliasili na Utalii, Maji, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Idara ya Mazingira, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar. Aidha, washiriki wengine ni kutoka katika Halmashauri zinazotekeleza Mradi za Mkalama, Micheweni, Magu, Nzega na Kondoa, pamoja waalikwa rasmi Daktari Moses Temi na Bwana Charles Mjema.


Share:

TFF Yasitisha Mkataba na Kocha Amunike Taifa Stars

Aliyekuwa kocha mkuu wa Taifa Stars Emmanuel Amunike, amefutwa kazi na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ikiwa ni siku chache zimepita baada ya timu hiyo kutolewa hatua ya makundi kwenye fainali za AFCON.

Taarifa iliyotolewa ya TFF leo, imeeleza kuwa pande mbili zimefikia makubaliano ya kusitisha mkataba huo.

''Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Kocha wa Timu ya Taifa “Taifa Stars” Emmanuel Amunike tumefikia makubaliano ya pamoja kusitisha mkataba baina yetu''.

Aidha TFF imeweka wazi kuwa itatangaza kocha wa muda atakaekiongoza Kikosi cha timu ya Taifa kwa mechi za CHAN.

Pia wamefafanua zaidi kuwa makocha wa muda watatangazwa baada ya Kamati ya Dharura ya Kamati ya Utendaji (Emergency Committee) itakapokutana Julai 11,2019.

Kwasasa shirikisho limebainisha kuwa mchakato wa kutafuta Kocha mpya umeanza mara moja.



Share:

Katibu Mkuu Wizara Ya Fedha Na Mipango Doto James Awataka Watumishi Kuwajibika Na Kuzingatia Maadili Ya Kazi

Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Fedha ya Mipango wametakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma katika kutekeleza majukumu yao.

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Doto James wakati wa kikao cha watumishi wa Wizara hiyo.

Bw. James alisema kuwa watumishi wote wanawajibu wa kufanya kazi kwa ufanisi na weledi na kwa kuzingatia nidhamu, maadili, sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa Umma.

“Ni wajibu wa kila mtumishi kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi  wote wanaohitaji huduma katika Wizara yetu” Alisema Bw. James.

Aidha Bw. James aliwapongeza Watumishi wa Wizara hiyo kwa kazi wanazozifanya hususan kazi ya uandaaji wa Bajeti Kuu ya Serikali iliyopishwa na Bunge hivi karibuni na kuwataka waendelee kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa Bajeti hiyo.

Kwa upande wa Watumishi wa Wizara hiyo waliupongeza uongozi wa Wizara hiyo kwa kutenga muda wa kuzungumza nao na kusikiliza changamoto mbalimbali zinazo wakabili pamoja na kuzitolea ufafanuzi.

Waliahidi kutatekeleza maelekezo yote aliyotolewa kwa uadilifu ili kuongeza ufanisi wa kazi kwa maendeleo ya nchi.


Share:

Waziri Mpango Atoa Tahadhari Kwa Taasisi Za Kifedha Kuwa Makini Na Mitandao Ya Kimataifa Ya Uhalifu.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango amezitaka taasisi za kifedha hapa nchini kuwa makini na mitandao ya uhalifu ya  kimataifa. 

Waziri Mpango amesema hayo leo Julai 8,2019  katika hafla fupi  ya kupokea  hundi ya gawio kwa  serikali kutoka benki ya NMB ambapo jumla ya Tsh.Bilioni 10.48 zimetolewa na Benki  hiyo kama gawio kwa serikali ambayo ni sehemu ya faida. 

Waziri mpango amesema pamoja na mafanikio ya benki Ya huduma za kibenki hapa nchini lakini bado kuna changamoto za uhalifu wa kimtandao ambapo Wizara yake imepokea  kesi na malalamiko mbalimbali yanayotokana na uhalifu  wa  mitandao. 

Hivyo Dokta Mpango ametoa tahadhari  kwa taasisi za kifedha  nchini  kuwa macho  na wahalifu na watakatishaji wa fedha   kupitia Mitandao ya kimataifa. 

Mwenyekiti wa bodi ya Benki ya NMB Prof.Joseph Semboje amesema kwa kipindi cha miaka  10 iliyopita Benki hiyo ilishalipa Tsh.Milioni 118 serikalini kama gawio. 

Naye Afisa mkuu wa Fedha kutoka benki ya NMB Bi.Ruth Saikuna amesema benki hiyo ilitengeneza faida ya Tsh.Bilioni 142 kwa  mwaka 2018 sawa na ongezeko la asilimia 3%.


Share:

TFF YAMTUMBUA AMUNIKE STARS

Shirikisho la Soka Nchini Tanzania limetangaza kuachana na kocha wa timu ya taifa Taifa Stars Emmanuel Amunike mara baada ya kufikia makubaliano ya pamoja kwa pande zote mbili kusitisha mkataba baina yao. 

Taarifa ya Shirikisho la Kabumbu Nchini Tanzania kwenda kwa vyombo vya Habari inasema kuwa Kocha atakayeiongoza Stars katika michezo ya CHAN atatangazwa hivi karibuni. 
Makocha wa muda watangazwa baada ya kamati ya Dharura ya kamati ya utendaji (Emergency Committee) itakapokutana Julai 11,2019. 

Huku mchakato wa kumpata Kocha mpya ukiwa umeanza mara moja.
Share:

AGIZO LA WAZIRI JAFO LATEKELEZWA KWA VITENDO WILAYANI PANGANI



KATIBU Tawala wa wilaya ya Pangani Mkoani Mwalimu Hassani Nyange akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Pangani akiwa na viongozi wengine wa Halamshauri hiyo wakati walipotembelea shule za Msingi Pangani na shule ya Sekondari Funguni kufuatilia utekelezaji wa agizo la Waziri Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Suleimani Jaffo la kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hapa nchini wanaimba nyimbo tatu za uzalendo ikiwemo ule wa Taifa,Tazama Ramani na Naipenda Tanzania
KATIBU Tawala wa KATIBU Tawala wa wilaya ya Pangani Mkoani Mwalimu Hassani Nyange akiuzngumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Pangani akiwa na viongozi wengine wa Halamshauri hiyo wakati walipotembelea shule za Msingi Pangani na shule ya Sekondari Funguni kufuatilia utekelezaji wa agizo la Waziri Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Suleimani Jaffo la kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hapa nchini wanaimba nyimbo za uzalendo ikiwemo ule wa Taifa,Tazama Ramani na Naipenda Tanzania kulia ni Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George
Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George kushoto akiwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani (DAS) Mwalimu Hassani Nyange kulia wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuzungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Pangani
Sehemu ya wanafunzi wa shule ya Msingi Pangani wakimsikiliza kwa umakini Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange
Sehemu ya wanafunzi wa shule ya Msingi Pangani
KATIBU Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Funguni
AGIZO La Waziri Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Suleimani Jaffo la kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hapa nchini wanaimba nyimbo za uzalendo ikiwemo ule wa Taifa,Tazama Ramani na Naipenda Tanzania limeanza kutekelezwa kwa vitendo wilayani Pangani mkoani Tanga.

Utekelezaji huo umeanza leo Julai 8 mwaka huu kwa Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani (DAS) Mwalimu Hassani Nyange ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo wilayani humo akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa wilaya hiyo kutembelea shule za Msingi Pangani na shule ya Sekondari Funguni kufuatilia utekelezaji huo.

Agizo hilo la Waziri Jaffo alilitoa hivi karibuni wakati akifunga mashindano ya Michezo ya Umoja wa shule za Msingi Tanzania (Umitashumta) yaliyokuwa yakifanyika mkoani Mtwara ambapo aliagiza kwamba wakati wanafunzi watakapofungua shule wanatakiwa kuimba nyimbo tatu kabla ya kuingia madarasani asubuhi Nyimbo hizo ni wimbo wa Taifa,Wimbo wa Uzalendo (Tanzania tanzania) na Tazama Ramani utaona nchi nzuri kwa maafisa elimu Kata na wakuu wa shule wasimamie hilo.

Akizungumza mara baada kikao cha wadau wa elimu kilichohusisha wakuu wa shule za msingi na sekondari,Waratibu Elimu Kata,Watu wa tume ya Utumishi wa walimu wa kudhibiti ubora wa elimu ambacho kilikuwa ni mahususi ya kuona namna ya kuendeleza utekelezaji wa agizo hilo na baadae kutembelea kwenye shule hizo kuona namna wanafunzi wanavyoweza kuimba nyimbo za uzalendo wanapokuwa shuleni na hivyo kujiridhisha.

Alisema kwamba wao kama wilaya wataendelea kulisimamia ipasavyo na kulitekeleza agizo hilo kwa vitendo huku wakianza na hatua ya kwanza kwa kuwaita kwenye kikao hicho huku akimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Isaya Mbenje na Wakuu wa Idara kwa kuweka mikakati ya kuona namna gani agizo hilo linatekelezwa kwa kuhakikisha wanaandika upya kwenye makaratasi na kubandikwa kila darasa wanalosoma wanafunzi.

"Lakini kubwa ni kwamba kila mwanafunzi achague kwenye somo wanayosoma achukue daftari moja aandika nyimbo hizo vizuri kwa nyuma kujikumbusha mara kwa mara kwa lengo la kuweza kuutambua na kuweza kuimba kwa ufasaha zaidi kila wakati ",alisema.

Hata hivyo Katibu Tawala huyo aliwaagiza Waratibu wa kata wahakikishe maelekezo yaliyotolewa yanafanyiwa kazi na kupita kwenye kukagua kuona kama nyimbo hizo zimefundishwa.

Awali akizungumza Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George alisema kwamba wamefika kwenye shule hizo kutekeleza agizo la Jafoi shule zao zirudi kwenye msingi ya kukumbushia nyimbo za uzalendo kwa wanafunzi.

Alisema pia wataendelea kuwajenga vijana kuhusu uzalendo wakiwa wadogo ili kutengeneza Taifa Bora la kesho ambalo litakuwa chachu ya maendeleo kwa watanzania

Naye Mkurugenzi wa Halmshauri ya wilaya ya Pangani Isaya Mbenje alisema kwamba ni imani yake kwamba watendaji wa sekta ya elimu watakwenda kufanyia kazi kwa kuweka uelewa wa pamoja.

Alisema kwamba uelewa huo unaweza kuwasaidia kuona namna ya utekelezaji wa agizo hilo la serikali katika kujenga nidhamu,uzalendo wa vijana wa shule za msingi na sekondari za serikali wilayani humo.

Hata hivyo naye pia Afisa Elimu Taaluma wa wilaya ya Pangani Marietha alisema kwamba wanamshukuru Waziri Jaffo ambaye alihuisha uzalendo wa nchi kutokana na kwamba watu walikuwa wamejisahau sana nyimbo hizo miaka ya nyuma zilizokuwa ngao lakini kutokana na kwamba hapo katikati walipotea na kusahau hivyo wanahaidi kufanya vizuri sana
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger