Thursday 16 March 2023

BUNGE LA AFRIKA LATUMA SALAMU ZA POLE VIFO VYA WATU 250 KUFUATIA KIMBUNGA FREDDY NCHINI MALAWI NA MSUMBIJI

...
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira na Wabunge wa Bunge la Afrika wakiwa wamesimama kuwakumbuka watu 250 waliofariki kufuatia Kimbunga Freddy kilichotokea nchini Malawi na Msumbiji.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog Afrika Kusini

Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) limetuma salamu za pole na rambirambi kufuatia vifo vya watu 250 katika za Malawi na Msumbiji kutokana na Kimbunga Freddy.

Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira amesema Bunge la Afrika limehuzunishwa na tukio la Kimbunga Freddy hivyo linatoa pole kwa nchi za Malawi na Msumbiji

Aidha, Chifu Charumbira amesema Bunge la Afrika lipo pamoja na Wamalawi na Msumbiji wote katika kipindi hiki kigumu. 

Rais huyo wa Bunge la Afrika pia ameshauri hatua madhubuti na maksudi zinapashwa kuchukuliwa ikiwa ni sehemu ya kupambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Akitoa taarifa kuhusu taarifa kuhusu madhara ya Kimbunga Freddy kilichoikumba ya Malawi na Msumbiji wakati wa Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini, Mbunge kutoka Malawi Mhe. Steven Mikaya amesema idadi ya watu waliofariki kutokana na Kimbunga Freddy nchini Malawi na Msumbiji hadi sasa ni watu 250 na manusura ni wengi na huduma za kijamii zimekosekana barabara zimeharibiwa, hakuna huduma ya maji , umeme umekatika, uharibifu mkubwa umefanyika hivyo panahitajika misaada ya kibinadamu.

Watu wengi na nyumba zao wamesombwa na matope katika mji mkuu Blantyre nchini Malawi ulioharibiwa zaidi baada ya kimbunga Freddy kupiga kusini mwa Afrika kwa mara ya pili, na kusababisha mafuriko ambayo yamewaua watu zaidi ya 250.


Vikosi vya uokozi vinaonya juu ya uwezekano wa kuwepo waathirika zaidi wa kimbunga hicho wakati vikiendelea kuwatafuta manusura kwenye maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko na maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na kimbunga Freddy.


Msemaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Malawi Felix Washoni amesema waliwapata watu kwenye miti, kwenye mapaa ya nyumba au katika maeneo ya miinuko.


Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) ukiongozwa na Rais wa Bunge la Afrika Mhe. Chief Fortune Charumbira unaendelea leo Machi 16, 2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini ambapo wabunge wanajadili mambo mbalimbali kuhusu Bara la Afrika.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira akizungumzia tukio la Kimbunga Freddy kilichotokea nchini Malawi na Msumbiji na kusababisha vifo vya watu 250
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira akizungumzia tukio la Kimbunga Freddy kilichotokea nchini Malawi na Msumbiji na kusababisha vifo vya watu 250
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira na Wabunge wa Bunge la Afrika wakiwa wamesimama kuwakumbuka watu 250 waliofariki kufuatia Kimbunga Freddy kilichotokea nchini Malawi na Msumbiji.
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira na Wabunge wa Bunge la Afrika wakiwa wamesimama kuwakumbuka watu 250 waliofariki kufuatia Kimbunga Freddy kilichotokea nchini Malawi na Msumbiji.
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) Mhe Chifu Fortune Charumbira na Wabunge wa Bunge la Afrika wakiwa wamesimama kuwakumbuka watu 250 waliofariki kufuatia Kimbunga Freddy kilichotokea nchini Malawi na Msumbiji.
Mbunge kutoka Malawi Mhe. Steven Mikaya akitoa taarifa kuhusu Kimbunga Freddy kilichosababisha vifo vya watu 250 nchini Malawi na Msumbiji
Mbunge kutoka Malawi Mhe. Steven Mikaya akitoa taarifa kuhusu Kimbunga Freddy kilichosababisha vifo vya watu 250 nchini Malawi na Msumbiji

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI



Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) ,Mhe. Chief Fortune Charumbira akizungumza kwenye Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) ,Mhe. Chief Fortune Charumbira akizungumza kwenye Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) ,Mhe. Chief Fortune Charumbira akizungumza kwenye Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 
Rais wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP) ,Mhe. Chief Fortune Charumbira akizungumza kwenye Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 
 Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika ukiendelea leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 
Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya AfCFTA , Wamkele Mene, akihutubia Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP)
Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya AfCFTA , Wamkele Mene, akihutubia Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP)
Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika ukiendelea leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 
Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika ukiendelea leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini 



Mkutano wa Kamati za Kudumu za Bunge la Afrika ukiendelea leo Machi 16,2023 katika ukumbi wa Bunge la Afrika Midrand Afrika Kusini.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog Afrika Kusini


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger