Wednesday, 16 January 2019

MILIPUKO NA MILIO YA RISASI YASIKIKA JIJINI NAIROBI, MAGARI YACHOMWA MOTO,WENGI WAJERUHIWA.

Na,Jovine Sosthenes. Taharuki iliibuka jana mjini Nairobi kufuatia shambulio la milipuko na risasi inayosadikiwa kufanywa na magaidi katika eneo la 14 Riverside Drive, katika Hoteli ya Dusit D2 jijini Nairobi, Kenya na kusababisha vifo vya watu watano na kujeruhi wengine tisa. Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Kenya, Shambulio hilo linadaiwa kutokea Januari 15,2019. Mda, saa 9 alasiri na kusababisha watu kadhaa kujeruhiwa huku magari manne yakichomwa moto na milio ya risasi ikidaiwa kusikika kutoka eneo la tukio. Bado wahusika wa shambulio hilo hawajajulikana lakini askari wa Kitengo cha…

Source

Share:

Tuesday, 15 January 2019

KAMPUNI YA GURU,MANISPAA YA ILALA WAANDAA TAMASHA KUWAKUTANISHA WAFANYABIASHARA

Na Heri Shaban,Dar es salaam. Kampuni ya Guru Planet Kwa kushirikiana na manispaa ya Ilala wanatarajia kufanya tamasha la wajasiriamali January 29 Mwaka huu. Tamasha hilo linatarajia kufanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja wilayani Ilala jijini Dar es Salam ambapo wajasiliamali watapata fursa mbalimbali. Akizungumza Dar es Salam leo mkurugenzi wa kampuni ya Guru Planet Nickson Martin alisema tamasha hilo wameshirikiana na Idara ya maendeleo ya jamii manispaa Ilala dhumuni la tamasha hilo kuwapa fursa Wajasiriamali waweze kutangaza biashara zao na kubadilishana uzoefu. “Katika tamasha hili litakuwa siku tatu mgeni…

Source

Share:

TZS 94.01 BILLIONS ZAKUSANYWA NA HESLB KATI YA JULAI– DESEMBA, 2018

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imekusanya jumla ya TZS 94.01 bilioni kutoka kwa wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu katika kipindi cha Julai – Desemba, 2018 na kuvuka lengo lake la kukusanya TZS 71.4 bilioni katika kipindi hicho. Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema leo jijini Dar es salaam kuwa makusanyo hayo yametoka kwa jumla ya wanufaika zaidi 198,659 ambao wamejiari au kuajiriwa katika sekta binafsi na umma. Wanufaika waliobainika na kuanza kulipa kati ya Julai – Disemba 2018 “Katika kipindi hicho cha…

Source

Share:

MKUU WA WILAYA AWAFUKUZA UKUMBINI MKURUGENZI , MWENYEKITI WA HALMASHAURI


Uamuzi wa mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya kuwaondoa ukumbini mkurugenzi na mwenyekiti wa halmashauri ya Hai waliokuwa wakiongoza kikao cha kamati ya fedha umezua taharuki kwa viongozi hao.

Mkurugenzi huyo, Yohana Sintoo na mwenyekiti, Helga Mchomvu na wajumbe wengine waliondolewa katika ukumbi huo huku mkuu huyo wa wilaya akiingia na watu wengine kwa ajili ya kutumia ukumbi huo.

Hata hivyo, akizungumza na Mwananchi leo jioni Jumanne Januari 15, 2019, Sabaya amesema aliwaondoa akiwataka kutumia ukumbi mwingine.

Amesema kikao hicho kilikuwa na wajumbe 10, aliwataka kuhamia ukumbi mdogo ili yeye ahudumie zaidi ya wamachinga 200 walioomba ukumbi huo mkubwa mapema.

Akisimulia tukio hilo leo, Mchomvu amesema kitendo hicho hakipaswi kufanywa na kiongozi huyo wa Serikali.

“Tulikuwa na kikao cha kamati ya fedha katika ukumbi wa Halmashauri. Tumeanza tangu saa 4 asubuhi hadi saa 6 mchana. Aliingia mkuu wa wilaya na kututaka kutoka nje ya ukumbi na kuamuru waliokuwa naye nje ya ukumbi huo, kuingia ndani,” amesema.
Na Janeth Joseph, Mwananchi
Share:

YANGA WAIBUTUA MWADUI 3-1

Nahodha wa timu ya Yanga, Ibrahim Ajibu anaanza na rekodi yake leo katika mchezo wake wa kwanza akiwa amevaa kitambaa cha unahodha baada ya kufunga bao la kwanza katika mchezo wao wa ligi dhidi ya Mwadui Uwanja wa Taifa.

Ajibu amefanikiwa kuandika bao hilo baada ya kupiga faulo akiwa nje ya 18 dakika ya 12 ikamshinda mlinda mlango na kuzama moja kwa moja langoni.

Dakika ya 18 Yanga walipata penati baada ya Tambwe kuchezewa rafu eneo la hatari ila Penalti hiyo ilipigwa na Ajibu iliokolewa na mlinda mlango wa Mwadui Anold Masawe.

Dakika 39 Ajibu alimpa pasi ya bao Amiss Tambwe akamalizia kwa kichwa na kipindi cha pili dakika ya 57 Fei Toto anafunga bao la tatu akimalizia pasi ya Ajibu.

Dakika ya 82 Mwadu wanapata bao la kufutia machozi kupitia kwa Salum Aiyee akimalizia pasi ya Ditram Nchimbi.
Share:

RAIS MAGUFULI ASITISHA ZOEZI LA KUONDOA VIJIJI NDANI YA MAENEO YA HIFADHI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kusitishwa mara moja kwa zoezi la kuviondoa vijiji na vitongoji vinavyodaiwa kuwepo katika maeneo ya hifadhi na amewataka viongozi wa wizara zote zinazohusika kukutana ili kubainisha na kuanza mchakato wa kurasimisha maeneo ya vijiji na vitongoji hivyo. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Januari, 2019 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangallah, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.…

Source

Share:

MAGAIDI WASHAMBULIA HOTELI YA KIFAHARI KENYA



Milipuko na milio ya risasi yasikika katika eneo la 14 Riverside, Nairobi
Milipuko miwili mikubwa ya risasi ilisikika na baadaye ufyatuaji wa risasi.
Share:

UKOSEFU WA DAMU HOSPITAL YA NYERERE DDH BADO NI KITENDAWILI.

Na,Mwandishi Wetu. Hospitali Teule ya Nyerere wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara inakabiliwa na uhaba wa damu kutokana na kasi ndogo ya uchangiaji na ongezeko la matumizi kwa wajawazito na watoto wachanga. Mratibu wa kitengo cha Damu Salama Mwita Kisaka alisema kwa mwezi wanatumia ziadi ya Unit 100 za damu,matumizi ambayo hayawiani na kasi ya kuchangia hali ambayo inawalazimu wanaohitaji kuleta ndugu zao. Akitoa ufafanuzi mbele ya kikundi cha Ujamaa na Ujilani Mwema Serengeti (Kichaumwese)kinachoundwa na vyama vyote vya siasa waliochangia unit 10 za damu ,alisema vikundi mbalimbali ikiwemo Vikoba…

Source

Share:

MO DEWJI AINGIA HASARA

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Mohamed Dewji, maarufu kama Mo, ambaye Oktoba mwaka jana alitekwa na watu wasiojulikana na kukaa naye kwa takribani siku tisa, amepata janga lingine, baada ya serikali kuchukua mashamba yake sita.  MFANYABIASHARA maarufu nchini, Mohamed Dewji, maarufu kama Mo picha mtandao Serikali imetangaza imeyafuta mashamba sita yenye ukubwa wa hekari 12,915.126 ya kampuni ya Mohamed Enterprises, ambayo Mo ndiye mtendaji mkuu wake, yaliyopo Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga. Uamuzi wa kufuta mashamba hayo unafuatia mapendekezo yaliyotolewa na Halmashuri ya Wilaya ya Korogwe kutokana na kutoendelezwa kwa muda…

Source

Share:

TOURE KUREJEA TENA UINGEREZA.

Na Shabani Rapwi, Dar es Salaam. Kiungo wa zamani wa klabu ya Manchester City, Yaya Toure, (35) amesema kuwa bado ana muda wa kuendelea kucheza soka angalau kwa miaka miwili au zaidi ndipo afikilie kustaafu kucheza soka. Toure ambaye kwa sasa hana timu baada ya klabu ya Olympiocos kusitisha mkataba wake kwa kushindwa kufanya vizuri kwenye klabu hiyo aliyodumu kwa muda wa miezi mitatu na alicheza mechi 5 alizopewa nafasi na kocha Pedro Martin. Akiongea kwenye kipindi cha Monday Nighat Football, Toure alisema “Huu sio mwisho wangu nataka kucheza tena,…

Source

Share:

WAZIRI AAGIZA KINA MBOWE WAACHIWE

Wito umetolewa kwa Mamlaka zenye dhamana nchini kuwaachia huru Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini pamoja na Mbunge wa Tarime Mjini Mh. Esther Matiko Wito huo umetolewa mapema leo na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii nchini, Mh. Lazaro Nyalandu. Nyalandu amesema kuwa jambo la kuwaachia huru viongozi hao ambao wapo mahabusu ya Segerea jijini Dar es salaam kwa kufutiwa dhamana na Mahakama ya Kisutu, lina tija sana kwa nchi na Watanzania kwa ujumla. Novemba 23, mwaka 2018, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliwafutia dhamana Mbowe pamoja na…

Source

Share:

WANANCHI WANGING’OMBE WAANZA UJENZI KITUO CHA AFYA, WAITAKA SERIKALI KUUNGA MKONO.

Na,Mwandishi Wetu. Wananchi wa kata ya Makoga wilayani Wanging’ombe mkoani Njombe wameanza ujenzi wa baadhi ya majengo ya kituo cha afya cha makoga lengo likiwa ni kutatua baadhi ya changamoto zinazokikumba kituo hicho kilichopo katika kata hiyo ili kunusuru upatikanaji wa huduma za afya kituoni hapo. Hatua hiyo inakuja kufuatia kituo cha afya makoga kukumbwa na changamoto nyingi ikiwemo upungufu wa wahudumu pamoja na ukosefu wa gari ya wagonjwa katika kituo cha afya kilichopo huku jengo lililopo likiwa limechoka. “Yaani huwa tunatafuta tu Magari kwa gharama ambazo sisi niwakulima hatuna…

Source

Share:

ZAIDI YA MILLIONI 902 KUNUNUA MAGARI,PIKIPIKI KUONGEZA NGUVU KWA WASIMAMIZI WA AFYA NCHINI.

  Serikali imetoa Takribani million 902 na LAKI TISA kwa ajili ya kununua magari 10 na pikipiki 35 ili kuongeza nguvu kwa waratibu na wasimamizi wa huduma ya afya kuweza kuwafikia watoa huduma katika mikoa yao kudhibiti magonjwa ya kifua kikuu na ukoma. Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu alieleza hayo jijini Dar es salaam ambapo alisema serikali imejikita katika kuzuia na kudhibiti ugonjwa wa kifua kikuu na ukoma ili kuweza kuwagundua wagonjwa na kuwapatia huduma ya matibabu. Waziri Ummy alisema lengo la serikali…

Source

Share:

BOT YAHAMISHA MADENI NA MALI ZA BANK M KWENDA AZANIA BANK….NI BAADA YA KUSHINDWA KUJIENDESHA.

Na.Mwandishi Wetu Benki kuu ya Tanzania (BOT) imehamisha madeni na mali zote za Bank M kwenda Azania Bank kutokana na Benki hiyo kushindwa kujiendesha. Uamuzi wa kuunganishwa kwa benki hizo ulifikiwa Januari 2, 2019 hii ikiwa ni baada ya kuiweka Benki M chini ya uangalizi tangu Agosti 2,2018. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Januari 15, 2019 Naibu Gavana wa BOT, Dk Benard Kibese amesema licha ya kufanyika kwa mikutano mingi kati ya wamiliki, bodi na uongozi ndani ya siku 90 zilizotolewa awali lakini hazikuzaa matunda. “Benki inapoonekana kutetereka…

Source

Share:

KORTINI KWA KUBAKA NA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI MWINGINE ACHOMA MOTO NYUMBA

Na,Naomi Milton Serengeti Thomas Mokiri(25) mkazi wa kijiji cha Issenye wilayani hapa amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili ikiwemo kumpa mimba mwanafunzi wa kidato cha tatu mwenye umri wa miaka(17). Akisoma mashtaka mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya Ismael Ngaile mwendesha mashtaka wa Jamhuri Faru Mayengela alisema katika shauri la Jinai namba 6/2019 mshitakiwa anakabiliwa na makosa mawili kosa la kwanza ni Kubaka kinyume na kifungu 130(1)(2)(e)na kifungu 131(1) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Kosa la pili ni kumpa mimba mwanafunzi kinyume na…

Source

Share:

GCLA KANDA YA KASKAZINI YAJIPANGA KUANZISHA MAABARA YA VINASABA VYA WANYAMA.

NA WAMJW, ARUSHA Mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali,kanda ya kaskazini – Arusha, ipo mbioni kuanzisha Maabara maalum ya vinasaba vya wanyama ambayo itasaidia kutambua asili ya mnyama ikiwemo wanyama waliopo ama waliokufa. Akizungumza wakati wa ziara maalum ya maafisa uhusiano waliotembelea Kanda hiyo leo, meneja kanda ya kaskazini Christopher Anyango abainisha kuwa kwa sasa wapo katika ukarabati wa jengo ambalo Maabara hiyo itakuwepo. Awali ujenzi wa jengo hilo ulisimama baada ya ufadhili wake kukoma na hivyo kuilazimu mamlaka kufanya ukarabati ili kujipatia sehemu ya kufanyia kazi. “Maabara…

Source

Share:

RAIS MAGUFULI ASITISHA MARA MOJA ZOEZI LA KUONDOA VIJIJI NA VITONGOZI MAENEO YA HIFADHI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kusitishwa mara moja kwa zoezi la kuviondoa vijiji na vitongoji vinavyodaiwa kuwepo katika maeneo ya hifadhi na amewataka viongozi wa wizara zote zinazohusika kukutana ili kubainisha na kuanza mchakato wa kurasimisha maeneo ya vijiji na vitongoji hivyo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Januari, 2019 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangallah, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Dorothy Mwanyika. 

Pamoja na agizo hilo Mhe. Rais Magufuli ametaka viongozi wa wizara husika kubainisha maeneo ya hifadhi za wanyamapori na misitu ambayo hayana wanyamapori ama misitu ili yagawiwe kwa wafugaji na wakulima ambao kwa sasa wanataabika kupata maeneo ya kufugia wanyama na kuzalisha mazao.

Mhe. Rais Magufuli pia ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia upya zoezi la uwekaji wa mipaka ya hifadhi na makazi, na kutumia busara katika uwekaji wa mawe ya mipaka hiyo ili kutowaondoa wananchi katika maeneo ambayo hayana ulazima wa kuwaondoa.

“Mimi sifurahii kuona wafugaji kila mahali wanafukuzwa, kama kuna eneo ambalo tunafikiri lilikuwa hifadhi ya wanyama lakini halitumiki, tutabadilisha sheria, tunalimega na tunaligawa kwa wafugaji, vivyo hivyo hata kwa wakulima kama kuna eneo tunaona ni hifadhi lakini halina msitu wala wanyamapori, na lina rutuba, na wakulima wanataka kulima nalo tunalimega tunawapa wakulima.

Baadaye tutajua kabisa eneo hili ni la hifadhi, hili ni la mifugo, hili ni la wakulima, hili ni la makazi. Kwa hiyo nyinyi Mawaziri na Makatibu Wakuu mkakae mkatangulize maslahi ya hawa tunaowaongoza ambao ni wakulima, wafugaji, wavuvi nakadhalika, lakini pia tunahitaji wanyamapori, sijasema sasa hifadhi zote za wanyama tunazimaliza, hapana, hifadhi za wanyama lazima tuzihifadhi” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ameagiza vijiji vyote 366 vilivyoainishwa kuwepo ndani ya maeneo ya hifadhi hapa nchini visiondolewe katika maeneo hayo na badala yake ametoa mwezi mmoja kwa viongozi wa wizara zote zinazohusika kubainisha maeneo ya vijiji hivyo na kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya sheria ili yawasilishwe katika kikao kijacho cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amefafanua kuwa ni lazima Serikali ifanye maamuzi haya sasa kwa kuwa idadi ya Watanzania imeongezeka hadi kufikia Milioni 55, idadi ya mifugo imeongeza hadi kufikia Milioni 35 na hivyo kuna ongezeko kubwa la mahitaji ya maeneo ya ardhi ikilinganishwa na wakati nchi inapata uhuru ambapo Watanzania walikuwa Milioni 9 na mifugo ilikuwa Milioni 10.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameagiza sheria ya vyanzo vya maji pia iangaliwe upya ili kutowazuia Watanzania wanaozalisha mazao kandokando mwa mito na ameelezea kutofurahishwa kwake na vitendo vya kufyeka mazao ya wakulima kwa madai kuwa wamelima ndani ya mita 60.

Halikadhalika Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuwasilisha kwake mapendekezo ya kufutwa kwa mashamba ambayo hayajaendelezwa na ameagiza wizara hiyo iendelee kumpelekea mapendekezo ya mashamba yote yaliyotelekezwa ili ayafute na wananchi wagawiwe kwa ajili ya kuyatumia kwa uzalishaji wa mazao na mifugo.

Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli amesema maagizo hayo hayana maana kuwa sasa wananchi waruhusiwe kuvamia maeneo ya hifadhi, na ametaka zoezi la uwekaji wa mipaka lifanyike haraka na kwa uwazi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
15 Januari, 2019
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger