Sunday 7 December 2014

BREAKING NEEEWZ:WAFUATAO WAMEITWA KWENYE USAILI WA MAGEREZA UTAKAOFANYIKA TAREHE 10-17/12/ 2014

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
                                                            
 Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG yafuatayo ni majina ya wanafunzi  mwaka waliochaguliwa kufanya usaili jeshi la magereza  mwaka 2014
Tunaendelea kutoa huduma yetu endapo utahitaji kuangaliziwa jina lako tafdhali fanya yafuatayo kwa gharama ya tshs.800 tu ambayo utaituma kwenda namba 0768260834-mpesa au 0653791475-tigo pesa
1.TUMA JINA LAKO KWENDA NAMBA 0768260834 MFANO:JUMA   PAUL(USAILI MAGEREZA)
2.TUTAKUJIBU NDANI YA DK.2 TU
3.HUTAJIBIWA HADI UTUME PESA.

KUANGALIA MAJINA HAYO BONYEZA HAPO CHINI;


04 Desemba, 2014
KUITWA KWENYE USAILI

Jeshi la Magereza linawatangazia wafuatao kufika kwenye usaili kwa nafasi walizoomba. Usaili huo utafanyika kuanzia tarehe 10/12/2014 mpaka tarehe 17/12/2014 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza Ukonga Jijini Dar es salaam kuanzia 2:00 asubuhi kwa mujibu wa tarehe za makundi kama yalivyoainishwa. Kwa wale wa kidato cha Nne na Sita waliosailiwa kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wasubiri maelekezo mengineyo. Aidha wale ambao hawakuona majina yao hapa wahesabu kuwa hawakufanikiwa.

Waombaji wanatakiwa kuzingatia  yafuatavyo;-
i.    Kuja na Vyeti halisi (Original Certificates) vya elimu na ujuzi
ii.    Kuja naCheti halisi cha kuzaliwa,
iii.    Hati za matokeo ya mitihani (Result Slip/Statements) hazitakubaliwa isipokuwa kwa wahitimu ambao vyeti vyao halisi havijatolewa na vyuo husika wakiwa na barua Maalum ya kuthibitisha kwamba vyeti halisi havijatolewa,
iv.    Wahusika watajitegemea kwa nauli za kuja na kurudi, chakula na malazi kwa kipindi chote cha usaili
Tangazo hili pia linapatikana kwenye Mbao za Matangazo zilizopo Bwalo Kuu la Magereza, tovuti ya magereza kwa anwani ya www.magereza.go.tz, gazeti la Uhuru la tarehe 05 Desemba 2014 sanjari na blog ya magereza kwa anwani ya www.magereza.blogspot.com

Imetolewa na Kamishna Jenerali wa Magereza

J.C.Minja
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA
Bofya HAPA kupata orodha ya wanaotakiwa kufika kwenye usaili
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger