Friday 1 March 2019

RAIS MAGUFULI ATOA NDEGE KUSAFIRISHA WANAOTAKA KWENDA KUMZIKA RUGE

...

Rais John Magufuli ametoa ndege ya Serikali kwa ajili ya kuusafirisha mwili wa marehemu Ruge Mutahaba utakaopelekwa Bukoba kwa ajili ya kuzika.



Msemaji wa Familia ya Mutahaba, Raymond Kashasha amesema hayo leo Ijumaa, Machi 1,2019 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Ruge anatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Kiziru wilayani Bukoba mkoani Kagera na atasafirishwa kutokea Dar es Salaam siku ya Jumapili, Machi 3,2019.

Pia ametoa ndege ya Air Tanzania kwa ajili ya watu wanaotaka kwenda kumzika Ruge ambayo itaondoka Dar es Salaam siku ya Jumatatu, Februari 4 asubuhi kwa gharama ya Sh 600,000 kwenda na kurudi.

Na  Hellen Hartley, Mwananchi
ANGALIA VIDEO HAPA
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger