Monday, 10 November 2025

MWANZA ILIVYOATHIRIKA NA DHAHAMA YA OKTOBA 29, HUDUMA MUHIMU ZA KIJAMII ZAKOSEKANA

...


Ghasia, vurugu na uharibifu mkubwa uliofanywa na magenge ya Vijana hapo Oktoba 29, 2025, umewaacha wananchi wa Mkoa wa Mwanza kukosa huduma muhimu za kijamii, huku pia mamia ya wananchi wakikosa ajira na kipato kutokana na matukio ya moto na wizi ulioangamiza maeneo yao ya kazi katika Eneo la Buhongwa Mkoani humo.

Kwa nyakati tofauti, magenge ya Vijana katika siku ya uchaguzi Mkuu wa Jumatano Oktoba 29, 2025, wakati wengine wakipiga kura kuwachagua Viongozi wao watakaowaongoza kwa miaka mitano ijayo, wao walivamia, kuiba na kuchoma moto Chuo cha Ufundi stadi VETA cha Buhongwa Mkoani Mwanza pamoja na kuiba na kuteketeza kwa moto Vituo vya uuzaji mafuta vya Olypic Petrol na Lake Oil Energies pamoja na kituo cha uuzaji wa bidhaa mbalimbali cha Empire store Kilichopo Igoma sambamba na magari yaliyokuwa yamepaki kwenye maeneo hayo.




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger