Tuesday 10 March 2015

ALICHOKISEMA ZITTO KUHUSU MCHAKATO WA YEYE KUVULIWA UANACHAMA NA KESI DHIDI YAKE,SOMA HAPA

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 

Mahakama  Kuu ya Tanzania, leo imetupilia mbali shauri lililofunguliwa na Zitto Zubeir Kabwe mwaka jana, akipinga kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kumjadili, akikitaka chombo hicho cha sheria, kukielekeza chama chake, kusubiri kwanza rufaa yake aliyokuwa amekata katika Baraza Kuu.
 
Mahakama iliyoketi chini ya Jaji Mziray, ilikubaliana na hoja za mawakili wa Chadema, waliosema kuwa ufunguaji wa kesi hiyo ulikiuka baadhi ya vifungu vya sheria na hivyo kumtaka mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kulipa gharama zote za kesi hiyo.

Baada  ya  hukumu  hiyo, Zitto  Kabwe amesema  hakuwa  na wito wa mahakamani leo na  Jaji  aliyekuwa  akiisikiliza  kesi  hiyo amehamishiwa Tabora, hivyo  mwanasheria  wake  ameenda  kufuatilia  mazingira  ya  hukumu  hio.
 
"Hatuna taarifa ya Jaji Mpya. Mwanasheria wetu anafuatilia na atatoa statement", ameandika  Zitto  Kabwe  katika  ukurasa  wake  wa  twitter.

Wakati Zitto akifungua kesi hiyo Januari mwaka jana, tayari Chadema ilikuwa imewafukuza uanachama Dr. Kitilya Mkumbo na Samson Mwigamba ambao pamoja na Zitto, walituhumiwa kupanga njama za kufanya mapinduzi ya uongozi ndani ya chama hicho.
  
Zitto alikuwa akitetewa na wakili Albert Msando wakati Chadema iliwakilishwa na Tundu Lissu, Peter Kibatala na John Mallya. 
 

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger