Thursday, 20 October 2016

PROF NDALICHAKO:WANAFUNZI WALIOKOSA MIKOPO KUPEWA

 View image on Twitter
waziri wa elimu sayansi na teknolojia prof ndalichako amewatupia lawama bodi ya mkopo elimu ya juu kuwa wanafanya kazi kwa mazoea amesema pamoja na kutumia jitiada za kusafisha watumishi bodi hiyo amesema wapo watumishi bado wanafanya kazi kwa mazoea;
 ndalichako amesema ameyasikia malalamiko kutoka kwa wananchi na anayafanyia kazi na amesema wanafunzi wapewe mikopo semista hii kwa mwaka wa kwanza na wote bila kufata mean tested.

amesema lengo la serikali ni kuwapa wote wahitaji amesema na kuiagiza bodi ya mikopo kuwapa kama mfumo wa zamani Pia bodi ya mkopo imekosea kuwapa wanafunzi shilingi elfu tano kwa miezi kama pesa za kujikimu amesema bora kutompa.
source.TBC
Share:

Selected bachelor students to join Mozambique-Tanzania Centre for Foreign Relations (CFR)-2016/2017


cfr_logo
Share:

TCU yaongeza muda wa udahili vyuo vikuu

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania TCU imetoa muda wa siku 3 kwaajili ya wanafunzi zaidi ya 4000 ambao wamekosa fursa ya kudahiliwa katika hawamu tatu za udahili zilizofanywa na tume hiyo
Kaimu mkurugenzi wa udahili na nyaraka wa TCU Dkt. Kokuberwa Mollel amesema udahili huo utaanza tarehe 24 hadi tarehe 26 mwezi huu kwaajili ya kozi mbalimbali ambazo bado hazijajazwa kwani tayari udahili umekamilika kwa wanafunzi wanaosomea masomo ya udaktari ambapo Jumla ya wanafunzi zaidi ya 2000 wamechaguliwa kati ya wanafunzi zaidi ya 10,000 waliotuma maombi yao
Dkt. Kokuberwa amesema wanafunzi wengi walioachwa kwenye usajili wameshindwa kutofautisha viwango vya ufaulu wao na vigezo vya vyuo husika hivyo wameaswa kuchagua kozi watakazo zikuta katika tume hiyo na kuacha kung'ang'ania kozi ambazo hawajakidhi vigezo vyake.

Share:

Dk Slaa Aingilia Kati Ugomvi wa Godbless Lema na RC Gambo,Huu Hapa ni Ujumbe Wake

Ugomvi wa maneno kati ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema limemuibua katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa aliyeandika ujumbe mrefu akimkingia kifua mbunge huyo.
Share:

TAARIFA MUHIMU KWA WANAFUNZI WOTE MLIOCHAGULIWA CHUO KIKUU UDOM 2016/2017

 Logo
Important information for accessing the University of Dodoma
From the Dodoma bus station, there are two common options of public transport to reach the University of Dodoma.
First, by Taxi
  • Around the Dodoma regional bus station, there are taxis for transportation services.
Share:

Waziri Mkuu Amsimamisha Kazi Mhandisi Wa Maji Lindi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Lindi (LUWASA), Mhandisi Adam Alexander (pichani mwenye mafaili) kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi pamoja na kushindwa kusimamia ujenzi wa kituo cha kuzalisha maji katika Manispaa ya Lindi.

Waziri Mkuu amemkabidhi Mhandisi huyo kwa Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Bw. Stephen Chami na kumuelekeza afanye uchunguzi zaidi juu ya suala hilo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana Jumatano, Oktoba 19, 2016  wakati alipotembelea mradi wa maji wa Ng'apa ambapo aliagiza nafasi hiyo ikaimiwe na Mkurugenzi Msaidizi wa mamlaka hiyo, Mhandisi Idrisa Sengulo.

"Kamanda wa TAKUKURU fanya mapitio ya kina ya mshahara wake. Yeye anasema analipwa Wizarani, mimi najua analipwa na LUWASA. Angalia kazi aliyokwenda kuifanya Dar es Salaam kama inalingana na siku alizokaa,” alisisitiza Waziri Mkuu.

Mhandisi hiyo anakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za ofisi pamoja na kupokea mshahara bila la kulipa kodi ya mapato ya mshahara (PAYE), kujilipa kiwango kikubwa cha posho pamoja na kusafiri kwa muda mrefu.

Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuvumilia kuona wananchi wanapata shida huku watendaji waliopewa dhamana ya kuwatumikia hawaonekani kwenye vituo vyao vya kazi. "Huyu nimemuita mimi aje huku, hadi jana alikuwa Dar es Salaam."

Alipoulizwa sababu za kutokuwepo ofisini kwake kwa muda mrefu, Mkurugenzi huyo alisema kwamba alikuwa Dar es Salaam akiandika maombi ya fedha kwa ajili ya kutatulia changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.

"Unatumia siku ngapi kuandika proposal, msomi unatumia mwezi mzima kuandika proposal na unakaa Dar es Salaam hata Katibu Mkuu wako hajui na huko unajilipa posho tu! Tena badala ya kulipwa sh.120,000 kwa siku wewe unajilipa sh.150,000. Hatuwezi kuvumilia hali hii,” amesema.

Waziri Mkuu amemaliza ziara yake siku tatu mkoani Lindi na amerejea jijini Dar es Salaam.
                        
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Share:

Kamati ya Bunge Yakataa faini ya 500,000/- Kwa Kila Kosa Barabarani

Kamati  ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala imekataa mapendekezo ya kufanyia marekebisho Sheria ya Leseni za Uchukuzi ya mwaka 1973 yenye lengo la kuongeza kiwango cha adhabu ya faini hadi kufikia asilimia 500 kwa watakaokiuka masharti ya leseni hizo.

Mapendekezo hayo yaliwasilishwa mbele ya kamati hiyo mjini Dodoma jana na Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra).

Baada ya kuyakataa mapendekezo hayo, kamati hiyo imetoa muda wa siku mbili kwa Sumatra kuhakikisha inawasilisha mbele ya kamati hiyo mapendekezo yanayokubalika.

Sumatra inapendekeza kuongeza kiwango cha adhabu ya faini kutoka kati ya Sh 10,000 na Sh 50,000 hadi Sh 200,000 na 500,000 kwa watoa huduma za uchukuzi, watakaokiuka masharti ya leseni zao.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Mchengerwa alisema mapendekezo hayo, yatazidi kuwaongezea mzigo Watanzania badala ya kuwasaidia. 
Alisema kiwango hicho cha faini kubwa, kamwe hakitazuia tatizo la ajali za barabarani, zaidi ya kuongeza ukubwa wa tatizo la rushwa.

“Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuwasaidia wananchi, lakini mapendekezo haya yatazidi kuwaongezea mzigo kwa sababu kiwango cha faini hizi kama kitapitishwa, watoa huduma za uchukuzi watahamishia hasara yao kwa wananchi,” alisisitiza.

Aliitaka mamlaka hiyo, kwenda kuyafanyia kazi tena mapendekezo hayo kwa kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuwasilisha viwango vya faini vinavyokubalika. 
Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo, Joseph Mhagama ambaye pia ni mbunge wa Madaba, alisema mapendekezo hayo hayana nyongeza yoyote, itakayoisaidia serikali katika kudhibiti tatizo la ajali barabarani.

“Kwa sasa serikali imeweka nguvu zake katika kupunguza ajali za barabarani, lakini kiwango cha faini hizi hakina uhusiano wowote na jitihada hizi zaidi ya kuiongezea Sumatra mapato na kuwapa mzigo walipa kodi,” alisema.

Akiwasilisha mapendekezo ya mamlaka hiyo mbele ya Kamati hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema mapendekezo ya marekebisho ya sheria hiyo, yamelenga  kuiboresha zaidi sheria hiyo ya leseni za uchukuzi.

Alisema marekebisho hayo, pia yatasaidia mamlaka hizo kuendana na mahitaji ya sasa hasa katika eneo la adhabu ya faini, hali itakayopunguza kiwango kikubwa cha kukiukwa kwa masharti ya leseni hizo za uchukuzi.
Share:

Wanavyuo 66,000 wakosa mikopo

 Image result for heslb.go,.tz
Dar es Salaam. Ahadi iliyotolewa na Rais John Magufuli wakati wa kampeni mwaka jana kwamba katika Serikali yake hakuna mwanafunzi atakayekosa mkopo wa masomo ya elimu ya juu imekuwa ngumu kutekelezeka.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kwamba kati ya wanafunzi 88,000 walioomba mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), wengi hawatapata.
Uwezo wa bodi hiyo ni kutoa mikopo kwa wanafunzi 21,500 pekee sawa na asilimia 24 na waliopatiwa hadi sasa ni wanafunzi 11,000 sawa na asilimia 12.
Takwimu hizi zinaonyesha kwamba zaidi ya robo tatu ya wanafunzi wanaohitaji mikopo watakosa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.
Share:

Magazeti Yote ya Tanzania Leo Oktoba 20, 2016 Yako Hapa

Share:

Wednesday, 19 October 2016

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU SEKOMU 3RD ROUND 2016/2017

Share:

MPYA:WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA ST.FRANCIS IRAKARA WAANIKA "MADUDU" YA CHUO HICHO HADHARANI,

 Image
Habari zenu,leo wanafunzi wa chuo kikuu cha st.francis ifakara wameuandikia uongozi wa maswayetu blog barua,ili tuifikishe mahala husika,naamini kila siku waziri wa elimu lazima usome blog hii,natumaini utaliona hili na kulitolea maamuzi siku si nyingi.
Share:

Scorpion afunguliwa mashtaka upya


Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imemfungulia mashtaka mapya Salum Njwete (Scorpion).Amefunguliwa mashtaka mengine yanayofanana na ya awali ya unyang’anyanyi wa kutumia silaha.

Hata hivyo Njwete amekana shtaka na kurudishwa rumande,huku Hakimu Flora Haule anayesimamia kesi hiyo akizuia dhamana.

Awali Mahakama hiyo ilimfutia mashtaka yanayomkabili Scorpion baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo na kutokana na maombi hayo, Hakimu Adelf Sachore alikubaliana na ombi hilo kwa kuzingatia kifungu namba 91 kifungu kidogo cha kwanza cha sheria ambacho kinampa Mamlaka Mkurugenzi Wa Mashtaka nchini (DPP) kuondoa shtaka mahakamani muda wowote ili mradi kama kesi hiyo haijatolewa hukumu.

Njwete anakabiliwa na shtaka la unyang'anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Saidi Mrisho.
Share:

BAVICHA WATOA TAMKO KUHUSU WANAFUNZI WENGI WA ELIMU YA JUU KUKOSA MIKOPO 2016/2017

Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa kuwa utawala huu wa Serikali ya CCM, chini ya Rais John Magufuli zaidi ya nusu ya wanafunzi waliodahiliwa kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu mwaka wa masomo 2016/2017, wako katika hatari ya kukosa fursa ya kupata elimu hiyo kwa sababu ambazo hazieleweki hadi sasa.

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari na vyanzo vingine, Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) imeweza kudahili takriban wanafunzi wapya 58,000 kwa ajili ya elimu ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini kwa mwaka huu wa masomo.

Lakini katika hali ambayo tunajua itaumiza vijana wengi na kuwasikitisha Watanzania, taarifa ambazo zimethibitishwa na Serikali ya Rais Magufuli kupitia kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo, ni kwamba zaidi ya nusu ya idadi hiyo ya waliodahiliwa na TCU kusoma elimu ya juu, hawatapata mikopo!

Hivyo ndoto za kutafuta mafanikio yao, kwa ajili ya jamii zao na taifa letu kwa ujumla zinaelekea kukatiliwa. Hili ni jambo kubwa na zito kwa sababu linagusa moja ya misingi muhimu ya taifa lolote lenye ndoto ya kutaka kuendelea, achilia mbali kuwa taifa lenye uchumi wa kati unaotegemea viwanda.

Kwa mujibu wa Gazeti la The Guardian la Oktoba 18, mwaka huu, Serikali ya CCM, chini ya Rais Magufuli imesema itawakopesha wanafunzi wapatao 24,000, idadi ambayo haifiki hata nusu ya wanafunzi wote waliodahiliwa na TCU.

Hata hivyo kauli hiyo ya Mkurugenzi wa Bodi, tumeichukulia kuwa si ya kweli hata kidogo, bali ya mtu anayejaribu kuficha mambo kwa ajili ya “nusu shari kuliko shari kamili”.

Tunasema hivyo kwa sababu hadi sasa Bodi hiyo hiyo, imeshatoa mikopo kwa wanafunzi 3,966 tu. Idadi hiyo ni sawa na asilimia 6 tu kati ya wanafunzi wote waliopata udahili wa kusoma elimu ya juu kwa mwaka huu.

Maana yake ni kwamba kuwakopesha vijana wapatao 24,000 ili wasome elimu ya juu bado nayo ni ahadi tu ya maneno, lakini uhalisia uliopo kwa vitendo hadi sasa ni kwamba Serikali ina uwezo wa kuwakopesha vijana wake 3,966 pekee nchi nzima.

Idadi hiyo ambayo serikali imeweza kuwakopesha mikopo, haifiki hata nusu ya jumla ya wanafunzi wanaopaswa kudahiliwa na mojawapo ya vyuo vikuu vikubwa nchini, mathalani Chuo Kikuu Dar es Salaam.

WAMEKOPESHWA CHAKULA NA KULALA, SI KUSOMA!
Aidha, kwa muda mrefu sasa, walau tangu kuanza kwa utaratibu wa serikali kuwakopesha wanafunzi kwa ajili ya elimu ya juu, inaeleweka kuwa HESLB imekuwa ikitoa mikopo kwa ajili ya vitu vitatu; ada, malazi na chakula.

Katika hali ambayo inazidi kushangaza na kuibua maswali kuwa kuna jambo kubwa ambalo linafichwa, BAVICHA tunazo taarifa kuwa hata hao wanafunzi asilimia 6 ambao bodi inadai imeshawapatia mkopo, katika vyuo vingi wamepata fedha kwa ajili ya CHAKULA NA KULALA tu.

Hawajalipiwa fedha ya ada (tuition fees hadi sasa).
Kwa mantiki hiyo ni kwamba, Serikali ya CCM, chini ya Rais Magufuli hadi sasa wiki ya tatu tangu vyuo vifunguliwe si tu kwamba imeshindwa kuwakopesha wanafunzi wote wanaostahili kupata mkopo kwa ajili ya elimu ya juu, bali hata imeshindwa hata kulipa fedha za ada kwa wanafunzi ambao tayari imeshawakopesha. Hali hii ikiendelea tutegemee kuona vyuo vikuu na taasisi zingine za elimu ya juu vikifungwa kwa sababu vitakuwa haviwezi kujiendesha.

Taarifa hizi za Bodi ya Mikopo zinapaswa kulishtua taifa letu na kila Mtanzania aone jinsi ambavyo Serikali ya CCM chini ya Rais John Magufuli haijajipanga na wala haijui inachokifanya katika kuhakikisha inatoa elimu bora kwa Vijana wetu.

Lakini pia zinathibitisha kuwa Serikali ya Rais Magufuli iko katika hali mbaya ya kifedha na hivyo inahitaji msaada wa fikra mpya nje ya CCM kuikwamua vinginevyo tujiandae kwa mwendelezo wa janga kubwa zaidi katika sekta ya elimu.

Tunamtaka Rais John Magufuli kujitokeza hadharani, na kuueleza umma wa Watanzania hatma ya Vijana waliokosa mikopo, na kama ahadi zake alizozitoa wakati wa Kampeni zilikuwa ni ulaghai au ghiliba za kutafuta kura?
 
Pia Rais Magufuli anapaswa kuwaeleza watanzania ikiwa ameshindwa utekelezaji wa ahadi zake ikiwemo Elimu bora, au akubali kuwa yeye ni Muongo kwa sababu wakati wa kampeni alisema nanukuu; “ETI NIWE RAIS HALAFU NISIKIE WANACHUO WAMEKOSA AU WAMECHELWESHEWA MIKOPO YAO, WATANIJUA MIMI NI NANI, KITU CHENYEWE KINAITWA MIKOPO HALAFU UNACHELEWESHA” Mwisho wa kunukuu.

Tunawataka Viongozi wa serikali za wanafunzi katika Vyuo Vikuu vyote nchini, kuungana pamoja ili kudai haki ya wanafunzi wenzao, tukitambua kuwa, baadhi ya Viongozi wa shirikisho la serikali za wanafunzi wa elimu ya Juu (TAHILISO) wamekuwa wakitumika kwa ajili ya CCM badala ya maslahi mahsusi ya wanafunzi na hivyo kuidhoofisha taasisi hii muhimu ya wasomi, hivyo umoja wao ni muhimu katika kuipata haki hii.

Tunatoa wito kwa taasisi mbalimbali za kutetea haki za vijana, asasi za vijana pamoja na mtandao wa wanafunzi Tanzania, kujitokeza hadharani na kuwapigania vijana hawa katika kuhakikisha wanapata haki yao ya msingi ya elimu.

Imetolewa leo Jumatano,19.10.2016
Patrobas Katambi
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU MOUNT MERU-TAWI LA MWANZA 2016/2017 1ST,2ND AND 3RD BATCHES

 Header_text
KUAONA MAJINA  -ARUSHA CAMPUS


KUONA MAJINA 1ST AND 2ND-MWANZA


KUONA MAJINA BATCH 3-MWANZA

Share:

Majina ya Waliopitishwa Kupata mikopo ya Elimu ya Juu chuo kikuu cha MUM 2016/2017 AWAMU YA PILI

Image
Share:

Download new Audio:Kingdom ft. Tshaka - NGA'RE NGA'RE

Hii hapa nyimbo mpyaa kutoka kwa kingdom akishirikiana na Tshaka ...Nyimbo inakwenda kwa jina la NGA'RE NGA'RE, .Unangoja nini Sikiliza na idownload hapo chini faster....


BOFYA HAPA KUDOWNLOAD
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO CHA UHASIBU TIA DAR (THIRD BATCH) 2016/2017

 Image result for TIA.AC.TZ

Selected Candidates for Bachelor Degree Programmes for 2016/2017 Academic Year-DSM Campus Third Batch

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger