Monday, 30 June 2014

HAWA NDIO WASHINDI WA TUZO ZA BET 2014,BEYONCE ACHUKUA 3

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Pharrell Williams na Missy Elliot wakifungua shoo ya utoaji tuzo za BET usiku wa kuamkia leo jijini Los Angeles.
Share:

AVEVA ACHAGULIWA KUWA RAIS MPYA SIMBA SC

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Amin Bakhresa akitangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Simba SC.
Share:

Sunday, 29 June 2014

TANGAZO LA ORODHA YA MAJINA YA KUITWA KAZINI 27 JUNI 2014,KWA WAOMBAJI WALIOFANYA USAILI TAR.05 HADI 06 JUNE

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY1
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Kumb. Na. EA.7/96/01/G/30 27 Juni, 2014 KUITWA KAZINI 

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kuanzia tarehe 05 hadi 06 Juni, 2014  kuwa walioorodheshwa katika tangazo hili wamefaulu usaili na wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri kama ilivyoonyeshwa katika tangazo hili.   Aidha, wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vipya vya kazi katika muda ambao umeainishwa katika barua zao za kupangiwa vituo vya kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) vya masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na mwajiri kabla ya kupewa barua ya ajira.  Kwa Waombaji Kazi walioitwa katika Wizara ya Maliasili na Utalii wote kwa pamoja wanatakiwa kuripoti Chuo Cha Taifa cha Utalii Tandika, Wilayani Temeke tarehe 14/07/2014 Saa 2:00 Asubuhi Bila kukosa.
Barua za kuwapangia vituo vya kazi kwa walioitwa katika Taasisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania zimetumwa kupitia anuani zao. Aidha, wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba mara nafasi za kazi zitakapotangazwa tena. 
ANGALIA MAJINA HAYO...HAPA CHINI
Share:

MAJINA MAPYA YA VIONGOZI CUF TAIFA BAADA YA UCHAGUZI MKUU

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
1.MWENYEKITI PROFESA IBRAHIM LIPUMBA
2.KATIBU MKUUU......MAALIM SEIF

3. Naibu Katibu Mkuu (Bara), Mhe. Magdalena Sakaya.

4. Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Mhe. Nassor Ahmed Mazrui.
Share:

MWENYEKITI WA CCM KATA YA BUSAMBALA BUTIAMA afariki dunia-baada YA MAJAMBAZI KUMUUA


Watu  wanadhaniwa  kuwa ni majambazi wamemuua kinyama kwa kupiga  risasi moja ya kichwani mwenyekiti  wa chama cha mapinduzi  kata ya Busambala wilayani Butiama mkoani Mara Bw Willison Opio mwenye umri wa miaka 6o huku kichwa chake kikisambaratishwa  kabisa na risasi hiyo.
Share:

HOTUBA YA MH.MIZENGO PINDA-WAZIRI MKUU WAKATIA AKIFUNGA SHUGHULI ZA BUNGE JANA DODOMA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
PG4A9702
UTANGULIZI

a)    Masuala ya Jumla

Mheshimiwa Spika,
1.    Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa Rehema kwa kutupatia uzima na afya hadi kufikia siku ya leo. Tumekuwepo hapa kwa takriban miezi miwili ambapo tumeweza kupokea na kujadili Taarifa za Mapitio ya Utekelezaji wa Kazi za Serikali kwa mwaka 2013/2014 na Mwelekeo kwa mwaka 2014/2015 kwa Wizara mbalimbali na hatimaye kupitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2014/2015.

2.    Napenda kutumia nafasi hii ya awali kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa kazi nzuri ya kutukuka ambayo wameifanya kwa nidhamu na ufanisi mkubwa, hususan wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Serikali na Mafungu ya Wizara za Kisekta. Kipekee niwashukuru Wajumbe wa Kamati ya Bajeti chini ya Uongozi mahiri wa Mheshimiwa Mtemi Andrew John Chenge, Mbunge wa Jimbo la Bariadi Magharibi kwa kazi yao nzuri ya kuchambua Bajeti ya Serikali na Sheria zinazoambatana na masuala ya Bajeti. Changamoto zilikuwa nyingi,   lakini   kwa   pamoja   tumekubaliana   na   kuafikiana. Kazi kubwa iliyoko mbele yetu ni kwenda kushirikiana na Wananchi katika utekelezaji wa Bajeti hii ili kuwaletea maendeleo.

Mheshimiwa Spika,
3.    Katika kipindi hiki tukiwa hapa Bungeni, yapo matukio ya kusikitisha yaliyotokea ambapo baadhi ya Waheshimiwa Wabunge walipoteza Wapendwa wao. Aidha, yapo matukio ya Kitaifa yaliyosababisha kupoteza maisha ya Ndugu, Jamaa na Marafiki. Napenda kutumia nafasi hii kuwapa pole Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote waliofikwa na misiba na majanga mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wote waliopotelewa na Ndugu, Jamaa na Marafiki.

Mheshimiwa Spika,
4.    Kipekee niwape pole ndugu, jamaa na marafiki waliopotelewa na ndugu zao na wote waliopata majeraha wakati kulipotokea Mlipuko wa Bomu pale Darajani, Zanzibar. Tukio hili la kusikitisha halipendezi kwa Nchi yetu. Niwaombe Wananchi wote kwa umoja wetu tushirikiane kuwa Walinzi katika maeneo yetu na kuwezesha kuwatambua mapema wale wote wenye nia mbaya ya kuharibu amani na utulivu katika Taifa letu.

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
2_0603b.jpg
Share:

TANGAZO KWA FORM IV WOTE MLIOKOSA NAFASI ZA KWENDA KIDATO CHA TANO 2014 ,SASA UTASOMESHWA BURE KABISA SOMA HAPA

INNOCENT-THE BLOGGER
Share:

Saturday, 28 June 2014

NAFASI MPYA ZA KAZI-KUJITOLEA KWA MUDA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

MATOKEO BRAZIL NA CHILE:BRAZIL YATINGA ROBO FAINALI KWA MATUTA,HONGERA CHILE

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


WENYEJI Brazil wameitoa Chile kwa penalti 3-2 katika mchezo wa hatua ya 16 Bora Kombe la Dunia mjini Uwanja wa Belo Horizonte, kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120.
Share:

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI - JUNI 29

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

MWANAMKE ASALIMISHA SHANGA ZA MAJINI KANISANI SOMA HAPA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mwanamke anayefahamika kwa jina la Asnath Terevaeli akikabidhi shanga kwa Mchungaji Kiongozi, (Frank Endrew) wa Kanisa la Ufufuo na Uzima mkoani Arusha.Katika hali ya kushangaza, mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Asnath Terevaeli hivi karibuni aliamua kukabidhi kanisani shanga za majini kwa kile alichodai kuwa, zimekuwa zikimtesa na kumfanya akose amani.
Share:

AJALI YA NOAH SINGIDA-WATATU WAFARIKI,KUMI WAJERUHIWA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Watu watatu wamekufa na wengine kumi wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Noha kupasuka tairi ya nyuma na kubingirita mara tatu katika kijiji cha Januka manispaa ya Singida.
Share:

BAI LA NBS LAPATA AJALI-KIMARA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Muonekano wa mbele wa basi la NBS T719 AZC baada ya kugonga basi la Princes Muro T892 BUR lililokuwa likitokea Dar
kwenda Mwanza eneo la Kimara.
Share:

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI-MASWAYETU BLOG

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
01_293fb.jpg
Share:

ADA VYUO VYA UALIMU JUU,YAPANDA ZAIDI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

\Serikali imepandisha maradufu ada kwa wanafunzi wanaosomea ualimu kwenye vyuo vya ualimu nchini kuanzia muhula ujao wa masomo.
Share:

BARCELONA YAMWINDA SUAREZ


Licha ya kukabiliwa na marufuku ya FIFA ya miezi minne kwa kumng'ata mlinzi wa Italia Giorgio Chiellini Barcelona ya Uhispania haijakata tamaa ya kumsajili mshambulizi machachari wa wa Uruguay Luiz Suarez.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger