Wednesday 7 December 2022

SAMIA, KINANA, MWINYI WACHAGULIWA KWA KISHINDO CCM, MAWAZIRI WATIKISA UJUMBE NEC

...
Msimamizi wa uchaguzi wa CCM, Dk Ali Mohamed Shein ambaye ni Rais mstaafu wa Zanzibar amemtangaza, Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kwa mara nyingine baada ya kupigiwa kura za ndio 1914 kati 1915, Abdulrahman Kinana kuwa Makamu mwenyekiti wa CCM Bara baada ya kutetea nafasi hiyo baada ya kupigiwa kura za ndio 1913 kati ya 1915 huku Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar,baada ya kupigiwa kura za ndio 1912.

Wakati huo huo idadi kubwa ya nafasi za wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) zimechukuliwa na mawaziri ambapowalioshinda ni pamoja na Angelah Kairuki ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Dk Ashatu Kijaji (Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwezekezaji), Angelina Mabula (Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi).


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger