Tuesday 27 December 2022

BINTI AZIKATA NA KUZIONDOA KABISA NYETI ZA BABA YAKE

...
Mwanamke anayefahamika kwa jina Grace Kihumba(30) mkazi wa Wang'ing'ombe mkoani Njombe anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumshambulia baba yake mdogo akiwa usingizini na kisha kuzikata sehemu za siri na kuziondoa.



Baada ya kukamatwa na kufanyiwa mahojiano na maofisa wa jeshi la polisi mwanamke huyo amesema amefanya hivyo kutokana na kukasirishwa na kitendo cha wanafamilia kuendelea kusherekea wakati yeye anaendelea kuumwa licha ya kutoa hela za matibabu kwa mzee huyo ambaye anadaiwa kuwa ni mtaalamu wa tiba asilia,kama ambavyo Kamanda wa jeshi la polisi mkowa Njombe Hamis Issa alivyobainisha wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.


Katika tukio jingine Kamanda Issa amesema jeshi hilo linamshikilia kijana anayefahamika kwa jina la Baraka Alfonce mkazi wa kitongoji cha Kimbila Ludewa mjini kwa tuhuma za kuhusika kumkata kiganja cha mkono bosi wake baada ya kutomlipa fedha kiasi cha elfu 65.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger