Wednesday, 18 November 2015
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO AWAMU YA NNE 2015/2016-BATCH 4
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Itakumbukwa kuwa wiki iliyopita, Bodi ilitoa orodha ya Awamu ya Tatu iliyokuwa na waombaji 6,915 waliopangiwa mikopo. Kati ya waombaji hao waliopangiwa mikopo, waombaji 4,642 ni walikua ni wale wanaojiunga na shahada ya kwanza katika vyuo mbalimbali nchini na waombaji 2,273 ni wanafunzi wanaojiunga na Stashahada (Diploma) ya Ualimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Kwa msingi huo, Bodi inapenda kuufahamisha umma kuwa hadi sasa imekwishawapangia mikopo jumla ya waombaji mikopo wenye sifa 48,469 wa mwaka wa kwanza. Katika awamu ya kwanza, Bodi ilitoa orodha yenye jumla ya waombaji 12,282; Awamu ya Pili wanafunzi 28,554; Awamu ya Tatu wanafunzi 6,915 na Awamu hii ya Nne wanafunzi 718 wamepangiwa mikopo.
Majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo kutoka katika awamu zote tatu yanapatikana kupitia mtandao wa Bodi wa olas.heslb.go.tz na tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Aidha, orodha hizo pia zimetumwa vyuoni kwa ajili ya taratibu za usajili.
Mwisho.
AWAMU YA NNE YA WANAFUNZI WALIOPANGIWA MIKOPO
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kuwafahamisha waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 kuwa imetoa orodha ya AWAMU YA NNE yenye jumla ya waombaji wa mwaka wa kwanza 718 waliopangiwa mikopo.Itakumbukwa kuwa wiki iliyopita, Bodi ilitoa orodha ya Awamu ya Tatu iliyokuwa na waombaji 6,915 waliopangiwa mikopo. Kati ya waombaji hao waliopangiwa mikopo, waombaji 4,642 ni walikua ni wale wanaojiunga na shahada ya kwanza katika vyuo mbalimbali nchini na waombaji 2,273 ni wanafunzi wanaojiunga na Stashahada (Diploma) ya Ualimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Kwa msingi huo, Bodi inapenda kuufahamisha umma kuwa hadi sasa imekwishawapangia mikopo jumla ya waombaji mikopo wenye sifa 48,469 wa mwaka wa kwanza. Katika awamu ya kwanza, Bodi ilitoa orodha yenye jumla ya waombaji 12,282; Awamu ya Pili wanafunzi 28,554; Awamu ya Tatu wanafunzi 6,915 na Awamu hii ya Nne wanafunzi 718 wamepangiwa mikopo.
Majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo kutoka katika awamu zote tatu yanapatikana kupitia mtandao wa Bodi wa olas.heslb.go.tz na tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Aidha, orodha hizo pia zimetumwa vyuoni kwa ajili ya taratibu za usajili.
Mwisho.
Tuesday, 17 November 2015
NDUGAI ASHINDA USPIKA KWA KURA 264 SAWA NA 70% YA KURA ZOTE
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mbunge
wa Kongwa (CCM) Job Ndugai ashinda kiti vcha Uspika kwa kura 264 sawa
na kura asilimia 70 huku mpinzani wake kupitia Chadema Goodluck Ole
Medeye akipata kura 109 huku wagombea wengine wakipata kura 0.
NDUGAI anakuwa Spika wa Bunge la 11 la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Monday, 16 November 2015
TAARIFA KWA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAHADA ZA UALIMU ELIMUMSINGI NA ELIMU YA SEKONDARI KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) KATIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
TAARIFA KWA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAHADA ZA UALIMU ELIMUMSINGI NA ELIMU YA SEKONDARI KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) KATIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwataarifu wote waliochaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) baada ya Mfumo wa CAS kuonyesha kuwa umechaguliwa kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma, utaratibu ni kusubiri UDOM na vyombo vyake vya ndani kuthibitisha majina hayo. Waliodahiliwa wanatakiwa kwenda chuoni baada ya kupata joining instructions na wito kutoka Chuo husika.
TAARIFA KWA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAHADA ZA UALIMU ELIMUMSINGI NA ELIMU YA SEKONDARI KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) KATIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwataarifu wote waliochaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) baada ya Mfumo wa CAS kuonyesha kuwa umechaguliwa kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma, utaratibu ni kusubiri UDOM na vyombo vyake vya ndani kuthibitisha majina hayo. Waliodahiliwa wanatakiwa kwenda chuoni baada ya kupata joining instructions na wito kutoka Chuo husika.
Kumekuwapo na wanafunzi waliosafiri kwenda kuripoti chuoni kabla ya
taratibu hizi kukamilika na hivyo kusababisha usumbufu kwao wenyewe na
kwa taasisi za NACTE na UDOM. Majina ya wanaotakiwa kwenda kuripoti na
tarehe za kuripoti mara zote hutolewa na chuo husika. Kwa kuwa majina
yamekwenda vyuoni kwa makundi (batches) sio makundi yote yamepitishwa na
katika mchakato wa ndani ya vyuo.
Baraza (NACTE) hutoa uchaguzi wake ili kuondoa usumbufu kwa wanafunzi kuangalia tovuti za vyuo mbalimbali kusaka majina yao. Iwapo kwa sababu zozote UDOM itashindwa kuwapokea baadhi ya waliochaguliwa, Baraza litawapa nafasi katika vyuo vingine. Ikumbukwe kuwa kuna vyuo vingi ambavyo havijapata wanafunzi wa kutosha.
Imetolewa na:
Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
15 Novemba 2015
Baraza (NACTE) hutoa uchaguzi wake ili kuondoa usumbufu kwa wanafunzi kuangalia tovuti za vyuo mbalimbali kusaka majina yao. Iwapo kwa sababu zozote UDOM itashindwa kuwapokea baadhi ya waliochaguliwa, Baraza litawapa nafasi katika vyuo vingine. Ikumbukwe kuwa kuna vyuo vingi ambavyo havijapata wanafunzi wa kutosha.
Imetolewa na:
Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
15 Novemba 2015


















































