Na Dotto Kwilasa, Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Mawaziri wa Wizara mbalimbali kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 18 Novemba, 2025.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi waandamizi wa Serikali, wawakilishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa dini pamoja na wageni mbalimbali, ikiashiria mwanzo mpya wa safari ya kuimarisha utendaji wa Serikali ya Awamu ya Sita.
Katika hotuba yake mara baada ya uapisho, Rais Samia amewataka viongozi hao wapya kufanya kazi kwa kasi, ubunifu na uadilifu ili kuhakikisha Serikali inaendelea kutekeleza mipango ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wote.
Amewakumbusha kuzingatia uwajibikaji, ushirikiano na kusimamia vizuri rasilimali za umma.
Uapisho huu unaendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuleta matokeo chanya, kuimarisha utawala bora na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.



0 comments:
Post a Comment