Tuesday, 29 November 2016
Monday, 28 November 2016
SERIKALI Yapiga Marufuku Kusoma Degree Bila Kupita Form Six

Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Pro.Joyce Ndalichako amepiga marufuku wanafunzi kujiunga na masomo ya Shahada (degree) bila kupita kidato cha sita. Marufuku hiyo itaanza rasmi katikals mwaka ujao wa masomo. Prof.Ndalichako emesema mfumo wa elimu huria umechangia kuzalisha wasomi butu kwa kupokea wanafunzi dhaifu kitaaluma.
Ndalichako amesema wanafunzi wanaofeli kidato cha nne na kwenda kusoma certificate na baadae diploma ili wajiunge vyuo vikuu hawataruhusiwa kujiunga na masomo ya shahada (degree) kama hawajarudia (reseat) masomo yao na kupata alama za kwenda kidato cha tano, na wafanye mitihani ya kidato cha sita na kufaulu ndipo wajiunge vyuo vikuu.
Katika utaratibu huo, wanafunzi wa kidato cha nne watakaoruhusiwa kusoma shahada (degree) bila kupita kidato cha 5 na 6 ni wale waliofaulu kidato cha 4 na wakachaguliwa kwenda kusoma katika vyuo vya ufundi daraja la kati (Technicians). Lakini wale wanaokosa "credit" za kuendelea form five na kuamua kwenda certificate mwisho wao utakuwa diploma.
Kuhusu "foundation courses" kwa wanafunzi wa kidato cha sita walioshindwa kupata sifa za kusoma degree, Ndalichako amesema Foundation course haimuongezei mtu sifa.
"Kama mtu amemaliza kidato cha 6 akashindwa kufikisha "points" za kujiunga chuo kikuu, asidahiliwe kwa kusoma foundatiom course. Anapaswa kurudia mtihani wa kidato cha 6 kwa sababu baraza la mitihani linatoa fursa ya kurudia mara nyingi iwezekanavyo. Foundation course haimuongezei mtu sifa kama hana sifa zinazotakiwa kitaaluma" Amesisitiza Ndalichako.
RAIS Magufuli Ampongeza Paul Makonda
Magufuli ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na Mkuu huyo wa Mkoa huo kwa njia ya simu wakati Makonda akiendelea na mkutano wa hadhara katika eneo la Mbezi Maramba Mawili jijini humo.
Amesema, juhudi anazozifanya Makonda ni za kuigwa na viongozi wengine katika mikoa yao kwani anasaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.
“Wananchi wana kero nyingi sana, lakini viongozi wao wangekuwa wanawasikiliza hata maswali wanayouliza hapo yasingeulizwa, nakupongeza sana Mkuu wa Mkoa natamani na viongozi wengine wangeiga mfano wako,”amesema Magufuli.
Rais alipigiwa simu na Makonda ili asaidie kutoa ufafanuzi kuhusu upana wa barabara zilizopo chini ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads) baada ya wananchi kulalamikia kuvunjiwa maeneo yao ili kupisha ujenzi.
Katika ufafanuzi wake, Rais Magufuli alisema suala la barabara kutoka Ubungo hadi Ruvu tayari wameshalitolea ufafanuzi mara nyingi.
Amesema akiwa Waziri wa Ujenzi wakati serikali inataka kupanua barabara ya kutoka Ubungo kwenda Kibaha kulitokea malalamiko ya aina hiyo na kesi kuhusu suala hilo namba 137 ilifikishwa mahakamani ambapo serikali ilishinda na baadaye yalitolewa maelekezo kuhusu maeneo yaliyopo katika hifadhi ya barabara.
Amesema baada ya ushindi huo kutoka Mahakama Kuu walichukua hatua ya kubomoa nyumba zote zilizokuwa katika hifadhi ya barabara kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1932 ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 1949 ikafanyiwa tena marekebisho mwaka 1954 na mwaka 1965.
Amesema Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 na Sheria ya Vijiji namba tano ya mwaka 1999 na Sheria ya Mipango Miji na Matumizi ya Ardhi ya mwaka 2007 zote zinatambua hifadhi ya barabara na kwa barabara ya Dar es Salaam kwenda Kibaha iliachwa kwa upana uliopo kama filta ya Jiji la Dar es Salaam.
“Mwito wangu kwa wananchi wazingatie sheria na sheria ni msumeno, tulitunga sheria sisi wenyewe hivyo ni wajibu wetu sisi serikali kusimamia sheria, lakini kama wanaona sheria haifai ni kiasi cha kwenda kulishauri Bunge libadilishe sheria ili barabara ya Ubungo iwe sentimita tano zipite bajaji tu, lakini ukweli unabaki palepale kwamba sheria ipo na haijawahi kubadilishwa,”amesema Rais Magufuli.
Aidha Magufuli aliipongeza Tanroads kwa kusimamia sheria kwani alisema itafika kipindi kutakuwa hakuna barabara nchini.
Rais Magufuli amesema pia kazi ya kuvunja nyumba zilizopo katika hifadhi ya barabara ipo pale pale kwa vile serikali imepata kiasi cha Sh bilioni 67 za kujenga barabara zinazobadilishana (interchange) katika eneo la Ubungo ambayo itakuwa ya ghorofa mbili au tatu ili kurahisisha usafiri.
“Ghorofa zote na majengo yatavunjwa bila fidia hata kama litakuwa jengo la Tanesco kwa sababu lazima tuzingatie sheria, lakini kama wananchi wataona wameonewa basi waende mahakamani,” alisema.
MTOTO WA MIAKA 11 ATUNUKIWA PHD TANZANIA
WAHITIMU, viongozi na wageni waliohudhuria Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu
cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mkoani Morogoro, waliingiwa na simanzi
wakati mtoto, Tamar Aaron Mbogho (11), alipojitokeza na kupokea Shahada
ya Udaktari wa Falsafa (PhD), akimwakilisha mama yake Swai Sophia
Faustin ambaye alifariki dunia miezi sita kabla ya kufika siku ya
mahafali.
Tamar, mtoto pekee wa marehemu, ambaye baba yake mzazi ni Mkuu wa Wilaya
ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, Aaron Mbogho alifika katika hafla hiyo
akiwa ameambatana na ndugu zake kadhaa, tayari kwa ajili ya kupokea
heshima hiyo kwa niaba ya mama yake.
Gazeti hili liliweza kuwasiliana kwa njia ya simu na Mbogho akiwa katika
kituo chake cha kazi Mwanga ambapo alisema Tamar alifika katika hafla
hiyo kupokea shahada hiyo kwa niaba ya mama yake.
Kwa mujibu wa Mbogho, mkewe Dk Sophia alifariki dunia Mei 21, 2016,
wakati huo akiwa ameshahitimu masomo yake kikamilifu na alisema Tamar ni
mtoto wa pekee wa Sophia.
"Alikuwa ni mmoja wa wahitimu waliopaswa kutunukiwa shahada hiyo kwa
sababu tayari alishahitimu na kubakia muda wa mahafali, lakini bahati
mbaya akafariki dunia kabla ya muda kuwadia,” alisema na kuongeza.
"Binti yetu alipenda kwenda kuchukua shahada ya mama yake na
alisindikizwa na ndugu zake wa familia. Ameniambia malengo yake ni
kusoma kwa bidii ili aweze kupata Shahada ya Udaktari wa Falsafa kama
mama yake, " alisema Mbogho.
Katika mahafali hayo yaliyofanyika juzi katika Kampasi ya Solomon
Mahlangu, Mazimbu, wahitimu 61 walifuzu na kutunukiwa Shahada ya
Udaktari wa Falsafa ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
Naibu Makamu Mkuu Taaluma wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Peter Gilla,
alisoma orodha ya watunukiwa ambapo pia alitaja jina la mwanafunzi
asiyekuwapo ambaye alifariki dunia, lakini akiwa amefuzu na anastahili
kupata Shahada ya PhD ya Chuo Kikuu hicho ambaye ni Sophia.
Hivyo, Mwenyekiti wa Mahafali hayo, Dk Benno Mrembuka, alimwongoza mtoto
Tamar kwenda kupokea shahada hiyo kutoka kwa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo
Fedha na Utawala, Profesa Yonika Ngaga, hali iliyoleta simanzi na huzuni
kwa washiriki waliokuwepo katika mahafali hiyo.
Baadaye Tamar alielekezwa kufika mbele ya meza kuu ili kuwapa mkono
wageni mbalimbali ambao walitumia nafasi hiyo kumfariji kutokana na
kumpoteza mama yake mzazi ambaye alikuwa ni mhitimu.
Katika hatua nyingine, Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa
Gerald Monela, alisema SUA imeendelea kutoa wahitimu wa Shahada ya
Sayansi na Ualimu katika masomo ya sayansi kwa ajili ya kukidhi mahitaji
makubwa ya walimu wa kufundisha shule za sekondari nchini.
Sunday, 27 November 2016
SERIKALI KUNUNUA NDEGE ZA KISASA KUIMARISHA ULINZI HIFADHI ZA TAIFA

SERIKALI imepanga kununua ndege za kisasa ili kuimarisha ulinzi katika Hifadhi za Taifa nchini.
Hayo
yamesemwa jana na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja
Jenerali Gaudence Milanzi wakati akihojiwa na kipindi maalumu cha
TUNATEKELEZA kinachorushwa hewani na kituo cha Televisheni ya Taifa
(TBC1).
Meja
Jenerali Milanzi anasema Serikali imeweka mfumo maalumkatika kulinda
hifadhi zilizopo na ili kuweza kukabiliana na ujangili unaojitokeza
katika hifadhi mbalimbali nchini.
“Sekta
ya Utalii nchini inachangia pato la taifa kwa takribani asilimia 17.5
na kutoa ajira kwa zaidi ya watumishi milioni 3 katika sekta mbali mbali
ya utalii nchini, hivyo ni vyema tukaweka mikakati madhubuti katika
kulinda vyanzo vilivyopo” alisema Meja Milanzi.
Aidha,
alisema kuwa Serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria
watu wote watakaobainika kujihusisha na ujangili pamoja na biashara ya
magogo ili kulinda hifadhi za Taifa na kuweza kuvutia watalii nchini.
Aidha
Meja Jenerali Milanzi aliitaka jamii kwa ujumla kuona umuhimu wa
kutumia nishati mbadala ili kulinda misitu iliyopo kwa kutunza mazingira
na hifadhi za taifa.
Mbali
na hayo Meja Jenerali Milanzi alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi
zinazovutia watalii wengi kutoka Marekani na Uingereza hivyo kuwataka
wananchi kuzingatia sheria na kanuni zinazosimamimia Hifadhi za Taifa
ili kuzudi kuvutia watalii nchini.
MADEREVA WA SERIKALI NA TAASISI ZA UMMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

KAMANDA wa
Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed Mpinga ametoa wito kwa
madereva wote ikiwemo madereva wa Serikali na Mashirika ya Umma
kuzingatia sheria za Usalama Barabarani.
Kamanda
Mpinga ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya kitaifa
ya “Abiria paza sauti” inayotarajiwa kuzinduliwa tarehe 28 Novemba,
mwaka huu.
Kamanda
Mpinga alisema kumekuwa tabia ya baadhi ya madereva hususani wa
Serikali na mashirika ya umma ya kutofuata sheria za usalama barabarani
kwa kuendesha magari kwa mwendokasi, na kuwaonya kuwa sheria ni msumeno
na inapaswa kufuatwa na kila mtu.
“Kumekuwa
na madereva hasa wa magari madogo kusafiri kwenda maeneo mbalimbali ya
nchi huku wakiwa hawana uzoefu wa kuendesha umbali mrefu na hivyo
kupelekea uvunjifu wa sheria za barabarani kwa kuendesha kwa mwendokasi
na kusababisha ajali” alifafanua Kamanda Mpinga.
Akifafanua
zaidi Kamanda alisema uzoefu unaonyesha kuwa katika kipindi hiki cha
kuelekea mwisho wa mwaka kumekuwa na ongezeko kubwa la magari
barabarani, na hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria za barabarani
ili kuweza kupunguza ajali za barabarani.
Kwa
upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama
Barabarani, Jackson Kalikumtima alisema lengo la kampeni ya Paza Sauti
ni kuhamasisha ushiriki kamilifu wa wananchi katika kukabiliana na ajali
kwa kuchukua hatua stahiki bila ya uwepo wa askari.
Pia
alisema kuwa kampeni hiyo imelenga kubadili tabia na mtazamo wa
madereva kuhusu usalama barabarani ili waendeshe kwa kuzingatia sheria
bila shuruti na kubadili mtazamo wa wananchi kuhusu usalama barabarani
ili watambue kuwa usalama barabarani ni jukumu la kila mmoja.
Naye Mwanasheria
wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, (ASP), Deus Sokoni alisema
mkakati wa kupunguza ajali barabarani katika kampeni hiyo umelenga
katika kutoa elimu kwa jamii ili kuona suala la usalama barabarani ni
jukumu la kila mmoja na si jukumu la Polisi pekee.
“hakuna
asiyetumia barabara duniani, hatutaki ajali tunataka kuishi salama,
hivyo kila abiria anawajibu wa kutunza na kutii sheria za barabarani “
aliongeza Mwanasheria huyo.
Mwenyekiti wa Chama
cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA), Hassan Mhanjama aliwataka abiria
wote nchini hususani wanaotajaria kusafiri mwishoni mwa mwaka
kuwasiliana na Mamlaka ya Usafirishaji SUMATRA pindi watakapopandishiwa
nauli mbali na taratibu zilizopo
HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBER TAREHE 27.11.2016
TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO





TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..





KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO

1

2

3

4

5

6

7

8

9

10





















