Monday, 16 October 2023
Sunday, 15 October 2023
WANAFUNZI JK NYERERE WAISHUKURU BARRICK KWA KUWA MDAU MKUBWA WA KULETA MAPINDUZI KATIKA SEKTA YA ELIMU NCHINI
Pia wahamasisha jamii kuacha vitendo vya uvamizi wa Mgodi wa Barrick North Mara
***
WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari Julius Kambarage Nyerere, iliyopo kijiji cha Nyamwaga wilayani Tarime, wameushukuru Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara kwa kuwajengea shule hiyo ambayo inachukua wanafunzi kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita wanaosoma masomo ya michepuo mbalimbali.
Aidha, wameishukuru Kampuni ya Barrick inayoendesha mgodi huo kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals, kwa jinsi ambavyo imeendelea kuwa mdau mkubwa wa maendeleo ya shule hiyo sambamba na kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha sekta ya elimu nchini.Katika kudumisha ubia na Serikali karibuni Barrick imetoa dola milioni 40 kwenye mpango wa ujenzi wa barabara na dola milioni 30 zaidi katika uboreshaji wa suhula za elimu ya juu nchini.
Walitoa shukrani hizo kupitia risala yao wakati Mahafali ya Saba ya Kidato cha Nne ya shule hiyo iliyofanyika shuleni hapo na kuhudhuriwa na viongozi mbambali wa kijamii, na Serikali akiwemo Diwani wa Kata ya Nyamwaga, Mwita Marwa Magige.
“Tunatoa shukrani za dhati kwa Mgodi wa Barrick North Mara kwani wamekuwa wadau wakubwa wa shule yetu, pia jitihada zinazofanywa na kampuni kuunga mkono Serikali kuboresha sekta ya elimu kupitia kuimarisha miundombinu ya shule na vifaa vya kufundishia kwa lengo la kuwezesha wanafunzi wengi zaidi kupata elimu bora,” walisema katika sehemu ya risala yao wakati wa hafla hiyo.
Walifafanua katika risala hiyo kuwa mgodi wa Barrick North Mara uligharimia ujenzi wa shule hiyo mwaka 2014, ambapo mwaka 2017 ilitoa wahitimu wa kwanza wa kidato cha nne.
Wanafunzi hao waliongeza kuwa baadaye shule hiyo ambayo imepewa jina la Baba wa Taifa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ilisajiliwa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita, ambapo mpaka sasa imepokea wa kidato cha tano wa awamu ya nne.
“Tunashukuru Mungu kwamba wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita katika shule yetu mwaka huu walifaulu na kuchaguliwa kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali na pia inaendelea kuwa na ufaulu mzuri wa wanafunzi wanaohitimu kidato cha nne kila mwaka.
“Tangu shule hii ianzishwe ufaulu wa kidato cha nne umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka. Elimu hii ya kidato cha nne inawajengewa wanafunzi msingi mzuri wa kujiunga na elimu ya juu. Pia imetujengea uwezo mzuri wa kujitambua na kufikiri,” risala hiyo iliongeza.
Wanafunzi katika risala yao pia walisema shule hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa ya huduma ya maji na kuomba Serikali na wadau wengine wa maendeleo kuitupia macho kwa hatua za utatuzi, ili kulinda usalama wa afya za wanafunzi, walimu na wafanyakazi wa shule hiyo.
Jumla ya wanafunzi 111 (wavulana 58 na wasichana 53) wanatarajiwa kufanya Mtihani wa Taifa wa kuhitimu kidato cha nne Novemba mwaka huu.
Wakati huo huo, wanafunzi hao kupitia igizo lao maalumu waliwataka vijana kujiepusha na vitendo vya uhalifu, ukiwemo uvamizi katika mgodi wa Barrick North Mara kwani vinaweza kukatisha ndoto zao kielimu,kuhatarisha maisha yao sambamba na kufifisha jitihada za uwekezaji nchini.
MAYAI SIO ANASA; VIONGOZI DODOMA WAHAMASIKA, WACHANGIA MAYAI, SIKU YA YAI DUNIANI
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi Rosemary Senyamule, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mh. Jaffar Shekimweri na Katibu Wa Ccm Mkoa wa Dodoma Mh. Pili Augustine Mbanga ni miongoni mwa viongozi walioguswa na na kampeni ya SAB Investment, ya Changia Yai.
Katika kuadhimisha siku ya Yai Duniani, kampuni hiyo ya SAB Investment iliandaa kampeni ya Changia Yai kuhamasisha jamii kukumbuka umuhinu wa kula Mayai na kusaidia Kugawa Mayai kwa Watoto waishio kwenye vituo vyenye uhitaji.
Kampuni hiyo ambayo iliweka Kambi katika Maonesho ya Dodoma Ya Sasa Si Dodoma ya Zamani Yalifanyika katika Viwanja vya Mashujaa vya Zamani na ambayo yalikutana na siku hiyo ya Yai Duniani na kuwezesha wadau mbalimbali kujuika kuchangia Mayai kama sehemu ya kujitoa kwa jamii katika Kusherehekea Siku ya Yai Duniani. ambapo viongozi hao wa serikali nao waliguswa na kushiriki.
Mkurugenzi wa SAB investment Saida Bwanakheri walio endesha zoezi hilo wakati akiabidhi makasha yenye mayai kwenye vituo hivyo vya watoto yatima vilivyopo jijini Dodoma alisema siku hii imewasaidia Kukumbusha jamii kuwa mayai kwa watoto na watu wazima, ni Muhimu kwa Afya.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule, ambaye ni mmoja wa wachangiaji amesema siku hiyo ya Yai inaweza kutumika vyema katika kuleta Hamasa na elimu kwa kuondoka pia Imani potofu juu ya ulaji wa Mayai akisema kuna baadhi ya watu wanakataza wajawazito kula mayai wakidai kuwa watazaa watoto wenye vipara .. lakini si kweli. zoezi la uchangiaji Mayai liligusa wengi na hivyo kusaidia vituo kadhaa Mjini Dodoma kufurahia siku hiyo.
Naye Mkuu wa Wilaya Dodoma Mh. Jaffar Shekimweri amewapongeza kampuni ya SAB investment ambayo ilianzisha kampeni hiyo kwenye kusherehekea Siku ya yai Duniani kwa kuhamasisha jamii ulaji na uchangiaji Mayai kwa Watoto wenye uhitaji.
Siku ya Yai Duniani huadhimishwa kila Ijumaa ya pili ya mwezi Oktoba kila mwaka. Siku hii hutumika kuheshimu nguvu ya virutubisho hivi na kueneza faida zake ambapo mwaka huu imeangukia tarehe 13 ya October 2023. Mkurugenzi wa SAB Saida Bwanakheri alisema "Kampuni ya SAB inajishughulisha na miradi ya ufugaji kuku tumesherehekea siku hii kwa mara ya kwanza na kupeleka ujumbe kuwa mayai sio anasa bali protein ya Bei nafuu inayopaswa kuliwa na watu wote.."
Alisema "Tumefanya hivyo kwa kukumbusha jamii pia kuvifikia vituo ya watoto Wenye Uhitaji kwani watoto Hawa wanastahiki kula Mayai katika kujenga Afya zao,"
Zoezi Hilo la Ugawaji Mayai kwa vituo vya watoto wenye uhitaji lilienda sambamba na utoaji wa elimu kuhusu Faida za Mayai"
Wakati akipokea Mayai hayo Mkuu wa kituo Cha Alrahman Orphanage Center Kilichopo Changombe Dodoma.Bi Fatma Abdalllah alisema amefurahishwa kuona siku hii inaadhimishwa na kuipongeza kampuni ya SAB kwahamasa ya kuchangisha Mayai kwa Watoto wenye uhitaji kwani mwanzoni hawakuona umuhinu wa Mayai nakusema inapita hata mwaka watoto hawali Mayai kwani pia watu wengi hawakumbuki kuchangia Mayai lakini kwa kujifunza umuhinu wa Mayai sasa wanakwenda kuweka kwenye ratiba zao na wanaamini kilichofanywa na kampuni hiyo Sasa kinakwenda kuamsha watu kuona umuhinu wa Kuchangia Mayai kwenye vituo na hatimaye kuboresha Afya za watoto vituoni.
Saida Bwanakheri Mkurugenzi wa SAB investment alisema kupitia kampeni hiyo wameweza kuvifikia vituo vitatu vya Dodoma ambavyo ni Al Rahmaan orphanage center Kilichopo chang'ombe karibu na chinangali sec school, Asmaa Binti Shams Orphanage Center na New Hope orphanage Cha Children and women organization pia wanaamini jamii inaweza kuamka kupambana na udumavu kwani Mayai ni protein rahisi kuliko nyama.
"Pamoja na kua tumeanza hili litakua ni zoezi endelevu hasa katika kuhakikisha tunafikia Mikoa inayoongoza kwa udumavu kwa kutoa elimu ya nguvu ya Yai na hata kusapoti kaya masikini kupata protein hii muhimu."
"Tunawashukuru Sana washirika wetu wote waliojumuika nasi katika kampeni hii ya CHANGIA YAI. Mungu akawaongeze walipopunguza, Hakika ilikuwa faraja Sana kuona tabasamu la watoto Hawa wakila Mayai."
LSF YATUNUKIWA CHETI CHA SHIRIKA BORA LINALOSAIDIA UKUAJI WA MASHIRIKA MADOGO YASIYO YA KISERIKALI NCHINI
Meneja wa Programu wa LSF Bw.Deogratius Bwire akipokea Cheti cha pongezi kutoka kwa Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango kama Shirika bora linalosaidia ukuaji wa Mashirika madogo yasiyo ya kiserikali nchini katika hafla ya ufungaji wa Jukwaa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali mkoani Dodoma.
***************************
Shirika la Legal Services Facility (LSF) linalojishughulisha na uwezeshwaji wa upatikanaji wa haki nchini limetunukiwa cheti cha pongezi kwa kuwa shirika linalofanya vizuri katika kujengea uwezo mashirika madogo nchini. Cheti hicho kimekabithiw na Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango katika Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali la mwaka 2023 lililofanyika jijini Dodoma
Kutunukiwa kwa cheti hicho kumetokana na juhudi zinazofanywa na LSF kwa takribani miaka 12 sasa katika kutoa ruzuku kwa mashirika yasiyo ya kiserikali zaidi ya 200 Tanzania bara na Zanzibar na pia kuyajengea uwezo wa kuwa na mifumo, kuwapatia ueledi kwenye maswala ya kifedha, kiprogram, utendaji, uongozi, kuonyesha matokeo. Aidha LSF imekuwa ikitoa elimu ya mara kwa mara kwa mashirika hayo hususani ya msaada wa kisheria juu ya sheria na mabadiliko yake ili kazi kwa ueledi katika kutatua changamoto mbalimbali za wananchini hussani wanawake na watoto
Mafanikio ya LSF yamewezeshwa chini ya ufadhil wa wadau wa maendeleo Ubalozi wa Dernmark na pia Umoja wa Ulaya. Ufadhili ambao umeleta tija kuja katika kuwezesha upatikanaji haki kupitia huduma za msaada wa kisheria bila gharama yoyote katika kila mkoa na wilaya ya Tanzania bara na Zanzibar
Akiongea kuhusu tuzo hiyo Mkurugenzi Mkuu wa LSF bi Lulu Ng’wanakilala amesema wamepokea kwa heshima kubwa pongezi hizo kutoka kwa Serikali chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii Wazee, watoto na makundi maalumua nakushukuru kwa kutambua mchango mkubwa unaofanywa na LSF katika kuchochea haki kwa wote lakini pia katika kuyajengea uwezo na kuyapatia ruzuku mashirika yasiyo ya kiserikali nchini na kuongeza kwamba watandelea kushirikiana na Serikali, wadau wa maendeleo ,mashirika binafsi pamoja na wadau wengine wengi ndani na nje ya nchi katika kutatua changamoto za wananchi hususani wanawake na watoto wakike ambao ndio waanga wakubwa wa vitendo vya ukosefu wa haki
“Tumepokea kwa furaha cheti hiki na tunaahidi kuendelea kufanya kazi kwa karibu na wadau wetu kwa kuwajengea uwezo na kuwawezesha kuwafikia wananchi wengi hususani walio maeneo ya pembezoni mwa nchi. Sambamba na hili sisi kama wadau wakubwa katika sekta hii tutaendelea kushirikiana na Baraza la Taifa la Mashirika Nchini NACONGO pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii katika kuandaa mkutano huu wa mwaka ili kuyanapata jukwaa mashirika yasiyo ya Kiserikali nchini pamoja na Serikali kuzungumza maswala muhimi ikiwemo mafanikio, changamoto na fulsa zilizopo katika undeshaji na utoaji huduma kwa wananchi. niwapongeze sana NACONGO pamoja na ofisi ya Msajili wa NGO nchini kwa kazi kubwa na nzuri ya kutuleta pamoja ila mwaka” alisema Ng’wanakilala
Jukwaa la mashirika yasiyo ya kisherikali lilifungwa na Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt Philip Isdor Mpango aligusia mambo mengi ikiwemo; kusisitiza kwa mashirika yasiyo ya kiserikali Kuzingatia uwazi na uwajibikaji katika utekelezaji miradi,Kuzingatia maadili ya kitanzania kwa kuheshimu mila na desturi za Tanzania na pia kufuata sheria na miongozo iliyowekwa nakuagiza baada ya mkutano utengenezwe mpango mkakati ambao changamoto zote zitaainishwa na mamlaka za utekelezaji.










































































