Tuesday 24 November 2020

WADAU WATAKA SERIKALI KUJIPANGA MPANGO WA TATU WA MAENDELEO

...

Mkuu wa kitengo cha Uwezeshaji na Utawala Bora wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Danford Sango akitoa neno la ukaribisho kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dk Tausi Kida (kulia) wakati wa mkutano wa mashauriano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendani wa UN Global Compact Network Tanzania , Bi Marsha Macatta Yambi akizungumza na wadau waalikwa wakati wa mkutano wa mashauriano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Mtafiti Mshiriki wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dr. Hoseana Lunogelo akiendesha mashauriano wakati wa mkutano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Mtafiti Mshiriki Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Prof Samuel Wangwe akizungumza wakati wa mkutano wa mashauriano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Biashara ya Utalii Wazawa (TLTO), Bw. Samwel Diah akielezea changamoto za utalii nchini ambazo zisizopatiwa ufumbuzi sekta hiyo haiwezi kusaidia kuinua maendeleo ya Tanzania wakati wa mkutano wa mashauriano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Meneja MKuu wa Hoteli ya Whitesand, Bi. Nadine Atallah akifafanua jambo katika mkutano wa mashauriano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Kilimo Taifa (ACT), Jitu V. Soni akizungumza katika kikao cha mashauriano cha mpango wa tatu wa maendeleo(FYDP III) nchini kilichofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wadau walioshiriki wa mkutano wa mashauriano kuhusu mpango wa maendeleo wa tatu (FYDP III) wenye lengo la kushirikisha zaidi sekta binafsi katika kuufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa kishindani uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.


Na MwandishiWetu
Serikali imeshauriwa kuhakikisha kwamba inakuwa na wataalamu wakisekta kama itataka kufanikisha lengo la kuwa nchi yaviwanda ifikapo mwaka 2025.

Kauli hiyo imetolewa na washiriki katika mkutano wa mashauriano wa sekta binafsi kuhusiana na matayarisho ya Mpango wa maendeleo wa miaka mitano unaotarajiwa kuanza kutekelezwa mwaka ujao.

Washiriki hao wamesema kwamba mambo yanayotendeka Wizara ya fedha na mipango pamoja na kauli nzuri zilizopo hazi ashirii kutoa ushirikiano kwa sekta binafsi iliiweze kushiriki kikamilifu katika uwezeshaji waukuaji wa uchumi.

Mmoja wa washiriki wa mkutano huou lioratibiwa na Taasisi yaUtafiti wa Uchumi naKijamii (ESRF) Samwel Diah alisema serikali imekuwa ikikazania kukusanya ushuruna kodi bila kuangalia uendelezaji wa sekta husika yautalii, kilimo au viwanda.

"Hili ni tatizo lakukosekana kwa wabobezi wanaojua sekta na kushughulikia changamoto kwa lengo la kusongesha mbele gurudumu la maendeleo"alisema Diah na kuongeza kwamba vijana wengi wahitimu wa shahadambalimbali wana vyeti vizuri lakini hawajui changamoto zinazokumba sekta hivyo kusaidia kutatua kutokana na kutokuwa na uzoefu katika sekta husika.

Alipendekeza kuwa katika rasimu hii inayoandaliwa yaMpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo wa awamu ya tatu kuwa na nafasi inayowatambua waliobobea katika fani ili waweze kutoa ushauri unaofaa katika uendeshaji wa dira mbalimbali za maendeleo.

Naye Jitu Soni ambaye ni Makamu Mwenyekikti wa Baraza la Kilimo la Taifa (ACT) alisema kwamba kuna haja ya kufanya kazi kwa pamoja kwa kuangalia misingi ya sekta na kuiunganisha ili iweze kutoa matokeo chanya.

Alisema ilikuwepo na maendeleo ya kilimo lazima kuwepo na viwanda vya kuwezesha kusindika bidhaa za kilimo ili ziweze kuwa katika hatua nyingine na hiii tasaidia sana katika kuimarisha kilimo chenyewe.

Alisema inasikitisha kuona kwambawakati taifa linategemea kilimo hakuna ufungamanishajiwa kilimo na viwanda na hivyo bidhaa nyingiz za kilimo kutokuwa na ushindani katika soko la dunia.

Pia alitaka kuwepo na uzalishaji wa wataalamu (skills) kwa lengo la kuhakikisha kwamba sekta zinanufaika na uwapo wao badala ya hali ya sasa kwamba wataalamu wanaozalishswa wanashindwa kukidhi mambo ya kitaalamu katika sekta zote ikiwamo ya kilimo.

Naye NadineAtallah alisema kwamba sekta ya utalii imekuwa ikizungumza kila mara kuhusu changamoto zake na imekuwa ikialikwa kila mahali kuelezea namna bora ya kupambana na changamoto hizo lakini mpaka leo hawajaona hatua zinazochukuliwa.

Alitaka kuwepo na mabadiliko ya kweli na kusikiliza ushauri wanaotoa kwa lengo la kuendeleza sekta hiyo na wala sio kukwamisha.

Baadhi ya wajumbe walisema kwamba japo inatakiwa kufikiri kuongeza watalii wa ndani kupambana na majanga na changamoto za sasa za sekta hiyo gharama zinazoambatana na uwekezaji zinafanya mtu wa kawaida Tanzania asiweze kutumia miundo mbinu iliyopo ya kitalii.

"Tusimung'unye maneno utalii wa kuzalishwa na wananchi hauwezekani kwa gharama zilizopo labda uandaliwe mkakati mwingine' alisema mmoja wa washiriki.

Akielezea DirayaTaifa (vision 2925) iliyotengenezwa miaka ya 1990, mmoja wawaasisi wa dira hiyo yenye mipango ya miaka mitano kwa awamu tatu, Profesa Samwel Wangwe alisema kusudia la mwanzo la mpango huo ni kuiweka Tanzania katika uchumi wakati wenye kipato cha dola 3000 kwa mwaka ifikapo mwaka 2025, huku viwanda vikichangia.

Aidha alisema ukuaji wa uchumi ulipangwa kuwa wa asilimia nane kila mwaka.

Aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchambuana kuweka fikira nzito zaidi za kusonga mbele hasa ikizingatiwa kwamba dira hiyo iko katika hatua za mwisho za utekelezaji wake.

Naye Profesa Nyange alisema kwamba nguvu zaidi zinatakiwa kuinua zaidi pato la taifa na pia kupunguza umaskini wa kupitiliza.

 Aidha alisema kwamba zifikiriwe njia za kuendeleza mabadiliko ya kweli katika kilimo na kuimarisha viwanda nchini.
"Naona kuna watu wanaanza kulima mashamba makubwa na uzalishaji wa kilimo kuongezeka haya nia mabadiliko mazuri lakini tunatakiwa kufanya zaidi.

Awali akifungua mkutano huo wa mashauriano kuangalia namna bora za utekelezaji wa ngwe ya tatu na ya mwisho katika mpango wa taifa wa Vision 2025, Mkuu wa kitengo cha Uwezeshaji na Utawala Bora wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Danford Sango aliwataka wajumbe kuhakikisha kwamba wanatoa mawazo yao kwa uhuru zaidi.

Alisema Taasisi hiyo iliyoanzishwa mwaka 1994 ina majukumu makubwa ya kitafiti na pia kusaidia kukutanisha sekta binafsi na umma kutengeneza mustakabali wa maendeleo ya taifa.

Anasema lengo lakuwa na mkutano huo ni kushauri namna bora ya kuwezesha mpango wa tatu wa taifa kuwa na uwezo mkubwa wa kutumia sekta binafsi kuwezesha mapinduzi ya viwanda na kilimo nchini.

Aliwataka washiriki kutoa ushauri wao namna ya kufanya uchumi wa Tanzania kuwa shindani katika soko la dunia.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger