Friday 1 March 2019

FREEMAN MBOWE NA ESTHER MATIKO WASHINDA RUFAA YA DHAMANA YAO DHIDI DPP

...
Mahakama ya Rufaa imetupilia mbali pingamizi la Serikali kupinga Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko kusikilizwa shauri lao la kuomba kupewa dhamana katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam.

Hivyo kesi ya Mh. Mbowe na Matiko inarudi Mahakama kuu kwa ajili ya kusikilizwa kama ilikuwa halali kwa Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu kufuta dhamana zao au hapana.

Novemba 23, 2018 Jaji Wilbard Mashauri akiwa Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, alifuta dhamana ya Mbowe na Matiko kutokana na kukiuka masharti ya dhamana.

Wawili hao walikata rufaa katika Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga uamuzi wa Kisutu kufuta dhamana yao ambapo rufani yao ilipangwa kwa Jaji Sam Rumanyika.

Hata hivyo, baada ya Mahakama Kuu chini ya Jaji Sam Rumanyika kusikiliza mapingamizi ya pande zote iliamua kuanza usikilizaji wa rufaa hiyo.

Upande wa serikali ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi ulidai kuwa wamekata rufaa katika Mahakama ya Rufani kupinga maamuzi yaliyotolewa na Mahakama Kuu.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger